MAHAKAMA KUU YAMGOMEA DK.SLAA

Na Happiness Katabazi
HATIMAYE Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imetupilia mbali kwa gharama pingamizi lilowasilishwa mbele yake na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema), Dk.Willbrod Slaa  lililokuwa likiomba mahakama hiyo ifute kesi ya madai iliyofunguliwa na mkewe Rose Kamili Slaa nee Sakum akiomba mahakama hiyo imzuie  mumewe Dk.Slaa asifunge ndoa na mchumba wake Josephine Mushumbusi.
Uamuzi huo ulitolewa jana na Jaji Laurnce Kaduri  ambaye alisema amepitia kwa kina pingamizi lilowasilishwa na Dk.Slaa na majibu yaliyojibiwa na mlalamikaji Rose anayetetewa  na wakili wa kujitegemea Joseph Thadayo na amefikia uamuzi wa kuona hoja zilizowasilishwa mbele yake na Dk.Slaa ziliomba mahakama hii iifute kesi ya msingi iliyofunguliwa na Rose  ni dhahifu na hivyo amezitupilia mbali.
Jaji Kaduli alisema  Dk.Slaa alikosea kudai kuwa  Rose  hakuwa na haki ya kufungua  kesi hiyo ya kumzuia asifunge ndoa na mchumba wake Josephine kwa taratibu za kisheria kwasababu   Slaa na Rose hawakuwai kufunga ndoa  ila kulikuwa na dhana  ya ndoa.
“Mahakama hii inaitupilia mbali tena kwa gharama pingamizi hilo la Dk.Slaa linalosema kuwa Rose hakuwa nahaki ya kupinga ndoa yake kwasababu hakuwa mke wake na wala hawajawai kufunga ndoa kwasababu sheria ya ndoa inasema mtu ambaye umeishawahi kuishi kama mke na mume kwa zaidi ya miaka miwili,sheria inawahesabu kama ni wana ndoa hivyo mahakma hii inasema Rose ana haki ya kufungua kesi ya kuzuia ndoa ya wadaiwa yaani Slaa na Josephine na mahakama inatupilia mbali pingamizi la Slaa na kwamba kesi ya msingi itakuja kutajwa mahakamani hapo Novemba 6 mwaka huu’alisema Jaji Kaduri.
Kesi hiyo ya madai ya ndoa Na.4/2012 ilifunguliwa mahakamani hapo na Rose dhidi ya Dk.Slaa na Josephine kwa mara ya kwanza mapema Julai mwaka huu, akiiomba  mahakama isikubali shauri hilo lipelekwe kwenye Bodi ya Maridhiano ya Masuala ya Ndoa ya kwaajili ya kupatanishwa. Dai la pili, Rose anaiomba mahakama itanganze yeye na Dk.Slaa bado ni wanandoa.Dai la tatu anaiomba mahakama itamke kuwa ndoa baina yake na Dk.Slaa bado halali kisheria na kwamba ndoa nyingine itakayofungwa kinyume na sasa ndoa hiyo itakuwa ni batili.
Katika dai lake nne, mlalamikaji ambaye ni Mbunge wa Viti Maalum(Chadema) huyo anadai mdaiwa wa pili(Josephine) alimshawishi mumewe(Dk.Slaa) kuivuruga ndoa yake na mumewe ambaye ni mdaiwa wa kwanza.
“Pia nia ya wadaiwa hao wawili ya kutaka kufunga waliyopanga ifungwe Julai 21 mwaka huu katika eneo lolote lile,ndoa hiyo ihesabike kuwa ni batili. Aidha anaiomba mahakama iwaamuru wadaiwa wamlipe fidia ya shilingi 50,000,000 kama gharama za matunzo ya watoto watoto wawili ambao Emiliana Slaa na Linus Slaa aliyezaliwa mwaka 1987 na kwamba walianza kuishi pamoja na Dk.Slaa kama mume na mke, ambao amekuwa akiwahudumia kwa tangu mwaka 2009 baada ya mume wake kumkimbia.
Pia anaiomba mahakama imwamuru mdaiwa wa pili(Josephine) amlipe fidia ya shilingi 500,000,000 kwasababu alimsababishia usumbufu mkubwa na kumharibia ndoa yake na kuongeza kwa kuimba mahakama hiyo impatie nafuu nyingine ambazo itaona inafaa.
Chanzo:Gazeti la Tanznaia Daima la Jumamosi, Oktoba 20 mwaka 2012.

SHEIKH PONDA KORTINI KWA UCHOCHEZI,WIZI

*DPP AFUNGA DHAMANA YA SHEIKH PONDA
Na Happiness Katabazi

HATIMAYE Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu(T), Sheikh Issa Ponda na wafuasi wake 49 jana walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam chini ya ulinzi mkali wa wanausalama kwa kosa la uchochezi na wizi wa malighafi zenye thamani ya Shilingi milioni 59.

Katika hatua nyingine Mkurugenzi wa Mashitaka(DPP),Dk.Eliezer Feleshi aliwasilishwa mahakamani hapo hati ya kuzuia Ponda asipewe dhamana chini ya kifungu cha 84(4) cha Sheria ya Mwenendo wa  Makosa ya Jinai ya mwaka 2002, ambapo kifungi hicho kinampa mamlaka DPP kufunga dhamana kwa mshtakiwa anayekabiliwa na makosa yanayodhaminika na  mahakama inakuwa imefungwa mikono hivyo mahakama inakuwa haina mamlaka ya kuipinga hati hiyo ya DPP hadi pale siku DPP atakapojisikia kuiondoa mahakamani hati hiyo.

Washitakiwa hao 50 ambao wanawake ni 12 na wanaume ni 40 wakati mshitakiwa wa nne ni mwanamke aitwaye Zaida Yusuf mwenye umri wa miaka 100, na wanatetewa na wakili wa kujitegemea Nassor Mansoor ambao wakati wanaingizwa na kuondoka kwenye viwanja vya mahakama hiyo ndani ya magari ya polisi na jeshi la Magereza  walikuwa wakisikika wakipaza sauti wakisema ‘Allah akbar, Allah akbar’.

Askari wa Jeshi la Polisi wakiwa wamevalia kombati huku wakiwa wamebeba silaha nzito na makachero wengine wakiwa wamevalia nguo za kiraia walianza kutanda ndani na nje ya viwanja hivyo tangu asubuhi na walifikisha mahakamani hapo washitakiwa hao kwa awamu mbili tofauti.

