KATABAZI: NIMEACHA KAZI GAZETI LA TANZANIA DAIMA



KATABAZI : NIMEACHA  KAZI GAZETI LA TANZANIA DAIMA
: KWASASA NI OFISA  HABARI CHUO KIKUU CHA BAGAMOYO(UB)

MIMI  Happiness Thadeo Katabazi (35), Leo Agosti 29 mwaka 2014 ndiyo siku yangu ya mwisho ya kufanyakazi Katika Gazeti la Tanzania Daima.

Nimeachakazi kwa Hiari yangu    katika Gazeti la Tanzania Daima linalotolewa na kampuni ya Free Media  Ltd  kwasababu Agosti  Mosi Mwaka huu,niliwasilisha notisi ya kuacha Kazi   na ombi  hilo lilikubaliwa na waliokuwa wakubwa wangu  wa Kazi.

Kwa heshima na taadhima napenda kutoa shukurani zangu za dhati kwa Mwenyezi Mungu Kwani alinipa Afya,Nguvu na maarifa nikaweza kulitumikia Gazeti la Tanzania Daima kwa Miaka nane sasa  kwa uaminifu na uadilifu wa Hali ya juu.

Kwasababu kwa Kipindi chote nilichofanya Kazi Kama Mwandishi wa Habari wa Gazeti Hilo sijawahi kuandika habari ambayo ilisababisha gazeti Hilo lifnguliwe kesi mahakamani.Namshukuru Mungu Katika Hilo.

Pia namshukuru mmiliki wa Gazeti la Tanzania kwani bila yeye kuanzisha Gazeti Hilo nisingepata ajira na limenilea.  Napenda kuwashukuru wafanyakazi wote wa gazeti hilo kwani tuliweza kufanyakazi pamoja licha wakati mwingine ilikuwa ikitokea Hali ya kutofautiana misimamo Katika baadhi ya mambo mbalimbali lakini yaliyopita Si ndwele tugange yajayo.

Navishukuru   vyombo vyote vya dola likiwemo Jeshi la JWTZ,Polisi, Magereza, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Kwani baadhi ya maofisa wa vyombo hivyo walikuwa wakinipa  ushirikiano wa kutosha Katika Kazi yangu ya uandishi wa Habari za mahakamani kwa Miaka 16 sasa. 

Nimevitaja vyombo hivyo Vya dola Kwani Mwandishi makini na mjanja wa  Habari za mahakamani nilazima afanyekazi kwa kutegemea Polisi, Askari Magereza na TAKUKURU.

Nawashukuru sana Askari na maofisa wote wa majeshi hayo Kwani tulifanyakazi  pamoja na nilijifunza mambo mengi sana kutoka kwenu.Mungu awabariki na nitaendelea kuthamini mchango wenu Kwangu Kwani mlinifundisha  mengi hasa Askari wa Jeshi la Polisi " Manjagu".

Navishukuru vyama Vya siasa Chama Cha Malpinduzi( CCM), CUF, NCCR- Mageuzi , CHADEMA, Tanzania Labour Party , DP na vingine Kwani katika Kipindi chote Cha Kazi yangu ya uandishi wa Habari niliweza kufanya Navyo Kazi kupitia viongozi wa juu,Kati na wanachama wa vyama hivyo.

Kwa namna ya kipekee  napenda kuishukuru  Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka(DPP), iliyokuwa ikiongozwa na DPP aliyemaliza muda wake hivi karibuni, Jaji DK.Eliezer Feleshi Kwani ni yeye Jaji Feleshi  na timu yake ya Mawakili wa serikali walikuwa wakinipa ushirikiano Katika Kazi yangu ya uandishi wa Habari za mahakamani kwa Miaka Saba yote aliyokuwa ameshika wadhifa   huo wa DPP.

Namshukuru sana Jaji Feleshi Mungu ampe Maisha Marefu Kwani Jaji Feleshi yeye binafsi alikuwa na hadi sasa ni  Mpenzi  wa makala na Habari zangu za mahakamani na nimshauri mkubwa sana wa mambo yangu binafsi,kazi na shule yangu. Feleshi mimi namchukulia kama ni kaka yangu, mwalimu na mshauri wangu wa kazi yangu ya uandishishi wa habari, na kozi yangu ya Sheria.

Jaji Feleshi amekuwa akinikosoa ninapoandika  Habari au makala ambazo alikuwa akiziona hazikidhi matakwa ya kisheria na usalama wangu binafsi na nchi.

Na hadi sasa ajachoka kunishauri na amekuwa akinitaka kabla ya kuandika niwenafanya utafiti kwanza na kweli ushauri wake nimeuzingatia kwani hivi sasa amekuwa akiniambia sasa anaona fahari kwani uandishi wa makala zangu umebadilika imetoka Katika ngazi ya kiharakati , Ujinga na umemfika ngazi ya Kisomi.Namshukuru sana Jaji Feleshi 'Msukuma'.

Naushukuru uongozi wa Mhimili  wa Mahakama nchini chini Jaji Mkuu Mstaafu, Agustino Ramadhani na Jaji Mkuu wa sasa Mohamed Chande Othman kwasababu kuna baadhi ya Majaji, wasajili,makarani, walinzi wa Mahakama na watumishi wa Kada mbalimbali wa  Mahakama walinipa ushirikiano na kunifundisha mambo mbalimbali ya jinsi mahakama na serikali inafanyaje kazi bila kuchoka wakati nilipokuwa Mwandishi wa habari za mahakamani bila kuchoka.

Pia navishukuru Vyanzo Vyangu vingine Vya Habari ambavyo ni Mawakili wa kujitegemea,walalamikaji, washitakiwa waliopo nje kwa dhamana na waliopo ndani ya magereza walikuwa wakinipa taarifa mbalimbali kuhusu Kesi mbalimbali na kuaniarifu mapema Kuwa siku Fulani mahabusu waliopo Katika baadhi ya magereza watagoma lini , nawashukuru sana na taarifa hizo nilikuwa nazifikisha mahali husika zinafanyiwa Kazi.

Hata hivyo nayashukuru  makundi mengine yote yaliyokuwa yakinipa ushirikiano Katika Utendaji wangu wa Kazi.

 Pia na washukuru wasomaji na wapenzi wa makala zangu na Habari za mahakamani Kwani kwa Kipindi chote hicho mlikuwa mkisoma makala na Habari zangu wengine mlikuwa mkinipinga na wengine mlikuwa mkiniunga mkono.

Licha ya kuacha Kazi Gazeti la Tanzania Daima, napenda Kusema wazi  Kuwa Kazi ya uandishi wa Habari hasa uandishi wa Habari za mahakamani ' umbea' ipo Kwenye Damu yangu, nitaendelea kuandika makala na kuchangia mijadala tofauti kupitia mitandao ya kijamii bila kuvunja Sheria za nchi.

Kwa sasa nimepata Kazi Chuo Kikuu Cha Bagamoyo(UB) na Makamu Mkuu wa Chuo hicho ni Profesa Balozi Costa Ricky Mahalu, chenye Makao Makuu Mikocheni  kwa Warioba Dar es Salaam, Kama Afisa Habari wa Chuo Kikuu hicho. 

Nawakaribisha waandishi wa Habari wenzangu hasa wale waandishi wa Habari za mahakamani na wananchi wengine  waje UB, ili waweze kupata elimu za  fani mbalimbali maana Ulimwengu wa sasa bila elimu ni tabu sana.

Waandishi wa Habari tukiitikia wito wa kukubali kwenda kujiendeleza kielimu Katika vyuo vikuu, ni wazi tutaondokana na tabia ya kukubali kutumiwa vibaya na Makundi yanayoasimiana kisiasa, Kibiashara kuchafua watu kupitia Karamu zetu, kujazana Ujinga ndani ya  vyumba Vya Habari .

Nafahamu neno Hilo linaweza kuwakera baadhi ya waandishi ambao hawataki  Mabadiliko na hawataki kujiendeleza kielimu kwasababu za kijinga Kuwa akienda shule kusoma Atakosa ' mishiko, safari'.Sijali, naamini nimesema kweli na Mungu atanilinda  na inawezekana ukiamua.

