NJAMA ZA KUIBA MAFAILI KESI ZA EPA YAFICHUKA

Na Happiness Katabazi

JESHI la Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limefanikiwa kuzima mpango wa baadhi ya makarani na wafanyakazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kutaka kuiba majalada ya watuhumiwa wa kesi katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), yaliyopo katika mahakama hiyo.

Vyanzo vyetu vya habari kutoka ndani ya mahakama hiyo, vilidai kuwa mkakati huo ulipangwa kufanyika juzi, majira ya saa 10:30 jioni, lakini ulizimwa na polisi.

Inadaiwa kuwa baada ya polisi kumi kutoka Kituo cha Polisi Kati, kufika katika mahakama hiyo, waliwatoa kwa nguvu makarani na wafanyakazi wa mahakama hiyo ambao walikuwa bado wamo ofisini wakati muda wao wa kazi ulishamalizika.

Kwa mujibu wa habari hizo, ujio wa polisi hao mahakamani hapo, ulitokana na mwito wa Hakimu Mkuu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Addy Lyamuya, aliyetoa taarifa za kuwapo mpango huo kwani alishangazwa na hatua ya makalani hao kuendelea kubaki ofisini wakati muda wao wa kazi ulishamalizika.

“Juzi jioni waandishi wakati mmeondoka, kulikuwa na kasheshe, polisi waliitwa kimya kimya na Lyamuya na walipofika, waliingia maofisini na kuanza kuwatoa kwa amri baadhi ya makarani wakati muda wa kazi umepita na inadaiwa kulikuwa na taarifa za kuwepo njama za kuibwa kwa mafaili ya EPA,”

“Na kwambia walitolewa mbio ofisini na kuambiwa kuanzia jana (juzi) makarani ambao mahakimu wao hawatakuwa wakiendesha kesi zaidi ya saa 9.30, hawaruhusiwi kuendelea kuwepo eneo hilo, vinginevyo watachukuliwa hatua,” alisema mmoja wa maofisa wa mahakama hiyo.

Alipohojiwa na waandishi wa habari juu ya tukio hilo, Mkuu wa Waendesha Mashtaka, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Charles Kenyela, alikiri kuwapo kwa tukio hilo.

Alisema siku hiyo, alikuwa njiani kuelekea nyumbani kwake, alipigiwa simu na mkubwa wake wa kazi bila kumtaja jina, akimtaka arudi Kisutu haraka kwa madai kuwa kulikuwa na tatizo.

“Ni kweli askari waliletwa na kwa mujibu wa taarifa nilizopata ni kwamba kuna baadhi ya makarani walikuwa wakiandaa barua ya dhamana ya aliyekuwa Meneja Utumishi na Utawala wa BOT, Amatus Lyumba, ambaye yupo rumande kwa kushindwa kutimiza masharti, wakati muda wa kazi umekwisha….zaidi ya hapo sijui,” alisema Kenyela.

Alipomfuata Lyamuya ili aelezee tukio hilo, alikiri kuita askari hao lakini alisema aliwaita kwa ajili ya kuimarisha usalama katika eneo hilo la mahakama.

“Ni kweli niliomba niletewe askari polisi ili waje kuimarisha ulinzi, hayo maswali mengine siwezi kuyajibu, nendeni mkawaulize hao makarani watawaeleza kutoka midomoni mwao kwani nao wanahaki ya kuzungumza,” alisema Lyamuya.

Wakizungumzia hali hiyo ya kuwepo tuhumu za kutaka kuibwa kwa majarada ya kesi za EPA, baadhi ya mawakili wa serikali walisema hilo linaweza kufanyika lakini wao wapo makini katika utunzaji wa vielelezo vitakavyowasilishwa kwenye kesi hizo.

Taarifa za kuwepo wingu la ufisadi katika kesi za EPA kwa mara ya kwanza ziliandikwa na gazeti hili mapema Desemba mwaka jana kwamba kuna baadhi ya watendaji wa mahakama wamezigeuza kesi hizo kuwa mradi wa kujipatia fedha toka kwa washtakiwa, hali iliyosababisha baadhi ya watendaji hao kutoaminiana.

Hali hiyo ilimfanya Msajili wa Mahakama ya Rufaa, Ferdnand Wambali kuwasili mahakamani hapo kuzungumza na mahakimu na makalani wao, akiwataka wawe makini na uendeshaji wa kezi za EPA.

Hadi sasa, jumla ya washtakiwa 21 wamefikishwa katika mahakama hiyo wakituhumiwa kwa wizi wa fedha za EPA zaidi ya sh bilioni 133, mali ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumamosi, Januari 31 mwaka 2009

SHAHIDI AZIDI KUIBUA MAPYA

Na Happiness Katabazi

MKUU wa kitengo cha uendeshaji wa huduma kwa wateja katika Commercial Bank of Africa, Ronald Manongi, ambaye ni shahidi wa pili katika kesi ya wizi wa sh bilioni 1.8 za EPA inayomkakili Farijala Hussein na Mweka Hazina wa CCM Mkoa wa Kigoma, Rajabu Maranda, jana alimaliza kutoa ushahidi wake kwa kuieleza mahakama kuwa hajawahi kupokea malalamiko toka Kampuni ya BC Cars Export Ltd ya Mumbai, India kwamba imedhulumiwa fedha na Kampuni ya Kiloloma & Brothers ya Tanzania.

Shahidi huyo, alieleza hayo jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, alipokuwa akijibu maswali ya wakili wa utetezi, Majura Magafu.

Alidai BC Cars Export Ltd yenye akaunti UK iliingiziwa fedha hizo kwa njia ya Telegraph Transfer (TT) na kampuni ya Kiloloma & Brothers ambayo ilikuwa na akaunti Commercial Bank of Africa.

Hata hivyo, alidai BoT haijawahi kuitaarifu benki yake kwamba sh bilioni 1.8 walizoiingizia Kiloloma & Brothers si malipo halali.

Ifuatayo ni sehemu ya mahojiano kati ya wakili Magafu na Shahidi Manongi:

Wakili: Jana (Juzi) wakati unaongozwa na msomi mwenzangu, Stanslaus Boniface, kutoa ushahidi, uliiambia mahakama kwamba baada ya kuona kiasi hicho cha fedha kimeingia kwenye akaunti ya washtakiwa ulipatwa na wasiwasi, eh ulimpigia simu Ofisa wa BoT? Tutajie jina lake tafadhali?
Shahidi: Iman Mwakosya ambaye pia anakabiliwa na kesi za EPA katika mahakama hii.
Wakili: Eeeh.. Mwakosya alikujibu nini kwenye mazungumzo yenu katika simu?
Shahidi: Aliniambia fedha hizo ni halali na BoT imezituma kwa Kiloloma & Brothers.
Wakili: Ulimuuliza Mwakosya ni kwa nini BoT inawalipa hizo fedha?
Shahidi: Alinijibu ni deni la EPA.
Wakili: BoT waliingizia fedha akaunti kwa Tsh au fedha za kigeni ambayo zina thamani gani?
Shahidi: Paundi 921,178.83.
Wakili: Kuna siku yoyote BoT waliwahi kuwaandikia kwamba malipo hayo si halali?
Shahidi: Hawajawahi kuiandikia benki yetu kwamba malipo hayo si halalali.
Wakili: Kuna siku wateja wangu walikiuka masharti ya benki mliyowapa kabla ya kufungua akaunti yao?
Shahidi: Sikumbuki kama waliwahi kukiuka masharti.
Wakili: Ni wakati gani benki inaweza kumwambia mteja hapo umekiuka taratibu?
Shahidi: Pale mteja anapokiuka taratibu za kibenki.
Wakili: Nyie benki mnaruhusiwa kuingilia matumizi ya fedha za mteja wenu?
Shahidi: Hatuingilii.
Wakili: Mteja anapokuja na leseni na deed of partnership ya kampuni yao zinazoonyesha wanafanya biashara mbili tofauti, yaani leseni inasema wanafanya biashara ya kukusanya manyoya halafu deed of partnership inasema wanakusanya madeni mnafanyaje?
Shahidi: Sisi tulimwangalia mdhamini wa Kiloloma & Brothers ambaye ni Rashhaz(T)Ltd, ambaye ndiye alimtambulisha kwetu tukawafungulia akaunti. Na kwa mujibu wa saini ya akaunti ya Rashhaz(T)Ltd inaonyesha Maranda ndiye mmiliki kwa kampuni hiyo.
Wakili: Utakubaliana na mimi benki yenu, suala la leseni na deed of pertneship mnalifumbia macho?
Shahidi: Kimya.
Wakili: Kimsingi mtakubaliana na mimi benki yenu, Kiloloma & Brothers hamna tatizo nayo?
Shahidi: Hatuna tatizo nayo.
Wakili: Benki yenu mliwahi kuona makubaliano ya Kiloloma & Brothers kuitumia fedha BC Cars Export Ltd?
Shahidi: Hatujawahi kuyaona.
Wakili: Benki yenu ilishawahi kupata malalamiko toka BC Cars Export Ltd kwamba wamedhulumiwa fedha zao na Kiloloma & Brothers?
Shahidi: Hatujawahi kupata malalamiko.
Wakili: Mnawaamini wateja wenu (washtakiwa)?
Shahidi: Tunawaamini ndiyo maana tuliendelea kufanya nao biashara.
Aidha shahidi wa tatu katika kesi hiyo, Meneja wa Kenya Commercial Bank Tawi la Mlimani, Twilumba Talawa (34), alidai yeye ndiye aliyewafungulia akaunti ya Kiloloma & Brother washtakiwa wakati huo akiwa Meneja Msaidizi Kitengo cha Huduma kwa wateja wa benki ya United Bank of Africa.
Ifuatayo ni sehemu ya mahojiano kati ya Wakili wa Serikali na shahidi:
Wakili: Agosti mwaka 2003 ulikuwa ukifanya kazi katika benki gani?
Shahidi: United Bank of Afrika (UBA).
Wakili: Kuna umoja wa biashara unafahamika kwa jina la Kiloloma & Brothers, uliufahamu lini na vipi?
Shahidi: Niliufahamu baada ya wateja wangu kufika ofisini kwa ajili ya kufungua akaunti.
Wakili: Angalia hii fomu, waliomba kufungua akaunti ya kampuni hiyo ni akina nani?
Shahidi: Farijara na Maranda.
Wakili: Watu hao wapo hapa mahakama ebu watambue?
Shahidi: Wale wawili walioketi pale kizimbani (anawanyooshea kidole).
Wakili: Fomu hiyo ya kufungulia akaunti ya kampuni hiyo ililetwa na nani ofini kwenu?
Shahidi: Farijara Hussein na fomu hiyo alinikabidhi mimi.
Ifuatayo ni sehemu ya mahojiano kati ya wakili wa utetezi Majura Magafu na shahidi:
Wakili: Je huyu Farijara na Maranda walileta leseni wakati wanafungua akaunti?
Shahidi: Ndiyo.
Wakili: Hiyo leseni benki inawasaidia nini?
Shahidi: Haitusaidii kitu. Kesi hiyo inaendelea kusikilizwa leo.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa,Januari 30 mwaka 2009

SHAHIDI AZIDI KUIBUA MAPYA

Na Happiness Katabazi

MKUU wa kitengo cha uendeshaji wa huduma kwa wateja katika Commercial Bank of Africa, Ronald Manongi, ambaye ni shahidi wa pili katika kesi ya wizi wa sh bilioni 1.8 za EPA inayomkakili Farijala Hussein na Mweka Hazina wa CCM Mkoa wa Kigoma, Rajabu Maranda, jana alimaliza kutoa ushahidi wake kwa kuieleza mahakama kuwa hajawahi kupokea malalamiko toka Kampuni ya BC Cars Export Ltd ya Mumbai, India kwamba imedhulumiwa fedha na Kampuni ya Kiloloma & Brothers ya Tanzania.

Shahidi huyo, alieleza hayo jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, alipokuwa akijibu maswali ya wakili wa utetezi, Majura Magafu.

Alidai BC Cars Export Ltd yenye akaunti UK iliingiziwa fedha hizo kwa njia ya Telegraph Transfer (TT) na kampuni ya Kiloloma & Brothers ambayo ilikuwa na akaunti Commercial Bank of Africa.

Hata hivyo, alidai BoT haijawahi kuitaarifu benki yake kwamba sh bilioni 1.8 walizoiingizia Kiloloma & Brothers si malipo halali.

Ifuatayo ni sehemu ya mahojiano kati ya wakili Magafu na Shahidi Manongi:

Wakili: Jana (Juzi) wakati unaongozwa na msomi mwenzangu, Stanslaus Boniface, kutoa ushahidi, uliiambia mahakama kwamba baada ya kuona kiasi hicho cha fedha kimeingia kwenye akaunti ya washtakiwa ulipatwa na wasiwasi, eh ulimpigia simu Ofisa wa BoT? Tutajie jina lake tafadhali?
Shahidi: Iman Mwakosya ambaye pia anakabiliwa na kesi za EPA katika mahakama hii.
Wakili: Eeeh.. Mwakosya alikujibu nini kwenye mazungumzo yenu katika simu?
Shahidi: Aliniambia fedha hizo ni halali na BoT imezituma kwa Kiloloma & Brothers.
Wakili: Ulimuuliza Mwakosya ni kwa nini BoT inawalipa hizo fedha?
Shahidi: Alinijibu ni deni la EPA.
Wakili: BoT waliingizia fedha akaunti kwa Tsh au fedha za kigeni ambayo zina thamani gani?
Shahidi: Paundi 921,178.83.
Wakili: Kuna siku yoyote BoT waliwahi kuwaandikia kwamba malipo hayo si halali?
Shahidi: Hawajawahi kuiandikia benki yetu kwamba malipo hayo si halalali.
Wakili: Kuna siku wateja wangu walikiuka masharti ya benki mliyowapa kabla ya kufungua akaunti yao?
Shahidi: Sikumbuki kama waliwahi kukiuka masharti.
Wakili: Ni wakati gani benki inaweza kumwambia mteja hapo umekiuka taratibu?
Shahidi: Pale mteja anapokiuka taratibu za kibenki.
Wakili: Nyie benki mnaruhusiwa kuingilia matumizi ya fedha za mteja wenu?
Shahidi: Hatuingilii.
Wakili: Mteja anapokuja na leseni na deed of partnership ya kampuni yao zinazoonyesha wanafanya biashara mbili tofauti, yaani leseni inasema wanafanya biashara ya kukusanya manyoya halafu deed of partnership inasema wanakusanya madeni mnafanyaje?
Shahidi: Sisi tulimwangalia mdhamini wa Kiloloma & Brothers ambaye ni Rashhaz(T)Ltd, ambaye ndiye alimtambulisha kwetu tukawafungulia akaunti. Na kwa mujibu wa saini ya akaunti ya Rashhaz(T)Ltd inaonyesha Maranda ndiye mmiliki kwa kampuni hiyo.
Wakili: Utakubaliana na mimi benki yenu, suala la leseni na deed of pertneship mnalifumbia macho?
Shahidi: Kimya.
Wakili: Kimsingi mtakubaliana na mimi benki yenu, Kiloloma & Brothers hamna tatizo nayo?
Shahidi: Hatuna tatizo nayo.
Wakili: Benki yenu mliwahi kuona makubaliano ya Kiloloma & Brothers kuitumia fedha BC Cars Export Ltd?
Shahidi: Hatujawahi kuyaona.
Wakili: Benki yenu ilishawahi kupata malalamiko toka BC Cars Export Ltd kwamba wamedhulumiwa fedha zao na Kiloloma & Brothers?
Shahidi: Hatujawahi kupata malalamiko.
Wakili: Mnawaamini wateja wenu (washtakiwa)?
Shahidi: Tunawaamini ndiyo maana tuliendelea kufanya nao biashara.
Aidha shahidi wa tatu katika kesi hiyo, Meneja wa Kenya Commercial Bank Tawi la Mlimani, Twilumba Talawa (34), alidai yeye ndiye aliyewafungulia akaunti ya Kiloloma & Brother washtakiwa wakati huo akiwa Meneja Msaidizi Kitengo cha Huduma kwa wateja wa benki ya United Bank of Africa.
Ifuatayo ni sehemu ya mahojiano kati ya Wakili wa Serikali na shahidi:
Wakili: Agosti mwaka 2003 ulikuwa ukifanya kazi katika benki gani?
Shahidi: United Bank of Afrika (UBA).
Wakili: Kuna umoja wa biashara unafahamika kwa jina la Kiloloma & Brothers, uliufahamu lini na vipi?
Shahidi: Niliufahamu baada ya wateja wangu kufika ofisini kwa ajili ya kufungua akaunti.
Wakili: Angalia hii fomu, waliomba kufungua akaunti ya kampuni hiyo ni akina nani?
Shahidi: Farijara na Maranda.
Wakili: Watu hao wapo hapa mahakama ebu watambue?
Shahidi: Wale wawili walioketi pale kizimbani (anawanyooshea kidole).
Wakili: Fomu hiyo ya kufungulia akaunti ya kampuni hiyo ililetwa na nani ofini kwenu?
Shahidi: Farijara Hussein na fomu hiyo alinikabidhi mimi.
Ifuatayo ni sehemu ya mahojiano kati ya wakili wa utetezi Majura Magafu na shahidi:
Wakili: Je huyu Farijara na Maranda walileta leseni wakati wanafungua akaunti?
Shahidi: Ndiyo.
Wakili: Hiyo leseni benki inawasaidia nini?
Shahidi: Haitusaidii kitu. Kesi hiyo inaendelea kusikilizwa leo.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa,Januari 30 mwaka 2009
Mwisho