Awamu ya kwanza ilikuwa ni ya msafara wa magari matatu  aina ya Defenda lenye namba za usajili PF 2118 na Z 442 BZ lilokuwa limebeba askari wa doria na Karandinga   aina ya Layland lenye namba za usajili STH 2508  ambalo gari hilo lilikuwa limewabeba washitakiwa wake kwa waume 49 ambao walikuwa wamevalia baibu,na baadhi ya wanaume walikuwa wamevalia kanzu na vilemba kichwani maarufu kama ‘haghal’ wengine zikiwa zimechanika na wengine wakionekana kushindwa kutembea kwasababu ya majeraha waliyokuwa nayo miguuni na wengine walionekana kushindwa kukaa kwa muda mrefu kwenye viti vya mahakama hiyo na hivyo kukaa chini ya sakafu ambao uliwasili mahakamani hapo saa 5:16 asubuhi na kupelekwa moja kwa moja kuketi katika ukumbi namba moja wa mahakama hiyo.

Kisha msafara wa pili ambao ulikuwa na magari manne yenye namba za usajili PT 0886 gari lilobeba maji ya kuwasha  ambalo ambapo katika msafara huu ndiyo uliwasili mahakamani hapo na mshitakiwa wa kwanza Ponda  saa 6:23 mchana chini ya ulinzi mkali wa makachero zaidi 20 na kisha kumpitisha mlango wa nyuma ya mahakama hiyo na kumuingiza haraka ndani ya ukumbi namba moja wa mahakama kwenda kuunganishwa na washitakiwa wenzie ambao waliketi ndani ya chumba hicho mapema tayari kwaajili kuanza kusomewa mashitaka yao.

Hakimu Mkazi Stewart Sanga alivyoingia ndani ukumbi huo wa mahakama na kuketi katika keti chake kabla ya mawakili kuanza kuzungumza chochote alianza kwa kusema kesi hiyo mpya namba 245/2012 kuwa yeye siye hakimu aliyepangwa kusikiliza kesi hiyo,uongozi wa mahakama hiyo umempanga Hakimu Mkazi Victoria Nongwa kusikiliza kesi hiyo na kwamba hakimu Nongwa yupo kwenye semina hivyo ana udhuru na alivyomaliza kusema maneno hayo alimtaka  Wakili Mwandamizi wa Serikali Tumaini Kweka na Zeberi Mkakatu kuanza kuwasomea mashitaka washitakiwa hao.

Wakili Kweka  alianza kueleza kuwa Sheikh  Ponda peke yake anakabiliwa na makosa matano isipokuwa washitakiwa wenzake 49 ambao wanakabiliwa na makosa manne ambayo makosa yote yanadhaminika kwa mujibu wa sheria.

Alidai shitaka la kwanza ni la kula njama kinyume na kifungu 384 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu ya mwaka 2012,kwamba Oktoba 12 mwaka huu, huko eneo la Chang’ombe Markasi washitakiwa wote walikula  kwa nia ya kutenda kosa hilo.

Wakili Kweka alidai shitaka la pili ni kwaajili ya washitakiwa wote  ambalo ni la kuingia kwa nguvu  kwa nia ya kutenda kosa  kinyume na kiufungu cha 85 na 35 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu  na kwamba  Oktoba 12 mwaka huu,  huko Chang’ombe  Markasi , kwa jinai  wasipokuwa na sababu  za msingi  washitakiwa hao waliingia  kwenye kiwanja kinachomilikiwa kampuni ya AgriTanzania  Ltd  kwania ya kujimilikisha  kiwanja hicho isivyo halali.

Kabla ya washitakiwa hakubali au kataa shitala hilo Ponda aliripoka na kusema yeye anakanusha shitaka hilo na kwamba washitakiwa wenzake nao wanalikanusha shitaka hilo,jambo ambalo lilikataliwa na Hakimu Sanga ambaye alimrisha kila mshitakiwa ajibu shitaka hilo kwa kinywa chake ambapo kila mshitakiwa kwa kinywa chake alikanusha shitaka hilo kinyume na alivyokuwa anataka Ponda iwe kwa yeye kukanusha shitaka hilo kwa niaba ya wenzake.

Wakili Kweka alilitaja shitaka la tatu kuwa ni  kujimilikisha  kiwanja kwa jinai kinyume na kifungu cha 86 na 35 cha sheria hiyo  na kwamba kati ya Oktoba 12-16 mwaka huu huko Chang’ambe  Markasi  pasipo na uhalali wowote washitakiwa wote  katika hali  iliyokuwa ikipelekea  uvunjifu wa amani  walijimilikisha  kwa nguvu ardhi  ya  kampuni ya Agritanza Ltd.

Shitaka la nne, wakili Kweka alidai ni la wizi  ambalo ni kinyume na kifungu cha 258  cha sheria ya Kanuni ya Adhabu ya mwaka 2002, na kuwa kati ya Oktoba 12-16 mwaka huu,  washitakiwa hao waliiba vifaa na malighafi,matofali 1500,nondo,Tani 36 za Kokoto vitu vyote hivyo vikiwa na thamani ya Sh 59,650,000 mali ya kampuni ya Agritanza Ltd.

Aidha shitaka la tano Kweka alidai ni la uchochezi ambalo linamkabili Sheikh Ponda peke yake  ambalo ni kinyume na kifungu cha 390 na 35 cha sheria hiyo  kwamba kati ya Oktoba 12-16 mwaka huu katika eneo hilo la Chang’ombe Markasi  kwa maelezo kuwa yeye ni Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu(T) aliwashawishi  wafuasi wake ambao ni washitakiwa hao  kutenda makosa hayo  na kwamba upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.

“Mheshimiwa hakimu pamoja na kuwasomea mashitaka hayo ambayo yanadhamana kwa mujibu wa sheria, Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), Dk.Elizer Feleshi kwa mkono wake amenituma kuwasilisha kwaniaba yake mahakamani hapo hati ya kufunga dhamana kwa mshitakiwa wa kwanza (Ponda) peke yake chini ya kifungu cha  148(4) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 2012’alidai wakili Kweka.

