Header Ads

UAMUZI KESI YA DOWANS WANUKIA

Na Happiness Katabazi
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imesema itatoa tarehe ya kutolea uamuzi wa ama tuzo ya fidia y ash bilioni 94 ya kampuni ya Dowans isajiliwe au isisajiliwe na mahakama hiyo kwa njia ya maandishi.


Hayo yalisemwa jana na Msajili wa Wilaya ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Projestus Kahyoza wakati akiarisha kesi hiyo ambayo ilifunguliwa na wakili wa Dowans, Kennedy Fungamtama kwaajili ya kuiomba mahakama hiyo iiweze kuisajili tuzo waliyoipewa Novemba 15 mwaka jana na Mahakama ya Kimataifa na Usuluhishi wa Migogoro ya Biashara(ICC) ambapo kesi hiyo ilikuja jana kwaajili ya kutajwa na kupangiwa tarehe ya kuja kutolewa uamuzi wa mapingamizi hayo.

Kahyoza alisema kesi hiyo jana anaiarisha yeye kwasababu Jaji Emilian Mushi anayeisikiliza kesi hiyo hayupo hivyo akasema tarehe ya uamuzi pande zote katika kesi hiyo ambazo ni Dowans yenye dhidi ya Tanesco, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Kituo cha Kutetea Haki za Binadamu (LHRC) na Timoth Kahoho kwa njia ya maandishi.

Wadai ambao ni Tanesco na wenzake katika kesi hiyo nao waliwasilisha mapingamizi wakiomba mahakama hiyo isiisajili tuzo hiyo ya Dowans.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Agosti 12 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.