SHAHIDI AZIDI KUIBUA MAPYA

Na Happiness Katabazi

MKUU wa kitengo cha uendeshaji wa huduma kwa wateja katika Commercial Bank of Africa, Ronald Manongi, ambaye ni shahidi wa pili katika kesi ya wizi wa sh bilioni 1.8 za EPA inayomkakili Farijala Hussein na Mweka Hazina wa CCM Mkoa wa Kigoma, Rajabu Maranda, jana alimaliza kutoa ushahidi wake kwa kuieleza mahakama kuwa hajawahi kupokea malalamiko toka Kampuni ya BC Cars Export Ltd ya Mumbai, India kwamba imedhulumiwa fedha na Kampuni ya Kiloloma & Brothers ya Tanzania.

Shahidi huyo, alieleza hayo jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, alipokuwa akijibu maswali ya wakili wa utetezi, Majura Magafu.

Alidai BC Cars Export Ltd yenye akaunti UK iliingiziwa fedha hizo kwa njia ya Telegraph Transfer (TT) na kampuni ya Kiloloma & Brothers ambayo ilikuwa na akaunti Commercial Bank of Africa.

Hata hivyo, alidai BoT haijawahi kuitaarifu benki yake kwamba sh bilioni 1.8 walizoiingizia Kiloloma & Brothers si malipo halali.

Ifuatayo ni sehemu ya mahojiano kati ya wakili Magafu na Shahidi Manongi:

Wakili: Jana (Juzi) wakati unaongozwa na msomi mwenzangu, Stanslaus Boniface, kutoa ushahidi, uliiambia mahakama kwamba baada ya kuona kiasi hicho cha fedha kimeingia kwenye akaunti ya washtakiwa ulipatwa na wasiwasi, eh ulimpigia simu Ofisa wa BoT? Tutajie jina lake tafadhali?
Shahidi: Iman Mwakosya ambaye pia anakabiliwa na kesi za EPA katika mahakama hii.
Wakili: Eeeh.. Mwakosya alikujibu nini kwenye mazungumzo yenu katika simu?
Shahidi: Aliniambia fedha hizo ni halali na BoT imezituma kwa Kiloloma & Brothers.
Wakili: Ulimuuliza Mwakosya ni kwa nini BoT inawalipa hizo fedha?
Shahidi: Alinijibu ni deni la EPA.
Wakili: BoT waliingizia fedha akaunti kwa Tsh au fedha za kigeni ambayo zina thamani gani?
Shahidi: Paundi 921,178.83.
Wakili: Kuna siku yoyote BoT waliwahi kuwaandikia kwamba malipo hayo si halali?
Shahidi: Hawajawahi kuiandikia benki yetu kwamba malipo hayo si halalali.
Wakili: Kuna siku wateja wangu walikiuka masharti ya benki mliyowapa kabla ya kufungua akaunti yao?
Shahidi: Sikumbuki kama waliwahi kukiuka masharti.
Wakili: Ni wakati gani benki inaweza kumwambia mteja hapo umekiuka taratibu?
Shahidi: Pale mteja anapokiuka taratibu za kibenki.
Wakili: Nyie benki mnaruhusiwa kuingilia matumizi ya fedha za mteja wenu?
Shahidi: Hatuingilii.
Wakili: Mteja anapokuja na leseni na deed of partnership ya kampuni yao zinazoonyesha wanafanya biashara mbili tofauti, yaani leseni inasema wanafanya biashara ya kukusanya manyoya halafu deed of partnership inasema wanakusanya madeni mnafanyaje?
Shahidi: Sisi tulimwangalia mdhamini wa Kiloloma & Brothers ambaye ni Rashhaz(T)Ltd, ambaye ndiye alimtambulisha kwetu tukawafungulia akaunti. Na kwa mujibu wa saini ya akaunti ya Rashhaz(T)Ltd inaonyesha Maranda ndiye mmiliki kwa kampuni hiyo.
Wakili: Utakubaliana na mimi benki yenu, suala la leseni na deed of pertneship mnalifumbia macho?
Shahidi: Kimya.
Wakili: Kimsingi mtakubaliana na mimi benki yenu, Kiloloma & Brothers hamna tatizo nayo?
Shahidi: Hatuna tatizo nayo.
Wakili: Benki yenu mliwahi kuona makubaliano ya Kiloloma & Brothers kuitumia fedha BC Cars Export Ltd?
Shahidi: Hatujawahi kuyaona.
Wakili: Benki yenu ilishawahi kupata malalamiko toka BC Cars Export Ltd kwamba wamedhulumiwa fedha zao na Kiloloma & Brothers?
Shahidi: Hatujawahi kupata malalamiko.
Wakili: Mnawaamini wateja wenu (washtakiwa)?
Shahidi: Tunawaamini ndiyo maana tuliendelea kufanya nao biashara.
Aidha shahidi wa tatu katika kesi hiyo, Meneja wa Kenya Commercial Bank Tawi la Mlimani, Twilumba Talawa (34), alidai yeye ndiye aliyewafungulia akaunti ya Kiloloma & Brother washtakiwa wakati huo akiwa Meneja Msaidizi Kitengo cha Huduma kwa wateja wa benki ya United Bank of Africa.
Ifuatayo ni sehemu ya mahojiano kati ya Wakili wa Serikali na shahidi:
Wakili: Agosti mwaka 2003 ulikuwa ukifanya kazi katika benki gani?
Shahidi: United Bank of Afrika (UBA).
Wakili: Kuna umoja wa biashara unafahamika kwa jina la Kiloloma & Brothers, uliufahamu lini na vipi?
Shahidi: Niliufahamu baada ya wateja wangu kufika ofisini kwa ajili ya kufungua akaunti.
Wakili: Angalia hii fomu, waliomba kufungua akaunti ya kampuni hiyo ni akina nani?
Shahidi: Farijara na Maranda.
Wakili: Watu hao wapo hapa mahakama ebu watambue?
Shahidi: Wale wawili walioketi pale kizimbani (anawanyooshea kidole).
Wakili: Fomu hiyo ya kufungulia akaunti ya kampuni hiyo ililetwa na nani ofini kwenu?
Shahidi: Farijara Hussein na fomu hiyo alinikabidhi mimi.
Ifuatayo ni sehemu ya mahojiano kati ya wakili wa utetezi Majura Magafu na shahidi:
Wakili: Je huyu Farijara na Maranda walileta leseni wakati wanafungua akaunti?
Shahidi: Ndiyo.
Wakili: Hiyo leseni benki inawasaidia nini?
Shahidi: Haitusaidii kitu. Kesi hiyo inaendelea kusikilizwa leo.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa,Januari 30 mwaka 2009
Mwisho

SHAHIDI AZIDI KUIBUA MAPYA

Na Happiness Katabazi

MKUU wa kitengo cha uendeshaji wa huduma kwa wateja katika Commercial Bank of Africa, Ronald Manongi, ambaye ni shahidi wa pili katika kesi ya wizi wa sh bilioni 1.8 za EPA inayomkakili Farijala Hussein na Mweka Hazina wa CCM Mkoa wa Kigoma, Rajabu Maranda, jana alimaliza kutoa ushahidi wake kwa kuieleza mahakama kuwa hajawahi kupokea malalamiko toka Kampuni ya BC Cars Export Ltd ya Mumbai, India kwamba imedhulumiwa fedha na Kampuni ya Kiloloma & Brothers ya Tanzania.

Shahidi huyo, alieleza hayo jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, alipokuwa akijibu maswali ya wakili wa utetezi, Majura Magafu.

Alidai BC Cars Export Ltd yenye akaunti UK iliingiziwa fedha hizo kwa njia ya Telegraph Transfer (TT) na kampuni ya Kiloloma & Brothers ambayo ilikuwa na akaunti Commercial Bank of Africa.

Hata hivyo, alidai BoT haijawahi kuitaarifu benki yake kwamba sh bilioni 1.8 walizoiingizia Kiloloma & Brothers si malipo halali.

Ifuatayo ni sehemu ya mahojiano kati ya wakili Magafu na Shahidi Manongi:
Wakili: Jana (Juzi) wakati unaongozwa na msomi mwenzangu, Stanslaus Boniface, kutoa ushahidi, uliiambia mahakama kwamba baada ya kuona kiasi hicho cha fedha kimeingia kwenye akaunti ya washtakiwa ulipatwa na wasiwasi, eh ulimpigia simu Ofisa wa BoT? Tutajie jina lake tafadhali?
Shahidi: Iman Mwakosya ambaye pia anakabiliwa na kesi za EPA katika mahakama hii.
Wakili: Eeeh.. Mwakosya alikujibu nini kwenye mazungumzo yenu katika simu?
Shahidi: Aliniambia fedha hizo ni halali na BoT imezituma kwa Kiloloma & Brothers.
Wakili: Ulimuuliza Mwakosya ni kwa nini BoT inawalipa hizo fedha?
Shahidi: Alinijibu ni deni la EPA.
Wakili: BoT waliingizia fedha akaunti kwa Tsh au fedha za kigeni ambayo zina thamani gani?
Shahidi: Paundi 921,178.83.
Wakili: Kuna siku yoyote BoT waliwahi kuwaandikia kwamba malipo hayo si halali?
Shahidi: Hawajawahi kuiandikia benki yetu kwamba malipo hayo si halalali.
Wakili: Kuna siku wateja wangu walikiuka masharti ya benki mliyowapa kabla ya kufungua akaunti yao?
Shahidi: Sikumbuki kama waliwahi kukiuka masharti.
Wakili: Ni wakati gani benki inaweza kumwambia mteja hapo umekiuka taratibu?
Shahidi: Pale mteja anapokiuka taratibu za kibenki.
Wakili: Nyie benki mnaruhusiwa kuingilia matumizi ya fedha za mteja wenu?
Shahidi: Hatuingilii.
Wakili: Mteja anapokuja na leseni na deed of partnership ya kampuni yao zinazoonyesha wanafanya biashara mbili tofauti, yaani leseni inasema wanafanya biashara ya kukusanya manyoya halafu deed of partnership inasema wanakusanya madeni mnafanyaje?
Shahidi: Sisi tulimwangalia mdhamini wa Kiloloma & Brothers ambaye ni Rashhaz(T)Ltd, ambaye ndiye alimtambulisha kwetu tukawafungulia akaunti. Na kwa mujibu wa saini ya akaunti ya Rashhaz(T)Ltd inaonyesha Maranda ndiye mmiliki kwa kampuni hiyo.
Wakili: Utakubaliana na mimi benki yenu, suala la leseni na deed of pertneship mnalifumbia macho?
Shahidi: Kimya.
Wakili: Kimsingi mtakubaliana na mimi benki yenu, Kiloloma & Brothers hamna tatizo nayo?
Shahidi: Hatuna tatizo nayo.
Wakili: Benki yenu mliwahi kuona makubaliano ya Kiloloma & Brothers kuitumia fedha BC Cars Export Ltd?
Shahidi: Hatujawahi kuyaona.
Wakili: Benki yenu ilishawahi kupata malalamiko toka BC Cars Export Ltd kwamba wamedhulumiwa fedha zao na Kiloloma & Brothers?
Shahidi: Hatujawahi kupata malalamiko.
Wakili: Mnawaamini wateja wenu (washtakiwa)?
Shahidi: Tunawaamini ndiyo maana tuliendelea kufanya nao biashara.
Aidha shahidi wa tatu katika kesi hiyo, Meneja wa Kenya Commercial Bank Tawi la Mlimani, Twilumba Talawa (34), alidai yeye ndiye aliyewafungulia akaunti ya Kiloloma & Brother washtakiwa wakati huo akiwa Meneja Msaidizi Kitengo cha Huduma kwa wateja wa benki ya United Bank of Africa.
Ifuatayo ni sehemu ya mahojiano kati ya Wakili wa Serikali na shahidi:
Wakili: Agosti mwaka 2003 ulikuwa ukifanya kazi katika benki gani?
Shahidi: United Bank of Afrika (UBA).
Wakili: Kuna umoja wa biashara unafahamika kwa jina la Kiloloma & Brothers, uliufahamu lini na vipi?
Shahidi: Niliufahamu baada ya wateja wangu kufika ofisini kwa ajili ya kufungua akaunti.
Wakili: Angalia hii fomu, waliomba kufungua akaunti ya kampuni hiyo ni akina nani?
Shahidi: Farijara na Maranda.
Wakili: Watu hao wapo hapa mahakama ebu watambue?
Shahidi: Wale wawili walioketi pale kizimbani (anawanyooshea kidole).
Wakili: Fomu hiyo ya kufungulia akaunti ya kampuni hiyo ililetwa na nani ofini kwenu?
Shahidi: Farijara Hussein na fomu hiyo alinikabidhi mimi.
Ifuatayo ni sehemu ya mahojiano kati ya wakili wa utetezi Majura Magafu na shahidi:
Wakili: Je huyu Farijara na Maranda walileta leseni wakati wanafungua akaunti?
Shahidi: Ndiyo.
Wakili: Hiyo leseni benki inawasaidia nini?
Shahidi: Haitusaidii kitu. Kesi hiyo inaendelea kusikilizwa leo.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa,Januari 30 mwaka 2009


SHAHIDI AMLIPUA NAIBU GAVANA

*Adai aliikingia kifua kampuni ya Maranda
*Adai waliwekewa bil. 1.8/- zimebaki 115,394/-

Na Happiness Katabazi

SHAHIDI wa pili katika kesi ya wizi wa sh bilioni 1.8 wa fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), inayomkabili Farijala Hussein na Mweka Hazina wa CCM Mkoa wa Kigoma, Rajab Shaaban Maranda, ameieleza mahakama kuwa aliyekuwa Naibu Gavana, Juma Reli, ndiye alimweleza asitilie mashaka ingizo la fedha katika Kampuni ya Kiloloma & Brothers.
Shahidi huyo, Mkuu wa Kitengo cha Uendeshaji wa Huduma kwa wateja katika Commercial Bank of Africa ambayo awali ilikuwa ikiitwa United Bank of Africa, Ronald Manongi, alidai washtakiwa hao ni wateja wa benki yao, walifungua akaunti ya kampuni Agosti 31 mwaka 2005 na Septemba 2, mwaka huo huo na kisha akaunti hiyo iliingiziwa sh 1,864,949,294.45 na BoT.
Kiloloma & Brothers ni kampuni inayodaiwa kuchota fedha za EPA na shahidi wa kwanza katika kesi hiyo, Ofisa Mtendaji Mkuu wa BRELA, Estreriano Mahingira, alipotoa ushahidi wake juzi alikana kwamba kampuni hiyo haijawahi kusajiliwa na ofisi yake.
Akitoa ushahidi wake huku akiongozwa na Wakili Kiongozi wa Serikali, Stanslaus Boniface, shahidi huyo alidai akiwa Mkuu wa Kitengo cha Uendeshaji wa Huduma kwa wateja wa benki hiyo, alishtushwa na hali hiyo ya ingizo la fedha ambalo limeingizwa kwenye akaunti hiyo ambayo tangu ifunguliwe ilikuwa na siku mbili.

