MABOSS IMTU KIZIMBANI. DPP AWAFUTIA KESI,WAKAMATWA TENA


MABOSS IMTU KIZIMBANI,DPP AWAFUTIWA KESI,WAKAMATWA TENA 
Na Happiness Katabazi
WAHADHIRI  wanne wa Chuo Kikuu Cha  Tiba Cha 
 IMTU ,Mbezi Dar es Salaam, wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni wakikabiliwa na makosa  mawili likiwemo kosa la  la kushindwa
Kufukia  viroba 83 vya viungo Vya binadamu. 

Mwendesha Mashitaka Mwandamizi wa Polisi Magoma Mtani Mbele ya Hakimu Kwey Rusemwa aliwataja washitakiwa Hao Kuwa ni   aliwataja washitakiwa Hao Kuwa ni   Venkat
Subbaiah(57),  Appm Shankar Rao (64), Prabhakar  Rai(69), Dinesh
Kumar(27).

Magoma alidai kuwa washtakiwa hao Julai 2014 katika eneo la Mpigi
Majohe  walishindwa  kufukia viroba 83 vya viungo vya binadamu
waliyoitumia kufundishia wanafunzi wa udaktari kinyume na kifungu cha
128 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu ya Mwaka 2002.

Alidai kuwa  washtakiwa hao kwa pamoja pia walishindwa kuandaa hati
kwa kampuni ya Corona  ya kuthibitisha  kufukiwa kwa mabaki hayo na washitakiwa walikana Mashitaka hayo na upande wa jamhuri ukadai upelelezi bado haujakamilika.

Hakimu Rusema Alisema ili washitakiwa wapate dhamana ni kila mshitakiwa awe wadhamini wawili ambao ni watanzania na
wanaofanya kazi kutoka kwenye taasisi zinazotambulika kisheria.

Kutokana na masharti hayo ya dhamana washtakiwa watatu waliyakamilisha
lakini mmoja wao alishindwa kuyakamilisha baada ya kuwa na mdhamini
ambaye si  raia wa Tanzania.

Wakati Taratibu hizo zikiendelee  , Wakili wa Serikali Salum Ahmed aliingia
mahakamani hapo na kuiomba mahakama kuifuta kesi hiyo chini ya kifungu
cha 91 (1) cha Mwenendo wa Mashauri ya Jinai (CPA) ya Mwaka 2002 kwa kuwa
Mkurugenzi wa Mashtaka  (DPP)   hana nia ya   Kuendelea na Kesi hiyo ambayo il ifunguliwa Jana Alasiri mahakamani hapo. 

Baada ya kuwasilishwa kwa ombi hilo, Hakimu Kwey Rusemwa aliwaachia
huru washtakiwa  hao, lakini muda mfupi baadaye walikamatwa na askari
wa jeshi la polisi na  kuwekwa chini yaulinzi mkali.

Baada ya Polisi kuwakamata washitakiwa Hao waliwekwa chini ya Ulinzi  baada ya muda mfupi   baadae walipandishwa Kwenye  gari  aina
ya Toyota Land Cruser lenye namba za usajili KXO 6 EFY na Toyota RV4
lenye namba za usajili T366 AVG na kuondoshwa Katika eneo Hilo la Mahakama na kupelekwa POLISI ambapo hadi waandishi wa Habari unaoendoka hatukuweza kufahamu wameenda kuifadhiwa Katika Kituo gani Cha POLISI. 

Wakati washtakiwa hao wanaotetewa na  Wakili   Gaudiosus Ishengoma
wakiwa chini ya ulinzi, wakili wao huyo alionyesha hali ya
kusikitishwa kwa kitendo hicho na kudai kuwa DPP aliwafutia mashtaka
wateja wake na kuwaachia huru ili awafungulie mashtaka mengine ambayo
hayana hata dhamana.

Chanzo: Facebook. WwwHappy Katabazi. Julai 29 Mwaka 2014

DPP:FELESHI: TUNATOA HAKI SI KUFUNGA WATU



DPP:FELESHI TUNATOA HAKI SI KUFUNGA WATU

Na Happiness Katabazi
" KATI ya Februali na Juni Mwaka huu, serikali katika kesi za jinai inawakilishwa na ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP),  imeweza kushinda jumla ya Kesi za jinai  259 Katika Mahakama zote nne za Mkoa wa Dar Es Salaam na ikajikuta imepoteza ushindi  kesi 76"

Takwimu hizo zimetolewa Jumatano ya wiki hii na Mkurugenzi wa Mashitaka(DPP), Dk.Eliezer Mbuki Feleshi Katika mahojiano Maalum na Tanzania Daima Jumapili,  ofisini kwake  jijiini Dar es Salaam, ambapo anasema  ushindi huo mnono umetokana na utendaji mzuri baina mawakili wa serikali, wapelelezi wa kesi  na mashahidi ambao walifika mahakamani kutoa ushahidi madhubuti ambao mwisho wa siku ulishawsii mahakama hizo kutoa hukumu za kuwatia hatiani washitakiwa na kuwaachilia huru.

Dk.Feleshi ambaye ni mtaalamu wa Sheria za makosa ya jinai, anazitaja Mahakama hizo Kuwa  ni Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar Es Salaam, Mahakama ya Wilaya ya Ilala, Temeke, Ilala na Kinondoni.

Anasema ofisi ya DPP inaendeshwa kwa mujibu wa Ibara ya 59B ya katiba a Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, Sheria  ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya Mwaka 2002 kuanzia kifungu ha 89 . Sheria ya Uendeshaji wa Mashitaka ya Taifa (NPS) ya Mwaka 2008


Anasema  Katika Kipindi Cha Februali  Mwaka huu, Kesi 98 za jinai washitakiwa walitiwa hatiani, Kesi 10 washitakiwa walishindwa Kesi , Kesi 31 zilifutwa,  Kesi Tisa ziliondolewa na  jumla ya Kesi zilizoisha Katika mwezi huo jumla zilikuwa  148.

