WABUNGE WA UKAWA NI WENDAWAZIMU?










WABUNGE WA UKAWA NI WENDAWAZIMU? 

Na Happiness Katabazi 
NOVEMBA 16 Mwaka huu,  Mwanasheria wa Chama cha Demokrasia ( CHADEMA) Tundu Lissu alinukuliwa akisema leo UKAWA wataakikisha wanafanya vurugu kwa kusimama ndani ya bunge na kuakikisha Rais Dk.John Magufuli hatoweza kuhutubia Bunge kwasababu Rais Magufuli siyo Rais na wao hawamtambui.

Kweli Leo saa Kumi jioni tumeshuhudia wabunge wanaounda umoja wa UKAWA wakifanya Fujo ndani ya Bunge tangu alipoingia Rais Magufuli, Rais wa Zanzibar, Dk.Mohammed Shein, Makamu wa Rais Zanzibar Balozi Seif Ally Idd, Makamu wa Rais Tanzania Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassa , Mkuu wa Tanzania Mohamed Othman Jaji Mkuu wa Zanzinzibar .

Wabunge wa UKAWA wakiwa wamesima wakati wakifanya Fujo hizo ambazo zimewashushia heshima Mbele za watu wenye akili timamu ,wazalendo wa kweli walikiwa wakisikika wakisema " Maalim Seif ,Maalim Seif". 

Maalim Seif Sharrif Hamad ambaye ni Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar na ambaye alikuwa ni mgombea urais Katika uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25 Mwaka huu, ambapo Tume ya Uchaguzi Zanzibar ( ZEC) ,ilibaini dosari Katika kura zilizopigiwa Zanzibar hivyo ikatangaza Kuufuta uchaguzi ule hadi tarehe nyingine serikali ya Zanzibar itakapotoa taarifa .

Tangu ZEC ifute Matokeo ya kura za Zanzibar tumeshuhudia Maalim Seif ,aliyekuwa mgombea urais Tanzania, Edward Lowassa ,Tundu Lissu na wana UKAWA wengine Mara Kadhaa wamejitokeza hadharani wakipinga uamuzi huo wa ZEC na kusema Hawatashiriki uchaguzi wa marudio.

Tukiachana na historia hiyo Turejee Katika mada yetu ya Msingi.Kwanza napenda Kusema kilichofanywa na Wabunge wa UKAWA Leo ni uhuni, na pia ni Ishara Mbaya kwa Wapiga kura waliowapigia kura wa aina hiyo kura zao zimepotea bure Kwani wameteua watu ambao ni wahuni maana mhuni anafanya vitendo Vya Uvunjifu wa Sheria, mila na desturi na ndicho kilichofanywa na wabunge wa UKAWA Leo.

Kitendo cha UKAWA kufanya Fujo  wakati rais Magufuli anakuja kuzindua Bunge ni kumuonea na pia ni kutojielewa.

 Maana Ibara ya 38(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inasema " Rais atachaguliwa na wananchi kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii na kwa mujibu wa sheria itakayoweka masharti kuhusu uchaguzi wa Rais ambayo itatungwa na Bunge kwa kufuata Masharti ya Katiba hii".

Sasa Magufuli ni rais aliye chaguliwa na wanachi waliowengi kwa mujibu wa Katiba .Sasa ni ajabu kikundi kidogo cha Wabunge wa UKAWA kinaibuka kinaanza kudharau maamuzi ya wananchi waliowengi waliomchagua Magufuli na Dk.Shein kuwa marais wetu.

Inashangaza sana hawa wabunge wa UKAWA ambao ni watunga wa Sheria ndiyo wamekuwa mstari wa Mbele kuvunja hizo Sheria ambazo zinasema Matokeo ya rais hayapingiwi nje ya Mahakama na ndani ya Mahakama.

Ibara ya 28 (2) (a)ya Katiba ya Zanzibar ya Mwaka 1984 inayozungumzia muda wa kuendelea na urais  inasema ; "  Kuongezwa kwa kipindi cha miaka mitano. 

(2) Kufuatana na maelezo ya kijifungu (1) cha kifungu hiki, Rais ataacha madaraka yake baada ya kumalizika miaka mitano kuanzia tarehe, ambapo:
(a) kama yeye ni mtu ambaye ndiye mara ya kwanza amechaguliwa kuwaRaischiniyaKatibahiialipokula kiapo cha uaminifu na kiapo cha kuwa Rais; n.

Hivyo matakwa ya Ibara hiyo  Kuwa  kama uchaguzi Mkuu utafanyika na mshindi  wa kiti cha  Urais atatangazwa rasmi na Tume ya Uchaguzi, hivyo muda wake wa kuendelea Mtu kuwa Rais ungemalizika kwa kufuatana na masharti ya Kifungu hicho.

Sasa Zanzibar ,ZEC ilifuta Matokeo ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 , na Rais aliyekuwa akimaliza muda wake ni Dk.Shein lakini kwakuwa ZEC ilifuta Matokeo ya uchaguzi hivyo Ibara ya 28(2)(a) ya Katiba ya Zanzibar ina mpa muda wa kisheria Dk.Shein kuendelea kushika wadhifa huo.


Ili  Rais wa Zanzibar apatikane kwa mujibu wa Katiba na sheria ya Uchaguzi nambari 11 ya Mwaka 1984, ZEC  inapaswa kuendesha uchaguzi na hatimae kumtangaza mshindi wa nafasi ya Urais ambae atashika madaraka hayo pale ambapo atakuwa ameapishwa rasmi kwa mujibu wa kifungu cha 31 cha Katiba ya Zanzibar.

Kitendo cha UKAWA kufanya Fujo  wakati rais Magufuli na Rais Shein anaingia kuzindua  Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni kumuonea na pia kumethibitisha wabunge wa UKAWA hawajielewi. 

Hivi Nyie wabunge wa UKAWA mnawazimu kichwani ?Mnaposema hamtambui Dk.Shein Kuwa ni Rais wa Zanzibar huyo Maalim Seif ananukuliwa akisema AMEOIOMBEA kufanya mazungumza na Rais Shein.

Sana Huyo Maalim Seif mnayemuita ni rais Tuonyesheni lini ZEC imemtangaza Maalim Seif ni rais wa Zanzibar ? Huo uhalali wa Nyie kumuita Maalim Seif ni rais mmepata wapi na kwa mujibu wa Katiba na Sheria hipi?

Ndiyo maana Minajiuliza kwamba hivi wabunge wa UKAWA uwenda ni wendawazimu.Kama Maalim Dk.Shein siyo rais wa Zanzibar basi Maalim Seif naye siyo Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar maana hadi sasa Maalim Seif ni Makamu wa kwanza wa Rais Zanzibar kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar.

UKAWA mlijiapiza Kuwa Leo mtaakikisha Rais hatoweza kuhutubia kutoka na Fujo mtakazo fanyia, sasa kwanini mmeshindwa kusimamia msimamo wenu huo wa kihuni na kuingia woga nakuamua kuingia woga baada ya kumuona Spika wa Bunge Job Ndugai kuwageuzia kibao?

Mashujaa gani Waoga? Nijuavyo Mimi Jemedari uwa haogopi wala hatishiki kwa maneno?Sasa Nyie mlijifanya majemedali  kuwa mtaakikisha Rais Magufuli autubii sasa mbona mmeshindwa kumzuia?

Kama mlijua nyie ni waoga wa mkono wa sheria hamtofanikiwa kumzuia Rais Magufuli  asihutubie Bunge Leo kwanini mliingia bungeni na kufanya Fujo kidogo  tu na mkashindwa kufanikiwa kudhibiti rais asihutubie?

Ombi langu kwa Uongozi mpya wa Bunge jipya ,kutokana na vitendo hivi Vya kihuni ambavyo vilishamiri na kukumbatiwa sana Enzi za Bunge la serikali ya awamu ya nne chini ya Rais Mstaafu Jakaya Kikwete na Leo Katika Hili Bunge jipya la serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dk.Magufuli  vione Haja sasa ya kutunga Kanuni Kali za kuwabana wabunge wanaofanya vitendo Vya kihuni ndani ya Bunge kama uhuni uliofanywa na wabunge wa UKAWA Leo .

