NIMEPONA TATIZO LA MACHO BILA KUVAA MIWANI

NIMEPONA TATIZO LA MACHO BILA KUVAA MIWANI

Na Happiness Katabazi

MEI 16 Mwaka 2017  saa tano asubuhi  nilikwenda Katika Hospitali ya Rufaa ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi ( JWTZ) Lugalo Dar es Salaam   ,kwaajili ya kuonana na Daktari wa macho ili anipatie  matibabu ya macho yangu ambayo yamenisumbua kwa Takribani Miaka  Nane  sasa maana nilishaanza kuona ukipofu unaninyemelea kabisa.

Nilipokelewa vizuri katika Hospitali hiyo na baadhi ya maofisa wa JWTZ ambao ni watumishi wa kikosi hicho cha JWTZ  ambao ni rafiki zangu kisha nikafuata taratibu zote za kumuona daktari na ilipofika saa 8:11 Alasiri  niliingia chumba cha daktari wa macho wa hospitali hiyo  ambayo mimi nilizaliwa   25/12/1979 hapo ambaye anaitwa Dk.Seth Japhet .

Dk.Seth alinipokea vizuri nanilipojitambulisha kwakwe kwa Majina yangu yote mawili ( Happiness Katabazi) alinitazama akaanza kucheka sana akaniuliza wewe ni Yule Mwandishi wa habari Happiness Katabazi usiyemuandika Katika makala Mchungaji Antony Lusekelo Kuwa ulimkuta akiwa amelewa na anafanya Fujo ?Nikavuta pumzi ,Kisha nikamjibu ndiyo Mimi.


Dk.Seth alinitaka nianze kujieleza hayo macho yangu yanatatizo gani hadi nikafika hatua ya kujileta Mwenyewe Hospitali kwaajili ya kupata matibabu.

Huku nikicheka ,nikamweleza Kuwa kwa Miaka Saba sasa Macho yangu yamekuwa yakinisumbua sana wakati ninapokuwa eneo lenye Giza na eneo ambalo halina Mwanga wa kutosha wakati wa usiku ambapo eneo Hilo Hilo lenye Giza watu wengine wanatembea na kuona vizuri ila Kwangu Mimi Inakuwa ni tatizo siyoni vizuri.

Mfano usiku unapoingia eneo ambalo lina Giza au Mwanga hafifu macho yangu hayaoni vizuri na ifikapo usiku njiani kama kuna Giza natembea kwa tabu ,Mara kwa Mara najikwaa,napiga watu vikumbo,natembea kwa kunyatanyata maana Sioni Mbali naona Giza.

Nilimweleza Dk.Seth kutokana na tatizo Hilo nilishakwenda Katika Hospitali zenye vitengo vya  macho Mara mbili   kwa Nyakati tofauti nakufanyiwa vipimo  na madaktari wote wa Wawili wa Hospitali hizo mbili tofauti ambazo (Majina yake nayaifadhi) kati ya Mwaka 2009 na 2014 waliniambia macho yangu ni mabovu sana hivyo wakanitaka ninunue miwani nivae haraka sana .

Dk.Seth akanihoji huku anacheka hiyo miwani iko wapi ?Nilimjibu miwani nilishaitupaga nalalani muda mrefu na nilimweleza kabisa  niliinunua hiyo miwani ile kwa Sh.150,000 Mwaka 2014 lakini roho yangu ilisita na kunikataza nisivae miwani.

Kweli nikaamua kabisa licha macho yalikuwa yakinitesa eneo lenye  Giza na mwanga wa hafifu nilisema kwa jina la Yesu sivai miwani na Mungu anitafutie  njia nyingine ya Kuponya hili tatizo la macho ambalo lilinifikisha Hatua ya kuonekana Mimi ni kichekesho Katika eneo la Giza hata kama ni ndani jinsi ninavyotembea kwa kunyatanyata  na kujiona siku za Kuwa kipofu zimekaribia .

Kweli Mei 16 Mwaka huu, Mungu alisikia  kilio changu na kwa uweza wake nilijikuta naenda   Hospitali ya Jeshi Lugalo na nikakutana na Dk.Seth ambaye kwanza kabisa naomba nimuombe msamaha Dk.Seth kwasababu  wakati akinipima macho alikuwa akinipima Taratibu mno na alichukua zaidi ya saa 1:30 .

