MAHAKAMA YATUPA KESI YA PINDA



MAHAKAMA YATUPA KESI YA PINDA 
Na Happiness Katabazi
HATIMAYE Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam,imetupilia Mbali Kesi ya Madai  ya Tanzania imetupilia mbali kesi dhidi ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda iliyofunguliwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) pamoja na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kwa sababu Imeona walalamikaji walikuwa hawana Haki ya kisheria ya kushitaki Pinda.

Kesi hiyo Na. 24/2013   ilikuwa ikisikilizwa chini ya jopo la majaji watatu waliokuwa wakiongozwa  Jaji Kiongozi Fakih Jundu, Jaji Dk. Fauz Twaib na Jaji Augustine Mwarija.

Jopo hilo lilitoa uamuzi huo jana ambapo jaji Jaji Jundu alisema anakubaliana na pingamizi la awali lilowasilishwa na wakili wa mdaiwa (Pinda), Ambaye ni Naibu Mwanasheri Mkuu wa Serikali,  George Masaju, AMBAlo lilikuwa likiomba  Mahakama itoe amri ya kuifuta Kesi hiyo kwasababu walalamikaji hawana Haki a kisheria ya kuwashitaki wadaiwa na kwamba Waliokuwa na Haki ya kushitaki Pinda ni wananchi na siyo Taasisi hizo za walalamikaji.
O
LHRC na TLS walimshtakiwa Waziri Mkuu Pinda pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kauli aliyoitoa bungeni Juni 20 mwaka jana.Ilidaiwa Katika   kipindi cha maswali ya papo kwa papo Waziri Pinda akijibu alisema, ‘ukifanya fujo…unaambiwa usifanye hiki ukaamua kukaidi, utapigwa tu, muwapige tu sababu tumechoka’.

 Jaji Jundu alisema, Masaju Aliwasilisha  pingamizi la awali akiomba  kesi hiyo itupwe kwa sababu mahakama hiyo haina uwezo wa kuisikiliza, waliofungua hawakustahili kuifungua na iko kwa ajili ya kupoteza MUDa wa Mahakama.

Katika uamuzi huo, majaji walikubaliana na hoja tatu za pingamizi kuwa walalamikaji katika kesi hiyo hawakuwa na haki ya kufungua kesi hiyo na kwamba walikosea taratibu za ufunguaji wa kesi kama hizo kwa kuwa walikiuka amri na kanuni zinazoongoza Mashauri ya Madai (CPC).

Katika hoja ya kwanza kuwa Pinda kama mbunge analindwa na Katiba, jopo hilo lilisema kuwa ni kweli wabunge wanalindwa na Katiba Ibara ya 100 (1) kuhusu haki na upendeleo (Previledge), yaani haki na uhuru wa mjadala na maoni. Hata hivyo, lilikataa hoja za utetezi kuwa wabunge wana kinga isiyo na mipaka ya kutokushtakiwa kwa kauli au jambo lolote walilolitamka bungeni.

“Ibara ya 100(1) ya Katiba haiwezi kujadiliwa mahali popote ikiwemo mahakamani, ibara hiyo inasema kwamba, kutakuwa na uhuru wa mawazo, majadiliano na utaratibu katika Bunge na uhuru huo hautavunjwa wala kuhojiwa na chombo chochote katika Jamhuri ya Muungano au katika mahakama au mahali penginepo nje ya Bunge.

“Ibara ya 100(2) inaweza kujadiliwa mahakamani, inasema kwamba bila kuathiri katiba hii au masharti ya sheria nyingine yoyote inayohusika, Mbunge yoyote hatashtakiwa au kufunguliwa shauri la madai mahakamani kutokana na jambo lolote alilolisema au kulifanya ndani ya Bunge au alilolileta bungeni kwa njia ya maombi, muswada, hoja au vinginevyo.