Kwa upande wake wakili wa shitakiwa hao Mansoor alidai anashangazwa na DPP-Dk.Feleshi kuwawasilisha hati hiyo ya kumfungia Ponda dhamana wakati dhamana ni haki ya Kikatiba na kwamba hati hiyo ya DPP imetaja sababu mbili ambazo ni mosi kwaajili ya usalama na sababu ya pili ni maslahi ya jamhuri.Nakuongeza kuwa sababu hizo hazijafafanuliwa kwa mabana na kudai kuwa washitakiwa wameishakaa kwa muda mrefu rumande na kwamba mshitakiwa wanne ni mwanamke mwenye umri wa 100 hivyo anaomba wapatiwe dhamana.

Akijibu hoja hizo wakili wa serikali Kweka alidai anashangazwa na hoja za wakili washitakiwa za kuikosoa hati hiyo iliyowasilishwa na DPP kwasababu kifungu cha 184(4) cha Sheria Makosa ya Jinai, kinasomeka wazi kuwa hati hiyo ya DPP  hata mahakama haiwezi kuipinga na kwamba inapowasilishwa mahakamani hati hiyo mahakama inakuwa imefungwa mikono  na kwamba mwenye mamlaka ya kuiondoa makamani hapo ni DPP mwenyewe siku atapoona inafahaa kuiondoa na sivinginevyo.

Hata hivyo hakimu Sanga alisema hivi baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili; “Kama nilivyokwisha sema tangu awali naingia kuanza kusikiliza kesi hii kuwa mimi siyo hakimu niliyepangwa kusikiliza kesi hii ,aliyepangwa kusikiliza kesi hii ni Hakimu Victoria Nongwa ambaye yupo kwenye semina  kwahiyo endapo pande zote mbili katika kesi hii mnataka kuwasilisha hoja zenu msubirini Hakimu Nongwa akimaliza semina yake mje muwasilishe hoja hizo mbele yake”alisema Hakimu Sanga.

Hata hivyo wakili washitakiwa Mansoor alionekana kutoridhishwa na jibu hilo aliinuka na kumuomba hakimu Sanga aiarishe kesi hiyo hadi leo ili washitakiwa 49 waletwe leo kwaajili ya kupatiwa dhamana kwasababu makosa yao yanadhamana lakini hakimu Sanga alisema haitawezekana kwasababu Hakimu Nongwa bado yupo kwenye semina na leo hatakuwepo mahakamani hapo na hivyo akaamuru washitakiwa hao warejeshwe rumande hadi Novemba mosi,kesi hiyo itakapokuja kwaajili ya kutajwa.

Baada ya  kesi hiyo kumaliza wanausalama walikuwa wamejazana kwa mtindo tofauti ndani ya ukumbi huo wa mahakama waliwataka waandishi wa habari na watu wengine watoke nje na ndani wabaki washitakiwa peke yake na wanausalama na kisha wakatolea mlango wa nyuma washitakiwa hao na kisha kwenye kuwapakiza kwenye mabasi ya Jeshi la Magereza, Karandika na Defenda tayari kwaajili ya kuanza safari ya kupeleka gerezani  ambapo magari ya askari wa usalama Barabarani walilazimika kuifunga barabara iliyopakana na mahakama hiyo kwa muda kwaajili ya kuruhusu msafara wa zaidi ya magari saba yaliyokuwa yamebeba washitakiwa hao,wanausalama kuelekea gerezani.

Baadhi ya watu waliofika mahakamani hapo kusikiliza kesi hiyo ,walizungumza na gazeti hili walisema wamefurahishwa na hatua ya serikali ya kuwafikisha washitakiwa hao mahakamani kwani Tanzania ni nchi inayoongozwa kwa Sheria na Katiba ya nchi na siyo sheria za dini ya Kiisilamu.
Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Oktoba 19 mwaka 2012.

VURUGU KWA KISINGIZIO CHA KUTETEA DINI YAKOMESHWE TANZANIA


Na Happiness Katabazi
OKTOBA 12 mwaka,taifa liliendelea kuandika historia mbaya ya vurugu za kidini huko Mbagala zilizosabishwa kundi kubwa la watu wanaodaiwa ni waumini wa dini ya Kiislamu wenye imani kali  zilizoambatana na kuchomwa moto na kuharibiwa kwa makanisa  ya Kikristo jijini Dar es Salaam, katika kile kilichoelezwa kuchukizwa na kitendo cha mtoto wa dini ya Kikristo ,Emmanuel Josephat (14) aliyedaiwa kukikojolea kukimwagia kitabu kitakatifu cha Kurani.
Kundi hilo liloonekana kufura kwa hasira , lifanya uhabifu huo walichukua hatua ya kufanya uhauribifu huo, baada ya kushindwa kwa jaribio la kukiteka kituo kidogo cha polisi cha Mbagala wilayani Temeke kwa nia ya kumpora mtoto huyo ambaye tayari alikuwa mikononi mwa jeshi la polisi ili waweze kumpiga.

Binafsi  nalaani uhuni huu uliofanywa na wahuni wale ambao ni mambumbumbu wa sheria na sheria na maadili ya dini yao ya Kiislamu kwani Tanzania ni nchi inayoongozwa kwa misingi ya sheria na siyo sheria ya dini ya Kiislamu.

 Aiingii akilini watu waliofanya vurugu zile  tayari wameishaitia litia taifa letu la mapigano ya kidini ,walielezwa  vizuri na jeshi la polisi Temeke watawanyike na kwamba jambo hilo wanalishughulikia kisheria wao wanakaidi amri ya jeshi hilo  kisha wakaanza kufanya fujo za kuchoma hadi makanisa.
Tuwailize hivi huo uhuni walioufanya wanayafahamu madhara yake kwa vizazi vya sasa na baadaye?Hivi hayo majengo (Makanisa) ambayo hayana mdomo, ndiyo yalimwagiza Josephat akakojolee kile kitabu cha Korani? Hivi nao waumini wa makanisa yaliyochomwa nao wakikosa subira wakaamua kulipiza kisasi ,nchi hii itakalika?

Ni maovu mangapi yanafanywa na watoto na ndugu  wetu tena ya kutisha kama ujambazi,ushoga,usagaji,wizi lakini mbona nyie wazazi mlianzisha vurugu za kidini Mbagala hamuonyeshi kukerwa na madhambi hayo ambayo yamekatazwa kwenye vitabu vya dini za Kiislamu na Kikristo?

