POLISI TEMEKE MMETUFURAHISHA WATANZANIA WENYE AKILI TIMAMU


Na Happiness Katabazi

JANUARI 27 Mwaka huu, Jeshi la Polisi Mkoa wa Temeke lilifanikiwa kuwadhibiti na kuwatawanya Waandamaji haramu wa Chama cha Wananchi CUF, na kuwashushua kisago kitakatifu wafuasi wale waliokuwa wamekaidi amri ya Jeshi ka Polisi iliyokuwa imeyapiga marufuku maandamano na mkutano ule.

Nimetazama zaidi ya Mara 20 video ya jinsi Jeshi la Polisi Temeke ' lilivyowachangamkia' yaani kuwashushia kipigo wavunja sheria wale , Nimefikia uamuzi wa kukubali Kuwa  Polisi Temeke siku ile walifanyakazi Yao ipasavyo na wanastahili pongezi .

Na siyo Siri hiyo video nimekuwa nikiisambaza kwa vijana ambao nawafahamu ni malimbukeni wa siasa za vyama Vya upinzani kwa makusudi ili waone faida waliyoipata wafuasi wenzao wa CUF walivyochezea kisago 'heavy',.

Vijana  wote na wengine ni watu wazima baada ya kumaliza kutazama video ile wameniakikishia Kuwa Kamwe hawatashiriki,wala kusogelea  maandamano haramu mAana video ile inayoonyesha jinsi Polisi walivyokuwa wakiwashushia kisago Waandamaji imewafundisha Kuwa Polisi siyo watu wa kuwachezea ovyo na kwa upande wa wanawake wamesema kupitia video hiyo hawapo Tayari kuingia Kwenye mahusiano ya kimapenzi na Askari Polisi maana ukimchokoza anaweza kuitoa roho yako kwa kipigo haraka sana.

Baadhi ya watu wamenukuliwa wakilalamika kwenye tafrani lile kuna mwanamke alipigwa na kudhalilshwa na polisin, minamuuliza mwanamke yule Kama alikwenda Kwenye maandamano Yale balaa lile la kipigo lingemkuta?Lisenge mkuta.Wanawake wenzake walikuwa Kwenye shughuli za kimaendeleo na wengine walikuwa wamekwenda VICOBA kuurejesha Marejesho Yao ,yeye akaona ni bora aende Kutenda jinai na akaishia kuchezea kichapo.

Mwanamke Yule na wenzake walijifanya wapo  juu juu Kama 'Ngoma za Daku 'kwa kushiriki maandamano haramu ya CUF kule Temeke Matokeo yake ukaambulia kipigo na Kesi juu.

Kwa kisago kile wewe mwanamke unapaswa ujiulize ni kwanini Mke wa Mwenyekiti wako wa CUF,Profesa Ibrahim Lipumba hakushiriki maandamano Yale haramu?

Nimesema kipondo kile kimenifurahisha mimi na watanzania wote wenye akili timamu na wanaochukia vitendo vya uvunjifu sheria kwani tayari huku  mitaani ,video hiyo inayosambazwa Kwenye mitandao ya kijamii imeishatoa Funzo kwa wale wasiyotaka kutii Sheria bila shuruti na pia imetoa Funzo kwa wale ambao hawapo karibu na walinzi wa vyombo Vya Ulinzi na Usalama Kuwa Askari wa Jeshi lolote siyo raia Mwenzenu na msipende kuwazoea zoea na kuwadharau .

Nimalizie kwa kuliombea Jeshi la Polisi pia liwageukie wafanyabiashara ambao HIvi sasa wamejigeuza miungu watu wanaamka asubuhi wanaamua Kufunga maduka ,hawatoi huduma eti wamegoma kwasababu mashine wanazouziwa na TRA ni za gharama sana na eti hawakupewa Mafunzo ya jinsi kuzitumia.

Tumeshuhudia tumepata Usumbufu mkubwa kutoka tabia hii chafu inayofanana na baadhi ya wafanyabiashara Dar es Salaam, Mwanza na kwingineko.

Minasema HIvi Kama mfanyabiashara anaona hawezi kumudu kununua hiyo mashine ambayo serikali inamtaka aitumie, basi aache kabisa kufanya biashara tumjue ,kuliko kila siku wanajifanya wanamsimamo wa kujifanya watagoma, wakifikisww kidogo wanafungua maduka.

Hawa nao pia wanastahili Kutiwa adabu kidogo ili akili iwakae sawa.Maana huo mchezo wao unasababisha shughuli za kiuchumi kwa baadhi ya watu kutikisika kwaajili ya mchezo huo.

Namalizia kwa kulipongeza Jeshi la Mkoa wa Kipolisi Temeke Dar es Dar es Salaam,   unaongozwa na Kamanda  Kihenya Kihenya mmenifurahisha sana Mimi binafsi,mwanangu Queen 'Malkia' ambaye ni 'Mke Mdogo'wa Boss wenu wa zamani IGP- Said Mwema kwa kutoa dozi nzito kwa wavunja Sheria wale. Wa CUF ambayo CUF Ng'ang'ari ya miaka ya 1995-2002 siyo CUF ya leo CUF ya leo ni sawa na joko la kibisa halina meno.Mungu awabariki sana Polisi Temeke.

Chanzo: Facebook: Happy Katabazi
Januari 31 Mwaka 2015.

TABIA HII ITAKOMA LINI?







