SERIKALI ILIBARIKI UNUNUZI JENGO LA UBALOZI-MAHALU

Na Happiness Katabazi

ALIYEKUWA Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, kuwa serikali ilikuwa ikifahamu suala la ununuzi jengo na ndiyo ilikuwa ikimwagiza kutafuta na kununua jengo la ofisi ya Ubalozi mjini Rome nchini Italia.



Balozi Mahalu alitoa maelezo hayo jana mbele ya Hakimu Mkuu Mfawidhi wa mahakama hiyo,Elvin Mugeta wakati alipokuwa akiongozwa kutoa utetezi wake na mawakili wake Alex Mgongolwa, Mabere Marando, Beatus Malima na Cuthbert Tenga ambapo kesi hiyo ikuja jana kwaajili ya mshtakiwa huyo kuendelea kujitetea mfululizo hadi kesho.

Awali kabla ya Mahalu kuanza kutoa utetezi wake wakili mwandamizi wa serikali Ponsian Lukosi, Ben Lincoln waliambia mahakama kuwa wamepata baadhi ya nyaraka za serikali ambazo ni mawasiliano kuhusu ununuzi wa jengo hilo yaliyokuwa yakifanywa na mshtakiwa huyo kipindi kile akiwa balozi nchini Italia na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa iliyokuwa ikiongozwa na Rais Jakaya Kikwete,waziri wa Ujenzi John Magufuri na Katibu Mkuu Kiongozi na serikali kwa ujumla wake ambazo ziliombwa na Mahalu ili aweze kuzitumia kujitetea na kwamba wamepata baadhi ya nyaraka halisi na zile ambazo ni vivuli na kwamba baadhi ya nyaraka ambazo mshtakiwa huyo anazo vivuli vyake wameshindwa kuzipata.

Itakumbukwa kuwa upande wa Jamhuri katika kesi hiyo mwaka juzi, uliambia mahakama hiyo kuwa wao siyo watunzaji wa nyaraka hizo na wala hauna hizo nyaraka ambazo Mahalu alikuwa akiwaomba awapatie hali iliyosababisha Oktoba mwaka jana , mahalu kuanza kujitetea kwa kutumia nyaraka vivuli na mahakama hiyo kuzikubali nyaraka hizo vivuli hali iliyosababisha wakili Lukosi kuiomba mahakama iarishe kesi hiyo ili wawende kuzitafuta nyaraka hizo na hatimaye jana upande wa jamhuri uliweza kuja na baadhi ya nyaraka za mawasiliano kuhusu ununuzi wa jengo hilo ambazo yaliyokuwa yakifanywa na Mahalu na serikali ambazo Mahalu alikuwa akizutumia jana kutolea ushahidi wake.

Alieleza mahakama kuwa kwa Mthamini wa majengo ya serikali M.Kimweli aliandika ripoti yake ya Julai 15 mwaka 2001 kwa serikali ambapo alisema baada ya kufanya ziara yake nchini italia na kufanya tathimini ya majengo matatu, anaishauri serikali ilinunue jengo la Villa kwani jengo hilo ni nzuri na kubwa kuliko majengo mengine yaliyopendekezwa kwani ni jengo la ghorofa moja juu ambalo likinunuliwa na serikali linaweza juu yakawa makazi ya maofisa wa ubalozi na chini ikawa ofisi ya ubalozi.

“Ni kiwa balozi Italia name nilipendekeza kwa serikali tena kupitia barua yangu moja ambayo nilimuandikia Katibu Mkuu Kiongozi, waziri wa wizara ya Mambo ya nje wakati huo alikuwa Kikwete na Wizara ya ujenzi iliyokuwa ikiongozwa na John Magufuli ambapo mwenye jengo aliandika tathimini yake iliyoonyesha jengo hilo lina thamani ya bilioni 11.117,ripoti ya Kimweli ilisema linathamani ya dola za kimarekani 3,000,000.
“Na ripoti ya ubalozi wetu nchini Italia iliandika ripoti yake iliyoonyesha jengo hilo linunuliwe kwa Euro 3,098.034 na kweli serikali ikalinunua jengo hilo kwa bei iliyotajwa sisi maofisa wa ubalozi na ililipa kwa njia ya mikataba miwili”alidai Profesa Mahalu.

Alidai kuwa wakati akiwa balozi aliwahi kufanya mawasiliano ya barua na aliyekuwa waziri wa Mambo ya Nje, Rais Kikwete kuhusu suala ya mikataba miwili ya ununuzi wa jengo hilo na Rais wa wakati huo Benjamin Mkapa alilizindua jengo hilo Februali 2003.

Aidha alidai kuwa Desemba 2001 Rais Kikwete alipokwenda mjini Rome kwenye mkutano wa nchi za SADC, ubalozi wa Tanzania kwa kushirikiana na wizara ya Mambo ya Nje ya Italia, ilimfanyia mpango wa kwenda kulitembelea jumba hilo sambamba na kumkutanisha na muuzaji wa jengo hilo ambaye ni mama wa makamu ambaye walifanya nae mazungu na mtoto wa mama huo ndiyo alikuwa mkarimani kwani mama huyo alikuwa hafamu lugha ya Kiingereza hivyo huyo mtoto ndiyo akawa anatafsiri mazungumzo yaliyokuwa yakizungumzwana Kikwete kwa lugha ya Kiingereza kwenda lugha ya kiitaliano.

“Mimi,maofisa usalama na rais Kikwete tuliudhulia mazungumzo hayo na nilimsikia Kikwete akimshukuru huyo mama kwa niaba ya serikali kuwa anamshukuru kwa kuiuzia jengo zuri kama lile na Yule mama alimweleza Kikwete kuwa jengo hilo ataliuza kwa mikataba miwili kwasababu serikali yetu tena kupitia Kikwete alimuahidi huyo mama kuwa ataakisha akifika Tanzania serikali itamtumia malipo ya awali Euro milioni moja na kwamba fedha hizo atatumiwa kabla ya mwishoni mwaka 2001:

“Baada ya kushukuru Kikwete alicheka na alimweleza mama huyo kuwa anamuarika Tanzania kuja kutembelea mbuga ya Ngorongoro na hiyo ndiyo shukrani yake kwa kwa Tanzania”alidai Mahalu.

Aidha aliendelea kujitetea huku akitumia nyaraka mbalimbali ambazo ni halisi na vivuli alidai na akazisoma nyaraka hizo ambazo zilikuwa zikisomeka na kuonyesha kuwa alikuwa akifanya mawasiliano kuhusu ununuzi wa jengo hilo na serikali ilimpa Baraka zote katika kulitafuta jengo hilo, kulinunua kwa bei hiyo lakini anashangaa serikali hiyo imekuja kumfungulia kesi ya uhujumu uchumi kuhusu ununuzi wa jengo hilo.

Hakimu Mugeta aliairisha kesi hiyo hadi leo ambapo Mahalu ambaye anashtakiwa na Grace Martin katika kesi hiyo ya uhujumu uchumi anaendelea kujitetea.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumatano, Februali 29 mwaka 2012.

WASHTAKIWA KESI YA 'SAMAKI WA MAGUFULI'WATIWA HATIANI


Na Happiness Katabazi

FEBRUALI 23 mwaka huu, Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam,iliandika historia mpya ya kutoa hukumu katika kesi uvuvi haramu maarufu ‘kesi ya Samaki wa Magufuli’ katika ukanda wa bahari ya Hindi katika eneo la Tanzania kwa kutumia meli ya Tawariq 1,ambapo iliwahukumu kwenda jela jumla ya miaka 30 au kulipa faini ya jumla ya shilingi bilioni 22.


Waliotiwa hatiani ni Nahodha , Hsu Chin Tai na wakala wa meli hiyo Zhao Hanguin.Walioachiliwa huru ni ,Hsu Shang Pao, Ca’ Dong Li na Chen Rui Hai ambao walikuwa wanatetewa na mawakili wa kujitegemea Ibrahim Bendera na John Mapunduzi.

Washtakiwa hao walikuwa wakikabiliwa na jumla ya makosa matatu.Kosa la kwanza ni la kuvua samaki bila leseni kinyume na kifungu cha 18(1) cha Sheria Uvuvi katika kina kirefu cha bahari.Kosa la pili ni kuchafua bahari na kuathiri viumbe vilivyomo ndani ya bahari kinyume na kifungu cha 67 cha Sheria hiyo na kosa la tatu ni kusaidia kutendeka kwa kosa hilo hilo la kuchafua bahari.

Sambambamba na kuwapatia washtakiwa hao adhabu hiyo, pia mahakama hiyo ilikubali ombi la Wakili Mkuu wa Serikali Biswalo Mganga ambaye ndiyo aliyekuwa akiliongoza jopo la mawakili wa serikali katika kesi hiyo lilokuwa linaomba mahakama hiyo itoe amri ya serikali iitafishe meli hiyo.

Jaji Agustine Mwarija alisema nahodha na wakala amewatia hatiani katika kosa la kwanza ambalo ni la kufanya uvuvi bila leseni ambapo kila mmoja atalipa faini ya Shilingi Bilioni moja au kwenda jela miaka 20 kila mmoja:

“Katika kosa la pili nimetia hatiani mshtakiwa mmoja tu ambaye ni Nahodha wa meli ambapo atapaswa alipe faini ya Shilingi bilioni 20 au kwenda jela miaka 10, na katika kosa la tatu mahakama hii inawaachiria huru washtakiwa wote kwasababu jamhuri imeshindwa kuthibitisha kosa hilo la kusaidia kutendeka kwa kosa hilo na kwamba adhabu zote hizo zinakwenda pamoja”alisema Jaji Mwarija.

Nasema kesi hiyo ni ya kihistoria kwasababu kesi ya aina hiyo ni ya kwanza kufunguliwa katika mahakama zetu hapa nchini tangu taifa hili lipate uhuru wake mwaka 1961.

Binafsi nilikuwa ni miongoni mwa waandishi wa habari za mahakamani wachache hapa nchini ambao nimeiripoti kesi hii mfululizo tangu ilipofunguliwa kwa mara ya kwanza Machi 2009 pale Kisutu hadi juzi Jaji Mwarija wa Mahakama
Kuu alipotoa hukumu yake.

Na kupitia hukumu hiyo binafsi napenda kutoa pongezi kwa jopo la mawakili wa serikali lilokuwa likiongozwa na Biswalo Mganga kwa kuweza kuithibisha kesi na mwisho wa siku wameweza kuuthibitishia umma kuwa nayo serikali ina mawakili wanaoweza kupambana mahakamani kisheria na mwisho wa siku wakashinda.

Kwani kuna dhana ambayo imejengeka hapa chini kuwa mawakili wazuri ni wale mawakili wa kujitegemea na mawakili wa serikali kuna mawakili wasio wa kitaaluma na mwisho wa siku ndiyo maana wamekuwa wakishindwa kufurukuta katika baadhi ya kesi wanazozifungua mahakamani kwa kishindo.

“Hukumu hii imetufurahisha sisi watanzania kwani tunaamini hukumu hiyo imethibitisha kuwa Tanzania siyo shamba la bibi ambalo kila mtu anakuja anaiba samaki wetu na kuondoka …pia hukumu hii ni somo tosha kwa wale wezi wa samaki katika eneo la nchi yetu ambao wanaingia bahari kinyemela wanavua samaki wetu kwa kutumia meli za kisasa;

‘Na tunapenda kutoa pongezi kwa ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka inayoongozwa na Dk.Eliezer Feleshi kwani kupitia mawakili wake wa serikali Biswalo Mganga, Dk.Deo Nangela, Prosper Mwangamila na Hamidu Mwanga kwani imethibisha bado serikali ina mawakili wenye uweledi wa kutosha katika tasnia ya sheria.

“Pia mashahidi na wapelelezi wa kesi hiyo kwani wamechangia kuuletea upande wa jamhuri ushindi katika kesi hiyo.Pia tunampongeza Waziri wa Ujenzi John Magufuli na mawaziri wenzake wa nchi za maziwa makuuu ambao walipokutana kwenye mkutano wakaazimia kuanza mapambano ya kuwasaka wavuvi haramu na hatimaye boti ya doria ya nchi rafiki iliweza kuwakamata washtakiwa hao wakiwa kwenye meli hiyo wakivua bila leseni:

Maneno hayo yaliyokuwa yakitolewa kwa nyakati tofauti na wananchi wa kada mbalimbali nje ya Mahakama ya Kuu Kitengo cha biashara ambapo hukumu hiyo ilisomwa ,ikiwa ni muda mchache baada ya Jaji Mwarija kumaliza kutoa hukumu yake.

Kwa wale ambao tulikuwa tukiudhuria kesi hii mwanzo mwisho, tutakubaliana kimsingi kuwa kesi hii ilikuwa na mlolongo mrefu wa taratibu kwani mashahidi, mawakili,jaji ,wazee wa baraza walipokuwa wakitoa hoja zao kwa lugha ya Kiswahili ama kiingereza, washtakiwa walikuwa hawaifahamu lugha hiyo, hivyo mahakama iliingia gharama ya kuwaleta wakalimani wa lugha zaidi ya nne kwaaajili ya kutafsiri kutoka lugha ya Kiswahili kwenda katika lugha ya Kiphilipino, Kichina,Kivietena na Kiingereza.

Hali ya mlolongo mrefu wa taratibu ilisababisha baadhi ya miongoni mwa waandishi wa habari wenzangu kuacha kuudhuria kesi hiyo kwa kile walichodai kesi hiyo inawachosha na kwamba wanasubiri siku ikija kutolewa hukumu ndiyo wataiandika.

Itakumbukwa kwamba mengi yalisemwa kuhusu kesi hii wapo waliosema Magufuli alikuwa akijitafuatia umaarufu wa kisiasa kupitia ukamatwaji wa meli hiyo, na wapo waliokuwa wakisema kuwa serikali itashindwa na mwisho wa siku itajikuta ikiwalipa washtakiwa hao fidia kubwa na kwamba fedha za walipa kinatumika kuwagharamia mahabusu hao ambao awali walikuwa 36 gerezani na mshtakiwa mmoja raia wa Kenya alifariki dunia baada ya kugoma kula kwa siku kadhaa.

Maneno hayo yaliyokuwa yakizungumza kichini chini na hata baadhi ya viongozi wa kubwa serikalini kwa njia moja au nyingine yalikuwa yakiwakosesha raha hata baadhi ya mawakili wa serikali waliokuwa wakiendesha kesi hiyo ambao binafsi nilikuwa napata fursa ya kuzungumza na mawakili hao lakini walikuwa wakiniakikishia kuwa wao watajitahidi kitaaluma katika kesi hiyo.

Kupitia hukumu hii serikali na watanzania kwa ujumla inapaswa tuamke na kuunga mkono juhudi zinazofanywa na serikali na nchi marafiki za kuwasaka wahalifu ambao wanatumia meli zao kuingia kwenye bahari yetu na kutuibia samaki bila sisi kufahamu na inaelezwa uhalifu huo uwaingizia kipata kikubwa sana.