Aidha Dk.Feleshi  alisema  Katika Kipindi Cha Juni Mwaka huu, Katika Mahakama zote hizo Katika Kesi za za jinai 161 washitakiwa walikuwa wakikabiliwa Katika Kesi hizo 161 walitiwa hatiani, Kesi Tisa washitakiwa waliachiriwa Huru na Mahakama baada ya kushinda Kesi hizo, Kesi 26 zilifutwa na Mahakama, Kesi  mbili  aliziondoa mahakamani baada ya kuona Haja ya kuendelea nayo na hivyo kuwafanya jumla ya Kesi 198 zilizoisha malizika Katika kipini Cha Juni Mwaka huu.

Akianisha idadi hizo za Kesi kila Mahakama zilizofunguliwa na kumalizika, Dk. Feleshi anasema Februali Mwaka huu Katika Mahakama ya Wilaya ya Temeke,Kesi 36 washitakiwa walitiwa hatiani,  Kesi nne washitakiwa waliachiliwa Huru, Kesi Tisa zilifutwa na jumla ya Kesi 51 zilimalizika Katika Mahakama hiyo ya Temeke.

Kwa upande wa Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni , serikali ilishinda jumla ya Kesi 37, ikashindwa Kesi Tatu  ambapo washitakiwa waliachiliwa Huru na Mahakama baada ya kuona upande wa jamhuri umeleta ushahidi dhahifu, Kesi 10 zilifutwa, Kesi nne  ziliondolewa na hivyo kufanya jumla ya Kesi 54 kumalizika Katika Mahakama Wilaya ya Kinondoni Katika Kipindi Cha Februali Mwaka huu.

Katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala, anasema serikali uliweza kushinda jumla ya Kesi 22, Hakuna mshitakiwa aliyeshitakiwa Kesi , Kesi 12 zilifutwa,na Kesi Moja iliondolewa na hivyo kufanya jumla ya Kesi za jinai 35 kumalizika Katika Kipindi hicho.

Anasema Katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar Es Salaam, serikali iliwza kushinda jumla ya Kesi Tatu, Kesi Tatu washitakiwa waliachiliwa Huru , Hakuna Kesi iliyokuwa  na Kesi mbili ziliondolewa na hivyo kufanya jumla ya Kesi nane kumalizika.

Katika Kipindi Cha Juni Mwaka huu, Dk.Feleshi  anasema  Katika Mahakama ya Wilaya ya Temeke, serikali ilishinda Kesi 45 kwa washitakiwa Kutiwa hatiani, Kesi mbili washitakiwa waliachiliwa huru, Kesi 13 zilifutwa, Kesi mmoja iliondolewa  na hivyo kufanya jumla ya Kesi 61 kumalizika.

" Katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni , upande wa jamhuri ilishinda jumla ya Kesi  30 , ikashindwa Kesi mbili , Kesi Tatu zilifutwa, Kesi Moja iliondolewa na hivyo kufanya Jumla ya Kesi za jinai 36 kumalizika" anasema Dk.Feleshi.

Aidha katika  Mahakama ya Ilala , upande wa jamhuri ilishinda Kesi 71, ikashindwa Kesi nne, Kesi sana zilifutwa na Hakuna Kesi iliyoondolewa na hivyo  kufanya jumla ya Kesi 82 kumalizika na kwamba Katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu , upande wa jamhuri ilishinda Kesi 15, ikashindwa Kesi Moja na Kesi Tatu zilifutwa  na Hakuna kesi iliyoondolewa na hivyo kufanya Katika Kipindi Cha Juni Mwaka huu, jumla ya Kesi 198zilimalizika.

' Kwa takwimu hizo hapo ambazo ni za Miezi Miwili tu zinathibitisha wazi kabisa upande wa jamhuri umeweza kushinda idadi kubwa ya Kesi ilizozifungua ambazo ni 259 na imeshindwa Jumla ya Kesi 19 Kati ya Februali na Juni Mwaka huu...sasa Huwa na washangaa sana wale watu ambao Kutwa wamekuwa wakitupoka bila Kuwa na ushahidi Kuwa serikali imekuwa ikishindwa Kesi nyingi mahakamani" anasema Dk.Feleshi.

" Minapenda kuongea na vyombo Vya Habari Kwa kutumia takwimu halisi ambazo zisizo za kupikwa....sasa Hao wanasema Kuwa kila siku upande wa serikali umekuwa  kila kukicha unashindwa Kesi zake mahakamani bila kutoa takwimu uwa nawashangaa sana ., ni kweli kuna baadhi ya Kesi serikali inashindwa lakini wakumbuke Ofisi ya DPP ipo kwaajili ya Kutenda Haki na siyo kutaka mshitakiwa aitwe hatiani hatakama Hakuna ushahidi:

" Ofisi ya DPP, Mahakama unafanyakazi Kwa kutumia vitabu Vya Sheria na siyo hisia na kufuata kelele za watu barabarani wanaotaka serikali Ishinde Kesi bila watu Hao kuisaidia ofisi a DPP Kama kwa Kuwaletea ushahidi mzuri Katika Kesi mbalimbali ili serikali ishinde Kesi. Na Mahakama itamtia  hatiani mshitakiwa baada ya kuridhishwa  na ushahidi na sio kelele za mitaani zinazopigwa na baadhi ya watu wanataka watu watiwe hatiani hata Kama Mahakama inaona haina Haja ya kufanya hivyo" anasema  Dk.Feleshi.