“Baada ya kuona fedha hizo zimeingia kwenye akaunti ya Kiloloma & Brothers nilifanya mambo mawili; kwanza nilitilia shaka hali hiyo na nikaandika taarifa ya shaka yangu kwa Kurugenzi ya Usimamizi wa Mabenki (BoT) na kuonyesha jinsi akaunti ya kampuni hiyo ilivyofunguliwa na kiasi hicho cha fedha kilivyoingia haraka kwenye akaunti hiyo,” alidai Manongi katika ushahidi wake.
Alidai barua yake ilijibiwa Septemba 25 mwaka 2005 na Naibu Gavana wa BoT, Juma Reli, ambaye mpaka sasa anashikilia wadhifa huo.
Sehemu ya barua hiyo inasomeka ‘Manongi taarifa yako mashaka kuhusu hali hiyo BoT imeipokea na tunakutoa wasiwasi kwamba kampuni hiyo inafanya kazi zake kihalali na ofisi yetu. Septemba 2, mwaka huo tuliingizia kiasi hicho, pia Agosti 17 mwaka huo huo, tuliingizia fedha kampuni ya Rashhaz (T) Ltd’.

Alieleza kuwa baada ya kupokea barua hiyo, aliwaandikia wateja wake (washtakiwa) barua, ili wamweleze hizo fedha zilizotoka BoT walipewa kwa ajili shughuli gani, watakuwa wakizitoa fedha kwenye akaunti yao kwa njia ya fedha taslimu au kuzituma nje ya nchi.
Manongi, alidai Septemba 26, mwaka 2005 wateja wake (washtakiwa) walijibu barua yake ya Septemba 19 mwaka huo huo, ambayo ilisainiwa na Rajabu Maranda ambayo ilieleza kwamba chanzo cha fedha hizo ni kibali cha kuruhusiwa na kampuni ya M/S BC Cars Export Ltd kudai deni lao.
Ifuatayo ni sehemu ya mahojiano kati ya Wakili Kiongozi wa Serikali, Stanslaus Boniface na Shahidi:
Wakili: Ieleze mahakama shughuli yako kubwa pale Benki ya Biashara ya Afrika?
Shahidi: Kuhakikisha benki yetu ina fedha za kutosha za kulipa wateja wetu, kusimamia idara ya huduma kwa wateja na kuhakikisha wateja wanapata huduma ipasavyo.
Wakili: Benki yenu ilianzishwa lini?
Shahidi: Mwaka 2002, wakati huo ilikuwa ikiitwa United Bank of Africa (UBA), lakini mwaka 2007 tulifanya mabadiliko ya jina na kwa sasa inatambulika kwa jina la Commercial Bank of Africa.
Wakili: Shahidi, hebu angalia hizo document zinaonyesha nini?
Shahidi: Zinaonyesha taratibu za kufungua akaunti.
Wakili: Hizo document mbili walipewa kina nani ?
Shahidi: Kiloloma & Brothers ambao ni Farijara na Maranda.
Wakili: Kuna mtu unamfahamu kati yao?
Shahidi: Namfahamu Farijara.
Wakili: Unamfahamu vipi?
Shahidi: Namfahamu katika uendeshaji wa Kiloloma & Brothers, alivyokuwa akija katika benki yetu na kuchukua fedha.
Wakili: Unaweza kumtambua hapa mahakamani amekaa upande gani?
Shahidi: Yule pale amekaa kushoto kizimbani na ndiye mshitakiwa wa kwanza katika kesi hii (alimnyooshea kidole).
Wakili: Fomu hii ya kuomba kufungua akaunti ina maelezo gani mengine?
Shahidi: Ina maelezo ya waombaji kuwa ni raia wa Tanzania, kampuni hiyo itaendeshwa na watu wawili ambao ni Farijala na Maranda.
Wakili: Huyu anayemtambulisha Kiloloma & Brothers kwa benki yenu ni nani?
Shahidi: Ni kampuni ya Rashhaz (T) Ltd.
Wakili: Benki yenu ina mahusiano gani Rashhaz (T) Ltd?
Shahidi: Rashhaz (T) Ltd walikuwa wamefungua akaunti kwenye benki yetu.
Wakili: Nani ni wamiliki wa Rashhaz (T) Ltd?
Shahidi: Kutokana na saini ya akaunti ya Rashhaz, kampuni hiyo inaonekana ni Rajabu Maranda.
Wakili: Hebu angalia fomu hii kwa makini inaonyesha Kampuni ya Kiloloma & Brothers nani ni wakurugenzi wake?
Shahidi: Farijara na Maranda.
Wakili: Fomu hiyo inaitwaje?
Shahidi: Deed of Partnership.
Wakili: Ifungue na uisome paragraph 4, inasemaje…soma kwa sauti.
Shahidi: Inasomeka kwamba Partners hao wamekubaliana kuanzisha ushirikiano kwa ajili ya kuanzisha biashara ya kuuza mafuta.
Wakili: Katika fomu hiyo fungua ukurasa wa nne, angalia paragraph ya 4.1, inasemaje?
Shahidi: Inasema partners hao watafanya biashara ya kuuza mafuta kwa pamoja kwa kutumia jina la Kiloloma & Brothers.
Wakili: Fomu hiyo ilikuja kwenye benki yenu?
Shahidi: Ilikuja kwenye idara yetu kufungua akaunti.
Wakili: Kitaalamu fomu hiyo inaitwaje?
Shahidi: Account Information.
Wakili: Hiyo fomu ukiiangalia imebeba taarifa gani?
Shahidi: Imebeba jina la Kiloloma & Brothers, P. o. Box 3983, Dar es Salaam. Pia inaonyesha aina ya akaunti waliyofungua kuwa ni Current Account, biashara ambayo inafanya na fomu hiyo ya kufungulia akaunti ya pamoja inaeleza Kiloloma & Brothers itafanya biashara ya kukusanya madeni na fomu hiyo ilijazwa na washtakiwa wote wawili.
Wakili: Umebaini kitu gani kipya baada ya kuzipitia hizo fomu mbili nilizokupatia hapa mahakamani?
Shahidi: Nimegundua majukumu mawili tofauti katika fomu hizi. Mosi, jukumu la kukusanya madeni na pili kuuza mafuta.
Wakili: Aina gani ya akaunti ilifunguliwa na Kilolomo & Brothers?
Shahidi: Current Account.
Wakili: Tutajie namba ya akaunti hiyo?
Shahidi: 0101305008.
Wakili: Baada ya akaunti hiyo kufunguliwa, wamiliki wa akaunti hiyo walipewa kitu gani na uongozi wa benki yenu?
Shahidi: Cheque Book na waliomba yenye leaf 25.
Wakili: Mbali na cheque book, kuna kitu kingine benki iliwapatia?
Shahidi: Nakumbuka ni hiyo cheque book ndiyo tuliwapatia.
Wakili: Hebu angalia hayo makabrasha ni kitu gani?
Shahidi: Ni statement of Account.
Wakili: Ya nani?
Shahidi: Kiloloma & Brothers.
Wakili: Kutoka benki gani?
Shahidi: Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) Ltd.
Wakili: Unapenda kutoa mahakamani itumike kama kielezo?
Shahidi : Ndiyo.
Wakili: Kampuni ya Kiloloma & Brothers ilifunguliwa rasmi tarehe ngapi?
Shahidi: Agosti 31, mwaka 2005.
Wakili: Wateja wako wakati wanafungua akaunti hiyo waliweka kiasi gani cha fedha?
Shahidi: Sh 500,000 tu kama walivyotakiwa na masharti ya benki siku hiyo.
Wakili: Baada ya hapo akaunti hiyo iliwahi kupata fedha?
Shahidi: Ndiyo, ilipata fedha toka BoT, Septemba 2, mwaka 2005.
Wakili: Kiasi gani hicho shahidi?
Shahidi: Sh 1,864,949,294.45.
Wakili: Hii fedha iliingia toka BoT kwa njia gani?
Shahidi: Kwa njia ya Telegraph Transfer (TT) toka BoT kuja kwenye akaunti ya Kilolomo & Brothers ambayo ipo kwenye benki yetu.
Wakili: Telegraph Transfer (TT) ni kitu gani hicho?
Shahidi: Ni njia ya utumaji fedha kwa kutumia Electronic.
Wakili: Zaidi ya hapo ilikuwaje?
Shahidi: Benki yetu wakati huo ikiitwa United Bank of Africa, ilipata barua toka BoT.
Wakili: Soma kwa sauti hiyo barua.
Shahidi: Ni barua ya Septemba 2 mwaka 2005 inakwenda kwa wakurugenzi wa Kilolomo & Brothers inayosomeka ‘out standing debt Uk pound 921,878.83 B.C Cars Exports Ltd ya Mumbai India.
Wakili: Barua hiyo ya BoT ilikuwa na ujumbe gani?
Shahidi: Ilikuwa na ujumbe kwamba BoT imeiingizia sh 1,864,949,294.45 kwenye akaunti ya kampuni hiyo iliyopo kwenye benki yetu.
Wakili: Hiyo barua ya BoT nakala yake alikuwa anapewa nani?
Shahidi: Mkurugenzi wa benki.
Wakili: Shahidi, hebu tuweke vizuri, Agosti 31, mwaka 2005 kampuni ilifunguliwa na Septemba 2 mwaka huo huo fedha hiyo iliingia, ulichukua hatua gani?
Shahidi: Mimi kama Mkuu wa Kitengo cha Uendeshaji, baada ya kuona fedha hizo zimeingia kwenye akaunti hiyo nilifanya mambo mawili.
Wakili: Yapi na yataje?
Shahidi: Kwanza nilitia shaka, nikaandika taarifa kwa Kurugenzi ya Usimamizi wa Mabenki nchini pale BoT na kueleza jinsi akaunti ilivyofunguliwa na kiasi cha fedha kilivyoingizwa haraka.
Wakili: BoT walikujibu hiyo taarifa ya mashaka yako?
Shahidi: Ndiyo walinijibu.
Wakili: Hiyo document ni ya nini?
Shahidi: Ni barua ya BoT kuja kwangu.
Wakili; Imeandikwa na nani hiyo barua?
Shahidi: Naibu Gavana.
Wakili: Inasemaje, soma tafadhari.
Shahidi: ‘Taarifa yako ya mashaka uliyoituma kwenye kurugenzi yetu tumeipokea na tunakutoa shaka usiitilie shaka Kampuni ya Kiloloma & Brothers kwani inafanya kazi zake kihalali na BoT ndiyo imewatumia fedha hizo’.
Wakili: Baada ya kupokea barua hiyo ya BoT ulifanya nini?
Shahidi: Sikuishia hapo niliwaandikia wateja hao barua ambao walinijibu wakisema chanzo cha fedha hizo ni realize of debt applied on behalf of principle M/S BC Cars Export Ltd.
Wakili: Ambayo ni nini kwa lugha nyepesi?
Shahidi: Kulipwa deni kwa niaba ya Principle wao ambao ni M/S BC Cars Export Ltd.
Wakili: Katika paraghraph ya barua hiyo waombaji wanasema wanafanya biashara gani?
Shahidi: Maranda anasema anafanyabiashara mpya ya kukusanya deni la kampuni ya nje ambapo deni hilo lipo Benki Kuu kwa miongo miwili.
Wakili: Eh Katika paragraph 4,3,2 isome taratibu ukiwa umetulia ili mahakama isikie?
Shahidi: Katika paragraph hiyo kushuka chini Maranda ananijibu wana kibali maalumu cha kutumia sehemu ya fedha iliyolipwa na BoT kutokana na makubaliano yao na Principle wao M/S BC Cars Exports Ltd na kwamba makubaliano yao yapo Benki Kuu.
Wakili: Soma pia paragraph ya 2 kutoka chini, katika barua ya washtakiwa hawa.
Shahidi: Imeeleza kampuni yao ni entitled katika fedha zilizolipwa na kamisheni hiyo imeidhinishwa na principle wao. Huo ndiyo ujumbe uliopo katika hiyo paragraph.
Wakili: Uliangalia kielelezo cha tano na kielelezo hiki cha saba, unasemaje?
Shahidi: Vinaonyesha walikubaliana na BoT kufanya hivyo na nikaruhusu akaunti yao iendelee kufanya kazi.
Wakili: Iambie mahakama Septemba 2 mwaka 2005 kulitokea nini kwenye akaunti ya washtakiwa?
Shahidi: Siku hiyo fedha iliingia kwenye akaunti na siku hiyo hiyo walitoa sh milioni 30.
Wakili: Septemba 5, mwaka huo, kulitokea nini kwenye akaunti hiyo?
Shahidi: Kulikuwa na cash withdraw fomu ya sh milioni 150 toka kwenye akaunti hiyo ya Kiloloma & Brothers.
Wakili: Hiyo cash draw form nani aliyeidhinisha kampuni hiyo ichukue fedha?
Shahidi: Mimi, kwa sababu nilikuwa Mkuu wa Kitengo.
Wakili: Nani aliombwa walipwe hiyo fedha?
Shahidi: Farijara na Maranda.
Wakili: Septemba 13 mwaka 2005 akaunti hiyo ya Kiloloma ilitokea nini?
Shahidi: Kampuni hiyo ilichukua cash milioni 100 kwa kutumia cheque book ya kampuni yao.
Wakili: Hebu taja namba ya cheque book ya kampuni hiyo?
Shahidi: 062352.
Wakili: Na Septemba 14 mwaka huo, akaunti hiyo ilikumbana na nini tena?
Shahidi: Hawa partners waliiomba benki yetu iwapatie Bankers Cheque.
Wakili: Kazi yake nini?
Shahidi: Ina thamani ya siku ile ile katika mabenki hapa nchini tofauti na cheque za watu binafsi. Na cheque bank ukitumia unaweza kulipwa siku hiyo hiyo. Walitupatia hundi namba 062353 tukawapatia cheque bank yenye namba 029421 iliyokuwa ikilipwa kwa Maranda na tulimlipa sh 284,700,000.
Wakili: Septemba 15 mwaka huo, kilitokea nini kwenye akaunti ya wateja hao?
Shahidi: Kiloloma walifanya cash with draw tena ya sh milioni 300 kwa njia ya hundi ya kampuni yao yenye namba 062354.
Wakili: Nani alikuwa akichukua hizo fedha?
Shahidi: Kiloloma & Brothers.
Wakili: Eh Septemba 28 mwaka huo kilitokea nini tena kwenye akaunti hiyo?
Shahidi: Kampuni hiyo kwa mara nyingine ilifanya cash with draw ya sh milioni 100.
Wakili: Kwa cheki namba ngapi?
Shahidi: Kwa hundi ya kampuni yao namba 0623550.
Wakili: Oktoba 7 mwaka mwaka huu huo, ni kilitokea kwenye akaunti ya wateja wako?
Shahidi: Walifanya tena cash withdraw ya sh milioni 20 kwa hundi ya kampuni yenye namba 062356.
Wakili: Shahidi usichoke, iambie mahakama Oktoba 19 mwaka huo huo tena nini kilitokea kwenye akaunti hiyo?
Shahidi: Kampuni hiyo ilituma fedha nje ya nchi kwa kutumia TT, paundi 200,000 kwenda kwa B.C Cars Export Ltd yenye akaunti HSBC United Kingdom. Na pamoja kutuma hela hiyo nje ya nchi walichukua sh milioni 100.
Wakili: Kitu gani kilitokea Oktoba 21 mwaka kwenye akaunti hiyo?
Shahidi: Walichukua tena cash withdraw sh milioni 45 na walichukua kupitia hundi ya kampuni yao yenye namba 062358.
Wakili: Oktoba 24 mwaka huo huo, kilitokea nini kwenye akaunti yao?
Shahidi: Vilitokea vitu viwili kwenye akaunti hiyo, mosi, walituma nje paundi elfu 150 kwenye kwa B.C Cars ya UK na jambo la pili Kiloloma & Brothers walinunua dola elfu 10 yenye jumla ya sh milioni 11.5 na walinunua kwenye benki yetu hizo dola na walitueleza wamefikia uamuzi wao kwa sababu hawana akaunti ya fedha za kigeni.
Wakili: Turudi nyuma kidogo ile paundi elfu 150 iliyotumwa kwa kampuni ya nje ina thamani kwa kwa fedha ya Tanzania?
Shahidi: 308,700,000.
Wakili: Desemba 6 mwaka 2005 nini kilitokea kwenye akaunti hiyo?
Shahidi: Walichukua tena cash withdraw milioni 5.2 kupitia hundi ya kampuni yao yenye namba 062360.
Wakili: Baada ya tarehe hiyo kumbukumbu zako zinasemaje kuna maagizo au matoleo katika akaunti hiyo?
Shahidi: Kumbukumbu zinanionyesha hakuna utoaji fedha hadi Novemba 8 mwaka 2006 alihamisha sh 41, 920 kwenda kwenye akaunti yao nyingine ya fedha za kigeni dola yenye namba 0101305019.
Wakili: Unasema hii akaunti ya kigeni ni ya nani vile?
Shahidi: Kiloloma & Brothers.
Wakili: Baada ya hapo.
Shahidi: Hakuna uhamisho wa fedha uliofanywa na wateja hao katika akaunti yao.
Wakili: Mbali na sh bilioni 1.8 zilizoingizwa na BoT kwenye akaunti hiyo, kuna fedha yoyote iliwahi kuingia kwenye akaunti hiyo?
Shahidi: Haijawahi kuingia fedha yoyote hadi sasa.
Wakili: Mpaka leo hii akaunti ya wateja hao ina akiba ya kiasi gani?
Shahidi: Ina akiba ya sh 115,394.94 tu.
Baada ya wakili Boniface kumaliza kumhoji shahidi, Hakimu Cypriana William alimtaka wakili wa utetezi Majura Magafu, aanze kumhoji shahidi.
Hata hivyo, Wakili Magafu alidai hawezi kumhoji shahidi huyo kwa sababu hana nyaraka za kibenki zilizotumiwa na Boniface, hivyo kuomba kesi iahirishwe hadi leo, ili upande wa serikali umpatie nyaraka hizo.

