WAHITIMU MAFUNZO JKT MLICHOKUWA MNAKITAFUTA MMEKIPATA



Na Happiness Katabazi
FEBRUALI 17 Mwaka huu, niliandika makala iliyokuwa na kichwa cha Habari kisemacho : ' WAHITIMU MAFUNZO JKT MNACHOKITAFUTA MTAKIPATA SOON'. 

Februali 23 Mwaka huu, niliandika makala nyingine iliyokuwa na kichwa cha Habari kisemacho : ' WAHITIMU MAFUNZO JKT KUMBUKENI MLIKULA KIAPO CHA UTII'. 

Na leo tena nimejitokeza tena kuandika makala hii yenye kichwa cha habari kisemacho ' WAHITIMU MAFUNZO JKT MLICHOKUWA MNAKITAFUTA MMEKIPATA'.

Makala  zote hizo zinapatika kupitia Blogg yangu ya www.katabazihappy.blogspot.com na ukurasa wangu Facebook: Happy Katabazi.

Kwa kifupi makala zangu zote hizo zilibeba ujumbe wa kukemea vikali tabia chafu na ya kidharimu na ya uvunjwaji wa Sheria za nchi zilizokuwa zilifanywa  na vijana waliotimu Mafunzo ya JKT ambao Februali 15 Mwaka huu, walifanya mkutano na waandishi wa Habari eneo la Msimbazi Center na Kusema kuanzia Februali 23,24,25 watafanya maandamano ya usiku na mchana Jijini Dar es Salaam, kushinikiza waruhusiwe kuonana na Rais Jakaya Kikwete kwasababu hawajapatiwa ajira.

Vijana Hao ambao elimu zao ni ndogo   minawaona uenda wanawazimu kichwani walifikia hatua ya kutoa baadhi ya  Siri za Mafunzo waliyoyapata JKT Mbele ya waandishi wahabari kwakusema Kuwa wamepata Mafunzo ya kijeshi na kutaja aina za silaha nzito wanazoweza kuzitumia na kwamba wanaweza kujiunga na vikundi Vya ugaidi Kama hawajapatiwa ajira wakati wanafahamu wazi Hakuna mkataba wowote waliingia na JKT wala serikali unaonyesha ni lazima serikali iwapatie ajira.

Pia Katika makala zangu hizo mbili ambazo zilizusha  mjadala mkali ambao wananchi wakiwemo wanausalama toka vyombo Vya Ulinzi na Usalama, maofisa wa serikali na wananchi wanaitakia Mema taifa Hilo walinipongeza  sana isipokuwa baadhi ya watu wachache waliojitambulisha Kuwa ni wahitimu wa JKT  walinitishia maisha.

Kwakuwa mimi ni miongoni mwa waandishi wa kike wachache sana nchini ambao ni jasiri  nilikuwa nikiwajibu hivi siwaogopi ,nakuwatajia eneo nilipo wanifuate wanidhuru kama wataweza na nilizaliwa siku moja na siku moja nitakufa na sitishiki na vitisho vyao. 

Niliwakumbusha wahitimu hao  wakumbuke walikula kiapo cha Utii kwa serikali Yao na hivyo hawapaswi kuvunja Sheria za nchi hii ikiwemo kusaliti Viapo vyao kwa kuandamana, Kugoma na kutaka kufanya uhasi .

Kwa nia njema niliwakumbusha kuwa  Mafunzo waliyoyapata kule 'jandoni' yaani JKT yanawataka  wawe na nidhamu na wa watii   viongozi wao Sheria na Jamii kwa ujumla na niliwaambia  kabisa madhara makubwa wanayoweza kuyapata kutokana na matendo Yao ya kiuwenda wazimu ya kutaka kushindana na dola.Hawakutaka kunisikia.

Ushauri wangu kupitia makala hizo waliuupuuza  lakini naamini kuanzia Februali 22,23 na 24 Mwaka huu, watakuwa kimoyo moyo wanakubali sasa Kuwa Mimi nilikuwa ni mtu mwema Kwao   na Laiti wangezingatia  Nasaha zangu katika zile makala yasingewakuta yaliyowakuta leo hii.

Mabalaha  yote yanayowakumba sasa ya Kukamatwa msobemsobe ,kulazwa maabusu  za polisi, kufunguliwa Kesi za jinai mahakamani na kufungiwa dhamana na Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), kutibiwa  chini ya Ulinzi Mkali wa Polisi, Kuanza kuishi kwa  Mashaka Kama 'wanaoga  barazani ' kwasababu dola linawaandama   yasingewafika.

Ila kwakuwa kwanza walinidharu na kuniona mi ni chizi na kuniita mwanamke Malaya , sina akili nilisema sawa Kwani Tayari nilishajua  vijana wanachezea Moto na hawafiiki Mbali watanasa kwenye nyavu na kweli wamenasana kwenye nyavu tena chap chap.

Kwani   Februali 15 Mwaka huu ,ndipo walipoanza mbio zao za Marathoni za kulichokoza dola kwa kufanya mkutano na waandishi wa Habari  nakuanika mikakati yao ya jinsi ya kuvunja sheria za nchi.

 Kesho yake Februali 16 mwaka huu,  Mungu alimlaani mwenyekiti wa Umoja wa wahitimu hao George Mgoba ambapo watu wasiofahamika  'watoto wa Mbwa'  Walimteka  kwa siku tatu na kumfanyizia.Na Jeshi la Polisi limesema linaendelea na uchunguzi wa kubaini tukio Hilo ni la kweli au ni Sinema ya Kihindi imetengenezwa na Mgoba na wenzake.