Mimi ni shahidi wa Hilo Kwani Mwaka 2009 -2010 nilipoanza kusoma kozi ya Cheti Cha Sheria Chuo Kikuu Cha Dar Es Salaam, kuna baadhi ya waandishi wenzangu walinicheka na kuniona chizi lakini nikamaliza Mwaka 2012- Juni 2013 nikasoma Diploma ya Sheria Katika Chuo Kikuu Cha Bagamoyo nikamaliza waliokuwa wananicheka Wakaanza kuniambia Kuwa walifikiri nilikuwa natania wakati nawaaga na kwenda Kusoma Sheria.

Waliposikia na kuniona Septemba  Mwaka 2013  nimeanza kusoma Shahada ya Sheria wameishia  Kusema Kuwa Kumbe nimedhamiria, na kwamba Mimi ni mwanamke wa Shoka na kwamba nitafika Mbali.

Nawatazama   kwasababu hawafahamu nawaza nini na ni kwanini MUNgu ananipa Nguvu na uwezo wa kusoma hivyo wakati Nasoma kwa tabu sana na kugeuka ombaomba wa Ada" Matonya'.

Licha Nasoma shule kwa dhiki na tabu lakini siku zinakwenda na shule ndiyo MUNgu akipenda  Julai Mwaka 2016 nitamaliza Shahada  ya kwanza ya Sheria.

Nimelazimika kujitolea mfano halisi Mimi licha sikupaswa kutaja adharani Kuwa Nasoma Kwa  dhiki, ili iwe ni amasa kwa wanahabari wenzangu ambao hawana mawazo kabisa ya kujiendeleza kielimu  Kuwa ukiamua na ukamtanguliza Mungu  inawezekana.

Mume wangu 'Rais Mdhurumiwa' Marehemu Dk.Sengondo Mvungi, Profesa Paramaganda Kabudi,Dk.Harrison Mwakyembe, Mwanangu ambaye ni mtoto wa mume wangu Marehemu Dk.Mvungi, ambaye ni Mkuuu wa Kitivo cha Sheria (UB) na Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Dk.Natujwa Mvungi hawa wote walikuwa ni waandishi wa Habari.

Tena  bora na DK. Mwakyembe na Dk.Natujwa walisomea  kozi ya uandishi wa Habari lakini  marehemu Dk.Sengondo Mvungi hakuwahi kusomea chuo chote kozi ya uandishi wa Habari licha alikuwa ni Mwandishi wa Habari wa Gazeti la Mzalendo na Dk.Mvungi alipelekwa kufanyakazi Gazeti la Mzalendo na Mwandishi Mkongwe nchini, Ndimara TIgambwage.

Lakini mwisho wa siku waliamua kukata shauri na kwenda vyuoni Vya elimu ya juu kusoma  fani ya Sheria na Leo hii wamekuwa ni msaada mkubwa kwa taifa hili Kwani wamekuwa wAkitumiwa na serikali, Jamii kutoa huduma ya taaluma Yao ya Sheria.

Hivyo binafsi nikiwa Natazama historia za  wasomi hawa, nimejifunza   jambo Moja Kuwa ukiamua kukata shauri kutaka kujiendeleza kielimu unaweza. Waandishi wenzangu ambao bado hamjakata shauri , hamjachelewa, anzeni sasa.

 Swahiba wangu Mchungaji  Christopher Mtikila tukutanapo au tupigianapo simu neno la lake la kwanza kuniambia ni "Saa ya Ukombozi...Mimi na Mjibu ni Sasa". 

Mataifa ya wenzetu yamepiga Hatua za kimaendeleo kwasababu waandishi wao wa Habari wameweza kwenda shule vizuri na Waandishi wao wengine wameamua kubobea Katika Nyanja Fulani , mfano Mwandishi wa Habari za mazingira amesomea kozi ya mazingira hivyo akiandika Habari inayohusu mazingira anaifahamu vizuri kwasababu.

Kama kweli waandishi wa Habari wa Tanzania tumedhamilia kulilitetea taifa letu maendeleo, basi tuzidi kujiendeleza kielimu na ikiwezekana tusomee fani nyingi tofauti na uandishi wa Habari ili mwisho wa siku uakiamu kuandika makala au Habari inayohusu labda mambo ya uchumi, Afya , Sheria unaiandika vizuri tena bila msaada wa Wanataaluma ya ya uchumi, Sheria au Afya kwasababu Tayari unakuwa unafahamu nini unachokiandika kwa mujibu wa taaluma hiyo.

Naamini tukiamua kujiendeleza kielimu miongoni mwenu 'mtakataa kugeuzwa geuzwa Kama  chapati'  na baadhi ya wanasiasa na Makundi mengine yenye Fedha ambayo ya natumia Fedha zao kuwahonga baadhi ya waandishi wa Habari kuchapisha Habari ambazo hazikidhi vigezo na zenye Lengo la kuchafua watu wengine.

Mwisho Nawashukuru wale wote walionishauri niende kusoma Sheria Kwani Leo hii naona faida ya ushauri wao kwani nimeweza kupanuka kifikra na kuwa imara katika fani yangu ya uandishi wa habari.Mungu awabariki sana.
Imeandaliwa na ; 
Happiness  Katabazi
Ofisa  Habari wa Chuo Kikuu Cha Bagamoyo(UB),
Mwanafunzi wa Mwaka wa pili wa Shahada ya Sheria(UB)
0716 774494.
Chanzo: Facebook: Happy Katabazi
Agosti 29 Mwaka 2014

KATABAZI ALIVYOAGWA TANZANIA DAIMA


KATABAZI NIKIAGWA NA WALIOKUWA WAFANYAKAZI WENZANGU  NDANI YA CHUMBA CHA HABARI CHA GAZETI LA TANZANIA DAIMA DAR ES SALAAM, LEO ASUBUHI AGOSTI 29 MWAKA 2014.
 NIWE MKWELI HIYO PICHA  YA KWANZA NILIJIKUTA  NAMWAGA MACHOZI WAKATI NAAGWA NA   'WAMBEA ' WENZANGU KWANI NIMEACHAKAZI HAPO NAKWENDA KUFANYAKAZI KATIKA CHUO KIKUU CHA BAGAMOYO (UB), CHENYE MAKAO YAKE MAKUU MIKOCHENI KWA WARIOBA, KAMA AFISA HABARI WA CHUO HICHO KILICHOPO MIKOCHENI KWA WARIOBA NA WAKATI HUO HUO NI MWANAFUNZI WA MWAKA WA PILI WA SHAHADA YA SHERIA.
NITAWAKUMBUKA SANA ' WAMBEA' WENZANGU'.
UANDISHI WA HABARI UPO NDANI YA DAMU YANGU NAAPA SITAACHA KUANDIKA MAKALA NA PIA SIKU MOJA MOJA NITAKUWA NAENDA MAHAKAMANI KUSIKILIZA KESI NA KUZIRIPOTI KUPITIA UKURASA WANGU FACEBOOK.





UB ILIVYOPANIA KUINUA ELIMU YA BIASHARA,UWEKEZAJI KIMATAIFA


UB ILIVYOPANIA KUINUA ELIMU YA BIASHARA,UWEKEZAJI KIMATAIFA

Na Happiness Katabazi

AGOSTI 11- 22  mwaka 2014, Chuo Kikuu cha Bagamoyo ( UB) kilichopo Mikocheni kwa Warioba Dar es Salaam, kiliandika historia mpya kwaniaba ya serikali Tanzania, kwa kuendesha  Mafunzo ya siku 14 ya jinsi ya kujadili mikataba ya Biashara na Uwekezaji  Kimataifa .

Mafunzo hayo ambayo yameshirikisha maofisa Biashara waandamizi toka serikali za nchi nane ikiwemo Tanzania na yalifadhiliwana na Taasisi ya Nordic Afrika ya Chuo Kikuu Cha Uppsalla , Sweeden  ambayo Taasisi hiyo ili wakilishwa na Profesa Francis Matambalya na mtandao wa vyuo vikuu vitano ambapo UB ni mwanachama wa mtandao wa (TANUP/PUTAna serikali   iliwakirishwa na  Biashara toka Wizara ya Viwanda na Biashara na Ofisa Biashara wa Wizara hiyo  Elia Mtweve.