TABII HII  ITAKOMA LINI?
Na Happiness Katabazi
KWA Miaka zaidi ya Sita  sasa ya Utawala wa Serikali ya awamu ya nne iliyopo madaraka tumeshuhudia baadhi ya viongozi wa juu Katika taifa hili na wananchi wa kawaida sura zao zikipachikwa Katika viwili viwili ambavyo siyo vyao .

Sura za baadhi ya viongozi wakati mwingine zimekuwa zikionekana Kutenda  na matendo machafu sana na kudhalilisha utu wao.

Aliyekuwa wa kwanza Kutengenezewa picha chafu ni Rais Jakaya Kikwete, mwaka 2009 ambayo picha iliyokuwa na sura yake iliwekwa kwenye Mtandao wa  Ze Utamu ambao hivi sasa Mtandao  haupo.

Baadhi ya watu tuliopata bahati ya kuona picha ile tulishtuka na binafsi nilipokuwa Mwandishi wa habari wa gazeti la Tanzania Daima, niliandika makala ya kumea  picha ile .

Makala ile ilikuwa na kichwa cha habari kisemacho (WAMILIKI WA ZE UTAMU WASAKWE), ambayo ilichapishwa kwenye gazeti la Tanzania Daima la Aprili 29 mwaka 2009.

Na kweli baada ya saa Chache  Mtandao huo au kuweza kuonekana tena Mtandaoni hadi Leo.

Watengenezaji wa picha hizo,wamekuwa wakiendelea bila kukoma na jana usiku Katika mitandao ya kijamii zimekuwa zikitambazwa picha mbili zenye sura inayofanana na Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nnchemba.

 Picha  hiyo ilinisikitisha  na kuanza kuwaarifu watu wangu wa karibu kwa kuwaonyesha hiyo picha na wengine wanafki walijifanya hawataki kuiona na wengine walisikitishwa na wengine walifurahia umdhalilishwaji alivyofanyiwa Nnchemba.

Na wanafki hao ambao wakikataa kuiona picha hiyo yenye sura ya Mwigulu  alivyodhalilishwa, lakini nawafahamu watu Hao ni mabingwa wa kutumia a picha  za utupu na wanazifurahia kimoyo moyo.

Ili makala yangu iwe na kielelezo nimeamua kutumia picha hiyo ambayo inasambazwa  ambayo inaoenekana kufanana na sura ya waziri Mwigulu Kama kielelezo.

Nashauri hata kama unamchukia vipi binadamu mwenzako,tusifikie Hatua ya kufanyia na  hivi, siyo vizuri Kwani tunaowadhalilisha kwa picha hizi Tukumbuke na wao wanastahili Kuwa Kuwa na heshima Mbele ya Jamii.

Tuache unafki na kuficha maovu tuinuke na tukemee vitendo hivi ..Pole Waziri Mwigulu na wengine wote mliopata majeraha kwa kufanyiwa udhalilishwaji   huu.

By Happiness Katabazi
31/1/2015




'WELI SPANA' NI DAWA TOSHA KWA WANASIASA WAKOROFI


* MBUNGE LUSINDE MUNGU AKUPE MAISHA MAREFU
Na Happiness Katabazi

LEO nimepata fursa ya kutaza tena Kipindi cha Bunge kilipoanza hadi kumalizika mchana kupitia Televisheni ya Taifa TBC 1 nakuona michango mbalimbali ya maoni kuhusu Hoja ya Dharula iliyawasilisha na Mbunge wa kuteuliwa watoto wa mjini wanawaita ni wabunge wa kuteuliwa ni ' Wabunge wa Lifti', James Mbatia.

Awali ya yote na kwa moyo mkunjufu napenda kutoa pongezi zangu za dhati kwa Mbunge wa Mtera ,Livingstone Lusinde kwa mchango wake alioutoa Leo bungeni asubuhi  Kwani umejaa ukweli mchungu kwa wa wakorofi ,wazushi na wanasiasa uchwara wa vyama baadhi ya vyama Vya upinzani ambao ni wazi wamefirisika kiajenda na walikuwa wamekusudia kuigeuza Kesi inayomkabili Ya Jinai Na. 25/2015 .

Iliyofunguliwa na Jamhuri dhidi ya Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi wa CUF, Jana Katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Da es Salaam, Kuwa ni Gia ya kujipatia Umaarufu wa kisiasa, kutaka kufanya jaribio la kumuundia mtego mwingine Waziri Mkuu Mizengo Pinda ili ang'olewe madarakani Kama walivyozoea lakini  jaribio Hilo Leo tena limekufa  kifo cha Mende mapema kabisa.

Ama kweli Ngoma ya kitoto yaani 'Ngoma ya wapinzani' ,Na kweli Ngoma ilivyoanzishwa na wapinzani Jana bungeni na Kuzusha tafrani hadi Bunge likaairishwa haijakesha ,hoja ya Mbatia aliyoianzisha kwa mbwembwe imemalizwa na Chikawe, Masaju,Lusinde, Said Mkumba ,Henri Shekifu , Sadifa Hamis Juma 'kilainiii Kama wana nawaa'

Nilimtazama na kumsikiliza Tundu Lissu na baadhi ya wabunge wenzake wa upinzani ,kwanza wakati wakachangia mada zao walikuwa wakionekana Kuwa na jazba Hali iliyosababisha kushindwa kujadili kwa vielezo kinzani taarifa ya Waziri wa Mambo ya Ndani , Mathias Chikawe.