Nyie mliotaka kumchukulia hatua Josephat kwasababu ametenda dhambi,mnauhakika kuwa nyie hamna dhambi hata chembe mbele ya binadamu wenzenu na Mungu?Na mkae mkijia  mkijua vurugu mlizozifanya ni dhambi mbele ya Mungu na sheria za nchi inayowaongoza.Hivyo mnapaswa pia mtubu na serikali iwachukulie hatua za kisheria kwani serikali kuendela kulea wa aina yenu ni hatari kwa usalama wa taifa letu huko tuendako.

Vongozi wa dini ya Kiislamu watusaidie katika hili kama Korani inawaruhusu  wauimini wake wasiheshimu mamlaka ya duniani au wajichukulie sheria mikononi dhidi ya mtu wanayemtuhumu ameidhalilisha dini yao?

Wote mlioenda kufanya fujo Mbagala,tuwaulize hivi ni watu wangapi tena waumini wa dini yenu ambao wengine ni viongozi mnawafahamu wanatuhuma mbaya wanaingia kwenye misikiti na mnakubali wawaongoze ni kwanini hata siku moja hatujawaona mkipandwa na jazba na kuanza kushughulikia watu hao kwa madai kuwa wanadhihaki kitabu hicho cha kurani ambacho wamekuwa wakikitumia kuombea dua mbalimbali wakati ni watu makatili na mafisadi?

Hivi mliofanya vurugu Mbagala mnakabiliwa na umaskini,wengine hamna hata uhakika wa kula chakula bora,umaskini umewakabili kama mimi.Ningewaona wa maana sana siku mngeandama kwa kufuata taratibu mfikishe vilio vyenu kwa serikali kuhusu ugumu wa maisha unaowakabili,miundo mbinu mibovu,lakini hilo limewashinda mkaona mjiingize kwenye ujinga huu ambao chanzo chake ni watoto wadogo kulumbana.

Imeanza kuwa ni mila na desturi sasa  katika kipindi hiki cha serikali ya awamu ya nne kwa baadhi ya waumini wa dini ya kiislamu hivi sasa hasa siku za Ijumaa, kuibuka kusikojulikana na kuanzisha vurugu   kama Mbagala, kuandamana bila taarifa hadi Wizara ya Mambo ya Ndani, kutoa matamko ya kushinikiza Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Mitihani ya Taifa, Dk.Joyce Ndelichako hajiudhuru, mara hawamtaki Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Simba,Sheikh Issa Ponda naye anawaongoza baadhi ya waislamu kwenda kuokoa na kudai mali za waislamu huko Chang’ombe,mara wanagomea kuhesabiwa kwenye Sensa na kisha kuwazuia watu wasiende kuhesabiwa kwenye sensa.
Kila siku ya Ijumaa ni siku ya Kuabudu kwa ndugu zetu wa dini ya kiislamu lakini hivi karibuni hususani hapa jijini Dar es Salaam, tumeanza kuona baadhi ya waumini wa dini hiyo wamekuwa wakiitumia siku hiyo kufanya mambo yao hayo ambayo wakati mwingine hayapendezi kusikika kwa watu wanaopenda amani.

Ikumbukwe kuwa Ibara ya 19(1),(2),(3) ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, ambazo zinatoa haki kwa mtu uhuru wa mawazo,imani na uchaguzi wa mambo ya dini,shughuli za uendeshaji  wa jumuiya za dini  zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya nchi.

Lakini Ibara ya 19(3) ya Katiba ya Nchi inasomeka hivi; “Hifadhi ya haki zilizotajwa kwenye ibara hii itakuwa chini ya taratibu  zilizowekwa na sheria ambazo ni muhimu  katika jamii ya kidemokrasia kwa ajili  ya usalama wa jamii,amani katika jamii,maadili  ya jamii na umoja wa wa kitaifa”.uhuru kwa mtu kwa mtu kuabudu.

Sasa vurugu hizi zinazoendelewa kufanywa na baadhi ya waislamu wachache  kwa kisingizio cha kuipigania dini yao,pia vurugu hizo zinakwenda kinyume na matakwa ya Ibara ya 19(3) ya Katiba ya Nchi.
 Naweza kusema jeuri hii waliyonayo baadhi ya waumini wa dini hiyo wanaoshiriki kiufanya vitendo vya uvunjifu wa amani uenda ni kwasababu kipindi kile baadhi yao walivyokamatwa kwa makosa ya kuwazuia watu wengine wasiende kuhesabiwa,wenzao wakaamua kuandamana tena bila kutoa taarifa polisi hadi wizara ya Mambo ya Ndani na hawakuchukuliwa hatua zozote na baada ya muda mfupi tukasikia wale waliokuwa wakishikiliwa na jeshi la polisi wakaachiwa, ndiyo maana uenda inayosababisha hata wafikie hatua sasa ya kujichukulia sheria mkononi kwasababu wameishajiona wao wapo juu ya sheria.

Leo hii taifa letu bado linakabiliwa na changamoto nyingi za kujiletea maendeleo ,tunashindwa kuzitafutia ufumbuzi na kufanyakazi kwa bidii lakini wachache wetu wameanza kuleta vurugu za kidini kwa sababu za kiupuzi kabisa ambazo mwisho wa siku zitakuja kutuletea madhara wote.
Napenda kuwashauri wale wote wanaotamani waione Tanzania leo hii ikiingia kwenye machafuko ya kidini, kisiasa,kikabila waame nchi waende kwenye nchi zenye machafuko ya kisasa,dini na ukabila wakaishi huko kwani huko ndiko hasa kunakowafaa wao ambao wamechoka kuishi kwenye nchi yetu yenye amani.

Mwisho naomba nimshauri Rais  Kikwete  na viongozi wengine wote walioshirikia nyadhifa za juu za uongozi wa kiserikali wawaeleze hao baadhi ya wauimini wa dini ya kiislamu kuwa sheria ni msumeno  na kwamba hakuna aliyejuu ya sheria na kwamba Tanzania haiongozwi na sheria ya dini ya Kiislamu wa Kikrito inaongozwa na sheria za nchi na kwamba kitendo cha serikali ya awamu ya nne kuwa na rais Kikwete,Jaji Mkuu Mohamed Chande Othman, Makamu wa Rais Kikwete,Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Rashid Othman,Mkuu wa Jeshi la Polisi Inspekta Jenerali Said Mwema, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dar es Salaam, Suleman Kova ni waislamu, isihakiwapi  uhalali wa wao kufanya vitendo vya uvunjifu wa sheria kwa hisia kwamba waislamu wenzao wameshika madaraka ya juu nchini watawatetea.

