UB YAMSHUKURU KIKWETE






Na Happiness Katabazi
UONGOZI wa Chuo Kikuu cha Bagamayo (UB), umemshukuru Rais Jakaya Kikwete kwa kuwateua wajumbe wawili wa Bunge la Katiba kutoka katika chuo hicho.
 Akizungumza na Tanzania Daima Jumatano, Naibu Mkuu wa chuo hicho, anayeshughulikia Fedha na Utawala, Dk. Elifuraha Mtaro, aliwataja wajumbe hao kuwa ni Profesa Costa Mahalu na Mkuu wa Kitivo cha Sheria, Dk. Natujwa Mvungi.
Dk. Mtaro alisema wabunge hao wawili ni waajiriwa wa UB, licha ya kuteuliwa kupitia makundi mawili tofauti.
Alisema Balozi Mahalu aliteuliwa kutoka kwenye kundi la dini na Dk. Natujwa ambaye ni mtoto wa aliyekuwa mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katika, marehemu Dk. Sengondo Mvungi, amepitia kundi la elimu.
“Kwa niaba ya uongozi wa UB, tunamshukuru Rais Kikwete kwa kuwateua wafanyakazi wetu wawili kwani uteuzi huo ni ishara tosha ana imani nao na pia ni sifa pia kwa UB kwa kutoa wasomi wawili wa sheria kwenda kuungana na wenzao katika Bunge la Katiba,” alisema Dk. Mtaro.
Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumatano. Februali 12 Mwaka 2014.

MADABIDA KIZIMBANI KWA ARVs FEKI




















Na Happiness Katabazi

MKURUGENZI wa Mashitaka(DPP), Dk.Eliezer Feleshi amemfikisha katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi(CCM), Mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhani Madabida na wenzake watano kwa makosa mbalimbali likiwemo kosa la kusambaza dawa za kupunguza makali ya ugonjwa wa ukimwi 'ARVs' ambazo zimeisha muda wa matumizi.

Mbele ya Hakimu Mkazi Nyigulila Mwaseba, wakili wa Serikali Shadrack Kimaro alidai kuwa mbali na Madabida, washitakiwa wengine ni Seif Salum Shamte ,Simon Msoffe, Fatma Shango ,Sadiki Materu na Evance Mwemezi na kwamba hati ya mashitaka ina jumla ya mashitaka matano.

Wakili Kimaro alilitaja kosa la kwanza ambalo linamkabili mshitakiwa wa kwanza, pili, tatu , nne ni la kusambaza dawa za ARVs zilizokwisha muda wa matumizi kinyume na kifungu cha 76(1) cha Sheria ya Taifa ya Vyakula, Madawa na Vipodozi ya mwaka 2003.

Alidai kuwa washitakiwa hao walitenda kosa hilo Aprili 5 mwaka 2011 Dar es Salaam, washitakiwa wakiwa na wadhifa wa Afisa Mtendaji Mkuu, Mkurugenzi wa Oparesheni, Meneja wa Masoko na Mhasibu Msaidizi wa Tanzania Pharmacetical Industries Ltd, kwa makusudi ,walisambaza dawa hizo kwa Bohari Kuu ya Madawa(MSD), Tinis 7776 ya dawa hizo wakionyesha zina 30mg + nevirapine 200mg +Lamivudine 150mg ikiwa na No.OC 01.85 zinazoonyesha zimetengenezwa Machi 2011 na zinamalizika muda wake matumuzi Februali 2013 wakijaribu kuonyesha dawa hizo ni hali kumbe siyo kweli.

Kosa la pili alidai ni kusambaza dawa hizo kinyume na sheria hiyo ambapo Aprili 11 mwaka 2011,washitakiwa walisambaza tena kiasi hicho cha dawa za ARV feki kwa Bohari Kuu ya Madawa(MSD) ambazo zilikuwa zinaonyesha zimetengenezwa MAchi 2011 na zitamaliza muda wake wa matumuzi Februali 2013, wakionyesha kuwa dawa hizo ni halisi kumbe sikweli.

Wakili Kimaro alilitaja kosa la tatu kuwa ni la kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu kinyume na kifungu cha 302 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu ya mwaka 2002, kuwa kati ya Aprili 12 na 29 mwaka 2011 Dar es Salaam, kwania ya kudanganya wote kwa pamoja walijipatia Dola za Kimarekani 98,506.08 sawa na Sh. 148,350,156.48 toka kwa MSD wakionyesha malipo hayo waliyolipwa yanatokana na wao kuipatia MCD kiasi kile cha dawa za ARVs.

Aidha alilitaja kosa la nne ni la kushindwa kuzuia kutendeka kwa makosa hayo kinyume na kifungu cha 382 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu ya mwaka 2002 linalomkabili (Materu na Mwemezi), kuwa Aprili 13 mwaka 2011 washitakiwa hao ambao ni waajiliwa wa MSD wenye wadhifa wa Meneja uhakiki wa ubora wa madawa wakijua wanatenda kosa walishindwa kutumia njia zinazowezekana kuzuia kosa hilo la MSD kukubali kununua ARVs feki zisinunuliwe.