Hali iliyosabisha taarifa hiyo ya Chikawe ambaye ni msomi wa sheria na alishawahi kuwa Mwanasheria wa Serikali kama alivyo Mwanasheria Mkuu wa Serikali George Masaju ambaye naye aliwahi kuwa Mwanasheria mzuri tu wa serikali na kazi alizozifanya na kusaidia serikali kushinda kesi kubwa Si za Kutafuta, zipo wazi.

Taarifa yake kubaki Kama ilivyo kwasababu walioleta hoja ya dharula na wachangiaji wa vyama ya upinzani wameshindwa kuilarua kwa vielezo taarifa hiyo ya Chikawe ambaye Profesa Ibrahim Lipumba yeye upenda kumuita Chikawe Kuwa ni ' Cheki Bob'.

Licha Lissu ambaye alikuwa ni mchangiaji wa kwanza alifanikiwa kumtikisa Spika Makinda kuhusu suala la uchache wa muda na Makinda akatikisa na Akaamua kuufuta uamuzi wake wa awali wa kuwapatia dakika Tatu kila mbunge kuchangia,badala ya Lissu Kumtikisa ndiyo Akaamua Kusema kila mbunge atachangia dakika Kumi .

Huo ni ushindi kwa msomi Lissu ambaye ujasiri wake siyo tu ni wa kuzaliwa nao pia una changiwa na fani ya Sheria aliyosoma pale Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.Hongera Lissu kwa ujasiri huo Kwani katika Hilo ulikumbuka Kanuni inasema je na ukainukuu.Wasomi wa Sheria tunasema ulifanya 'citation'.
Nilichojifunza kwa kwa wabunge wachache wa upinzani Leo kupitia michango Yao kwanza Wengi wao wanapenda kukuza jambo dogo lionekane kubwa, Kutenda matendo ambayo yanazidi kuporomosha heshima ya viongozi wa upinzani na upinzani kwa ujumla, uongo na unafki na kushindwa kujadili mada iliyopo mezani na kuamua kuingiza mada ambazo siyo mada iliyokuwa imepangwa kujadiliwa Leo.

Baadhi ya wabunge wa upinzani Leo waliochangia Walijikuta kujitolea Mifano Yao binafsi Kuwa wamewahi kupigwa na kubambikiwa Kesi na Polisi na kuzungumzia kifo cha Mwanahabai Daud Mwangosi.

Kwa hiyo  ni wazi hawa Tayari wanaupande(bias). Na wakasahau taarifa ya waziri Chikawe ilikuwa ikielezea tukio Moja tu la Temeke lilitokea Januari 27 Mwaka huu ,lilomuusisha Lipumba na Si vinginevyo.

Mfano mzuri Mbowe alipokuwa akichangia pamoja na Kusema alikaa muda mrefu Polisi Central Dar es Salaam, kuakikisha Lipumba anapata dhamana alitumia muda mwingi kueleza eti na yeye alishawahi kupigwa na Bomu, mashine gun na Hao Hao Polisi.

Sasa watu wenye akili timamu tunajiuliza HIvi kweli MTu upigwe na silaha zote hizo nzito yaani Bomu, Mashine Gun halafu uendelee Kuwa mzima tu?Huu sio uongo Mkuu jamani ?

Si ni Mbowe huyu huyu Bunge lilopita baada ya Bunge Hilo kutaja maazimio ya Bunge kuhusu Sakata la Escrow , Mbowe alisimama Bungeni na kumtaka waziri Mkuu Pinda azidishe Ukali maana eti Pinda amezidi Kuwa mpole ndiyo mAana mambo yanavurugika.

Haya tusaidieni Tushike la Mwenyekiti wa Chadema,Mbowe aliyemtaka Pinda awe Mkali au Tushike Mwanasheria wa Chadema, Lissu anayetaka kwa Nguvu zote Pinda aachie ngazi?

Pia Nilichojifunza wabunge wa upinzani wengine ni wasahaulifu akiwemo Lissu.Wametaka Pinda ajiuzuru kwasababu Juni 20 mwaka 2013  ,Pinda alisema ndani ya Bunge wale wote watakao kaidi sheia za nchi watapigwa  na kwamba kauli hiyo eti Ndiyo maana polisi wanaendelea kupiga watu na kwa sababu hiyo Pinda ajiuzuru.Ni aibu ya aina yake.

Kwa faida yenu Nyie wabunge wasahaulifu na msiotaka kufanya utafiti Kabla ya kuzungumza .

Kituo Cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC),  Chama cha Wanasheria Tanganyika, Agosti Mosi Mwaka 2013 kulifungua Kesi ya Kikatiba Na.24/2013 Katika Mahakama Kuu Kandaya Dar es Salaam, dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Pinda 

Juni 6 Mwaka 2014 , jopo la majaji watatu Dk.Fauz Twaibu, Augustine Mwarija na Fakhi Junfu, walitoa uamuzi wa awali wa Kesi hiyo ambapo jopo hilo lilikubaliana na pingamizi la awali lilokuwa limewasilishwa na Wakili wa wadaiwa ambaye alikuwa ni Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambaye kwa sasa ndiye Mwanasheria Mkuu wa serikali Masaju Kuwa walalamikaji walikuwa hawana haki ya kuwashitaki washitakiwa , waliokuwa wanahaki ya kumshitaki Pinda na Mwanasheria Mkuu kuhusu Kauli hiyo ya Pinda ni wanachi na siyo Taasisi hizo  (Legal Person) .