“Mwananchi mmoja mmoja aliyeathika na jambo lililozungumzwa na mbunge bungeni anaweza kushtaki lakini si taasisi kama ilivyo katika kesi hii,”alisema.
Alisema kutokana na sababu hizo, mahakama inatupilia mbali kesi hiyo kwa sababu waliofungua kesi, LHRC na TLS hawakustahili kisheria kufungua kesi hiyo kwa sababu hawakuathirika.

Chanzo: Gazeti la Tanzania Daima la Jumamosi, Juni 7 Mwaka 2014



NABII BRUNO KINUNDA,KIONGOZI WA KANISA LA ELISHADAI

 Kiongozi wa Kanisa la ELISHADAI, NABII Kanali Mstaafu wa (JWTZ), Bruno Kinunda.






KUJADILI MUUNGANO ISIWE DHAMBI , USALITI




Na Happiness Katabazi
KADRI siku zinavyozidi kusonga mbele, ile  kasumba ya kumhesabu mtu yeyote  anayekosoa jambo lolote linalousu upande mmoja wa Muungano wa Zanzibar na Tanzania Bara Kuwa ni msaliti,anataka kuuvunja Muungano huo, inaanza kupoteza Nguvu.

Pia ile Hali ya woga waliyokuwa nayo Watanzania Bara Wengi yakuogopa kujitokeza adharani kutoa hoja zinazokosoa baadhi ya mapungufu ya nayo fanya au yaliyofanywa  na baadhi ya wazanzibari au serikali yake,au baadhi ya manufaa wanayoyapata Wazanzibar Katika Muungano, Kwa kisingizio Cha Kuogopa kutolewa lugha chafu toka Kwa baadhi ya wanasiasa wa Zanzibar ,unatoweka kwa kasi ya ajabu.

Nasema hivyo Kwasababu miaka ya nyuma ilidaiwa  Kuwa kuna baadhi ya wanasiasa   (Majina ninayo),  Kuwa waliwahi kushughulikiwa kimya kimya tena kikamilifu  na vyama vyao kwa kisingizio tu wanasiasa  Hao walikuwa wanapinga Muungano.

Lakini kwa mujibu wa baadhi ya wanasiasa hao  ambao niliwahi kupata fursa ya kuzungumza  nao ana kwa ana wengine kupitia Kwa watu wangu wa karibu,  hawakuwahi kufikiria kuvunja Muungano, isipokuwa walikuwa na mtazamo tofauti kuhusu baadhi ya mambo ndani ya Muungano na walikuwa wanataka  yarekebishwe kwa njia ya Amani.

Kumbe Mitazamo hiyo ilichukuliwa vibaya na Waliokuwa na madaraka Kipindi hicho, wakatumia njia zao kuwashughulikia watu Hao kikamilifu.

Lakini Kwa baadhi ya wanasisasa  hawakuwa na nia Mbaya na ukweli siku zote utasimama, Leo hii Tunaona  baadhi ya wanasiasa waliosurubiwa kule Zanzibar kimya kimya Kwa fitna eti ni Wapinga Muungano,Leo hii Mungu  amewajalia ameruhusu wamepewa madaraka makubwa ndani ya Serikali ya Zanzibar na Tanzania Bara na ule uongo Waliokuwa wamepakaziwa Kuwa ni Wapinga Muungano na endapo wa wakipewa madaraka watavunja Muungano, sijui zimezikwa Katika makaburi gani.

Mei 27 Mwaka huu,ni baadhi ya ni kielelezo cha   hayo niliyoyasema hapo juu,Mbunge wa Nkasi Kaskazini (CCM), Ally  Kessy aliwashambulia  Wazanzibar, kwamba hawana sababu ya kulalamikia kutaka haki sawa kwenye kila jambo la muungano wakati hawachangii kitu kwenye Serikali ya Muungano.

 Mbunge huyo aliyeamua kujilipua , alitoa kauli hiyo ndani ya Bunge, wakati akichangia hoja ya hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa mwaka wa fedha 2014/2015, inayoongozwa na Waziri  Bernad Membe.