Shitaka la tano ni la kuisababisha hasara kinyume na kifungu cha 57(1) na 60 cha Sheria ya Uhujumu Uchumi ya mwaka 2002, kuwa kati ya Aprili 5 na Aprili 30 mwaka 2011 washitakiwa wote kwa makusudi walishindwa kutimiza wajibu wao na kusababishia MSD hasara ya Sh.148,350,156.48 kwa kuiuzia ARV feki.

Washitakiwa walikana mashitaka yote na wakili Kimaro alidai upelelezi bado haujakamilika na Hakimu Mwaseba alisema kila mshitakiwa apate dhamana ni lazima atoe fedha taslimu au kusalimisha hati isiyoamishika yenye thamani Sh. 13.5.

Ni Madabida na Sedekia peke yao ndio hadi jana saa nane mchana waliweza kutumiza masharti hayo ya dhamana na mahakama iliwapatia dhamana na washitakiwa wengine waliosalia walishindwa kutimiza masharti hayo na hivyo hakimu akaamuru wapelekwe gerezani na akaiarisha kesi hiyo hadi Februalia 24 mwaka huu, itakapokuja kwaajili ya kutajwa.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Februali 11 mwaka 2014

VIGOGO TBA WAHUKUMIWA KWA KURUHUSU UJENZI JENGO LINALOCHUNGULIA IKULU






 Na Happiness Katabazi

HATIMAYE Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, imewahukumu adhabu ya kwenda jela miaka tisa kila mmoja au kulipa faini ya Sh.Milioni 15 kila mmoja aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu  wa wakala wa majengo nchini (TBA,)Makumba Togolai Kimweri    na Richard Maliyaga waliokuwa wakikabiliwa na kesi ya matumuzi mabaya ya madaraka ya kuruhusu ujenzi wa ongezeko wa maghorofa sita zaidi katika Jengo refu linalochungulia Ikulu Dar es Salaam.
Hukumu hiyo ilitolewa jana na Hakimu Mkazi Sundi Fimbo ambaye kwa sasa ni Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Kilosa, alianza kwa kuikumbusha mahakama kuwa hati ya mashitaka ya kesi ina jumla ya makosa matano na   iliyofunguliwa chini ya Kifungu cha 31cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na RushwaNo 11 ya mwaka 2007.
Hakimu Fimbo alilijata kosa la kwanza lilikuwa ni la kuruhusu ujenzi wa jengo hilo lenye ghorofa 12 bila kufanya upembuzi endelevu na kosa la pili ,tatu, nne la  ni la kutoa kibali cha kujengwa kwa jengo hilo wakati hawakuwa na mmlaka ya kutoa kibali hicho ni Mamlaka ya Mipango Miji ya  Manispaa ya Ilala ndiyo ilikuwa na mamlaka ya kutoa kibali cha kufanyiwa marekebisho ya matumizi ya jengo hilo na kosa la tano ni la matumuzi mabaya ya madaraka ambao washitakiwa hao walitumia madaraka yao vibaya kwakuruhusu mabadiliko sakafu katika ujenzi huo ambao mabadiliko hayo yaliruhusu kinyume cha sheria  kuongeza idadi ya ujenzi zaidi wa ghorofa saba kwenda juu wakati jengo hilo lilistahili kujengwa ghorofa sita tu na hivyo kufanya jengo hilo sasa kuwa na jumla ya ghorofa 12.Mshitakiwa wa kwanza anakabiliwa na kosa la kwanza,pili na la tano wakati mshitakiwa wapili anakabiliwa na kosa la tatu,nne na tano.
Hakimu Fimbo alisema kwanza anashangwa hadi sasa Manispaa ya Ilala ilishindwa kuchukua hatua kuhusu ujenzi wa jengo hilo lilojengwa kinyume na sheria  ambalo lipo katika ukanda wa (security Zone),wakati Sheria inaipa mamlaka Manispaa ya Ilala kuchukua hatua na kwamba kutokana ushahidi uliotolewa mahakama yake imefikia uamuzi wa kuona ghorofa la saba hadi 12 yalijengwa kinyume na sheria.
 “Ajabu sana kwani Manispaa ya Wilaya ya Ilala  ilikuwa na mamlaka ya kuchukua hatua za kisheria kuhusu ujenzi wa jengo hilo ambalo umekiuka sheria za nchi lakini ilishindwa kufanya hivyo…sasa nafikiri kupitia hukumu hii naona ni muda muafaka sasa kwa Manispaa hiyo kutekeleza yale hukumu hii ya mahakama kuhusu ujenzi wa jengo hilo ambalo haujakithi matakwa ya sheria za nchi”alisema Hakimu Fimbo.