Februali 22 Mwaka huu, wahitimu hao tena waliitisha mkutano na waandishi habari eneo la  Msimbazi Center na kutaka iundwe Tume huru ya kuchunguza nani alimteka Mgoba na kwamba Machi 23 Mwaka huu hawataandamana tena wanajipa muda wa kwenda kujipanga zaidi. 

Na kwa wahitimu hawa mi nalazimika Kuwaita ni wendawazimu walipomaliza mkutano huo na wakatoka eneo la walilofanyia mkutano na kuanza safati ya kuelekea hospitali ya Taifa ya Muhimbili alipokuwa amelazwa Mgoba huku wakiwa wengi hali iliyosababisha  Polisi kuwazuia getini kuingia kumuona Mgoba na Polisi kuimarisha Ulinzi eneo Hilo na kuwakamata baadhi ya wahitimu na kwenda kuwaifadhi Katika Kituo Central.

Ilipofika Februali 23 Mwaka huu, Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova  aka ' Marketing Officer '  wa Jeshi la Polisi alifanya  mkutano na waandishi wahabari na Kusema Kuwa kwanza Jeshi lake linafanya uchunguzi kujua ninani alimteka Mgoba na Je ni kweli alitekwa Kama alivyodi , akawataka wahitimu wa Mafunzo ya JKT kuanzia siku hiyo wakome kabisa kufanya maandamano wala mikutano Jijini Dar es Salaam na kwamba  wanawashirikiria wahitimu Kadhaa kwa makosa ya kufanya mikusanyiko haramu na uchochezi na kumtaka Makamu Mwenyekiti wa umoja wa wahitimu hao Kokote alipo  ajisalimishe Mara Moja Katika Kituo chochote cha Polisi.

Tamko Hilo la Marketing Officer wa Jeshi la Polisi Yaani Kamanda Kova  liliwadhiirishia sasa serikali Imechoka na vitendo vyao na imeanza kuwashughulikia Hali iliyosababisha Kunywea kabisa na adabu zao Kuzitia mfukoni.

Minasema asante sana vyombo vyote Vya serikali vilivyofanya kazi usiku na mchana hadi mkafanikiwa kuwasambaratisha hawa wahitimu wa JKT Kwani Katika makala zangu zile mbili niliomba sana serikali kupitia mamlaka zake ziamke usingizini zianze ' kutroti' na wahitimu hao wa JKT ambao wamekosa adabu na nidhamu.

Baadhi ya wahitimu  walinipigia simu nakuniita  Mimi ni   Malaya na hawara yangu  yangu Rais Jakaya Kikwete,Nina utaka  UDC  sina akili na matusi ya kila aina na vitisho Vya kila aina.

Sasa serikali imeishawabananisha kila kona na kuwadhoofisha  na wengine ndiyo mmefunguliwa Kesi na dhamana mmemfungiwa, mmepelekwa gerezani hadi siku DPP atakapojisikia  kuondoa mahakamani hati ya kuwafungia dhamana.

Binafsi sina Shaka kule magerezani mlikopelekwa Jana kuna  mahabusu wanaume wanatabia za kibazazi  wamewapokea  kwa shangwe na sijui kama mtasalimika. 

Hatutaka kusikia Mkilalamika   mahakamani Kama wale viongozi wa dini ya Kiislamu  ambao walikuwa wakijifanya vijogoo kule Zanzibar ambao ni viongozi wa Mihadhara  ya Kiislamu UAMSHO, wanaokabiliwa na Kesi Katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam,walalamika sana Kuwa wamelawitiwa na kuaribiwa vibaya sehemu za Siri wakiwa gerezani .

Je hadi sasa mazito yaliyowafika na jinsi mlivyosambaratishwa na mnaendelea kushughulikiwa, bado mnaendelea na msimamo wenu wa kuniona Mimi ni Malaya Sina na  na mwendawazi?

Kwa upupu huo ambao Tayari serikali kupitia Kamanda  Kova na Manjagu wake ,  DPP- Biswalo Mganga wamewamwagia na unawawasha hivi sasa mnajikuna Umesababisha mfyate mkia, bado tu mnaendelea kunichukulia Mimi sina akili?

Hakuna Mashaka wala ubishi Mimi Happiness Katabazi  ni mwanamke  jasiri sana, nina akili kuwazidi Nyie wendawazimu ambao licha mlipitia Mafunzo ya uaskari nimewatikisa vizuri sana na kufanikiwa kuwavuruga akili zenu ,kusambaratisha mipango yenu hadi hivi  sasa mmeishia kuanza kutumia mbinu za kunipigia simu na kunitumia SMS za maswali ya kipuuzi ambazo zina lengo la kunidadisi Mimi ni nani? 

Kwa akili Zenu Fupi mna mbinu Zenu za kijinga nawaakikishia hamtakaa mfanikiwe hicho  mnachotaka kunifanyia  maana mnatumia mbinu za kijinga jinga Kutafuta taarifa zangu mbinu ambayo hata mwanangu Queen 'Malkia' hawezi kuzitumia  Kutafuta taarifa za Mtu.

Aliyewaambia Nina Shida ya Kuwa na bwana lofa   Katika Kipindi hiki cha Takribani wiki Moja tangu nilipoandika jumla ya makala Tatu kwa mpigo zinazokemea matendo yenu nyie baadhi ya wahitimu wa mafunzo ya JKT ya Uvunjifu wa nani? 