Akizungumza Katika siku ya Kufunga Mafunzo hayo Ijumaa iliyopita Katika Hoteli ya Habour View Da Es Salaam,  Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Bagamoyo(UB), Profesa Costa Rick Mahalu aliishukuru Taasisi ya Nordic Afrika ya Chuo Kikuu Cha Uppsalla, Sweedn kilichowasilishwa na Mtanzania ambaye ni mwadhiri wa Uchumi wa Chuo hiyo nchini Sweeden, Profesa Matambalya  kukubali ombi la Chuo Kikuu Cha Bagamoyo la kufadhiliwa Mafunzo ya jinsi kuandaa majadaliano ya Biashara na uwekezaji  kwa maofisa wa fani ya Biashara toka nchi  nane ambapo Tanzania kupitia Chuo Kikuu Cha Bagamoyo.

Profesa Mahalu pia alisema  anaishukuru  serikali ya Tanzania kukubali Mafunzo hayo ambayo ya naenda kusababisha Chuo Kikuu Cha Bagamoyo Oktoba Mwaka huu kuanzisha  shahada mpya ya jinsi ya kuanda mjadala ya Kibiashara na uwekezaji ambayo itakuwa ni shahada ya kwanza kuanza kutolewa Katika vyuo vikuu hapa nchini na nchi zilizoshiriki Katika Mafunzo hayo, yaendeshwe hapa nchini.

Profesa Mahalu alisema  washiriki wa Mafunzo hayo walitokea nchi Tanzania ambayo ni Mwenyeji,   Kenya, Uganda, Burundi, Rwanda, Lesotho, Kongo, Malawi, Ethiopia, Zambia na Madagascar.Na Baadhi wa washiriki ni maofisa wa juu wa serikali wa nchi wanazotoka na mmoja ni Mkurugenzi  wa Taasisi za Sekta Binafsi nchini Lesotho, Thabo Quesi na wengine wanatoka Vyuo Vikuu Vya vya mataifa Yao.

' Kwa Kuwa Mafunzo haya yameletwa UB, Kwaniaba ya Chuo Kikuu Cha Bagamoyo, tunaahidi kufanya mradi wa Mafunzo haya ni endelevu na unakuwa  kwa kasi Kwani Tayari tumeishaanzisha Taasisi mpya itakayokuwa chini ya Shule ya Biashara na Utawala ya UB inayoongozwa na Dk.Lenny Kasoga  ambapo Taasisi hiyo itakuwa inatoa  Mafunzo ya jinsi ya kuandaa majadiliano ya Kibiashara na uwekezaji :

" Nanaiomba serikali kupitia Wizara ya Viwanda na Biashara iruhusu maofisa wake wa Biashara waje kusoma shahada hiyo Kwani shahada hiyo itakuwa ni mpya na itawasaida maofisa Biashara wetu kukabiliana na tatizo la kushindwa kufanya vizuri Katika eneo la majadiliano na Biashara ya Kimataifa na wananchi wengine Waje kusoma kozi hiyo" anasema Profesa Mahalu.

Profesa Mahalu Alisema Seneti ya UB Imefikia uamuzi wa kuwatunuku  uprofesa kuwa maprofesa  wa UB, wasomi wanne waliobobea Katika fani Biashara na kutokana na Seneti imejiridhisha Kuwa wasomi Hao wamefanya mambo Makubwa kupitia taaluma ya Biashara .

Aliwataja wasomi Hao Kuwa ni Dk.Dickson Yeboah ambaye ni Mfanyakazi wa Shirika la Biashara la Dunia (WTO) yenye makao yake makuu  Geneva Uswiss, Dk.Francis Matambalya,Dk. Baoudoiun Michael na Mkurugenzi wa Mtangamano  wa Biashara toka Wizara ya Viwanda na Biashara nchini, Lucas Saranga Kuwa maprofesa.Na kwamba kuanzia siku hiyo ya Agosti 22 Mwaka huu ,wasomi Hao wametunukiwa Kuwa ni maprofesa.

Aidha Balozi Mahalu anasema sherehe za ufungwaji wa Mafunzo Yale uliambatana na kuwatunuku uprofesa na pia kuzindua Mtandao wa vyuo vikuu vitano  (TANUP/PUTA)  ambavyo vyuo vikuu hivyo vi nafanyakazi Kwa kushirikiana ambapo ulizinduliwa Mtandao huo.

Mkuu wa Shule ya Biashara na Utawala ya Chuo Kikuu Cha Bagamoyo, Dk.Lenny Kasoga , Profesa Lucas  Saranga, Profesa Yeboah ,Profesa Matambalya , Profesa Baoudoiun na Profesa Vale Karugaba ambao wote walikuwa ni wakufunzi katika mafunzo hayo kwa nyakati tofauti walisema waliweza kuwafundisha washiriki wa mafunzo hayo mambo makuu matano:

Moja, kiwango cha biashara na uwekezaji kilichofikiwa.Pili, misingi ya uwekezaji  na mazingira ya biashara katika ngazi ya kimataifa, Tatu; Uchambuzi wa uwiano wa ushindani  wa kibiashara na uwekezaji ngazi ya kimataifa. Nne; Nadharia  ya majadiliano ya Biashara na uwekezaji kwa   vitendo.Tano; kushiriki kwa majadiliano ya Biashara  na uwekezaji.

Aidha Matambalya ambaye Taasisi yake ndiyo Imebadili Mafunzo hay ya kwanza kutolewa nchini anasema yeye ni Mtanzania na anafanyakazi Katika Taasisi hiyo ya kigeni ya Nordic ,Uppsalla,Uswiss ataakikisha huo mradi wa Mafunzo ambao wameupeleka UB, unakuwa endelevu na Taasisi yake itaendelea kufadhili ili Watanzania wengi waweza kusoma kozi hiyo ili mwisho wa siku taifa liweze kuondokana na tatizo la Kuwa na wataalamu wasiyobobea Katika eneo la majadiliano ya Biashara na uwekezaji na kuingia mikataba na wawekezaji .

Kwa upande wake  Aliyekuwa mgeni rasmi katika kufunga mafunzo hayo ,Mkurugenzi Msaidizi  wa Idara ya Elimu ya Juu serikali imewataka   washiriki wa mafunzo ya jinsi ya kujadili  mikataba ya Biashara na uwekezaji   kutumia taaluma hiyo waliyoipata kwaajili ya kuleta manufaa kwa mataifa Yao.

Dk. Mbwambo kwaniaba ya Waziri wa wizara hiyo, Dk.Shukuru Kawambwa anasema  serikali  inakipongeza Chuo Kikuu Cha Bagamoyo (UB), kwa kuandaa Mafunzo hayo ambayo yameshirikisha maofisa wajuu wa serikali mbalimbali Kwani kupitia Mafunzo Hao maofisa Hao wameweza kubadilishana uzoefu wa masuala ya nchi zao kuhusu Sekta ya masoko na uwekezaji.

Dk.Mwambo anasema  kila kukicha baadhi ya nchi za Africa zimekiwa zikigundulika kuwa na utajiri mkubwa aridhini na mfano mzuri ni nchi ya Tanzainia ambayo imegundulika kuwa ina nishati ya gesi , madini hivyo kupitia mafunzo hayo  kwa upande wa Tanzania  Wizara ya Viwanda na Biashara iliwakirishwa na maofisa wake Wawili wameweza kupata ujuzi ambao utaki saidia serikali ya kuweza kufanya vizuri Katika uandaaji wa masoko na uwekezaji wafanyabiashara wa Kimataifa watakaokuwa wanakuja kuwekeza nchini.

' Nchi nyingi za Afrika ikiwemo Tanzania zimegundulika Kuwa na  utajiri mfano Tanzania hivi sasa imegundulika Kuwa na  nishati ya gesi hivyo Mafunzo hayo yataisidia nchi kuondokana na tatizo kuingia mikataba na wawekezaji wa kigeni ambayo italeta tija kwa mataifa ya nchi zinazoendelea.

Nao washiriki wa Mafunzo hayo Bifou Lufuma toka Serikali ya Kongo na Thabo Quesi  (Lesotho) na Elia Mtweve kutoka Tanzania wanasema Mafunzo hayo yamewajengea uwezo na kwamba watakuwa mabalozi wazuri Katika maeneo Yao ya Kazi na kwamba wanaiopongeza UB kuendesha Mafunzo ambayo ni ya kwanza kutolewa hapa nchini.