Pia imekuwa ikielezwa kuwa kuna matajiri ambao wanamiliki meli zao kazi yao kubwa ni kujua msimu huu ni msimu wa kuvua samaki, basi matajiri hao uajiri vijana na kupeleka meli hizo bahari na kisha kuvua samaki wa aina tofauti bila kibali cha nchi husika na kisha uenda kuziuza samaki hizo katika mataifa tajiri na huko ujipatia fedha nyingi.

Kwangu mimi nawaona watu wa aina hiyo ni wahalifu kama walivyowahalifu wa makosa ya kuuza dawa za kulevya, unyang’anyi wa kutumia silaha na makosa mengine makubwa tu.Kwani kupitia uhalifu huo wa kuvua samaki bila kibali cha nchi husika ni wazi wanadhurumu rasilimali za nchi husika ambazo rasilimali hizo zikitumika vizuri zinaweza kusaidia kuongeza pato la nchi husika.

Ieleweke wazi kuwa hivi sasa ukitembelea mabucha yanayouza samaki , ule uhakika wa kupata samaki aina ya Sato kwa muda wote hakuna tena kwani aina hiyo ya samaki hivi sasa imeanza kuwa bidhaa hadimu tena bila ya kuwepo kwa taarifa zinazoeleweka.

Novemba 21 mwaka 2011, washtakiwa hao walimaliza kujitetea , ikiwa siku chache baada ya mahakama hiyo kuwaona washtakiwa hao watano wanakesi ya kujibu na kuwaachilia huru washtakiwa 31 kwasababu mahakama iliona hawana kesi ya kujibu.Kesi hiyo imekuwa ikiwahusisha wakalimani wa lugha zaidi ya nne tangu ilipofunguliwa katika mahakama hiyo ya chini hadi mahakama Kuu.

Machi 2009 washtakiwa hao walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kisha kesi hiyo ikahamishiwa Mahakama Kuu mbele ya Jaji Njegafibili Mwaikugile na kisha ikaamishiwa kwa jaji Razia Sheikh ambaye aliendesha kesi hadi mapema mwaka jana alipojitoa.

Baada ya washtakiwa kumtaka ajitoe kwasababu hawana imani na yeye kwakuwa jaji huyo alitupilia mbali ombi la lilotaka washtakiwa hao wapewe dhamana ambapo jaji huyo alitupilia mbali kwa maelezo kuwa kwa mazingira ya kesi hiyo hawezi kuwapatia dhamana washtakiwa kwasababu washtakiwa hao ni raia wa kigeni na endapo atawapa dhamana wataenda kuishi wapi haki iliyosababisha wakili wa utetezi John Mapinduzi kuwalisha ombi la kumkataa jaji huyo na jaji huyo mwishowe alijitoa na akasema ameamua kujitoa siyo kwasababu ya kukataliwa na wakili Mapinduzi.

Walikuwa wakikabiliwa na makosa ya kuvua samaki bila leseni, kuharibu mazingira katika kina kirefu cha ukanda wa Bahari ya Hindi eneo la Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kusaidia kutendeka kwa kosa hilo.

Mungu ibariki Tanzania ,Mungu ibariki Afrika

0716 774494
www.katabazihappy.blogspot.com

Chanzo:Gazeti la Tanzaia Daima la Jumanne, Februali 28 mwaka 2012

WASHTAKIWA 'KESI SAMAKI MAGUFULI' JELA MIAKA 30




Na Happiness Katabazi

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, jana iliandika historia mpya kwa hatua yake ya kuwatia hatiani washtakiwa wawili wa kesi ya uvuvi haramu katika Ukanda wa Tanzania maarufu ‘Kesi ya Samaki wa Magufuli’ na kuwahukumu kwenda jela jumla ya miaka 30 au kulipa faini ya jumla ya Shilingi bilioni 22.



Sambamba na hilo mahakama hiyo imeridhia ombi Kiongozi wa jopo la mawakili wa serikali lilokuwa likiongozwa na Wakili Mkuu wa Serikali Biswalo Mganga aliyekuwa akisaidiwa na Dk.Deo Nangela ,Prosper Mwangamila na Hamidu Mwanga aliloliwasilisha chini ya kifungu cha 351 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 2002 , ambalo aliomba mahakama hiyo itoe amri ya meli hiyo kutaifishwa na serikali ya Tanzania


Washtakiwa katika kesi hiyo ambao walifika mahakamani hapo jana ni Nahodha wa meli hiyo Hsu Chin Tai na wakala wa meli hiyo Zhao Hanguin, Hsu Shang Pao, Ca’ Dong Li na Chen Rui Hai ambao wanatetewa na mawakili wa kujitegemea Ibrahim Bendera na John Mapunduzi.

Jaji Agustine Mwarija ndiye jana aliketi kwenye kiti cha enzi kuanzia saa 4:01-6:45 mchana na kuanza kuisoma hukumu hiyo ambayo ilikuwa
ikisubiriwa kwa shauku kubwa na watanzania wenyewe na mataifa mengine hususani taifa la China ambalo washtakiwa wake watano ndiyo walikuwa wakikabiliwa na kesi hiyo ambayo jana ilitolewa hukumu.

Jaji Mwarija ambaye alianza kusoma hukumu hiyo kwa mtindo wa kukumbusha mashtaka yanayowakabili wa shtakiwa hao, hoja zilizotolewa na mashahidi wa upande wa Jamhuri na mawakili wake na utetezi uliotolewa na washtakiwa wenyewe na mawakili wao ambao ni Ibrahim Bendera na John Mapinduzi na vielelezo vilivyowasilishwa mahakamani hapo na upande wa Jamhuri.

Jaji Mwarija alisema washtakiwa hao walikuwa wakikabiliwa na makosa matatu:Kosa la kwanza ni la kuvua samaki bila leseni kinyume na kifungu cha 18(1) cha Sheria Uvuvi katika kina kirefu cha bahari.Kosa la pili ni kuchafua bahari na kuathiri viumbe vilivyomo ndani ya bahari kinyume na kifungu cha 67 cha Sheria hiyo na kosa la tatu ni kusaidia kutenda kosa.

Alisema ili mashtaka hayo yathibitishwe alijuliza maswali yafuatayo , je meli hiyo ya Tawariq 1 ilikuwa na leseni ya kuvua? samaki waliokutwa kwenye meli hiyo walikuwa wamevuliwa katika ukanda huo? na washtakiwa hao walivyokamatwa walikuwa ndani ya meli hiyo ambayo inadaiwa kuvua samaki bila leseni?

Jaji Mwarija alisema kwa mujibu wa maelezo ya onyo yaliyotolewa na Hsu Chin Tai (Nahodha) na Zhao Hanguin ambaye ni wakala wa meli hiyo nahodha wa meli hiyo alikiri kuwa ni kweli meli hiyo ilikuwa ikifanya shughuli za uvuvi katika ukanda huo na kwamba ni kweli meli hiyo ilivyokamatwa Machi 8 mwaka 2009 na boti ya askari wa doria wa nchi za Tanzania,Afrika Kusini,Botswana na leseni yake ilikuwa ikimaliza muda wake Desemba mosi mwaka 2008 na kwa upande wake wakala huyo wa meli alikiri kuwa kampuni yake ndiyo iliyoshughulika meli hiyo kutoka Bandari ya Mombasa kuja Tanzania.

Alisema kwakuwa maelezo hayo ya onyo ya washtakiwa hao wawili yameonyesha washtakiwa hao wanakili kuwa meli hiyo ilifanya uvuvi katika katika eneo hilo na kwamba walikuwa wakiitumia leseni hiyo ambayo ilikuwa imeishamalizika muda wake na hivyo wakati meli inakamatwa Machi 3 mwaka 2008 leseni hiyo ilikuwa imeshakwisha muda wake na kwamba tani 296 za samaki na kilo tatu za utumbo wa samaki hao zilikamatwa ndani ya meli hiyo na samaki hao wakiwa wanavuja damu kuwa ni dhahiri washtakiwa hao walitumia meli hiyo kufanya uvuvi katika katika ukanda wa bahari wa Tanzania.

“Mahakama hii baada ya kujiuliza maswali hayo mahakama hii inasema upande wa jamhuri umeweza kuthibitisha kesi yao kwa washtakiwa hao wawili ambao ni Nahodha na wakala na imewaachiria huru washtakiwa watatu kwasababu ushahidi haujawagusa. Nahodha na wakala nimewatia hatiani katika kosa la kwanza la kufanya uvuvi bila leseni ambapo kila mmoja atalipa faini ya Shilingi Bilioni moja au kwenda jela miaka 20 kila mmoja:

“Katika kosa la pili nimetia hatiani mshtakiwa mmoja tu ambaye ni Nahodha wa meli ambapo atapaswa alipe faini ya Shilingi bilioni 20 au kwenda jela miaka 10, na katika kosa la tatu mahakama hii inawaachiria huru washtakiwa wote kwasababu jamhuri imeshindwa kuthibitisha kosa hilo la kusaidia kutendeka kwa kosa hilo na kwamba adhabu zote hizo zinakwenda pamoja”alisema Jaji Mwarija.

Baada ya kuwatia hatiani washtakiwa hao jaji huyo alitoa fursa kwa mawakili wa washatkiwa waseme lolote kabla ya hajatoa adhabu ndiyo wakili Bendera aliinuka kwenye kiti na kupinga hoja wakili Mganga iliyodai serikali imepata hasara katika kuendesha kesi hiyo kwani meli hiyo hipo na samaki walikamatwa na washtakiwa walitoa ushirikiano wa kutosha tangu walipokamatwa hadi jana walipo hukumiwa.

“Mtukufu jaji washtakiwa uliowakuta na hatia ni raia wa kigeni na wamekaa gerezani kwa takribani miaka mitatu sasa na hiyo ni adhabu tosha na siyo tu ni raia wa kigeni bali ni raia wa China ambao China ni nchi rafiki wa Tanzania na Nahodha ni mtu mzima ana miaka 63 na ana familia.

“ …na kwakuwa tayari wakili wa Mganga ameishawasilisha ombi la kutaka meli itaifishwe na kesi hii imekuwa ikiripotiwa sana na vyombo vya habari hali iliyosababisha washtakiwa wamearibika kisaikolojia na kwakuwa serikali haifanyi biashara tunaomba serikali iifanyie tathimini meli hiyo ina gharama ya kiasi gani na kisha mwenye meli aambiwe ailipe serikali gharama hiyo ili serikali isiendelee kubeba mzigo wa kuitunza meli hiyo kwani tayari vyombo vya habari vimeishaanza kuripoti kuwa meli hiyo inayoshikiliwa imeanza kuzama”alidai wakili Bendera.

Jaji Mwarija alisema kuhusu ombi la Wakili Mkuu wa Serikali Biswalo Mganga liloomba meli ya Tawariq 1 ambayo ilikuwa ni kielelezo cha kwanza, itaifishwe, mahakama hiyo imekubali ombi hilo kwa sababu kifungu cha 18(1) cha Sheria ya Uvuvi katika kina kirefu cha bahari ,kinaeleza mahakama ina mamlaka ya kutaifisha chombo kilichotumika kutendea kosa na kwamba katika kesi hiyo meli hiyo ilitumika kufanya uvuvi haramu.

“Nimeangalia mazingira ya kesi hii, meli hiyo imekuwa na maji mengi tofauti na hali hiyo imenifanya niamini meli hiyo ilikuwa ikifanya uhalifu huo katika eneo la Tanzania kwa mbinu za aina yake na meli hiyo imeonyesha ilikuwa haitambuliwi na mamlaka husika:

“….Na hili kukomesha uhalifu wa aina hii mahakama hii itatoa amri ya kuitafisha meli hiyo kuanzia sasa ili iwe fundisho kwa meli nyingine zinazokuja kufanya uhalifu katika Ukanda wa Tanzania na pia sitatoa amri yoyote kuhusu wale samaki waliokamatwa kwenye meli hiyo na kisha wakagaiwa kwenye taasisi mbalimbali za serikali na washtakiwa kama hawajalidhika wana haki ya kukata rufaa ”alisema Jaji Mwarija.

Baada ya hukumu hiyo kutolewa, wananchi mbalimbali waliofika katika Mahakama Kuu Kitengo cha Biashara wakiwemo watumishi wa Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi na mabaharia wa serikali ambapo hukumu hiyo ndipo iliposomwa ,waliipongeza ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini inayoongozwa na Dk.Eliezer Feleshi kwa ushindi huo kwani ushindi wa kesi hiyo ni wa kihistoria kwani tangu nchi hii ipate uhuru haijapata kufunguliwa kesi ya aina hiyo katika mahakama za hapa nchini na kwamba hukumu hiyo imedhiirisha kuwa Tanzania siyo shamba la bibi ambalo kila mtu anakuja kuvua samaki kiholela.

Kwa upande wake wakili wa utetezi John Mapinduzi alisema anakusudia kukata rufaa katika mahakama ya rufaa dhidi ya hukumu hiyo kwani hawajaridhishwa na hukumu hiyo.

Novemba 21 mwaka jana, washtakiwa hao walimaliza kujitetea , ikiwa siku chache baada ya mahakama hiyo kuwaona washtakiwa hao watano wanakesi ya kujibu na kuwaachilia huru washtakiwa 31 kwasababu mahakama iliona hawana kesi ya kujibu.Kesi hiyo imekuwa ikiwahusisha wakalimani wa ligha zaidi ya nne tangu ilipofunguliwa katika mahakama hiyo ya chini hadi mahakama Kuu.

Machi 2009 washtakiwa hao walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kisha kesi hiyo ikahamishiwa Mahakama Kuu wakikabiliwa na makosa ya kuvua samaki bila leseni, kuharibu mazingira katika kina kirefu cha ukanda wa Bahari ya Hindi eneo la Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kusaidia kutendeka kwa kosa hilo.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Februali 24 mwaka 2012.

WASHTAKIWA 'KESI SAMAKI WA MAGUFULI' JEL MIAKA 30

Na Happiness Katabazi

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, jana iliandika historia mpya kwa hatua yake ya kuwatia hatiani washtakiwa wawili wa kesi ya uvuvi haramu katika Ukanda wa Tanzania maarufu ‘Kesi ya Samaki wa Magufuli’ na kuwahukumu kwenda jela jumla ya miaka 30 au kulipa faini ya jumla ya Shilingi bilioni 22.


Sambamba na hilo mahakama hiyo imeridhia ombi Kiongozi wa jopo la mawakili wa serikali lilokuwa likiongozwa na Wakili Mkuu wa Serikali Biswalo Mganga aliyekuwa akisaidiwa na Dk.Deo Nangela ,Prosper Mwangamila na Hamidu Mwanga aliloliwasilisha chini ya kifungu cha 351 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 2002 , ambalo aliomba mahakama hiyo itoe amri ya meli hiyo kutaifishwa na serikali ya Tanzania


Washtakiwa katika kesi hiyo ambao walifika mahakamani hapo jana ni Nahodha wa meli hiyo Hsu Chin Tai na wakala wa meli hiyo Zhao Hanguin, Hsu Shang Pao, Ca’ Dong Li na Chen Rui Hai ambao wanatetewa na mawakili wa kujitegemea Ibrahim Bendera na John Mapunduzi.