Hakimu William, ambaye ni Naibu Mwenyekiti wa Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi, pia anasaidiana na Naibu Msajili wa Mahakama Kuu, Phocus Bambikya na Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Saul Kinemela kuendesha kesi hiyo.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Alhamisi, Januari 29 mwaka 2009

SERIKALI YACHARUKA VIGOGO BOT KORTINI

MINARA PACHA

.Ni Liyumba na mwenzake Deogratius Kweka
.Wadaiwa kusababisha hasara ya bilioni 221/-
.Wakosa dhamana, wapelekwa rumande Keko
.Ulinzi mkali, makachero watanda Kisutu Dar

Na Happiness Katabazi

KWA mara nyingine, Serikali imeonyesha makucha yake kwa watumishi wa umma wanaotuhumiwa kutumia vibaya madaraka yao hivyo kuisababishia hasara ya mabilioni ya fedha.

Katika hatua hiyo, Serikali jana iliwafikisha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, aliyekuwa Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Amatus Liyumba na Meneja Mradi wa benki hiyo, Deogratius Kweka.

Watuhumiwa hao wanadaiwa kutumia vibaya fedha za umma kwa kuidhinisha ujenzi wa minara Pacha ya BoT maarufu kama ‘Twin Tower’.

Liyumba ambaye amestaafu kazi ya utumishi wa umma pamoja na mwenzake wamefunguliwa kesi hiyo ya jinai Na. 27 ya mwaka huu.

Wakili Kiongozi wa Serikali, John Wabuhanga aliyesaidiana na wakili Mwandamizi wa Serikali, Fredrick Manyanda na Tabu Mzee kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), alidai mbele ya Hakimu Mkazi, Hadija Msongo, kwamba watuhumiwa hao wanakabiliwa na mashtaka matatu.

Wakili Wabuhanga alidai kwamba shitaka la kwanza linamkabili mshitakiwa wa kwanza ambalo ni matumizi mabaya ya ofisi ya umma kwamba kati ya mwaka 2001-2006 akiwa mwajiri wa serikali aliidhinisha ujenzi wa minara pacha bila baraka za uongozi wa juu wa benki hiyo.

Shitaka la pili, ambako alisema pia linamkabili mshitakiwa wa kwanza peke yake ambalo ni kuidhinisha malipo ya ujenzi huo bila kibali cha Bodi ya Wakurugenzi wa Benki Kuu.

Wabuhanga alidai kuwa shitaka la tatu ni kuisababishia serikali hasara ambalo shitaka hilo linawakabili washtakiwa wote, akidai kwamba kati ya mwaka 2001-2006, wakiwa ni watumishi wa umma, kwa makusudi au kwa kushindwa kuwa makini na kazi yao waliisababishia serikali hasara ya sh bilioni 221.

Hata hivyo washtakiwa wote ambao muda wote walikuwa wakijifuta jasho wakati wapo kizimbani walikana mashtaka hayo.

Akitoa masharti ya dhamana hakimu Msongo alisema ili mshitakiwa apate dhamana ni lazima kila mmoja awe na wadhamini wa wawili wa kuaminika ambao watasaini bondi au kuwasilisha hati yenye thamani ya nusu ya kiasi wanachotuhumiwa kuisababishia serikali hasara.

Sharti jingine ni washtakiwa kuacha hati za kusafiria mahakamani na kila Ijumaa watahitajika kuripoti ofisi za Takukuru na kutotoka nje ya Dar es Salaam bila ya kibari cha korti.

Nusu ya kiwango wanachodaiwa kuisababishia serikali ni sh bilioni 110 hivyo kila mmoja wao atapaswa kusaini bondi au kuwasilisha hati yenye thamani ya sh bilioni 50.

Sekunde chache baada ya hakimu Msongo kutoa masharti hayo ndugu na jamaa wa washtakiwa hao waliokuwa wameketi viti vya nyuma kufuatilia shauri hilo, walitoka kwenye viti hivyo kimya kimya na kwenda kwenye benchi walilokuwa wameketi mawakili wa utetezi na kuwakabidhi hati za mali kama njugu ili zitumike kuwadhamini washitakiwa.

Mawakili wa utetezi Alexander Kyaruzi na Osca Msechu waliomba mahakama hiyo wateja wao kudhaminiwa kwa hati za nyumba zenye zaidi ya thamani ya sh milioni 600 na kuongeza hati hizo wamekuja nazo mahakamani hapo.

Kutokana na hali hiyo, Wakili Mwandamizi wa Serikali, Fredrick Manyanda, alisimama haraka na kuiomba mahakama kutokubali ombi hilo kwa sababu upande serikali unahitaji kupata muda wa kukagua kwa umakini vielelezo hivyo kama ni za kweli au la.

“Mheshimiwa hakimu tunaomba hati hizo zisitumike leo kuwadhamini washtakiwa kwani sisi upande wa serikali tunaitaji kupata muda wa kuzipitia kwa kina hati hizo zinataka kutumika kuwadhamini washtakiwa ili tujue ni za kweli au la,” alisema Manyanda.

Hakimu Msongo, alikubalina na ombi la Manyanda na kutoa amri kwamba washtakiwa kwenda rumande huku wakisubiri upande wa serikali ukamilishe kazi ya kuzikagua hati hizo.

Hakimu huyo aliahirisha kesi hiyo hadi Februari 10, mwaka huu, kwa ajili ya kutajwa kwa mara ya pili.

Awali, watuhumiwa hao walifikishwa mahakamani hapo saa nne asubuhi na maofisa wa Takukuru, kabla ya kupanda kizimbani saa nane mchana katika ukumbi namba mbili wa korti hiyo huku wote wawili wakiwa wamebeba maji ya kunywa aina ya Kilimanjaro.

Kwa wakati wote wakiwa wameketi kwenye gari hilo nje ya mahakama kabla ya kupanda kizimbani, makachero wa Takukuru walikuwa wameimarisha ulinzi mkali katika eneo ambalo gari hilo limeegeshwa.

Tanzania Daima Jumatano, lililokuwepo mahakamani hapo hadi saa tisa na nusu alasiri, liliwashuhudia watuhumiwa hao wakipelekwa katika Mahabusu ya Keko, chini ya ulinzi mkali wa makachero wa polisi na Takukuru.

Kufikishwa kwa watuhumiwa hawa jana mahakamani kuna kumetokana kwa kelele nyingi zilizopigwa na makundi mbalimbali ya wananchi vikiwemo vyama vya upinzani vilivyoongozwa na Mbunge wa Karatu (Chadema), Dk.Willbroad Slaa na vyombo vya habari kwamba ujenzi wa minara hiyo una wingi la ufisadi kwani gharama zilizotumika kujenga ni kubwa ikingalishwa na gharama halisi.

Hata hivyo, kwa mujibu wa taarifa ya ukaguzi wa Benki Kuu ya mwaka 2005, zilionyesha kwamba ujenzi wa Benki hiyo utagharimu sh bilioni 500.

Hii ni mara nyingine kwa vigogo wanaotuhumiwa kutumia vibaya madaraka kufikishwa kortini kwani mwishoni mwa mwaka jana, Serikali iliwafikisha mahakamani waliokuwa Mawaziri waandamizi wa awamu ya tatu ya uongozi wa nchi hii, Basil Mramba (Fedha) na Daniel Yona (Nishati na Madini) pamoja na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Gray Mgonja kwa kuisababishia Serikali hasara sh bilioni 11.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumatano, Januari 28 mwaka 2009

BRELA YAMKAANGA MARANDA

Na Happiness Katabazi

SHAHIDI wa kwanza katika kesi ya wizi ya bilioni 1.8 wa Fedha za Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) kupitia Benki Kuu (BoT), Afisa Mtendaji Mkuu wa (BRELA) Esteriano Mahingila, ameikana kampuni ya Kiloloma&Brothers inadaiwa kuchota kiasi hicho cha fedha kuwa haijawahi kusajiliwa na ofisi yake.

Washtakiwa katika kesi hiyo ya jinai namba 1163 ya mwaka jana Farijara Hussein na kada wa CCM, Rajab Shaban Maranda , ambao kwa mujibu wa jarada la kampuni ya Kiloloma&Brothers wao ni wakurugenzi ambao pia wanaruhusiwa kuchukua fedha kwenye akaunti ya kampuni hiyo ambayo inadaiwa kuwa bandia .

Mahingira ambaye alikuwa akiongozwa na Wakili Kiongozi wa Serikali, Stanslaus Boniface aliambia mahakama kwamba ofisi yake inaitambua kampuni iitwayo Kiloloma Bros enterprises ambayo Mkurugenzi wake alikuwa akiitwa Charles Isaack Kissa kabla ya mkurugenzi huyo kubadilisha jina na kuitwa Chares Isaack Kissa.

Alisema kwa mujibu wa jalada kampuni ya Kiloloma Bros Enterprises ambayo BRELA inalo, namba yake ya usajili ni 151025 na ilitolewa na ofisi yake April 4 mwaka 2005.

Alibainisha kuwa ofisi hiyo ilionyesha kuwa ingefanya biashara ya kuuza vifaa vya maofisini (stestionaries) na ofisi hiyo ipo nyumba namba 7 mtaa wa Iramba Magomeni jijini.

Katika jalada linaloonyesha kampuni ya Kililoma&Brothers lilitolewa mahakamani hapo na wakili wa serikali Boniface, linaonyesha kwamba namba ya usajili wa kampuni hiyo inafanana na namba ya usajili ya Kiloloma Bros Enterprises, tarehe na anwani ya kampuni hiyo ya Kilolomo Bros pia zinafanana na Kilolomo&Brothers .

Maelezo hayo ambayo yalikuwa yakisomwa na Boniface yalisababisha wananchi walikuwa wakifuatilia kesi hiyo ambayo jana ilianza kusikilizwa kwa mara ya kwanza kushikwa na butwaa.

Katika kesi hiyo inaongozwa na jopo mahakimu wakazi Naibu Mwenyekiti wa Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi,Cypriana William akisaidiana na Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ,Phocus Bambikya pamoja na Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Saul Kinemela.

Mahingira aliieleza mahakama kuwa licha ya tarehe, namba za usajili, ofisi za kampuni hiyo kufanana katika hati mbili za usajili wa kampuni hiyo Brella haijawahi kuisajili kampuni ya Kiloloma&Brothers ambayo ndiyo inayodaiwa mahakamani hapo kuchota sh 1,864,949,294.45 mali ya BOT.

“Kwa kifupi Kiloloma&Brothers ofisi yangu haijawahi kuisajili na wala haipo kwenye orodha ya makampuni ambayo tumewahi kuyasajili, hatuwezi kutoa namba moja ya usajili wa kampuni mbili” alisema Mahingira

Aliongeza kuwa kutoa namba mbili ni kosa la jinai chini ya Sheria ya Sheria za Biashara Na.25 ya mwaka 1975”

Ifuatayo ni sehemu ya mahojiano kati ya wakili Kiongozi wa Serikali Boniface na Shaidi:

Wakili: Ieleze mahakama shughuli yako kubwa pale BRELA ni nini?

Shahidi:Kusimamia shughuli za utawala, pia kushughulika na uchambuzi na kukubali au kukataa maombi ya kuanzisha kampuni na kuweka saini kwenye hati ya kampuni zinazoanzishwa.

Wakili:Usajili wa makampuni unaanzaje?

Shahidi:Mwombaji anaza kujaza fomu ya kusajili jina la kampuni na fomu hiyo inaonyesha anwani ya makazi,jina la biashara anayotaka kuifanya,majina au jina la mmiliki wa kampuni hiyo, uraia wa mwombaji, na katika fomu hiyo kuna kipengele kinachoonyesha kama mwombaji huyo alishawahi kusajili kampuni kwa jina kama hilo na tarehe ya kuaza biashara.

Wakili:Akishajaza hiyo fomu nini kinafuata?

Shahidi:Mwombaji anapaswa kuileta ofisini kwetu na atamkabidhi ofisi ya msajili ambayo atamweleza kiasi cha malipo kisha anaenda kulipa kwa mhasibu.

Wakili:Kisha mhasibu anafanyaje?

Shahidi:Mhasibu anagonga mhuri unaoonyesha terehe ya kulipiwa hiyo fomu kisha anampatia risiti.

Wakili:Mahakama inataka kufahamu Kiloloma Bros kama unaifahamu?