Aiwezekani mbunge aliyechaguliwa na wananchi anafika bungeni anashindwa kujiheshimu ,kuwawakilisha wananchi wanaamua Kujitoa fahamu nakuanza kufanya matendo ya kihuni na ya kiuwenda wazimu halafu eti hamna Kanuni za kuwabana wabunge wahuni wa aina hiyo Spika anaishia Kusema tu ' eti wabunge wanaofanya Fujo toka nje'.

Hii haitoshi,kuna haja ya Kufungwa Kanuni ambazo zitasema mbunge atakayefanya Fujo bungeni afungiwe kuingia bungeni na akafunguliwe Kesi Katika Mahakama za kiraia.Upuuzi huu unaofanywa Mara kwa Mara na wabunge hasa wa Chadema, CUF unawadhalilisha viongozi wetu, Bunge letu na pia kuwashushia hadhi wabunge walioufanya uhuni huo.

Hotuba iliyotolewa Leo na Rais Magufuli Leo ambayo ili nzuri na imetoa mwelekeo wa serikali yake na kwa mujibu wa Spika Ndugai amesema hotuba hiyo ikajadiliwa Katika kikao kijacho.

Swali langu Je hawa wabunge wa UKAWA ambao wameshindwa kusikiliza hotuba ya Rais Magufuli bungeni Leo, sasa Je ukifika wakati wa hotuba yake kujadiliwa bungeni Je nao wanachangia maoni Yao Kwenye hiyo hotuba ambayo Imebadili mambo mengi kuhusu wananchi wa taifa hili wakiwemo Wapiga kura wao?

Wabunge wa UKAWA mnatakiwa kukomaa kisiasa  Kwani mlichaguliwa na wananchi ili mkawatumikie ndani ya Bunge lakini Leo mmejishushia hadhi  kwa kufanya fujo ndani ya Bunge .

Mnaitaji Kuwa na mikakati ya maana si kwa faida yenu tu baki kwa faida ya wananchi na Ustawi wa taifa kwa ujumla.Jifunzeni kumpinga mtu kwa kufuata staha,Sheria na Kanuni.

Bunge ni Chombo Kilichoanzishwa kwa mujibu wa Ibara ya 62 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 .

Aidha Ibara  64(1)ya Katiba hiyo inasema: "  Mamlaka yote ya kutunga sheria juu ya mambo mengine yote yahusuyo Tanzania Bara, yatakuw mikononi mwa Bunge".

Mtu  mwenye stahaa ,anayejitambua Kuwa yeye ni kiongozi yaani mbunge ambaye ni myunga sheria, anayejiheshimu  hawezi kuamua kufanya uhayawani kama uliofanywa leo na wabunge wa UKAWA ndani ya bunge letu tukufu.

UKAWA eleweni uchaguzi umekwisha aliyeshinda kashinda,aliyeshindwa kashindwa.Yaliyopita yamepita ,rejesheni mshikamano wenu wabunge wote bila kujali itikadi za vyama kwa lengo la kuletea taifa maendeleo.

Maana kama Mnasema hamtambui  Rais Magufuli kwanini nyie wabunge wa UKAWA jana mlikubali kushiriki uchaguzi wa Waziri Mkuu ndani ya Bunge?Maana jina la Waziri Mkuu Kassim Majaliwa lililetwa Bungeni ili mlithibitishe na Rais Magufuli ambaye mmedai hamtambui.

WABUNGE wa UKAWA ebu acheni wazimu ,fanyenikazi kwa maslahi ya wananchi waliowatuma bungeni.Na Nyie wabunge wa CCM baadhi yenu acheni tabia ya kurusha vijembe kwa wabunge wa upinzani Kwani Bunge Hilo siyo la vyama ni Bunge la wananchi. 
UKAWA ni wendawazimu maana mwendawazimu ufanya matendo tofauti na ya kushangaza mbele ya jamii ya watu wenye akili timamu.Na wabunge wa UKAWA leo wamefanya kitendo cha sawa na wendawazimu.Naomba kutoa hoja.


Mungu ibariki Tanzania

Chanzo: Blogg: www.katabazihappy.blogspot.com
Facebook: Happy Katabazi
0716 774494
20/11/2015.

RAIS MAGUFULI UMEINGIA CHAKA



Na Happiness Katabazi

IBARA ya 72 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 inasema ;
"Iwapo mtu yeyote mwenye madaraka katika utumishi wa Serikali, madaraka ya aina iliyotajwa katika ibara ya 67(2)(g) ataamua:-
(a) kuwa mgombea uchaguzi wa Rais au wa nafasi nyingine yoyote chini ya Katiba hii;
(b) kugombea uongozi wa ngazi yoyote katika chama cha siasa kinyume na masharti ya ajira,
mtu huyo atahesabiwa kuwa utumishi wake umekoma tangu tarehe yake ya kuwa mgombea uchaguzi au ya kugombea uongozi katika chama cha siasa.".

Ibara ya 67(2)(g) ya Katiba ya nchi inasema ; "  ikiwa mtu huyo ameshika madaraka ya afisa mwandamizi katika utumishi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano, isipokuwa madaraka ambayo Rais aweza au anatakiwa kukabidhi kwa Mbunge kwa mujibu wa Katiba hii au sheria iliyotungwa na Bunge;

 Kanuni ya  Utumishi wa Umma ( Gorvement Standing Order ya mwaka 2009    ya 20(2) (e)  inakataza Wakili wa Serikali asijihusishe na siasa.

Nimelazimika kuanza na nukuu za Ibara hizo za Katiba na Kanuni hiyo ya Utumishi wa umma kwasababu makala yangu Leo itamjadili hasa masuala Kadhaa ikiwemo taarifa ya Msemaji wa serikali Assah Mwambene ambaye alisema   Rais John Magufuli ametengua uteuzi wa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dk.Tulia Ackson  na Katibu wa Bunge Jana hiyo hiyo akasema amepokea uteuzi wa rais Magufuli Kuwa amemteua Dk.Ackson Kuwa Mbunge .

Sasa taarifa ya Msemaji wa serikali Mwambene Jana inasema Rais Magufuli ametengua uteuzi wa Naibu Mwanasheria Mkuu wa serikali Dk.Ackson  wakati Ibara ya 72  ya Katiba ya nchi inasema ; Iwapo mtu yeyote mwenye madaraka katika utumishi wa Serikali, madaraka ya aina iliyotajwa katika ibara ya 67(2)(g) ataamua:-

Ibara ya 72(b) kugombea uongozi wa ngazi yoyote katika chama cha siasa kinyume na masharti ya ajira, mtu huyo atahesabiwa kuwa utumishi wake umekoma tangu tarehe yake ya kuwa mgombea uchaguzi au ya kugombea uongozi katika chama cha siasa.".

Kwa maana hiyo utumishi wa umma wa Dk.Ackson ulikoma   Novemba 11 Mwaka huu alipoenda kuchukua fomu ya Kugombea Uspika.

Hivyo basi Rais Magufuli kwa mujibu wa Ibara ya Ibara 72(b) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Mwaka 1977 ,hajatengua uteuzi huo ,kwasababu Ibara hiyo inasema wazi kabisa mtumishi wa umma mwenye aina ya Cheo kilichotajwa  Katika Ibara ya 67(2)(g) ya Katiba ya nchi akigombea Uongozi wa ngazi yoyote Katika Chama cha siasa kinyume na Masharti ya ajira kama alivyofanyiwa Dk.Ackson ,mtu Huyo atahesabiwa  Kuwa utumishi wake umekoma tangu tarehe yake ya Kuwa mgombea uchaguzi au ya Kugombea Uongozi Katika Chama cha siasa.