Kessy alichangia hoja hiyo akijibu hoja ya Kambi Rasmi ya Upinzani iliyosema kuna upendeleo mkubwa na uwiano usio sawa kati ya Tanzania Bara na Visiwani katika uteuzi wa mabalozi wa Tanzania nje ya nchi.

Kessy  alisema kwa zaidi ya miaka 20 , Zanzibar, haichangii kitu katika Serikali ya Muungano, lakini ndio vinara wa Kulalamika  na kutaka usawa kwenye kila jambo., Kauli iliyozua zogo Kwa dakika zisizopungua tano.

Wakati  akiendelea kuchangia hoja hiyo, Mbunge wa Chakechake, Mussa Haji Kombo (CUF), aliomba mwongozo wa Naibu Spika dhidi ya kauli hiyo.

“Mheshimiwa Spika, kuna mwendawazimu mwingine ni mtu anayepiga piga mawe hovyo, mwingine anakuwa mtu wa kuchekacheka, akipita anaweza kuwa anacheka tu ‘kwekwekwe’, na mwendwazimu mwingine ni yule anayeongea ovyo  mbele ya watu wenye heshima zao kama tulivyo humu ndani.

Baada ya Naibu Spika Job Ndugai kuarisha Bunge , imeelezwa kuwa wabunge kutoka Zanzibar waliwahi kutoka nje kumkabili Kessy. Mbunge wa Magogoni, Kombo Khamis Kombo, Sanya Mohammed Sanya na wabunge wengine wa CUF, walimzonga Kessy, kutaka kumpiga.

Kama si uwepo wa baadhi ya wabunge wa CCM walioamua kumuweka kati Kessy, mbunge huyo angepigwa na wabunge kutoka Zanzibar ambao walionyesha dhahiri kukerwa na kauli zake.

Ibara ya 17 (1) Cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 , inasomeka HIvi: " Kila raia wa Jamhuri  ya Muungano anayo Haki ya kwenda  kokote  katika Jamhuri ya Muungano  na kuishi  Katika sehemu  yoyote, kutoka  nje ya nchi na kuingia, na pia haki ya kutoshurutishwa  Kuhama au kufukuzwa  kutoka  Katika Jamhuri ya Muungano.

Sasa kwa mujibu wa Ibara hiyo, tu muulize huyu Mbunge wa Magogoni , Kombo Khamis Kombo, amepata wapi madaraka ya kutaka Kessy azuiwe kwenda Zanzibar? 

HIvi tukisema Kombo Ndie Kinara wa UBaguzi na amevunja  Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977  ya Kutaka Kessy asiruhusiwe kwenda Zanzibar, tutakuwa tumekosea?

 Wale wabunge wa Zanzibar walipaswa watuambie tena kwa njia ya Amani na kuongea bila Ruhusu  ya Spika Ndugai mithili ya watu walipandisha mashetani, Kuwa  Kessy alisema uongo, siyo kwa vitendo vile Vya kiuni walivyovifanya ndani ya Bunge Kwa Kuzua  tafrani  ndani ya bunge na nje ya Bunge bila kufuata Taratibu wakati wao ni Watunga Sheria.

Minamuunga mkono Kessy kwamba baadhi ya Wanzanzibar kwasababu wanazozijua wao wamekuwa vinara wakulalamika  kila kukicha kwamba Wanzanzibar wanaonewa , Mara Muungano uvunjwe,wananyonywa  sana na Tanzania Bara na hawaoni faida ya Muungano na kwamba wabaya tuwaachie Zanzibar Yao.

Sasa kosa la Kessy hapa liko wapi hadi wabunge Hao wazanzibari wamsonge vile?  Kessy amesema ukweli Kuwa ni kweli baadhi ya wazanzibar wamekuwa ni vinara wakilalamika na kutaka uwiano sawa Katika kila jambo la Muungano wakati Zanzibar inachangia kidogo.

Kwani  si kweli Tanzania Bara inachangia pato kubwa Katika Muungano kuliko Zanzibar?Shida inatoka wapi ? Mbona nafasi nyingi za uongozi huko Zanzibar zimeshikwa na wazanzibar Mbona Watanzania Bara hawalalamiki Katika Hilo?