Shahidi:Naifahamu

Wakili:Lini ulianza kuifahamu?

Shahidi:Kwakweli nilianza kuifahamu pale tatizo la EPA liliposhika kasi kwamba kampuni hiyo ilishiriki kuchota fedha za EPA.

Wakili:Huna namna nyingine ya kuitambua kampuni hiyo?

Shahidi:Kwakweli sina namna nyingine ninayoitambua kwani pale ofisini makampuni ni mengi.

Wakili:Unalitambua jalada ya kampuni ya Kiloloma Bros?

Shahidi:Ndiyo nalitambua vyema kwani lina saini yangu ikiwemo namba ya usajili ya kampuni namba 151025 na nyaraka zingine zilizopo ndani ya jalada hili zina saini yangu na itoshe kusema kwamba kampuni hii ilisajiliwa kihalali na kampuni yangu.

Wakili:Soma kwa nguvu kwa sauti, kichwa cha habari kwenye hilo jarada kimeandikwaje?

Shahidi:Registor Of Bussines Name.

Wakili:Ungependa kulitoa jalada hilo lipokelewe na mahakama hii kama kidhibiti?

Shahidi:Ndiyo.

Jopo lilipokelewa kama kidhibiti namba moja.

Wakili:Jina la Biashara linaitwaje?

Shahidi:Kiloloma Bros.

Wakili:Nini kazi ya kampuni hiyo?

Shahidi:Office Equipment and Stationers.

Wakili:Nani hasa alikuwa mwombaji wa kusajiliwa kampuni hiyo?

Shahidi:Chalres Isaack Kissa kabla ya kubadilisha jina na kuitwa Chares Isack Kissa.

Wakili:Alikuwa ni raia wa Tanzania?

Shahidi:Ndiyo.

Wakili:Alilipa shilingi ngapi kama ada ya usajili?

Shahidi:Elfu sita.

Wakili:Katika maombi yake alionyesha biashara yake hiyo ataifanyia wapi?

Shahidi:Nyumba namba 7, Magomeni Mtaa wa Iramba.

Wakili:Hati ya Usajili namba 151025 ilitolewa na nani?

Shahidi:Mimi.

Wakili:Search report ilikuja lini ofisini kwenu?

Shahidi:Januari 11 mwaka 2008, kuna mtu alikuja pale ofisini na kutaka ufanyike upekuzi wa kampuni ya Kiloloma Bros na hati hiyo inaonyesha hakuna jina linalofanana na kampuni hiyo.

Wakili:Katika kambukumbu zako , kuna mabadiliko yaliyoombwa au kutolewa na kampuni hiyo?

Shahidi:Hakuna ombi la kufanyika kwa mabadiliko kupokelewa au kukataliwa na BRELA.

Wakili:Kuna jina la Biashara linaitwa Kiloloma&Brother Enterprises unaifahamu?

Shahidi:Si ifahamu.

Wakili:Hiyo Namba ya hati ya usajili 151025 iliyotolewa April 14 mwaka 2005, hiyo hati imesainiwa na nani?

Shahidi:Saini hii inataka kufanana na yangu lakini siyo yangu.

Wakili:Nani wanaonyesha ni wamiliki wa kampuni hiyo?

Shahidi:Ni Farijara Hussein na Rajab Shaban Maranda ndiyo wamilimiki wa Kiloloma &Brother Entreprises.

Wakili:Inaonyesha biashara wanafanyia wapi?

Shahidi:Nyumba namba 7 Mtaa wa Iramba-Magomeni.

Wakili:Nani wanaonyesha ni wamiliki ya akaunti ya Kiloloma &Brothers Enterprises?

Shahidi:Farija na Maranda.

Wakili:Angalia kwa makini hayo majalada ya makampuni hayo mawili yanaonyesha yamesajiliwa siku na terehe tofauti?

Shahidi:Inaonyesha zimesajiliwa siku na tarehe moja.
Wakili:Katika taratibu za ofisi yenu mnaweza kusajili makampuni mawili kwa namba moja?

Shahidi:Hairuhusiwi hata kidogo.

Wakili:Angalia kidhibiti namba namba moja na kidhibiti namba mbili(majarada) yanaonyesha sehemu gani ofisi hizo zilipo?

Wakili:Inaonyesha pia kampuni ya Kilolomo&Brother inafanya shughuli zake katika nyumba namba 7 mtaa wa Iramba –Magomeni.

Baada ya wakili wa serikali kumaliza kumhoji shahidi, hakimu William alimtaka wakili wa utetezi Majura Magafu aanze kumuuliza maswali shahidi huyo, lakini hata hivyo Magafu alionyesha kushitushwa na hali hiyo na kusema kwamba hawezi kuuliza maswali kwa wakati huo hadi azungumze na wateja wake na kuomba shauri hilo liahirishwe kwa muda ili aweze kuzungumza na wateja wake.

Ombi ambalo lilikubaliwa na jopo hilo ambapo ilipofika saa 6:15 lilirejea mahakamani hapo na Magafu kuanza kumuuliza maswali shahidi huyo ambapo hata hivyo shahidi huyo alikuwa akiyapangua maswali Magafu kwa umakini na kujiamini.

Jopo hilo liliarisha kesi hiyo hadi leo ambapo shahidi wa pili ataanza kutoa ushaidi wake.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumatano, Januari 28 mwaka 2009

MBATIA UPO SAHIHI,TUUNDE TUME

Na Happiness Katabazi

TAIFA linapoingia kwenye giza la ufisadi, inawezekana watu wakaamini kwamba kila mtu ndani ya taifa hilo ni fisadi.Kwa kufananisha na msemo ule ule kuwa “Samaki mmoja akioza basi wote wameoza ndani ya tenga”.

Ukitafakari kwa kina msemo huu utapingana nao kwani si rahisi samaki mmoja akioza ndani ya tenga basi wote wawe wameoza.

Nimelazimika kutumia msemo huu kwa kuwa ninataka kuangalia upande wa pili wa shilingi, hasa tunapoangalia mafisadi waliopo ndani ya nchi.

Nchi inapokuwa na mafisadi haimaanishi basi watu wote waliopo ndani ni mafisadi, kwani ufisadi ni uovu na ushetani.

Tunajua, raia wengi ni watu wema wanaoamka asubuhi kwenda kwenye shughuli zao halali bila kufanya ufisadi.

Lakini ufisadi unapofikia viwango vya kutumia vyombo vya dola na taasisi za umma, basi ufisadi huo ni mkubwa kupindukia na unaitwa ufisadi kabambe, kwa Kiingereza (grand corruption).

Sasa mbinu za kupambana na ufisadi wa aina hii huwa hazipo katika sheria za nchi, kwa kuwa baadhi ya sheria za nchi hutumika kuufanikisha ufisadi kabambe.

Mfano, ufisadi kabambe unaotumiwa na vyombo vya dola unaanzia kwenye sera ambazo zinaongoza serikali katika utendaji wake wa kila siku.

Sera ikishabuniwa, hata ikiwa potofu, ikatungiwa sheria na ikapitishwa na Bunge, ambalo ndilo chombo kilichopewa jukumu la kutunga na kusimamia sheria, huwa ni halali.

Kwa hiyo ukichukua sera ya kuuza nyumba za serikali kuwa ni wazo potofu lililoingia kwenye vichwa vya watawala wa nchi hii, basi wazo hilo lilipokubaliwa na dola, limefanikishwa kisheria na watendaji wa serikali wakauziwa nyumba za serikali.

Sera haijali nani amenunua nyumba hizo, lakini ukweli ni kwamba uuzaji wa nyumba za serikali ni ufisadi.

Ni kitendo cha kulinyang’anya taifa rasilimali yake iliyokusudiwa kuwahifadhi watendaji wa serikali wanapokuwa kwenye ajira za umma.

Matokeo yake ni kwamba nyumba hizo huuzwa kwa bei hafifu, japo zina thamani kubwa, jambo ambalo ni wizi kwa kila anayenunua nyumba hizo.

Lakini wafanyakazi wa serikali wenye stahili ya kupata nyumba kama vile majaji wanajikuta wanapanga kwenye hoteli za kitalii kwa gharama kubwa zinazolipwa na serikali.

Mzigo huo wa kulipa gharama za watendaji hao anatwishwa mlalahoi ambaye kila kukicha anakamuliwa kwa kodi mbalimbali.

Huu ni mfano wa wazi wa serikali ovu. Je, wale wote wanaoguswa na sera hii ama kwa kutunga ama kwa kunufaika nayo tuwaiteje? Mafisadi au manyang’au?
Hapo ndipo ninapounga mkono wazo la Chama cha NCCR-Mageuzi lililotolewa na Mwenyekiti wake, James Mbatia, katika tamko la chama hicho Januari 11 mwaka huu, kwamba yapo mambo ya kifisadi ambayo ufumbuzi wake unahitaji Tume ya Ukweli na Maridhiano ‘Truth Commission’.
Tume hiyo iwe na watu wachache, wasafi, wasio na masilahi katika ufisadi husika, watakaopewa mamlaka na sheria ya kuchunguza ufisadi wa aina hii ambao umeelekezwa kwa kutumia dola na sheria zake.

Tume kama hiyo itakuwa na mamlaka ya kuwaita watuhumiwa ili waeleze ukweli na pia wasio tuhumiwa kuja mbele ya tume hiyo kuthibitisha ukweli na kisha kuainisha uovu uliotendeka na kuupatia ufumbuzi.

Wengine japo ni watuhumiwa watahitajika kukubali uovu wao japo kama walipotenda ulikuwa halali kisheria, wakishakiri, sheria iwape fursa ya kuomba msamaha kurejesha mali ya umma na pengine kufidiwa kama itaonekana inafaa.

Tuone jinsi tutakavyowafidia watendaji wetu wawili walioguswa na sera za uuzaji wa nyumba.
Mtu wa kwanza ni ofisa wa serikali aliyeomba kununua nyumba ya serikali na ikathaminishwa kuwa ina thamani labda ya sh milioni 50, ofisa huyo akakubali na kuinunua nyumba hiyo.

Mtu huyu anastahili kuombwa radhi katika tume hiyo kwamba ameuziwa nyumba kwa sera mbovu ambayo ni kinyume cha masilahi ya nchi.

Kwa hiyo yeye akubali kurejesha nyumba ile na akubali kupokea sh milioni 50 na kifuta jasho.
Kwa lugha nyingine, huyu si fisadi, huyu ni mhanga ‘victim’ wa sera ya kifisadi.

Lakini mfano, mtendaji wa pili wa serikali hapa tumchukulie katibu mkuu wa wizara anayechukua fedha za serikali sh milioni 600 kukarabati nyumba ya serikali anayoishi na kisha kujiuzia nyumba hiyo kwa sh milioni 50.

Huyu ni fisadi, tena dawa yake Tume ya Ukweli na Maridhiano ikishagundua ukweli huo ni kupeleka ukweli kwa Mkurugenzi wa Mashtaka ili aweze kumuandalia mashtaka na kumfikisha mahakamani ili ahumiwe kwa kosa la kuiba mali ya umma.

Na hilo ndilo pendekezo la Mbatia, licha ya baadhi ya watu kutokumuelewa vyema wakaishia kuibuka kwenye vyombo vya habari kumpinga.

Kwamba wapo watu itabidi wapelekwe mahakamani na sheria ya ufisadi itungwe kuhakikisha watu wa aina hii wanapata adhabu.

Sasa wanaompinga Mbatia ni kina nani? Na je, waliompinga walipata fursa ya kuisoma hotuba ya Mbatia kwa kina au waliamua kumkosoa bila kurejea hotuba yake aliyoitoa kwa maandishi?

Au waliamua kumkosoa baada ya baadhi ya magazeti kuripoti kwamba Mbatia anataka mafisadi wasamehewe?

Tujenge utamaduni wa kujenga hoja kwa vielelezo, hivyo mtu mwenye akili timamu anapotaka kumkosoa mtu kwanza ni lazima ajiridhishe na hoja anazotaka kuzitoa dhidi ya mtu huyo ili mwisho wa siku asionekane kichekesho mbele ya jamii.

Tanzania ni yetu sote na tuendelee na utamaduni wetu wa kukosoana kwa hoja na kupongezana panapostahili na si kukurupuka kama baadhi yetu wanavyofanya.

Tusipojirekebisha tutakuwa tukijenga taifa la wachochezi na majuha.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumatano la Januari 28 mwaka 2009

DITOPILE AAGA KEKO KWA VURUGU KORTINI

na Happiness Katabazi

MWANZO wa ngoma ni lele. Vurugu, kejeli na mbwembwe zisizo na msingi zilizoanza kufanywa na ndugu na jamaa wa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Ukiwaona Ditopile Mzuzuri na kupigiwa chapuo na vituko vyake mwenyewe, jana vilitawala eneo la Mahakama Kuu, wakati shauri la mauaji ya bila kukusudia lilipofikishwa hapo kwa ajili ya kusikilizwa kwa ombi la dhamana.

Ndugu na jamaa hao wa Ditopile ambaye amekuwa katika mahabusu ya Keko tangu Novemba mwaka jana, wakisaidiwa na polisi waliokuwa katika sare na mavazi ya kiraia, walianzisha vurumai kubwa kuwazuia wanahabari kumkaribia au kumpiga picha mwanasiasa huyo ambaye alipewa dhamana.

Vurugu hizo ambazo zilisababisha waandishi kadhaa kujeruhiwa na wengine kuharibikiwa vitendea kazi vyao, zikiwamo kamera, ziliambatana na kurushiana makonde na maneno kati ya wanahabari hao kwa upande mmoja na jamaa na ndugu wa Ditopile, waliokuwa wakisaidiwa na polisi.

Matukio hayo yaliyokwenda sambamba na kuwamwagia maji wanahabari na kutoa maneno ya kuidhalilisha serikali na hata viongozi wake wakuu, yalifanywa na baadhi ya ndugu na jamaa hao wa Ditopile waliothibitisha pasipo shaka kuwa walikuwa ni watu wasio na staha, walioshindwa kujiheshimu, wapungufu wa hekima, waliokosa subira na walioamua kwa makusudi kuidharau mahakama na taaluma ya habari.

Vurugu hizo zilianzia ndani ya jengo la mahakama majira ya saa 8:59 na kumalizikia nje ya geti la mahakama hiyo saa 9:50 alasiri, wakati Ditopile aliyekuwa katika ulinzi mkali huku akiwa amevaa kofia yake ya ‘pama’ akitoka nje ya jengo la Mahakama Kuu.

Wanahabari wa Tanzania Daima waliokuwapo eneo la Mahakama Kuu katika Barabara ya Kivukoni walikuwa miongoni mwa watu waliokumbwa na zahama hiyo ambayo ilisababisha Joseph Zablon, ambaye ni mpiga picha kujeruhiwa sehemu za mdomoni.

Kikubwa kilichoonekana kuwakera polisi, ndugu na jamaa za Ditopile ni wajibu wa kikazi wa wanahabari hao kufanya juhudi za kumfikia mwanasiasa huyo aliyekuwa amezingirwa kwa lengo la kumficha, huku yeye mwenyewe akiwa amejiinamia.

“Tokeni zenu, sisi ndio wenye nchi…siku zote nazi haishindani na jiwe ni lazima itapasuka. …ni mtu wa karibu sana na Dito ambaye ni ndugu yetu, mnafikiri atakubali rafiki yake asote muda wote, haiwezekani na ndiyo kaishapata dhamana, yupo huru na nyie ‘wambea’ endeleeni kuandika weeee! Hadi kalamu zenu ziishe wino…ndiyo hivyo, kaisharejea uraiani.

