Header Ads

JAJI LYIMO AAGWA

Na Happiness Katabazi
JAJI Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Fakihi Jundu amesema kuwa mchango wa kitalaamu uliotolewa na Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu, Vicent Lyimo utabaki kuwa alama na kumbumbuku katika mhimili wa mahakama nchini.


Jundu aliyasema hayo jana wakati akiongoza sherehe za kitaaluma za kumuaga jaji Lyimo ambaye amestaafu kazi ya ujaji kwa mujibu wa Katiba Septemba 12 mwaka huu ambapo alisema mchango wake katika kuamua kesi mbalimbali alizoziamua na shughuli za kiutawala alizozifanya ,mhimili huo utaendelea kuziheshimu na kuzithamini.

“Jaji Lyimo leo mahakama kuu inakufanyia sherehe ya kitaaluma ya kukuaga baada ya wewe kutimiza umri wa kustaafu kwa mujibu wa Katiba ya nchini, hivyo kwaniaba ya Mahakama Kuu ya Tanzania napenda kuchukua fursa hii kukutakia afya na maisha mema wewe na familia yako katika maisha yako mapya ya kustaafu …na tunakukuakikishia kuwa yale yote mazuri uliyoyatenda katika ukiwa mtumishi wa umma tuyaenzi”alisema Jaji Kiongozi Jundu.

Kwa upande wake Jaji mstaafu Lyimo akisoma hotuba yake alianza kwakumshukuru Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Tanga, Mussa Kipenga ambapo alisema alipoteuliwa kuwa jaji alipangiwa kituo cha kazi cha Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba ambapo huko alikutana na Jaji Mussa Kipenga ambaye ndiye alikuwa Jaji Mfawidhi wa Kanda hiyo ambapo alisema ushirikiano mkubwa wa kikao na Jaji Mussa.

Jaji Lyimo alisema hadi amefikia muda wa kustaafu, ataendelea kumheshimu na kumshukuru Jaji Kipenka ambaye kwa sasa ndiye Jaji Mfawidhi Kanda ya Tanga na kuongeza kuwa utendaji kazi wake mzuri ulichangiwa kwa kiasi kikubwa na ushirikiano wa kikazi alioupata awali alipoteliwa kuwa jaji toka kwa Jaji Kipenda na familia yake.

Aidha alisema bado mhimili wa mahakama unakabiliwa na changamoto mbalimbali ambazo zinatakiwa zitatuliwe licha ya Tume ya Kurekebisha Sheria imekuwa ikifanyakazi nzuri ya kutoa misaada ya vitendea kazi, mafunzo kwa mahakama.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Alhamisi, Septemba 15 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.