Aliyewaambia Mimi nataka kuolewa na mwanamme ambaye tayari mwanaume huyo ameishautangazia  umma Kuwa Hana ajira, mgomvi kwa serikali ,anakubali kutumiwa na wanasiasa ambao ni wanaume wenzake nani?Tena mnikome sina Fedha za kulea mwanaume  ambaye Hana ajira na Hana nidhamu na anayehatarisha Usalama wa nchi.Mnikome.

Mlisema Mimi misina akili kwasababu zile makala zangu zimewakera, minasisitiza Mimi Nina akili nyingi sana kuliko Nyie Kwani Mimi sasa Naishi huru Nyie mnaishi Kwa Mashaka kwa kuhofia kushughulikiwa na dola.

Mlisema Mimi sina akili na mwendawazimu na Malaya ,Minasema Nina akili sana ndiyo maana kupitia makala zangu kuhusu Nyie, sijafunguliwa Kesi za jinai, Polisi hawajanikamata wala kunisaka zaidi ya kunipa BIG UP kwa makala nzuri, DDP hajanifungulia Kesi na kunifungia  dhamana na wala siishi gerezani Kama mlivyoanza kuishi gerezani Jana .

Haya Nyie wenye akili timamu Leo hii kikowapi Mbona inaelezwa mlivyokuwa mlivyotiwa nguvuni na wanaume wenzenu mlikuwa mnaangua kilio na kuomba msamehewe msipelekwe mahakamani na gerezani?


Hapo Mwendawazimu ni Katabazi au Nyie wahitimu wa Mafunzo ya JKT? Jibu ni Jepesi ni baadhi ya wahitimu wa Mafunzo ya JKT ndiyo wendawazimu na ndiyo maana dola linawashughulikia kikamilifu wao na siyo Happiness Katabazi.

Mlivyoona makala zimeandikwa na mwanamke yaani mimi kwasababu napenda kujipodoa ,mimi raia nyie mmepitia mafunzo ya JKT basi mkanichukulia 'poa'? Hivi mnafahamu kuwa nipo kwenye taaluma ya uandishi wa kwa miaka 15 sasa?  Na Karamu yangu ni Kali sana makala zangu mbili mlizozibeza zimekuwa ni Moja ya Kisu kilichotumika kuwachinja Nyie ? Ndio mjifunze kuwa karamu ina nguvu.

Msimdharau Mtu  msiyemjua, na kumbukeni Kuwa Mwanamke ana Nguvu sana katika mambo mengi tu .Mwanamke anaweza Kujenga famila au Kuibomoa.Mwanamke pia  anaweza  hata Kuaribu kazi ya mume wake.

Sasa kwa taarifa yenu kutokana na ufedhuli wenu mliyoufanya  hata majeshi yetu hayawezi  kuwapa ajira kwasababu mmethibitisha Pasipo Shaka kwamba hamna nidhamu na hampaswi tena  kuaminiwa  kupewa kazi hizo za kijeshi Kwani endapo mkipewa mnaweza kukodisha silaha zetu kwa wahalifu ili wa zifanyie  Uhalifu au mvujishe Siri za Jeshi kwa maadui zetu. 

 Mbona Nyie Askari wa JKT mliojifanya mnaakili Mbona mnaishia gerezani na Kesi ya jinai mmefunguliwa na mmeishakuwa watumwa wa Mahakama? 

Na makala zangu zimemchangia na zitaendelea kutoa hamasa kwa vyombo vya dola vizidi kuwashughulikia  kikamilifu ili mpone huo wendawazimu wenu unaowasumbua vichwani ambao ulikuwa unawatuma kufanya vurugu na kukiuka viapo mlivyokula na mafunzo mliyofunzwa mafunzo JKT.

Askari gani mmepita JKT mlivyo rejea  uraiani mnakubali  kutumiwa kirahisi na  wanasiasa  toka Chama Kimoja cha siasa ambacho Chama hicho kimekuwa na rekodi ya kufanya maandamano na vurugu kila kukicha.

Hivi hamkumjua  Hao wanasiasa  ndiyo  tabia zao za Kupenda kuwatumia hata wanafunzi wa baadhi ya vyuo vikuu wafanye migomo na wanafunzi wakigoma na kupigwa na Polisi na kufikishwa mahakamani yeye wao wakaa Mbali? 

Leo ni familia Zenu na wazazi wenu ndiyo wanaangaika kuwaletea Chakula gerezani na kuwafanya wakose Furaha na Amani ndani ya mioyo Yao kwasababu mmefunguliwa Kesi na mnaishi gerezani.

Askari gani mnakubali kurubuniwa na Raia kirahisi namna hii? Ndiyo aliwaaidi Kuwa eti uchaguzi Mkuu wa Mwaka huu, Chama chao kitakamata  dola na Nyie ndiyo mtakuwa Jeshi jipya la serikali ya Chama hicho ambacho kwa sasa ni Chama cha upinzani.

Haya tambo Zenu, vibweka vyenu ,mikwara yenu imeishia wapi hivi sasa? Mbona mmekuwa wapole ghafla?Si mlitutangazia kuwa ni mmepata mafunzo ya kijeshi na mnaweza kutumia silaha.

Sasa inakuwaje askari nyie wenye mafunzo ya kijeshi mnadai kiongozi wenu ameweza kutekwa  kilaini  na wanawake,  polisi ambao hawana mafunzo Ya kijeshi wanafanikiwa kuwakamata kiraini kama wanakamata Kuku Bandani? Ni kihoja cha aina yake.