Kimoyo moyo   Nikawa namlaumu Dk.Seth Kuwa mkono wake mzito, anafanya Kazi Taratibu Kwani Mimi nilikuwa nataka nikitoka hapo Hospitali niende Kazini kwangu Mikocheni Kisha jioni niende zangu GYM  nikafanye  mazoezi ya viungo kama kawaida yangu.


Baada ya kumaliza kumpatia historia ya tatizo langu la macho, alianza kunipima macho yangu Taratibu bila haraka kwakuniweka vifaa Kwenye macho huku akivibadilisha na akawa ananitaka  nisome maandishi yaliyokuwa yametundikwa mbele ukutani .Nikafanya hivyo kama alivyonielekeza.

Alipomaliza kunipima hiyo awamu ya kwanza ,Dk.Seth akaingia awamu ya pili ya upimaji wa macho yangu ambapo hiyo awamu ya pili alininyunyizia  dawa ya Matone ndani ya macho yangu na Alipomaliza akanitaka nikaa nje ya chumba anachopimia macho na nifumbe macho yangu nisifumbue hadi dakika 25 zipite ataniita tena Nirudi ndani ya hicho chumba aendelee kunifanyia vipimo Vya macho.Nilitii maelekezo yako.

Kweli Nilifanya hivyo huku nikiwa na baadhi ya Wanajeshi na manesi ambao ni marafiki zangu wakinicheka na kunitania Kuwa ndiyo Tayari nimeishakuwa kipofu. 

Baada ya dakika 25 kumalizika Mwanajeshi mmoja alinishika mkono huku nimefumba macho hadi ndani ya chumba cha Dk.Seth  nikaa Kwenye Kiti , Dk.Seth akanitaka nifumbue macho nikafumbua.

Tukaingia awamu ya Tatu ya matibabu  ambayo Dk.Seth alichukua tena vifaa akaziwekea Kwenye macho yangu na kunitaka nisome maandishi yaliyokuwa yamebandikwa ukutani ni kayasoma vizuri.  


Baada ya dakika 10 kupita Dk.Seth akaniondoa Katika hicho chumba akaniamishia Katika chumba kingine ambacho kilikuwa kimefungwa vifaa Vya kupima wagonjwa wa macho kilikuwa na Giza Kwani alikuwa amezima taa. 

Tukaingia  awamu ya nne ya Upimaji ndani ya chumba hicho ambacho alinivaisha  vifaa Vya kupimia macho Kwenye macho yangu na kusogeza zile mashine za kupimia macho karibu kabisa na macho yangu ambazo zilikuwa Mbele yangu.

Alivyomaliza awamu hiyo ya nne ya matibabu, aliwasha taa ndani ya chumba hicho kukawa na Mwanga akanitaka Nije Kwenye viti vilivyokuwa Kwenye meza ya kuzungumzia mgonjwa na Daktari anieleze alichokibaini Katika macho yangu baada ya kufanya vipimo vyote hivyo.

Dk.Seth ambaye siyo mzungumzaji sana kama Mimi Kwani wakati wote Mimi ndiyo nilikuwa natawala mjadala kwasababu napenda kudadisi vitu hivyo nilikuwa namchimba anieleze mambo mbalimbali yahusianoyo na macho bila kujua.

Nilienda kukaa nae meza Moja Katika hicho chumba ambapo Anaongea kwa Taratibu akasema amebaini macho yangu bado hayajafikia Hatua ya kutakiwa nivae miwani na uchunguzi wake wa kitabibu umebaini tatizo langu la kushindwa kuona vizuri Gizani ,usiku ni kwasababu ninakabiliwa na upungufu mkubwa VITAMIN A mwilini na kwamba upungufu huo ndiyo umenisababishia matatizo hayo.

" Happiness,naheshimu taaluma yangu ya udaktari wa macho na jinai tendea haki kweli kweli.....sitakuandikia uvae miwani kwasababu uchunguzi wa vipimo haujanionyesha Unatakiwa uvae miwani kwasasa  ,wewe una upungufu wa VITAMIN A mwilini hivyo  nakuandikia vidonge vyenye vitamin na Madini mbalimbali ukameze jumla ni vidonge 90 " alisema Dk.Seth.