 Kwa  mujibu wa Kanuni ya 20(2)(e) ya Utumishi wa Umma Dk.Ackson alikuwa na cheo cha Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali  ulikoma siku alipoenda kuchukua fomu ya kugombea uspika Novemba 11 mwaka huu na Novemba 14 mwaka huu, Kamati Kuu ya chama chake CCM kilipoteua jina lake, Job Ndugai na Dk.Mwinyi kugombea uspika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo hata hiyo jana Dk.Mwinyi,Dk.Ackson  walitangaza kujitoa na kumuacha Ndugai peke yake kama mgombea spika kupitia CCM.

Hivyo, basi kitendo cha Rais Magufuli  kumteua Dk.Ackson  kuwa mbunge wa kuteuliwa na kutuambia kwamba ametengua uteuezi wake kama Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali  si sahihi kwa sababu kwa mujibu wa sheria nilizo zinukuu hapo juu alishasita kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Kabla ya Jana rais kutengua uteuzi wake.

Alichokifanya Rais Magufuli   ni kuthibitisha tu labda kuwa Dk. Ackson  hafai  kuendelea kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali  hivyo hata kumteua kuwa mbunge si jambo sahihi sana hasa katika ulimwengu huu wa demokrasia ya vyama vingi licha Rais anayo mamlaka ya Kumteua kuwa miongoni mwa wabunge 10 wanaoteuliwa na rais kama ilivyoanishwa Katika Ibara ya 66(1)(e) ya Katiba ya Nchi.

Itakumbukwa Kuwa Novemba 15 Mwaka huu, baada ya Kamati Kuu ya CCM kuteua majina matatu ya makada wake Kuwa miongoni mwa wagombea wa uspika ambapo Majina hayo yalipaswa yapelekwe Jana Katika Kikao cha wabunge wa CCM ili jana hiyo hiyo  lipatikane  jina Moja tu la mgombea wa CCM ambalo litaenda kushindana na wagombea Uspika wa vyama Vya upinzani.

Sasa cha kushangaza Jana asubuhi ilitolewa taarifa ya kwa umma Kuwa Rais ametengua uteuzi wa Dk.Ackson na wakati huo huo Katibu wa Bunge Dk.Thomas Kashilila akatangazia umma kuwa amepokea taarifa za uteuzi kuwa Rais Magufuli amemteua Dk.Ackson Kuwa Mbunge wa kuteuliwa .

Na saa  Chache baadae Jana hiyo hiyo Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye alizungumza na waandishi wa Habari Kuwa aliyekuwa mgombea Uspika Dk.Ackson na Dk.Mwinyi wamejitoa Katika kinyang'anyiro hicho cha uspika hivyo wameacha Ndugai Kuwa mgombea pekee ambaye amepita bila kupingwa na saa Chache baadaye Jana hiyo eti Dk.Ackson ameenda kuchukua fomu za Kugombea nafasi ya unaibu Spika kupitia CCM.Mmhhhh.

Watu tunaofikiri sawa sawa tumeona matukio hayo manne yaliyotokea ndani ya saa zisizo zaidi nane kwa siku Moja tu yaani Jana yanayomhusisha Dk.Nackson ya rais kutengua uteuzi wake, rais Kumteua Ubunge, yeye Dk.Nackson Kujitoa dakika za mwisho Katika kinyang'anyiro Uspika na Dk.Ackson kwenda kuchukua fomu ya Naibu Spika ,siyo ya kawaida na ya nachezwa na watu wazito hasa ambayo mwisho wa siku yameanza kumchafulia sifa Magufuli ambaye Mara zote Katika kampeni zake alikuwa alidai atalinda Sheria za nchi .

Hivi kwanini Magufuli umeamua kujiingiza Katika mtego huu mchafu  mapema kiasi hiki? Rais Magufuli sikufichi  umeanza kujitia madoa na baadhi ya watu Taratibu Tumeanza kukutilia Shaka ?

Huyu Dk.Ackson  kavunja wazi wazi Sheria hiyo ya Utumishi wa umma lakini wewe Rais Magufuli ambaye  wakati ulipolishwa kiapo na Jaji Mkuu, Othman Chande ,Novemba 5 Mwaka huu pale Uwanja wa Taifa uliapa Kuwa utailinda na kuifadhi Katiba , sasa huku Kumteua Dk.Ackson  ambaye amevunja Sheria ya utumishi wa umma wazi wazi na kuiletea sifa mbaya ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kujiingiza Katika siasa wakati akijua hatakiwi kuvunja Sheria.

Najua kuna watu hamtaelewa kwa nini nasema Dk.Ackson amekiuka sheria kugombea uspika wakati yeye ni mwanasheria wa serikali katika cheo cha Naibu mwanasheria Mkuu. 

Ni hivi, makatazo ya kisheria juu ya watumishi wa umma kujihusisha na siasa yamegawanyika katika sehemu mbili, ambayo yanafanya watumishi wa umma wagawanyike katika makundi mawili.

 Kundi la kwanza la watumishi wa umma kwa mujibu wa kanuni ya 20 ya kanuni za utumishi wa umma, hawa ni marufuku kabisa kujihusisha na siasa. Kwa maana nyingine hata kama walipoteuliwa walikuwa wanachama wa vyama vya siasa, mara baada ya uteuzi wanapaswa kurudisha kadi zao au kusitisha uanachama wao. Katika kundi hili wapo askari wapo majaj, mahakimu, wanasheria wa serikali, watumishi ofisi ya msajili wa vyama vya siasa na tume ya uchaguzi.

Kundi la pili, ni watumishi wa kawaida ambao sio askari wala hao niliowataja hapo juu.

 Hawa wanaruhusiwa kujihusisha katika mambo ya siasa, yaani kuwa wanachama na kushiriki shughuli zote za kisiasa isipokuwa tu, hawaruhusiwi kugombea uongozi kwenye vyama vyao vya siasa, nahata pale watakapogombea kwenye nafasi za kisiasa utumishi wao unakoma baada ya kuteuliwa na tume ya uchaguzi au kuteuliwa na rais kuwa wabunge. Dk.Ackson hayupo kwenye kundi hili. Yeye yupo kwenye kundi la kwanza. 

Alichofanya Dk.Ackson ni sawa na leo hii ajitokeze jaji wa Mahakama Kuu akiwa jaji hivyo hivyo aende kuchukua fomu ya kugombea uspika kwa tiketi ya CHADEMA au CCM kisha apitishwe kabisa na chama chake. 

Baada ya hapo Rais ndio aseme nimefuta uteuzi wa mamlaka yako kama jaji, ila nakuteua kuwa mbunge, kwa mujibu wa katiba. Hii si sahihi hata kidogo.

 Je hivi ndiyo rais Magufuli anatuonyesha jinsi anavyotekeleza matakwa ya  kiapo  cha kulinda   Sheria za nchi alizoapa kuzilinda kwa  kumtunuku fasta fasta Ubunge wa kuteuliwa Dk.Ackson ikiwa ni saa Chache tangu utengue uteuzi wake ambao hata hivyo pia umma haujaelezwa Sababu za rais  kutengeua  uteuzi wa Dk.Ackson ambaye aliteuliwa Kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Septemba 9 Mwaka huu na Novemba 11 akajiingiza Kwenye siasa kwenda kuchukua fomu ya kugombea uspika wakati akiwa mtumishi wa umma na Hukutangaza kujihudhuru?

Hivi rais Magufuli kwanini ukuona ni busara Kuwa ulipotangaza kutengua uteuzi wake ,ungetulia watu wasahau alichokitenda basi ipite hata miaka kadhaa au miezi fulani ndiyo umpe madaraka mengine watu wasingehoji na kuanza kukutilia mashaka .

Lakini rais wetu Magufuli unafahamu kabisa bado kuna mijadala ya wananchi kuhusu kilichotendwa na Dk.Ackson za kujihusisha na siasa wakati haruhusiwi kufanya hivyo,wewe sijui huku lions hilo au sijui umeliona ila kwasababu unazozijua umeamua kupuuza ukaamua kusema eti umetengua uteuzi wake na ghafla umemteua mbunge na muda huo huo Dk.Ackson kajitoa kwenye kugombea uspika badala yake kaenda kugombea unaibu Spika.