Mwandishi wa makala hii ni:
Ofisa Habari wa Chuo Kikuu Cha Bagamoyo (UB)
0716 774494
Blog:www.katabazihappy.blogspot.com
Facebook: Happy Katabazi
Chanzo: Gazeti la Tanzania Daima la Jumamosi, Agosti 30 Mwaka 2014







HAKIMU GABRIEL MIRUMBE AFARIKI DUNIA

HAKIMU GABRIEL MIRUMBE AFARIKI DUNIA
Na Happiness Katabazi
HAKIMU Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, Gabriel Mirumbe amefariki Dunia Jana Agosti 25  Katika Hospitali ya TMJ.

Akizungumza na waandishi wa Habari  za mahakamani Leo ofisini kwake Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Isaya Halfani alisema Mirumbe amefariki Jana na msiba hupo Mbezi Salasala na anatarajiwa kuzikwa Alahmisi wiki hii.

Binafsi Kama Mwandishi wa Habari za mahakamani kwa Miaka 16  sasa , nilimfahamu hakimu Mirumbe tangu alipokuwa Hakimu wa Mahakama ya ila ya ya Kinondoni Mwaka 1999- 2001  na pia akaamishiwa Mahakama mbalimbali ikiwemo Mahakama za mkoa wa Kigoma na Kisha a karejeshwa Katika Mahakama ya Kisutu na Kisha akaamishiwa Mahakama Kuu Kanda ya Dar Es Salaam na Mwaka Jana akarejeshwa Katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na hadi mauti unafika Jana alikuwa ni Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Nitamkumbuka Hakimu Mirumbe kwa mambo mengi Vituko vyake ambavyo siwezi kuviandika Katika makala hii, ila Nitamkumbuka Mirumbe kwani Mwaka 1999 alipokuwa Hakimu wa Wilaya ya Kinondoni, alipotoa hukumu ya Kumfunga kifungo cha Mwaka mmoja gerezani Mwenyekiti wa Chama Cha Demokracty ( DP), Mchungaji Christopher Mtikila.

Mirumbe alimpatia Adhabu hiyo Mtikila ambaye ni Kinara wa kushinda Kesi baada ya kumkuta na hatia ya Kutenda kosa la kutoa maneno ya uchochezi ambayo haya stahili kutolewa na kiongozi wa dini.

Mtikila alimshitakiwa kwa kosa la kutoa maneno ya uchochezi ambapo Mtikila alivieleza vyombo Vya Habari Kuwa Chama Cha Mapinduzi( CCM), kimembana Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama hicho Marehemu Horace Kolimba.Na Mtikila alitumikia Kifungo hicho Katika Gereza la Keko na alimaliza kutumikia Kifungo hicho hadi Mwaka 2000.

Hata Hivyo Mtikila alikata rufaa Mahakama Kuu Kanda ya Dar Es Salaam, rufaa yake kupinga hukumu hiyo na rufaa yake ilitupwa lakini pia Mtikila tayari ameishawasilisha ombi la kuomba Mahakama ya Rufaa Ifanyie mapitio hukumu ya Mahakama Kuu.

Pia Nitamkumbuka Hakimu Mirumbe Kwani alikuwa ndiye Aliyekuwa Hakimu wa kwanza kuipangiwa kusikiliza Kesi ya Madai ya kuomba Rushwa iliyokuwa ikimkabili Mtangazaji wa Televisheni ya Taifa (TBC), Jerry Murro na wenzake  ambapo alisikiliza harakahara na siku shahidi wa mwisho wa upande wa jamhuri  aliyekuwa akiongozwa kutoa ushahidi wake na Naibu Mkurugenzi wa Mshitaka marehemu Stanslaus Boniface.

Alipomaliza  kutoa ushahidi wake Hakimu Huyo ambaye alikuwa alisikiliza Kesi hiyo kwa mtindo wa aina yake mAana wakati mwingine mashahidi walipokuwa wakitoa ushahidi wao Hakimu Mirumbe alikuwa amelala na kutuacha waaandishi na watu waliokuwa walisikikiza Kesi wafinyana na kucheka vicheko Vya chini chini , Hakimu Huyo aliinuka na Kutoa uamuzi wa kumuona Murro na wenzake wana Kesi ya Kujibu.

Hata hivyo baadaye uongozi wa Mahakama ulimuondoa Mirumbe Katika Kesi hiyo na Kesi ya Murro ikapangwa kusikilzwa kwa Hakimu Frank Moshi ambaye alisikiliza Kesi hiyo na alitoa hukumu ambapo alimwachiria Huru washitakiwa wote baada ya kuwaona hawana hatia.

Pia Nitamkumbuka Hakimu Mirumbe ambaye hadi anakufa alikuwa ni miongoni mwa Mahakimu wanaosikiliza Kesi ya wizi wa Sh.Bilioni 6 inayomkabili MTu na Mdogo wake ambao ni wafanyabiashara Johnson Lukaza na Mwesigwa Lukaza na kiongozi wa jopo wanaosilikiza Kesi hiyo ni Jaji Edson Mkasimongwa na Pamela.

Baada ya kupata taarifa za kifo Cha Hakimu Mirumbe, nilimpigia simu Mtikila na kumweleza Mirumbe amefariki na amepokeaje msiba huo , Mtikila amenijibu maneno yafutatayo na ninayo nukuu hapa na kaniruhusu niyanukuu:

" Mirumbe amechelewa kufa  alitakiwa afe mapema kwasababu mshahara wa dhambi ni mahuti...wakati aliponifunga Kifungo Cha Mwaka mmoja gerezani siku hiyo anatoa hukumu ambayo hakunipa nafasi ya kujitetea Alisema ananifunga kwasababu amepewa shinikizo na viongozi wa juu wa serikali hivyo alinifunga jela kwa kutonipa nafasi ya kujitetea kwa Kigezo tu anawafurahisha wakubwa wa serikali ya CCM:

" Hivyo Mirumbe amekufa na amekwenda jehanamu Kwani kuna dhambi nyingine hata ukitubu  MUNgu akusamehi na MUNgu hajamsamehe Mirumbe kwasababu alinitendea dhambi Mimi mtumishi wa MUNgu ambaye niliongozwa na Roho mtakatifu Kusema CCM ndiyo iliyomuua Kolimba" Alisema Mtikila.

Nawashauri wasomi wenzangu  wangu kwa wasomi wa sheria na watumishi wa mahakama, mazuri  yaliyoachwa na Hakimu Mirumbe , tuyafuate na Mabaya alitoa acha tusiyafuate.

Mungu aweke mahali panapostahili roho ya Hakimu Gabriel Mirumbe.

Chanzo: Facebook: Happy Katabazi
Agosti 26 Mwaka 2014

SERIKALI YAKIPONGEZA CHUO KIKUU CHA BAGAMOYO (UB)




SERIKALI YAKIPONGEZA CHUO KIKUU CHA BAGAMOYO
Na Happiness Katabazi
SERIKALI imewataka   washiriki wa mafunzo ya jinsi ya kujadili  mikataba ya Biashara na uwekezaji   kutumia taaluma hiyo waliyoipata kwaajili ya kuleta manufaa kwa mataifa Yao.

Rai hiyo imetolewa jana na Mkurugenzi  Msaidizi Idara ya Elimu ya Juu ya Wizara ya Elimu ya Juu,  Dk.Jonathan Mbwambo kwaniaba ya Waziri wa wizara hiyo, Dk.Shukuru Kawambwa  wakati akifunga  Mafunzo hayo ya siku 14 yaliyoshirikisha maofisa wa juu wa fani ya biashara wa serikali za nchi nane ambayo yaliratibiwanna Chuo Kikuu Cha Bagamoyo(UB) ambayo yalifadhiliwa na Chuo Kikuu Cha  Nordric Africa Institute, Uppsalla cha nchini Sweeden chini ya Profesa Francis Matambalya na kuwezeshwa na Mtandao wa Vyuo Vikuu Vitano TANAUP/PATU  ambapo UB, ni mjumbe wa Mtandao huo.

Dk.Mwambo Alisema kwanza serikali  inakipongeza Chuo Kikuu Cha Bagamoyo (UB), kwa kuandaa Mafunzo hayo ambayo yameshirikisha maofisa wajuu wa serikali mbalimbali Kwani kupitia Mafunzo Hao maofisa Hao wameweza kubadilishana uzoefu wa masuala ya nchi zao kuhusu Sekta ya masoko na uwekezaji.

