Header Ads

Viongozi wetu wamefilisika kisiasa kiasi kwamba sasa ngono ndiyo siasa?

Na Happiness Katabazi

HIVI karibuni kumekuwa na habari kubwa kuhusu kinachosadikiwa kuwa ni mahusiano yasiyofaa baina ya wabunge wawili wa jinsia tofauti. Mahusiano hayo ya kimapenzi yamekuwa yanaandikwa na kupewa nafasi kubwa kama habari za kitaifa.

Yawezekana kuwa habari kama hizi zikielezea ngono haramu au hata isiyo haramu miongoni mwa habari zinazovutia wasomaji na kuzua minong'ono ya hapa na pale.

Lakini tukumbuke kwamba sisi taifa linaloitaji kujenga misingi imara ya utamaduni.Taifa lisilo na mipaka kuhusu mahusiano ya jinsia na ngono ni taifa la hayawani.

Kumbe basi misingi ya kimaadili inayofundishwa na taasisi za dini itasaidia kulielekeza taifa kuwa na tabia njema.
Yapata miaka mitatu imepita sasa Mama Terry Ghamudu, aliwai kukemea utamaduni wa machangudoa kuamia Dodoma wakati wa vikao vya bunge.

Badala ya kusifiwa mwanaharakati huyo alidhibitiwa na kuitwa mbele ya Kamati ya Maadili ya Bunge akidaiwa kwamba amewadharilisha wabunge.

Na muda mfupi tangu mwanaharakati huyo kukemewa na kamati hiyo, baadhi ya vyombo vya habari viliendelea kuripoti habari za ngono zinazowahusu baadhi ya wawakilishi wetu na viongozi wengine waliopo kwenye medani ya siasa na kwingineko.

Leo zimechapishwa habari zinazoonyesha utovu wa nidhamu na maadili miongoni mwa baadhi ya wabunge hata kama wahusikawataweza kudhibiti kwamba habari hizo si za kweli kisheria, bado mjadala kuhusu maadili ya taifa kuhusu mahusiano ya kijinsia unabakia pale pale.

Imefika sasa wakati kujiuliza kama viongozi wetu wamefilisika kisiasa kiasi kwamba sasa ngono ndiyo siasa.?Labda ngono yaweza kutumiwa kisiasa na makundi yanayo hasimiana.

Kwa hilo la ngono tunaweza kujiuliza kama habari zilizochapishwa hivi karibuni kuhusu Mbunge wa CHADEMA, Zitto Kabwe na Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Amina Chifupa, kuwa na mahusiano ya kingono si mchezo mchafu wa kisiasa baina ya makundi yanayosadikiwa kuwa yatagombea kiti cha Uenyekiti wa UVCCM mwaka kesho?.

Sitaki kumtetea mtu yoyote kati ya Zitto na Chifupa katika hili ila ni vyema kutaadharisha kuhusu mmonyoko wa maadili ya viongozi unaojionyesha sasa miongoni mwa viongozi wetu.

Tuchepuke kidogo tujikumbushe habari tuhuma za ngono na hata za kusambaratisha ndoa kadhaa zilizokuwa zikiripotiwa kwenye vyombo vya habari siku za nyuma ambazo habari hizo zilikuwa zikimhusisha Chifupa moja kwa moja.

Tangu akiwa Mtangazaji wa Redio Clouds, Chifupa amekuwa akiandamwa na kashfa za ngono na katika kumbukumbu zangu hazionyeshi kwamba alikuwa akikanusha madai hayo zaidi ya akiwa kwenye kipindi cha Bambataa, kutumia muda mrefu kurusha vijembe kwa maasimu wake.

Kashfa hizo za kuvuruga ndoa za watu, zilisababisha mwaka 2005, wananchi wengi kuitaadharisha UVCCM, isipitishe jina la Chifupa awe mbunge kwa maelezo kwamba endapo atachaguliwa ,atapeleka mipasho bungeni, bunge litakuwa halina heshima machoni mwa wananchi wake kwakuwa waliamini na kusadiki kwamba mbunge huyo angeenda kuendeleza tabia hiyo kwenye bunge hilo tukufu.

Na sasa tunaweza kusema kwamba utabiri huo uliotabiriwa na wananchi hao pamoja na magazeti kadhaa, umetimia kwani ni kipindi cha mwaka mmoja nanusu tangu akiingie bungeni tayari ameishakumbwa na kashfa ya ngono na mbunge Zitto, hali iliyopelekea mumewe kumtwanga talaka.

Binafsi sipendi kufurahia matatizo ya wenzangu lakini Amina, alipoteuliwa kuwa mbunge alipaswa akumbuke alitabiriwa mambo gani na wanachi na pia aachane na mambo ambayo hayafai kufanywa na kiongozi kama yeye na mama wa familia kama yeye.