Jaji Agustine Mwarija ndiye jana aliketi kwenye kiti cha enzi kuanzia saa 4:01-6:45 mchana na kuanza kuisoma hukumu hiyo ambayo ilikuwa
ikisubiriwa kwa shauku kubwa na watanzania wenyewe na mataifa mengine hususani taifa la China ambalo washtakiwa wake watano ndiyo walikuwa wakikabiliwa na kesi hiyo ambayo jana ilitolewa hukumu.

Jaji Mwarija ambaye alianza kusoma hukumu hiyo kwa mtindo wa kukumbusha mashtaka yanayowakabili wa shtakiwa hao, hoja zilizotolewa na mashahidi wa upande wa Jamhuri na mawakili wake na utetezi uliotolewa na washtakiwa wenyewe na mawakili wao ambao ni Ibrahim Bendera na John Mapinduzi na vielelezo vilivyowasilishwa mahakamani hapo na upande wa Jamhuri.

Jaji Mwarija alisema washtakiwa hao walikuwa wakikabiliwa na makosa matatu:Kosa la kwanza ni la kuvua samaki bila leseni kinyume na kifungu cha 18(1) cha Sheria Uvuvi katika kina kirefu cha bahari.Kosa la pili ni kuchafua bahari na kuathiri viumbe vilivyomo ndani ya bahari kinyume na kifungu cha 67 cha Sheria hiyo na kosa la tatu ni kusaidia kutenda kosa.

Alisema ili mashtaka hayo yathibitishwe alijuliza maswali yafuatayo , je meli hiyo ya Tawariq 1 ilikuwa na leseni ya kuvua? samaki waliokutwa kwenye meli hiyo walikuwa wamevuliwa katika ukanda huo? na washtakiwa hao walivyokamatwa walikuwa ndani ya meli hiyo ambayo inadaiwa kuvua samaki bila leseni?

Jaji Mwarija alisema kwa mujibu wa maelezo ya onyo yaliyotolewa na Hsu Chin Tai (Nahodha) na Zhao Hanguin ambaye ni wakala wa meli hiyo nahodha wa meli hiyo alikiri kuwa ni kweli meli hiyo ilikuwa ikifanya shughuli za uvuvi katika ukanda huo na kwamba ni kweli meli hiyo ilivyokamatwa Machi 8 mwaka 2009 na boti ya askari wa doria wa nchi za Tanzania,Afrika Kusini,Botswana na leseni yake ilikuwa ikimaliza muda wake Desemba mosi mwaka 2008 na kwa upande wake wakala huyo wa meli alikiri kuwa kampuni yake ndiyo iliyoshughulika meli hiyo kutoka Bandari ya Mombasa kuja Tanzania.

Alisema kwakuwa maelezo hayo ya onyo ya washtakiwa hao wawili yameonyesha washtakiwa hao wanakili kuwa meli hiyo ilifanya uvuvi katika katika eneo hilo na kwamba walikuwa wakiitumia leseni hiyo ambayo ilikuwa imeishamalizika muda wake na hivyo wakati meli inakamatwa Machi 3 mwaka 2008 leseni hiyo ilikuwa imeshakwisha muda wake na kwamba tani 296 za samaki na kilo tatu za utumbo wa samaki hao zilikamatwa ndani ya meli hiyo na samaki hao wakiwa wanavuja damu kuwa ni dhahiri washtakiwa hao walitumia meli hiyo kufanya uvuvi katika katika ukanda wa bahari wa Tanzania.

“Mahakama hii baada ya kujiuliza maswali hayo mahakama hii inasema upande wa jamhuri umeweza kuthibitisha kesi yao kwa washtakiwa hao wawili ambao ni Nahodha na wakala na imewaachiria huru washtakiwa watatu kwasababu ushahidi haujawagusa. Nahodha na wakala nimewatia hatiani katika kosa la kwanza la kufanya uvuvi bila leseni ambapo kila mmoja atalipa faini ya Shilingi Bilioni moja au kwenda jela miaka 20 kila mmoja:

“Katika kosa la pili nimetia hatiani mshtakiwa mmoja tu ambaye ni Nahodha wa meli ambapo atapaswa alipe faini ya Shilingi bilioni 20 au kwenda jela miaka 10, na katika kosa la tatu mahakama hii inawaachiria huru washtakiwa wote kwasababu jamhuri imeshindwa kuthibitisha kosa hilo la kusaidia kutendeka kwa kosa hilo na kwamba adhabu zote hizo zinakwenda pamoja”alisema Jaji Mwarija.

Baada ya kuwatia hatiani washtakiwa hao jaji huyo alitoa fursa kwa mawakili wa washatkiwa waseme lolote kabla ya hajatoa adhabu ndiyo wakili Bendera aliinuka kwenye kiti na kupinga hoja wakili Mganga iliyodai serikali imepata hasara katika kuendesha kesi hiyo kwani meli hiyo hipo na samaki walikamatwa na washtakiwa walitoa ushirikiano wa kutosha tangu walipokamatwa hadi jana walipo hukumiwa.

“Mtukufu jaji washtakiwa uliowakuta na hatia ni raia wa kigeni na wamekaa gerezani kwa takribani miaka mitatu sasa na hiyo ni adhabu tosha na siyo tu ni raia wa kigeni bali ni raia wa China ambao China ni nchi rafiki wa Tanzania na Nahodha ni mtu mzima ana miaka 63 na ana familia.

“ …na kwakuwa tayari wakili wa Mganga ameishawasilisha ombi la kutaka meli itaifishwe na kesi hii imekuwa ikiripotiwa sana na vyombo vya habari hali iliyosababisha washtakiwa wamearibika kisaikolojia na kwakuwa serikali haifanyi biashara tunaomba serikali iifanyie tathimini meli hiyo ina gharama ya kiasi gani na kisha mwenye meli aambiwe ailipe serikali gharama hiyo ili serikali isiendelee kubeba mzigo wa kuitunza meli hiyo kwani tayari vyombo vya habari vimeishaanza kuripoti kuwa meli hiyo inayoshikiliwa imeanza kuzama”alidai wakili Bendera.

Jaji Mwarija alisema kuhusu ombi la Wakili Mkuu wa Serikali Biswalo Mganga liloomba meli ya Tawariq 1 ambayo ilikuwa ni kielelezo cha kwanza, itaifishwe, mahakama hiyo imekubali ombi hilo kwa sababu kifungu cha 18(1) cha Sheria ya Uvuvi katika kina kirefu cha bahari ,kinaeleza mahakama ina mamlaka ya kutaifisha chombo kilichotumika kutendea kosa na kwamba katika kesi hiyo meli hiyo ilitumika kufanya uvuvi haramu.

“Nimeangalia mazingira ya kesi hii, meli hiyo imekuwa na maji mengi tofauti na hali hiyo imenifanya niamini meli hiyo ilikuwa ikifanya uhalifu huo katika eneo la Tanzania kwa mbinu za aina yake na meli hiyo imeonyesha ilikuwa haitambuliwi na mamlaka husika:

“….Na hili kukomesha uhalifu wa aina hii mahakama hii itatoa amri ya kuitafisha meli hiyo kuanzia sasa ili iwe fundisho kwa meli nyingine zinazokuja kufanya uhalifu katika Ukanda wa Tanzania na pia sitatoa amri yoyote kuhusu wale samaki waliokamatwa kwenye meli hiyo na kisha wakagaiwa kwenye taasisi mbalimbali za serikali na washtakiwa kama hawajalidhika wana haki ya kukata rufaa ”alisema Jaji Mwarija.

Baada ya hukumu hiyo kutolewa, wananchi mbalimbali waliofika katika Mahakama Kuu Kitengo cha Biashara wakiwemo watumishi wa Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi na mabaharia wa serikali ambapo hukumu hiyo ndipo iliposomwa ,waliipongeza ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini inayoongozwa na Dk.Eliezer Feleshi kwa ushindi huo kwani ushindi wa kesi hiyo ni wa kihistoria kwani tangu nchi hii ipate uhuru haijapata kufunguliwa kesi ya aina hiyo katika mahakama za hapa nchini na kwamba hukumu hiyo imedhiirisha kuwa Tanzania siyo shamba la bibi ambalo kila mtu anakuja kuvua samaki kiholela.

Kwa upande wake wakili wa utetezi John Mapinduzi alisema anakusudia kukata rufaa katika mahakama ya rufaa dhidi ya hukumu hiyo kwani hawajaridhishwa na hukumu hiyo.

Novemba 21 mwaka jana, washtakiwa hao walimaliza kujitetea , ikiwa siku chache baada ya mahakama hiyo kuwaona washtakiwa hao watano wanakesi ya kujibu na kuwaachilia huru washtakiwa 31 kwasababu mahakama iliona hawana kesi ya kujibu.Kesi hiyo imekuwa ikiwahusisha wakalimani wa ligha zaidi ya nne tangu ilipofunguliwa katika mahakama hiyo ya chini hadi mahakama Kuu.

Machi 2009 washtakiwa hao walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kisha kesi hiyo ikahamishiwa Mahakama Kuu wakikabiliwa na makosa ya kuvua samaki bila leseni, kuharibu mazingira katika kina kirefu cha ukanda wa Bahari ya Hindi eneo la Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kusaidia kutendeka kwa kosa hilo.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Februali 24 mwaka 2012.

HAWA NDIYO WALIOILETEA SERIKALI USHINDI KESI YA SAMAKI WA MAGUFULI



Kushoto ni wakili Mkuu wa Serikali Dk.Deo Nangela, Biswalo Mganga na Hamidu Mwanga ambao walikuwa wakiiwakilisha serikali katika kesi ya uvuvi haramu katika Ukanda wa Tanzania na kufanikisha serikali kushinda kesi hiyo leo.

NIKIWA NA MAWAKILI WA SERIAKALI KESI YA SAMAKI WA MAGUFULI



Happiness Katabazi nikiwa na Mawakili Wakuu wa Serikali waliokuwa wakiiwakilisha upande wa Jamhuri katika kesi uavuvi haramu kwa kutumia meli ya Tawariq 1, muda mfupi baada ya Jaji Agustine Mwarija kumaliza kutoa hukumu ya kesi hiyo kulia ni Dk.Deo Nangela,Biswalo Mganga na Hamidu Mwanga

WAKILI KIBATALA AWA MAKAMU WA RAIS TLS




Na Happiness Katabazi

WAJUMBE wa Chama cha Wanasheria cha Tanganyika(TLS) kimemchagua kwa kura nyingi wakili wa kujitegemea Peter Kibatala(33) kuwa Makamu wa Rais wa chama hicho.



Wanachama wa chama hicho walimchagua Kibatala kushika wadhifa huo hivi karibuni katika mkutano wa mwaka wa chama hicho uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa(ICC) mkoani Arusha ambapo Kibatala na wakili Mpare Mpoki ambaye alikuwa akitetea wadhifa wake wa umakamu wa rais waligombea nafasi hiyo na mwisho wa siku Kibatala aliibuka mshindi kwa kupata kura 374 na Mpoki akapata kura 295.

Sambamba na uchaguzi huo wa kiti cha umakamu wa Rais, pia ulifanyika uchaguzi wa kumchagua rais wa chama hicho ambapo aliyekuwa rais wa chama hicho ambaye alikuwa akitetea kiti chake Farancis Stolla alifanikiwa kuibuka mshindi kwa kupata kura za ndiyo 510 na kumshinda kwa mbali mpinzani wake ambaye Protase Ishengoma ambaye alipata kura 116.

Akizungumza na Tanzania Daima kuhusu ameupokeaje ushindi huo, wakili Kibatala ambaye anamtetea aliyekuwa Mgombea Ubunge Jimbo la Segerea(Chadema), Fred Mpendazoe katika kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 ya jimbo hilo ambalo yalimtangaza Dk.Makongoro Mahanga (CCM) kuwa mshindi, alisema ameupokea kwa furaha ushindi huo na anawashukuru wajumbe waliompigia kura za ndiyo kwani kushinda kwake wadhifa huo kumeandika historia mpya katika chama hicho kuwa inashikiriwa na wakili kijana na kwamba anaamini atashirikiana na safu ya uongozi wa TLS kuchapa kazi kwa maslahi ya nchi kwa kutumia msaafu wa sheria.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Alhamisi, Februali 23 mwaka 2012.

HUKUMU 'KESI YA SAMAKI WA MAGUFULI' LEO

Na Happiness Katabazi

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, leo inatarajiwa kutoa hukumu dhidi ya raia wa tano wa wa China wanaokabiliwa na kesi ya uvuvi haramu katika ukanda wa Tanzania kwa kutumia meli ya Tawariq 1 maarufu kama ‘Kesi ya Samaki wa Magufuli’.


Washtakiwa hao Hsu Chin Tai, Zhao Hanguing, Hsu Shang Pao, Ca’ Dong Li na Chen Rui Hai wanatetewa na mawakili wa kujitegemea Ibrahim Bendera na John Mapinduzi.

Hukumu hiyo inayotarajiwa kusomwa na Jaji Agustine Mwarija leo kufuatia washtakiwa hao kumaliza kujitetea Novemba 21 mwaka huu, ikiwa siku chache baada ya mahakama hiyo kuwaona washtakiwa hao watano wanakesi ya kujibu na kuwaachilia huru washtakiwa 31 kwasababu mahakama iliona hawana kesi ya kujibu.

Machi 2009 washtakiwa hao walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kisha kesi hiyo ikahamishiwa Mahakama Kuu wakikabiliwa na makosa ya kuvua samaki bila leseni, kuharibu mazingira katika kina kirefu cha ukanda wa Bahari ya Hindi eneo la Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Alhamisi, Februali 23 mwaka 2012.

KWA HILI, NAMKUMBUKA MEJA JENERALI KALEMBO




Na Happiness Katabazi

JESHI la Ulinzi katika nchi yoyote ile duniani ni chombo maarufu na muhimu sana. Hakuna njia nyingine ya kumwelezea shujaa wa nchi isipokuwa kupitia taswira ya mwanajeshi.

Na ndiyo maana Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) ni chombo cha kujivunia kwa kuwa huliletea taifa letu sifa ya ukakamavu, nidhamu na uwezo mkubwa wa ulinzi wa mipaka ya nchi.
Panapotokea maafa, mara zote tegemeo kubwa la raia ni jeshi lao la ulinzi, kwa kuwa wanajeshi wa jeshi hilo ndio wenye sifa, maarifa, mbinu na vifaa vya kuokoa. Na kwa kawaida wanajeshi ni vipenzi wakubwa wa wananchi wao.

Katika mada yangu ya leo nitajadili kuhusu hali ya uchafu na mwonekano mchafu na usiopendeza katika makazi ya wanajeshi wetu wanaoishi katika maghorofa ya JWTZ Mwenge jijini Dar es Salaam.

