HAPPINESS KATABAZI

TUMSHUKURU MUNGU KWA KILA JAMBO(Aprili 29/2013)

HAPPINESS KATABAZI vs.DPP.DK.FELESHI

Happiness Katabazi mwandishi wa habari za mahakamani 'aka'(Mbea wa mahakamani) na rafiki yangu Mkurugenzi wa Mashitaka(DPP) ,Dk.Eliezer Feleshi.(Aprili 15/2013

HONGERA JESHI LA POLISI KWA KUKAMILISHA HARAKA UPELELEZI KESI YA LWAKATARE






Na Happiness Katabazi

APRILI 13 mwaka huu, kupitia mitandao yangu ya kijamii ya www.katabazihappy.blogspot.com na Facebook; happy katabazi niliweka makala yangu iliyokuwa na kichwa cha habari kisemacho ‘ Komeni kujadili mwenendo wa kesi ya Lwakatare nje ya mahakama’.

Kwa kifupi tu ndani ya makala hiyo nilikuwa nawakemea baadhi ya wanasiasa na waandishi wa habari ambao walikuwa wakiijadili mwenendo wa kesi hiyo nje ya mahakama ambayo mawakili wakuu wa serikali Ponsia Lukosi, 
Prudence Rweyongeza na Peter Mahugo wanaoiendesha kesi hiyo tangu ilipofunguliwa kwa mara ya kwanza Machi 18  mwaka huu, na kisha kesi hiyo ikafutwa ikajafunguliwa Machi 20 mwaka huu na ikapewa Na.P1,7/2013,  Machi 22 mwaka huu, kesi hiyo ilipokuja kwaajili ya kutajwa mbele ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, Alocye Katemana walisema wazi kuwa upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika na kesi hiyo ikaarishwa hadi Aprili 30 mwaka huu, itakapokuja kwaajili ya kutajwa.



Nikiri wazi kuwa baada ya kuiweka makala hiyo kwenye mitandao hiyo ilisomwa na wengi na kuwa wengine walionikosoa kwa hoja zisizo na mashiko kwani walishindwa kujikita kwenye hoja yangu iliyokuwa ikikemea makundi hayo iache tabia ya kuingiria uhuru wa mahakama na iliwasisitiza waheshimuwa mgawanyo madaraka.

Lakini kundi jingine lilinipongeza kwa makala hiyo na ninashukuru pia kwani kwa njia moja au nyingine mawazo yangu hayo yaliyokuwa yamewekwa kwenye makala hayo  ambayo yalikuwa yakikataza baadhi ya wanasiasa na waandishi wa habari kaacha kuijadili kesi hiyo nje ya bunge kwani kufanya hivyo ni kuingilia uhuru wa mahakama.

Wiki iliyopita Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Angella Kairuki , Mbunge wa Kigoma Mjini Peter Serukamba na baadhi ya wabunge wengine wakati wakiwa bunge wakichangia hotuba ya Ofisi ya Rais, ambazo hotuba zao ziliwasilishwa bunge na waziri Steve Wassira , George Mkuchika, baadhi ya wabunge walikuwa wakichangia maoni ya bajeti hizo na wengine na walipokuwa wakitaka kuijadili kesi ya Lwakatare , Waziri Kairuki na Serukamba na Wasira walimwomba Spika wa Bunge Anna Makinda na Naibu wake Job Ndugai wawazuie wabunge wasijadili kesi ya Lwakatare kwani ipo mahakamani, na endapo bunge likiruhusu hilo ,ni wazi bunge litakuwa linaingia uhuru wa mahakaman.

Nawapomgeza viongozi hao kwani mawazo yao hayo yalishabiana na mawazo yangu hayo niliyokuwa nimeyaandika katika makala hiyo iliyokuwa na kichwa cha habari kisemacho “KOMENI KUJADILI KESI YA LWAKATARE NJE YA MAHAKAMA’.

Na siyo siri tangu bunge likataze jambo hilo lisijadiliwe nje ya mahakama naweza kusema katazo hilo limesaidia kwa kiasi fulani kwani wale wanasiasa na waandishi wa habari ambao walifikia mbali sana kwakusema kesi hiyo ni ya kubambika ,wamepunguza kasi ya kujadili kesi hiyo na watu tunajiuliza kasi ile ya kuijadili kesi hiyo ya kaka yangu Lwakatare nje ya mahakama imeishia wapi?