Napata wasiwasi Kuwa uenda wale wabunge waliozua tafrani uenda walikuwa na ajenda Yao nyingine wakasingizia Kessy amewakara.  Maana haiingii akili ni kabisa kilichosemwa na Kessy Ndio kiwapandishe jazba na kutaka kumpiga wakati Kessy aliyoyasema siyo  mambo mapya  na wabunge  hao walishindwa kutoa vielelezo  vinaonyesha  kuwa Kessy aliyosema ni ya  uongo.

Kessy amekuwa jasiri Kati ya wanasiasa wachache wa Tanzania Bara ambao Wengi wao wamekuwa na mtazamo sawa Kama wa Kessy, lakini wamekuwa wakisemea  chini chini  kwa  kisingizio Kuwa wanaogopa kutolewa lugha chafu kutoka kwa  baadhi ya wazanzibar na kuambiwa Kuwa wanataka kuvunja muungano.

Ndio mAana Katika hili Nampongeza Kessy kwa ujasiri  wake wa kulisema Hilo adharani. Na ieleweke wazi tamko Hilo la Kessy Kwa watu wenye akili timamu hawawezi kuona Kauli hiyo ya Kessy it's sababisha   Muungano wetu ambao ni wa mfano  wa kuigwa , ukavunjika au tukasema Kauli hiyo inaashiria kuwabagua Wanzanibar. 

Siku zote Spika Anna Makinda awapo Bungeni amekuwa aliwakumbusha wabunge Kuwa mambo yanayo jadiliwa ndani ya Bunge yaishie ndani ya Bunge,wabunge Hao wajiende kuyajadili nje ya Bunge?

Tuwaulize Hao baadhi ya wabunge toka Zanzibar ambao imeelezwa Kuwa Muda  mfupi baada ya Spika Ndugai kuairisha  Bunge mchana , Mei 27 Mwaka huu, mchana baada ya Muda  mfupi mvutano huo baina wabunge wazanzibari na Kessy Kuibuka ,kumvizia Nje ya Bunge na kuanza kumzonga Kessy, hawaoni walikuwa wanajidhalilisha na kujishushis  heshima zao Mbele ya watu wenye akili timamu na wanao wafahamu na kupuuza agizo Hilo la Makinda?

Kama siyo nongwa na kama gubu la mke mwenza Ni kitu gani? .Jambo limetokea Ndani ya Bunge, Spika Ndugai  akalitolea msimamo ,kwanini wabunge Hao wazanzibari waende laze jambo Hilo nje ya Bunge Kama siyo Nongwa kitu gani?

Hivi Zanzibar na wazanzibari siku hizi wamegeuka Kuwa miungu watu hadi Hawataki wasemwe au wakosorewea? MAana Mifano siyakutafuta, ukisema adharani Zanzibar siyo nchi....utajuta kuzaliwa wakati  Ibara ya 1 ya Katiba ya nchi inasema hivi: " Tanzania ni nchi moja  na ni Jamhuri ya Muungano".

Na Ibara ya 2 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inasomeka hivi: " Eneo la Jamhuri ya Muungano ni eneo lote la Tanzania Bara na eneo lote  la Tanzania Zanzibar, na ni pamoja na sehemu yake ya Bahari Tanzania inapakana nayo."

Lakini kuna baadhi ya wanasiasa uchwara toka Zanzibar kwa sababu wanazozijua wamekuwa wakipotosha ukweli huo kwa kusema Zanzibar ni nchi.Na tungali tukikumbuka Yaliyomkuta Waziri Mkuu Mizengo Pinda ambaye ni msomi wa sheria kutoka kwa baadhi ya wabunge wa siasa kwa hatua yake ya kusema kuwa Zanzibar siyo nchi.

Wasomi wa Sheria tunafahamu Kuwa Zanzibar siyo nchi kwasababu ina kosa sifa ya kutokuwa na huwezo wa kuingia mikataba na mataifa ya nje , haina jeshi, haina sarafu yake .