Kwa wale ambao tunayafahamu maghorofa hayo tangu miaka ya 1980 na wale wanaopita njia katika maeneo hayo kwasasa watakubaliana na mimi kwamba maghorofa hayo hayavutii tena mbele za macho ya watu kutokana na uchakavu, na baadhi ya wakazi wa maghorofa hayo kushindwa kuimarisha usafi ndani na nje ya inalozunguka eneo hilo.

Ningali nikiyakumbuka maghorofa hayo tangu kipindi kile cha miaka ya 1980-1990 maghorofa hayo yalikuwa yanamuonekano mzuri kwani wakazi waliokuwa wakikaa kwenye maeneo hayo walikuwa wakihakikisha wanayafanyia usafi vya kutosha sambamba na kukata majani yanayoota nje ya maghorofa hayo na kuhakikisha chemba za maji machafu hazitiririshi maji machafu ovyo.

Lakini hali ilivyo hivi sasa katika eneo hilo si ya kuridhisha kwani baadhi ya maghorofa hayo nyavu za kuzuia wadudu wasiingie ndani zimelika vibaya sana na hakuna dalili za wakazi hao kuweka nyavu nyingine.

Licha ya nyavu hizo kutokuwekwa na baadhi ya wakazi katika nyumba hizo pia, wengine wanaishi umo utakuta wamening’iniza nguo zao ndani katika madirisha hayo na mwananchi anayepita nyuma ya maghorofa hayo uziona zikiningia.Sasa sijui hizo nguo za ndani ambazo nyingine ni magagulo ndiyo mapazia?

Ukitazama baadhi ya nyumba hizo utajiuliza wameshindwa kupata fedha za kununulia mapazia ya kutundika madirishani kwani tunachokishuhudia sasa ni nguo za ndani ndio zinatawala kutundukiwa kwenye madirisha hayo.Ni aibu sana.

Ukitazama kwenye baadhi ya kuta za maghorfa hayo hivi sasa utaona kuta nyingi zimechorwachorwa na kuandika maandishi yasiyopendeza na watu wasiyojulikana hali inayosababisha kuwaona wanajeshi wanaoishi hapo wameshindwa kuwathibiti wanaofanya vitendo hivyo ambavyo navyo vinashusha heshima ya wanajeshi wetu wanaoishi humo mbele ya machoni kwa raia.

Nyasi zimejiotea kinyemela katika makazi ya eneo hilo na hatuoni dalili ya wakazi wa eneo kuzikata na kuzichoma moto.Lakini wananchi watambue wakati hali hii ikiendelea kutamalaki katika makazi hayo ya wanajeshi wetu, serikali yetu imekuwa katika vita kuutokomeza ugonjwa wa Maralia.

Ileweke wazi kuwa wananjeshi wetu wanaokaa kwenye nyumba za jeshi wanakaa bure katika nyumba hizo yaani hawalipii kodi, na katika hilo misipingani nalo.Lakini mina hoji inakuwaje serikali kwa moyo safi imewapati nyumba bure lakini nyie baadhi ya wanajeshi wetu mnaoishi humo mshindwe kuzitunza matokeo yake mnazivuja ili mwisho wa siku zisidumu kwa muda mrefu?

Hivi watangulizi wenu waliokuwa wakiishi humo wangezifuja, leo hii mngezikuta nyumba hizo bure leo hii?

Je hizo nyumba za umma mnazozifuja kwa makusudi mngekuwa mmezijenga kwa fedha zenu binafsi mngethubutu kuzifuja hivyo?Maana kuna wengine mnaishi kwenye hayo maghorofa lakini mnajenga nyumba zenu uraiaini Je ikitokea wapangaji wenu watakaokuja kupangisha nyumba zenu mkawashuhudia wanazivuja nyumba zenu mtakubalia?

Hivi mpendwaje nyie wanajeshi na askari wetu mnaishi kwenye nyumba za umma bure,halafu mnakubali nyumba hizo zifujwe na nyie wenyewe au familia zenu?

Nafahamu kuwa kuna watu wanaweza kudai kuwa ni muda mrefu sasa wizara ya Ulinzi haijatoa fedha za kukarabati maghorofa hayo, lakini mjiulize hivi siku ugonjwa mlipuko ukitokea au maralia watakaopata madhara wa kwanza si nyie wakazi wa eneo hilo?

Kwahiyo naamanisha kwamba siyo kila kitu sisi watanzania tusubiri serikali itenge fungu, mwanajeshi analipwa mshahara na malupulu kibao hivi anashindwa ni kununua pazia, kununua kopo la rangi kupaka katika nyuma anayoishi?

Mbona wengi wenu mnapata fedha za kunywea pombe katika mabwalo ya jeshi ambazo tena miongoni mwenu tunawashuhudia mkiagiza bia kwa fujo? Au mnasubiri atokee mwandishi wa habari mkorofi aiingie katika makazi hayo kinyemela apige picha inayoonyesha hali halisi halafu kisha azichukue picha hizo azisambaze kwenye mitandao ya kijamii aseme hayo ndiyo makazi ya wanajeshi wote JWTZ ndiyo muanze kuchukua hatua?

Na kustaajabisha ni hawa hawa baadhi ya wanajeshi wanaume wenye vyeo vya chini ambao wanaishi katika maghorofa na kambi nyingine za jeshi ambao wanashindwa kusimamia usafi katika makazi wanayoishi, pindi wanapofika katika vituo vyao vya kazi alfajiri wanakuwa wamevalia sare za JWTZ safi na ushiriki kufanya usafi katika vituo vyao vya kazi kama kupiga deki,kusafisha uwanja na kazi nyingine.

Na hili nalishuhudia karibu kila siku asubuhi ninavyopita pale nje ya Makao Makuu ya Jeshi la Wananchi Upanga(Ngome), Kikosi cha 521 Hospitali Kuu JWTZ na Kikosi cha 34 na vikosi vingine vya hapa jijini Dar es Salaam.

Na uchafu huu unanifanya ni mkumbuke mzee Meja Jenerali Mstaafu Said Kalembo enzi zile za miaka 1980 akiwa ofisa wa JWTZ alijiwekea utaratibu mkali wa mara moja kwa mwezi wa kukagua usafi katika makambi ya jeshi hapa jijini na ama hakika wakazi tuliokuwa tikiishi kwenye makambi hayo tuliakikisha makambi hayo yanakuwa masafi muda wote.

Kwa wale wanaomfahamu Kalembo, ni binadamu na kiongozi anayependa usafi na ndiyo maana hata alivyokuwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga, aliweza kuwanyosha wakazi wa jiji kwa kutenga siku moja ya juma ya kila mwananchi kufanya usafi na kweli alifanikiwa jiji hilo hadi anaondoka lilikuwa wakazi wa eneo hilo wataendelea kumkumbuka katika hilo.

Chini ya Uongozi wa Jenerali Davis Mwamunyange kuna hatua za maendeleo zimepigwa na ninapongeza katika hili. Ila namuomba kiongozi huyo wa JWTZ wasikubali kuwafumbia macho wanajeshi wote wanaokaa kwenye makambi ya jeshi kisha wanayafuja kwa makusudi kwa uchafu kwani ,kwani akumbuke baadhi ya makambi hayo yamejengwa kwa fedha za walipa kodi na makazi hayo yakiwa katika hali ya uchafu yatasababisha wananchi kuwadharau wanajeshi wanaishi humo.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika

0716 774494: www.katabazihappy.blogspot.com

Chanzo:Gazeti la Tanzania la Jumanne, Februali 21 mwaka 2012

DOWANS YAIBWAGA TENA TANESCO MAHAKAMANI

Na Happiness Katabazi

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imetupilia mbali ombi la Shirika la Umeme (TANESCO) lilokuwa linaomba mahakama iwaruhusu kukata rufaa katika Mahakama ya Rufaa nchini kupinga hukumu ya Mahakama Kuu iliyotolewa Septemba 28 mwaka jana,ambayo iliruhusu tuzo ya Kampuni ya Dowans iliyopewa na Mahakama ya Kimataifa ya Usuhuhishi wa migogoro ya Kibiashara(ICC) isajiliwe hapa nchini kwasababu hiyo haina mamlaka ya kuwaruhsu kwenda katika mahakama hiyo ya juu nchini.

Tuzo hiyo ya dola za Marekani milioni 65 (takriban sh bilioni 94) iliyotolewa Novemba 15, mwaka (2010); tuzo na (ICC).

Uamuzi huo ulitolewa jana na Jaji Dk.Fauz Twaibu wakati kesi hiyo ilikuja kwaajili ya kutoa uamuzi kuhusu pingamizi la awali lilowasilishwa na wakili wa mdaiwa (Dowans), Kennedy Fungamtama ambalo liliomba mahakama hiyo itupile mbali ombi la mlalamikaji lilokuwa linaomba mahakama hiyo iwapatie kibali cha cha kwenda kuikatia rufaa hukumu iliyotolewa na Jaji Emilian Mushi wa mahakama kuu, Oktoba mwaka jana.

Jaji Dk.Twaibu alisema baada kusikiliza hoja za pande zote mbili anatupilia mbali ombi hilo kwasababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kuwaruhusu kwenda kukata rufaa mahakama hiyo ya juu na kwamba Tanesco bado wana njia nyingine ya kufika mahakama ya rufaa na siyo njia hiyo waliyoitumia ya kuomba ridhaa katika mahakama kuu kukata rufaa na uamuzi huo unatokana na mazingira halisi ya kesi hiyo yalivyo.

“Kutokana na mazingira ya kesi hii na tangu ilipofunguliwa kule ICC, mkataba ulioingiwa na pande hizi mbili umenifanya nifikie uamuzi wa kulikataa ombi la Tanesco na ninaiarisha kesi hii hadi Machi 18 mwaka huu, mahakama hii siku hiyo itakuja kulisikiliza ombi la Tanesco linalotaka mahakama hiyo itoe amri ya kusitisha utekelezwaji wa hukumu ya mahakama kuu ambayo iliisajili tuzo ya Dowans”alisema Jaji Twaibu.

Oktoba mwaka jana, Tanesco waliwasilisha ombi hilo lililokataliwa jana kutaka waruhusiwe kukata rufaa katika mahakama ya rufaa na Januari mwaka huu, wakili wa Dowans ,Fungamtama aliwasilisha pingamizi hilo la awali ambalo jana lilitolewa uamuzi huo.

Kuwasilishwa kwa ombi hilo mbele ya Jaji Twaibu na Tanesco kupitia wakili wa kampuni ya uwakili ya Rex Attoney ,Hawa Sinare ,kulitokana na hukumu ilitolewa na Jaji Emilian Mushi , Septemba 28 mwaka jana alikubali ombi la Dowans la kusajili tuzo waliyopewa na ICC isajiliwe na mahakama ya Tanzania. aidha, jaji aliiamuru TANESCO kulipa gharama zote za uendeshaji wa kesi hiyo, na Dowans ianze taratibu za kukazia hukumu ya Mahakama ya ICC.

Jaji Mushi alisema baada ya kuipitia hukumu ya ICC amebaini kuwa haina makosa ya kisheria kama anavyodai mlalamikaji, na ndani ya hukumu hiyo alikuta kiambatanisho ambacho ni mkataba kati ya TANESCO na Dowans uliosainiwa Juni 23, mwaka 2006; na kufafanua kwamba pande zote mbili katika mkataba huo zilikubaliana kwamba uamuzi wa ICC ndiyo utakuwa wa mwisho, na utazibana pande zote mbili na hautaweza kukatiwa rufaa.

Jaji huyo alisema kifungu cha 14 (f) cha mkataba huo kinasomeka hivi: “The parties waive any right to challenge or contest the validity or enforceability of this arbitration agreement or any arbitration proceeding or award brought in conformity with this section.” Kwa tafsiri nyepesi, Fungamtama alisema kifungu hicho kinasema, TANESCO na Dowans katika mkataba wao walikubaliana kwa maandishi kuweka kando haki za kupinga au kuhoji mwenendo na tuzo zitakazotolewa na baraza la usuluhishi.

Jaji akasema: “Sasa kwa mujibu wa mkataba huo ni wazi kuwa TANESCO na Dowans walikubaliana kuwa endapo utatokea mgogoro baina yao utapaswa upelekwe ICC tu na ICC itakapotoa hukumu ya mgogoro baina yao, pande hizo mbili hazitakuwa na mamlaka ya kuikatia rufaa hukumu hiyo ya ICC.

Jaji alisema hoja ya TANESCO kuwa mwenendo wa hukumu ya ICC ulikuwa na mapungufu ya kisheria, haikupaswa kupelekwa mbele yake kwani Tanasco walikuwa ni wadaiwa katika kesi iliyofunguliwa ICC na walipaswa kuiwasilisha hoja hiyo ICC kabla ya mahakama hiyo ya kimataifa kutoa hukumu yake na kuikumbusha TANESCO kuwa ni yenyewe iliyoingia mkataba wa POA na Dowans ambao kwa ridhaa yao waliridhia kuwa hukumu itakayotolewa na ICC haitakatiwa rufaa.

Septemba 6 mwaka huu, Jaji Emilian Mushi alitoa uamuzi wa kuyatupilia mbali maombi ya wanaharakati waliokuwa wakiongozwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) ambao waliiomba mahakama hiyo ikatae kusajili tuzo iliyotolewa na Mahakama ya ICC kwa kampuni ya Dowans Holdings SA(Costa Rica) na Dowans Tanzania kwa sababu wanaharakati hao hawana haki wala mamlaka ya kupinga hilo.

Mahakama ya ICC ilitoa hukumu ya kesi ya Dowans dhidi ya TANESCO, Novemba 15 mwaka jana baada ya kampuni hiyo kuishinda TANESCO katika kesi yake ya kudai fidia ya kuvunjiwa mkataba iliyokuwa imefunguliwa rasmi Novemba 20 mwaka 2008 na kupewa Na. 15947/VRO ambapo Mahakama ya ICC iliitia hatiani TANESCO kwa kosa la kuvunja mkataba na Dowans na ikaiamuru iilipe fidia ya dola za Marekani milioni 65 na riba ya asilimia 7.5.

Hukumu hiyo ya ICC, muda mfupi baada ya kutolewa ilizusha malumbano makali baina ya wananchi, wanaisiasa, mawaziri na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kutoa kauli zinazopishana huku wachache wakitaka serikali iilipe Dowans na wengine wakisema kulipwa fidia kampuni hiyo ni ufisadi.

Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta, ndiye aliyekuwa akinukuliwa na vyombo vya habari kuhamasisha umma na serikali isiilipe Dowans. Kwa upande mwingine, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Fredrick Werema na Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, walitaka Dowans ilipwe, hali iliyosababisha baadhi ya wananchi kuwashambulia kwa maneno makali wale wote waliokuwa wakitaka Dowans isajiliwe kisha ilipwe tuzo yao.