Hivi serikali na CCM mnafikiri Watanzania wote hatuna akili hadi tushindwe hata kung'amua  usanii 'Perliament Drammer' unaoendelea hapo ambao sikufichi rais wangu Magufuli umekutia doa kabisa tena mapema.

Sawa Rais Magufuli unaweza Kusema wewe siyo Mpiga kura wa kumchagua Spika na Naibu Spika hivyo Katika hili hausiki.

Lakini Kwa mazingira ya matukio hayo manne yaliyofanyika siku Moja ya Jana yanayomhusisha Moja kwa Moja Dk.Ackson ni Ngumu sana watu kuamini Kuwa Ufahamu Sinema yote inayochezeka  na huyo Dk.Ackson ambayo wajuzi wa mambo tumeng'amua muda mrefu na ndiyo maana nakutadharisha rais Magufuli Kuwa Katika hili watu wameanza kupata Mashaka na wewe Kuwa na wewe ndiyo wale wale na CCM ni ile ile.

Tunajiuliza  ni lazima awe yeye tu? huku ameteuliwa akachukue fomu ya kugombea uspika, hapo hapo anateuliwa Kuwa Mbunge , halafu tena tunasikia amejitoa kugombea uspika 
saa chache baadaye ameenda kuchukua fomu ya kugombea unaibu spika tena ndani ya siku Moja ya Jana?

 Hivi, haiwezekani Dk.Ackson akatosha kuwa mbunge tu asubiri kwa imani aliyopewa na Rais labda atateuliwa kuwa waziri au aendelee kutumikia kama mbunge? iwaje tena kugombea unaibu spika? Hapa ndipo zinapokuja hisia za watanzania wengine kwamba huenda huyu anatumwa lakini si yeye kwa utashi wake. Na hili linaweza kumtia doa rais Magufuli.

Hivi sini rais Magufuli huyu huyu Kwenye mikutano yake ya kampeni alikuwa akisema katika serikali yake hatomvumilia mtu anayevurunda na kuvunja Sheria na kwamba hata muamishia eneo Moja au kumpeleka sehemu nyingine na wala hatosubiri   mchakoto na kwamba mtu huyo aliyovurunda mchakato huo ataukuta kwao.

Sasa Dk.Ackson ambaye alikuwa mtumishi wa Mwandamizi wa serikali yake amevunja Sheria ya utumishi kwa kujiingiza wazi wazi Kwenye siasa Mbona hatujaona akifanya alichokisema Kwenye kampeni Matokeo yake Anadai ametengua uteuzi wake na saa hiyo hiyo anamteua Kuwa Mbunge?

Mbona Rais alipoenda kutembelea Hospitali ya Muhimbili hivi Karibuni alibaini uzembe wa kutisha ikiwa ni pamoja mashine hazifanyakazi ,sasa Mbona hatukuona akimtimua Kazi Yule Mkurugenzi badala yake aliagiza Mkurugenzi Huyo aamishiwe Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ili apangiwe Kazi nyingine?

Aidha siku hiyo aliyoenda Hospitali ya Muhimbili ,taarifa ya Ikulu ilieleza pia alibaini eti Bodi ya wa kurugenzi ilikuwa imemaliza  muda wake wa kisheria Miezi miwili iliyopita na kwamba eti akatangaza kuivunja ile Bodi ya wakurugenzi ya Muhimbili.

Sasa sijui ni Mwandishi wa Habari wa Rais ndiyo aliandika taarifa hiyo kimakosa Kuwa rais ameivunja Bodi ya Muhimbili na umma ukaamini hivyo?  Ila najiuliza hivi inawezekana je rais avunje Bodi ambayo ilikuwa Tayari imeishamaliza  muda wake kisheria?

  Bodi ambayo bado haijamaliza muda wa Uhai wake kisheria ndiyo inaweza kuvunjwa . Sasa taarifa ya Ikulu Kusema rais alivunja Bodi ya Muhimbili ambayo Ikulu hiyo hiyo imesema Tayari Bodi ilikuwa imeishamaliza  muda wake minaona siyo sahihi na mnafanya Rais Magufuli aonekane ni Kituko Mbele za watu .

Dk.Ackson licha ni msomi ameandika historia hii ambayo kwa kiasi fulani siyo nzuri kwa sasa kuwa ni Mwanamke wa kwanza Tanzania kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu serikali na msomi mwenye shahada tatu za sheria ambaye ameshika wadhifa huo kwa kipindi kifupi sana ukilinganisha na watangulizi wake .

Septemba 9 Mwaka huu aliteuliwa kushika wadhifa huo na Novemba 11 mwaka huu  akiwa na wadhifa huo na huku akijua hapaswi kuwa mwanasiasa alienda kuchukua fomu za uspika hali iliyosababisha kuzuka kwa mjadala na Novemba 16  Rais katengua uteuzi wake, na yeye akajitoa kwenye kinyanganyiro cha uspika halafu saa chache baadaye akachukua fomu za kugombea nafasi ya unaibu spika.

Na kitendo cha Dk.Ackson Kujitoa Katika mbio za Spika dakika za mwisho kwa kiasi Fulani zinaweza kuhalalisha zile taarifa zisizo rasmi kuwa aliingia au kuingizwa  Kugombea Uspika kwaajili ya kuwawekea kauzibe baadhi ya wagombea ambao walikuwa na ushawishi mkubwa kwa wabunge na wananchi wengi walitamani waingizwe hata tatu bora kama wanasiasa aina ya Samuel Sitta na wengine  ambao majina Yao yalifyekwa na Kamati Kuu Katika hatua za awali na kurudisha jina la Dk.Ackson, Ndugai,Mwinyi ambapo hata hivyo dakika za Mwisho Dk.Ackson ,Mwinyi walitangaza Kujitoa.Kweli siasa siyo chafu ila wachezaji ndiyo wachafu.

Hivi kabisa Msomi mzima wa aina yake anaweza kuamua kujilipua   kwenda kuchukua fomu za Uspika na Kamati Kuu ikapitisha jina lake Kisha dakika za mwisho anajitoa licha ni Haki yake halafu saa Chache huyu huyu Ackson ambaye tunamuuita msomi anaamua kwenda kuchukua fomu ya Kugombea unaibu Uspika? Kweli?

Anapaswa aseme ni kwanini aliamua kuanza kuchukua fomu ya Uspika vikao vikampitisha na dakika za mwisho Kujitoa halafu dakika za mwisho eti anaenda kuchukua fomu ya unaibu Uspika? 

Dk.Ackson anapaswa aeleze umma ni lini alijiunga na CCM?Na Je Oktoba Mwaka huu alipokuwa akiendesha Kesi ya mita 200 Katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar Es Salaam iliyofunguliwa na Kada wa Chadema, Kibatara Tayari alikuwa ni ni Mwana CCM au alikuwa bado?

Lakini pia CCM inatakiwa ieleze umma Dk.Ackson alijiunga na CCM lini?Na Je Kanuni na Katiba ya CCM inataja sifa zipi kwa mwanachama anayeruhusiwa kugombea uspika au madaraka yoyote katika CCM awe na ni mwanachama kwa muda gani?

Je mwanachama ambaye amejiunga leo hii na CCM anaruhusiwa kuchukua fomu ya kuwania nafasi ya uongozi ndani ya CCM? Maana Dk.Nackson alichukua fomu ya Uspika Novemba 11 mwaka huu akagombea na Novemba 14 mwaka huu, Kamati Kuu ya CCM ikamteua yeye na wenzie watatu kugombea nafasi ya uspika.

Sawa tufanye basi wakati siku hiyo Dk.Ackson ambaye alikuwa bado rais Magufuli ajatengua uteuzi wake alikuwa basi alishajiudhuru wadhifa huo, Tuelezwe alijiudhuru lini?Na kama alijiudhuru Mbona taarifa ya serikali ya Jana imesema rais Magufuli ametengua uteuzi wa Dk.Ackson?Kitendo cha rais Kusema ametengua inamaana Dk.Ackson hakuwa amejihudhuru.