Dk.Mwambo alisema kila kukicha baadhi ya nchi za Africa zimekiwa zikigundulika kuwa na utajiri mkubwa aridhini na mfano mzuri ni nchi ya Tanzainia ambayo imegundulika kuwa ina nishati ya gesi , madini hivyo kupitia mafunzo hayo  kwa upande wa Tanzania  Wizara ya Viwanda na Biashara iliwakirishwa na maofisa wake Wawili wameweza kupata ujuzi ambao utaki saidia serikali ya kuweza kufanya vizuri Katika uandaaji wa masoko na uwekezaji wafanyabiashara wa Kimataifa watakaokuwa wanakuja kuwekeza nchini.

 Kwa upande wake Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Bagamoyo(UB), Profesa Costa Mahalu  Alisema UB,  nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania zimekuwa  zikikabiliwa na matatizo  ya jinsi ya kuandaa masoko na kuandaa mikataba yenye tija na wawekezaji hivyo kupitia Mafunzo hayo yamesaidia kuwajengea uwezo washiriki kwenda kukabiliana na Changamoto hiyo.

Profesa Mahalu  Alizitaja nchi zilizoshiriki Katika Mafunzo hayo ya Kimataifa Kuwa ni wenyeji Tanzania, Kenya,Uganda, Burundi, Rwanda, Lesoto, Kongo, Malawi ,Ethiopia , Zambia na Madagascar.

Alisema UB Katika Mwaka mpya wa masomo     inaanza kutoa Shahada ya jinsi ya kujadili mikataba ya biashara na uwekezaji   ili iweze kuwajenga wanafunzi wengi wa Watanzania waweze kuwa bora katika eneo hilo la masoko na kuandaa mikataba ya kuiingia na wawekezaji katika sekta mbalimbali.

Aidha Balozi Mahalu Alisema Seneti ya UB, imemuidhinisha Dk.Dickson Yeboah kutoka Geneva Uswiss, Dk.Francis Matambayla, Dk. Baoudoiun Michael na Mkurugenzi wa Mtangamano wa Biashara toka Wizara ya Viwanda na Biashara nchini, Lucas Saronga Kuwa Maprofesa wa UB.

Kwa upande wake Profesa Francis Matambalya toka  Taasisi ya Nordic Africa  ya Chuo Kikuu Cha Uppsala, cha nchini Sweden ambao ndiyo waliofadhili Mafunzo hayo Alisema Kuwa yeye ni Mtanzania na anampenda nchi yake na ataakikisha kila Mara Taasisi hiyo ya Sweden inaleta Fedha kwaajili ya kuendesha Mafunzo hayo ili nchi za Tanzania na Africa kwa ujumla ziondokane na tatizo la kutokuwa na wasomi waliobobea Katika eneo Hilo la kuandaa masoko na jinsi ya kuandika mikataba na wawekezaji wa kigeni Katika sekta mbalimbali.

Chanzo: Gazeti la Tanzania Daima la Jumamosi,Agosti 23 Mwaka 2014


JAJI BWANA NDIYE MWENYEKITI MPYA BARAZA LA CHUO KIKUU HA BAGAMOYO(UB)

JAJI  BWANA NDIYE MWENYEKITI MPYA WA BARAZA LA CHUO KIKUU CHA BAGAMOYO(UB)

Na Happiness Katabazi
BODI ya Wadhamini ya Chuo Kikuu Cha Bagamoyo(UB), imemteua  Jaji wa Mahakama ya Rufaa nchini, Dk.Stephen Bwana Kuwa Mwenyekiti mpya wa Baraza la chuo hicho.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Jana Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Bagamoyo(UB), Mikocheni Dar Es Salaam, Dk.William Kudoja alisema  Bodi ya Wadhamini ya chuo hicho ambayo Inaongozwa na Professa Paramaganda Kabudi Ndiyo ilimteua Jaji Bwana kushika wadhifa huo mpya baada ya kuona Ana sifa za vigezo Vya kushika wadhifa huo.

Dk.Kudoja ambaye ni Naibu Makamu Mkuu wa UB anayeshughulikia Taaluma, alisema jaji Bwana ambaye pia ni Jaji wa Mahakama ya Kimataifa ya Makosa  ya Jinai (ICC) ya nchini Cambodia.

Jaji Bwana aliwahi kushika nyadhifa mbalimbali Kama Jaji wa Mahakama Kuu  Seychelles 1994-1999, Jaji wa Mahakama Rufaa ya Seychelles 2004-2009 , Kaimu wa Rais wa Mahakama hiyo ya Rufaa ya Seychelles kuanzia  Mwaka 2006-2008.

Mbali na kushika nyadhifa hizo Jaji Dk.Bwana  pia aliwai Kuwa Mshauri wa Benki ya Dunia kuhusu  Uboreshaji  wa Shughuli za Mahakama Afrika Kati ya Mwaka 2003-2008, Msajili wa Mahakama ya rufaa nchini Mwaka 1989-1994 na Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania  Mwaka 1989  na Hakimu na Hakimu Mkazi Mwaka 1974.

Dk.Kudoja alisema Mwenyekiti huyo wa Baraza la UB, Jaji Bwana atawaongoza wajumbe  wajumbe 19 wa Baraza Hilo kutekeleza majukumu hayo ambao nao wanapitishwa na Bodi ya Wadhamini wa chuo hicho na watatekeleza majukumu waliyopewa.

Mbali na Jaji Bwana  Alisema wajumbe wa Baraza Hilo ni Profesa Esther Mwaikambo kutoka Taasisi ya Vyuo Vikuu Binafsi(IES), Mkurugenzi wa Taasisi ya Elimu ya juu nchini, Dk.Sylvia Temu, Mkurugenzi Mtendaji Mstaafu wa Kituo Cha Uwekezaji nchini(TIC), Emmanuel Ole Naiko, Vicent Jonas, Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi, George Simbeye, Wakili Mwandamizi wa Serikali Malata Gabriel , Mhadhiri wa Sheria wa chuo hicho, Baraka Mkami, Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Halima Kihemba, Makamu Mkuu wa chuo hicho ambaye pia ni Mjumbe wa Bunge la Katiba, Profesa Costa Mahalu, Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Mercy Sila, Dk.William Kudoja

Aidha Alisema wajumbe wengine ni Naibu Makamu Mkuu wa UB anayeshughulikia Fedha, Dk. Elifuraha Mtalo, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Kilimo Sokoine  anayeshughulikia Taaluma Profesa Peter Gillah, Mwenyekiti wa Kampuni ya Proin Promotions Limited Johnson Lukaza, Mathias Massawe, Mkurugenzi wa Sayansi na Teknolojia Katika Wizara ya  ya Mawasiliano ,Sayansi na Teknolojia Profesa Evelyn Mbede, Balozi na Wakili mwandamizi nchini Mwainaidi Sinare Maajar, Wakili wa kujitegemea Vulfrieda Mahalu na Mkuu wa Shule ya Elimu ya UB, Profesa Elias Bayona.

Chanzo: Gazeti la Tanzania Daima la Jumapili, Agosti 17 Mwaka 2014.

HONGERA DK.FELESHI,MKASIMONGWA KUTEULIWA KUWA MAJAJI


HONGERA JAJI DK. FELESHI, MKASIMONGWA KUTEULWA KUWA MAJAJI

Na Happiness Katabazi
RAIS Jakaya Kikwete Jana  alimteua aliyekuwa  Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP),Dk.Eliezer Mbuki Feleshi "Msukuma' (47) na wasomi wengine washeria nchini akiwemo Aliyekuwa Katibu wa Jaji Mkuu, Edson Mkasimongwa " Raia wa Msumbiji' '  Kuwa  Majaji wa Mahakama Kuu  ya Tanzania.

Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo Vya Habari iliyonysha  Majaji hao wataapishwa Na rais Kikwete Agosti 15 Mwaka huu, Ikulu Dar Es Salaam.

