Header Ads

MNYIKA APINGA N'GUMBI KUSAMEHEWA ADA YA KESI

Na Happiness Katabazi

MBUNGE wa Jimbo la Ubungo kwa tiketi ya (CHADEMA), John Mnyika ameiomba Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, kutupilia mbali ombi la mlalamikaji katika kesi ya kupinga ubunge wake Hawa Ng’umbi(CCM) linalotaka mahakama hiyo impatie msamaha wa kutolipa Sh milioni 15 kama dhamana ya kesi aliyoifungua kwasababu hana uwezo wa kulipa kiasi hicho.


Ng’umbi katika kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 ambayo yalimtangaza Mnyika kuwa mshindi, ana mashtaki Mwanasheria Mkuu wa Serikali, John Mnyika na aliyekuwa msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo ambapo Mnyika anatetewa na wakili wa kujitegemea Edson Mbogoro.

Kwa mujibu ya Mnyika ambayo anapinga ombi hilo la mlalamikaji(Ng’umbi) la kutaka asamehe kulipa kiasi hicho ambayo yamewasilishwa Mahakama Kuu na wakili wake Mbogoro, Mnyika ametaja sababu tano za kutaka ombi hilo likataliwe kwasababu mlalamikaji huyo katika maombi yake hajataja sababu zinazoonyesha yeye hana uwezo wa kulipa kiasi hicho cha fedha.

“Tena tunaomba mahakama kuu ilitupe ombi kwasababu naamini huyu mlalamikaji kwanza ni Mkuu wa Wilaya ya Bukombe na ana vyeo vingine hivyo ana uwezo wa kiuchumi ambao unamruhusu kulipa mahakamani gharama hiyo ya fedha ….hivyo tunaiomba mahakama hii tukufu isikubali huo msamaha wake wa kukataa kulipa kiasi hicho cha fedha kwakuwa ana uwezo wa kulipa gharama hiyo”alidai Mnyika.

Kesi hiyo inakuja leo kwaajili ya kutajwa mbele ya Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam.Ng’umbi ambaye naye alikuwa ni mgombea ubunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya CCM, alifungua kesi hiyo Na.107/2010 Machi 22 mwaka huu, akitaka mahakama hiyo itengue ushindi wa Mnyika.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Aprili 5 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.