Uamuzi huo wa Mahakama Kuu kuhusu Kauli hiyo ya Pinda upo na hadi sasa naandika makala hii bado Mahakama ya Rufaa haijatengua uamuzi huo hivyo bado ni uamuzi halali na Unatakiwa uwafuatwe na sisi wasomi wa Sheria tunautumia Kama 'refence'.

Sasa nashangaa sana wabunge wetu Hao wanaotaka  Pinda  ajiuzuru wakati Mahakama Kuu ilishatoa uamuzi wa Kesi hiyo na Kesi ile ilifutwa Katika Hatua za awali.

Kweli sasa nalazimika kuamini maneno ambayo yamekuwa yalisemwa na Pinda  aka ' Mchawi' ,Kuwa anaandamwa kwa uzushi na kuchafuliwa kwasababu tu ametangaza kimya kimya Kugombea urais.

Maana misioni 'connection' ya hoja ya dharula ya Mbatia hapa na wabunge wa upinzani kulazimisha Pinda, ajiuzuru.

Kupitia michango hiyo ni wazi kabisa kuna baadhi ya wanasiasa wanamchukia Pinda.Haiwasaidii na ni dhambi kumchukia binadamu mwenzako.

Jana Bungeni wabunge wa upinzani walichukua muda mwingi kuleta tafrani bungeni hadi bunge likaairishwa , tukajua leo watakuja na michango kabambe kumbe hakuna kitu ,wameshindwa kujadili taarifa ya waziri Chikawe.

Na matokeo yake mbunge mmoja wa CUf akaishia kuligeuza Bunge Hilo lisijui ni Kanisa Ka ufufuo na uzima wa kufufua marehemu waliokufa na kuanza kusoma Majina aliyedaiwa ni ya marehemu waliouwawa Unguja na Pemba.

Minajiuliza kuna ufufuo wa marehemu pale Bungeni?  Hayo Majina ya marehemu ingekuwa ni vyema angeyaleka kwenye makanisa yanayofufua wafu Kama yapo lakini siyo bungeni.

Mbunge Habib Mnyaa amesema Lipumba alishasemehe Mauji yale ya Unguja na Pemba, haya Nyie baadhi ya wabunge wa CUF Kama siyo kiherehere cha kujadili bungeni Mauji ya marehemu yake na kuyataja Majina ya marehemu wale ni kitu gani?

Ni kiherehere na Kufirisika Kiajenda .Maana Mwenyekiti wa Chama chenu cha CUF Lipumba, alishasemehe Mauji Yale, kilichowawasha kitu gani Kuja kujadili Mauji yake bungeni kitu gani?

Nafahamu nitawakera sana wale watu wanaopenda ukorofi na wasiyoaka kutii sheria bila shuruti na ambayo kutwa wamekuwa wakishitiki maandamano haramu.Mtanisamehe sana.

Leo katika makala hii namuomba sana Waziri Chikawe katika bajeti ijayo aliombee jeshi ka polisi fedha za kununulia Weel Spana nyingi sana ili zianze kutumiwa na jeshi ka polisi kuwarekebisha akili wananchi wakorofi ambao wameonekana ngozi,akili zao kuwa ngumu sana kama gari aina ya Fiati hali inayosababisha wakipigwa virungu ,virungu vinavunjika.

Weel Spana Katika zama hizi hasa kuelekea Katika wakati wa kupiga kura za maoni ya Katiba Pendekezwa Aprili 30 na uchaguzi Mkuu Mwaka huu unatarajiwa kufanyika Oktoba Mwaka huu, Polisi wa zitumie sana Katika kurekebisha akili za wananchi wakorofi ambao wamekuwa wagumu kutii Sheria Kama shuruti na Miili Yao imekuwa ni migumu Kama Gari aina ya Fiati hivyo Weel Spana ni matumizi sahihi kabisa kwa watu waina hiyo.

Polisi msitumie tena silaha za Moto wala virungu,tumieni Weel Spana kurekebisha akili za hawa wavunja Sheria za nchi kwa makusudi Hali inayo sababisha wananchi wasiyo na hatia na mali zao kuumizwa , wananchi kuishi na wasiwasi na shughuli za uchumi kwenda kwa kusuasua kwasababu ya wapumbavu wachache wenye Malengo ya kujipatia Mtani wa kisiasa kwa kuvunja Sheria za nchini.

Mtu ambaye siyo mkorofi, na havunji Sheria ni Nadra sana kukutana na Weel Spana wala virungu Vya Polisi.

Kumbukeni hata Katiba ya Nchi inatoa haki na inamtaka aliyepewa haki hiyo ambaye ni Mwananchi kutimiza wajibu wake kwa mujibu wa Sheria.

Katiba inasema kila Mwananchi anajukumu la kulinda Sheria za nchi zisivunjwe.Pia Mhimili wa serikali upo pale kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Sheria na kamwe haiwezi kumuona Mwananchi anafungwa Sheria kwa makusudi halafu imuache bila kumchukulia Hatua.

 Kwa maoni yangu Matumizi ya Weel Spana kwa Jeshi la Polisi HIvi sasa ni muhimu sana ili Weel Spana ziweze kurekebisha akili za hawa wananchi ,wanasiasa wakorofi na wavunja Sheria za nchi.