Haya wale mabwana zenu waliokuwa  wanawatumia kwa Siri na Nyie mkakubali kugeuzwa geuzwa Kama Chapati na bwana Zenu   yaani wanasiasa  ili muanzishe vurugu hapa nchini, Mbona hajajiokeza Kuwatetea au kumpelekea uji  au supu ,Mgoba Hospitalini au Kuwapeleka Chakula gerezani wale wahitimu wa JKT walipelekwa gerezani Jana?

Ndiyo mkome  na ndiyo muwajue wanasiasa uchwara wa nchi hii walivyo na roho mbaya za kupenda kuwatumia vibaya watoto wawenzao wafanye vurugu ili wapate umaarufu katika siasa na pindi dola ikibaini njama hiyo ikaanza kuwashughulikia wanasiasa hao uwa wanakaa mbali utafikiri hakuwatuma kufanya matendo yale.

Chezea Kamanda Kova aka 'Marketing Officer  wa Jeshi la Polisi'? lazima utadeki Bahari na kweli wahitimu wa JKT mmedeki Bahari. 

Poleni sana kwa mazito yakiyowakuta na yatakayoendelea kuwakuta baadhi ya wahitimu mafunzo JKT na ndiyo muanze sasa Kuwa wapenzi wa makala zangu Kwani  licha ya Mimi Kuwa Mwandishi wa Habari  pia ni msomi wa Sheria hivyo makala zangu nyingi zinasisitiza watu kuheshimu Utawala wa Sheria Kwani Kifungu cha 8 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu ya Mwaka 2002, inasema kutojua Sheria sio kinga ya kutoadhibiwa.

 Wahitimu wa Mafunzo ya JKT mlichokuwa Mnakitafuta mmekipata.Hongera DPP - Mganga, Kamanda Kova na vyombo vyote Vya Ulinzi na Usalama kuwapatia kile walichokuwa wakikitafuta wahitimu Kwa Takribani wiki Moja.

Maana walichokuwa wakitafuta ni kulala selo za Polisi na kweli baadhi Yao wamelala, kufunguliwa Kesi ya jinai kweli wamefunguliwa Kesi ya jinai Jana ,na walikuwa wanahamu kubwa sana ya kwenda kuishi gerezani na kupata ajira gerezani  ili waweze kulala mabazazi ,wash enzi wa tabia na kweli DPP - Mganga amewatimizia Haja Yao ya Kupenda kwenda kulala gerezani DPP amewafungia dhamana. 

Asante sana DPP- Mganga umenifurahisha sana kwa uamuzi huo wa kisheria wa kuwafungia dhamana washitakiwa Hao kwasababu Kifungu cha 148(4) cha   Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya Mwaka 2002, kinakupa mamlaka wewe  DPP  Kuwasilisha mahakamani kwa maandishi hati ya kumfungia  dhamana kwa maslahi ya taifa mshitakiwa yoyote anayekabiliwa na Kesi ya jinai ambayo ina dhamana.

Itakumbukwa kifungu hicho cha 148(4) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 2002, kilitumiwa na aliyekuwa DDP- Dk.Eliezer Feleshi  a mbaye hivi sasa ni  Jaji wa Mahakama Kuu Kamda ya Dar es Salaam, kati Kesi ya uchochezi Na.245/2012 Jamhuri dhidi ya Sheikh Ponda na wenzake 49 Katika Mahakama ya Kisutu .

Kesi hiyo ilifunguliwa rasmi Oktoba 18 Mwaka 2012 na ikimalizika rasmi Mei 9 Mwaka 2013 ,Ponda Kipindi chote hicho alikuwa akiishie gerezani kwasababu DPP alimfungia dhamana na aliachiwa siku hiyo ya Mei  9 mwaka 2013 siku hukumu ya kesi hiyo ilipotolewa ambapo alitiwa hatiani kwa kosa moja tu la kuingia kwa jinai katika kiwanja cha Chang'ombe Markaz ambapo alifungwa kifungo cha mwaka mmoja nje.

Hata hivyo Ponda alikataka rufaa   Mahakama Kuu Kanda a Dar es Salaam kupinga hukumu ya Mahakama ya Kisutu,ameweza kushinda rufaa yake mwaka 2014 Kwani Mahakama Kuu imetengua hukumu ya Mahakama ya Kisutu iliyomfunga Kifungo cha Mwaka mmoja .

Hata hivyo  Agosti mwaka 2013 DPP alimfungulia kesi mpya ya uchochezi Ponda inayoendelea katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro na DPP  Akawasilisha tena hati ya kumfungia dhamana Hali nayosababisha hadi sasa Ponda kuendelea kusota Katika Gereza la Segerea na siku ya Kesi yake anasafirishwa hadi Mkoani Morogoro chini ya Ulinzi Mkali.

Safi sana DPP- Mganga ,lazima wavunja Sheria watambue upo na na hutasita kutumia Kifungu hicho kwa washitakiwa wowote na ulipoteuliwa Kuwa DPP niliandika makala ya kukuelezea wewe ni MTu wa aina gani sasa nafikiri hawa makorokoro hawakuisoma ndiyo maana wakawa wanaovunja Sheria za nchi na kusahau nchi hii Inaongozwa kwa mujibu wa Sheria.