Na  mwanafunzi wa Sheria akipewa  swali Katika mitihani akiulizwa  Kuwa Zanzibar ni nchi au siyo Nchi, akijibu   Zanzibar ni nchi, basi mwanafunzi Huyo akae akijua amekosa.

Sasa kinachonisikitisha  ni hawa wanasiasa uchwara ambao wanapotosha umma kwa makusudi kwakusema Zanzibar ni nchi kamili wakati si kweli.Tabia hiyo ikome.

Kessy alivyokuwa   akichangia hoja yake Bungeni wiki hii, Alisema   Kwa  zaidi ya Miaka 20 , Zanzibar haichangii Muungano yaliyompata wote ni mashahidi. Mbona hata Kazi iliyofanywa na Mungu ya  uumbaji inasahihishwa na binadamu?

 Mfano Leo hii mwanaume ananibadilishia jinsia yake, wanawake wenye rangi nyeusi wanajipaka mikorogo mikali na Kumeza madawa ili wawe weupe na baadhi ya wanawake wenye Matiti madogo wanaenda mahospitali Makubwa kufanyiwa upasuaji ili wawe na Matiti Makubwa.Wengine wanameza madawa kuongoza ukubwa wa jinsia ya Kiume.

Sasa Kama baadhi ya binadamu tumefika Hatua ya kukosoa Kazi ya Mungu wetu na wala mungu  hapigi  kelele wala kutukana watu,anajua atatuadhibu Kwa  njia gani, kwanini Nyie baadhi ya wazanzibari mnapokosolewa mnatoa lugha chafu, mnataka Kessy asiruhusiwe Kuja Zanzibar? 

Kwani Zanzibar ni Mbinguni au peponi  hadi Kessy akizuiliwa Kuja huko ndiyo itabidi aende Kwenye Moto  wa milele Jehanamu?

Wabunge wetu jifunzeni Kujenga hoja Kwa vielelezo na mjenge  utamaduni wa Kupenda kujisomea  , siyo Kujibu  hoja ya mbunge mwenzio kwa kutumia lugha zisizojulikana na  stahaa, vitisho.

Haisaidii Kwani zaidi ninachokiona Kwa  Mwenendo huo Bunge linatuaribia watoto na Jamii Kwa  ujumla Kwa lugha chafu na vitendo Vya kihuni vinavyofanywa na baadhi ya wabunge ambao Jukumu la kufikiri wamelibinafsisha  na hawataki  kufikiri na kufanya utafiti Kabla ya kujadili mada mbalimbali.

Nasisitiza tena kuwa naupenda Muungano na sipendi Muungano huu uvunjike bila Sababu zisizo na Msingi, ila nilazima wazanzibari Wakubali Kuwa Zanzibar  ni ndogo ukilinganisha na ardhi ya Tanzania Bara pia Hakuna ubishi Kuwa idadi ya wanzanzibar ni ndogo ukilinganisha na Watanzania Bara .

Nawapenda  Wazanzibari , sina  chuki nao na wengine ni marafiki zangu wa karibu na tunaishi vizuri .Na siyo wazanzibar wote ni wakorofi, ni wachache wakorofi ambao ni wanasiasa na wengine wanatumiwa na wanasiasa wenye uchu wa madaraka na wasioutaka Muungano kuleta Chokochoko, na wasivumiliwe watu hawa.

Nimalizie Kwa Kusema kuwa Katika hili Nampongeza  Kessy kwa Ushujaa wake wa Kusema hayo aliyoyasema adharani bila kujificha na alichokisema kuhusu Baadhi ya wazanzibari ni kweli tupu na wala siyo ugomvi,  Kwani kuna watu wanazungumzia hayo aliyoyasema Kessy vichochoroni kwa kisingizio cha Kuogopa kutukanwa na baadhi ya Wazanzibari. 