Hata hivyo anasema  ofisi yake HIvi sasa kupitia Kanda zake zote nchini zitaanzisha  utaratibu wa kutoa takwimu za Kuonyesha ni Kesi ngapi serikali ilizifungua mahakamani kwa kila baada ya Miezi mitatu, na serikali ikashindwa Kesi ngapi, imeshinda Kesi ngapi, Kesi ngapi zimeondolewa, na ngapi zimefutwa  ili umma uweze kufahamu ukweli ni upi na mpotoshaji na mwenye Lengo la kupaka Metope serikali Katika Jamii ni nani Kwani HIvi sasa imejengeka tabia ya watu kuzungumza Kuwa serikali imekuwa ikishindwa Kesi nyingi mahakamani bila kutoa takwimu KWA umma Hali inaosababisha umma kuamini  upotoshaji huo.

" Naniachokiona HIvi sasa baadhi ya Kesi ambazo zimekuwa zikiliripotiwa sana na vyombo Vya Habari ikitokea serikali ikishindwa basi baadhi ya watu wanaanza kusema serikali inashindwa Kesi kila siku....ni kweli kuna baadhi ya Kesi ambazo zimekuwa zikivuta hisia za watu Wengi serikali imeshindwa ila kuna Kesi nyingi sana serikali imeshinda ambazo wananchi na Nyie waandishi wa Habari hamzijui na wala hamtaki kuziripoti, serikali imeshinda na rekodi zipo Katika OFISI yangu na Mahakama zote nchini" anasema.
 
Swali: Kwa nini magereza hayaishi
wafungwa?

Jibu: Maana  yake watu kila kukicha wanafungwa.

Swali : Je mshitakiwa kufungwa au kukutwa na hatia na mahakama ni lazima?
Jibu: Hapana  kama ushahidi hautoshi ni haki
ya mtu kuachiwa huru. 

Swali: Je mahakama ni lazima kuendelea na kesi
hata kama kuna kitu kimetatiza?

Jibu: Sio  lazima, mahakama yaweza
kufukuza mashtaka hadi mashahidi wapatikane kama kesi
imekaa muda mrefu bila mashahidi kutokea, hivyo hivyo Jamhuri
inaweza kuiondoa kesi mahakamani pale inapokuwa na sababu
za kufanya hivyo. 

Swali: Je Jaji Mstaafu Mark Bomani  alipowatuhumu mawakili wa serikali siku hizi wamekosa weledi katika tasinia ya uendeshaji wa mashitaka na ndiyo maana serikali hivi sasa imekuwa ikishindwa kesi kila kukicha,alikuwa sahihi?

Jibu: Hapana  wote Jaji Bomani ambaye nae aliwahi Kuwa DPP, aliongea Hilo kwa nadhalia   na vitu vya kufikirika  tu ndiyo maana hakutoa  takwimu japo yupo sawa  kama dhana ni kwamba kila kesi ikienda mahakamani upande wa 
Jamhuri itawalazimisha au kuwashawishi kutoa ushahidi
ilimradi mtu afungwe. 


Chanzo: Gazeti la Tanzania Daima Jumapili, Julai 27  Mwaka 2014

MAKUWADI WA WAGOMBEA URAIS CCM WADHIBITIWE








Na Happiness Katabazi
TANZANIA ni nchi ambayo wananchi wake kwa ridhaa yao waliamua taifa Lao liongozwe kwa utawala wa Sheria na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977.

Sisi wasomi wa fani ya Sheria tunasema Katiba ndiyo Sheria  mama na inapotekea Kifungu chochote Cha Sheria nyingine kina kwenda kinyume na Ibara yoyote ya Katiba , basi Kifungu hicho kitahesabika na Mahakama Kuwa ni Kifungu  batiri Kwani kina kwenda kinyume na Ibara Fulani ya Katiba ya nchi yetu.

Mapema wiki iliyopita Jaji Joseph Warioba aliibuka na kutaja sifa za mgombea urais ambaye anafaa kuiongoza  Tanzania baada ya uchaguzi Mkuu kumalizika Mwaka 2015. Miongoni mwa sifa alizozitaja Jaji Warioba alisema rais ajae awe kijana, wazo ambalo zimezua mjadala wengine wakimuunga mkono wengine wakimpinga.

Na Kwa upande mwingine naweza Kusema Kuwa mtazamo huo wa Warioba ndiyo Kama umewazindua usingizini makuwadi wa kambi za wagombea urais wa mwaka 2015 ambapo ni kweli makuwadi hao wamezinduka nakuanza kutumia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kuwafagilia wagombea wao watarajiwa wa kiti ha urais na kuwasiliba makada wa CCM ambao wanatajwatajwa kugombea urais.

Na sisi waandishi wa Habari  tusipokuwa makini na hawa baadhi ya wanasiasa uchwara wetu wa hapa nchi na makuwadi wao,  tutajikuta kuanzia wiki iliyopita hadi Oktoba  mwakani, tutajikuta vyombo vyetu vya habari tunashindwa kuchapisha Habari  za kuchochea maendeleo ya nchi  na Matokeo   yake tunaanza  kununuliwa na kukubali kuchezewa akili zetu na makuwadi wa wagombea watarajiwa wa Kiti Cha urais  Kuwa tunazipa kipaumbele Habari za Kuwafagilia wagombea wao.

Tuwe macho na mchezo huu machafu, Kwani binafsi Nina  uzoefu na hili Kwani Kipindi kile Cha kuelekea mchakato wa kumpata rais wa Mwaka 2005, Nilikuwa ni mwandishi wa gazeti la Mtanzania enzi Waliokuwa makuwadi wa wagombea urais Mwaka 2005 ,walianza mapema kuwaweka  mifukoni baadhi ya wahariri na waandishi  na hatimayeKukazuka misuguano ndani ya vyumba Vya Habari wa baina ya baadhi wahariri na wahariri kwa kushinikiza  baadhi ya wahariri wachapishe Habari na makala za kuwapamba wagombea urais wao.