Awali ya yote napenda kutoa pongezi kwa Rais  Kikwete Kwa kuteua jumla ya Majaji 20 jana, idadi ambayo ni kubwa na ni Kama imetekeleza ahadi zake ambazo amekuwa akizitoa  kupitia hotuba zake  mbalimbali Katika siku ya Sheria nchini ambayo ufanyika mwanzoni mwa wiki ya kwanza ya Februali kila Mwaka ambapo binafsi nimekuwa nikiudhuria na amekuwa akihaidi  Kuwa   Katika Utawala wake ataakikisha  anateua   idadi kubwa ya Majaji ili idadi ya Majaji nchini iongezeke na idadi hiyo iende kumaliza mlundikano wa Kesi mahakamani na  Hilo amelitimiza  kwa Mara ya Tatu sasa.

Kwa faida ya wananchi wasiyomfahamu Jaji mteule Mkasimongwa. Mkasimongwa ameishawahi Kuwa Hakimu Mkazi  Katika Mahakama mbalimbali hapa nchini na Kabla ya Kuwa Hakimu aliwahi Kuwa karabiner wa Mahakama na Akaamua kujiendeleza na fani ya Sheria na hatimaye akawa Hakimu na mwisho wa siku Jana akatandika   historia mpya kwa  Rais   Kikwete Kumteua  Kuwa Jaji wa Mahakama Kuu nchini.

Kwa wale tuliokuwa  tunafuatilia na kuudhuria   Kesi ya matumizi mabaya ya madaraka iliyokuwa inamkabili Aliyekuwa Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala wa Benki Kuu, Amatus Liyumba  Katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar Es Salaam, ilikuwa ikisikilzwa na jopo la Mahakimu wakazi watatu Mkasimongwa, Lameck Mlacha na Jaji mteule Benedict Mwingwa. Siku ya kutoa hukumu Jopo Hilo lilitofautiana kimaamuzi. 

Ambapo Mkasimongwa alitofautiana na wenzake ' yeye kwa upande wake alitoa hukumu ya kumwachiria Huru Liyumba " Decent Judgement' lakini  Mlacha na Jaji Mteule Mwingwa walitoa hukumu ya Kumtia hatiani Liyumba Kifungo Cha Miaka miwili gerezani ambapo hukumu ya Mahakama iliyohesabiwa ni hukumu iliyotolewa na Mahakimu wale Wawili na hukumu ya Mkasimongwa ikitunzwa Kwenye rekodi ya Mahakama.

Mkasimongwa Kabla ya Kuwa Katibu wa Jaji Mkuu, alikuwa ni Mwenyekiti wa Baraza la Ushindani. Pia Mkasimongwa ndiyo kiongozi wa jopo la Mahakimu wanaosikiliza Kesi ya wizi wa sh Bilioni Sita (EPA), inayowakabili ndugu Wawili Johnson Lukaza na Mwesigwa Lukaza Katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, ipo Katika Hatua ya usikilizwaji.

Hivyo Mkasimongwa Kuwa Jaji inawafundisha makarani  wa Mahakama Kuwa ,wakiamua kujiendeleza kielimu Kama Alivyofanya Mkasimongwa ambaye  ni mzaliwa wa Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara , ipo siku nao wanaweza kutoka Katika Kazi ya ukarani Kuwa Hakimu na jaji pia.

Hongera sana rafiki yangu Mkasimongwa ambaye yeye amekuwa akinitania Mimi na Mzee wangu Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufaa, Laurian Karegeya Kuwa sisi ni raia  wa Rwanda kwasababu sisi ni Wanyambo tunaotokea wilaya ya Karagwe Mkoani Kagera na kwamba twende nchini Afrika Kusini , tukamzike ndugu yetu Patrick Kalegeya ambaye alikuwa ni Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa wa Rwanda ambaye aliuwawa nchini Afrika Kusini.

Na mimi ( Katabazi) na Jaji Kalegeya  tumekuwa tukimtania sana tu Mkasimongwa Kuwa yeye ni Raia wa Msumbiji na tunashangaa sana huyu Jaji Mkuu Mohamed Chande Othaman kukubali Kuwa na Katibu wake ambaye  ni raia wa Msumbiji yaani Mkasimongwa na kwamba tu najiandaa kwenda Idara ya Uhamiaji kwenda kutoa taarifa Kuwa Jaji Mkuu Othaman anamuhifadhi raia Huyo  wa Msumbiji na kwamba Ndio mAana wakazi wa Mtwara wanachoma Mahakama kule mkoani Mtwara Hawachukulii Hatua kwasababu raia mwenzio wa Msumbiji ni Katibu wa Jaji Mkuu. Hongera Mkasimongwa.

DK.ELIEZER  MBUKI FELESHI ' MSUKUMA'

Dk.Feleshi ni DPP wa kwanza  kushika wadhifa wa Ukurugenzi wa Mashitaka akiwa na umri Mdogo kuliko watangulizi wake na Ndie DPP aliyevunja rekodi ya kukaa Katika Kiti hicho kwa  muda mrefu ukilinganisha na watangulizi wake tangu Tanzania ilipota Uhuru wake. 

Hakuna Shaka wala ubishi kwamba Mimi Happiness Katabazi ndiye nilikuwa Mwandishi pekee nchini ambaye nilianza na kumaliza kufanyakazi kwa karibu sana na DPP-Feleshi na Timu yake ya waendesha Mashitaka ambayo Mimi niliipachika  jina la " Siafu wa DPP'

Dk.Feleshi Ana shahada ya Uzamivu   ya Criminology and Penalogy ya Chuo Kikuu Cha Dar Es Salaam.

Kwa Wenzangu na mie tunaofuatilia masuala ya kisheria hapa nchini, huwezi kuzungumzia Kesi Abdalah Zombe na wenzake,Basil Mramba, Kesi za EPA, Kesi za utakatishaji Fedha, Uvuvi haramu, matumizi Mabaya  ya madaraka, ugaidi, maandamano haramu, uchochezi, DECI, Kesi ya Vigogo wa Suma JKT, dawa za kulevya,Pembe za ndovu bila ya kumtaja au kumkumbuka Dk.Feleshi na vijana wake yaani Mawakili wa serikali Kwani ndiyo walikuwa akizifungua Kesi hizo na kuziendesha mahakamani.

Binafsi Nitamkumbuka Feleshi ambaye ni kaka yangu na rafiki yangu na amekuwa Mshauri wangu mkubwa hasa Katika Maisha yangu binafsi, Kazi  na Katika harakati zangu za kujiendeleza kielimu Katika fani ya Sheria Kwani nikutanapo naye uwa napenda kumwambia Kuwa  ipo siku nitakuja kuandika historia ya Kuwa DPP mwanamke nchini tunacheka sana na yeye pia amekuwa akipenda kuniita Binti wa Kinyambo,Binti wa Katabazi na kunitania  Kuwa Mimi ni raia wa Rwanda na Mimi na mwambia  yeye ni Msukuma na Wasukuma wanafuga Nyoka.

Katika Utawala wa Feleshi , aliruhusu maofisa wake  (Mawakili wa serikali) kutoa ushirikiano  wa hali na mali kwa sisi waandishi wa Habari za mahakamani na kweli tulipewa.

Feleshi ambaye kwa sasa ni Jaji Mteuli, siyo tu alikuwa ni Chanzo Cha Habari Kwa sisi waandishi wa Habari za mahakamani, Bali Feleshi wakati mwingine alijigeuza Kuwa mwalimu kwa sisi waandishi wa Habari ambao tulikuwa tutafika ofisini kwake kumuuliza kuhusu taarifa mbalimbali zinazohusu Kesi mbalimbali  ambazo tulikuwa Tunataka tuziandike bila kufahamu Kuwa tukiandika Habari hizo Mwisho wa siku tunavuruga Kesi na kuupa wakati mgumu upande wa jamhuri Katika Kesi hiyo.

Dk.Feleshi alikuwa akitusikiliza na kueleza faida na Hasara za kuandika taarifa hizo wakati vyombo Vya dola zinazifanyia  Kazi, na tulikuwa tuna mwelewa na kweli baadhi ya  waandishi wa Habari za  mahakamani tuliokubali kusikiliza nasaa za Dk. Dk.Feleshi za kututaka twende tukasome Sheria na tuwe wazalendo  na tuwe na subira na kufanya utafiti kwanza Kabla ya kuanika Habari,  Matunda ya ushauri wa Feleshi ambaye ni Mbobevu  wa masuala ya uendeshaji wa kesi za jinai nchini,  tumeanza kuyaona.