Pamoja na kuteuliwa kuwa mbunge,Chifupa, tulikuwa tukimsikia kwenye vyombo vya habari akiomba apigiwe nyimbo za mipasho zilizojaa vijembe, akitamba yeye na mumewe Mpakanjia hawaachani kamwe na kwamba yeye ndiye mwenye hati miliki na wanawake wengine ni wapita njia lakini wakati binadamu anapanga yake na mungu anapanga yake pia Mei 3, mwaka huu mbunge huyo aliyekuwa akijigamba hayo yote alitwanga talaka na mumewe huyo ambaye alikuwa akisema anampenda sana.

Ni huyu huyu Chifupa tulisikia taarifa zake kwamba alikwenda kigamboni kumpora picha za harusi baba wa msichana ambaye Mohamed Mpakanjia, hivi karibuni alidaiwa kuwa amefunga naye ndoa kinyemelewa wakati mkewe akiwa bungeni.Ni huyu huyu Amina tulimsikia kwamba yeye ni kiongozi wa kikundi cha Alqaida ambapo alithubutu kwenda kumfanyia vurugu msanii mmoja wa luninga akimtuhumu kuwa alikuwa akitembea na mumewe pale Chuo Cha Uandishi wa Habari DSJ Dar es Saalam.

Sasa sisi watanzania tunaamini wawakilishi wetu hawawezi kufanya mambo kama hayo adharani sasa inapotokea ndani ya bunge letu tunakuwa na viongozi wanaofanya mambo kama hayo siyo siri bunge linadharaulika na pia hata UVCCM iliyopitisha jina la Chifupa awe mbunge.

Chifupa tambua, kashfa kama hizo ambazo zinaelekezwa kwako ni mbaya na ukae ukijua hazitakuathiri peke yako kwani zitamuathiri hata mtoto wako katika maisha yake kwakuwa mtoto wako atakuwa anakwenda shule kule shule atakutana na wanafunzi wenzake wataanza kumdhalau au kumtolea maneno ya kejeli ya kuhusu wewe,huoni kwamba mtoto ataaribikiwa Kisaikolojia kwa kashfa zako na pia hata kukosa raha ya kusoma?

Na pia kwa kashfa kama hizo pia zinaleta sifa mbaya kwa familia ya wazazi wako.Leo watu wataogopa kukejeli adharani lakini pindi utakapotoka madarakani watakukejeli adharani na usiwafanye lolote. Ushauri wa bure kwako ni kwamba jiepushe na mambo ambayo kiongozi kama wewe upaswi kuyafanya na pia kaa chini utafakari ni kwanini wewe umekuwa ukiandamwa na kashfa za namna hiyo kisha fungua ukurasa mpya naamini mungu atakuongoza.

Hata hizi kashfa zikibainika si za kweli lakini kwanini mke wa Mfalme awe anatuhumiwa kutokua mwaminifu katika jamii inayomzunguka kila kukicha?

Hebu turejee kwenye mada yetu, upo usemi kwamba rushwa yaweza kuwa fedha,mali au mapenzi.Je ni viongozi wangapi wako madarakani kutokana na nguvu ya rushwa ya fedha,mali au ngono?.

Kwenye mantiki ya kijinsia taifa letu lina utamaduni butu kuhusu mahusiano ya kingono.Ngono kati ya mwanaume na wanawake wengi inachukuliwa kuwa ni sifa kwa maana kuwa mwanamme huyo anadhihirisha kuwa yeye lijali.Hiyo ni sifa.

Lakini ngono kati ya mwanamke na wanaume wengi inadhiirisha kuwa mwanamke huyo ni malaya tena kahaba aliyepindukia.Hiyo ni sifa mbaya na mwanamke wa namna hiyo udhalilishwa na kuoneka ni mchafu mbele ya jamii.

Hivyo basi wakati umefika sasa kuangalia upya utamaduni wetu na kuweka misingi sawa na udhibiti sawa kwenye maadili yetu yanayohusiana na ngono.

Lakini pia tutaadharishe kila mwananchi /viongozi kuhusu usemi usemao 'kila mla cha mwenzie na chake pia huliwa' gwiji wa muziki wa taarabu nchini Marehemu Issa Matona, alishawai kutoa usemi huo katika moja ya nyimbo zake.

Hivyo basi kwa wanaume na wanawake wanaoshiriki kuvunja ndoa za wenzao wasisikitike hapo kesho wanapokuta ndoa zao zimeingiliwa, zimevunjika na kusambaratishwa.Hayo ndiyo tunayoyaona katika habari hizi zinazozagaa kuhusu ngono za viongozi.

Mungu ibariki Afrika,Mungu inusuru Tanzania
0755312859:katabazihappy@yahoo.com:www.katabazihappy.blogspot.com

1 comment:

Alex Mwalyoyo said...

Siasa za kupakana matope ni kitu cha kawaida sana katika chama hiki, wala sishangai! Kwani hatukumbuki yaliyotokea wakati wa kampeni za kugmbea "Utawala" mwaka 2005? Bi Chifupa katumika kama mbuzi wa kafara tu, wala tusimhukumu sana. Hata hivyo, ikumbukwe kuwa Bi Chifupa alinyang'anya mume wa mtu ndipo yeye akaolewa, kwa hiyo "What goes around comes around".

Powered by Blogger.