Kilichofanywa na baadhi ya wabunge kutoka Zanzibar siku hiyo Kwa kisingizio eti Kessy ametoa Kauli ya kuwabagua wazanzibar, ni Cha kiuni na hakikustahili kufanywa na wabunge Hao ambao waliaminiwa na wananchi wao wakawapiga kura lakini Matokeo yake wabunge Hao mapema wiki hii wamejigeuza wahuni wa mitaani na kufanya vitendo vile Vya kihuni.

Mhuni, na watu wasiyojiheshimu   ndiyo wanaofanya vitendo Kama vile lakini Kamwe MTu anayejiheshimu ,Anastaa,  uvumilivu wa kisiasa hawezi kufanya uhuni ule uliofanywa na baadhi ya wabunge wazanzibar. Huo ndiyo ukweli, jirekebisheni, na Muungano wetu unaendelea kudumu na wanaotaka kuuvuruga kwa maslahi Yao binafsi washughulikiwe.

Tuendelee kudumisha Muungano wetu.


Chanzo: Gazeti  la Tanzania Daima la Jumapili ,Juni Mosi Mwaka 2014.












KESI YA PONDA YADODA DAR


KESI YA PONDA YADODA DAR 
Na Happiness Katabazi
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imearisha Kesi ya kuomba Kesi ya uchochezi ilipofunguliwa Katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro isimame hadi rufaa iliyokatwa na Kiongozi wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu, Sheikh Ponda Issa Ponda, kwasababu upande wa mlalamikaji(Ponda), haujapewa majibu  na upande wa jamhuri.

Ponda aliwasilisha mahakamani hapo ombi la Kuomba Mahakama hiyo itoe amri ya Kuzuia Kesi ya ya uchochezi inayomkabili Morogoro ,isiendelee kusikilizwa hadi pale rufaa yake aliyoikata mapema Mwaka Jana ya Kapinga hukumu iliyotolewa Na Mahakama ya Kisutu Mei 9 Mwaka Jana, ambayo ilimtia hatiani Kwa kosa la kuingia Kwa jinai Katika Kiwanja Cha Markas Chang' ombe, ambapo Mahakama hiyo ilimfunga Kifungo Cha nje Cha Mwaka mmoja, lakini Agosti Mwaka Jana, alifikishwa Katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro akikabiliwa na Kesi mpya ya uchochezi na kutenda kosa wakati yupo chini ya uangalizi wa Kifungo Cha Mwaka mmoja nje.

Wakili Mwandamizi wa serikali Bernad Kongora ambapo katika kesi hiyo. Upande wa jamhuri ni mdaiwa, Mbele ya Jaji  Lawrence Kaduri alidai Kuwa Kesi  hiliyo ilikuja kwaajili ya kutajwa na kwamba hata hivyo upande wa Mawakili wa Ponda umedai hapo Tayari kwaajili ya kuendelea kwasababu bado hawajapatiwa Hati kinzani na upande wa jamhuri.

Wakili Kongora alidai wao Tayari walishawasilisha hati kinzani mahakamani ,na kwamba Tayari upande wa jamhuri umewasilisha pingamizi la kupinga ombi Hilo la Ponda na Jaji Kaduri aliarisha Kesi hiyo hadi Juni 16 Mwaka huu, itakapokuja kwaajili ya kusikilizwa, hata hivyo Ponda na kuwepo mahakamani.

Chanzo:www.katabazihappy.blogspot.com
Mei 30 Mwaka 2014.

MKURUGENZI TANESCO,MKEWE KORTINI



Na Happiness Katabazi
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU), ilimfikisha Katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Da es Salaam, aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umeme(TANESCO), William Mhando na Mkewe Eva Mhando pamoja na maofisa wengine wa serikali makosa mbalimbali likiwemo kosa la matumizi Mabaya ya madaraka na kughushi.

Mbali na Mhando na Mkewe ambao wanatetewa na wakili wa kujitegemea Jamhuri Johnson, washitakiwa wengine ni Francis Machalange ambaye ni Mhasibu Mkuu wa Tanesco,Sophia Misidai  ambaye ni Mhasibu Mkuu  na Naftali Kisinga  ambaye ni Ofisa Ugavi wa Shirika Hilo.