Wahitimu Mafunzo JKT ' washitakiwa ' ile Ikulu mliyokuwa mnataka kwenda mmekwenda sasa tena bila maandamano Kwani basi la Jeshi la Magereza limewaogopesha lifti hadi Ikulu(Gerezani).

Na bila Shaka mmeishaonana na Rais wa Ikulu hiyo ambaye ni Bwana Jela na na ni naimani  ameishawapatia ajira mliyokuwa Mnaitafuta kwa njia haramu.

Naamini tutakuwa tu naonana Katika likizo yenu fupi ambayo ni ya saa Chache kila baada siku 14 kuanzia Leo pale kwa Pilato Katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na mtakuwa mkitusimulia mnaendeleaje na ajira yenu mpya na jinsi mnavyoifanya huko gerezani na Hali hii ya Joto Kali bila Shaka mnajituma sana.

Embu nyie wahitimu wa JKT 'washitakiwa' wa kumbukeni na wahitimu wenzenu mliokuwa mna watetee Katika umoja wenu nawao ili Polisi, DPP na bwana Jela waweze Kuwapa ajira gerezani Badala ya kufanyiwa usajili na kuonekana wanasifa Kama Zenu za kupewa ajira gerezani.

Hakika mmeishia onyesha mna sifa ya kupata ajira gerezani ajira ambayo mnaijua  nyie ,hongereni kwa kupata ajira ndani ya Gereza.Hongereni sana.

Ila nawashangaa mmeupoteza muda wenu mwingi kushiriki mafunzo ya JKT Kama mngefahamu mapema   Moja kwa Moja gerezani kwa kutumia njia hii mliyoingilia jana gerezani na bwana jela akawapa ajira nafikiri hadi KWA muda wote huo ningekuwa mmepata na Promosheni.

Hata hivyo hamjachelewa sana kwa Sababu tangu Jana mlipofikishwa  gerezani mmepata Mafunzo mapya kutoka kwa walimu wanaoitwa NYAPARA .Nyapara hawapatikani JKT wala sehemu nyingine yoyote isipokuwa Magerezani.Hongereni sana.
 
Namalizia Kwa Kusema Kuwa wale mabwana waliokuwa wanawatuma Kutafuta hiyo Kazi ya kwenda gerezani, Mtakapostaafu yaani kutoka gerezani mtawapelekea Habari Kamili Kuwa hiyo Kazi mliyoipata huko gerezani ni kanzi bomba sana. Naamini hivi  sasa  mmekuwa watamu Kama  Mcharo.

Mnaleta ujasiri wa Albino wa kutembea usiku tena katika mikoa ya Kanda ya Ziwa peke yako  lazima utekwe ,ukatwe viungo na uuwawe kikatiri.Ndiyo Nyie wahitimu wa JKT mlikuwa mnalichezea dola limewashughulikia. 

Kutoka Jeshi la Kujenga Taifa (JKT)  hadi jeshi la Magereza  yaani jeshi la kulinda Wafungwa na mahabusu ,hiyo ni ajira nzuri kwenu  ambayo mlikuwa mkiisaka kwa udi na uvumba na vitisho.

Kwa kuwa serikali ya awamu ya Profesa Jakaya Kikwete ni sikivu sana na inawapenda mno Jana imeamua kuwapatia ajira hiyo rasmi huko Katika Gereza la Segerea.Hongera serikali kwa kutekeleza ombi la wahitimu Hao wa Mafunzo ya JKT kwa vitendo.

Hongereni kwa kupata ajira hiyo ambayo Hakuna Shaka mlikuwa mkiitafuta sana na kweli Mungu Amesikia kilio chenu.

 Washindi  wa mbio za Marathoni kutoka Msimbazi  Center, Msitu Kibaha ,  Hospitali ya Taifa Muhimbili, Central Polisi ,Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu  Mpaka Gereza la Segerea   wajulikana jana nao Si wengine ni viongozi wa umoja usiyo rasmi  wa wahitimu wa JKT wa wahitimu wa JKT nao ni Mgoba  ambaye amecheza filamu ya Kihindi na wenzake ambayo stering uwa anakufa, Makamu Mwenyekiti Parali Kiwango, Katibu Linus Steven na wahitimu wengine Emmanuel Mwasyembe, Ridhiwani Ngowi na Jacob Mang’wita.

Mbele ya Hakimu Mkazi Frank Moshi  mawakili wa serikali Wakili wa Serikali,  Nassoro Katuga akisaidiwa na Tumaini Kweka, Hellen Moshi, Janethroza Kitali na Inspekta Jackson Chidunda,  walidai   kuwa Februari 15 mwaka huu katika eneo la Msimbazi Centre, Ilala Dar es Salaam, washitakiwa walipanga njama za kutenda kosa.
 
Alidai siku hiyo katika eneo hilo, walifanya mkusanyiko usio halali kwa lengo la kuandamana kwenda kwa Rais kulazimisha wapewe ajira katika utumishi wa umma, jambo ambalo ni kinyume cha sheria na lingesababisha uvunjifu wa amani. 

Walikana shitaka na upande wa jamhuri ukasema upelelezi bado haujakamilika na kwamba DPP amewasilisha hati ya kuwafungia dhamana na Hakimu Moshi akesema kwa Kuwa DPP amewasilisha hati hiyo Mahakama yake imefungwa mikono haiwezi kuwapatia dhamana hiyo akaamuru washitakiwa wote wapelekwe gerezani hadi Machi 6 itakapokuja kwaajili ya kutajwa.