Maana aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Fredrick Werema alipo andika barua ya kujihudhuru ,Rais Jakaya Kikwete alitoa taarifa ya Kusema amekubali ombi la Jaji Werema la kujihudhuru wadhifa huo.

inamruhusu Mwanachama ambaye amechukua fomu ya Uspika Novemba 11 Mwaka huu, Kugombea 
Hivi kwa watu tunaofikiri sawa sawa Dk.Ackson kwa kitendo Chake hicho kilichonyesha wazi Kuwa hakuwa amedhamiria Kugombea nafasi ya Uspika bali aligombea kwa ajenda mahususi ambayo amefanikiwa na anajiona ni Shujaa ila atambue Mashujaa wote wakishakufa vitani na anaamua Kugombea unaibu Spika.

Hivi hata CCM Mbona hamkomi na kujifunza?uchaguzi Mkuu uliomalizika Jasho limewatoka kwasababu baadhi ya wananchi waliichukia CCM kutokana na mambo kama haya haya ya kisanii Sani na Ujinga Ujinga .

Hivi huko CCM kote Hakuna watu wa Kugombea unaibu Spika, au kupitisha Majina matatu wagombea Uspika ambao angalau hawaandamwi na tuhuma mpya kama Dk.Ackson hadi mng'ang'ane na Dk.Ackson kama gundi?

Nafahamu Dola la CCM likiamua Dk.Ackson awe Naibu Spika wa Bunge kwa Vyovyote vile Atakuwa .

Itakumbukwa Kuwa Enzi Rais Jakaya Kikwete alipokuwa rais alikuwa akifanya kila jitihada za kumbeba kwa mbeleko Zakhia Meghji lakini umma ulipaza sauti kila alipokuwa ataka kufanya jaribio la Kumrudisha Kwenye uwaziri umma ulipaza sauti Kuwa awamtaki na hatimaye mwisho wa siku aliishia Kumteua Kwenye vyeo Vya CCM.

Pia Enzi za Kikwete tulishuhudia aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini ,Eliachim Maswi,David Jairo na Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo kwa Nyakati tofauti waliandamwa na tuhuma za Escrow na Jairo akituhumiwa kuhonga wabunge na kelele zilivyo zaidi Katibu Mkuu Kiongozi alisimamisha Kazi Jairo,Maswi ili kupisha uchunguzi na Muhongo alijiudhuru kupisha uchunguzi.

Katibu Kiongozi aliunda Kamati yake kuchunguza tuhuma hizo kwa watumishi hao wa umma na uchunguzi ulipokamilika ulitoa ripoti ambayo ilionyesha watendaji wote Hao hawana hatia na Maswi akarejeshwa Kazi na amateuliwa Kuwa Katibu Tawala Mkoa wa Manyara, Muhongo amegombea Ubunge ameshinda. 

Novemba 14 Mwaka huu ndiyo  nilianza  kumjadili kupitia makala yangu iliyokuwa na kichwa cha ( DK.TULIA ACKSON HUFAI KUENDELEA KUWA NAIBU MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI).

Kwasababu  yeye ni mwanasheria kutuhumiwa kujiingiza Kwenye siasa wakati ni mtumishi wa umma CCM na serikali yake hata kama itaziba Pamba masikioni Kuwa tutakuwa Naibu Spika ambaye kwanza baadhi ya wabunge watakuwa hawamuheshimu kwasababu Tayari alipokuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa serikali alivunja Sheria za utumishi wa umma hivyo sidhani kama Atakuwa akiwataka wabunge wakorofi watii Sheria na Kanuni za Bunge watamtii ipasavyo zaidi zaidi ataambulia kurushiwa vijembe tena a jiandae na Hilo.

Ifike mahali tukubaliane Hilo ni doa analo Mgombea Naibu Spika wa CCM Dk.Ackson na litasumbua yeye binafsi , Bunge,CCM ,rais Magufuli ,sasa na  mbele  ya safari. 

Dk.Ackson nataka utambue hata Kipindi kile Anne Makinda naye alikuwa na kundi la watu wazito nyuma walimsaidia Akawa  Spika kwa kigezo eti ni zamu ya wanawake lakini Leo hii lile kundi la watu lilokuwa likimuunga mkono Makinda limempa Kisogo  na yeye kwa kuwa ni mtu mzima na mwanasiasa Mkongwe alisoma   alama za Nyakati Akaamua mapema kabisa ili kulinda heshima akatangaza  kung'atuka siasa.

Sasa na wewe ambaye Katika vita hii ya Uspika ya Mwaka 2015 umeonekana  Mwamba sana kwasababu una genge la watu lina kuunga mkono na ndiyo maana unatamba utakavyo unaharibu huku unateuliwa huku ,unaachia nafasi ya uspika dakika za mwisho unaenda kugombea nafasi ya unaibu ni haki yako ila nakuomba utambue jambo moja hao wanaokuwezesha uwe na nguvu hizo hipo siku watakuachia udondoke mwenyewe na hawatakuokota. 

Usione ufahari leo hii kupata hivyo vyeo vya chapchap .Kuwa makini na watu hao sana na ujiulize ni kwanini wakupe Nguvu wewe ghafla ghafla katika CCM,serikali ilihali wewe ni kijana mdogo mdogo na Si mtu mwingine? Bahati nzuri wanasiasa Wengi siyo watu wakuaminika sana. 

Sina chuki na Dk.Ackson ,nampenda, ana elimu nzuri,na siwezi kusema leo hii hafai kuwa Naibu Spika wakati bado hajashika wadhifa ila shida yangu ni moja tu ni hilo doa la kujihusisha kwenye siasa akiwa ni mtendaji wa umma litakutafuna.Minamtakia mafanikio katika kinyang'anyiro hicho ,Mungu amsaidie .Dk.Ackson akikisha ukipata nafasi hiyo unafanyakazi Kazi vizuri ili watu wanadhani huwezi wakose la Kusema.Naomba kutoa hoja.
RAIS MAGUFULI UMEINGIA CHAKA
Na Happiness Katabazi

IBARA ya 72 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 inasema ;
"Iwapo mtu yeyote mwenye madaraka katika utumishi wa Serikali, madaraka ya aina iliyotajwa katika ibara ya 67(2)(g) ataamua:-
(a) kuwa mgombea uchaguzi wa Rais au wa nafasi nyingine yoyote chini ya Katiba hii;
(b) kugombea uongozi wa ngazi yoyote katika chama cha siasa kinyume na masharti ya ajira,
mtu huyo atahesabiwa kuwa utumishi wake umekoma tangu tarehe yake ya kuwa mgombea uchaguzi au ya kugombea uongozi katika chama cha siasa.".

Ibara ya 67(2)(g) ya Katiba ya nchi inasema ; "  ikiwa mtu huyo ameshika madaraka ya afisa mwandamizi katika utumishi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano, isipokuwa madaraka ambayo Rais aweza au anatakiwa kukabidhi kwa Mbunge kwa mujibu wa Katiba hii au sheria iliyotungwa na Bunge;

 Kanuni ya  Utumishi wa Umma ( Gorvement Standing Order ya mwaka 2009    ya 20(2) (e)  inakataza Wakili wa Serikali asijihusishe na siasa.

Nimelazimika kuanza na nukuu za Ibara hizo za Katiba na Kanuni hiyo ya Utumishi wa umma kwasababu makala yangu Leo itamjadili hasa masuala Kadhaa ikiwemo taarifa ya Msemaji wa serikali Assah Mwambene ambaye alisema   Rais John Magufuli ametengua uteuzi wa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dk.Tulia Ackson  na Katibu wa Bunge Jana hiyo hiyo akasema amepokea uteuzi wa rais Magufuli Kuwa amemteua Dk.Ackson Kuwa Mbunge .