Ibara ya 39(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 , inaanisha wazi sifa  za mtu  kuchaguliwa Kuwa   Rais wa Tanzania.

Ibara 39(1) (a) ni raia  wa kuzaliwa wa Jamhuri  ya Muungano kwa mujibu  wa Sheria  ya Uraia;
(b) Ametimiza  umri wa Miaka  arobaini:
(c) ni Mwanachama , na  mgombea  aliyependekezwa na Chama Cha siasa;
(d) ambazo sifa  za kumwezesha kuwa Mbunge  au Mjumbe  wa Baraza  la Wawakilishi; 

(e) Katika  Kipindi cha Miaka  Mitano  Kabla  ya Uchaguzi  Mkuu hajawahi  Kutiwa  hatiani Katika  Mahakama  yoyote  kwa kosa lolote  la kukwepa  kulipa  kodi yoyote  ya Serikali.

Ibara 39(2) Bila  ya kuingilia haki  na Uhuru  wa mtu  Kuwa  na  yake , kuamini dini atakayo, kushirikiana na wengine na kushiriki shughuli  za umma kwa mujibu  wa Sheria  za nchi , mtu  yeyote  hatakuwa  na sifa  za kuchaguliwa  kushika  Kiti Cha Rais wa Jamhuri ya Muungano  Kama Si Mwanachama na mgombea aliyependekezwa na Chama Cha siasa":

Ni kweli Ibara  ya 18 (a) ya Katiba ya nchi inasema ' kila mtu  anao Uhuru wa Kuwa na maoni na kueleza  fikra zake'.

Lakini je huu ni wakati mwafaka wa wazee wetu hawa kujitokeza adharani Kusema mgombea urais wa Mwaka 2015 awe kijana?  Hivi Ibara ya 39 ya Katiba inasema mgombea urais ajae awe ni kijana?. 

Huyo mgombea urais kijana Mbona basi hatuambiwi  ujana wake ni wa umri gani? au Tayari Katiba mpya imeishapatikana na Ibara ya kuruhusu mgombea urais kijana imeisha wekwe na imeanza kufanyakazi? Maana Ibara ya 39(1) (b) inasema mgombea urais awe Ametimiza Miaka 40. 

Binafsi mtu yoyote atakayeapishwa na Jaji Mkuu wa Tanzania baada ya uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015 kumalizika Kuwa ndiye rais wa Tanzania , minitamuunga mkono na nitamkubali Kuwa ndiye rais wa nchi yangu.

Lakini tujitazame sasa nchi yetu HIvi sasa inaelekea Kwenye Uchaguzi wa serikali za mitaa, badala ya kuamasisha wanachama wa vyama vyao na wananchi kwa ujumla kushiriki uchaguzi huo wa serikali za mitaa badala yake wazee wetu Hao wanatoa matamshi ambayo ni wazi yameibua misuguano Katika kambi za wagombea urais watarajiwa.

Minafikiri ni jambo Jema kwa sasa Kwa  vyombo Vya Habari kutoa kipaumbele kwa kuchapisha Habari za kuamasisha maendeleo zaidi na kuibua maovu na kutoa dira Katika mambo mbalimbali na kupaza  sauti za wanyonge kupitia kalamu Zenu, hawa " wanasiasa uchawara' wanaotumia makuwadi wao  ambao hivi sasa wamekuwa wakiwasaka waandishi wa wawaingize  kwenye kambi  zao kwa njia mbalimbali .

Makuwadi hao wengi wao wakiwa ni wanaume moja ya mbinu chafu wanayotumia kuwateka waandishi wajiunge na kambi zao ni fedha na kujaribu kuanzisha ghafla mahusiano ya kimapenzi na waandishi wa kike ambao wanachama waandishi Hao watawasaidia Katika kambi zao.

 Makuwadi hao  ambao HIvi sasa wa kujiunga  kwa Wingi  Kwenye  Facebook kwa majina yao halisi na ya kufikirika na kuomba  Kwakasi urafiki kwa waandishi wa habari ambao nao wamejiunga na facebook  ili kila siku wawe wanafanya mawasiliano na baadhi ya waandishi ili wajenge ukaribu kupitia facebook na kupata taarifa mbalimbali za kila siku za mwandishi husika na waandishi wengine, kutufuatilia nyendo zetu wanahabari eti tutakutanaga na watu gani, tu napenda nini, Mara wajisemesha wanataka kuanzisha magazeti hivyo wanataka waandishi wanaowataka wao wawapate mbinu za kitaaluma za jinsi ya kuanzisha magazeti na kutuahidi mishahara minono.

Kwa Bahati Mbaya au nzuri kuna baadhi ya waandishi wa Habari , Njama hizi za makuwadi hawa bado hawajazibaini  ila kikubwa Cha makuwadi hawa wanachokitaka hasa ni Kuwa karibu na Waandishi wa Habari ili waweze Kuwa wanapata taarifa zinazohusu kambi za mahasimu zao Kwani wanaamini nao Hao mahasimu wao nao wanatumia waandishi wa Habari na waandishi wa Habari tunasifika kwa sifa ya kutojua kutunza Siri na sifa hiyo imekuwa Ikitimiza kikamilifu na makuwadi wa kambi za wagombea urais kushikishana adabu.

 Ukimtazama Huyo mtu  anayemfuata  Mwandishi Kuwa eti anataka kuanzisha Gazeti, hafanani kabisa na hayo anayosema.Ni vichekesho vitupu. Ni hatari sana na Ujinga wa aina yake mgombea urais mtarajiwa kwa sasa kuwatumia makuwadi wake wa msafishe jina na wampambe na kuumuuza kupitia vyombo Vya Habari na Mitandao ya kijamii.