Malumbano hayo nje ya mahakama yalisababisha pia Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuunda Kamati ya Wabunge kujadili hukumu hiyo na kisha wabunge watatu wa chama hicho, George Simbachawe (Kibakwe), Mbunge wa Karagwe, Gosbert Blandes, Mbunge wa Viti Maalumu, Angellah Kairuki na raia wengine wanne kufungua kesi ya Kikatiba Na. 5/2011 dhidi ya Waziri wa Nishati na Madini, Mwanasheria Mkuu wa Serikali na TANESCO ambayo imeanza kusikilizwa mbele ya jopo la majaji watatu wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Njegafibili Mwaikugile, Agustine Shangwa na Projest Rugazia.

Kwa mujibu wa hati ya madai, walalamikaji hao wanaiomba mahakama itoe amri ya kuizuia serikali isiilipe Kampuni ya Dowans na endapo malipo hayo yatafanywa kwa kampuni hiyo ni wazi wadaiwa hao ambao wanaiwakilisha serikali kwa ujumla watakuwa wamevunja ibara 26(2),27(1) na 27 (2) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 ambazo mahakama hiyo ina wajibu wa kuilinda ibara hizo zisivunjwe.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Februali 21 mwaka 2012

MAKALLA awasaidia wanake Mvomero

Na Mwandishi Wetu, Mvomero
MBUNGE wa Jimbo la Mvomero Amos Makalla amekisaidia kikundi cha akinamama mshikamano group shingi milioni moja kwa ajili ya kukuza mtaji wa shughuli za uzalishaji mali.

Msaada huo umekabidhiwa juzi kwa kiongozi wa mshikamano group Bi Mariam Mdabwa ambaye alimshukuru sana mbunge kwa utekelezaji wa ahadi yake aliyoitoa hivi karibuni baada ya kikundi kumsomea risala ya kuomba msaada huo“ndugu wana kikundi mmeona?wananchi mmeona?sh milioni moja na laki tano hizi hapa,makalla ni mkweli si mbabaishaji kama wanasiasa wengine yeye anatoa cash hatoi cheki feki”alisema bi mariam.

Kwa upande wake makalla aliwataka wanakikundi kutumia msaada huo kukuza mtaji na shughuli za uzalishaji mali“jamani hii ni mbegu ipandeni izae.

Aidha amewapongeza wanakikundi kwa kuanzisha kikundi na amewataka makundi mengine kuiga mfano wa mshikamano group na akawaakumbusha kuwa umoja ni nguvu utengeno ni udhaifu.“Ndugu zangu taasisi za fedha zinapenda kusaidia vikundi hivyo tukiungana ni rahisi taasisi hizo zinapotoa mikopo zaweza kutusaidia na sisi tulioungana”.

MWENENDO KESI YA MRAMBA TAYARI

Na Happiness Katabazi

HATIMAYE Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, umesema kuwa mwenendo wa kesi ya matumizi mabaya ya ofisi ya umma na kuisababishia serikali hasara ya sh bilioni 11.7 inayomkabili aliyekuwa waziri wa fedha Basil Mramba na wenzake, umekamilika.

Hayo yalisemwa jana na Jaji John Utamwa aliyekuwa anasaidiwa na mahakimu wakazi Saul Kinemela na Sam Rumanyika wakati kesi hiyo ilipokuja kwaajili ya kutajwa na kuangalia mwenendo wa kesi hiyo kama umekamilika.

Jaji Utamwa alisema hatimaye mwenendo wa kesi hiyo umekamilika na kwamba anatoa siku saba kwa mahakama hiyo ziwe zimeishazipatia pande mbili katika kesi hiyo mwenendo huo wa kesi ambao umechukua muda mrefu kuandaliwa.

Jaji Utamwa alisema upande wa utetezi utapaswa uwasilishe majumuisho yao ya kuwaona wanakesi ya kujibu au la Machi 27, nao upande wa jamhuri uwasilishe majumuisho yao kwa njia ua maandishi Aprili 17 na endapo upande wa utetezi unataka kuwasilisha majumuisho ya nyongeza uwasilishe Aprili 30.

Aidha alisema kesi hiyo itakuja kwaajili ya kutajwa Machi 26 na kwamba Mei 2 itakuja kwaajili ya jopo hilo kuangalia kama hizo amri za mahakama zimetekelezwa.

Januari mwaka jana upande wa Jamhuri katika kesi hiyo unawakilishwa na upande Naibu Mkuruegenzi wa Mashtaka Stanslaus Boniface na Shadrack Kimaro ulifunga ushahidi wake na hivyo kesi hiyo kwa kipindi chote hicho hadi jana kesi hiyo ilikuwa inakuja kutajwa mahakamani kwasababu mwenendo wa kesi hiyo ulikuwa bado haujakamilika kuandaliwa.

Mbali na Mramba washtakiwa wengine ni aliyekuwa waziri wa Nishati na Madini Daniel Yona na Katibu Mkuu Mstaafi wa wizara ya Fedha na Uchumi, Gray Mgonjwa ambao wanakabiliwa na makosa ya matumizi mabaya ya ofisi ya umma na kuisababishia serikali harasa ya shilingi bilioni 11.7.

Katika hatua nyingine upande wa Jamhuri katika kesi ya kukutwa na simu gerezani inayomkabili aliyekuwa Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala wa Benki Kuu, Amatus Liyumba ulishindwa kumsomea maelezo ya awali mshtakiwa huyo kwasababu wakili wa mshtakiwa huyo Majura Magafu hakuwepo mahakamani na hivyo Hakimu Mkazi Stewart Sanga akaiairisha kesi hiyo hadi Machi 15 mwaka huu.

Chanzo:Gazeti la Tanzania la Jumamosi, Februali 18 mwaka 2012

UPELELEZI KESI YA KIBANDA UMEKAMILIKA

Na Happiness Katabazi

UPANDE wa Jamhuri katika kesi ya uchochezi inayomkabili Mhariri Mtendaji na wa Gazeti la Tanzania Daima, Absalom Kibanda na mwandishi Samson Mwigamba umeiambia Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika.

Sambamba na hilo Hakimu Mkazi Waliarwande Lema anayesikiliza kesi hiyo jana saa sita mchana alilazimika kuifuta hati ya kukamatwa kwa washtakiwa hao aliyoitoa saa tatu asubuhi wakati kesi hiyo ilipokuja kutajwa baada ya mawakili wa washtakiwa ambao ni John Mhozya, Juvenalis Ngowi na Nyaronyo Kichere kwenda kumfuata hakimu huyo ambaye alikuwa nje ya chumba chake cha kuendeshea kesi kumweleza kuwa washtakiwa hao walikuwepo katika eneo la mahakama hiyo tangu saa mbili asubuhi na walikuwa wamesimama karibu na chumba kilichokuwa kikiendeshewa kesi hiyo lakini hawakusikia karani wala askari polisi akiwaita kuingia mahakamani.

Saa nne asubuhi wakili wa serikali Elizabeth Kaganda aliingia ndani ya chumba hicho cha kuendeshea kesi bila ya washtakiwa na mawakili wao kuwepo na kuieleza mahakama kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika na kwamba wanaomba wapangiwe tarehe ya kuja kuwasomea maelezo ya awali washtakiwa na pia akaiomba mahakama itoe hati ya kukamatwa kwa washtakiwa kwasababu wameshindwa kutokea mahakamani hapo wakati shauri hilo likiendelea na ombi hilo lilikubaliwa na hakimu Lema ambaye aliairisha kesi hiyo hadi Machi 7 mwaka huu, kesi hiyo itakapokuja kwaajili ya washtakiwa kusomewa maelezo ya awali.

Baada ya Hakimu huyo kuairisha kesi hiyo washtakiwa hao ambao walikuwa wamesimama kwenye kordo ambalo linatazamana na mlango wa chumba ambacho hakimu huyo alikuwa akiendeshea kesi hiyo na hakimu huyo akafunga mlango huo na kuondoka kwenda katika ofisi nyingine iliyopo ndani ya mahakama hiyo na ndipo mawakili washtakiwa wakaanza kumtafuta wakili Kaganda kumweleza hawakusikia kesi yao ikiitwa na kwamba walikuwepo katika eneo hilo la mahakama tangu saa mbili asubuhi.

Kufuatia hali hiyo gazeti ambalo lilikuwepo ndani ya eneo hilo la mahakama tangu saa mbili asubuhi na kuwashuhudia washtakiwa na mawakili wao wakiwa wamesima katika eneo la maegesho ya magari na kisha washtakiwa hao na mawakili hao wakaenda kusimama katika eneo la mapokezi la mahakama hiyo ambalo limepakana na chumba anachoendeshea kesi hakimu huyo kwa muda wote huo hadi pale walipokuja kuelezwa kuwa kesi hiyo imeishamalizika bila ya wao kuwepo mahakamani na kutokana na hali hiyo hakimu Lema ametoa hati ya kukamatwa kwa washtakiwa na kwamba Lema ameishatoka ofisini kwake.

Hali iliyosababisha mawakili washtakiwa hao kuanza kuhaha kumsaka Hakimu Lema ambaye alikuwa amekwenda kwenye ofisi nyingine iliyopo ndani ya mahakama hiyo na kufanikiwa kumpata na kumweleza kuwa wao na washtakiwa walikuwepo ndani ya viwanja vya mahakama hiyo tangu saa mbili asubuhi na kwamba hawakusikia kesi yao ikiitwa na ilipofika saa sita wakili wa serikali Kaganda aliwaita mawakili wa washtakiwa na waandishi wa habari na kuwaeleza kuwa amekubali maelezo ya mawakili washtakiwa na kwamba ile amri aliyoitoa ya kukamatwa kwa washtakiwa kwa kushindwa kutokea mahakama ameifuta.

Desemba 21 mwaka jana, washtakiwa hao walifikishwa mahakamani hapo na wakili Kaganda alidai wanakabiliwa na kosa moja la kuwashawishi askari na maofisa wa jeshi la polisi, magereza na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ) kutoendelea kuitii serikali iliyopo madarakani kwa sasa ambayo inaongozwa na Rais Jakaya Kikwete kinyume na kifungu cha 46(b),55(10(a) na 35 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Wakili Kaganda alidai Novemba 30 mwaka huu,gazeti la Tanzania Daima la siku hiyo toleo Na.2553 lilichapisha waraka uliokuwa na kichwa cha habari kisemacho “Waraka Maalum kwa Askari wote” ambao uliandikwa na mshtakiwa huyo kupitia safu yake ijulikanayo kwa jina la ‘Kalamu ya Mwigamba’.

Alidai kupitia walaka wake huo kwa makusudi na kwa nia kuvunja sheria za mamlaka ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, aliwashawishi askari na maofisa wa jeshi la polisi, Magereza na JWTZ kutoendelea kuiiti serikali iliyopo madarakani.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Alhamisi, Februali 16 mwaka 2012

JAJI AZIONYA PANDE ZINAZOPINGANA CUF

Na Happiness Katabazi

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imewashauri mawakili wa pande mbili katika kesi ya kutaka mahakama itamke kuwa uamuzi wa Baraza Kuu la Chama cha Wananchi (CUF), uliomvua uanachama Mbunge wa Jimbo la Wawi, Hamad Rashid, kuwa ni batili iliyofunguliwa na mbunge huyo na wenzake 10, waachane na tabia ya kuleta pingamizi za awali kwani zinasababisha kesi hizo na zingine kutomalizika mapema.

Jaji Augustine Shangwa alitoa onyo hilo jana wakati kesi hiyo ilipokuja kwa ajili ya kuanza kusikilizwa, lakini ikashindikana baada ya mawakili wa Hamad, Fancis Stolla na Augustine Kusalika na Job Kyelalio anayetetea Bodi ya Wadhamini CUF kuiambia mahakama kuwa wamewasilisha pingamizi za awali hivyo wanaomba kesi hiyo isianze kusikilizwa.

“Januari mwaka huu tulivyokutana hapa tulikubaliana kwamba kesi hii hadi kufikia Machi iwe imeishatolewa hukumu…leo kesi hii ilikuja kwa ajili ya kuanza kusikilizwa lakini nimeshangaa kuona nyie mawakili wa pande zote mbili eti mmeibuka na pingamizi mkitaka kesi ya msingi isianze kusikilizwa kwanza.

Hizi pingamizi zenu mlizoleta leo mna haki ya kisheria kuzileta ila ninawashauri muachane na mchezo huu wa kuleta pingamizi mara kwa mara kwani husababisha kesi kushindwa kumalizika kwa haraka na mwisho wa siku mahakama inashindwa kueleweka mbele ya jamii,” alisema Jaji Shangwa.

Hata hivyo Jaji alizitaka pande zote kumweleza pingamizi hizo ni zipi ambapo kila wakili alieleza pingamizi lake na mwishowe Jaji akautaka upande wa mlalamikaji kuleta pingamizi lake kwa njia ya maandishi Februari 20 na upande wa mdaiwa kuwasilisha majibu yake Februali 24 na kwamba kesi hiyo itakuja kwa ajili ya kutajwa Februari 28, mwaka huu.

Wakili wa mlalamikaji, Francis Stolla, alisema kuwa wanaiomba mahakama ikitupe kiapo cha mdaiwa ambacho kiliapwa na wakili wake Twaha Tasilima kwa sababu ni batili kisheria kwa kuwa muapaji alipinga madai ya Hamad kuwa amri ya mahakama haikupelekwa katika ofisi za chama, Buguruni Januari 4 mwaka huu saa sita mchana na karani wa mahakama na kikakataliwa kupokelewa na mlinzi wa ofisi hiyo.

Pia aliomba mahakama hiyo ikatae pingamizi la wakili wa mdai lilotaka Hamad aitwe mahakamani hapo ahojiwe kuhusu maelezo aliyoyatoa kwenye kiapo chake ambacho alikitumia kufungulia kesi yake ya msingi kwa sababu ombi hilo limeletwa mapema mno kabla ya ombi la msingi halijaanza kusikilizwa.

Januari 4 mwaka huu saa nne asubuhi, Jaji Shangwa alitoa amri ya muda ya kuzuia Bodi ya Wadhamini wa CUF kuwavua uanachama Hamad na wenzake hadi kesi ya msingi iliyofunguliwa itakapokuja kusikilizwa.

Chanzo:Gazeti la Tanzania la Jumanne, Februali 15 mwaka 2012

SI KILA MTU ANAFAA KUWA KIONGOZI




Na Happiness Katabazi

KWA muda mrefu miongoni mwa wasomi na wananchi wa kawaida wamekuwa na mawazo tofauti kuhusu viongozi wanapatikanaje na ni hasa anastahili kuwa kiongozi.

Wapo wanaoamini kwamba uongozi ni karama au kipaji anachozaliwa nacho mtu, lakini kuna wengine wanaamini mtu anaweza kufundishwa kuwa kiongozi.Kwa upande mwingine wapo wanaoamini kwamba akiwa na sifa za kuzaliwa na akapewa mafunzo ya uongozi huyo ndiye kiongozi anayefaa.

Lakini wote hawa ukubaliana na jambo moja kwamba si kila mtu hata asiyekuwa na sifa anaweza kuwa kiongozi. Kimsingi kiongozi lazima awe na sifa zinastahili ikiwa ni pamoja na uelewa wa mambo, maono, awe ni mfano bora kwa wanaowaongoza na asiyetanguliza maslahi yake binafsi.