Itakumbukwa kuwa Aprili 22 mwaka huu, Kaimu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Issa Mungulu aliwaeleza waandishi wa habari kuwa upelelezi wa kesi tuhuma za ugaidi inayomkabili  Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chadema, Wilfred Lwakatale na mwenzake Joseph Ludovick umekamilika na kwamba jeshi la polisi litapelekea jalada hilo kwa Mkurugenzi wa Mashitaka(DPP)-Dk.Eliezer Feleshi kwaajili ya hatua za kisheria kuhusu kesi hiyo.

Tamko hilo la Kaimu DCI-Mungulu kwa niaba ya jeshi la polisi ndiyo limenisukuma kuandika makala hii ya kulipongeza jeshi la polisi kwani  limeanza kukamilisha upelelezi wake haraka hasa ukizingatia kesi hiyo iliyozua mjadala mkubwa nchini ilifunguliwa Machi  20 mwaka huu. Na Aprili 22, Jeshi la Polisi linautangazia umma kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika.

Hakika hatua hii ni ya kupongeza kwani imedhiirisha kuwa hivi sasa jeshi la polisi limeanza kuondokana na kusuasusa kwa kukamilisha haraka upelelezi wa kesi mbalimbali.

Naweza kusema kwa kipindi cha mwaka huu, tu katika kesi ambazo zinafuatiliwa na umma kwa karibu ,upelelezi wa kesi ya Lwakatare nao umechukua muda mfupi kukamilika kwani kesi ya kwanza ambayo nimeiripoti pale katika mahakama ya hakimu mkazi kisutu ambapo upelelezi ulichukua siku mbili kukamilika ni kesi ya jinai Na.125/2013, Jamhuri dhidi ya wafuasi 53 wa Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu,Sheikh Ponda Issa Ponda  ilidumu mahakamani hapo kwa siku 32 tu tangu ilipofunguliwa rasmi Februali 18 na kutolewa hukumu Machi 21 mwaka huu.Ambapo Hakimu Sundi Fimbo aliwatia hatiani washitakiwa kwa makosa matatu ya kufanya mkusanyiko haramu, kukaidi amri ya jeshi la polisi ambapo kila kosa aliwahukumu kwenda jela mwaka mmoja,Na hivyo wafungwa hao ambao hivi sasa wanaishi Magereza tofauti nchini wanatumikia adhabu ya mwaka mmoja tu gerezani.

Kwa kuwa mimi ni mwandishi wa habari za mahakamani kwa zaidi ya miaka 14 sasa, hupenda kuzilipoti kesi nyingi tangu zinapofunguliwa hadi zinapomalizika na kesi ikishatolewa uamuzi na mahakama nimejenga utaratibu wa kuandika makala inayohusu kesi husika, hivyo hata hukumu ya kesi hiyo ya wafuasi wa Ponda baada ya kutolewa hukumu, niliandika makala  ambayo niliiweka kwenye mitandao yangu ya kijamii yaani www.katabazihappy.blogspot.com na Facebook.happy katabazi ; ambayo ilikuwa na kichwa cha habari kisemacho (HONGERA OFISI YA DPP,POLE WAFUASI WA SHEIKH PONDA).

Ambapo ndani ya makala hiyo nililipongeza jeshi la polisi kwa kukamilisha haraka tena kwa kasi ya ajabu upelelezi wa kesi hiyo ya wafuasi wa Ponda, ambapo wasitakiwa walitenda makosa Februali 15 mwaka huu,na Februali 18 wakafikishw a mahakamani, na baada ya kusomewa mashitaka mawakili waandamizi wa serikali   Bernad Kongora, Bernad Kongora,Peter Ndjike,na Joseph Mahugo,walieleza upelelezi umekamilika na kesho yake Februali 19, kesi hiyo ilikuja kwaajili ya washitakiwa kusomewa maelezo ya awali na walisomewa na siku iliyofuata mashahidi wa upande wa Jamhuri ambapo shahidi wa kwanza alikuwa Mkuu wa upelelezi Kanda Maalum ya Dar es Salaam(ZDCO), Hemed Msangi alitoa ushahidi wake.

Wafuasi hao walifanya maandamano haramu Februali 15 mwaka huu, wakitaka kwenda ofisi ya DPP, ili wamshikinikize ili aweze kuindoa hati yake ya kumfungia Ponda dhamana aliyowasilisha katika mahakama ya Kisutu siku ya kwanza Ponda na wenzake walipofikishwa mahakamani Oktoba 18 mwaka jana, kwa makosa ya uchochezi na wizi wa malighafi za Sh.milioni 59 .

Wakati kesi ya Ponda na wenzake 49 inakuja kutolewa hukumu Mei 9 mwaka huu. 