Alisema anaukataa utetezi wa washitakiwa uliokuwa ukidai kuwa hawakuwa wakijua kumruhusu mwekezaji ambaye ni Kampuni ya Royal Orchard Inn kujenga maghora zaidi juu kwani kuna vielelezo vilivyotolewa na wakili wa Takukuru, Leonard Swai kuwa kuna barua ya Katibu Mkuu Kiongozi iliyokuwa ikienda kwa kwashitakiwa hao ikiwaambia waombe kwanza kibari kwa mamlaka ya Mipango Miji  cha mabadiliko ya matumizi ya adhi katika Kitalu Na. 45 na 46 Mtaa wa Chimala ,lakini kwa maslahi yao binafsi walipuuza agizo la barua hiyo na kuamua kujitwisha madaraka ambayo hawana wakaamua kuruhusu ongezeko la ujenzi wa ghorofa za saba zaidi juu.
‘Kwa hiyo mahakama hii inakataa utetezi wao kuwa walikuwa hawana taarifa iliyowataka waombe kibali cha mabadiliko ya matumuzi ya ardhi hiyo ambayo ni eneo la Ukanda wa Usalama,…kama washitakiwa hao wasingevunja kifungu cha 32 cha Sheria ya Makazi No. 8 ya mwaka 2007 ni wazi mwekezaji ambaye ni kampuni ya Royal Orchard Inn Ltd asingeweza kunufaika  katika mkataba wa jengo hilo ambalo ni baina ya serikali na kampuni hiyo:
“Ni sahihi kabisa kama washitakiwa hao wasingevunja sheria , hakuna njia mwekezaji hiyo angeweza kupata uniti 19 ni kama amepangisha na anachukua kodi kila mwezi na kwamba kifungu cha 31 cha Sheria ya Takukuru ya mwaka 2007 kinaonyesha washitakiwa walinufaika binafsi na ujenzi huo wa ghorofa hilo kinyume na sheria  na kwa maana hiyo mahakama upande wa jamhuri umeweza kuthibitisha kesi yake bila kuacha mashaka”alisema hakimu Fimbo.
 Baada ya kuwatia hatiani na kabla ya kutoa adhabu  aliwataka mawakili wa pande zote mbili kusema chochote kama wanacho ambapo wakili wa Takukuru, Leonard Swai alieleza kuwa hana rekodi za washitakiwa kuwa kama huko nyuma waliwai kutiwa hatiani kwa makosa ya jinai ila akaiomba mahakama itoe adhabu kwa wengine ambao wamekuwa wakijijengea majengo bila kufuata sheria na hasa ukizingatia jengo hilo linapaka na Ikulu lina urefu wa ghorofa 12 wakati kisheria lilitakiwa liwe na urefu wa ghorofa sita lakini washitakiwa hao kwa maslahi yao binafsi wakavunja sheria na kuruhusu ujenzi zaidi wa ghorofa hilo ambalo ni refu nalipo security zone na linaatarisha usalama wa makazi ya Rais wa nchini(IKULU).
Kwa upande wa wakili wa washitakiwa Henri Masaba, Pascal Kamala aliomba mahakama hiyo itoe adhabu nyepesi kwasababu washitakiwa hao watendaji wa mara ya kwanza ya  mara ya kwanza na kwamba ni wagonjwa.
Hakimu Fimbo akitoa adhabu alisema kila kosa moja ni jela miaka mitatu au kulipa faini ya Sh.milioni tano kwa kila kosa.Hivyo kila mshitakiwa atakwenda jumla ya miaka tisa kwasababu kila mshitakiwa na akabiliwa na jumla ya makosa matatu au atalipa jumla ya Sh.milioni 15 .
Hata hivyo washitakiwa wote wameweza kulipa faini ya Sh.milioni 15 kwa kila mmoja mahakamani hapo na wameachiwa huru.
Akizungumza na waandishi wa habari za mahakamani nje ya mahakama baada ya hukumu hiyo kutolewa, wakili wa Takukuru, Swai alisema kwanza amefurahishwa na hukumu hiyo nzuri na ambayo ni salamu kwa wale wote wanaojenga majengo kiholelaholela na pia ni sifa kwa PCCB kwani kesi hiyo iliendeshwa na PCCB, na kwamba kifungu cha 40 (1) na (2) cha Sheria ya PCCB, inaipa mamlaka PCCB ndani ya miezi sita kuanzia hukumu ilipotolewa na mahakama kuhusu kesi yoyote iliyoshitakiwa kwa sheria ya PCCB, kutaifisha mali husika na katika mazingira ya kesi hii, PCCB ndani ya muda huo ambao umewekwa kisheria unayo mamlaka ya kutaifisha ghorofa ya 7-12 ya jengo hilo ambalo mahakama imesema ghorofa hizo zilijengwa kinyume na sheria.
Julai mwaka 2013 washitakiwa walifikishwa mahakamani hapo wakikabiliwa na mashitaka hayo waliyotiwa hatiani nayo jana ambapo ni jumla ya makosa matano.

Chanzo:www.katabazihappy.blogspot.com; Februali 11 mwaka 2014.