Baadhi ya wapinzani  wanajifanya hawana akili wanaovunja Sheria makusudi hivyo basi Weel span zikitumiwa kwenye Miili Yao Sitasaidia sana kurekebisha akili zao zikae sawa.

Naheshimu mchango wa vyama Vya upinzani nchini ,ila nawashauri kadri siku zinavyozidi kwenda waanze Kujenga tabia ya Kuwa na subira, Kuwa wa kweli Katika baadhi ya mambo mnayo ya jadili Bunge Kwani watu wengine wanaowaaminiwa sana kila macho sema sasa inapotokea kiongozi wa upinzani  nayeye Kusema uongo watu watapoteza Imani na Nyie Kama baadhi ya wananchi walivyopoteza Imani na viongozi wa CCM na serikali.

Binafsi Lissu namheshimu sana lakini kwa kitendo alichokifanya Leo cha kusimama ndani ya Bunge na Kusema uongo Kuwa eti TBC  wamezima Matangazo Yao ili umma usiangalie kinachojadiliwa Bunge wakati sisi tulikuwa tu naendelea kutazama Bunge na kumuona yeye kupitia Televisheni jinsi anavyosema uongo wa wazi ambao umemshushia asilimia Fulani ya uaminifu  kwa wafuasi wake Leo, siyo tabia nzuri.

Lissu msomi wa Sheria ni lazima alisoma somo la Legal Research wakati akisoma shahada ya Sheria ambalo somo Hilo linamtaka msomi yoyote wa Sheria anapojadili jambo lazima awe amelifanyia utafiti.

Sasa Leo Lissu kaka yangu uliteleza kwa kwa Kusema Bila kufanya utafiti Kuwa TBC imezima matangazo yake wakati TBC hadi kufanya hivyo. 

Nguvu nyingi na vitendo Vya Fedha Jana wapunge wa upinzani mlevi fanya bungeni kushinikiza Jana hoja ya Mbatia ijadiliwe lakini hao kujadiliwa ikajadiliwa Leo na Leo yenyewe Nyie mliojifanya mnauchungu wa kuijadili Wengi wenu mlitoka nje ya mada.

Matokeo yake Spika Makinda kamaliza kwa Kusema Bunge lake lina Ruhusu Kesi inayomkabili Lipumba iendelee na anamshukuru wabunge waliochangia hawajaingilia Mwenendo wa Kesi.

Hivyo Lipumba watoto wa mjini kwa hitimisho Hilo la Bunge kuhusu hoja ya Mbatia iliyokuwa ikikuhusu wewe ni kwamba ' hadithi yetu imeishaa hapo'. 

Kashda ,na vibweka vyote Vya wana UKAWA wenzio bungeni vikijaribu kukunusuru wewe vimegonga mwambwa, na hivyo unaendelea kuangaika na Kesi hiyo ya jinai inayokukabili ,Mbatia na Mbowe na wabunge wengine waliokuwa wanajaribu kukusemea bungeni Jana na Leo muda Si mrefu hutawaona Jijini Dar es Salaam, watakuwa kwenye kampeni Katika majimbo yao yanafanya kampeni, hutawaona tena wakikusindikiza Katika Mahakama ya Kisutu. Hiyo inaitwa kila Mtu atabeba  msalaba wake Mwenyewe.

Nasisitiza tena Weli Spana ni kifaha muhimu sana HIvi sasa kutumiwa na Polisi  kurekebisha akili za wapinzani wakorofi na wavunja Sheria za nchi.

Mungu ibariki Tanzania
Chanzo: Facebook: Happy Katabazi
0716 774494
Januari 29 Mwaka 2015




ASKARI SHUPAVU LAZIMA APITE DEPO



* WALINZI WA LIPUMBA HAWAKUPITA DEPO NDIYO MAANA SIYO SHUPAVU 

Na Happiness Katabazi
WALINZI  wa Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba siyo Askari  shupavu kwasababu hawajapita Depo na Lipumba ona haja sasa ya kuajiri walinzi wengine wapya ambao wana Mafunzo na mbinu za kisasa za Kupambana na maadui wako. 

Haiingii akilini Mlinzi wa kiongozi mkubwa kama Lipumba anakubali kudhibiti wa kirahisi  namna   ile na polisi halafu kufurukuta kidogo mbele ya wanaume wenzio 'polisi' ushindwe.

Bora Lipumba uniajiri Mimi niwe mlinzi wako Kwani kwa video hii ni wazi Huna walinzi imara na ipo siku watakuja kukutelekeza kwenye Majanga Kama ya aina hiyo ili wazinusuru nafasi zao.

Tunaambiwa Kuwa mlinzi anayemlinda kiongozi yupo Tayari kufa yeye kwanza  ili kuakikisha anamnusuru kiongozi anakuwa salama Katika balaa lolote. Profesa Lipumba au walinzi wako Hao ni Makorokoroni?

Video hii ,Polisi wameweza kuwazingira  na kuwatandika kirahisi na kumchukua kiraini  Boss wao Lipumba ambaye Lipumba wakati akiwa mikononi   mwa wanaume 'Polisi' alionekana Kuwa mpole sana na nidhamu ya hali ya juu utafikiri siyo Lipumba huyu tunayemfahamu ambaye awapo majukwaani na Katika mikutano ya waandishi wa Habari uwa anajifanya mwanaume  Jabari wa kuongea na Kumea mambo utafikiri anaweza kurusha ngumi,Kumbe wapi.