“Au hamna habari kwamba Ditopile alikuwa Best Man wa …na hadi sasa ni marafiki, na nyie waandishi wa habari kwa akili zenu zilivyo ndogo mnafikiri anapenda anavyokaa jela…duniani hakuna haki, haki ipo mbinguni, utawala huu ni kujuana na wakubwa, mambo yatakunyookea,” ni maneno yaliyokuwa yakitoka kinywani mwa mmoja wa watu waliokuwa wamejumuika katika kundi la ndugu na jamaa wa Ditopile.

Alipotoka katika eneo hilo, Ditopile aliingizwa katika gari dogo aina ya Toyota Ballon, lenye namba za usajili T723ADF, la rangi ya fedha, lililokuwa likisindikizwa na Land Rover (Defender) ya Polisi yenye namba za usajili, T212AMV.

Muda mfupi baadaye, polisi waliokuwa katika eneo hilo, waliwaeleza waandishi wa habari kuwa, msafara huo kwanza ulielekea Keko kuchukua vitu mbalimbali vya mwanasiasa huyo, kabla ya kwenda nyumbani kwake.

Baada ya msafara huo kuondoka saa 9:30, ndugu wa Ditopile na askari kanzu waliobaki mahakamani hapo waliendelea kutupiana makonde na waandishi wa habari huku ndugu hao wakiendelea kutoa lugha ya matusi na kumwaga maji kwenye kamera za wapiga picha ili ziharibike.

Sekunde chache, hali ilibadilika baada ya mamia ya raia ambao waliungana na waandishi wa habari kuwafokea askari ambao awali walikuwa wakisaidia kumficha Ditopile asipigwe picha na kuwazuia waandishi wasimfikie.

“Polisi gani nyie, mnafanya kazi kwa kujipendekeza badala ya kulinda usalama wa raia na kutuliza ghasia lakini nyie ndio mmekuwa chanzo cha vurugu…na kwa taarifa yenu, kwa picha hii mliyoionyesha hapa tumeamini kabisa hapa hakuna kesi,” alisikika akisema mwananchi mmoja aliyekuwa mahakamani hapo na akajitambulisha kwa jina la Dk. Hassan Zubeir.

Miongoni mwa wanahabari waliopata athari kutokana na vurugu hizo ni mpiga picha wa magazeti ya Majira, Business Times na Spoti Starehe, Patrick Spear, ambaye mbali ya kamera yake kuharibiwa alichaniwa vifungo vya shati lake.

“Vurugu hizi zinazofanywa na ndugu wa mtuhumiwa kila kukicha, tena mahakamani, zinaipaka matope serikali na Jeshi la Polisi, na serikali ikae ikijua tayari wananchi wengi wana wasiwasi wa haki kutendeka…haiwezekani hawa ndugu kila kukicha wanafanya vurugu mahakamani na hawachukuliwi hatua,” alisema Mpiga Picha Mkuu wa gazeti la TheCitizen, Mpoki Bukuku.

Awali kabla ya vurugu hizo, Ditopile alipandishwa kizimbani saa 5:20 asubuhi akiwa chini ya ulinzi mkali, huku mahakama ikiwa imefurika mamia ya wananchi waliokuwa na shauku ya kujua kulikoni.

Mmoja wa mawakili wa Ditopile, Profesa Jwani Mwaikusa, aliiomba mahakama impatie dhamana mteja wake kwa kuwa shitaka linalomkabili linadhaminika na kwamba mteja wake ni mtu anayejiheshimu na kuaminika mbele ya jamii, hivyo hawezi kuruka dhamana.

Upande wa Mwanasheria wa Serikali, ulidai mahakamani hapo kuwa haukuwa na pingamizi kuhusu ombi hilo, kwa kuwa dhamana ni haki ya kila mtu.

Baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili na kuzichambua, Jaji Augustine Mwarija, alitoa dhamana kwa masharti ya bondi ya sh milioni 60. Mshitakiwa alitakiwa kutoa bondi ya sh milioni 20 na wadhamini wawili ambao kila mmoja wao alitakiwa kutoa bondi ya sh milioni 20 kila mmoja.

Mtuhumiwa alitakiwa kukabidhi hati yake ya kusafiria polisi na akatakiwa kutotoka nje ya Dar es Salaam bila ruhusa ya polisi, na akatakiwa pia awe akiripoti kwa Kamanda wa Upelelezi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam.

Ditopile aliletwa mahakamani hapo saa 2:54 asubuhi na msafara wa polisi na akapitishwa kwenye mlango unaotumiwa na majaji.

Muda mfupi baada ya majaji na viongozi wa mahakama hiyo kubaini mchezo huo, waliwafokea polisi hadharani na kusema kitendo hicho kimefanywa kinyume cha taratibu za mahakama.

Naye Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Philophr Lyimo, alikiri kutokea kwa tukio hilo na akasema mahakama hiyo imekerwa na tabia ya polisi hao na kuongeza kuwa, tayari ameshawasiliana na Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Alfred Tibaigana, ili aweze kuwachukulia hatua askari wake.

“Ule mlango unatumiwa na majaji, hata sisi tumeshindwa kuelewa ni kwa nini wamempitisha katika mlango ule na huku Ditopile ni mtuhumiwa kama mtuhumiwa mwingine….siyo siri tumekerwa na tumeshawaambia kabla ya saa sita leo mchana (jana) wajieleze.

“Hii ni mahakama na watu wanakuja kutafuta haki hapa. Sasa polisi wanapofanya mambo kama haya ambayo nasema yana lengo la kuichafua mahakama yetu, hatuwezi kuyavumilia. Ni lazima wachukuliwe hatua,” alisema Lyimo.

Chanzo:Gazeti la Tanzania la Ijumaa Septemba 2 mwaka 2007
;::Sitaisahau vurugu hizi kwani zimeweka historia mbaya katika mahakama ya Tanzania

KINARA WA RICHMOND KORTINI

Na Happiness Katabazi

HATIMAYE, serikali jana imemfikisha mahakamani mtu anayetajwa kuwa kinara wa kashfa ya Richmond.

Mtuhumiwa huyo, Naeema Adam Gile, alipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, kwa tuhuma za kughushi na kutoa taarifa za uongo kwa watumishi wa serikali.

Gile, alifikishwa mahakamani hapo kimya kimya saa 8:05 mchana, na kusababisha waandishi wa habari wanaoripoti habari za mahakamani kushindwa kujua kinachoendelea huku wengine wakiwa wakimekwisha kuondoka.

Wakili Kiongozi wa Serikali, Stanslaus Boniface, aliyekuwa akisaidiana na Wakili Mwandamizi wa Serikali, Frederick Manyanda, alidai mbele ya Hakimu Waliarwande Lema kwamba, mshitakiwa huyo anakabiliwa na mashtaka matano ambayo aliyatenda kwa nyakati tofauti.

Wakili Boniface alidai kuwa, Machi 13, 2006, jijini Dar es Salaam, mshitakiwa akiwa na dhamira ya kutenda kosa, alighushi hati ya nguvu ya kisheria (power of attorney) inayoonyesha imetolewa na Hamed Gile, ambaye ni Mwenyekiti wa Kampuni ya Richmond LLC ya Texas, Marekani, kwamba amemruhusu kufanya shughuli za kampuni hiyo hapa nchini.

Wakiri Boniface alidai kwamba, shitaka la pili ni kutoa taarifa za uongo, kuwa Machi 20 mwaka 2006, katika eneo la Ubungo, Umeme Park, Barabara ya Morogoro, mshitakiwa alitoa hati hiyo ya nguvu ya kisheria inayomuidhinisha yeye kwamba ameruhusiwa kufanya kazi ya kampuni hiyo ya Marekani hapa nchini.

Aliendelea kudai kuwa, shitaka la tatu linalomkabiri mtuhumiwa huyo ni kutoa taarifa za uongo kwa watumishi wa umma na kwamba Julai 20, 2004 eneo la Ubungo Umeme Park, alitoa taarifa ya uongo kwa wajumbe wa Bodi ya Zabuni ya Shirika la Umeme (TANESCO). Kwamba Richmond LLC ya Texas, Marekani, ina uwezo wa kuzalisha umeme wa megawati 100 kwa Tanzania ili wajumbe wa bodi hiyo waweze kumpendekeza kupewa tenda ya kutoa huduma hiyo.

Katika shitaka la nne, alidai Juni, 2006 jijini Dar es Salaam, mshitakiwa alitoa taarifa za uongo kwa wajumbe wa timu ya majadiliano ya serikali, kuwa Kampuni ya Richmond LLC ya Texas, Marekani, ina uwezo wa kuzalisha umeme kwa kiwango hicho ili apewe tenda hiyo.

Wakili Boniface ambaye amejizolea sifa tangu kuanza kufikishwa mahakamani kwa watuhumiwa wa kesi za wizi wa fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) alidai shitaka la tano la mshitakiwa huyo ni la Julai, 2006, ambapo mshitakiwa akifahamu na kwa ulaghai, alitoa hati ya nguvu ya kisheria iliyotolewa Machi 3, mwaka huo iliyokuwa ikimuonyesha kuwa ameruhusiwa na Mwenyekiti wa Kampuni, Hemed Gile, kufanya kazi za kampuni hiyo hapa nchini.

Hata hivyo, mshitakiwa alikana mashtaka yote na upande wa serikali ulisema upelelezi bado haujakamilika na kwamba hauna pingamizi na dhamana.

Wakili wa kujitegemea, Kato Zake, anayemtetea mshtakiwa, aliiomba mahakama impatie dhamana mteja wake kwa sababu afya yake si nzuri na anatarajiwa kwenda nje ya nchi kwa ajili ya matibabu.

Hata hivyo habari zilizopatikana mahakamani hapo zilieleza kuwa hati ya kusafiria ya mshitakiwa inashikiliwa na polisi. Hakimu Lema alisema uamuzi wa kumpatia dhamana mshtakiwa atautoa leo na aliamuru mshitakiwa apelekwe rumande.

Wakati huo huo, waandishi wa habari wanaoripoti habari za mahakamani jana walionekana kukerwa na hatua ya Hakimu Lema kuendesha kesi hiyo kwenye ‘chamber’ wakati mahakama za wazi mahakamani hapo zilikuwa wazi.

Waandishi hao walieleza kuwa hatua hiyo ya Hakimu Lema, iliwapa wakati mgumu kusikiliza mwenendo wa shauri hilo.

Gile amefikishwa mahakamani ikiwa ni takriban mwaka mmoja sasa baada ya aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa, aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi na mwenzake aliyekuwa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Ibrahim Msabaha, walilazimika kujiuzulu nyadhifa zao kwa kashfa hiyo ya Kampuni ya Richmond.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumatano, Januari 15 mwaka 2009

KINARA WA RICHMOND KORTIN

Na Happiness Katabazi

HATIMAYE, serikali jana imemfikisha mahakamani mtu anayetajwa kuwa kinara wa kashfa ya Richmond.

Mtuhumiwa huyo, Naeema Adam Gile, alipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, kwa tuhuma za kughushi na kutoa taarifa za uongo kwa watumishi wa serikali.

Gile, alifikishwa mahakamani hapo kimya kimya saa 8:05 mchana, na kusababisha waandishi wa habari wanaoripoti habari za mahakamani kushindwa kujua kinachoendelea huku wengine wakiwa wakimekwisha kuondoka.

Wakili Kiongozi wa Serikali, Stanslaus Boniface, aliyekuwa akisaidiana na Wakili Mwandamizi wa Serikali, Frederick Manyanda, alidai mbele ya Hakimu Waliarwande Lema kwamba, mshitakiwa huyo anakabiliwa na mashtaka matano ambayo aliyatenda kwa nyakati tofauti.

Wakili Boniface alidai kuwa, Machi 13, 2006, jijini Dar es Salaam, mshitakiwa akiwa na dhamira ya kutenda kosa, alighushi hati ya nguvu ya kisheria (power of attorney) inayoonyesha imetolewa na Hamed Gile, ambaye ni Mwenyekiti wa Kampuni ya Richmond LLC ya Texas, Marekani, kwamba amemruhusu kufanya shughuli za kampuni hiyo hapa nchini.

Wakiri Boniface alidai kwamba, shitaka la pili ni kutoa taarifa za uongo, kuwa Machi 20 mwaka 2006, katika eneo la Ubungo, Umeme Park, Barabara ya Morogoro, mshitakiwa alitoa hati hiyo ya nguvu ya kisheria inayomuidhinisha yeye kwamba ameruhusiwa kufanya kazi ya kampuni hiyo ya Marekani hapa nchini.

Aliendelea kudai kuwa, shitaka la tatu linalomkabiri mtuhumiwa huyo ni kutoa taarifa za uongo kwa watumishi wa umma na kwamba Julai 20, 2004 eneo la Ubungo Umeme Park, alitoa taarifa ya uongo kwa wajumbe wa Bodi ya Zabuni ya Shirika la Umeme (TANESCO). Kwamba Richmond LLC ya Texas, Marekani, ina uwezo wa kuzalisha umeme wa megawati 100 kwa Tanzania ili wajumbe wa bodi hiyo waweze kumpendekeza kupewa tenda ya kutoa huduma hiyo.

Katika shitaka la nne, alidai Juni, 2006 jijini Dar es Salaam, mshitakiwa alitoa taarifa za uongo kwa wajumbe wa timu ya majadiliano ya serikali, kuwa Kampuni ya Richmond LLC ya Texas, Marekani, ina uwezo wa kuzalisha umeme kwa kiwango hicho ili apewe tenda hiyo.

Wakili Boniface ambaye amejizolea sifa tangu kuanza kufikishwa mahakamani kwa watuhumiwa wa kesi za wizi wa fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) alidai shitaka la tano la mshitakiwa huyo ni la Julai, 2006, ambapo mshitakiwa akifahamu na kwa ulaghai, alitoa hati ya nguvu ya kisheria iliyotolewa Machi 3, mwaka huo iliyokuwa ikimuonyesha kuwa ameruhusiwa na Mwenyekiti wa Kampuni, Hemed Gile, kufanya kazi za kampuni hiyo hapa nchini.

Hata hivyo, mshitakiwa alikana mashtaka yote na upande wa serikali ulisema upelelezi bado haujakamilika na kwamba hauna pingamizi na dhamana.

Wakili wa kujitegemea, Kato Zake, anayemtetea mshtakiwa, aliiomba mahakama impatie dhamana mteja wake kwa sababu afya yake si nzuri na anatarajiwa kwenda nje ya nchi kwa ajili ya matibabu.

Hata hivyo habari zilizopatikana mahakamani hapo zilieleza kuwa hati ya kusafiria ya mshitakiwa inashikiliwa na polisi. Hakimu Lema alisema uamuzi wa kumpatia dhamana mshtakiwa atautoa leo na aliamuru mshitakiwa apelekwe rumande.

Wakati huo huo, waandishi wa habari wanaoripoti habari za mahakamani jana walionekana kukerwa na hatua ya Hakimu Lema kuendesha kesi hiyo kwenye ‘chamber’ wakati mahakama za wazi mahakamani hapo zilikuwa wazi.

Waandishi hao walieleza kuwa hatua hiyo ya Hakimu Lema, iliwapa wakati mgumu kusikiliza mwenendo wa shauri hilo.

Gile amefikishwa mahakamani ikiwa ni takriban mwaka mmoja sasa baada ya aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa, aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi na mwenzake aliyekuwa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Ibrahim Msabaha, walilazimika kujiuzulu nyadhifa zao kwa kashfa hiyo ya Kampuni ya Richmond.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumatano, Januari 15 mwaka 2009


SHAHIDI BRELA ATOBOA SIRI

Na Happiness Katabazi

SHAHIDI wa pili katika kesi ya wizi wa sh milioni 207 katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) mali ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Naibu Msajili wa Brela, Andrew Mkapa, ameiambia mahakama kuwa ofisi yake iligundua Kampuni ya Rashhaz (T) Ltd haikuwasilisha ripoti ya marejesho ya kila mwaka baada ya vyombo vya habari kulivalia njuga sakata la EPA.