Dunia imebahatika kupata viongozi wenye sifa za namna hii na mifano hao viongozi si ya kutafuta kwa maana ni wengi. Kule Afrika Kusini, kulikuwa na Nelson Mandela, alikuwa na uelewa wa mambo na msomi wa hali ya juu alitanguliza maslahi ya watu wa taifa lake weupe kwa weusi hata akafungwa gerezani miaka 27 kwa sababu hiyo

Tukirejea Tanzania tunaweza kumtaja Baba wa Taifa Julius Nyerere, ambaye alipenda na taifa na watu wake na hata muda mfupi ya kuaga dunia alitamka wazi atawaombea wananchi wa taifa hili kwa mwenyezi mungu. Nyerere aliwahi kusema Ikulu ni mahali patakatifu na pana mzigo mzito wa kuwatumikia wananchi waliona matatizo mbalimbali kama umaskini na kadhalika.

Nyerere alikuwa msomi mbobevu na mwenye shahada kadhaa za vyuo vikuu kadhaa.Mwenye maono, na mwenye msimamo dhabiti katika yale aliyoyaamini. Kiongozi huyu aliyeweza kuibua viongozi wengine wenye sifa kama za kwake na pengine ni za kipekee mathalani marehemu Moringe Sokoine, ambaye aliwahi kuwa Waziri Mkuu wa nchi hii.

Nyerere alijenga vyuo vya kuwafunza watu uongozi akijua kwamba anatengeneza uongozi wa baadaye wa taifa lake kwa bahati wanafunzi wake wengi , wamesaliti mafunzo aliyowapa. Taifa letu la Tanzania lilipata bahati kubwa wakati wa uongozi wa Nyerere, viongozi waliheshimika ndani na nje ya nchi.

Waliheshimika kwa sababu walijiheshimu, walifuata maadili, walikuwa na moyo wazalendo na kutanguliza maslahi ya taifa mbele na hawakuwa wabinafsi wala wasanii. Viongozi hawa walipokuwa wakitamka jambo au kutoa maelekezo kwa watendakazi chini yao, wananchi kwa ujumla walisikilizwa na maelekezo yalikuwa yakitekelezwa kwa vitendo bila kupuuzwa.

Leo hii viongozi wetu wengi wanatoa maelekezo wanaishiwa kukosolewa na wananchi na watalaamu mbalimbali.

Lakini kama alivyoimba mwanamuziki maarufu wa muziki wa kizazi kipya Lady J Dee, ‘Siku hazigandi’, enzi za uongozi na viongozi walio na uwezo wa kutupeleka kule kunakostahili hivi leo zinaoneka kama zimetoweka.

Sifa na vigezo vya mtu kuchaguliwa kuwa kiongozi leo hii si tena zile sifa njema, taifa hili sasa linashuhudia watu wakipata uongozi kwa sababu ya mahusiano yao na watu fulani wenye sauti katika jamii na nguvu ya fedha.

Wengine wanakuwa viongozi kwa sababu hapo zamani au hata sasa wana uhusiano wa kimapenzi na wenye mamlaka ya kuteua. Kwa upande mwingine wapo viongozi ambao madaraka yao yametokana na undugu na kiongozi fulani mkubwa, wengine kwa kisingizio cha kufuata nyayo za wazazi wao, waume zao au wake zao na kuwa mabingwa wa fitna.

Kwa kuwa hizi ndio zimeanza kuwa sifa za mtu kupata uongozi wa kiongozi katika taifa letu hii leo tunashuhudia uongozi uliolegalega kwa namna ambayo haijawahi kutokea katika historia ya nchi yetu.

Leo hii viongozi wetu hawasemi kitu kikasikilizwa na watendaji waliopo chini yao wala kikatekelezwa na wananchi ipasavyo. Viongozi wengi wanaonekana kupwaya katika nafasi zao, kwani wengi wanadaiwa hawana uwezo kuwashawishi utendaji kazi na wao wenyewe hawaonekani kumudu majukumu yao.

Cha kustaabisha zaidi baadhi ya viongozi hawaonekani kuwa na mvuto tena wa kusikilizwa na kupata utii unaostahili kutoka kwa wananchi. Hayo yote ni kwa sababu ya viongozi wetu kukosa sifa machoni pa jamii na katika baadhi ya viongozi kuanzia ngazi ya chini tulionao si viongozi wenye uelewa mpana wa mambo, maono, uzalendo na maadili.

Endapo tutaendelea kuwa na viongozi wanaopwaya kiasi hiki, taifa letu litasahau habari ya kutokomeza umaskini na kusonga mbele kimaendeleo sana sana tutapiga hatua kurudi nyuma siku hadi hadi siku.

Lakini hatima ya nchi hii katika suala la uongozi lipo mikononi mwa wananchi,wananchi ndiyo tunatakiwa tusimame sasa na kusema viongozi wasio na sifa sasa basi.

Tufike mahali ambapo hatutamchagua kamwe kiongozi mbinafsi, anayeandamwa na tuhuma za ufisadi, mlaghai, mbumbumbu, asiye na dira wa mwelekeo eti kwasababu tu kundi lake linanguvu kubwa ya kifedha na kutuhonga wapiga kula pilau.

Tena sasa hivi imeibuka mchezo mchafu wa baadhi ya wanasiasa wanautaka urais ,mwaka 2015 kujipitisha katika ,makanisa kuanza kujipigia kambeni na kuwarushia vijembe mahasimu wao.Nasisitiza tena viongozi wa aina hii hawatufai kwani wanamdhihaki mungu pia.
Kama wananchi hatutajali, tukumbuke kuwa dereva asiye na sifa za kuwa dereva akiendelea kupewa usukuni siku atakaposababisha ajali likawa janga la kitaifa, tutakaopoteza uhai ni sisi wananchi na dereva (kiongozi) huyo atatokomea kusikojulikana atakimbilia kule alikohifadhi fedha ambazo yeye na wenzake waliuibia umma.

Ni kweli jamii za wanadamu zinahitaji viongozi na viongozi hao lazima wawe watu. Hivyo ingawa viongozi wote ni watu lakini si kila mtu anafaa kuwa kiongozi.

Yule ambaye hawawezi kufikiri kwamba jamii anayokusudia kuiongoza atafanyia nini, bali anafikiri jamii imfanyie nini hatufai.

Yule ambaye yupo tayari kuuza mwili wake ili apate nafasi ya uongozi hatufai. Yule ambaye yupo tayari kutoa na kupokea rushwa ili apate uongozi hatufai.

Na yule aliyeanza kufanya usanii wa kampeni za kusaka urais wa mwaka 2015 leo hii katika makanisa hapa nchini hatufai kabisa.Yule ambaye anamsingizia uongo mwenzake ili kujipatia uhalali machoni pa wananchi hatufai.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika

0716 774494

www.katabazihappy.blogspot.com

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Februali 14 mwaka 2012

VIONGOZI WA AINA HAWAFAI




Na Happiness Katabazi

HAPA nchini hivi sasa kwa kasi ya aina yake umezuka mtindo unaofanywa na baadhi ya viongozi wa makanisa ya kuwaalika baadhi ya wanasiasa kuudhulia katika makanisa hayo kwaajili ya kuongoza shughuli za harambee.

Na katika harambee hizo tumeshuhudia baadhi ya wanasiasa hao wanaoarikwa kuongoza harambee hizo au kuudhulia misa mbalimbali, ugeuza harambee hizo kuwa majukwaa ya kuwapiga vijembe wanasiasa wenzao ambao wanahasimiana kisiasa na wengine wemekuwa wakiwaita wanaisasa wenzao ambao nao wamekuwa wakienda makanisani humo kuwa ni mafisadi ambao wamekuwa wakitumia makanisa hayo kujisafisha katika tuhuma hizo za ufisadi zinazowakabili.

Binafsi sipingi viongozi hao wa makanisa kuwaalika wanasiasa kwenda kuongoza shughuli mbalimbali makanisani na sipingi wanasiasa kwenda kuudhulia harambee hizo.

Licha tayari kuna taarifa zisizopendeza ambazo bado hazijathibitishwa kuwa kuna baadhi ya viongozi wa dini kwa tamaa ya fedha na wengine tayari wameishakuwa kwenye kambi za wanaotajwa kuwania rais mwaka 2015 wamekuwa wakimwalika mwanasiasa mwenye nguvu ya fedha ambaye wanaamini wakimwita kwenye harambee zao atawachangishia fedha nyingi na hivyo harambee yao itakuwa imefana kwani watakusanya fedha nyingi.

Na hivyo wale wanasiasa ambao hawana nguvu ya kifedha wamekuwa hawapewi kipaumbele cha kualikwa na viongozi hao wa makanisa.

Kumekuwepo na taarifa kuwa nao hao wanasiasa wamekuwa wakifanya ushawishi kwa njia wanazozijua ili waweze kualikwa kwenye makanisa ambayo yanawafuasi wengi ili waweze kuudhulia kwenye ibada na baada ya ibada kumalizika, viongozi wa makanisa uwapa fursa ya kuhutubia na hapo ndiyo wanasiasa hao hawa ambao wanatufanya sisi waumini ni majuha tusiojua wanachikitafuta huko makanisani ni nini ,upata fursa ya kuwarushia makombora ya maneno ya shombo mahasimu wao wa kisiasa kwa kuwaita ni mafisadi hawafai kuwa viongozi.

Kwa kweli hali hii inasikitisha na kutisha kwani unapoona taifa lina viongozi wa kisiasa hasa wale wa chama tawala (CCM), wamekuwa vinara wa kucheza mchezo huo hatari wa kwenda kufanya ghiliba za wazi makanisani, ni hatari sana na hali hii isipotokomezwa ni wazi ipo siku Mungu atachoka kuona waumini wake wanafanyiwa ghiliba na usanii na wanasiasa hawa makanisani na hivyo ataamua kuwaadhibu wanasiasa hao na makuwadi wao, na wasije kulia na mtu.

Yaani tumefika mahali pabaya sana kama nchi hivi sasa, zile tabia zetu za kihuni, ujanja ujanja,usanii na utapeli na uongo tulizokuwa tunazifanyia nje ya nyumba za ibada hivi sasa shetani ametutawala mioyoni mwetu atuziogopi tena nyumba hizo za ibada , tumevaa ujasiri na kuamua kuziingiza tabia hizo za kishetani ndani ya nyumba za ibada tena bila wasiwasi .

Kwanza minashangaa sana ni kwanini hawa wanaotajwa na wapambe wao kuwa watagombea urais katika uchaguzi mkuu ujao,mbona wameanza vurugu za kampeni mapema kiasi hiki tena kwa njia ya kujitafutia lana kwa mwenyezi mungu kwani wanaanza kampeni zao kwa kutumia makanisa?

Hivi urais wa Tanzania umekuwa ni rahisi rahisi kiasi hiki?

Baadhi ya wapambe wa hao wanaotajwa kutaka kugombea urais wamekuwa wakinieleza kuwa wanachelewa kulala kwasababu mara kwa mara wamekuwa wakikutana kwenye vikao vyao vya siri kwaajili ya kuimarisha kambi zao na kupanga mikakati ya kuwadhoofisha maadui wa kambi yao kwa njia tofauti ikiwemo njia ya kuwaibulia tuhuma kupitia vyombo vya habari.

Ieleweke wazi mchezo huu ni hatari kwa umoja wa taifa letu kwani utaanza kuleta matabaka ya kidini.

Binafsi napingana na hao wanasiasa ambao wamekuwa wakialikwa na makanisa hayo kwenye shughuli hizo halafu wakifika kwenye shughuli hizo wanaanza kurusha vijembe kwa mahasimu wao kisiasa licha hawawataji majina lakini mtu mwenye akili timamu na anafuatilia vijembe hivyo,utabaini wazi mwanasiasa huyu anampiga kijembe mwanasiasa fulani ambaye hayupo kwenye kundi lake linalomuunga mkono katika harakati zake za kusaka ukubwa.

Hivi kanisani si ni mahali pakuongelea mambo ya mungu,kutubu kama ulivyafanya mambo mabaya ili usamehewe na kumshukuru mungu kwa baraka na hiyo ndiyo hasa maana ya ibada.

Leo hii wanasiasa wetu hao ambao kwa mujibu wa watu wao wa karibu na wapo wanatueleza kuwa vinara hao na wapambe wao ambao wanapishana kwenye makanisa tofauti kuwa wameanza kampeni za kusaka urais wa mwaka 2015,wawapo kwenye ibada hizo wanatoa hotuba za kuwapiga vijembe mahasimu wenzao wa kisiasa hali inayofanya tujiulize kama kweli tunaamini kanisani ni mahali ambapo watu wanaenda kumshukuru mungu,kutubu na kumsifu mungu, ,sasa hizo dondo za kisasa zinazotolewa na wanasiasa hao zinaingiaje?

Kama Yesu alivyosema kuwa ya Kaisali mpe Kaisali na ya Mungu mpe Mungu.Ufisadi na mbio hizo za urais mnaziingizaje makanisani? Yaani ni sawa na mdudu kaingiaje kwenye kokwa la embe?

Biblia inasema Mtu hataishi kwa mkate tu ila neno la mungu. Lakini pia tunatambua mwanadamu hawezi kuishi kwa neno la mungu tu na ndiyo maana tunatafuta na kisha tunatoa sadaka na dhaka kwenye nyumba zetu za ibada.

Kwa hiyo mkate tunaoupata sisi binadamu baada ya kuutafuta, uutoa kwenye nyumba zetu za ibada kwa njia ya sadaka na dhaka na hiyo ni sehemu pia ya ibada ya kufanya nyumba zetu za ibada ambazo uendeshwa kwa neno la mungu au Mtume Mohamad kwa njia ya ibada.

Kwa hiyo hata watumishi wa mungu wanaopokea sadaka hizo zile zinazotolewa kiwango kikubwa cha waumini wao hasa hao wanasiasa zinatoka katika mapato halali ya waumini wao wanaozileta makanisani na hizo harambee.

Kama watumishi hao wa mungu watasisitiza kupokea mapato tuu,basi mwisho wa siku makanisa yatajikuta yakipokea sadaka ambazo zimepatikana kwa njia ya kihalifu.

Mtu maisha yake yote kasoma kamaliza ,akaajiliwa kuwa mtumishi wa umma,akaacha kazi hiyo akajiunga kwenye medani ya siasa kama Mbunge,waziri,mjumbe wa NEC.Kote huku mapato yake yanajulikana.

Ghafla mtu wa aina hiyo anajifanya (raimu sana)yaani mtu mwema anaibukia katika makanisa tofauti anachangia mamilioni ya shilingi,mapato ambayo yakikusanywa yanazidi kipato chake kinachotambulika na mamlaka ya vyombo husika.