Dk.Seth ambaye alichukua zaidi ya dakika tano kutafakari kunichagulia vidonge vitakavyonifaa ambayo siyo tu vina ' Vitamin A 'peke yake ,akafungua makabrasha yake akasema ameamua kunichagulia dawa hii ambayo siyo dawa ni virutubisho inaitwa  ONCE A DAY    ( Vitamins and Food Supplements ) akasema Kwenye Bima ya Afya pia ipo .

Katika mazungumzo yetu nilimweleza Mimi uwa Nina desturi ya kumeza ( Food Supplement) yaani virutubisho vyenye baadhi ya vitamin ila hivyo virutubisho havina Vitamin A. 

Akanipongeza Kwa Hilo akaniambia hiyo ya ONCE A DAY ambayo box moja lina jumla ya vidonge 30 aliyoniandikia ina mchanganyiko wa vitamin nyingi na Madini mbalimbali ambayo binadamu anatakiwa awe nayo mwilini na kwamba madini ,vitamini baadhi zikikosekana mwilini binadamu Huyo lazima atapatwa na tatizo la kiafya na ni wachache Wanaofahamu Hilo Kwani Wengi hawafahamu Umuhimu wa Food Supplement and Mineral .

Baada ya Kumaliza kuniandikia  hivyo vidonge ,akaniambia ile dawa ya macho aliyoniwekea Machoni iliyokuwa kwa mtindo wa kimiminika Katika awamu ya pili ya matibabu kwa siku nne kuanzia siku hiyo aliyoniwekea Machoni sitaweza kusoma maandishi madogo Kwenye simu,kompyuta,hata karatasi ila nitaweza kutembea  na kweli Hilo likatokea tangu   Jumanne jioni ya (16/5/2017) nilipomaliza kupata matibabu nikaenda Duka la madawa la Nakiete lililopo Mwenge Dar es Salaam, nakuchukua hizo ONCE A DAY boxi tatu.

Siku ya Ijumaa ya 19/5/2017  macho yangu yakaanza kuona Mbali Na uwezo wa kuona hata Kwenye Mwanga ukaongezeka kupita siku zile ambazo nilikuwa sijapewa Tiba hiyo na Dk.Seth wa Hospitali ya Jeshi Lugalo.

Kwa kweli nilimshukuru Mungu kwakunikutanisha na Dk. Seth  ambaye yeye alipingana na maamuzi ya madaktari wenzake wa Hospitali zingine ambao wao walivyonipima Miaka ya nyuma kwa tatizo Hilo Hilo la Mimi kushindwa kuona Gizani ambao wao walisema tatizo langu linanitaka nivae miwani uamuzi ambao hata Mimi nilipatwa Mara mbili lakini Dk.Seth akaja na uamuzi wake ambao ulisema macho yangu hayastahili kuvaliwa miwani Kwasabababu tatizo lilokuwa likinisumbua  ni upungufu wa VITAMIN A mwili hivyo akanitaka nikale  vyakula vinaongeza  Vitamin  A kwa Wingi  mwilini ,pia nianze kumeza ONCE A DAY ili nipate Vitamin A  kwa haraka na akanitaka kwa siku Moja nimeze vidonge vitatu yaani asubuhi,mchana na jioni.

Kweli nimemeza vidonge hivyo jumla 90 na tatizo Hilo limekwisha kabisa natembea kwa miguu siku hizi usiku,tena Umbali mrefu bila kupiga watu vikumbo, kuanguka,kujikwaa au kutumbukia Kwenye mashimo maana siyo Siri miguu yangu ina harama nyingi zilizotoka na na kujikwaruza usiku kwasababu ya Macho yangu yalikuwa hayana uwezo wa kuona mbalimbali Nyakati za usiku hasa sehemu yenye Mwanga Hafifu.