Ninachofahamu mimi hao viongozi hao enzi za ujana wao walifanya juhudi wakajiendeleza kielimu wakasoma kwa shida,wakapata ajira na wakaonyesha jutuhudi katika utendaji kazi wao huko kwenye majeshi,na kwenye ulingo wa siasa hadi leo hii wameweza kupata madaraka hayo ya juu ambayo kwa ujinga wenu tu nyie mnaofanya vurugu mnaanzisha vurugu kwa mwamvuli wa kutetea dini ya kiislamu na mkikaa vijiweni baadhi yenu mnajitapa kuwa hakuna wakuwachukulia hatua kwasababu hivi sasa viongozi wa juu wa nchi ni Waislamu wenzenu.

0716 774494
Chanzo:www.katabazihappy.blogspot.com ; Oktoba 17 mwaka 2012

FREDRICK SUMAYE UPO SAHIHI

 

Na Happiness Katabazi
JUMAPILI iliyopita waziri mkuu mstaafu Fredrick Sumaye alifanya mkutano na waandishi wa habari na kueleza kusikitishwa kwake baadhi ya vyombo vya habari hapa nchini kuandika habari kuhusu yeye ambazo alidai hazina ukweli wowote na kwamba hana mpango wa kukiama chama chake cha CCM.

Sumaye ambaye alishindwa kwenye kinyang’anyiro cha kugombea ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM,wilayani Hanang’ mkoani Manyara,bila woga alisema CCM imegubikwa na rushwa ya kimtandao na kutaadhalisha kama tatizo hilo lisipotatuliwa mapema linawaweza kuleta madhara makubwa.

Lakini Sumaye alisema licha ya CCM kukabiliwa na tatizo hilo hayupo tayari kukiama chama hicho kama gazeti moja lilivyoandika wiki iliyopita kuwa anataka kuamia Chadema ni wazushi.Na alituasa sisi wanahabari kuzingatia maadili ya kazi yetu na siyo kuandika habari za uzushi ambazo mwisho wa siku Tanzania inaweza kujikuta inaingia kwenye machafuko kama nchi za jirani zilizowai kuingia kwenye vita ya wenyewe kwa wenyewe kwa sababu ya vyombo vya habari kuandika habari zilizokuwa zikiibua uhasama.

Bila kuchelewa mimi binafsi naunga mkono tamko hilo la Sumaye kwani amesema ukweli na ametumia haki yake ya Kikatiba iliyoanishwa wazi katika Ibara ya 18(a) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 inayosema hivi ‘kila mtu anao uhuru wa kuwa na maoni na kueleza fikra zake;”.

Nafahamu fika kuwa kuna watu watambeza Sumaye kuwa rushwa ndani ya CCM kaiona leo baada ya kushindwa nafasi ya ujumbe wa NEC ?, lakini minasema ni afadhali leo hii Sumaye ameweza kuwa jasiri na kutueleza tatizo hilo kwani hata Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Dk.Edward Hosea analifahamu fika tatizo hilo na ndiyo maana wakati wa uchaguzi Dk.Hosea amekuwa wakiwamwaga mashushushu wake kwenye chaguzi hizo.

Hii ni mara ya pili kwa Sumaye kuwahasa wanahabari, mara ya kwanza aliviasa vyombo vya habari aliposhinda kesi yake aliyoifungua Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam mwaka 2006 dhidi ya Gazeti la Tanzania Leo ambalo limekufa hivi sasa ambalo lilichapisha habari ya uongo ambayo ilisababisha Sumaye achukiwe na wananchi tena na kumbuka wakati habari hiyo inachapishwa taifa lilikuwa likikabiliwa tatizo la uhaba wa vyakula iliyosema Sumaye anamiliki Shilingi Trilioni tatu kwenye akaunti yake na Sumaye alishinda kesi,uongozi wa gazeti hilo ulishindwa kuleta ushahidi na haukuwa na huwezo kuwamlipa fidia Sumaye kama walivyoamriwa na mahakama na matokeo yake mmiliki wa gazeti hilo alienda kwenye mkutano ulioitishwa na Sumaye kwa waandishi wa habari na mmiliki huyo alienda kuomba msahama na kukiri habari ile ilikuwa ya uongo.

Na si Sumaye wala Dk.Hosea tu, hata Rais Jakaya Kikwete naye alishaitaka TAKUKURU kuwashughulikia wana CCM wanaoa rushwa na si hivyo tu Kikwete alishawai kusema ndani ya CCM watu hawaaminiani na kwamba mtu hawezi kumwachia glasi ya maji mwenzie kwa kuhofia kuthuliwa.Pia Kikwete alishawahi kusema ndani ya serikali unakuta Waziri asemeshani na Naibu wake au Katibu Mkuu wa wizara yake. Sasa misioni Sumaye amekosea wapi,nasisitiza yupo sahihi kama alivyokuwa Kikwete ambaye alitueleza siri hizo tena za hatari zinazowahusu wanachama wake na wateule wake ambazo tulikuwa hatuzijui.Nawapongeza viongozi wote hao kwa kuwa wawazi kwetu na tuwaunge mkono kwa uwazi huo siyo kuwalaumu.

Hakuna ubishi kwa sisi tunafuatilia kwa undani na ukaribu siasa zinazofanywa na vyama vingi vya siasa kama CCM,Chadema,TLP. CUF tuhuma za rushwa zimekuwa kiibuliwa na wanachama wa vyama hivyo licha kwa upande wa vyama vingine vimekuwa vikikabiliwa na tuhuma za kupeana vyeo kwa mtindo wa undugu,fedha,kiukanda na rushwa ya ngono.

Sumaye ametusaidia kupaza sauti kuhusu rushwa nyakati za uchaguzi ndani ya chama hicho lakini pia binafsi namuuliza Sumaye yeye au wapambe wake nao hawakushiriki kwa namna yoyote hata kutoa rushwa ya senti moja kwa wapiga kura wale wa uchaguzi ule?Au naye Sumaye alitoa rushwa wapiga kura wakatafuta fedha zake na wakamchinjia baharini ndiyo maana kaamua kulalamika adharani?