Mbinu  hii jamani ilishapitwa na wakati Kwani sio kila mbinu aliyoitmia  Mtu Fulani kufanikisha jambo Fulani kwa  wakati Fulani akafanikiwa kupitia mbinu hiyo, halafu na wewe Leo hii Katika mazingira yaliyokwisha badilika na wewe unaamua kutumia mbinu ile ile aliyotumia mwenzio Miaka 10 iliyopita  utafikiri unaweza kufanikiwa. Unaweza usifanikiwe Kwani kila zama na kitabu Chake jamani.

Tena kaunzia sasa serikali kupitia Idara ya Habari Maelezo iwe macho na Katika kutoa vibali Vya kusajiliwa magazeti mapya Kwani hawa makuwadi wa wanasiasa haw ashindwi kuanzisha magazeti kwaajili ya Kazi Moja ya kuchapisha Habari za kuchafua wagombea wenzao kwa kuzuliana Habari za uzushi na kampeni zikiisha magazeti Yao wanafunga.

Kambi yoyote ya mgombea urais HIvi sasa inaona  silaha  yake kubwa ya kupata ushindi ndani ya CCM ili apitishwe Kugombea urais, ni kambi iliyofirisika kimkamati mapema.

HIvi Karibuni Kamati ya Maadili ya CCM, ilitoa Adhabu kwa wanachama wake Kadhaa ambao iliwakuta na hatia ya kufanya kampeni za ugombea  urais Kabla ya wakati na ikawaweka chini ya uangalizi....lakini sasa Mbona HIvi Karibuni tumemsikia Naibu Waziri wa Mawasiliano , Sayansi na Teknolojia , January  Makamba Akisema Kuwa atagombea .

Hakuna Sheria ya nchi inayombana MTu kutangaza Mapema nia yake ya Kugombea urais Kabla ya wakati lakini Kamati ya Maadili ya CCM, iiliwatia hatiani akiwemo Edward Lowassa, Bernad Membe na wengine kwa maelezo Kuwa wamekiuka Maadili ya CCM kwa kufanya matendo yanayoonyesha wameanza kampeni mapema, sasa tuiulize CCM, Makamba haijamsikia ?Au Kunya anye Kuku akinya Bata Kaarisha ?

Maana Membe,Lowassa na wagombea wengine hadi sasa Hawajawahi kujitokeza adharani kutamka  Kuwa watagombea urais na walichukuliwa ikiwemo kupewa onyo Kali.

Ila  kilichopo mitaani na ndani ya vyumba Vya Habari ni kushuhudia  baadhi ya watu wanaojitambulisha Kuwa wapo karibu na Lowassa na Membe  kuwa makada hao maarufu ndani ya CCM na wapo 'msituni' wanajifua kimya kimya   na kwamba watagombea urais Mwaka 2015.Tusubiri Tuone.

Minasema yote Kheli  na MUNgu hawatangulie ila kinachonikera ni hawa makuwadi wa baadhi ya watu wanaotajwa  Kugombea urais kuanza  mapema  kuwapigia chapuo wagombea wao na kuanza kutumia mbinu chafu za kuwachafua wagombea wenzao kupitia vyombo ya Habari na Mitandao  ya kijamii wakati bado muda rasmi wa kuanza kampeni haujatangazwa. 

Hata hivyo kuna taarifa zisizo rasmi huku mitaani zinadai Kuwa hawa vijana wanatajwatajwa Kugombea urais ni danganya toto na kwamba Hao vijana ( siyo Makamba) wanatumika Kama Chambo na baadhi ya makada maarufu wa CCM ambao Tayari kila kukicha wanatajwa Kuwa watagombea urais, ili wapoteze Lengo na hatimaye wananchi waanze kuwajadili vijana Hao Kumbe vijana Hao wanakazi Maalum ya kuwakinga wagombea husika wasizongwe kwa wakati huu na wananchi. Ipo siku Mungu  ataanika ukweli.

Ikumbukwe kuwa  miongoni mwa hawa walio jitokeza adharani HIvi sasa   kupendekeza eti rais ajae awe ni kijana, alipo ingia ramsi madarakani Rais Jakaya Kikwete,  Desemba 21 Mwaka 2005  , baadhi yao ndiyo waliokuwa wa kwanza kuinanga serikali inayoongozwa na rais (Kikwete), ambaye tuliaminishwa kuwa ni rais kijana.

Kwa Kuwa  Rais Kikwete ni   " Mkubwa wa Akili'  , aliwapatia madaraka mbalimbali karibu wote Waliokuwa wakosoaji wa serikali yake na walivyokosa haya wakosoaji  hao walikubali madaraka hayo kwa mikono miwili , wakachekelea   waliyopewa na rais Kikwete ambae alivyoingia madarakani walikuwa wanamuita ni rais ' mhuni, msanii, cheki bobu  na hana akili na hataweza kuingoza Tanzania na ni rais anayependa kuchekacheka ovyo ovyo hata Katika mambo yasiyostahili kucheka".

Waliokuwa wakimdhihaki Kikwete Wengi walikuwa wakiwaunga mkono waliokuwa wagombea wao wa urais Katika kampeni za uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2005" wagombea wao walishindwa.

 Wakaanza  kulipa kisasi kwa kuikosoa serikali ya awamu ya Nne inayoongozwa na Rais Kikwete,  lakini Kumbe serikali ya Kikwete nayo ilikuwa na vijana wake Kama Amos Makalla ambaye kwasasa ni Naibu Waziri wa Maji, walianza kujibu mapigo kwa wakosoaji wa serikali ya Kikwete na mwishowe Kikwete alikuja kuwatea wakosoaji Katika Nafasi mbalimbali ikiwemo Bunge la Katiba, Tume ya Marekebisho ya Katiba iliyokuwa Ikiongozwa na Jaji Warioba.