Nyie vinara wa wahitimu wa Mafunzo ya JKT  Kuanzia   jana mnaitwa ' Wajelajela Gwaaa'. Mlichokuwa   mnakitafuta mmekipata tena haraka sana,hongereni.Kazaneni sana huko gerezani.Ajira za kumwaga Tanzania na atakae ajira na aje.

Mungu Ibariki Tanzania
Chanzo: Facebook: Happy Katabazi
Februali 25 Mwaka 2015.









WAHITIMU MAFUNZO JKT KUMBUKENI MLIKULA KIAPO CHA UTII










WAHITIMU MAFUNZO JKT KUMBUKENI MLIKULA KIAPO CHA UTII

Na Happiness Katabazi
FEBRUALI 15 Mwaka huu, wahitimu wa Jeshi la Kujenga Taifa(JKT), kupitia Mwenyekiti wa Umoja wao huo,George Mgoba aliutangazia umma Kuwa ikifika Leo Februali 23,23 na 25 Mwaka huu, wahitimu wa Mafunzo ya JKT  watafanya maandamano ya usiku na mchana   kushinikiza kuonana na Rais Jakaya Kikwete ili awasikilize matatizo yanayowakabili ikiwemo ukose tu wa ajira.

Mgoba  ambaye vyombo Vya Habari Vya Juzi na Jana vimeripoti habari iliyowanukuu watu wake wa  karibu ambao walidai  Mgoba Amelazwa Katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwasababu alitekwa  na watu wasiyojulikana na kumjeruhi na kumasababishia maumivu makali mwilini Mwake.

Na Tayari Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jana amenukuliwa na vyombo Vya Habari akisema amepata  taarifa za tukio Hilo na Ofisi yake inafanya uchunguzi na uchunguzi ukikamilika atatoa taarifa.

Kwa Kuwa kisheria Jeshi la Polisi ndiyo lenye jukumu la Kutolea taarifa matukio ya Uhalifu, hivyo sote Hatuna budi kusubiri taarifa hizo za uchunguzi zitakazotolewa na jeshi la Polisi Kama ni kweli alitekwa na kufanywa unyamana wa na kwanini watu Hao walifikia Hatua hiyo  ya Kutenda hivyo Kama inavyodaiwa.

Pole sana Mgoba Kama kweli umekutwa na mkasa huo.Pole sana ila naamini Kama kweli umefanyiwa unyama huo wahusika watabainika na watachukuliwa Hatua kwasababu Jeshi la Polisi ni Chombo makini na kina uzoefu mkubwa wa kuchunguza matukio ya kihalifu tena zaidi ya tukio Hilo watu wanalodai umetendewa na washitakiwa uwa wanakamatwa na kufikishwa mahakamani.

Tukiachana na hayo , Turejee Kwenye mada yetu ya Msingi ambayo inawauliza hawa wahitimu wa JKT Leo watafanya yale maandamano Yao Kama walivyotuaidia kwa mbwembwe nyingi licha tayari mpiganisha vita wao (Mgoba) kaisha jeruhiwa na Katibu wao amekamatwa Kabla  ya 'vita 'kuanza?

Inaelezwa Kuwa Askari Wawapo vitani ,Askari mmoja akifa au kujeruhiwa wale Askari waliokuwa salama morali ya kupigana vita ndiyo inapanda na wanazidi kupigana vita kwa  moyo na Nguvu zao zote.

Sasa Leo hii inakuwaje kwa Nyie wahitimu wa JKT ambao mlijinasibu Kuwa mmepata Mafunzo ya kijeshi mna rudi wote mstari wa nyuma Kabla ya tarehe ya kuanza kupigana  'vita 'kuanza kwa kisingizio eti kiongozi wenu ametekwa na kuumizwa?

Ndiyo maƱana Katika makala yangu iliyokuwa na kichwa cha Habari kisemacho: ' WAHITIMU MAFUNZO JKT MNACHOKITAUTA MTAKIPATA SOON'. 

Ndani ya makala hiyo nilieleza wazi Nyie  siyo Wanajeshi na hamjapata Mafunzo ya wanayapata Askari wa JWTZ ndiyo mAana kwanza mipango yenu ni dhaifu, hamna nidhamu ya kijeshi na mnadhalilisha wakufunzi wenu waliowafunza JKT na uenda mlijifunza kupigana na mishale.

Baadhi ya watu waliojitambulisha ni wakufunzi wa Mafunzo hayo baada ya kusoma makala hiyo walinipigia simu na kumitolea vitisho na matusi juu, wala sikutishika na wengine baada ya kusikia Mgoba ametendewa unyama walinipigia na kunishukuru kwa kuwataadharisha na kwamba kilichomkuta Mgoba limewaogopesha na hawatashiriki tena maandamano hayo Kwani wamebaini miongoni mwa wakufunzi wa JKT wameanza kusalitiana hivyo hawataki ugomvi na dola wala kuandamana kwanza wanabiashara zao zinawaingizia kipato na kwamba miongoni mwa wahitimu Hao wanaajenda za kutumiwa na baadhi ya vyama Vya siasa kulea vurugu nchini wamewabaini.

Tangu niliposikia Jemedali wao Mgoba Kuwa ametekwa nimejiuliza ,Jemedali gani anatekwa kirahisi  hivyo tena na watu wanaodaiwa ni wanawake?

Nimebaki na Mashaka Je taarifa za kutekwa kwake Je ni Sinema ya Kihindi ambayo Sinema  ya Kihindi ni kawaida stelingi anakufa Badala ya kusave.