Sasa taarifa ya Msemaji wa serikali Mwambene Jana inasema Rais Magufuli ametengua uteuzi wa Naibu Mwanasheria Mkuu wa serikali Dk.Ackson  wakati Ibara ya 72  ya Katiba ya nchi inasema ; Iwapo mtu yeyote mwenye madaraka katika utumishi wa Serikali, madaraka ya aina iliyotajwa katika ibara ya 67(2)(g) ataamua:-

Ibara ya 72(b) kugombea uongozi wa ngazi yoyote katika chama cha siasa kinyume na masharti ya ajira, mtu huyo atahesabiwa kuwa utumishi wake umekoma tangu tarehe yake ya kuwa mgombea uchaguzi au ya kugombea uongozi katika chama cha siasa.".

Kwa maana hiyo utumishi wa umma wa Dk.Ackson ulikoma   Novemba 11 Mwaka huu alipoenda kuchukua fomu ya Kugombea Uspika.

Hivyo basi Rais Magufuli kwa mujibu wa Ibara ya Ibara 72(b) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Mwaka 1977 ,hajatengua uteuzi huo ,kwasababu Ibara hiyo inasema wazi kabisa mtumishi wa umma mwenye aina ya Cheo kilichotajwa  Katika Ibara ya 67(2)(g) ya Katiba ya nchi akigombea Uongozi wa ngazi yoyote Katika Chama cha siasa kinyume na Masharti ya ajira kama alivyofanyiwa Dk.Ackson ,mtu Huyo atahesabiwa  Kuwa utumishi wake umekoma tangu tarehe yake ya Kuwa mgombea uchaguzi au ya Kugombea Uongozi Katika Chama cha siasa.

 Kwa  mujibu wa Kanuni ya 20(2)(e) ya Utumishi wa Umma Dk.Ackson alikuwa na cheo cha Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali  ulikoma siku alipoenda kuchukua fomu ya kugombea uspika Novemba 11 mwaka huu na Novemba 14 mwaka huu, Kamati Kuu ya chama chake CCM kilipoteua jina lake, Job Ndugai na Dk.Mwinyi kugombea uspika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo hata hiyo jana Dk.Mwinyi,Dk.Ackson  walitangaza kujitoa na kumuacha Ndugai peke yake kama mgombea spika kupitia CCM.

Hivyo, basi kitendo cha Rais Magufuli  kumteua Dk.Ackson  kuwa mbunge wa kuteuliwa na kutuambia kwamba ametengua uteuezi wake kama Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali  si sahihi kwa sababu kwa mujibu wa sheria nilizo zinukuu hapo juu alishasita kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Kabla ya Jana rais kutengua uteuzi wake.

Alichokifanya Rais Magufuli   ni kuthibitisha tu labda kuwa Dk. Ackson  hafai  kuendelea kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali  hivyo hata kumteua kuwa mbunge si jambo sahihi sana hasa katika ulimwengu huu wa demokrasia ya vyama vingi licha Rais anayo mamlaka ya Kumteua kuwa miongoni mwa wabunge 10 wanaoteuliwa na rais kama ilivyoanishwa Katika Ibara ya 66(1)(e) ya Katiba ya Nchi.

Itakumbukwa Kuwa Novemba 15 Mwaka huu, baada ya Kamati Kuu ya CCM kuteua majina matatu ya makada wake Kuwa miongoni mwa wagombea wa uspika ambapo Majina hayo yalipaswa yapelekwe Jana Katika Kikao cha wabunge wa CCM ili jana hiyo hiyo  lipatikane  jina Moja tu la mgombea wa CCM ambalo litaenda kushindana na wagombea Uspika wa vyama Vya upinzani.

Sasa cha kushangaza Jana asubuhi ilitolewa taarifa ya kwa umma Kuwa Rais ametengua uteuzi wa Dk.Ackson na wakati huo huo Katibu wa Bunge Dk.Thomas Kashilila akatangazia umma kuwa amepokea taarifa za uteuzi kuwa Rais Magufuli amemteua Dk.Ackson Kuwa Mbunge wa kuteuliwa .

Na saa  Chache baadae Jana hiyo hiyo Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye alizungumza na waandishi wa Habari Kuwa aliyekuwa mgombea Uspika Dk.Ackson na Dk.Mwinyi wamejitoa Katika kinyang'anyiro hicho cha uspika hivyo wameacha Ndugai Kuwa mgombea pekee ambaye amepita bila kupingwa na saa Chache baadaye Jana hiyo eti Dk.Ackson ameenda kuchukua fomu za Kugombea nafasi ya unaibu Spika kupitia CCM.Mmhhhh.

Watu tunaofikiri sawa sawa tumeona matukio hayo manne yaliyotokea ndani ya saa zisizo zaidi nane kwa siku Moja tu yaani Jana yanayomhusisha Dk.Nackson ya rais kutengua uteuzi wake, rais Kumteua Ubunge, yeye Dk.Nackson Kujitoa dakika za mwisho Katika kinyang'anyiro Uspika na Dk.Ackson kwenda kuchukua fomu ya Naibu Spika ,siyo ya kawaida na ya nachezwa na watu wazito hasa ambayo mwisho wa siku yameanza kumchafulia sifa Magufuli ambaye Mara zote Katika kampeni zake alikuwa alidai atalinda Sheria za nchi .

Hivi kwanini Magufuli umeamua kujiingiza Katika mtego huu mchafu  mapema kiasi hiki? Rais Magufuli sikufichi  umeanza kujitia madoa na baadhi ya watu Taratibu Tumeanza kukutilia Shaka ?

Huyu Dk.Ackson  kavunja wazi wazi Sheria hiyo ya Utumishi wa umma lakini wewe Rais Magufuli ambaye  wakati ulipolishwa kiapo na Jaji Mkuu, Othman Chande ,Novemba 5 Mwaka huu pale Uwanja wa Taifa uliapa Kuwa utailinda na kuifadhi Katiba , sasa huku Kumteua Dk.Ackson  ambaye amevunja Sheria ya utumishi wa umma wazi wazi na kuiletea sifa mbaya ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kujiingiza Katika siasa wakati akijua hatakiwi kuvunja Sheria.

Najua kuna watu hamtaelewa kwa nini nasema Dk.Ackson amekiuka sheria kugombea uspika wakati yeye ni mwanasheria wa serikali katika cheo cha Naibu mwanasheria Mkuu. 

Ni hivi, makatazo ya kisheria juu ya watumishi wa umma kujihusisha na siasa yamegawanyika katika sehemu mbili, ambayo yanafanya watumishi wa umma wagawanyike katika makundi mawili.

 Kundi la kwanza la watumishi wa umma kwa mujibu wa kanuni ya 20 ya kanuni za utumishi wa umma, hawa ni marufuku kabisa kujihusisha na siasa. Kwa maana nyingine hata kama walipoteuliwa walikuwa wanachama wa vyama vya siasa, mara baada ya uteuzi wanapaswa kurudisha kadi zao au kusitisha uanachama wao. Katika kundi hili wapo askari wapo majaj, mahakimu, wanasheria wa serikali, watumishi ofisi ya msajili wa vyama vya siasa na tume ya uchaguzi.

Kundi la pili, ni watumishi wa kawaida ambao sio askari wala hao niliowataja hapo juu.

 Hawa wanaruhusiwa kujihusisha katika mambo ya siasa, yaani kuwa wanachama na kushiriki shughuli zote za kisiasa isipokuwa tu, hawaruhusiwi kugombea uongozi kwenye vyama vyao vya siasa, nahata pale watakapogombea kwenye nafasi za kisiasa utumishi wao unakoma baada ya kuteuliwa na tume ya uchaguzi au kuteuliwa na rais kuwa wabunge. Dk.Ackson hayupo kwenye kundi hili. Yeye yupo kwenye kundi la kwanza. 

Alichofanya Dk.Ackson ni sawa na leo hii ajitokeze jaji wa Mahakama Kuu akiwa jaji hivyo hivyo aende kuchukua fomu ya kugombea uspika kwa tiketi ya CHADEMA au CCM kisha apitishwe kabisa na chama chake. 