Hivyo serikali, CCM, Watanzania wote tuwe macho na watu wa haina hii Kwani Tusikubali kuruhusu msuguano huu uanze sasa kushika kasi tena kupitia vyombo Vya Habari ni wazi hata Habari za kimaendeleo kwa ujumla wake ,  habari kuhusu jinsi vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vinavyofanya kazi ya kuwadhibiti wahalifu  na kuakisha nchi yetu naendelea kuwa na amani na usalama, uchumi wetu, Kilimo, elimu sitakuwa hazisikiki kwa mapana yake Matokeo Habari za wagombea urais Mwaka 2015 ndiyo zitakuwa zinabeba uzito Kwenye vyombo Vya Habari. Tusikubali wendawazimu huu na Hao makuwadi wadhibitiwe mapema mAana siku zote wapambe wana Nguvu  kuliko wenye Mali.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika
Chanzo: www.katabazihappy.blogspot.com
Facebook: Happy Katabazi
Julai  8 Mwaka 2014.
Simu: 0716 774494


KESI YA KUPINGA UCHAGUZI TIMU YA SIMBA YATUPWA





KESI YA KUPINGA UCHAGUZI SIMBA YATUPWA
Na Happiness Katabazi
HATIMAYE Mahakama Kuu Kanda ya Dar Es Salaam, imekataa kutoa amri ya Muda ya Kuzuia kufanyika kwa uchaguzi Mkuu wa Simba ulipangwa kufanyika Kesho ,kwasababu Maombi hayo  ya zuio yaliyowalishwa jumahtatu wiki hii na wanachama watatu wa simba, hayapo mAhakamani hapo kisheria.

Uamuzi huo uliokuwa ukisubiriwa kwa shahuku kubwa na wapenzi wa Soko nchini, uliotolewa Jana saa Kumi jioni Na Jaji Augustine Mwarija  ambaye Alisema amesikiliza hoja za pande zote mbili tangu Jana asubuhi na kwamba Mahakama yake imejiridhisha pasiposhaka Kuwa ombi Hilo la zuio halipo mahakamani kisheria hivyo Mahakama yake haiwezi kutolea uamuzi ombi lolote ambalo halipo mahakamani kisheria.

Jaji Mwarija Alisema licha la ombi Hilo la zuio kutokuwepo mahakamani kisheria pia ombi Hilo la zuio Kabla ya wakati  na kwamba kisheria huweZi kuleta ombi la zuio la MUDa wakati Hakuna Kesi ya Msingi ilipofunguliwa mahakamani na kwamba kwa shauri Hilo la wanachama Hao wa simba , bado hawajafungua Kesi ya Msingi ila wamewasilisha ombi la kuomba Mahakama Iwapo Kibali Cha kuwaunganisha wanachama wengine 66 ili nao wawe walalamikaji Katika Kesi ya Msingi ya kumshitaki Mwenyekiti wa simba KWA kuvunja Katika na kwamba hadi Jana asubuhi ombi Hilo la kuomba wanachama Hao kuunganishwa lilikuwa halijasikilizwa.

" Sasa Kwa Kuwa katika Mahakama hii wanachama Hao watatu walikuwa bado hawajafungua Kesi ya Msingi Mahakama hii haiwezi kukubali kutolea maamuzi Maombi Yao ya zuio la MUDa kwasababu kisheria huwezi kutoa amri ya zuio la Muda bila ya kuwepo Kesi ya Msingi mahakamani na hata hivyo ombi hili la zuio la Muda limewasilishwa Kabla ya wakati na kwasababu hiyo Mahakama hii inayatupilia Mbali Maombi ya zuio la MUDa"Alisema Jaji Mwarija.

hata hivyo uamuzi huo ilisababisha wanawake Wawili wanaodaiwa Kuwa ni wanachama wa simba ,walizirai mahakamani hapo na Kisha Kubebwa na kuingizwa Kwenye Gari na kuondolewa Katika eneo Hilo la Mahakama.

Akizungumzia uamuzi huo wa Mahakama, Wakili wa wadaiwa , Juma Nassor Alisema amesikitishwa na uamuzi huo Kwani haulengi kuleta umoja na Amani Katika TIMU ya simba.

Kabla ya Maombi ya zuio la Muda kuanza kusikilizwa Jana ,  Jaji Mwarija alianza kusikiliza ombi  la Mwanachama mmoja wa Simba, Shaban Omar ambaye alikuwa akitetewa na Wakili Jerome Msemwa  lilokuwa liloomba Mwanachama Huyo aunganishwe na awe miongoni mwa wadaiwa katika Kesi hiyo lakini hata hivyo Jaji Mwarija Jana muda mwingi alilazimika Kuwafundisha matakwa ya Sheria yanasemaje na alimwambia Msemwa ombi Hilo la Mteja wake limeletwa wakati siyo mwafaka, ushauri ambao baadae Wakili Msemwa alikubaliana na ushauri wa jaji Huyo na Akaamua kuliko ndoa ombi hilo.

Ombi la Kuzuia uchaguzi kilianzia kusikilizwa Jana saa nne asubuhi,  Wakili wa walalamikaji Revocatus Kuuli alianza kwa kuiambia Mahakama Kuwa wamewasilisha Maombi mawili ,ombi la kwanza la kuomba uchaguzi wa simba usimamishwe na ombi la pili wanaomba wapatiwe Kibali Cha wanachama wengine kuunganishwa Katika Kesi Yao ya Msingi itakayofunguliwa baada ya kupata Kibali hicho.

" Lakini Leo asubuhi, Wakili wa wadaiwa amewasilisha kiapo akiniambia wateja wake ambao ni wadaiwa Kuwa wamekuwa liana na Maombi yetu yote hayo na kwasababu hiyo basi tunaimba Mahakama itoe amri yake" Alidai Wakili Kuuli.