Mwendesha Mashitaka wa TAkukuru, Leonard Swai , Mbele  ya Hakimu Mkazi Frank Moshi alidai kosa la kwanza linamkabili Mhando peke yake ambalo  ni kosa la matumizi Mabaya ya madaraka  kinyume na Kifungu Cha 31 haSheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na. 11 ya Mwaka 2007.

Kuwa Kati ya Aprili Mosi na Desemba 31  Mwaka 2011 huko Tanesco makao makuu, Akiwa ni mwajiriwa  na mwenye wadhifa huo wakati akienda majukumu yake Kwa makusudi  alishindwa kutaka maslahi yake kuhusiana na kampuni ya usambazaji wa Santa Clara , kampuni ambayo wakurugenzi wake ni Mke wake Eva Mhando na watoto wake , kitendo ambacho kilisababisha  kampuni ya Santa Clara kupewa mkataba wa kusambaza vifaa Vya Ofisi kwa Tanesco vyenye Thamani sh.884,550,000 KWA kukiuka Maadili ya Tanesco na Sheria ya uongozi wa Maadili ya umma na kusababisha kampuni hiyo kupata faida I siyo halali ya sh. 31,747,000.

Wakili wa Swai akili taja kosa la pili ambalo  ni kwaajili ya Eva Mhando, ni kughushi kinyume na Kifungu Cha 333,337 Cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu ya Mwaka 2002, Kuwa Kati ya Januari 6 na Julai  30 ya Mwaka 2011 , Katika sehemu zisizojulikana ndani ya Dar es salaam,  KWA Dhamira ya kughushi ripoti ya ukaguzi wa mahesabu  kwamba ilikaguliwa na kampuni ya  Finx Capital  House kwamba kampuni ya ya Sant Lara ilikaguliwa Mwaka 2010 jambo alilokuwa akijua ni uongo.

kosa la Tatu ni la kughushi pia ambalo  linamkabili  Eva,  Kuwa Kati Agosti 9 Mwaka 2011 Jijini Dar es Salaam, KWA Dhamira ya kughushi hati ya kuamisha hisa kwa Lengo la Kuonyesha kwamba aliamisha hisa zake 200 zenye Thamani ya sh.10,000 Kwenye kampuni inayoitwa Sant Clara KWA  Eveta John Shing'oma. Huku akijua ni uongo.

Swai alikutana kosa jingine AMBAlo linamkabili Eva kuwa ni la Kuwasilisha Nyakirang'ani za uongo Kinyume na Kifungu Cha 342 ya Sheria ya Kanuni ya Adhabu ya Mwaka 2002, Kuwa Kati ya Agosti 5 Mwaka 2011 , Makao Makuu ya Tanesco, akijua ni uongo aliwasilisha Nyaraka hizo zilizoghushiwa Kwa Katibu wa Bodi yaTenda ya Tanesco, ile taarifa ya Fedha ilikuonyesha  kampuni ya Sant Clara  KWA Kuonyesha kwamba ripoti hiyo ya mahesabu iliandaliwa na Finx Capital Houes ambayo ilikaguliwa taarifa ya Fedha ya Sant Clara Kwa Desemba 2010 suala AMBAlo akijua ni uongo.

SHITAKA la tano KWA Eva ambaye ni Mke wa Mhando,ni la kujatia Fedha KWA njia ya udanganyifu kinyume na Kifungu cha302 chaSheria ya Kanuni ya Adhabu ya mwaka2002', Kati ya Aprili Moja na Oktoba 31 Mwaka 2011, Akiwa Mkurugenzk Mtendaji wa Sant Clara KWA nia ya Kudanganya alijatia sh 31,747,000 kutoka Tanesco kupitia Usambazi wa vifaa Vya ofisi KWA    Tanesco baada ya Kuwasilisha Nyaraka za uongo ambazo ni ripoti ya ukaguzi wa Fedha KWA Mwaka 2007/2008 na orodha ya mi katana mikubwa ya Miaka miwili kuanzia Mwaka 2011  kwa Katibu  wa Bodi ya Tendaya Tanesco Kwa Lengo la Kuonyesha kwamba kampuni ya Santa Clara ilikuwa Imetimiza vigezo Vya awali Vya kupewa Tenda ya usambazaji wa vifaa Vya ofisi KWA Mwaka 2011 KWA Tanesco.