Sikuwepo kwenye uchaguzi wa CCM wilaya ya Hanang’ hivyo inaniwia vigumu kumuhukumu Waziri Mary Nagu kuwa alitoa rushwa ndiyo akashinda U-NEC au Sumaye alitoa rushwa fedha zake zikaliwa bure.

Nigeukie hoja ya Sumaye alivyoviasa vyombo vya habari kuwa vizingatie maadili ,ni kweli namuunga mkono Sumaye kwani hata mimi nimeishawahi kuandika makala zaidi ya nne ya kuwaasa wanahabari wenzangu kuwa baadhi yetu tumekuwa tukiandika habari ambazo ni za uongo,uzushi,kuchafua watu wasiyo na hatia kwa makusudi jambo kwanza linadhalilisha taaluma ya habari na pia kuwaletea madhara makubwa watu wasiyo na hatia.

Ifike mahala sasa wale waandishi wahabari wenzetu wanaokubali kutumika vibaya kuandika habari zisizozingatia vigezo ambazo zinawazulia uongo na kuwachafua baadhi ya wananchi wenzetu wakiwemo viongozi,taasisi,vyama na serikali ambao wengine wana umri kama wazazi wetu kuwa na hofu ya Mungu na kuanza kujiuliza hivi habari hiyo ya uongo na uzushi unayoiandika dhidi ya watu hao ndiyo habari ya uongo na uzushi ingeandikwa dhidi yako au mzazi,mkeo,mume wako wako au ndugu yako ungejisikiaje?

Mnaowatendea ubaya kwa makusudi kupitia karamu zenu ni binadamu hawajatolewa Nyongo,wanaumia na wanapata madhara na kuwashushia heshima na wengine wanaweza kuvumilia na wengine hawana moyo wa kuvumilia na siku nao watakapoamua kutumia njia haramu kuwadhuru wanahabari wanaowachafua,tusijekulalamika wala kuandamana.

Kwani hata rais Kikwete mwaka 2008 alipokwenda Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kumtazama Mkurugenzi Mtendaji wa Gazeti la Mwanahalisi,Saed Kubenea aliyekuwa amelazwa hapo kwaajili ya kumwagia kimiminika kinachodhaniwa kuwa ni Tindikali usoni alitutaka waandishi wa habari tujilinde na kujiadhari kwani habari na makala tunazoandika siyo kila mtu anazifurahi ,kuna wengine zinawaumi wanashindwa kuvumilia wataamua kutushughulikia.

0716 774494

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Oktoba 12 mwaka 2012.

MAOFISA ELIMU KORTINI KWA WIZI


Na Happiness Katabazi

MAKAIMU Afisa elimu wa Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam, jana walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam wakikabiliwa na makosa ya matumizi mabaya ya madaraka ya kuibia serikali jumla ya shilingi milioni11.8.

Mawakili wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Alen Kasamala na Sophia Gula mbele ya Hakimu Mkazi Agnes Mchome waliwataja washitakiwa hao kuwa Clara Nyongeja, Elizabeth Thomas,Mercy Nyalusi,Simon Pilla na Joseph Kaika.

Wakili Kasamala alidai kosa la kwanza la matumizi mabaya ya madaraka ni kinyume cha kifungu cha 31 cha Sheria ya kuzuia na kupambana na Rushwa ya mwaka 2007 ambapo linawakabili washitakiwa wote  katika ya Februali  mwaka 2010, Dar es Salaam mshitakiwa wa kwanza akiwa   ni mwajiriwa  wa Wizara ya Fedha  kama mtaalamu wa Kompyuta,mshitakiwa wa pili,tatu na tano wakiwa ni waajiriwa makaimu afisa elimu wa manispaa ya Ilala,mhasibu wakati akitekeleza majukumu yake kwa makusudi walitumia madaraka yao vibaya  kwa kushindwa kusimamia na kukagua  nyaraka za malimbikizo ya mishahara za walimu wa  23 wa Manispaa ya Ilala ambazo nyaraka hizo ziliwasilishwa na walimu hao kwa washitakiwa hao yenye thamani ya shilingi 11,825,000 na kisha kumlipa malimbikizo hayo  Simon Pilla ambaye ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya MSingi ya Juhudi na Ukonga.

Kasamala alidai shitaka la pili ni la matumizi mabaya ya madaraka ambalo linamkabili Simon Pilla kuwa Machi mosi mwaka 2010 katika Shule ya Juhudi  akiwa ni mwajiriwa  wa manispaa ya Ilala alitumia madaraka yake vibaya kwa kumlazimisha George Masinde  ambaye ni Mwalimu wa Shule ya Msingi UKonga  kuwamchia yeye malimbikizo ya mishahara anayodai  ambayo ni sh 3,900,000.

Aidha katika shitaka la nne linamkabili tena Pilla kuwa Machi 2 mwaka 2010 katika shule ya msingi Juhudi akiwa ni mwalimu mkuu wa shule hiyo  alimlazimisha Bahati Said  mwalimu wa shule ya ya msingi Ukonga  kuwamchia  yeye hayo malimbikizo hayo anayoyadai sh. 3,895,000 kwaajili ya kujinufaisha yeye na fedha hizo.

Wakili huyo alidai shitaka la nne ni la matumizi mabaya ya madaraka  ambalo linamkabili tena Pilla  ambapo Machi 2 mwaka 2010 katika shule ya Juhudi  akiwa ni mwalimu mkuu wa shule hiyo  alimlazimisha Ester Mdachi  ambaye ni mwalimu wa shule ya msingi Ukonga kuwamchia yeye malimbiko ya mishahara anayodai ili yaweze kumnufaisha yeye mshitakiwa ambayo ni shilingi 4,030,000.

Na kwamba shitaka la tano ni la matumuzi mabaya ya madataka ambapo Machi 3 mwaka 2010 alimlamizisha Mwaija Chowo kuwachia yeye malimbikizo ya mishahara anayodai ambayo ni sh 3,000,000 ili yaweze kumnufaisha mshitakiwa huyo.

Wakili huyo wa serikali alidai shitaka la sita ni la wizi ambapo Pilla ,Machi 3 mwaka 2010  akiwa ni mwalimu Mkuu wa shule ya Juhudi na mwajiriwa  wa manispaa ya wilaya ya Ilala alimwibia mwajiri wake jumla ya shilingi 11,825,000.