Baada ya kupata Tiba hiyo ya kumeza virutubisho hivyo (ONCE A DAY) ambayo imeniponya ,niliwaeleza watu wangu wa karibu Kuwa jamani Nilichojifunza kitu Kimoja Kuwa siyo kila mtu mwenye tatizo la macho anastahili kuandikiwa na Daktari avae miwani, wengine wanaupungufu wa vitamini na Madini mwilini lakini baadhi ya madaktari wasiyo na weledi au tamaa tu ya kutaka kuuza miwani wamekuwa wakiwaandikia wagonjwa wa macho wa kavae miwani wakati hawastahili kuvaa miwani wanau upungufu wa Vitamin A mwilini kama Mimi Happiness Katabazi ambaye madaktari Wawili wa Hospitali mbili tofauti walishawahi kunipima macho tena wala hawa kuchukua muda mrefu kunipima kwa umakini kama alivyonipima Dk.Seth wa Lugalo Hospital ambaye yeye alikataa kunipa miwani akasema sistahili kuvaa miwani bali anastahili kumeza vidonge Vya kuongeza Vitamin A ili viweze kujisaidia macho yangu kuona vizuri.

Mama yangu Mzazi yeye alipimwa akapewa miwani kwasababu hawezi kusoma, kuandika wala kutumia simu bila kuvaa miwani na hata akishavaa miwani ili aanze kutumia simu au kusoma magazeti,Biblia lazima hiyo Biblia ,simu ataisogeza karibu kabisa na Macho huku akiwa amekunja sura ndani ya miwani ndiyo anaweza kusoma.

Mama yangu mzazi ambaye Julai mosi mwaka huu anatimiza umri wa miaka 60 naye ametumia Box mbili za ONCE A DAY hivi sasa ameacha kabisa kuvaa miwani na Kasema havai tena Kwani lishe mbovu zina sababisha baadhi ya watu washindwe kuona halafu madaktari wanawaandikia wavae miwani na Ngozi yake imekaa vizuri tofauti na Kabla hajaanza kutumia ONCE A DAY .

Aidha kuna rafiki yangu ambaye ni Ofisa wa Polisi mstaafu naye alikuwa anavaa miwani Macho yake haya wezi  kuona Mbali licha anavaa miwani nikampa Ushuhuda wangu naye akaenda kununua ONCE A DAY  anameza na Jana usiku  nimewasiliana naye amenieleza   hivi sasa Macho yake yana anga za  sana kupita zamani  na uwezo wa kuona Mbali ,kusoma umeongezeka  ukilinganisha na siku za nyuma Kabla ya kuanza kutumia Once A  Day hadi anajishangaa.

Hadi Jana usiku niliwasiliana naye Ofisa Huyo wa Polisi mstaafu ambaye asema jana ameanza kutumia box la pili la ONCE A DAY amesema hivi sasa yupo Katika  Hatua za mwisho za kuacha kabisa kutumia miwani Kwani macho yake yanaona vizuri hivi sasa kutokana na kumeza vidonge hivyo na kwamba hivi sasa amefikia hatua ya kukaa siku hata tatu bila kuvaa miwani na anaweza kutumia simu ,kusoma maandishi ya mbali na karibu bila Shida yoyote.

Aidha kuna baadhi ya watu ambao nao wana tatizo la macho kama niliyokuwa nayo Mimi nao nimpe washauri licha wanatumia miwani wameze ONCE A DAY Kwani mama yangu Mzazi alikuwa anatumia miwani baada ya kumtaka ameze ONCE A DAY amemeza vidonge 60 ambavyo ni box mbili miwani havai tena na ngozi yake imekaa vizuri tofauti na awali.

Tujiulize ni wangapi kumbe wanatatizo la upungufu wa VItamin A mwilini ambao unasababisha macho yasione vizuri kama mimi ( Happiness) walipimwa na madaktari wakaambiwa wavae miwani wakakubali wanavaa miwani wakati ukweli ni kwamba imekuja kubainika tatizo lao la macho halikustahili kuambiwa wavae miwani?

Hivi daktari unavyompa tiba isiyo sahihi mgonjwa wako ,ufikiri kuwa unamsababishia mathara makubwa huyo mgonjwa wako Mbele ya safari?

Tujiulize mimi ( Happiness ) ningekubaliana na maagizo ya wale madaktari wawili mwaka 2009 na 2014 walionitaka nivae miwani mimi nikagoma leo macho yangu siyangekuwa yameishaaribika bure ? Siyo vizuri baadhi ya madaktari Mnachotufanyia baadhi ya wagonjwa wenu.