Akitoa ushahidi huo mbele ya Hakimu Mkuu Mfawidhi, Addy Lyamuya, shahidi huyo alidai licha ya ofisi yake kuisajili kampuni hiyo, haijawahi kupitia faili la kampuni hiyo kuona kama ilikuwa ikiwasilisha ripoti ya mahesabu ya kila mwaka (Annual Report).

“Tuligundua kampuni hii haijawasilisha ripoti hiyo baada ya vyombo vya habari kulivalia njuga sakata la EPA, ndipo tuliitisha majalada ya makampuni yote, ili tuweze kuyapitia, lakini kabla hatujafikia kulikagua jalada la kampuni ya Rashhaz (T) Ltd, DPP na Takukuru walifika ofisini na kuondoka na baadhi ya majalada likiwemo jalada la kampuni hiyo,” alieleza shahidi huyo.

Ifuatayo ni sehemu ya mahojiano kati ya wakili Majura Magafu na Mkapa:

Wakili: Katika ushahidi ulioutoa jana(juzi) ulisema kampuni hiyo ilisajiliwa kihalali?
Shahidi: Ndiyo
Wakili: Ulisema miongoni mwa mahusiano kati ya Brela na makampuni baada ya kusajiliwa ni kampuni husika kuwasilisha Annual Report?
Shahidi: Ni kweli
Wakili: Kwa mujibu wa sheria za ofisi yenu Annual Return zinatokana na nini?
Shahidi: Inatokana taarifa za kampuni na zinapaswa kuambatana na vitu vitatu kwanza kuna fomu ya kujaza Annual Return, jina la kampuni, mahali ilipo ofisi, wahusika na anwani ya posta, fomu hiyo inapaswa kuambatanishwa na taarifa ya Mkaguzi wa Mahesabu na taarifa ya hasara na faida iliyopata kampuni kwa mwaka.
Wakili: Katika ushahidi wako uliieleza mahakama kwamba kampuni hiyo haijawahi kuwasilisha Annual Return tangu iliposajiliwa Septemba 12 mwaka 2003 . Je ni utaratibu gani unachukuliwa na Brela wakati kampuni inaposhindwa kuwasilisha taarifa hiyo?
Shahidi: Msajili anapogundua hilo, kwamba kampuni imefanya hivyo anaiandikia barua ya kuwakumbusha ni kwa nini hawawasilishi Annual Return.
Wakili: Kwa mujibu wa kumbukumbu zenu lini mligundua kampuni ya Rashhaz haijawasilisha hiyo ripoti?
Shahidi: Tuligundua pale kizaazaa cha EPA kilipopamba moto kwenye vyombo vya habari na ndipo maofisa wa ofisi yetu waliitisha majalada ya makampuni kwa ajili ya kuanza kuyakagua.
Wakili: Ilikuwa lini?
Shahidi: Novemba mwaka 2007
Wakili: Huoni kwamba Brela hampo makini na kazi yenu?
Shahidi: Tatizo ofisi yetu inatumia muundo wa zamani wa kuhifadhi mafaili badala ya kutumia teknolojia ya kompyuta, hivyo inatuwia vigumu kupitia mafaili yote kwa wakati mmoja kwa sababu mafaili ni mengi mno, lakini pia hiyo tutaichukulia kama ni changamoto kwetu.
Wakili: Mliwaandikia barua wakurugenzi wa kampuni hiyo, ili waweze kuwasilisha Annual Return?
Shahidi: Hatukuweza kuwaandikia kwa sababu hayo majalada ambayo tulipanga tuanze kuyakagua yaliitishwa haraka na DPP, Eliezer Feleshi na Takukuru.
Wakili: Je, DPP na Takukuru wameisharudisha majalada hayo Brela?
Shahidi: Hadi leo ninavyotoa ushahidi bado hayajarudishwa.
Wakili: Hivi kampuni isiyoleta ripoti ya marejesho ya kila mwaka, Brela mnaichukulia imetenda kosa lipi kisheria?
Shahidi: Tunachukulia ni kosa la jinai linaloweza kumfikisha mhusika mahakamani.
Wakili: Je, hilo kosa la jinai limeainishwa kwenye Sheria ya Kanuni ya Adhabu au sheria ya makampuni?
Shahidi: Kosa hilo limeainishwa kwenye sheria ya makampuni.
Wakili: Ni adhabu zipi zimeanishwa kwa mtu anapokuwa na hatia?
Shahidi: Faini kwenye hiyo sheria ili mhusika akileta hiyo ripoti anapigwa penati.
Wakili: Kwa unavyoelewa kampuni hiyo imeshawahi kuburuzwa mahakamani?
Shahidi: Hapana.
Wakili: Unakubaliana na mimi kwamba kampuni hiyo ni halali?
Shahidi: Ndiyo, lakini ni kampuni iliyolala.
Wakili: Katika madhumini 27 yaliyoainisha makubaliano ya awali kati ya kampuni hiyo na ofisi yenu; kuna madhumuni yanayoonyesha kuwa kampuni hiyo itakuwa na jukumu la kukusanya madeni?
Shaihidi: Kweli, yameainisha.
Wakili: Katika makubaliano hayo ya awali hakuna kifungu kilichoonyesha kampuni hiyo inaweza kuingia mkataba na serikali au kampuni yoyote?
Shahidi: Kuna kipengele kinaonyesha kampuni hiyo inaruhusiwa kukusanya madeni.

Baada ya shahidi huyo kumaliza kutoa ushaidi wake, Wakili Kiongozi wa Serikali, Stanslaus Boniface, aliiomba mahakama iairishe kesi hiyo hadi Jumatatu, kwani jana wameshindwa kuleta mashahidi.

“Tunaomba shauri hili liairishwe kwani mashahidi hawajaweza kufika leo lakini hata hivyo Summon tuliyowapa ilikuwa ikionyesha tarehe za mbele si ya leo (jana) kuja kutoa ushahidi, hivyo wametafutwa leo (jana) alfajiri hawakuweza kupatikana, ila tunaahidi Jumatatu watafika na kutoa ushahidi,” alieleza Stanslaus Boniface.

Ombi ambalo lilikubaliwa na Hakimu Lyamuya na kuairisha shauri hilo hadi Jumatatu.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumamosi, Januari 24 mwaka 2009

'MADILU' AMKATAA HAKIMU

Na Happiness Katabazi

MTUHUMIWA wa kesi ya unyang’anyi wa kutumia nguvu, Ezekiel Matitu, maarufu kwa jina la ‘Madilu’, ambaye anadaiwa kukubuhu kuwapora na kuwajeruhi wanawake, jana aliwasilisha ombi la kutaka Hakimu Henzron Mwankenja ambaye anasikiliza hiyo kujiondoa.

Madilu aliwasilisha ombi hilo mbele ya Mwankenja katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, na kueleza amelazimika kuwasilisha ombi hilo kwa sababu hana imani naye hakimu.

Mwenedesha Mashtaka, Abubakar Mrisha jana alileta shahidi wa mwisho katika kesi hiyo namba 1023 ya mwaka jana, ili aweze kutoa ushahidi, lakini ilishindikana baada ya hakimu Mwankenja kueleza majalada yote ya kesi yanayomkabili mshtakiwa huyo yameitishwa kwa Hakimu Mkuu Mfawidhi Addy Lyamuya.

“Ombi lako nimelipokea ila siwezi kulitolea uamuzi, pia shahidi hataweza kutoa ushahidi wake leo hadi majalada yatakaporudishwa, hivyo naahirisha kesi hadi Jumanne ijayo,” alisema Mwankenja.

Mapema Januari mwaka huu, baadhi ya mashahidi katika kesi hiyo, walidai mshtakiwa huyo ni mzoefu wa kufanya uhalifu huo kwa sababu anakabiliwa na kesi 11 za aina hiyo.

Katika kesi hiyo, mshtakiwa huyo na wenzake wawili wanadaiwa kuwa Januari 29 mwaka jana, walimuibia Kasongo cheni za dhahabu za mkononi na shingo, simu mbili za mkononi vitu vyote vikiwa na jumla ya sh 1,140,000 na kabla ya kuiba alimtishia kwa silaha za jadi na kumjeruhi.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumamosi, Januari 24 mwaka 2009

WANAFUNZI MLIMANI WAACHIWA KWA DHAMANA

Na Happiness Katabazi

HATIMAYE Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (DARUSO), Anthony Machibya, na wenzake wanne wanaokabiliwa na shtaka la kufanya mkusanyiko kinyume na sheria, wameachiwa kwa dhamana.

Washtakiwa hao waliachiwa kwa dhamana baada ya kutimiza masharti ya dhamana yaliyotolewa na Hakimu Victoria Nongwa wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam.

Masharti hayo ni kuwa na mdhamini ambaye ni mwajiriwa wa serikali, atasaini dhamana ya sh 500,000. Pia washtakiwa hawataruhusiwa kwenda eneo la Chuo Kikuu hadi wapate ruhusa ya mahakama na kuliripoti kila Ijumaa katika Kituo cha Polisi Oysterbay.

Mbali ya Machibya, washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Katibu wa Mtandao wa Wanafunzi Nchini(TSNP), Owawa Stephen; na wengine ni Sabinus Pius, Titus Ndila na Issa Paul.

Washtakiwa hao walitimiza masharti ya dhamana jana mchana na kulakiwa na baadhi ya waadhiri na wanafunzi wenzao nje ya viwanja vya mahakama hiyo.

Jumatano iliyopita, washtakiwa hao walifikishwa mahakamani wakikabiliwa na shtaka la kufanya mkusanyiko kinyume na sheria.

Washtakiwa hao walidaiwa kutenda kosa hilo Januari 19 mwaka huu, saa nne asubuhi eneo la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kwa madhumuni ya kutenda kosa, washtakiwa walitengeneza mazingira ya kuhatarisha uvunjifu wa amani wakati zoezi la udahili wa wanafunzi wa mwaka wa tatu na wa nne ukiendelea.

Pia ilidiwa washtakiwa hao walibeba mabango yenye maneno ‘Laiti Nyerere angefufuka leo angelia machozi, kweli Kikwete umesahau umaskini wako;” maneno ambayo yameelezwa yamejielekeza kujenga chuki kwa watu wengine na hatimaye kuweza kuleta uvunjifu wa amani. Kesi itatajwa Februari 7 mwaka huu.

Chanzo:Gazeti la Tanzania la Jumamosi, Januria 24 mwaka 2009

WASHTAKIWA EPA WABADILISHIWA MASHTAKA

Na Happiness Katabazi

UPANDE wa serikali katika kesi ya wizi wa sh bilioni 3.8 katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), mali ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), jana ulibadilisha hati ya mashtaka katika kesi hiyo na kumuongeza mshitakiwa mmoja.

Mbele ya Hakimu Waliwande Lema, Wakili wa Serikali, Mganga Biswalo, alidai hati hiyo ina mashtaka sita na kumuunganisha Mtanzania mwenye asili ya Kiasia, Aya Somai, kuwa mshitakiwa wa tatu katika kesi hiyo.

Washtakiwa wengine katika kesi hiyo ambao walikuwapo tangu awali ni Farijara Hussein, Rajabu Shaaban Maranda, ambaye ni kada wa CCM, Iman Mwakosya, Anna Komu na Sophia Joseph, ambao ni maofisa wa BoT.

Akiwasomea mashitaka hayo, Biswalo alidai kati ya mwaka 2002-2005, walikula njama, kughushi, kuwasilisha nyaraka za uongozo BoT wakionyesha kuwa Kampuni ya Mibale Farm imepewa idhini na kampuni ya India kudai deni la sh 3,868,805,737.13.

Washtakiwa wote walikana tuhuma hizo na Hakimu Lema aliamuru mshtakiwa Somai kupelekwa rumande hadi Januari 26 mwaka huu, ili aweze kupata fursa ya kupitia masharti ya dhamana yaliyotolewa wakati kesi hiyo ilipofunguliwa Novemba 4 mwaka jana. Washitakiwa wengine wapo nje kwa dhamana.

Wakati huo huo, upande wa serikali katika kesi namba 1158 ya mwaka jana ya wizi sh bilioni 1.186 mali ya BoT, inayomkabili Bahati Mahenge na wenzake wanne umebadilisha hati ya mashtaka na kuieleza mahakama kwamba upelelezi wa shauri hilo umekamilika.
Mbali na Mahenge, washtakiwa wengine ni Manase Makale, Davis Kamungu, Godfrey Mosha na Edda Makale.

Katika kesi hiyo, washitakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka tisa likiwemo shitaka la kula njama, kughushi, wizi, kuwasilisha nyaraka za uongo na kwamba katika tarehe tofauti kati ya mwaka 2003-2005, walighushi hati zilizoonyesha Kampuni ya Marubeni ya India imetoa idhini kwa Kampuni ya Changanyikeni Residential Complex ambayo mkurugenzi wake ni Samson Mapunda ambaye jina lake halipo imepewa idhini ya kurithi deni hilo.

Kesi imeahirishwa hadi Februari 9 mwaka huu, itakapokuja kwa ajili ya washtakiwa kusomewa maelezo ya awali.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Januari 23 mwaka 2009

KWA HILI NAPINGANA NA HAKIMU LYAMUYA

Na Happiness Katabazi

JUMANNE ya wiki hii nilikuwa miongoni mwa waandishi wa habari tuliokutana na fedheha ya kufungua mwaka ; fedheha ya kukataliwa kuripoti kesi hiyo eti kwa kuwa tulikuwa hatuna kibali!
Kadhia hiyo ilitukuta wakati tukifuatilia moja ya kesi ya wizi wa Fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje katika Benki Kuu (BoT) sh milioni 207 inayomkabili mweka hazina wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Kigoma, Shaban Maranda, na wenzake watatu, ambayo ilikuwa inaanzaa kuunguruma kwa mara ya kwanza.

Fedheha hiyo ilitupata saa 8:42 mchana pale Hakimu Mkuu Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Addy Lyamuya, ambaye alikuwa ameketi katika kiti chake cha enzi.

Akisaidiana na hakimu mkuu mkazi ambaye ni Katibu wa Jaji Mkuu, Egnas Kitusi, na Hakimu Mkuu Mkazi, Naibu Msajili wa Mahakama Kuu, John Utamwa, na kwa mara ya kwanza tangu mahakama hiyo ianze kusikiliza kesi za EPA, walikuwa wakisikiliza kesi hiyo kwa kutumia vipaza sauti na kompyuta za mkononi ‘Laptop’.

Mbali na Maranda, washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Madeni ya Benki Kuu ya Tanzania, Iman Mwakosya, Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo hicho, Anna Komu na mwanasheria wa benki hiyo, Bosco Kimela.

Kama ilivyo ada kwa sisi waandishi tunaoripoti habari za mahakamani tulifika mapema asubuhi, tayari kwa ajili ya kuanza kuwasikiliza mashahidi wa upande wa mashtaka, wakianzia na Peter Noni na kisha turejee maofisini kuipasha jamii habari zilizojiri katika kesi hiyo .

Ilipofika saa tano asubuhi wanahabari waliingia chumba namba mbili cha mahakama hiyo na kuanza kufuatilia shauri hilo ambalo liliahirishwa kwa mara mbili mfululizo na ilipotimu saa nane waandishi wote tulitakiwa kutii amri ya Lyamuya, ambayo awali ilitaka watu wote warejee kwenye chumba hicho tayari kwa kuipokea hati mpya ya mashtaka ambayo awali iliamriwa upande wa serikali ukaifanyie marekebisho.

Saa 8:11 tuliingia katika chumba hicho na wakili mwandamizi wa serikali Fredrick Manyanda ambaye aliwasomea mashtaka sita washtakiwa hao kwa mujibu wa hati ya mashtaka waliyoifanyia marekebisho.