Baada ya hapo Rais ndio aseme nimefuta uteuzi wa mamlaka yako kama jaji, ila nakuteua kuwa mbunge, kwa mujibu wa katiba. Hii si sahihi hata kidogo.

 Je hivi ndiyo rais Magufuli anatuonyesha jinsi anavyotekeleza matakwa ya  kiapo  cha kulinda   Sheria za nchi alizoapa kuzilinda kwa  kumtunuku fasta fasta Ubunge wa kuteuliwa Dk.Ackson ikiwa ni saa Chache tangu utengue uteuzi wake ambao hata hivyo pia umma haujaelezwa Sababu za rais  kutengeua  uteuzi wa Dk.Ackson ambaye aliteuliwa Kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Septemba 9 Mwaka huu na Novemba 11 akajiingiza Kwenye siasa kwenda kuchukua fomu ya kugombea uspika wakati akiwa mtumishi wa umma na Hukutangaza kujihudhuru?

Hivi rais Magufuli kwanini ukuona ni busara Kuwa ulipotangaza kutengua uteuzi wake ,ungetulia watu wasahau alichokitenda basi ipite hata miaka kadhaa au miezi fulani ndiyo umpe madaraka mengine watu wasingehoji na kuanza kukutilia mashaka .

Lakini rais wetu Magufuli unafahamu kabisa bado kuna mijadala ya wananchi kuhusu kilichotendwa na Dk.Ackson za kujihusisha na siasa wakati haruhusiwi kufanya hivyo,wewe sijui huku lions hilo au sijui umeliona ila kwasababu unazozijua umeamua kupuuza ukaamua kusema eti umetengua uteuzi wake na ghafla umemteua mbunge na muda huo huo Dk.Ackson kajitoa kwenye kugombea uspika badala yake kaenda kugombea unaibu Spika.

Hivi serikali na CCM mnafikiri Watanzania wote hatuna akili hadi tushindwe hata kung'amua  usanii 'Perliament Drammer' unaoendelea hapo ambao sikufichi rais wangu Magufuli umekutia doa kabisa tena mapema.

Sawa Rais Magufuli unaweza Kusema wewe siyo Mpiga kura wa kumchagua Spika na Naibu Spika hivyo Katika hili hausiki.

Lakini Kwa mazingira ya matukio hayo manne yaliyofanyika siku Moja ya Jana yanayomhusisha Moja kwa Moja Dk.Ackson ni Ngumu sana watu kuamini Kuwa Ufahamu Sinema yote inayochezeka  na huyo Dk.Ackson ambayo wajuzi wa mambo tumeng'amua muda mrefu na ndiyo maana nakutadharisha rais Magufuli Kuwa Katika hili watu wameanza kupata Mashaka na wewe Kuwa na wewe ndiyo wale wale na CCM ni ile ile.

Tunajiuliza  ni lazima awe yeye tu? huku ameteuliwa akachukue fomu ya kugombea uspika, hapo hapo anateuliwa Kuwa Mbunge , halafu tena tunasikia amejitoa kugombea uspika 
saa chache baadaye ameenda kuchukua fomu ya kugombea unaibu spika tena ndani ya siku Moja ya Jana?

 Hivi, haiwezekani Dk.Ackson akatosha kuwa mbunge tu asubiri kwa imani aliyopewa na Rais labda atateuliwa kuwa waziri au aendelee kutumikia kama mbunge? iwaje tena kugombea unaibu spika? Hapa ndipo zinapokuja hisia za watanzania wengine kwamba huenda huyu anatumwa lakini si yeye kwa utashi wake. Na hili linaweza kumtia doa rais Magufuli.

Hivi sini rais Magufuli huyu huyu Kwenye mikutano yake ya kampeni alikuwa akisema katika serikali yake hatomvumilia mtu anayevurunda na kuvunja Sheria na kwamba hata muamishia eneo Moja au kumpeleka sehemu nyingine na wala hatosubiri   mchakoto na kwamba mtu huyo aliyovurunda mchakato huo ataukuta kwao.

Sasa Dk.Ackson ambaye alikuwa mtumishi wa Mwandamizi wa serikali yake amevunja Sheria ya utumishi kwa kujiingiza wazi wazi Kwenye siasa Mbona hatujaona akifanya alichokisema Kwenye kampeni Matokeo yake Anadai ametengua uteuzi wake na saa hiyo hiyo anamteua Kuwa Mbunge?

Mbona Rais alipoenda kutembelea Hospitali ya Muhimbili hivi Karibuni alibaini uzembe wa kutisha ikiwa ni pamoja mashine hazifanyakazi ,sasa Mbona hatukuona akimtimua Kazi Yule Mkurugenzi badala yake aliagiza Mkurugenzi Huyo aamishiwe Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ili apangiwe Kazi nyingine?

Aidha siku hiyo aliyoenda Hospitali ya Muhimbili ,taarifa ya Ikulu ilieleza pia alibaini eti Bodi ya wa kurugenzi ilikuwa imemaliza  muda wake wa kisheria Miezi miwili iliyopita na kwamba eti akatangaza kuivunja ile Bodi ya wakurugenzi ya Muhimbili.

Sasa sijui ni Mwandishi wa Habari wa Rais ndiyo aliandika taarifa hiyo kimakosa Kuwa rais ameivunja Bodi ya Muhimbili na umma ukaamini hivyo?  Ila najiuliza hivi inawezekana je rais avunje Bodi ambayo ilikuwa Tayari imeishamaliza  muda wake kisheria?

  Bodi ambayo bado haijamaliza muda wa Uhai wake kisheria ndiyo inaweza kuvunjwa . Sasa taarifa ya Ikulu Kusema rais alivunja Bodi ya Muhimbili ambayo Ikulu hiyo hiyo imesema Tayari Bodi ilikuwa imeishamaliza  muda wake minaona siyo sahihi na mnafanya Rais Magufuli aonekane ni Kituko Mbele za watu .

Dk.Ackson licha ni msomi ameandika historia hii ambayo kwa kiasi fulani siyo nzuri kwa sasa kuwa ni Mwanamke wa kwanza Tanzania kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu serikali na msomi mwenye shahada tatu za sheria ambaye ameshika wadhifa huo kwa kipindi kifupi sana ukilinganisha na watangulizi wake .

Septemba 9 Mwaka huu aliteuliwa kushika wadhifa huo na Novemba 11 mwaka huu  akiwa na wadhifa huo na huku akijua hapaswi kuwa mwanasiasa alienda kuchukua fomu za uspika hali iliyosababisha kuzuka kwa mjadala na Novemba 16  Rais katengua uteuzi wake, na yeye akajitoa kwenye kinyanganyiro cha uspika halafu saa chache baadaye akachukua fomu za kugombea nafasi ya unaibu spika.

Na kitendo cha Dk.Ackson Kujitoa Katika mbio za Spika dakika za mwisho kwa kiasi Fulani zinaweza kuhalalisha zile taarifa zisizo rasmi kuwa aliingia au kuingizwa  Kugombea Uspika kwaajili ya kuwawekea kauzibe baadhi ya wagombea ambao walikuwa na ushawishi mkubwa kwa wabunge na wananchi wengi walitamani waingizwe hata tatu bora kama wanasiasa aina ya Samuel Sitta na wengine  ambao majina Yao yalifyekwa na Kamati Kuu Katika hatua za awali na kurudisha jina la Dk.Ackson, Ndugai,Mwinyi ambapo hata hivyo dakika za Mwisho Dk.Ackson ,Mwinyi walitangaza Kujitoa.Kweli siasa siyo chafu ila wachezaji ndiyo wachafu.

Hivi kabisa Msomi mzima wa aina yake anaweza kuamua kujilipua   kwenda kuchukua fomu za Uspika na Kamati Kuu ikapitisha jina lake Kisha dakika za mwisho anajitoa licha ni Haki yake halafu saa Chache huyu huyu Ackson ambaye tunamuuita msomi anaamua kwenda kuchukua fomu ya Kugombea unaibu Uspika? Kweli?