Ni lazima sasa tujiulize hiyo ziada imetoka wapi? Na hoji hilo kwa sababu tusije tukafika mahali wahalifu wakafadhili shughuli za kijamii kwa mbwembwe na wakaheshimika na wale na watu wenye maadili na wasiyo na uwezo wa kifedha wakaonekana ni watu wa ovyo kwa kuwa tu hawana fedha za ziada ya kutoa kwenye harambee makanisani.

Maana siku zote mtu ambaye hana fedha yaani maskini anaonekanaga ni mtu asiye na akili kabisa kwasasa kila jambo analotaka kufanya hawezi kulifanya kwasababu ya kukosa fedha ya kulifanya na mwishowe anaishia kuonekana hana akili.

Nafikiri taasisi zetu za dini zijiulize thamani ya makanisa yao,baadhi ya waumini wao na wasiyowa waumini wao kuwachangia mapesa mengi bila taasisi hizo kujiuliza mapato halali ya ziada ya hao wanaoongoza harambee makanisani ambazo taarifa zinadai ,hiyo ni mbinu moja wapo wa kujisafishia njia ya kuwania urais mwaka 2015.

Ieleweke kuwa makanisa na misikiti yanapaswa yapokee mapato halali siyo haramu.Makanisa kukubali kupokea mapato kutoka kwa ambao ikaja kubainika ni mapato haramu ,makanisa yatakuwa nayo yameshiriki kwa njia moja au nyingine kutenda uhalifu huo(accomplice).

Aidha vyombo vyetu vya dola ambavyo vinaendeshwa kwa gharama kubwa na kodi za wananchi kufanyakazi zake ili pia viweze kuwachunguza watu wenye mapato ya ziada,hadi wananchi wanashtukia. Je havilijui hili? Na kama imelijua hilo,vimechukua hatua gani?

Mungu ibariki Tanzania, mungu Ibariki Tanzania

0716 774494

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumatano, Februali 8 mwaka 2012

ADHABU MBADALA IAMASISHWE



Na Happiness Katabazi

FEBRUALI 3 mwaka huu, Tanzania ilikuwa ikiazimisha Siku ya Sheria(Law Day) ambayo kitaifa ilifanyika katika viwanja vya Mahakama Kuu kanda ya Dar es Salaam, ambapo Rais Jakaya Kikwete ndiye alikuwa mgeni rasmi ambapo mwenyeji wake alikuwa ni Jaji Mkuu Mohamed Chande Othman.

Kauli mbiu ya sherehe hiyo ambayo ni ishara ya ufunguzi rasmi wa shughuli za mwaka mpya wa mahakama ni “Adhabu Mbadala katika kesi za jinai :Faida zake”.

Ambapo Rais Kikwete, Jaji Mkuu Othman, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali George Masaju na Rais wa Chama cha Wanasheria cha Tanganyika(TLS), Francis Stolla ndiyo waliopata fursa ya kusoma hotuba zao ambazo zilijadili kauli mbiu hiyo kwa kina isipokuwa hotuba ya Rais Kikwete ambaye alikuwa wa mwisho kusoma hotuba yake ambayo ilikuwa fupi na alianza kwa kutoa neon la kujiami mapema kuwa yeye siyo mwanasheria kitaaluma kwahiyo hotuba yake haitazungumzia kwa undani masuala ya kisheria kuhusu kauli mbiu hiyo ila anaishauri mahakama itoe elimu na faida kuhusu matumizi adhabu mbadala ili umma uweze kuelewa faida zake.

Jaji Mkuu Othman katika hotuba yake siku hiyo ambayo gazeti hili inayo nakala yake alisema duniani kuna wafungwa na mahabusu milioni 9.8. Leo katika kila Watanzania 100,000 kuna takribani wafungwa na mahabusu 88. Mwaka 2008, walioongoza duniani ni Marekani ambapo kwenye kila watu 100,000 kulikuwa na wafungwa na mahabusu 756 .Hali nchini nyingine ilikuwa hivi:Rwanda 604,Afrika Kusini 335, Uingereza 153 na Kenya 130. Duniani nchi iliyokuwa na idadi ndogo kabisa ya mahabusu na wafungwa ni India ambayo kwa kila watu 100,000 ilikuwa na wafungwa na mahabusu 25 tu.

Alisema Desemba mosi mwaka jana, Tanzania ilikuwa na wafungwa na mahabusu 38,080 .Kati yao wafungwa walikuwa 18,978 na mahabusu 19,102. Uwezo wetu wa hifadhi magerezani ni nafasi 29,552. Matokeo ni wastani wa zaidi ya asilimia 29 ya msongamano pia uwiano kati ya wafungwa na mahabusu kwa muda mrefu umekuwa karibu nusu kwa nusu.

“Idadi kubwa ya mahabusu gerezani ambayo hairidhishi inachangiwa haswa na ucheleweshaji wa uchunguzi wa makosa ya jinai, upatikanaji wa mashahidi, mwendo mrefu wa kesi na mlundikano wa mashauri mahakamani, upatikanaji wa mwenendo wa mashauri na nakala za hukumu kuwezesha rufani kusikilizwa, masharti ya dhamana na uwezo wa watuhumiwa kutimiza masharti ya dhamana”alisema Jaji Othman.

Jaji Othman alisema pamoja na kupungua kwa wimbi kubwa la ujambazi lililotokea wakati serikali ya awamu ya nne ilipoingia madarakani, mwaka 2005 idadi muhimu ya wafungwa magerezani imechangiwa na matokeo ya uhalifu yaliyoainishwa kama adhabu kifungo cha miaka mitano hadi maisha, sheria zinazotoa kama sharti muda maalum wa kifungo(mandatory sentences), sheria zinazoainisha kama amri adhabu za chini za kifungo na mategemezi ya kupindukia ya adhabu ya kifungo kuliko adhabu zisizo kifungo.

“Suala si la idadi tu.Changamoto nyingine ni kwamba nafasi ya kuhifadhi wafungwa na mahabusu magerezani ni ndogo .Bado tuna tatizo sugu la msongamano haswa kwenye magereza ya mjini na usipodhibitiwa , unaweza kuwa adhabu ya pili.Kila mtu aliyetiwa hatiani kisheria na mahakama kwa kosa la jinai anastahili adhabu”anasema.

Jaji huyo alisema kwenye makosa ya jinai Sheria inaipa Mahakama busara ya uamuzi na uwezo wa kutoa kiwango cha adhabu stahili. Busara ya kutoa adhabu ina mipaka.Ikipindukia, mahakama za juu zina uwezo wa kuisahihisha ,aidha adhabu kali au ndogo sana iliyotolewa na mahakama za ngazi za chini na hivyo ndivyo wanavyowajibishana.

Aidha anasema kuna sheria nyingine kama Sheria ya Chini(Minimum Sentence Act,Cap 90), na Sheria Maalum ya Makosa ya Kujamiana(SOSPA) (Sexual Offences Special Provisions Act, 1998) ambazo zimeiondolea mahakama busara ya kutoa adhabu kwa kuainisha kama amri adhabu lazima za kifungo cha muda mrefu. Hilo linahusu makosa kama yale ya kijinsia, ujambazi na wizi wa mifugo.



“Kwa uzoefu wa nchi nyingi kuna njia mbili kuu za kuponyesha msongamano na kuhitimisha malengo ya adhabu.Ya kwanza ni kujenga na kuendelea kujenga magereza kwa kasi zaidi kila hapo idadi ya wafungwa na mahabusu itakapozidi nafasi za hifadhi.Na ukubwa wa magereza ya nchi unapimwa na mambo mawili; watu wangapi wanaoingia na wangapi wanaotoka kila siku”alisema.

Anasema njia zote hizo zina gharama. Kwa upande mmoja , ni zile za serikali kuwahifadhi na kuwailisha walio magerezani ambayo hapa nchini lishe ya kila mmoja wao ni takribani sh 2,300 kwa siku au sh bilioni 32 kwa mwaka na za usimamizi wa magereza. Kwa upande mwingine ni gharama za amani na usalama ambazo jamii itazibeba endapo mhalifu atatumikia adhabu mbadala kwenye jamii.Kwa vyovyote vile jamii ikumbuke kuwa sio kila mhalifu ana stahili adhabu ya kifungo , wengine wanastahili adhabu mbadala.



“Kwenye kutafuta jibu la kudumu inabidi serikali na jamii ipime gharama , madhara na lawama za kifungo gerezani na gharama, madhara na lawama za adhabu mbadala kwenye jamii. Ni ipi kati ya hizo njia mbili ina uwezo zaidi wa kurekebisha wafungwa,haswa wale wenye makosa madogo madogo warisudie tena uhalifu watakapo rejea uraiani,yenye uwezo wa kuwafidia waathirika wa kosa na kulinda jamii.Tukizingatia yote hayo njia muafaka ni kujenga suluhisho linaloweza kujihimili.Hoja siyo tu kuwa mkali wa uhali bali ni kuwa mwerevu wa uhalifu”alisema.

Adhabu mbadala ;alisema wanapozungumzia adhabu mbadala wanamaanisha ni adhabu yoyote ambayo siyo kifungo gerezani.Miongoni mwa malengo na faida za adhabu mbadala ni kupunguza msongamano wa wafungwa magerezani, kushusha gharama za kuendesha magereza,kumuwezesha mtenda kosa kujiunga tena uraiani kwa urahisi, kumpa nafasi afidie jamii kwa kufanya kazi za maendeleo au za jumuiya na hatimaye kumpa nafasi aweze kuishughulikia familia yake.

Hivi sasa Tanzania inaitaji wafungwa walipa kodi,sio wawe mzigo kwa walipa kodi.

Adhabu mbadala :Amri ya Huduma ya Jamii ; Jaji Othman alisema moja kati ya adhabu mbadala yenye kipaji kikubwa kuhitimisha malengo adhabu humuwezesha mhalifu kujirekebisha na kufidia jamii kwa kosa alilotenda na vile vile kupunguza msongamano ni amri hizi za Huduma ya Jamii chini ya Sheria ya Huduma ya Jamii chini ya kifungu cha 3(1)(a)(b) cha Sheria hiyo, amri hizo hutolewa na mahakama kwa mtuhumiwa aliyetiwa hatiani kwa kosa la jinai ambalo adhabu yake haizidi kifungo cha miaka mitatu pamoja au bila ya faini au kifungo kinachozidi muda huo ambacho mahakama inaona kifungo cha miaka mitatu au chini pamoja au bila ya faini kinastahili amri ya huduma ya jamii.

Makosa hayo ni kama yale ya wizi wa maungoni , kupokea mali ya wizi ,kujipatia mali ay fedha kwa njia ya udanganyifu, kutumia lugha ya matusi ,kufanya fujo au kuvunja amri halali ya mahakama. Anawataka wananchi waelewe mahakama haina mamlaka ya kutoa adhabu mbadala kama hizi, kwenye makosa makubwa ya jinai kama yale ya ubakaji,ujambazi na kupatikana na madawa ya kulevya.

Kazi za jamii zilizoainishwa kisheria ni za kusafisha mazingira, usafi wa mabustani na maeneo ya ofisi za serikali,halmashauri na hospitali,ujenzi wa barabara au shule,kupanda miti na kuchimba mitaro ya maji na kazi hizo lazima ziwe kwa manufaa ya jamii pia kazi hizo hazi a malipo.

“Safari huanza kwa hatua, sheria hii ina upeo lakini bado haijatumiwa kikamilifu.Kwanza ,sheria hiyo inatumika kwenye mikoa 12 tu nayo ni Dar es Salaam, Mtwara,Dodoma,Kilimanjaro,Mwanza,Mbeya,Iringa,mArusha,Tanga,Mara,Kagera na Shinyanga.Pia tangu sheria ianze kufanya kazi mwaka 2005 hadi kufikia Oktoba 2011, ni wafungwa 3144 tu walioadhibiwa amri za huduma ya jamii”alisema.

Aidha anaeleza kuwa viungo muhimu katika utekelezaji wa sheria hiyo ni mahakimu, maofisa wa Huduma Jamii wa Mkoa na Wilaya, Maofisa Magereza,Halmashauri na wale wa serikali za mitaa pamoja na watendaji wa Kata na kuwa mafanikio ya kishindo yatapatikana ikiwa wote watashirikiana na kushikamana.

Kwa upande wake Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju alisema kumekuwepo na falsafa nyingi siku hadi siku juu ya aina ipi ya adhabu ambayo inaweza kupunguza au kukomesha uhalifu katika jamii. Falsafa hizi zimegawanyika katika Nyanja mbili.Nyanja moja inasema adhabu ya kifungo jela inafaa zaidi kukomesha au kuzuia uhalifu.Nyanja nyingine inasema adhabu mbadala ndiyo inayofaa zaidi kuliko ile ya kumpeleka jela mhalifu.

Masaju alisema Nyanja hizo mbili uleta mvutano kwa wanafalsafa ,taasisi mbalimbali za serikali na jamii na hata kwa watu binafsi.Kwa ujumla hakuja jibu muafaka juu ya adhabu ipi inaifaa jamii katika kukomesha makosa ya jinai,kwani kila adhabu ina umuhimu na upungufu wake.Jambo la msingi la kuzingatia ni kwamba adhabu yoyote inayolengwa kutolewa ni budi iwe ndiyo yenye manufaa kwa jamii na kwa mhalifu husika kwa wakati huo kutegemeana na jinsi kosa lilivyotendeka.

Masaju alisema wafungwa wanaopelekwa gerezani ni wa makosa yenye aina na uzito mbalimbali.Kuna wafungwa wenye makosa makubwa ambao wamekuwa sugu na hawawezi kubadilika, lakini pia kuna wafungwa ambao ni mara yao ya kwanza kufanya uhalifu na makosa yao ni madogomadogo.Kwa kuyachanganya makundi haya gerezani kundi la mwisho huambukizwa mbinu za kutenda uhalifu wa makosa makubwa huko jela na wakitoka nje hutumia mbinu hizo katika kutenda uhalifu mkubwa katika jamii.Hivyo aina ya makosa yanayostahili kifungo cha jela isipoangaliwa vyema inayafanya magereza yetu kuwa viwanda vya kuzalisha wahalifu sugu.

“Matumizi sahihi ya adhabu mbadala yanaweza kupunguza madhara ya kifungo cha jela endapo adhabu mbadala itawekewa mfumo wa kutumika vilivyo katika jamii yetu.Faida ya adhabu hii kwa kifupi ni kama ifuatavyo huimarisha na kuboresha huduma za jamii, kumwezesha mfungwa kukaa na kuhudumia familia yake,kifungo cha nje huchochea wahalifu kuchukia uhalifu,kupunguza matumuzi ya serikali katika kuendesha kazi za magereza,kupunguza msongamano wa wafungwa gerezani,kuokoa rasilimali watu,kuwaepusha wahalifu wapya kujifunza tabia za uhalifu uliokubuhu”alisema Masaju na kushangiliwa.

Aidha alisema changamoto ambazo inakumbana nazo katika matumizi ya adhabu mbadala ni nyingi na miongoni mwake ni jamii kushahibikia zaidi mila na desturi zinzohusudu adhabu ya kifungo.