Binafsi wakati mwingine uwa na wanazarau sana wanaume wanapenda sana kuongeaongea sana huku mitaani na kujifanya wenyewe ni wanaume washoka hawaogopi kitu.

Kwasababu wanaume Wengi wa Ana hiyo nimewashuhudia sana wakifikishwa mahakamani,Polisi au wakiwa magerezani kwakweli wanakuwa na nidhamu ya Hali ya juu, Isipokuwa Swaiba wangu Mchungaji Christopher Mtikila ,huyu ni mwanaume wa Shoka na Nina mkubali sana Kwani hata akiwa mikononi mwa Polisi,Magereza yeye ujasiri wake upo pale pale na kidogooo pia 'mume wangu wa zamani', Mwenyekiti wa Chama cha TLP, Agustine Mrema.

Wito wangu kwa wananchi Tusikubali kushiriki maandamano yanayovunja Sheria za nchi ambayo yamekatazwa mwisho wa siku mtaishia kula kisago na  Fedha za kujitinia majeraha ni tabu kupata, Mwenzenu Lipumba Jana kaugua kidogo Maradhi ya moyo kukimbizwa haraka Hospitali ya mAana kutibiwa, Nyie Maskini wenzangu nani aliwapatia Fedha ya kwenda kujitibia  majeraha?

By Happiness Katabazi
Januari 29 Mwaka 2015.

PROFESSA LIPUMBA ' UMEBUGI MEN'


PROFESSA LIPUMBA 'UMEBUGI MEN'
Na Happiness Katabazi
JANUARI 27 Mwaka huu, jeshi la Polisi Mko wa Kipolisi Temeke, liliamua kutumia Nguvu kuwatawanya wafuasi wa Chama cha Wananchi (CUF) na kufanikiwa kumkamata Mwenyekiti wa Taifa wa Chama hicho Profesa Ibrahim  Lipumba na wenzake .

Polisi walidai wamekiuka sheria za nchi ikiwemo Kutenda kosa  la kukaidi amri ya Jeshi Hilo iliyozuia wasiandamane.

Kwa mujibu wa taarifa ya Jeshi la Polisi , ilisema CUF il iliandika barua ya kuomba Kibali cha kufanya maandamano na mkutano eneo la Mbagala Zakhem Jana lakini Jeshi Hilo lilikataa ombi Hilo na Kabla ya kufika siku ya Jana Jeshi Hilo lilikuwa limeishakipelekea Chama cha CUF, barua ya Jeshi Hilo inayozuia CUF isifanye maandamano Jana na CUF na Lipumba hadi Jana alikuwa hajawasilisha maandishi pingamizi la amri hiyo ya Jeshi la Polisi.

Matokeo yake Profesa Lipumba na wafuasi wake Jana waliamua kutoka ofisini Kwao huku wakitembea  kwa miguu kwa kisingizio Kuwa wanaenda kuairisha mkutano huo.

Lakini Wakati Lipumba na wenzake wakitumia mbinu hiyo ya kutoti waliyofikiti itawasaidia kuwapiga chenga ya mwili Polisi ,na CUF wakisahau Msemo usemao 'katika msafara wa Mamba,Kenge Pia wamo'.

Jeshi la  Polisi kupitia 'mawashawasha wao' yaani makachero wao ,muda mrefu sana Kumbe walikuwa wameishaibini mbinu hiyo ya Lipumba na wafuasi wao ya kukaidi kiaina amri ya jeshi la Polisi iliyotaka CUF wasiandamane.

Hiyo Polisi gani kwenye akili timamu angeshindwa kubaini hiyo mbinu ya CUF waliyoitumia Jana ilikuwa na Lengo la kukaidi amri ya Jeshi la Polisi iliyowataka za wasiandamane?


Ndipo Jeshi la Polisi lipoutangazia umati ule wa CUF Kuwa watawanyike kwasababu wanachokifanya ni kinyume cha Sheria lakini baadhi ya wafuasi waliokaidi ndiyo Polisi waliamua kutumia mabomu ya Machozi na kuwaadhibu waliokaidi na Kisha Kumtia nguvu ni  Lipumba Ambaye ndiye alikuwa Kinara wa maandamano hayo haramu.

Ieleweke wazi kuna taarifa Kuwa Lipumba anataka Kugombea Ubunge jimbo la Temeke kwasababu amechoka Kugombea nafasi ya urais ambayo ameishagombea zaidi ya Mara Tatu na amekuwa akishindwa.

Kwa hiyo kumbukizi hiyo ya Mauji ya waliokuwa wanachama wa CUF kule Pemba ambayo alikuwa akiyaongoza Jana ,ilikuwa ni Karatasi ya kisiasa iliyokuwa imepangwa kutumiwa na Lipumba kuanza kujipitisha kwa wakazi wa Jimbo la Temeke lakini wajuzi wa mambo wamelibaini Hilo Mapema wanamcheka Ujinga.

Wafuatiliaji wa siasa za nchi hii tunajiuliza  ni kwanini kabla ya mwaka Huu wa uchaguzi mkuu , Lipumba na CUF yake imekuwa haifanyi kumbukizi hiyo kwa Maandalizi makubwa kiasi hicho hadi Mwaka huu wa uchaguzi Mkuu wa 2015 ndiyo Lipumba na Chama Chake kiwe na kimuemue cha kufanya kumbukizi hiyo kwa Maandalizi kabambe?