Kosa la Sita KWA kwaajili ya mshitakiwa Francis Mchalange, Sophia Misidai na Naftali Kisinga.ALILItaja kosa Hilo Kuwa ni la matumizi Mabaya a madaraka kinyume na Kifungu Cha 31 Cha Kupambana na Kuzuia Rushwa ya Mwaka 2007.

Kuwa  Oktoba  17 Mwaka 2011,  Katika Makao makuu Tanesco, wakiwa ni waajiliwe wa Tanesco Kama Wahasib wa Kuu wa Tanesco na Afisa Ugavi , na wakiwa wajumbe wa Kamati  ya Kutathimini Tenda Na. PA/001/11/HQ/G/011 kwaajili ya usambazaji wa OFISI KWA Mwaka wa Fedha Kama ilivyopitishwa na Mtendaji Mkuu wa Tanesco Katika kutekeleza majukumu Yao, KWA kukusudia walitumia vibaya madaraka Yao KWA kutoa maelezo ya uongo kwa avoid ya Tenda KWA  Lengo la Kuonyesha Kuwa Kampuni ya Sant Clara ni kampuni bora na inavigezo ambayo ilistahili kupewa hiyo Tenda kusambaza vifaa Vya ofisi hapo Tanesco ,kitendo kilichosababisba kampuni ya Sant Clara kupewa kampuni ya kusambaza vifaa Vya ofisi Kwa Tanesco, vyenye Thamani ya sh 884,550 ,000 KWA kuvunja Sheria na kufanya kampuni ya Sant Clara kujipatia faida I siyo halali kiasi Cha sh 31,747,000 na kwamba upelelezi wa Kesi hiyo umekamilika.

Hata hivyo washitakiwa wote walikana Mashitaka na Hakimu Moshi Alisema ili washitakiwa wa late dhamana ni lazima kila mmoja awe na wadhamini Wawili wa kuaminika ambao watasaini bondi ya Sh.milioni nane kwa kila mmoja na kwamba mshitakiwa yote hata ruhusiwa kutoka  nje ya Dar e salaam bila Kibali, na washitakiwa Hao walitimiza Masharti hayo lakini Wakili Swai aliomba Mahakama. Iarishe Kesi Kwa MUDa ili waende kuakiki barua za wadhamini na Hakimu Moshi akaamuru washitakiwa wapelekwe mahabusu ya Mahakama hiyo hadi saa Saba mchana ili Mahakama ije kuona Kama wadhamini Hao wanataka Katika Ofisi  walizozisema.

Ilipofika saa Saba washitakiwa Hao walirejeshwa tena kizimbani ambao Wakili Takukuru, Swai alidai Kuwa Tayari wameishakamilisha uchunguzi wao kuhusu barua za wadhamini wa washitakiwa na kwamba ni kweli wadhamini Hao ni wadhamini wa kuaminika na kuomba Mahakama iwapatie DHA

KWA upande wake Hakimu Moshi aliwapatia DHAMANA washitakiwa Hao na akaairisha Kesi hiyo hadi Juni 13 Mwaka huu, Kesi hiyo itakapokuja kwaajili ya washitakiwa kusomewa maelezo ya awali.

Katika hatua nyingine wafanyakazi wa Tanesco ndio wamejitokeza kuwadhamini washitakiwa wote isipokuwa mshitakiwa Machalange naye mdhami Mmoja aliyemdhamini ni mfanyakazi wa Tanesco na mmoja ni mtumishi wa mahakama.

Chanzo: Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Mei 27 Mwaka 2014.