“Jopo hili limekubaliana na hati mpya na kwa sababu hii, shahidi wa upande wa serikali apande kizimbani aanze kutoa ushahidi, ila wanahabari wekeni peni zenu chini, kwani hamna kibali cha mahakama cha kuripoti kesi hii…hivyo ni marufuku kuripoti kesi hii bila kuwa na kibali,” aliamuru Lyamuya.

Baada ya hakimu Lyamuya kutoa amri hiyo, shahidi wa kwanza wa upande wa mashtaka katika kesi hiyo namba 1162 ya mwaka jana, Peter Noni , ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Mpango Mkakati wa BoT, alipanda kizimbani na kuapishwa na wakili wa serikali, Mganga Biswalo, kabla ya kuanza kutoa ushahidi wake.

Kutokana na hali hiyo, wanahabari tulitoka nje ya mahakama na kuelekea kwenye viwanja vya mahakama kwani uamuzi huo ulitukera kama si kutuchefua.

Kama kweli nchi yetu ina sheria inayopiga marufuku mwandishi kuandika wakati kesi inaendelea bila ya kuwa na kibali, basi mtakubaliana nami kwamba Lyamuya naye ameshiriki kikamilifu kuwasaidia waandishi wa habari kuivunja sheria hiyo.

Nasema ameshiriki kuivunja sheria hii kwa sababu siku hiyo aliwaona waandishi wakiandika mwenendo wa kesi hiyo tangu asubuhi na pia kuna kesi nyingine za EPA zinazowakabili washtakiwa wengi lakini siku zote amekuwa kimya.

Pia kuna kesi nyingine ambazo zipo mbele yake rekodi zake tunazo , waandishi tumekuwa tukirekodi mwenendo wa mashauri ya kesi hizo na alikuwa akituona lakini hakuwahi kutoa amri kama hiyo.

Kwa hiyo kama siku zote hizo alikuwa anatuona tulikuwa tukiivunja hiyo sheria ambayo hataki kuweka wazi ni sheria namba ngapi bali anaishia kusema hiyo ni sheria ya nchi, nadhani anastahili kuadhibiwa na mabosi wake kwa sababu miaka nenda rudi amekuwa kimya juu ya sheria hiyo.

Na kama sheria hiyo ipo basi kuanzia Jaji Mkuu Agustino Ramadhani, aliekuwa Jaji Kiongozi, Salum Masati, Jaji Laurian Kalegea, Jaji William Mandia, majaji na mahakimu wengine nao tunasema wameshiriki kikamilifu kutusaidia sisi wanahabari kuivunja sheria hiyo kwani tumekuwa tukiingia kwenye kesi wanazoziendesha na kurekodi mwenendo wa kesi hizo bila ya kupata kibali cha mahakama.

Tujiulize Jaji Mkuu na majaji wenzake ambao wanaruhusu wanahabari kuripoti mwenendo wa kesi bila ya kibali je ni wadhaifu wa kusimamia sheria za nchi kuliko hakimu Lyamuya?
Pia tujiulize hakimu Lyamuya ni makini? Kwani kama Lyamuya ni makini alipaswa kuwaondoa wanahabari kabla ya shauri hilo kuanza.

Au viongozi ambao wameapa kulinda Katiba na Sheria za nchi wanafaidika kwa namna moja au nyingine kwa ufunjifu wa sheria hiyo hadi wakati mwingine wanafumbia macho wanahabari wanaoivunja sheria hiyo?

Ni Lyamuya huyu huyu wiki iliyopita tulifika ofisini kwake tukamweleza kuwa tunataka kujua ombi la Katibu Mkuu Mstaafu, Gray Mgonja, la kutaka aruhusiwe kutoka nje ya Dar es Salaam limefikia wapi; alisema alikuwa anampatia jalada karani wake atupeleke kwa Hakimu Henzron Mwankenja ndiye angetupa taarifa na kusema tayari jalada hilo alikuwa amelishughulikia kiutawala.

Nimuulize Lyamuya wakati anatupa jibu hilo na kutukabidhi karani wake atupeleke kwa Mwankenja mbona hukutudai vitambulisho?

Ni huyu huyu Lyamuya, mara kadhaa sisi waandishi tunaoshinda mahakamani hapo kuripoti kesi mbalimbali, tumekuwa tukimfuata kupata ufafanuzi kuhusu baadhi ya kesi na amekuwa mgumu kutupa ushirikiano!

Akiamua kutoa ushirikiano anatoa huku akitoa sharti kwamba mwandishi mmoja ndiyo aingie kuzungumza naye kwa niaba ya waandishi wa vyombo vya habari. Siyo siri baadhi ya watendaji wa mahakama hiyo wamekuwa wakilalamikia utendaji wake.

Je haya siyo matumizi mabaya ya madaraka? Maana tusiishie kuwafikisha wakina Basil Mramba na Daniel Yona kwa shtaka la matumizi mabaya ya ofisi ya umma wakati kuna watumishi wa umma wanatumia madaraka yao vibaya kwa kukataa kutoa ushirikiano kwa wanahabari.

Ieleweke wazi waandishi wa habari katika hili hawataki kutunishiana misuli na Mahakama ya Tanzania.Tunaheshimu na kuipenda mahakama yetu.

Ila tunachotaka kuona uongozi wa Mahakama unatengeneza mara moja vitambulisho maalum kwa ajili ya waandishi wanaofika kila siku katika mahakama zetu zote na kuripoti kesi mbalimbali ambazo wananchi wana haki ya kikatiba kujua kinachoendelea katika mashauri hayo na si vinginevyo.

Siyo utaratibu usiotekelezeka ulitolewa juzi na Lyamuya wa kuwataka wanahabari eti kila watakapotaka kuingia kwenye kesi hata kama ni zaidi ya tatu waende kwa mahakimu husika na kujiorodhesha. Nasema utaratibu huu hautekelezeki katika zama hizi za utandawazi.

Hivi kitendo cha Lyamuya cha kuwatoa waandishi wa habari siku ile bila kuwaeleza utaratibu hata kama kilikuwa ndani ya sheria pia kilitudhalilisha waandishi wa habari mbele ya hadhara iliyokuwa imefurika katika mahakama hiyo, kwani tulionekana si chochote katika ujenzi wa taifa.
Lyamuya fahamu kuanzia sasa sisi wote tunajenga nyumba moja hivyo hatuna sababu ya kugombea fito.

Natoa changamoto kwa Lyamuya kufungua milango wazi kwa wanahabari na kutoa ushirikiano wa hali na mali pale unapohitajika kufanya hivyo.

Kwani pamoja na mashauri mengine kuwepo mahakamani hapo lakini kwa sasa Watanzania wengi macho na masikio yameelekezwa kwenye mahakama hiyo ya Kisutu anayoingoza kujua hatima za kesi hizo hivyo atakaposhindwa kutoa ushirikiani atakuwa anawapa wakati mgumu wanahabari.

Na endapo atafanya hivyo atakuwa amemaliza ile minong’ono ya chini chini inayotolewa na baadhi ya watendaji wa mahakama hiyo dhidi yake kwamba amekuwa ni kero katika utendaji wa mahakama hiyo.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa 23 mwaka 2009

SHAHIDI AMSHUSHIA MZIGO MAREHEMU BALLALI

*Adai alikuwa na utaratibu mbaya wa malipo ya EPA
*Adai alikuwa akitoa maagizo ya malipo kwa mdomo
*Ni Mkurugenzi wa Idara ya Mipango na Mkakati BoT
*Naibu Msajili BRELA naye atoa ushahidi mzito kortini

Na Happiness Katabazi

SHAHIDI wa kwanza katika kesi ya wizi wa sh milioni 207 katika Akanuti ya Madeni ya Nje (EPA), mali ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), ameiambia Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam kuwa aliyekuwa Gavana wa BoT, marehemu Daudi Ballali, alikuwa na utaratibu mbaya wa kulipa madeni ya fedha za EPA.

Shahidi huyo ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Mipango na Mkakati wa BoT, Peter Noni, alieleza hayo jana mbele ya Hakimu Mkuu Mfawidhi, Addy Lyamuya, wakati akijibu swali la wakili wa utetezi, Mabere Marando. Mawakili wengine wa upande wa utetezi ni Majura Magafu na Masaki Masatu.

Alidai utaratibu ambao haukuwa rasmi ambao walikuwa wakiutumia ni kwa wadeni kwenda kuona na Gavana wa BoT, Ballali, kisha gavana huyo kuyapeleka madai hayo kwa katibu wa benki kwa ajili ya kuhakikiwa na baadaye kupekekwa kwake (Noni) ambaye wakati huo alikuwa Mkurugenzi wa Uchumi na Sera na alikuwa akipendekeza madeni hayo yalipwe na kurudishwa tena kwa gavana kwa ajili ya kulipwa.

“Wakati mwingine madeni hayo yalikuwa yakilipwa kwa shinikizo la wanasheria wa wadai na Gavana (Ballali), alikuwa akitoa maagizo yasiyo ya kimaandishi kwa watendaji husika akidai walipwe haraka, ili benki isipate aibu ya kuburuzwa mahakamani na wadeni hao,” alidai Noni.

Hata hivyo, alidai wakati serikali inapata uwezo wa kulipa madeni hayo, BoT ilikuwa ikitumia programu nne tofauti za kulipa madeni, ambazo zilikuwa zikitumika miaka ya 1986 -2002 na baada ya kipindi hicho hapakuwepo programu rasmi ya kulipa madeni, ila madeni ya EPA yaliendelea kulipwa bila utaratibu rasmi.

Ifuatayo ni sehemu ya mahojiano kati ya mawakili wa utetezi na shahidi Noni:

Wakili: Nitakuwa sahihi nikisema washtakiwa wa pili, wa tatu na wa nne walikuwa wakitekeleza maagizo ya Ballali kwa kulipa madeni hayo?
Shahidi: Ndiyo.
Wakili: Kwa kuwa hakukuwa na taratibu rasmi, hivi mdai alikuwa anafikisha malalamiko yake wapi?
Shahidi: Kwa gavana ambaye kipindi hicho alikuwa ni Daudi Ballali, ambaye kwa sasa ni marehemu.
Wakili: Mbali ya Gavana, hakukuwa na ofisa aliyekuwa anamsaidia kazi hiyo gavana?
Shahidi: Alikuwa ni Naibu Gavana.
Wakili: Ni nyaraka zipi ambazo mdai alitakiwa kuziwasilisha kwa Gavana au Naibu wake?
Shahidi: Barua ya kuomba kulipwa na uthibitisho wa deni.
Wakili: Ni kitu gani kiliisaidia BoT kutambua mdai anayestahili kulipwa?
Shahidi: Tulitumia data base za NBC.
Wakili: Hizi data base zilikuwa chini ya nani?
Shahidi: Chini ya Kurugenzi ya Uchumi na Sera ya BoT ambayo mimi nilikuwa naingoza.
Wakili: Baada ya madeni, ombi la kulipwa deni kuhakikiwa na Idara ya Madeni, yalikuwa yanapelekwa wapi?
Shahidi: Kwanza yalikuwa yanapelekwa kwa Sekretari wa benki, kisha kwa gavana.
Wakili: Huyu sekretari ana kazi gani?
Shahidi: Ni mtaalamu wa sheria.
Wakili: Katika ushahidi wako uliotoa ulisema umekoma kuwa Mkurugenzi wa Uchumi na Sera Machi, mwaka 2005, nani alirithi nafasi yako?
Shahidi: Issac Kilato.
Wakili: Inawezekana mtu akaleta deni bila kupitia huo mlolongo?
Shahidi: Haikuwa kawaida.
Wakili: Hamkuona huo utaratibu usio rasmi wa kulipa madeni ungehatarisha Benki Kuu?
Shahidi: (kimya).
Wakili: Unaweza kukumbuka idadi ya watu waliolipwa?
Shahidi: Sina kumbukumbu.
Wakili: Mteja wangu, Anna Komu alinieleza kwamba hata wewe unafahamu kwamba yeye hakuwa na mamlaka ya moja kwa moja ya kuidhinishwa kulipwa kwa deni? Kweli?
Shahidi: Ni kweli.
Wakili: Pia Komu alinieleza kwamba mwaka 2004 wewe hukuridhika na utaratibu usio rasmi wa kulipa madeni ya EPA na ulimshauri gavana uundwe uratibu mpya ambao utatumika kulipa madeni, lakini gavana alikukatalia?
Shahidi: Eeh…ni kweli nilikuwa na nia hiyo, lakini nilimweleza gavana katika mazungumzo, lakini sikuwa nimeweka nia hiyo kwa maandishi.
Wakili: Una ushahidi wowote kwamba kuna wadeni waliwasilisha moja kwa moja maombi yao kwa mshitakiwa wa pili, wa tatu na wa nne, ili walipe deni?
Shahidi: Sina ushaidi huo.
Aidha, shahidi wa pili katika kesi hiyo, ambaye ni Naibu Msajili wa BRELA, Andrew Mkapa, alipanda kizimbani majira ya saa tisa alasiri akiongozwa na wakili kiongozi wa serikali, Stanslaus Boniface, kutoa ushaidi wake ambapo aliithibitishia mahakama hiyo kwamba Kampuni ya Rashhaz (T) Ltd ilisajiliwa kwenye ofisi anayoingoza.
Ifuatayo ni sehemu ya mahojiano kati ya wakili huyo na Mkapa:
Wakili: Nani wakurugenzi wa kampuni hiyo?
Shahidi: Wakati inasajiliwa Septemba 12 mwaka 2003, wakurugenzi walikuwa ni Rajabu Shaaban Maranda na Maranda Rajab Maranda, ambao pia ni wanahisa wa hiyo kampuni.
Wakili: Katika anwani yao ya makazi walisema wanaishi wapi?
Shahidi: Wakurugenzi wote wanaishi Mbezi Beach - Kitalu namba 24 W-Tangibovu.
Wakili: Walieleza BRELA ofisi yao ipo wapi?
Shahidi: Walieleza kwenye jalada la kusajili hiyo kampuni kwamba ofisi yao ipo Tangibovu, House of New BP.
Wakili: Alisema baadaye kampuni iliwasilisha fomu namba 14 ambayo inatolewa na ofisi yetu inayoonyesha mabadiliko ya wakurugenzi na kwamba Mkurugenzi mpya anaitwa Jaffer Hussein Jaffer na aliteuliwa kushika wadhifa huo Desemba 8 mwaka 2003 na walituambi Jaffer ni Mtanzania anaishi Mburahati kitalu 606, NHC, Dar es Salaam.
Wakili: Tangu kampuni hiyo isajiliwe ilishawahi kuwasilisha ripoti ya mahesabu ya mwaka ya kampuni?
Shahidi: Haijawahi kuwasilisha.
Wakili: Kisheria kama kampuni haiwasilishi ripoti hiyo ya mwaka, mnaichukuliaje?
Shahidi: Tunaichukulia kuwa ni dormant.
Wakili: Katika majukumu ya hiyo kampuni waliyoyainisha kuyafanya, kuna sehemu inaonyesha watakuwa na jukumu la kukusanya madeni?
Shahidi: Hapana.
Hakimu Lyamuya aliahirisha kesi hiyo hadi leo na kuutaka upande wa mashitaka kumleta shahidi wa tatu, ili shahidi wa pili atakapomaliza kuhojiwa na mawakili wa utetezi, shahidi wa tatu aweze kutoa ushahidi wake.
Kesi hiyo inamkabili Mweka Hazina wa CCM Mkoa wa Kigoma, Rajab Maranda na maofisa wa BoT, Iman Mwakosya, Anna Komu na Bosco Kimela, ambao wanadaiwa kuiibia benki hiyo jumla ya sh milioni 207.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Januari 23 mwaka 2009