Wakili wa walalamikaji, Revocatus Kuuli alidai Kuwa anaomba 
 asubuhi wakili anaye mtetea Mwenyekiti wa Timu a Simba, Ismail Aden Rage na Bodi ya wadhamini wa timu hiyo, Juma Nassor , aliliieleza mahakama kuwa baada ya wakili wa walalamikaji Revocatus Kuuli, kuwapatia nakala ya madai yao, upande wa wadaiwa wamekubaliana na madai ya walalamikaji kuwa madai yao mawili yaliyoomba mahakama hiyo itoe amri ya muda ya kuzuia uchaguzi mkuu wa timu hiyo uliopamgwa kufanyika kesho na ombi la pili liloomba mahakama hiyo iwapatie Kibali Cha kuruhusu wanachama wengine waunganishwe Kama walalamikaji Katika Kesi ya Msingi itakayofunguliwa mahakamani halo mara baada ya kupata kibali ha mahakama.

Wakili Nassor alieleza Kuwa Sababu hiyo mmoja wa wadaiwa Katika Kesi hiyo Hamis Kilomoni kwaniaba ya wadaiwa wote amewasilisha Maombi hayo chini ya kiapo ambayo wadaiwa na wapingani na Maombi ya walalamikaji anaomba Kuzuiwa KWA uchaguzi Mkuu, Kwani ni wazi Kesi hiyo ilipofunguliwa na wanachama watatu Wa simba imenyesha picha Msingi wake ni mtafaruku uliotokana baada ya baadhi ya wagombea wanafasi Mbalimbali Katika uchaguzi huo, waliondolewa Kuwa wagombea na Kamati ya Uchaguzi ya Simba.

"Mtukufu Jaji Lengo letu sisi wadaiwa ni kwamba Tunataka kuona Amani, umoja, mshikamano uimalike ndani ya Simba, uchaguzi huu usiwe Chanzo Cha kuleta VURUGU, mpasuko ndani ya Simba...hivyo sisi wadaiwa tunaomba wale wagombea ambao waliondolewa katika uchaguzi Kwa Sababu mbalimbali , nak waruhusiwe Kugombea  ili Amani na utulivu na umoja uwepo Kwenye klabu ya simba na kwamba tumekubaliama Kesi hii twende tukamalize nje ya Mahakama" Alidai Wakili Nassor.

Wakili Nassor aliomba Mahakama Kifungu Cha 9 Cha Sheria ya Mashauri ya Madai ya Mwaka 2002, kuondoa Kesi hiyo jambo ambalo Jaji Mwarija alisema Wakili Nassor.

Ilipofika saa tano, Jaji Mwarija aliarisha Kesi hiyo hadi saa 7:30 mchana ili aje atoe maamuzi ya ama Kuzuia uchaguzi wa simba au laa.

Ilipofika Muda huo, Mawakili Hao wa pande mbili waliambia Mahakama Kuwa Kesi ilipoarishwa walikuwa na wakakubaliana maridhiano wa Lengo la kuamasisha umoja ndani ya simba hivyo Wakili Kuuli akaomba Mahakama itoe amri ya kuliandoa shauri Hilo mahakamani ili waende kujimaliza nje ya Mahakama.

kitendo ambacho Mara kwa  Mara kilifanya Jaji Mwarija Kuwauliza Mawakili wa pande zote mbili Kuwa hayo maridhiano Yao wameyawasilisha chini ya Kifungu gani Cha Sheria Kwani kilichopo mahakamani hakionyeshi Kama pande hizo mbili zimelidhiana na kwamba kuna Sita za wagombea na kwamba tarehe ya uchaguzi isogezwe Mbele wala wagombea Waliondolewa Kwenye uchaguzi waruhusiwe Kugombea.

" Hii ni mahakama na Mahakama inatakiwa itoe amri kutokana na Maombi yaliyowasilishwa Mbele yake KWA mujibu wa Sheria husika, sasa Maharishi tena shauri hili hadi saa 10 jioni  ili niwape MUDa Nyie Mawakili wa pande zote mbili Muende kuweka hayo maelezo yenu mapya Katika hati yenu ya maridhiano Kisha tukirejea saa Kumi jioni nitakuja kutoa uamuzi ambao ni wa kisheria " Alisema JAJI Mwarija.

Juni 23 mwaka huu, wananchama Hao watatu kupitia Wakili wao Kuuli walifungua   mahakamani hapo Maombi hayo madogo, Na.291/2014  Josephat Waryoba, Said Lly Monero na Hassan Hassan, ambao wanamshitaki Rais wa Timu ya Simba, Ismail Aden Rage na Bodi ya Udhamini ya Timu  hiyo.

Kwa mujibu wa hati hiyo inayonyesha walalamikaji wana jumla ya Madai matatu ambayo dai la kwanza wakiomba Mahakama hiyo itoe amri ya kuwazuia wadaiwa kuitisha uchaguzi Mkuu uliofangwa kufanyika Kesho.

CHANZO: Gazeti la Tanzania Daima la Jumamosi, Juni 28 Mwaka 2014.



ALIYEKUWA MKURUGENZI WILAYA YA ILALA ASHINDA KESI


ALIYEKUWA MKURUGENZI ILALA ASHINDA KESI
Na Happiness Katabazi
HATIMAYE Mahakama ya Wilaya ya Ilala Dar es Salaam, imemuachia huru aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Ilala, John Lubuva na wenzake wanne waliokuwa wanakabiliwa na mashtaka matatu likiwemo la kuisababishia Serikali hasara ya Sh bilioni 1.7. 
 
Mbali na Lubuva washtakiwa wengine ni Mhandisi Mkuu wa Idara ya Maji, Idd Kisisa, Mkuu wa Idara ya Sheria na Ulinzi, Anderson Msumba na Mwanasheria Andrew Kanonyele.
 
