Header Ads

WAWILI KORTINI KWA UGAIDI DAR


WAWILI KORTINI KWA UGAIDI DAR  

Na Happiness Katabazi
WIMBI la  Kuwafikisha  washukiwa wa makosa ya ugaidi mahakamani limezidi kushika kasi kwa Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), Dk. Eliezer Feleshi  Jana kuwafikisha watu Wengine Wawili kwa makosa mawili ya ugaidi Katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar Es Salaam.

Mbele ya Hakimu Mkazi  Frank Moshi, Mawakili waandamizi wa serikali Bernad Kongora, George Baraso na Peter Njike walidai Kesi hiyo ugaidi Na.31 ya Mwaka 2014 na kwamba washitakiwa Hao ni Kassim Salum Nassoro na Said Shehe Sharifu.

Wakili Njike alidai kosa la kwanza ni la kula Njama Kutenda kosa la ugaidi  kinyume na Kifungu cha 27(c) Cha Sheria ya Kuzia Ugaidi ya Mwaka 2002 na kwamba  washitakiwa hao Katika tarehe tofauti  Kati ya Januari  2013 na Juni  2014 katika maeneo tofauti  Katika eneo la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , walikuwa Njama Kutenda kosa  kimyume Cha Sheria hiyo kwa kuwaajili  watu ili washiriki kufanya matendo ya ugaidi.

Wakili Njike Alilitaja kosa la pili Kuwa kuwaajili watu ili washiriki kufanya vitendo Vya ugaidi  kinyume na Kifungu  Cha 21(b) Cha Sheria ya Kuzia Ugaidi ya Mwaka 2002. Kuwa  washitakiwa wote  Katika tarehe tofauti  Kati ya Januari  2013 na Juni 2014 katika maeneo tofauti  ya eneo la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , kwa makusudi wakikubali  kumwajili Sadick  Absaloum  na Farah Omary  ili washiriki Kutendavitendo ugaidi na kwamba upelelezi wa Kesi hiyo bado haujakamilika.

Kwa upande wake Hakimu Moshi aliwataka washitakiwa wasijibu chochote kwasababu Mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza Kesi hiyo na kwamba ni Mahakama Kuu ndiyo yenye Mamlaka ya kusikiliza Kesi hiyo na akaairisha hadi Agosti 6 Mwaka huu itakapokuja kwaajili ya kutajwa ambapo upande wa jamhuri Ulidai siku hiyo utawasilisha ombi Lao.

Julai 17 Mwaka huu, itakumbukwa DPP, aliwafikisha watu 17 mahakamani hapo KWA makosa ya ugaidi..

Chanzo: Gazeti la Tanzania Daima la IJumaa, Agosti Mosi Mwaka 2014.

No comments:

Powered by Blogger.