Anapaswa aseme ni kwanini aliamua kuanza kuchukua fomu ya Uspika vikao vikampitisha na dakika za mwisho Kujitoa halafu dakika za mwisho eti anaenda kuchukua fomu ya unaibu Uspika? 

Dk.Ackson anapaswa aeleze umma ni lini alijiunga na CCM?Na Je Oktoba Mwaka huu alipokuwa akiendesha Kesi ya mita 200 Katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar Es Salaam iliyofunguliwa na Kada wa Chadema, Kibatara Tayari alikuwa ni ni Mwana CCM au alikuwa bado?

Lakini pia CCM inatakiwa ieleze umma Dk.Ackson alijiunga na CCM lini?Na Je Kanuni na Katiba ya CCM inataja sifa zipi kwa mwanachama anayeruhusiwa kugombea uspika au madaraka yoyote katika CCM awe na ni mwanachama kwa muda gani?

Je mwanachama ambaye amejiunga leo hii na CCM anaruhusiwa kuchukua fomu ya kuwania nafasi ya uongozi ndani ya CCM? Maana Dk.Nackson alichukua fomu ya Uspika Novemba 11 mwaka huu akagombea na Novemba 14 mwaka huu, Kamati Kuu ya CCM ikamteua yeye na wenzie watatu kugombea nafasi ya uspika.

Sawa tufanye basi wakati siku hiyo Dk.Ackson ambaye alikuwa bado rais Magufuli ajatengua uteuzi wake alikuwa basi alishajiudhuru wadhifa huo, Tuelezwe alijiudhuru lini?Na kama alijiudhuru Mbona taarifa ya serikali ya Jana imesema rais Magufuli ametengua uteuzi wa Dk.Ackson?Kitendo cha rais Kusema ametengua inamaana Dk.Ackson hakuwa amejihudhuru.

Maana aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Fredrick Werema alipo andika barua ya kujihudhuru ,Rais Jakaya Kikwete alitoa taarifa ya Kusema amekubali ombi la Jaji Werema la kujihudhuru wadhifa huo.

inamruhusu Mwanachama ambaye amechukua fomu ya Uspika Novemba 11 Mwaka huu, Kugombea 
Hivi kwa watu tunaofikiri sawa sawa Dk.Ackson kwa kitendo Chake hicho kilichonyesha wazi Kuwa hakuwa amedhamiria Kugombea nafasi ya Uspika bali aligombea kwa ajenda mahususi ambayo amefanikiwa na anajiona ni Shujaa ila atambue Mashujaa wote wakishakufa vitani na anaamua Kugombea unaibu Spika.

Hivi hata CCM Mbona hamkomi na kujifunza?uchaguzi Mkuu uliomalizika Jasho limewatoka kwasababu baadhi ya wananchi waliichukia CCM kutokana na mambo kama haya haya ya kisanii Sani na Ujinga Ujinga .

Hivi huko CCM kote Hakuna watu wa Kugombea unaibu Spika, au kupitisha Majina matatu wagombea Uspika ambao angalau hawaandamwi na tuhuma mpya kama Dk.Ackson hadi mng'ang'ane na Dk.Ackson kama gundi?

Nafahamu Dola la CCM likiamua Dk.Ackson awe Naibu Spika wa Bunge kwa Vyovyote vile Atakuwa .

Itakumbukwa Kuwa Enzi Rais Jakaya Kikwete alipokuwa rais alikuwa akifanya kila jitihada za kumbeba kwa mbeleko Zakhia Meghji lakini umma ulipaza sauti kila alipokuwa ataka kufanya jaribio la Kumrudisha Kwenye uwaziri umma ulipaza sauti Kuwa awamtaki na hatimaye mwisho wa siku aliishia Kumteua Kwenye vyeo Vya CCM.

Pia Enzi za Kikwete tulishuhudia aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini ,Eliachim Maswi,David Jairo na Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo kwa Nyakati tofauti waliandamwa na tuhuma za Escrow na Jairo akituhumiwa kuhonga wabunge na kelele zilivyo zaidi Katibu Mkuu Kiongozi alisimamisha Kazi Jairo,Maswi ili kupisha uchunguzi na Muhongo alijiudhuru kupisha uchunguzi.

Katibu Kiongozi aliunda Kamati yake kuchunguza tuhuma hizo kwa watumishi hao wa umma na uchunguzi ulipokamilika ulitoa ripoti ambayo ilionyesha watendaji wote Hao hawana hatia na Maswi akarejeshwa Kazi na amateuliwa Kuwa Katibu Tawala Mkoa wa Manyara, Muhongo amegombea Ubunge ameshinda. 

Novemba 14 Mwaka huu ndiyo  nilianza  kumjadili kupitia makala yangu iliyokuwa na kichwa cha ( DK.TULIA ACKSON HUFAI KUENDELEA KUWA NAIBU MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI).

Kwasababu  yeye ni mwanasheria kutuhumiwa kujiingiza Kwenye siasa wakati ni mtumishi wa umma CCM na serikali yake hata kama itaziba Pamba masikioni Kuwa tutakuwa Naibu Spika ambaye kwanza baadhi ya wabunge watakuwa hawamuheshimu kwasababu Tayari alipokuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa serikali alivunja Sheria za utumishi wa umma hivyo sidhani kama Atakuwa akiwataka wabunge wakorofi watii Sheria na Kanuni za Bunge watamtii ipasavyo zaidi zaidi ataambulia kurushiwa vijembe tena a jiandae na Hilo.

Ifike mahali tukubaliane Hilo ni doa analo Mgombea Naibu Spika wa CCM Dk.Ackson na litasumbua yeye binafsi , Bunge,CCM ,rais Magufuli ,sasa na  mbele  ya safari. 

Dk.Ackson nataka utambue hata Kipindi kile Anne Makinda naye alikuwa na kundi la watu wazito nyuma walimsaidia Akawa  Spika kwa kigezo eti ni zamu ya wanawake lakini Leo hii lile kundi la watu lilokuwa likimuunga mkono Makinda limempa Kisogo  na yeye kwa kuwa ni mtu mzima na mwanasiasa Mkongwe alisoma   alama za Nyakati Akaamua mapema kabisa ili kulinda heshima akatangaza  kung'atuka siasa.

Sasa na wewe ambaye Katika vita hii ya Uspika ya Mwaka 2015 umeonekana  Mwamba sana kwasababu una genge la watu lina kuunga mkono na ndiyo maana unatamba utakavyo unaharibu huku unateuliwa huku ,unaachia nafasi ya uspika dakika za mwisho unaenda kugombea nafasi ya unaibu ni haki yako ila nakuomba utambue jambo moja hao wanaokuwezesha uwe na nguvu hizo hipo siku watakuachia udondoke mwenyewe na hawatakuokota. 

Usione ufahari leo hii kupata hivyo vyeo vya chapchap .Kuwa makini na watu hao sana na ujiulize ni kwanini wakupe Nguvu wewe ghafla ghafla katika CCM,serikali ilihali wewe ni kijana mdogo mdogo na Si mtu mwingine? Bahati nzuri wanasiasa Wengi siyo watu wakuaminika sana. 

Sina chuki na Dk.Ackson ,nampenda, ana elimu nzuri,na siwezi kusema leo hii hafai kuwa Naibu Spika wakati bado hajashika wadhifa ila shida yangu ni moja tu ni hilo doa la kujihusisha kwenye siasa akiwa ni mtendaji wa umma litakutafuna.Minamtakia mafanikio katika kinyang'anyiro hicho ,Mungu amsaidie .Dk.Ackson akikisha ukipata nafasi hiyo unafanyakazi Kazi vizuri ili watu wanadhani huwezi wakose la Kusema.Naomba kutoa hoja.

Mungu ibariki Tanzania 
Chanzo: www.katabazihappy.blogspot.com
Facebook: Happy Katabazi
0716 774494
17/11/2015.