 Akisoma hukumu hiyo Hakimu Mkazi, Juma Hassan alisema kuwa upande wa mashtaka ambao ni Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), umeshindwa kutoa vielelezo vinavyoonyesha ni kwa jinsi gani ubomoaji wa nyumba zilizopo Tabata Dampo ulikuwa ni kinyume cha sheria.
 
Alidai kuwa Lubuva na wenzake walikuwa na kibali kinachoruhusu bomoabomoa ya eneo hilo kwani walitekeleza agizo la Mahakama ya Ardhi iliyotaka wakazi hao wahame katika eneo hilo kwani walikuwa wanaishi kinyume na sheria.
 
“Pamoja na upande wa mashtaka kuleta malalamiko ya watu walionewa lakini hakuna mlalamikaji  hata  mmoja aliyekuja kuthibitisha kuhusu madai ya uvunjwaji wa nyumba zao kama wameonewa,” alisema Hakimu Juma.
 
Alisema kuwa pamoja na kwamba wakazi 88 wa eneo hilo walilipwa fidia ya Sh milioni 20 kila mmoja licha ya kuwa kila nyumba ilikuwa na thamani yake, fedha hizo zililipwa kimakosa kwani hawakuwa na hati inayoonesha umiliki halali wa eneo hilo.
 
Mkurugenzi Lubuva na wenzake walikuwa wanakabilikwa na shtaka la kubomoabomoa nyumba za wakazi wa eneo la Tabata Dampo kinyume na sheria pamoja na kutumia vibaya madaraka yao, kula njama na kuisababishia hasara Serikali.
 
 Washtakiwa kwa mara ya kwanza walifikishwa mahakamani Julai, 2011, wakidaiwa kuwa Februari 28, 2008, walikula njama na kutenda kosa la kuvunja nyumba za makazi ya watu katika kiwanja namba 52 kilichopo Barabara ya Mandela, eneo la Tabata, Dar es Salaam.
 
Chanzo: Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne , Julai 2 Mwaka 2014.
 












KESI YA DK.MAHANGA YA KUGHUSHI VYETI VYA WALIMU YATUPWA



Na Happiness Katabazi
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar Es Salaam, imeifuta Kesi ya Madai ya kashfa iliyokuwa imefunguliwa na Naibu Waziri wa Kazi, Ajira  na maendeleo ya vijana, Dk. Makongoro Mahanga dhidi ya Mwanaharakati ,Kainerugaba Msemakweli na wenzake kwa Madai Kuwa alighushi vyenu Vya elimu, kwasababu Dk.Mahanga ameshindwa kutokea siku ya Kesi yake.

Mbali na Msemakweli wadaiwa wengine ni Mwandishi wa Gazeti la Nipashe, Muhibu Saidi , Mhariri Mtendaji  wa Gazeti Hilo na Kampuni ya The Guardian Limited Waliokuwa wanatetewa na Wakili wa kujitegemea Michael Ngaro.

Uamuzi huo umetolewa na Jaji Salvatory Bongole  Kesi hiyo Ya Madai Na. 145/2009 , ambaye Alisema Amefikia uamuzi huo kwasababu Wakili wa mlalamikaji Kennedy Fungamtama na mlalamikaji wamekuwa hawafiki mahakamani bila kutoa taarifa na kwamba kuna ushahidi unaonyesha wito wa wa Kuitwa Mahakama ulikuwa ukiwafikia kwa  wakati.

Jaji Bongole alisema  ametumia amri Tisa kanuni ya nane ya Sheria  ya Madai ya Mwaka 2002 na kwamba Amemfutia Kesi hiyo kwa gharama.

Kwa mujibu wa hati ya Madai ,Dk.Makongoro alikuwa akiomba wadaiwa wamlipe jumla ya Fedha sh.Bilioni Tatu Kama faida ya madhara aliyoyafanya kutokana na Habari ya uongo iliyochapishwa na wadaiwa Katika Gazeti la Nipashe la Oktoba 19 Mwaka 2009 iliyokuwa na kichwa Cha Habari kisemacho " Vyeti Vya Elimu: Mawazir Sita wanasa".

Habari Hilo ilikuwa ikisomeka Kama ifuatavyo: " Mawaziri Sita na wabunge. Wa njem wametawanyika  kuwamo Katika orodha  ya watuhumiwa 19 waliomzushia Vyeti vyao Vya elimu ...wanasiasa hao  Wametumia Vyeti Vya kughushi na Kuwasilisha Katika ofisi za umma kwamba sana elimu hio, kitu ambacho si kweli....Kuwasilisha Nyaraka za kughushi  Katika ofisi ya umma ni kinyume Cha Ktiba na Sheria za nchi...Msemakweli aliwataja Manaibu Waziri, Dk.Makongoro Mahanga ( Kazi,Ajira na Maendeleo ya Vijana).... 

" Vigogo Hao  waliwaghilibu wananchi wa majimbo  wanayowawakilisha na kuwafanya wa late UBUNGe na Mwana KWA kutumia shahada hizo za kujipachika, wamesema kuaminika na kupewa nafasi za kisiasa na kimya wala...Dk.Mahanga ameghushi Sita za Kuwa Ana shahada. Ya uzamivu (Daktari wa falsify)  wakati hawawajui kusoma shahada hiyo wakati wowote na mahali popote Duniani".

Dk.Mahanga Alidai Habari hiyo ni ya uongo na ilikuwa na Lengo la kushuhudia heshima yake hasa ukizingatia yeye ni kiongozi wa juu serikalini na ni mwansiasa na wapiga kula wake wanamuamini hiyo Habari hiyo ili letter madhara makubwa na hivyo akaiomba Mahakama ikaamuru washitakiwa wamlipe fidia sh.bilioni Tatu na Gazeti la Nipashe n ichapishwe Habari ya kumwomba Radhi na itamke Kuwa Habari ili ya awali ilikuwa ni ya uzushi.

Chanzoz:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Julai 2 Mwaka 2014.