Wakati Leo nikitoa Ushuhuda huu kwa umma ,napenda Kusema Kuwa kwanza unapopatwa tatizo mshirikishe Mungu ili akusaidie kutatua tatizo lako kwa kutumia watu waliosahihi hapa duniani kwasababu mimi nilimshirikisha Mungu katika tatizo hilo na kweli akanitafutia mtu "Dk.Seth" akanipa matibabu sahihi ambayo yameniponya.

Aidha  nimejifunza pia ukileta ubishi katika  katika  baadhi ya mambo ,ubishi unalipa / faida  wakati mwingine kwasababu bila ya mimi kukaidi maagizo ya wale madaktari wawili waliyonipa kati ya mwaka 2009/ na 2014 walionipima na kuniambia nastahili kuvaa miwani na nikainunua lakini nikagoma kuivaa .

Je  ningekuwa nimekubalina nao ningeivaa miaka yote hiyo kumbe tatizo langu limekuja kubainika sikustahili kuvaa miwani leo hii macho yangu siyangekuwa yamearibika kabisa? Ubishi wakati mwingine unalipa .

Lakini kingine Nilichojifunza na ninachotaka Kuwaasa wagonjwa, ndugu wa wagonjwa muwapo mahospitalini   waache tabia ya kuwalazimisha madaktari wanachotoka wao na Kuwalazimisha madaktari wawatibie harakaharaka waondoke  ,hii tabia tuache Mara Moja haitasaidii zaidi ya kutuaribia Kwani Daktari naye ni binadamu anaweza akakerwa na hiyo tabia akaamua Kumpa huduma mbovu mgonjwa.

Nakemea tabia hiyo kwasababu hata Mimi siku hiyo hiyo ya 16/5/2017 nilipokuwa nikitibiwa macho hospitalini hapo, kimoyo moyo nilikuwa nakereka na Dk.Seth alivyokuwa ananipima macho Taratibu .

Bahati nzuri sikuropoka nilivumilia Kumbe ndiyo Dk.Seth alikuwa ananiponya kwa kutumia Taaluma yake. 

Hivyo Tujenge tabia ya kuwapa nafasi madaktari pindi wafanyapo Kazi zao ,tuwavumilie tusiwaingilie wala kuwaharakisha wafanyapo Kazi Yao ya kitabibu.

Kingine Nilichojifunza wakati Leo nikitoa Ushuhuda huu ni kwamba Kuwa siyo kila mtu anayesumbuliwa na ugonjwa wa macho anastahili kuandikiwa na Daktari avae miwani .Kwani Maradhi ya macho yanasababishwa na sababu mbalimbali na matibabu ya macho ni tofauti.

Natoa Rai kwa umma Kuwa makala   hii isitafsiliwe Kuwa inaamasisha  wagonjwa wa macho waliopimwa wakabainika wana matatizo ya macho Na wakatakiwa wavae miwani  na wanavaa miwani hadi sasa waache kuvaa kwasababu ya makala hii imetoa Ushuhuda wa jinsi Mimi, mama yangu Mzazi tulivyopimwa Tunaambiwa tuvae miwani Mimi nikakaidi ila mama yangu Mzazi kwa zaidi ya Miaka Kumi Ana anavaa miwani ila baada ya kutumia ONCE A DAY ameamua kuachana na miwani kwasababu anaona vizuri kuliko hata akivaa hiyo miwani .


Shukurani zangu za dhati nazipeleka Kwa Uongozi wa Kikosi cha 521 Hospitali  ya Rufaa ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi ( JWTZ) kinachoongozwa na Brigedia Jenerali Dk.Paul Masawe   ambaye kitaaluma ni daktari wa magonjwa moyo ambaye ni miongoni walioniimiza sana nianze kufanya mazoezi ya kupunguza mwili Mwaka 2011 alipokuwa na Cheo Cha kwasababu aliniona na uzito mkubwa sana ,wafanyakazi wa hospitali hiyo na Dk.Seth na Mwenyezi Mungu. 

Mungu ampe Afya na Maisha Marefu Dk.Seth Japhet wa Hospital ya Rufaa ya Jeshi Lugalo na ninaamini kupitia Mimi utawaponya Wengi zaidi.