Kuna ajenda gani ya siri ya kumbukizi hii ya mauji ya Pemba.Yaani msiba utoke Pembe - Zanzibar halafu maandamano ya kumbukizi ikafanyiwe Mbagala - Dar es Salaam, wakati wakazi wa Mbagala siyo wafiwa wa Msiba wa kumbukizi hiyo ya Mauji ya Pemba?

Watoto wa mjini tunasema Profesa Lipumba una Lako jambo na Si jingine ni unataka Ubunge wa Jimbo la Temeke. Lipumba Umebugi Men.

Hao marehemu mnaowafanyia kumbukizi nao waliotuhumiwa kuwachinja Askari wa Jeshi la Polisi huko Zanzibar , Mbona CUF haifanyi kumbukizi ya kukumbuka Askari wale waliochinjwa?

 Kila siku wabunge Bungeni wanaomba Jeshi la polisi liongezewe fedha za kununulia vitendea kazi kama mabomu, silaha za kisasa, virungu, uniform Na Polisi waboreshewe mishahara na makazi Yao.

Nauliza mnataka hivyo virungu Vya Polisi,mabomu ya Machozi yanayomilikiwa na Jeshi la Polisi  hayo mabomu ya Machozi yakatumike kufanyia Uvuvi haramu wa Samaki? Au hivyo virungu Vya Polisi mnataka Wapewe watu wa Kabila la Wamasai wakatumie virungu hivyo kuchungia Ng'ombe na Mbuzi?

Virungu na Mabomu ya Machozi ni matumizi sahihi kwa watu wakorofi Kama Lipumba na wenzake .

Cha Msingi hapa ni wananchi watii Sheria bila shuruti .Ukitii Sheria bila shuruti utakuwa umeepuka kupigwa virungu na mabomu ya machozi,mitama,nakozi na Matoke na kung'atwa na Mbwa wa Polisi.

Binadamu wote ni sawa Mbele ya Sheria na Ibara ya 13(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 , inasomeka HIvi; ' Watu wote ni sawa mbele ya Sheria  na wanayo haki , bila ya ubaguzi wowote ,kulindwa  na kupata haki sawa  Mbele ya Sheria'.

Kwa Tafsiri nyepesi ya Ibara hiyo ,Jeshi la polisi limetekeleza matakwa ya ibara hiyo kwa kukukamata wewe na wenzako licha unayo madaraka makubwa na kukufikisha katika mkondo wa sheria kwasababu watu wote ni sawa mbele ya sheria.

Kwani wasomi wa sheria tunaposema  Usawa mbele ya sheria  basi usawa huo auangalii umri wa ,elimu ,itikadi wala rangi kwani binadamu wote ni sawa mbele ya jicho la sheria.

Nalipongeza Jeshi la Polisi chini ya IGP- Ernest Mangu kwa kuzinduka usingizini sasa kuanza kuwatia 'displine' viongozi wa juu wa vyama Vya siasa Kama Lipumba Jana mlivyomtia adabu .

Nalipongeza sana mAana hawa viongozi wa juu wa baadhi ya vyama siasa ni Kama mashetani wamekuwa na tabia chafu ya kuwana na ajenda zao binafsi za kuleta Uvunjifu wa Amani nchini ambazo wafuasi wao Wengi hawazijui wanaamua kuwaunga mkono mwisho wa siku wafuasi wao Ndio wanaishia kushughulikiwa na Jeshi la Polisi.

Rais wa Zimbambwe  Robert Mugabe na Rais wa Uganda ,Yoweri Mseveni  huwa hawataki kuendekeza viongozi wa aina hiyo, wanausalama wa majeshi hayo uwa wanaanza kuwashughulikia kwa vipigo vitakatifu Hao viongozi wa juu wa vyama Vya upinzani na viongozi wa juu wa Makundi mengine ambayo yanaamasisha wafausi Hao washiriki maandamano haramu.

Tulimshuhudia Rais Mugabe alivyotoa adabu aliyekuwa kiongozi wa upinzani nchini Zimbabwe ,Tsvangirai na rais Mseveni alipomtia adabu Besige hadi Leo hii hao vinara wa Chokochoko wamefyata Mkia.

Enzi za Utawala wa Rais Benjamin Mkapa wakati jeshila Polisi likiongozwa na IGP- Omar Mahita aliweza kudhibiti na kumaliza Nguvu za baadhi ya wanasiasa wa upinzani na wanaharakati uchwara waliokuwa hawana ajenda zenye mashiko waliokuwa wakikaidi amri ya Jeshi la Polisi .


Mchana wa Leo ,Mbunge wa kuteuliwa James Mbatia aliliomba Bunge liairishwe ili waweze kujadili hoja ya kwanini Jeshi la Polisi limempatia ' mkong'oto heavy ' Lipumba Jana Kwani eti Lipumba ni kiongozi mkubwa,watoto na waandishi wa Habari walioumizwa Jana.

Spika Anne Makinda akitumia mamlaka yake na Kusema ametumia madaraka yake kuimuru serikali Kesho ije kujieleza bungeni kuhusu tukio Hilo.

Wakati Makinda akitoa agizo Hilo, baadhi ya wabunge  kwakweli mi nadiriki kuwaita ni wendawazimu na ambao hawana nidhamu wala staha,waliinuka na kuanza kupinga agizo Hilo la Makinda tena bila kutoa kipengele gani kinawaruhusu kufanya hivyo hali iliyosababisha zogo Kuzuka bungeni utafikiri watu wapo Sokoni.