Kwani waandishi wakongwe wa Habari za mahakamani (Katabazi), Bernad James(Citzen), wanafunzi wa sheria wa Chuo Kikuo Kikuu cha Bagamoyo(UB) na Faustine Kapama(Daily News) (OUT), tupo Katika vyuo hivyo tu naendelea kusoma shahada ya Sheria na siku hizi wala hatupati Shida ya kujua lugha za kisheria na tunazungumza lugha Moja na Wanasheria.Nakushuru sana Dk.Feleshi.

Hakika mchango wako Dk.Feleshi kwa sisi wanahabari wa Habari za mahakamani tutahukumbuka na ushauri tutauzingatia, na kwakuwa hivi sasa umeama toka Kwenye Mhimili wa serikali kwenda Kwenye Mhimili mpya wa Mahakama, tutakutana huko na tutaendeleza harakati zetu za kukuza utawala na uwelewa wa Sheria.

Dk.Feleshi kutoka uwakili wa serikali ambao Wakili wa serikali awapo  mahakamani uwa anaiomba  Mahakama, na sasa Feleshi amekuwa Jaji anakuwa sasa ni mtu  wa kutoa Haki na kutafsiri Sheria "Precedent" na kukubali au kukata Maombi ya yanayowasilishwa Mbele yake na pande mbili Katika Kesi husika.Nitacheka sana siku nikimuona Dk.Feleshi akiwa amekaa  Katika Kiti ha Enzi Kama Jaji  anasikiliza Kesi na sitojali " Contempt of Court".

Ikumbukwe siku Chache   baada ya Dk.Feleshi kuteuliwa Kuwa DPP, ndipo Tanzania ili achana na utaratibu wa maofisa wa Polisi Kuwa waendesha mashitaka.Polisi wa lirudishiwa jukumu Lao la upelelezi na Mawakili wa serikali chini ya Ofisi ya DPP ndiyo ikachukua jukumu la Kuwa linaendesha Kesi za jinai mahakamani.

Poleni Ofisi ya DPP,Kwani mlimzoea Boss wenu Feleshi lakini ndiyo hivyo Rais  Kikwete kampa jukumu jipya la Ujaji.Ombi langu Kwa DPP ajaye aendeleze mazuri yaliyoachwa na Feleshi na Mabaya asiyafuate na aje na mikakati yake Mipya ambayo ataona yataongeza   tija Katika ofisi hiyo.

Nawatakia kila la kheri Majaji wataeule wote akiwemo Feleshi, Mkasimojwa, Mwingwa ,mungu awatangulie Katika nafasi hiyo mpya , Muende mkatende Haki kwa mujibu wa Sheria. 

 Agosti 14 Mwaka 2014: Chanzo: www.katabazihappy.blogspot.com: Facebook: Happy Katabazi.

TUJIKUMBUSHE MAKALA HII ILIYOCHAPISHWA NA GAZETI LA TANZANIA DAIMA JUMAPILI ,APRIL 15 MWAKA 2007

DPP KIJANA ANAYEINGIA OFISINI NA MSAAFU WA SHERIA 
Na Happiness Katabazi

ELIEZER MBUKI FELESHI

.Ndiye DPP mpya Tanzania, ana miaka 39
.Apania kumfuta tongotongo Rais Kikwete
.Aliungurumisha kesi ya MV Bukoba
.Adai ilijaa mambo ya ajabu, ataka kutungia kitabu
.Uhaba wa wanasheria wampasua kichwa

HIVI karibuni Rais Jakaya Kikwete, alimteua mwanasheria mwandamizi wa serikali, Eliezer Mbuki Feleshi (39), kuwa Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP). Uteuzi wa Feleshi ambaye alijizoelea sifa nyingi wakati wa kesi ya MV Bukoba aliposhiriki kama mwendesha mashitaka msaidizi na mchango mkubwa alioutoa katika tume ya kuchunguza mauaji ya wafanyabishara wanne wakazi wa Mahenge, ambayo iliwatia hatiani polisi, umekuwa ukielezwa na baadhi ya watu kama muarobaini wa ofisi hiyo. Katika makala hii MWANDISHI WETU HAPPINESS KATABAZI, anamuhoji jinsi alivyoupokea uteuzi huo, na pia alivyojiandaa kukabiliana na changamoto za ofisi hiyo.

Swali: Kuteuliwa kwako na Rais Jakaya Kikwete, kuwa Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) katika umri mdogo ulionao, kumedhihirisha jinsi rais alivyo na imani na utendaji kazi wako, umeupokeaje uteuzi huo?
Jibu: Nimeupokea kwa heshima kubwa. Natambua kuwa rais ananiamini na ndio maana akafikia uamuzi wa kunitwisha mzigo huu mzito katika umri mdogo nilionao.
Lakini uteuzi wangu nina hakika umezingatia sifa zilizowekwa kikatiba za mtu anayestahili kuteuliwa kushika wadhifa huu, binafsi ninafarijika kwamba, Mheshimiwa Rais aliisoma katiba kabla ya kuniteua, na aliporidhika, ndipo akaniteua.
Ni fahari kwangu, familia yangu, vijana wenzangu na taifa kwa ujumla, kuwa na vijana wanaoweza kuaminiwa na kukabidhiwa majukumu makubwa kama hili la kuongoza ofisi nyeti na kubwa.
Kazi iliyopo ni kuhakikisha kuwa simuangushi rais wangu na Watanzania kwa ujumla, nimepania kuwaonyesha kuwa vijana tunaweza kazi.

Swali: Umejipanga vipi kuthibitisha kuwa unaweza?

Jibu: Jambo la msingi ambalo nitalizingatia siku zote, nitakapokuwa katika ofisi hii, ni kutekeleza majukumu yangu kwa kuzingatia taratibu na misingi ya sheria ambayo ndio muhimili mkuu wa ofisi hii.

Misahafu ya sheria haidanganyi hata siku moja, na mimi ni muumini wake mkubwa, siku zote nimekuwa muumini wa sheria na ninaziishi, na kwa imani yangu hiyo ambayo imenipa mafanikio tangu nikiwa ngazi za chini, naamini nitafanya kitu kitakachomtoa tongotongo rais wangu.

Mimi na wenzangu tumeshajipanga, na bado tunaendelea kujipanga, sina cha kueleza zaidi katika hili…, unajua ofisi kama hizi ndugu yangu mambo mengine yanabaki ya kiofisi, lakini ninachotaka kuwaambia Watanzania ni kwamba, nitaiendesha ofisi hii kwa kufuata taratibu na sheria za nchi.

Bahati nzuri ni kwamba, kuna maofisa wengi tu hapa waliobobea katika fani ya sheria ambao utendaji wao, ninaamini kabisa kuwa hauna shaka hata kidogo, na tangu awali nilikuwa nikifanya nao kazi pamoja, na kwa ushirikiano wa dhati.
Majukumu tuliyokuwa tukitekeleza pamoja hapo awali, si kwamba yatabadilika baada ya mimi kuingia ofisini hapa, hapana, kimsingi ni yale yale, lakini ninachotaka tufanye kwa sasa ni kuhakikisha tunasonga mbele kukabiliana na changamoto zilizopo kwa kuwa nyakati zinabadilika kwa kasi sana.
Na ieleweke kuwa ofisi ya DPP ni ya kikatiba, si ya mtu binafsi, wala haitawaliwi kwa msingi wa umri, bali inaongozwa na mtu anayeonekana kuwa na sifa ya kupewa wadhifa huo. Watangulizi wangu waliteuliwa kushika wadhifa huo si kwa kuwa na umri mkubwa, bali kwa kuwa walikuwa na sifa za kuongoza ofisi hii.

Swali: Kuna malalamiko mengi ya kucheleweshwa kwa upelelezi wa kesi, hasa za mauaji, hili umelipangia mkakati gani?