Wakili Kasamala alidai kosa la saba ambalo ni mbadala wa kosa la sita ambalo alipokea fedha za rushwa Machi 3 mwaka 2010 akiwa ni mwalimu Mkuu wa Shule ya Juhudi ,shilingi 3,000,00 kutoka kwa Mwaija Chowo mwalimuwa shule ya msingi Ukonga ili asichukuliwe hatua za kinidhamu   kwakuwa Mwaija alikuwa akikabiliwa na kosa la kushindwa kumpatia malimbikizo ya mshahara na kuongeza upelelezi wa kesi hiyo umekamilika .

Washitakiwa walikana mashitaka na hakimu Mchome alisema ili washitakiwa wapate dhamana ni lazima kila mmoja asaini bondi ya shingi milioni  tano na hakimu huyo akatoa hati ya kuitwa maakamani kwa mshitakiwa wa pili na watatu (Thomas na Nyalusi) ambao hawakuwepo mahakamani hapo na akaiarisha kesi hiyo hadi Oktoba 24 mwaka huu, itakapokuja kwaajili ya kutajwa na washitakiwa wote walitimiza masharti ya dhamana.
Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Oktoba 12 mwaka 2012.

MRAMBA AYASUTA MASHITAKA YAKE

Na Happiness Katabazi

WAZIRI wa fedha wa zamani, Basil Mramba ameendelea kuyasuta mashitaka yanayomkabili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, na kudai kuwa siyo yeye aliyeiarika nchini kampuni ya Alex Stewart,wala kuiongezea mkataba wa nyongeza kampuni hiyo na wala kuiarifu kuwa ilikuwa imeteuliwa na serikali ya Tanzania kuwa imeshinda tenda na kwamba inahitajika kuja kufanyakazi hapa nchini wala kuingia mkataba na kampuni hiyo.

Mramba aliyasema hayo mbele ya jopo linaongozwa na Jaji John Utamwa, Sam Rumanyika na Hakimu Mkazi Saul Kinemela wakati alipokuwa akihojiwa na wakili wa Waziri wa Nishati na Madini wa zamani, Daniel Yona na Katibu Mkuu Mstaafu wa Wizara ya Fedha, Gray Mgonja, (Elisa Msuya na Profesa Leonard Shaidi), baada ya juzi wakili wa Mramba (Peter Swai) kumaliza kumuongoza mshitakiwa huyo kutoa utetezi wake.

Mramba ambaye alikuwa akijibu maswali ya wakili Msuya kwa kutumia nyaraka mbalimbali ambazo zinaonyesha ziliandikwa na Benki Kuu na kusainiwa na marehemu Gavana Daudi Balali zikionyesha kuwa ni BoT, ndiyo iliarika kampuni hiyo kuja kufanyakazi ya kukagua dhahabu nchini na siyo yeye kama inavyodaiwa katika kosa la pili katika hati ya mashitaka na upande wa jamhuri na kwamba ni Benki kuu ndiyo iliiandikia barua kampuni hiyo kuifahamisha kuwa imeshinda tenda na kwa hiyo BoT inaoipatia mkataba wa nyongeza wa kuendelea kufanyakazi ya ukaguzi wa madini.

“Kwanza nayashanga hayo mashitaka kuwa eti mimi na Yona na Mgonja ndiyo tuliiarika hapa nchini kampuni hiyo, ukweli umeanishwa kwenye nayaraka hizi ambazo zimetolewa mahakamani kama utambulisho ambazo zionyesha wazi ziliandikwa na BoT kwa kampuni hiyo sasa nashangazwa leo hii nashitakiwa mimi kwa kosa hilo ambalo halina ukweli wowote”alida Mramba.

Alindelea kudai kuwa aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Andrew Chenge katika barua yake ya Mei 2 mwaka 2003 aliyomuandikia Yona  nakala kwa waziri wa Fedha ,BoT katia maoni yake Chenge alisema anakubaliana na ushauri wa serikali wa kuileta nchini kampuni hiyo ije ifanyekazi  na kwamba hakukuwepo ulazima wa kulipeleka jambo hilo kwenye bodi ya ukaguzi wa dhahabu  na alitoa ushauri wa kisheria kuhusu mkataba huo ambao uliingiwa na BoT na kampuni hiyo kuwa taratibu zote zilifuatwa na akashauri kuhusu mkataba huo kuwa hauitaji leseni  na akaelekeza kuwa gharama za kodi, gharama za uendeshaji wa mradi huo zitabebwa na serikali.

Jana mawakili hao walimaliza kumhoji Mramba na ilikuwa ikitakiwa wakili Kiongozi wa upande wa Jamhuri Fredrick Manyanda aanze kumhoji Mramba lakini hata hivyo wakili Manyanda alidai hakuwa tayari jana kufanya hivyo anaomba akajiandae  lakini hata hivyo Jaji Utamwa aliamua kuiiarisha kesi hiyo hadi Novemba 28-30 mwaka huu, ambapo itakuja kwaajili ya mawakili wa serikali kuanza kumhoji Mramba na jaji huyo akatoa hati za wito wa kuitwa mahakamani mashahidi wa mshitakiwa huyo ambapo shahidi mmoja wapo ni Chenge.
Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Oktoba 12 mwaka 2012.