Jamani, Kama Bunge la Tanzania ambalo wabunge wake ndiyo watunga Sheria na Ndio baadhi Yao wanakuwa wakwanza kutoheshimu na kutii maagizo ya kiongozi wao yaani Spika, HIvi tunaweza Kusema tunawatunga Sheria kweli ?

Nikisema kuna baadhi ya wabunge wa upinzani ni wendawazimu nitakuwa nakosa?Nidhamu na busara kwa wabunge Hao wa upinzani Iko wapi? Eti hawa ndiyo Watanzania turuhusu vyama Vya upinzani kiongozi taifa hili kwa tabia Kama hizi za kiuwenda wazi?haiwezekani.

Mbatia aliyoyasema Leo Bungeni HIvi haramu Mbele ya Wanasheria wa namuona ni Mtu wa ajabu sana?

Maana Kifungu cha 8 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu ya Mwaka 2002, inasema kutofahaumu Sheria siyo kinga yakutoadhibiwa.

Mbatia haelewi Sheria na Huyo Lipumba hawaelewi Sheria hivyo ndiyo mAana wanafikiri hawawezi kufadhiliwa.Mnajidanganya. Mbatia Leo bungeni Kasema eti waliwahi kuzungumza na Rais wa Nchi wakasema eti viongozi wa juu nawatapigwa? 

HIvi rais wa nchi, IGP ni Sheria?Rais wa nchi, IGP wote Taasisi zao zimeanzishwa kwa mujibu wa Sheria na wanatakiwa wafanyakazi zao kwa mujibu wa Sheria.Kama kweli mlikubaliana hiyo basi waliamua kuwageuza viongozi wa upinzani 'Mambululala' kwasababu hamfahamu Sheria na Nyie kwa Ujinga wenu mkakubaliana.

Mbatia acha Sheria Ufuate mkono wake , Mbona Halima Mdee, Sheikh Ponda Issa Ponda walivyoamua tea na kufikishwa mahakamani Mbona hatukukona ukisimama bungeni kuomba Bunge liarishwe ili Mjadili kwanini Mdee ,Ponda wamepigwa na kufikishwa mahakamani?

Na kwa taarifa yenu Nyie wabunge ambao mmezusha zogo Bunge Leo kwa Shinikizo la kutaka ombi la Mbatia la kujadili kipigo kwa Lipumba lijadiliwe Leo, kwa taarifa yenu sisi wasomi wa Sheria tunasema imekula kwenu, Kwani Tayari Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), Biswalo Mganga kaishamwandilisha hati Mashitaka Lipumba na atafikishwa mchana huu Katika Mahakama ya Kisutu Dar es Salaam .

Na akishasomewa Mashitaka ya nayomkabili ndiyo basi tena Bunge linakuwa limefungwa mikono kujadili Kesi iliyopo mahakamani. Kwa Tafsiri nyepesi  Nyie wabunge 'wendawazimu' mliozusha zogo Leo Bungeni mmejiaribia wenyewe .

Mlijiona mnaakili sana kuliko Spika Makinda.Mnamzarau kwasababu ni mwanamke? Sasa mjanja nani Kati ya Nyie wabunge 'machizi' na Makinga?Mjanja ni Makinda na Jeshi la Polisi na Ofisi ya DPP.

Kama mnampenda sana Lipumba jichangisheni Fedha kumuwekee  Mawakili wazuri au pandeni  Ndege nendeni makamuwekee dhamana Katika Mahakama ya Kisutu.

Nashauri Kanuni na sheria ya Bunge ifanyiwe mabadiliko ambayo yataingizwa kipengele cha kuruhusu matumizi ya virungu na mabomo ya machozi  yatumike ndani ya bunge pindi wabunge wakorofi wanapozusha ukorofi ndani ya bunge n kusababisha muda wa bunge kuairishwa kwasababu ya vuugu hizo.

Tumeishabaini Sababu ya wewe Lipumba kuamisha  msiba wa Pemba Kuja Mbagala ni kwasababu  wewe Lipumba umeanza  kampeni za Ubunge jimbo la Temeke Kama mlivyokubalana na viongozi wenzio wa UKAWA katika vikao vyenu vya siri  kuwa nyie viongozi wa juu wa vyama vinavyounda UKAWA  mgawane majimbo yaani mkagombee ubunge badala ya urais kwani tayari mmeishaona nafasi ya urais hampati.Hilo limejulikana.

Profesa Lipu
Kama una huruma na Marehemu  wale siungeenda Pemba ukawakusanya wafiwa Ukawapikia  Pilau na Biliani na Tende na Haruwa ungewapatia na ungeita na viongozi wa dini na Kisomo mngewasomea marehemu wale.

Fanya Kama Mwenyekiti wa Makampuni  ya IPP, Reginal Mengi yeye anawaonea huruma Maalbino,walemavu wa viungo hivyo kila Mwaka amenitengea siku Moja kuwaandalia Mlo wa Mchana anakula nao na kuwasaidia.

Lipumba Janja yako ya kutaka Ubunge jimbo la Temeke imejulikana, na siyo kosa kisheria kutaka Kugombea jimbo ila kosa ni kukaidi amri Hali za mamlaka husika.Usitumie Kumbukumbu za misiba ya watu kujifanyia kampeni katika jimbo ka Temeke, mizimu ya marehemu Hao itakusurubu. Lipumba umebugi  Men.

Chanzo: Happy Katabazi
Januari 28 Mwaka 2015.