Jibu: Kesi ni ushahidi, na ushahidi unapatikana kwa kuukusanya. Jamii inao wajibu wa kushirikiana na taasisi zinazofanya upelelezi ili kuharakisha kazi ya kukusanya ushahidi. Kwa nyakati fulani wananchi wamekuwa waoga kutoa ushahidi au wakati mwingine kuutoa kwa wasiwasi.
Kuna wakati wapelelezi wamezorota kufanya kazi zao na kuna wakati wamejitahidi, ila wanakwamishwa na nyenzo.
Kwa sababu hiyo, sipingi kuwa kuna malalamiko kama hayo kutoka kwa jamii, yapo, na ili kukabiliana na hali hiyo, nitaanza kwa kulifanyia kazi tatizo la vitendea kazi, pili ofisi yangu itafanya jitihada za makusudi za kuwaomba wananchi kushirikiana na waendesha mashitaka katika kukusanya ushahidi.
Kikubwa ni kuwaelimisha wananchi kuwa, wanayo sehemu yao ya kutoa taarifa dhidi ya wapelelezi wasio waadilifu, hasa kama wapelelezi wanawazungusha kupokea ushahidi wanaowapelekea, ninaamini nitafanikiwa kuondoa malalamiko hayo.

Swali: Idara yako ina wataalamu mahiri wa kutosha kuweza kukabiliana na changamoto zinazoikabili sasa?

Jibu: Wataalamu wazuri wapo, ila ukweli ni kwamba, hawatoshi. Hili ni tatizo. Mmmm, ni tatizo hili... Nchi ni kubwa na inayo mahitaji mengi. Na idara hii ni eneo lenye changamoto nyingi na kubwa. Hivyo kuna kila sababu ya kuwatambua kwa karibu wataalamu wachache waliopo na kuwathamini, na hili ni kwa idara zote zilizo chini ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Swali: Kuna mpango wa kutenganishwa kwa wapelelezi wa kesi za jinai na waendeshaji wa kesi za jinai, utekelezaji wake utaanza hili?

Jibu: Inatakiwa ieleweke kuwa, hapatakuwa na wakati wa mpelelezi na mwendesha mashitaka kufanya kazi bila ushirikiano wa karibu, kutokana na kutegemeana kwa kazi zao.

Kinachokusudiwa kufanyika ni kuiwezesha Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka kuwa na waendesha mashitaka wa kutosha ili wao kama waendesha mashitaka, wafanye kazi ya kuendesha mashitaka na wapelelezi waimarishe kazi ya kupeleleza na kuwasaidia waendesha mashitaka kupata ushahidi.
Hivyo askari polisi wanaoendesha kesi leo kwa kupewa kazi hiyo na DPP, watapata fursa nzuri ya kufanya kazi za kupeleleza kesi za watuhumiwa mbalimbali. 
Uimarishaji wa mkakati huu ulishaanza, na mwaka ujao wa fedha tunatumaini, baadhi ya maeneo ya nchi yetu, wataanza kushuhudia kesi zikiendeshwa na maofisa kutoka ofisi ya DPP, kuanzia ngazi ya wilaya.

Swali: Hili la kutengenisha majukumu haya likifanyika, ofisi yako itakuwa na mamlaka gani ya kuhakikisha kesi zinaendeshwa katika muda unaotakiwa?

Jibu: Upelelezi ni taaluma iliyo na mafunzo, mbinu na miiko yake, na haitegemei zoezi la kutenganisha kazi ya upelelezi na uendeshaji mashitaka. Hivyo tangu awali wapelelezi wanatakiwa kupeleleza kesi kwa umahiri na haraka. 
Lakini ni matarajio yangu kuwa Ofisi ya DPP itakapoanza kuendesha kesi nchi nzima au katika maeneo machache, polisi waliokuwa awali wanahusika kwenye zoezi la kuendesha mashitaka, watapata fursa nzuri ya kuongeza nguvu kwenye eneo la upelelezi.

Swali: Unazungumziaje madai kuwa baadhi ya mawakili wa serikali hawana ujuzi wa kutosha, na kwamba mishahara midogo inawafanya baadhi yao, wajihusishe na vitendo vya rushwa?

Jibu: Ujuzi haununuliwi, unatokana na mafunzo na utendaji wa mtu mwenye bidii ya kujifunza, kuna mawakili wengi wanafanya kazi vizuri ingawa wana mishahara midogo.
Mshahara mdogo si kigezo cha kula rushwa. La msingi ni kuangalia jinsi ya kumwezesha wakili awe na mshahara mzuri, utakaomwezesha kupangilia mambo yake kwa uhakika, aweze kununulia vitabu vya kujisomea na nyenzo nyingine za kazi, jambo ambalo viongozi wetu wanapaswa kuliangalia kwa jicho makini.

Swali: Una maoni gani kuhusu watu wanaopinga mamlaka makubwa aliyonayo DPP?

Jibu: Katiba iko wazi, na sioni sababu ya kuliongelea hili. Huenda kinachoweza kuangaliwa ni kama kuna ukiukwaji au matumizi mabaya ya madaraka ya DPP. Unajua DPP kama taasisi, hawezi kuwa na tatizo, ila tatizo linaweza kuwa kwa mtu anayeweza kutumia madaraka hayo vibaya, kitu ambacho kitahitaji ushahidi.

Swali: Unaridhika na mfumo wa uendeshaji mashitaka hapa nchini?

Jibu: Siyo mmbaya, naweza kusema unaridhisha, lakini pia ni lazima nikiri kuwa kuna mapungufu yanayosababishwa na uhaba wa vitendea kazi.
Kama nilivyoeleza awali, wataalamu hawatoshi na kuna tatizo la mashahidi kutokupatikana kuja kutoa ushahidi, na hasa katika maeneo yaliyo na mila na desturi za kufanya mapatano ya kutozana fidia.

Swali: Ni tukio gani unalolikumbuka, liwe zuri ama baya katika maisha yako?

Jibu; Ninayo mambo mengi, lakini kubwa ni kesi ya MV Bukoba ambayo nilikuwa mwendesha mashitaka, nikimsaidia Wakili Mkuu wa Serikali W.C. Magoma.
Kesi hii ilikuwa ya mauaji, mamia ya watu walipoteza maisha yao, mashahidi wengi walipokuja mahakamani na kutoa ushahidi, ilinibidi kuwa makini sana, kulikuwa na mambo ya ajabu sana katika kesi hiyo, ni vigumu kuelezea, labda kama kuna siku nitaandika kitabu, nitaeleza kwa unaga ubaga.
Mahakama ilikuwa ikigubikwa na simanzi kila siku kesi hii ilipokuwa ikisikilizwa, kama binadamu, hata mwendesha mashitaka kuna wakati unakuwa na majonzi kama hao waliofiwa na ndugu na jamaa zao, lakini kazi kwanza, nilikuwa natakiwa kusimamia ukweli.

Swali: Tueleze historia ya maisha yako kwa mapana zaidi.

Jibu: Nimezaliwa Julai mosi, mwaka 1967, katika Kijiji cha Malya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza, nikiwa mtoto wa mwisho kati ya watoto tisa wa familia yetu ya mzee Mussa Mbuki Feleshi na mama yangu Ruth N’gweshemi.
Baba yangu alikuwa mchungaji wa Kanisa la African Inland Church na mama alikuwa mama wa nyumbani.

Baba yangu alifariki mwaka 1973 kwa ajali ya gari na mama yeye alifariki mwaka 1991, wakati huo nikiwa mwanafunzi wa sheria katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Nimesoma Shule ya Sekondari Shinyanga, baadaye nilijiunga na Shule ya Sekondari Galanos mkoani Tanga ambako nilisoma kidato cha tano na sita.

Baada ya kumaliza kidato sita nilijiunga na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT Ruvu).
Nilijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwaka 1991, nikichukua shahada ya kwanza ya sheria na kuhitimu mwaka 1994. mwaka 2003 nilirudi tena Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kusoma shahada ya uzamili ya sheria (Masters in Law), nilihitimu mwaka 2005.
Kabla ya kuteuliwa kuwa DDP, nilikuwa Mwanasheria wa Serikali na kituo changu cha kazi kilikuwa mkoani Mwanza. 

 PhD in Law Criminology and Penology. Nina mke mmoja, Suzana Majija, ambaye ni mwalimu wa Shule ya Msingi Nyamagana mkoani Mwanza na tuna watoto wanne. 

0716 774494
www.katabazihappy.blogspot.com
facebook: Happy Katabazi

Chanzo;Gazeti la Tanzania Daima Jumapili, April 15,2007