 Niitimishe kwa Kusema nilichokigundua Kuwa Kumbe siyo kila mgonjwa anayedai anasumbuliwa na matatizo ya macho basi Daktari anaona Tiba inayomfaa nikimpatia Tiba ya kuvaa miwani tu Kumbe sasa kupitia Ushuhuda wangu huu wa makala hii mtakubaliana na Mimi Kuwa siyo wote wanaovaa miwani ya macho au waliondikiwa wavae miwani ya macho kama Tiba siyo sahihi Kwani wengine hawakustahili kuandikiwa wavae miwani Kwani tatizo Lao la macho ni la kama langu mie ( Happiness) la upungufu mkubwa wa VITAMIN A mwili ambao ulisababisha macho yangu yashindwe kuona sehemu yenye Giza na yenye Mwanga hafifu  hivyo madaktari wale wawili walipaswa wanishauri nikale vyakula vyenye Vitamin A au waniandikie nikanunue vidonge vyenye madini na vitamin nimeze ili niongeze vitamini A mwili na baadhi ya madini. Ndugu zanguni Akili Kumkichwa.

Mwandishi wa Makala hii ni ;

Ofisa Habari wa University Of Bagamoyo (UoB ) na Mwanasheria.

Chanzo: Facebook: Happy Katabazi

21/6/2017






















TANGULIA 'KIFAA' AFANDE MWAUZI




TANGULIA  'KIFAA' AFANDE MWAUZI

Na Happiness Katabazi

JANA mchana maofisa wa tatu wa ngazi ya juu Jeshi la Polisi ambao ni marafiki zangu katika mazungumzo nao ya kawaida tu walinijulisha kuwa wamefiwa na mfanyakazi mwenzao ambaye ni Kamishna Mwandamizi Msaidizi wa Jeshi la Polisi (SACP) Lutenta   Modest Mwauzi  ambaye alifariki Juni 12 Mwaka huu na akazikwa Jana Kijijini Kwao Ibwera,Bukoba Mkoani Kagera. 


Taarifa hizo zilisababisha siku nzima ya Jana nikose na nimwage Machozi kwasababu SACP- Mwauzi licha ni ' Nshomile ' mwenzangu pia aliwahi Kuwa mwalimu wangu wa kozi ya Sheria ngazi ya Cheti.

Kwa Tuliofundishwa na mwalimu wa SACP -Mwauzi ' Kifaa' enzi hizo wakifundisha pamoja na Afande Nasser Mwakambonja ambaye ni ofisi wa Juu wa Jeshi la Polisi na ni Mwanasheria Kitaaluma .

Alishawahi Kuwa Mkuu wa Kitengo cha Sheria  wa Sheria Jeshi la Polisi, mratibu wa silaha ndogondogo small arms and light weapons , 

Afande Mwakambonja na Afande Nasser Mwakambonja waliopata fursa ya kufundishwa nao somo la Criminal Law na Criminal Procedure walipata fursa Adimu ya kuwafahamu Polisi wanapokuwa wakifanyakazi zao kwasababu masomo hayo mawili Tulifundishwa na maofisa Hao wa Polisi ambazo Sheria hizo ndiyo zinaongoza makosa yote ya jinai ambayo makosa yote ya jinai yanashughulikiwa na Taasisi kama Jeshi la Polisi mfano kukamata,kuhoji na kupeleleza .Kifngu cha 10 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya Mwaka 2002 inatoa jukumu Hilo kwa Ofisa wa Polisi.

SACP- Mwauzi ' Kifaa' ,kifo Chako Mimi binafsi kimeniuzunisha sana tena Kwani Natambua mchango wako Katika elimu ya Sheria ya nchi hii , na mchango wako  Katika taifa hili.

Mwauzi ni Ofisa wa Polisi alikuwa siyo mtu wa kujikweza na hata ungekutana naye mitaani usingefikiri ni Polisi mwenye Cheo cha juu ndani Aidha alipenda utani sana.

Nitaendelea kukumbuka ule usemi wako wako iliyowahi kuniambia hivi ; " Ukiwa mwimbaji Kwaya lazima uje kutabasamu". Kila nikikumbukaga huo Msemo wako nacheka sana.

Nilizoea nikifika Ofisi za Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Dar Es Salaam,Kwenye majukumu yangu pia nilikuwa nikipita Ofisini wake kumsalimia sasa kwakuwa umefariki Duniani ndiyo sitakuona tena.Nimeumia sana.