Mgoba alidai wanamafunzo ya kijeshi na wameiva kimafunzo inakuwaje alizidiwa akili na Hao watu wasiyojulikana Kumteka kirahisi hivyo wakati yeye ni Jemedali wa Askari wale zaidi ya Miaka 200 ambao walijinasibu Kuwa wanamafunzo ya kijeshi?

Yaani Jemedali gani wa 'vita' anakubali  kuitikia wito wa kila mtu anayemuita na kwenda kuonana nae?

Kama Jemedari 'Mgoba' amekubali kuitikia wito huo ambao tumeelezwa Kuwa ni wa wanawake ni kweli basi Hao watekaji wanawake ni kiboko na wakiamua hata Leo hii kutumia mbinu hiyo hiyo kuwaita baadhi ya wahitimu Hao ,basi watawadhuru   wahitimu wote kwa njia hiyo ya kidharimu.

Mininachofahamu hivi sasa kutekwa wanatekwa watu wenye ulemavu wa ngozi Albino ambao viungo vya ni dili kubwa na serikali na Jamii kwa ujumla Inaangaika  kutokomeza mauji hayo.

Wengine nao baada ya kusikia taarifa Kuwa Mgoba katekwa wakasema amejiteka Hakuna wakumteka na asitake 'kucompite' na albino na kwamba anataka kuaribu vichwa vya habari vya magazeti na kwamba eti Mwenyekiti wa Chama cha Malbino akimsikia hata mwelewa kabisa kwasababu wanaotekwa ni Albino na taifa lipo vitani kulaani mauji  na utekwaji wa Albino  na siyo watu wasiyo na ulemavu wa Ngozi Kama Mgoba .

Wengine wakasema Angekuwa ametekwa  na kutupwa katika machimbo ya madini kama Geita  wangesema wafanyabiashara wa madini walikuwa wanataka kufanyia mwili wake mambo ya kishirikina lakini Mgoba anadai katekwa na kutupwa msitu wa Mkoa wa Pwani ambako hakuna machimbo ya madini kuna machimbo ya Kokoto ,wanapata mashaka na taarifa hizo.

Wasiwasi  wangu kwa wahitimu wa mafunzo ya JKT ambao mnajifanya mnakiherehe na mpo juu juu kama ngoma za daku katika huo umoja wenu wa kujifanya mnaakili zaidi kuliko wale askari wanaolifahamu ndani nje majeshi yetu.

Jitambueni kuwa nyie bado mi watoto wadogo sana, subirini maelekezo kutoka kwa baba yenu (serikali) ,mkitaka kulazimisha kupewa mnachokitaka mtaonekana ni mamluki.

Askari mdogo yaani mwenye Cheo cha chini siku zote anapokea maelekezo na amri kutoka kwa afande wake anayemzidi cheo na anatakiwa atekeleze maelezo hayo.

Hayo mambo ya kulazimisha na vitisho  mnayotaka kufanya siyo mazuri, Kwani Nyie bado ni  watoto wadogo mnataka Kubeba Mzigo mzito ambao hamuuwezi Kuubeba.

Kwanini watu wasianze kuamini mnatumiwa na mabwana Zenu kufanya hayo Mlivyokuwa mmepanga kuyafanya? Siku 'mkifinywa' mtawataja hao mabwana zenu wanaowatumia kufanya hayo mliyokuwa mmepanga kuyafanya Leo.

Mkae mkijua mkivuka mstari serikali itawashughulikia na Hao mabwana Zenu  wanaowatumia siku mkianza kushughulikiwa wasianze Kulalamika Kuwa Jeshi la Polisi limetumia Nguvu nyingi kuwadhibiti wahitimu Mafunzo ya JKT.

Nawashauri achaneni na mawazo hayo ya Kudai kupatiwa kitu kwa mashinikizo mwisho wa siku mtakao kuja kuaribikiwa ni Nyie binafsi siyo siyo mabwana Zenu wanaowatuma kufanya hayo mnayoyafanya.

Mwenye masikio na asikie na atakayeshupaza shingo na ashupaze ,ushauri wangu Ndio huo wahitimu Mafunzo JKT rudini mtaani mkafanyie kazi  ujuzi mlioupata mlipokuwa JKT na sio kujiunga Katika umoja huo ambao nadiriki Kusema Malengo ya umoja huo yatazamwe upya na mamlaka husika kwasababu Tayari kupitia tamko Lao Katika vyombo Vya Habari limeonyesha umoja huo sio wa kuachwa HIvi hivi tu bila kutazwa kwa karibu na vyombo Vya dola.

Pole Mgoba kwa kuugua,Nina Imani waliokufanyia uhuni huo Kama inavyoelezwa na Hao watu wako wakaribu watakamatwa na Sababu ya wewe kufanyiwa hivyo utajulikana.

Waswahili wanamsemo wao usemao 'usiku wa deni haukawii kukucha'.
 Jumatatu Ndio Leo Imefika wale wahitimu wa Mafunzo ya JKT ambao mlinitolea lugha za vitisho kuwa mtaniua,mtanibaka,mkatumia njia ya kijinga kabisa  ya kunitongoza kwa wingi Kwenye Mtandao,na kunisifia Mimi ni mwanamke mrembo mnaitaji kuonana na mimi haraka ili mnidhuru kirahisi bila kufahamu  na Mimi ni 'Mkubwa wa akili' kuliko Nyie , nikawa nawacheka Ujinga. 