“Imekuwa ni desturi ya jamii yetu kuridhika na kung’ang’ania mfumo wa adhabu ya kifungo gerezani hivyo kutaka kila mhalifu apelekwe gerezani.Kutokana na mazoea hayo hata wapo wahalifu ambao nao wanajenga utamaduni wa kuthamini zaidi adhabu ya kifungo kuliko adhabu mbadala ambazo zimewekwa na sheria.Mtu akielewa kuwa akifanya kosa hatafungwa jela kwa mara nyingi haogopi kutenda kosa hilo.

Hiyo ni kwa sababu jela ndiyo mahala pekee panapowatisha watu wote ambao kwa mazoea wanapaswa kuishi kwa uhuru na kujitawala.Mtazamo huo huwafanya hata baadhi ya wadau wanaohusika na utoaji na usimamizi wa adhabu kuhimiza kutolewa kwa kifungo cha jela kuliko adhabu mbadala.

Hata hivyo Masaju alisema baadhi ya watendaji ambao hawana maadili wanatumia adhabu hii kinyume na madhumuni ya sheria.Wanatoa adhabu ndogo isiyostahili kwa minajili ya kutimiza malengo yao maovu ya kujinufaisha wenyewe kwa kupitia utoaji wa adhabu mbadala.Tabia hiyo kwa nyakati Fulani imechangia vitendo vya wananchi kujichukulia sheria mikononi na kuwaadhibu wahalifu kwa mwamvuli wa watu wenye hasira kali.

Aidha Masaju alimaliza kwa kusema ni vyema umma uzingatie mifumo yote miwili ya adhabu ile ya kifungo na ile kifungo cha nje zina umuhimu wake kulingana na aina za makosa na mazingira ya jamii yetu.Kwa hali hiyo basi adhabu zote ziendelee kutumika kwa lengo linalokidhi mahitaji ya jamii na sheria za nchi ambayo ni kutokomeza uhalifu na kuwa na jamii salama na inayodumisha maridhiano katika Nyanja za kiuchumi na kijamii.

Kwa upande wake Rais wa Chama cha Wanasheria cha Tanganyika(TLS), Francis Stola alisema ni suala la mrundikano wa wafungwa na mahabusu magerezani ni jambo linalosumbua vichwa vya wengi hasa zile taasisi ambazo kimsingi zimebeba jukumu hilo.

Naye Rais Jakaya Kikwete aliita mahakama itoe elimu kwa umma kuhusu faida ya adhabu mbadala na kwamba hakuna ubishi kuwa msongamano magerezani upo, unakera na kwamba anaamini kuwa endapo adhabu mbadala ikianza kutolewa kikamilifu na mahakimu itasaidia kupunguza msongamano.

Rais Kikwete pia alipongeza jitihada za kimaendeleo zilizopigwa na mhimili wa Mahakama chini ya Jaji Othman na akawahidi kuakikisha atakikisha Mfuko wa Mahakama unaongezewa fedha ili mahakama iweze kufanyakazi zake kikamilifu kwani unaposema huru wa mahakama ni pamoja na mahakama hiyo kuwa na fedha za kujiendesha katika majukumu yake.

Sherehe hizo ziliitimishwa kwa Jaji Mkuu Othman kukagua gwaride maalum liloandaliwa na askari wa Jeshi la Polisi, ikiwa ni ishara ya ufunguzi rasmi wa shughuli za mahakama kwa mwaka huu.

0716 774494

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima Jumapili, Februali 5 mwaka 2012

KATABAZI VS MUTUNGI



Happiness Katabazi nikiwa na Msajili wa Mahakama ya Rufaani nchini, Francis Mutungi leo asubuhi katia Mahakama ya Rufaa, muda mfupi baada ya Jaji Mkuu Mohamed Chande Othaman kuanza mkutano wake na waandishi wa habari ambapo, alisema siku ya Sheria itafanyia nchini Februali 3 mwaka huu, kesho na Rais Jakaya Kikwete atakuwa mgeni rasmi.

KIKWETE MGENI RASMI YA SHERIA LEO

Na Happiness Katabazi

JAJI Mkuu wa Tanzania Mohamed Chande Othman amesema rais Jakaya Kikwete leo anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika siku ya sheria nchini ambapo wadau mbalimbali watapa fursa ya kujadili kauli mbiu ya sherehe hiyo isemayo “Adhabu mbadala katika kesi za jinai: Faida zake katika Jamii”.

Jaji Chande aliyasema hayo jana katika mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika katika Mahakama ya Rufani Tanzania jijini Dar es Salaam, wakati akitangaza rasmi kuwa leo ni siku ya Sheria nchini ambapo leo ni miaka 12 tangu ilipoanza kuazimishwa hapa nchini mwaka 1999 chini ya Jaji Mkuu Mstaafu, Francis Nyalali.

Jaji Chande ambaye alikuwa ameambatana na Msajili wa Mahakama ya Rufani Francis Mutungi mbaye jana ilikuwa ni mara ya kufanya mkutano na waandishi wa habari hapa nchini tangu alipoteuliwa na Rais Kikwete kushika wadhifa huo, alisema wadau mbalimbali akiwemo yeye wataijadili kauli mbiu hiyo kupitia hotuba zao ambapo aliwataka wananchi wengi kujitokeza katika sherehe hiyo ambayo ukutanisha viongozi wa mihimili mitatu ya nchini, wanachi wa kada tofauti na kwamba vituo vya mahakama kote nchini zinaadhimisha sherehe hiyo.

Katika hatua nyingine Jaji Chande alisema ili majaji na mahakimu waende na wakati katika kuendesha mashauri mbalimbali mahakama hiyo tayari imeanzisha utaratibu wa kuwapeleka majaji na mahakimu katika kozi fupi na endelevu katika Chuo cha Uongozi wilayani Lushoto. Na kwamba kila jaji atakayeteuliwa atalazimika kuudhulia kwanza mafunzo mafupi yatayomsaidia kuweza kutenda kazi yake ya kijaji.

“Hakuna mahakama isiyokosea ila kuna makosa mengine majaji na mahakimu wanaweza kuyaepuka hivyo ndiyo maana uongozi wa Mahakama hivi sasa umefikia uamuzi huo wa kuwapeleka kwa awamu majaji na mahakimu wake katika Chuo cha Uongozi Lushoto ili waweze kupata mafunzo na utaratibu huo umeishakamilika na mwaka huu, unaanza kutekelezwa kwa vitendo.

Alipoulizwa swali na mwandishi wa habari hizi ni kwanini kila mwaka sherehe ya siku ya sheria imekuwa ikifanyika kitaifa jijini Dar es Salaam, alisema hakuna sababu maalum inayoulazimisha mhimili kufanya sherehe hiyo hapa jijini ila mahakama italifanyiakazi jambo hilo kwa siku zijazo.

ChanzoGazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Februali 3 mwaka 2012.

MAHAKAMA IBADILIKE,IENDE NA WAKATI



Mahakama ibadilike,iende na wakati
Na Happiness Katabazi

KESHO Februali 3 mwaka huu, Mahakama ya Tanzania,inasherehekea siku ya Mahakama(Law Day). Sherehe hii ufanyika mara moja kwa mwaka na ufanyika tarehe za mwanzoni za mwezi Februali.

Kufanyika kwa sherehe hiyo ni ishara ya ufunguzi rasmi wa shughuli za mahakama kwa mwaka huu wa 2012. Itakumbukwa kuwa mahakama yetu imejiwekea utaratibu wa mwezi Desemba-Januari , Majaji na mahakimu uenda likizo kwaajili ya mapumziko na kisha kurejea maofisini rasmi mwanzoni Februali, baada ya sherehe hiyo kufanyika.

Mwaka huu sherehe hiyo ambayo itafanyika kesho na Rais Jakaya Kikwete atakuwa mgeni rasmi na mwenyeji wake atakuwa Jaji Mkuu Mohamed Chande Othman katika maazimisho hayo yatakayofanyika kitaifa jijini Dar es Salaam.

Kauli mbiu ya sherehe hiyo kwa mwaka huu inasema “Adhabu mbadala katika kesi za jinai:Faida zake katika Jamii”
Ni wazi kauli mbiu hiyo kwa wale wadau wa mahakama na utawala wa sheria itakuwa ni changamoto kwao.

Hakuna ubishi kuwa mhimili wa mahakama hapa nchini hivi sasa umeweza kupiga hatua za kimaendeleo kwa kadri ilivyoweza na unakuza utawala wa sheria kila kukicha kutokana na kutoa maamuzi mbalimbali ambayo mengine yamekuwa yakiripotiwa katika vyombo vya habari.

Baadhi ya hatua za maendeleo yaliyopigwa ni ukarabati na ujenzi wa baadhi ya mahakama, baadhi ya mahakama kufungwa teknolojia ya ya kisasa ya kurekodi mwenendo wa kesi,watumishi wengi kujiendeleza kielimu, kutoa hukumu mbali zilizohusisha kesi zilizokuwa zikiwahusu watu wenye majina makubwa kwenye jamii na kisha wengine mahakama ikawatia hatiani na wengine kuachiliwa huru.

Hatua nyingine ni ile iliyochukuliwa chini ya uongozi wa Jaji Mkuu Mstaafu Agustino Ramadhani enzi za uongozi wake kuweka kanuni amewafanya majaji wote wa mahakama kuu kuwa ni majaji wa Mahakama Kuu Kitengo cha Ardhi. Kwani kwa mujibu wa Jaji Ramadhani nakumbuka mwaka juzi nilivyofanya mahojiano naye alisema alifikia uamuzi huo baada ya kuona mahakama kuu kitengo cha Ardhi kina majaji wachache wakati mashauri ya ardhi katika mahakama hiyo ni mengi hali inayosababisha kesi kuchelewa kumalizika kwa wakati.
Na hata Msajili wa Mahakama Kuu Kitengo cha Ardhi Lameck Mlacha katika mkutano wake na waandishi wa habari ofisini wake mapema mwaka jana, alisema hivi sasa mlundikana wa mashauri ya migogoro ya ardhi katika mahakama hiyo unapungua kwa kasi ukilinganisha na miaka ya nyuma.

Katika hili mahakama inastahili pongezi kwani migogoro ya ardhi imekuwa ikiibuka kila kukicha mahakamani, katika mabaraza ya Kata, Wizarani.

Tukiachana na hilo baadhi ya hatua hizo za maendeleo zilizopigwa, lakini bado mhimili huo wa mahakama ambao umepewa jukumu la kutoa haki katika Ibara ya 107A ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 ni kama zifuatazo.

Uhaba wa vyumba vya kuendeshea kesi, bado idadi ya mahakimu ni ndogo ukilinganisha na mahitaji ya kila siku,baadhi ya mahakama huko mikoani ngazi ya wilaya na mahakama za Mwanzo zipo katika mazingira mabovu ambayo yanaitaji kufanyiwa marekebisho ili hata watendaji wa mahakama waweze kujisikia wanafanyakazi kwenye ofisi zenye hadhi ya kuwa ofisi ya mahakama.
Nikiwa mwandishi wa siku nyingi wa habari za mahakamani hapa hususani zile za mahakama za mkoa wa Dar es Salaam, nimeshuhudia mahakama za mji huu ambao karibu mahakama zote zenye hadhi ya wilaya, Hakimu Mkazi Kisutu, Mahakama Kuu na Rufaa,waandishi wa habari uweka kambi kwa siku zote za juma kwaajili kuripoti kesi mbalimbali zinafunguliwa na kuendelea katika mahakama hizo.
Hakuna ubishi hivi sasa mhimili wa mahakama hivi sasa kupitia majaji na mahakimu wanatambua kazi ya waandishi wa habari ndiyo maana uwaruhusu waandishi wa habari kuingia ndani ya vyumba vya mahakama kusikiliza kesi wanazoziendesha kwa kuwapatia nafasi za viti, kuwapatia ushirikiano wa kuwafafanulia baadhi ya maneno ya kisheria ambayo wamekuwa hawayaelewi,kuwapatia majalada ya kesi kuyasoma na katika kesi ambazo zimekuwa zikufuatiliwa na umma Hakimu Mkuu Mfawidhi wa Mahakama ya Kisutu, Elvin Mugeta na Msajili wa Mahakama ya Rufaa Francis Mutungi siku moja kabla uwa wanatoa maelekezo kwa watendaji wao chini wa kuwatengea sehemu maalum ambapo mabechi kwaajili ya waandishi wa habari kuja kuketi ili waweze kuripoti kesi hiyo.

Na mfano hai wa viongozi hao wa mahakama kutoa ushirikiano wa aina hiyo kwa waandishi wa habari za mahakama ni siku mwaka juzi siku ile jopo la majaji saba wa mahakama ya Rufaa lilokuwa likiongozwa na Jaji Mkuu Mstaafu Agustino Ramadhani, kesi ya mauji iliyokuwa ikimkabili aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi mkoa wa Dar es Salaam, (ACP),Abdallah Zombe na wenzake, kesi ya kulawiti iliyokuwa ikimkabili mwanamuzi nguli wa Dansi, Nguza Vicking na mwanae Papii Kocha , kesi ya kula njama na kuomba rushwa ya shilingi milioni 10 iliyokuwa ikimkabili aliyekuwa Mtangazaji wa Shirikila la Utangazaji la TBC1,Jerry Murro.
Binafsi nilishiriki kuwasilisha mara kadhaa maombi ya kuomba mahakama iwawekee nafasi waandishi wa habari za mahakama kwa Hakimu Mugeta na Mutungi kwa njia simu na kweli viongozi hao waliweza kutekeleza ombi hilo kwa vitendo.

Tunashukuru sana na hiyo ni ishara kwamba hivi sasa mahakama inatambua mchango wa waandishi wa habari katika utendaji wa kazi wa mhimili huo ambao kwanjia moja au nyingine vinashirikiana na vyombo vya habari na wadau wengine kukuza utawala wa sheria na kuubarisha umma maamuzi yanayotolewa na mhimili wa mahakama.

Hivyo wakati mahakama kesho ikianza mwaka mpya wa Mahakama,sisi waandishi wa habari za mahakama tunamuomba Jaji Mkuu Mohamed Chande na timu yake iweke mashine (Photocopy mashine)ya kutolea nakala katika mahakama zake ambazo tutakuwa tukilipia ili wadau wa mahakama waondokane na usumbufu wa kwenda umbali mrefu kusaka huduma hiyo, pia sisi waandishi wa habari tunaomba tutengewe angalau chumba kimoja pale Mahakama ya Kusitu na Mahakama Kuu ambacho kitakuwa na kompyuta kwaajili ya kuweza kuwasaidia kuandika habari za mahakama na kuzituma maofisini kwao mapema, wakati wakisubiria kuingia mahakamani kuudhulia mashauri mengine yanayoendeshwa mchana na kumalizika wakati mwingine jioni.Naamini hayo yakifanyika na mengine zaidi yakiboreshwa mahakama yetu itakuwa inazidi kwenda na wakati.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika

0716 774494
Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Alhamisi, Februali 2 mwaka 2012