Aidha SACP-Lutenta Mwauzi Mbaye ni Mwanasheria Kitaaluma  Utakumbukwa sana ' wagonga fegi ' wenzio.

Pole Jeshi la Polisi ,familia, ndugu Jamaa na marafiki kwa kuondokewa na Mpendwa wetu SACP - Mwauzi.

Mungu aiweke roho ya SACP-Mwauzi Mahali panapostahili.

Mwandishi wa Makala hii ni ; 
Ofisa Habari wa University of Bagamoyo(UoB)
Chanzo: Facebook: Happy Katabazi
16/6/2017

MIPANGO YENU YA UDHALIMU DHIDI YANGU NIMEIBAINI



Na Happiness Katabazi

LEO Mchana Mara ya kwanza mtu mwenye namba 0624 317172  alijitambulisha kwa jina la Justine alijitambulisha yeye ni mwanakywa ya wa Kanisa la KKKT Temeke ,wanataka kurekodi video hivyo wamepewa namba yangu ili ni wasaidie kuwaandikia Makala nikamwambia nilishaachaga Kazi Katika magazeti ila msaada nitakao mpa ni kumu unganisha na waandishi wa Habari wa Gazeti la Tanzania ,Happy Mnale akawaandikie hiyo makala Yao.

Nikamtaka anitumie ujumbe mfupi  whatsup ili nione namba yake ili nimrushie namba ya Happy Mnale na kweli Nikafanya hivyo nitamtumia .

Baada ya muda mchache mtu Huyo aliyekuwa akijifanya Mwema sana Kwangu na kunisii sana nionane naye Mimi moyo wangu ukawa inasita ,akanipigia tena simu yangu akisema Tayari wameishaonana na Happy  Mnale na amewapokea vizuri na wameishafanya mahojiano naye ya makala hivyo hiyo makala itachapishwa Katika Gazeti la Tanzania Daima la Jumapili ya wiki hii na anaishukuru  Sana kwa wema wangu.

Mtu Huyo nikiwa na Askari wa JWTZ ( namuifadhi kwa jina) nikuzungumza naye alipiga tena simu nikakatisha mazungumzo na Askari Huyo wa JWTZ ambaye nilikuwa nazungumza naye nakumpa ushauri wa kitaaluma  nisimamisha mazungumzo naye nikapokea simu ya Huyo mtu aliyedai yeye ni mwimbaji wa kwaya ya KKKT akaniuliza  mchana ule nikipo wapi nikamjibu Si desturi yangu kutaja sehemu nilipo kama msaada nimeishampa.

Saa Tisa nikiwa na mazungumzo na rafiki yangu ambaye ni mtumishi wa umma Kwenye Gari lake mtu Huyo ( Justine) alipiga simu tena Kabla ya kupokea nilimweleza Huyo dada ambaye ni rafiki yangu Kuwa huyu mtu uenda ametumwa kunidhuru na kuniteka Kwanini analazimisha kuonana na Mimi harakahara kawakati Shida yake nimeishatatulia kama makala nimeishamuunganisha na Mwandishi wa Habari Happy Mnale ,Nikajikuta Nasema YESU ni saidia nikapokea simu yake akasema anaomba aonane namimi nikamsisitiza Aiwezekani.

Saa 12 jioni ya leo roho yangu ikanituma nivunje ratiba yangu ya kwenda mazoezi (GYM) nikaenda kukaa sehemu kubadilishana mawazo nawatu namba hiyo ya ( Justine) ikanitumia ujumbe mfupi ukisema NAWEZA KUKUONA? kwakuwa sikuwa nimeikariri namba yake nimamjibu wewe nani? Hakujibu hadi hivi sasa saa nne usiku.

Saa Mbili usiku Leo nikapokea simu kutoka Mama na Mdogo wangu zikinihoji niko wapi natafutwa vibaya sana nikamatwe wamepewa na watu wameambiwa Kuwa Hao watu walienda hadi Ofisi za Tanzania Daima kuniuliza.

Haraka sana akili ikanituma nimpigie simu Mwandishi wa Habari Happy Mnale kumhoji nakumwonya asijaribu kunificha chochote aseme .