 Na hadi Jana usiku mkajitamba Kuwa lazima mtanidhuru na mtaandamana na kwamba Hakuna cha  kuwazuia lazima Leo mtafanya maandamano hamuogopi Polisi Kwani kwenu Nyie 'Polisi ni Raia wakakamavu.

Sasa usiku wa deni ndiyo umeishakucha ingieni uwanjani tuwaone na msitoe kisingizio cha Mwenyekiti wenu anaumwa kuumwa kwake yeye hakuzui mambo mengine ya Jumuiya yenu yasimame  na msipoingia mtaani Leo kufanya hayo maandamano yenu haramu ya usiku na mchana  nitawafananisha na 'mademu' mAana siku zote madem ndiyo wamekuwa na sifa ya kutoa tisho vikubwa lakini wakiminywa au kutishwa kidogo wanafyata Mkia.

Nitoe rai kwa Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi,Jenerali Davis Mwamunyange  atoe tamko la kufunga mjadala huu unaondeshwa na wahitimu wa JKT kwani ni wazi sasa matendo yao yanadhihirisha yanataka kucheza na ofisi ya Yake ya JWTZ nakutaka kumwandikia rekodi mbaya ya kustaafu  kwako.

Sasa ni wazi kupitia Kundi Hilo la vijana waliohitimu JKT kuna siasa chafu nyuma yake ambazo zinadaiwa kufanywa na Chama Kimoja cha siasa ambacho chama hicho kimekuwa ni mahiri sana ya kuratibu migomo,maandamano hapa nchini.

 JKT na JKU ni sehemu ya JWTZ  na kiongozi wa JWTZ ni wewe Mwamunyange .Leo Wahitimu wa JKT wamefanya waliyoyafanya na wameanika nia yao ovyo ya kutaka kusaliti viapo vyao na ukosefu sa adabu ws kuwaamlisha viongozi wao wafanye wanavyotaka wao badala Viongozi waaamlishe wanavyotaka wao, wasipodhibitiwa hawa siajabu kesho tutasikia nao wahitimu JKU nao wakaibuka kwa madai kama haya na kwa njia haramu Kama hizi za kutumia njia haramu za kuingiza siasa chafu kwa kutumia Majina ya majeshi yetu.

Jeshi Lina Sheria  na Mahakama zake  (Court  Martial) .Askari anapokosea kijeshi upelekwa Katika Mahakama hiyo na kuadhibiwa kwa mujibu wa Sheria za kijeshi. Hivyo wahitimu Wa Mafunzo ya JKT msitake kuingiza masuala ya kijeshi uraiani, waende wanawasilishe Madai Yao ambayo wao wanaona ni ya Msingi kule Jeshini tujue Moja.

Uliona wapi mtoto anamtishia nyau baba yake? Nadhani wenye mamlaka watachukua hatua   Leo wamefanya vijana wa JKT Kesho tunaweza kusikia wahitimu wa JKU ,Naomba  hatua zikichukuliwe na hatua zikisha chukuliwa ni wazi wale wanaowatuma watajitokeza kuwatetea.

Wahitimu wa Mafunzo JKT Kumbeni  mlikula kiapo na Askari yoyote anayesaliti kiapo cha utii kwa serikali yake adhabu yake ni moja tu na iko wazi ni kifo.

Uwenda Hilo mmelisahau   ndiyo maana mmeamua kufanya hayo Mlivyokuwa mmepanga kuyafanya Leo .Acheni Kwani ni wazi mtaumia Kwani Tanzania Inaongozwa  kwa mujibu wa Sheria na ni nchi yenye   Amani na Watanzania na vyombo vyao Vya Ulinzi na Usalama hata siku Moja havitakubali kuwaona  Nyie au Mtu yoyote anafanya vitendo Vya kuhatarisha  Usalama wa taifa hili halafu wakawaacha salama lazima watawashughulikia kikamilifu.

Kumbukeni pia Msemo usemao'Nazi haishindani na jiwe,lazima nazi itapasuka itapasuka. 

Hivyo Nyie wahitimu wa mafunzo ya JKT ni Nazi na serikali ni jiwe.Acheni kutumiwa vibaya na Chama hicho cha siasa kwani mwisho wa siku mtakao umia ni Nyie sio wao kwasababu Nyie ndiyo mnaingia mstari wa Mbele wao wanakuwa wamejificha nyuma.

Na kwa taarifa yote mnayoyafanya yanafahamika, ila kwakuwa mnajifanya mmenificha Gizani hamuonekani Kumbe mmenificha Kwenye mawingu mnaonekana.

Acheni wazimu huo nendeni mkafanyekazi za kuwaingizia kipato na kujenga taifa achaneni na tabia ya kutumia utambulisho wa Jeshi kutumiwa kufanya saisa chafu zinazo hatarisha Usalama wa taifa hili.

Mwisho vitisho vyenu dhidi yangu si viogopi,nilishatishiwa sana na watu wenye mabavu zaidi yenu ila kwakuwa nafanyakazi yangu kwa maslahi ya taifa langu na Kutenda haki na kuwarudisha kundi ni Nyie wahitimu wa Mafunzo ya JKT mnaotaka kusaliti Viapo vyenu Vya Utii kwa serikali ya yetu,Mungu atanilinda na wala siwaogopi niwaakikishie nipo imara na ni nafanya mambo yako Kama kawaida.

Chanzo: Facebook: Happy Katabazi
Februali 23 Mwaka 2015.