RAIS MWINYI APANDA KIZIMBANI KUTOA USHAHIDI KATIKA KESI YA KUIBIWA SH.MIL 37


Na Happiness Katabazi
RAIS mstaafu wa awamu ya pili, Ally Hassan  Mwinyi amefuata nyayo za Rais wa awamu ya tatu,Benjamin Mkapa kwa kufika katika Mahakama ya Hakimu MKazi Kisutu Dar es Salaam, na kupanda kizimbani na kutoa ushahidi katika kesi za jinai zilizofunguliwa mahakamani hapo na Mkurugenzi wa Mashitaka nchini(DPP), Dk.Eliezer Feleshi dhidi ya washitakiwa wa kesi hizo za jinai.
Rais Mwinyi jana alitua katika mahakama hiyo huku akiongozwa na maofisa Usalama wa Taifa(TISS)  kuja kutoa ushahidi katika kesi ya jinai Na. 201/2012 iliyofunguliwa na upande wa Jamhuri dhidi ya wakala wa Mwinyi Abdallah  Nassoro  Mzombe(39),mbele ya Hakimu Mkazi Genivitus Dudu  ambapo mshitakiwa huyo ambaye ni Mfanyabiashara  na mkazi wa Kinondoni Mkwajuni anashitakiwa kwa makosa ya   kumuibia Rais Mwinyi Sh. 37,440,000 zikiwa ni kodi ya pango  katika nyumba mbili zinazomilikiwa na rais huyo mstaafu.
Kabla ya Mwinyi kuanza kwa kesi hiyo jana, rais huyo mstaafu alipelekwa kna kuifadhiwa kwa muda kwenye chumba namba moja cha mahakama hiyo kwaajili wakili wa serikali  Charles Anindo kumuandaa kiongozi huyo kutoa ushahidi huo na wakati huo huo  maafisa wanne wa usalama wa taifa walikuwa wakifanya dolia kali ndani na nje ya chumba hicho alichokuwa ameifadhiwa kiongozi huyo.
Ilipofika saa   5:05 asubuhi, askari mmoja wa jeshi la Magereza alimtoa mshitakiwa Zombe katika mahabusu ya mahakama hiyo na kisha kumpandisha kizimbani kwaajili ya kesi yake kuanza kusikilizwa.
Baada ya mshtakiwa huyo kupandishwa kizimbani na askari huyo wa Jeshi la Magereza, waandishi wa habari za mahakamani tuliokuwepo mahakamani hapo nao walijiandaa kuingia katika chumba cha kuendeshea kesi hiyo ili waweze kusikiliza kesi hiyo,  lakini waandishi hao walipowakaribia maofisa usalama hao ,wanausalama hao waliwazuia kuingia ndani  ya chumba cha kusikilizia kesi hiyo  na wanausalama hao wakawahoji wanahabari hao kuwa wao ni wakinanani?

Miongoni mwa maofisa usalama hao ,mmoja wao aliwauliza waandishi wa habari kuwa wanakwenda wapi?
Waandishi wa habari: Tunataka kuingia kwenye hicho chumba kusikiliza kesi hiyo ya mshitakiwa anayedaiwa kumibia rais Mwinyi.
Afisa usalama: Nyie ni wakina nani?
Jibu :  Waandishi wa habari za mahakamani.
Afisa usalama: mmeambiwa kuna mahakama humu?
Jibu: Ndiyo hiyo ni mahakama.
Baada ya waandishi wa habari kumjibu hiyo,  afisa  huyo wa usalama alinyoosha mkono na kuzuia waandishi  kuingia kwenye mahakama hiyo. “Msiingie humu ndani  haiwahusu”.  Baada ya kuambiwa hivyo na mwanausala huyo ilitubidi  tukaa nje hadi saa 6:21 mchana na muda huo ndiyo kesi hiyo ilipamalizika kusikilizwa na tukamuona  rais Mwinyi akitoka ndani ya chumba hicho na kuongozwa na maafisa usalama hao kwenda nje ya mahakama hiyo na kisha kupanda gari aina ya Land Cruiser lenye namba za usajili T 914 BJT na kisha kuondoka katika viwanja vya mahakama hiyo.
Licha ya jitihada hizo za wanausalama kuzuia waandishi wa habari za mahakama kuingia ndani ya chumba cha mahakama kusikiliza ushahidi uliokuwa ukitolewa na rais Mwinyi, lakini waandishi hao nao walitumia mbinu zao na wakafanikiwa kupata hati ya mashitaka ya kesi hiyo ambayo ilifunguliwa mahakamani hapo Agosti  21 mwaka huu, na waandishi wa habari za mahakamani kwa kipindi chote hicho hawakuwa wakifahamu kuna kesi ya aina hiyo ilikuwa imefunguliwa mahakamani hapo.
Kwa mujibu wa hati hiyo ya mashitaka ambayo waandishi wa habari za mahakama walifanikiwa kuipata mahakamani hapo jana ,upande wa Jamhuri unadai  Mzombe anadaiwa kufanya makosa hayo kinyume na kifungu cha 258 na 273 (b) (e) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu ya Sura ya 16 ya mwaka 2002.
  
Siku hiyo ya Agosti 21 mwaka huu, ilidaiwa  kuwa  kati ya Januari Mosi, mwaka 2011 na Julai 2012 huko Mikocheni ,  Mzombe akiwa Wakala wa rais huyo mstaafu, alimwibia  Sh 17,640,000  ambazo ni pato la kodi ya nyumba yake  iliyopo eneo la Mikocheni  wilaya ya Kinondoni.
Iliendelea kudai kuwa kiasi hicho cha fedha ambacho Mzombe alimwibia rais Mwinyi kilikuwa ni kodi ya pango la nyumba namba 481,  iliyopo kwenye ploti A ,huko Mikocheni ya mwaka 2011/2012 na 2012/2013.
Aidha Mbali anadaiwa kuwa  kati ya Januari Mosi, mwaka 2011 na Julai 10, mwaka huu huko Msasani Village  wilaya ya Kinondoni, mshtakiwa  huyo alimwibia tena rais huyo mstaafu Sh 19,800,000  ambayo ilikuwa ni kodi ya nyumba namba 55 iliyopo kwenye Kitalu C .
Iliongezwa kudaiwa kuwa kiasi hicho cha fedha kilikuwa ni kodi ya pango la nyumba hiyo la mwaka  2011/2012 na 2012/2013, hata hivyo mshitakiwa huyo alikana mashitaka yote  na yupo rumande hadi oktoba 22 mwaka,itakapokuja kuendelea kusikilizwa.
Itakumbukwa kuwa Mei 7 mwaka Rais Mkapa alifika mbele ya Hakimu Mfawidhi  wa mahakama ya Kisutu,  Elvin Mugeta m katika kesi ya uhujumu uchumi iliyokuwa ikimkabili aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu na Grace Martin kutoa ushahidi katika kesi hiyo ambapo alikuwa alikuwa ni shahidi wa Mahalu  ambapo Agosti 9 mwaka huu, Hakimu Mugeta alitoa hukumu ya kesi hiyo ya kihistoria na kuwaachiria huru washitakiwa wote kwa madai kuwa upande wa jamhuri wameleta ushahidi dhahifu ambao umeshindwa kuishawishi mahakama imtie hatiani Mahalu na Grace.
Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumatano, Oktoba 10 mwaka 2012.