Mnale akasema nikweli Yule mtu niliyemwelekeza kwake mchana ambaye alijitambulisha ni muimba kwaya anaitaji kuandikiwa makala alifika ofisini kwake na akatoa nje ya Ofisi yake akampeleka nje ya Ofisi wa kamuuliza maswali Mnale wakishinikiza Mnale a walete ofisini Kwangu Mnale ni kweli hapajui ofisini Na nikweli Mnale hapajui ofisini Kwangu na Mnale Katika mazungumzo yangu naye alinitaadharisha misiseme hayo waliolezwa na Hao watu ambao wakijitambulisha kwakwe kama ni maofisa  wa serikali na vitambulisho wakamuonyesha ila iwe Siri baina ya Mnale na Huyo mtu ambaye kwa mujibu wa Mnale anasema walikuwa ni kundi la watu zaidi ya Watano na wakiwa na mwanamke mmoja.

Mnale najua utachukia kwa kuyaandika yote uliniambia nisiyaandike kuhusu mazungumzo yako na hao watu na mazungumzo yangu mimi na wewe nimelazimika kufanya hii kwasababu ya usalama wangu.

Nimejiuliza kama hao ni maofisa wa serikali  kweli na wananitafuta mimi na simu yangu wanayo kwanini hawajanipigia simu kunitaka niende kituo chochote cha polisi kwa mahojiano na hatua zaidi za kisheria?
 
Kama kweli mtu Huyo mwenye namba hii     0624 317172 ( Justine)        aliyejitambulisha ni mwimbaji kwaya anataka kuandikiwa makala ,kama kweli alikuwa nania njema na Mimi Kwanini aendelee kunisumbua Kwenye simu na kwanini afike Ofisi za Gazeti la Tanzania Daima hayo mahojiano ya Makala ha kuyafanya  Matokeo yake wamweleze  Mnale Kuwa Lengo Lao siyo kuandikiwa makala Lengo ni kumsaka Happiness Katabazi wa mkamate na  Mnale asitoe Siri ?

Mungu yupo na naweza na atanilinda na siku zote ananilinda na ndiyo maana mmepanga mipango yenu michafu kwa siri na dhamira yangu ilikuwa ni njema na msaada mlioutaka nikawasaidia ndiyo maana mipango yenu dharimu mliyoipanga kwa siri Mungu ameianika. 

Na kwa taarifa yenu wewe Justine ambaye namba yako hivi sasa haipatikani na genge lako Nyie siyo kwanza kunipangia mipango ya kidharimu na kunijia na mbinu za kipuuzi kama hizi lakini Mungu aliniokoa.Amini Mungu yupo na at alisambaratisha mipango yenu.

Nasiwaogopi ,Jeuri yangu ni Yesu na Mkae mkijua na Mimi siyo "Mwepesi kihivyooo"  na ndiyo maana majaribo yako yote ya kunishawishi nionane nawewe yameshindikana na ni Mungu wangu aliingilia Kati akasambaratisha mipango yenu.

Nawarahisishia Kazi kama nyie ni wanausalama kweli wa serikali jitajeni Nyie ni wanausalama toka Kituo gani  cha Polisi nitakuja Mwenyewe kuliko njia za kipuuzi mnazotumia za kujifanya Kuwa ni watu wa dini kwakuwa mmesikia Mimi nasali basi mkaamua kuiniingilia Gia hiyo.Poleni sana.

Na Nina Mashaka kama Nyie kweli ni wana Usalama kweli wa serikali ila kwa Mungu hamfichi mnafki itabainika kweli Nyie ni wanausalama toka serikalini kama mlivyomweleza Happy Mnale mkataka asinieleze Kuwa Nyie siyo wanausalama ila kwakuwa Mnale ni rafiki yangu nanimepokea Kazi hawezi nificha chochote maana tunasaidiana naye Katika Shida na raha.Mungu amfichi mnafki atawasukuma Mtaje mnachonitafutia.


Mungu ibariki Tanzania 

Mwandishi wa Makala hii ni ;
Ofisa Habari wa University of Bagamoyo(UoB) na Mwanasheria
Blogg: www.katabazihappy.blogspot.com
Chanzo: Facebook: Happy Katabazi
0716 774494
23/5/2016.