Kwa wasomi wa sheria tunafahamu faida ya upelelezi kukamilika kwa haraka kwani upelelezi wa kesi unapokamilika kwa haraka ,unaisadia pia kesi iliyopo mahakama kutochukua muda mrefu kumalizika na mshitakiwa kujua mapema hatima yake.

Kwani hakuna ubushi kuna kesi zinachukua zaidi ya mwaka mmoja upelelezi kukamilika na matokeo yake washitakiwa ambao wanakabiliwa na kesi zisizo dhamana kusota gerezani muda mrefu.

Na kwa mujibu wa makosa ya kesi inayomkabili Lwakatare, makosa hayo hayana dhamana hivyo Lwakatare tangu alipofunguliwa kesi anaishi katika Gereza la Segerea akisubiri hatima ya kesi yake. 

Hivyo basi kitendo cha jeshi la polisi kuutangazia umma kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika ni wazi sasa umefanya kesi hiyo kupiga hatua nyingine ya kisheria. Kwani kesi hiyo ambayo Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu haina mamlaka ya kuisikiliza, mawakili wa serikali siku wakifika mahakamani na kuieleza mahakama kuwa upelelezi wa shauri umekamilika, hatua nyingine ya kisheria inayofuata ni kwa mujibu wa tarehe itakayopangwa na mahakama ni kwamba  upande wa jamhuri kuwasomea washitakiwa hao maelezo ya kina ya kesi hiyo inayowakabili (Committal Proceeding) .

Baada ya ya zoezi hilo la kuwasomea (Committal Proceeding) , mahakama itatangaza kuifunga kesi hiyo katika mahakama hiyo ya hakimu mkazi na kisha jadala la kesi hiyo litaamishiwa Mahakama Kuu kwaajili ya kesi hiyo kuanza kusikilizwa rasmi,ambapo siku ya kwanza washitakiwa hao watasomea mashitaka yao na kisha wataruhusiwa kujibu (Plea).

Na hatua nyingine za kuletwa kwa mashahidi zitaendelea.Hadi hapo shauri hilo litapofikia tamati kwa mahakama kutoa maamuzi yake au DPP  akiona hana haja ya kuendelea na kesi hiyo anaweza kuifuta kesi hiyo chini kifungu cha 91(1) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 2002.
Kwani fursa hiyo ya kujibu mashitaka hayo walinyimwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi,kwani mahakama ya hakimu mkazi haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo.

Kwa tamko hilo la jeshi la polisi kuwa upelelezi umekamilika ni wazi linaweza kuwa funzo pia kwa wale wote wakiwemo baadhi ya wanahabari wenzangu  waliokuwa waikijadili kesi ya Lwakatare nje ya mahakama  kwa kuandika makala na habari zenye mawazo ya kijinga ambayo hayana msingi wowote wa kisheria na yaliyokuwa na lengo la kutaka kuiondoa kesi hiyo ambayo imefunguliwa kwa mujibu wa Sheria za nchi ianze kujadiliwa nje na watu ambao hawana mamlaka ya Kimahakama.

Ni rai yangu kwa wale waandishi wote ambao walikuwa wakiandika makala zao kujadili kesi hiyo na wengine kufikia hatua ya kusema kesi hiyo ni ya kubambika, na wakati wakiandika kuwa kesi hiyo ni ya kubambika utafikiri walikuwa na ushahidi na hilo kumbe hawana , kama ni kweli wanampenda kaka yangu Lwakatare na siyo wanafki na walikuwa na lengo la kuipotisha kesi hiyo , basi wakusanye vielezo vyao vya kuonyesha kesi hiyo ni ya kubambika ili siku kesi hiyo itakapoanza kusikilizwa waje wawe mashahidi wa upande wa washitakiwa na waonyeshe vielelezo hivyo, maana kuzungumza jambo hilo kuwa mshitakiwa fulani amebambikiwa kesi wakati hufanyi jitihada zozote za kufika mahakamani siku ya kesi na kutoa vielelezo, hakutamsaidia mhusika na jamii itakuhesabu kuwa wewe ni mbumbumbu na mnfaki.

Napenda kuwaasa  baadhi ya  wanahabari wenzangu kuwa  tujenge utaratibu wa kuheshimu mgawanyo madaraka, majukumu ya wanataaluma wenye taaluma zingine na kwamba tusikubali kugeuzwa kuwa ‘Microphone Political Party’.  Tusimame kwenye maadili ya taaluma yetu kwaajili ya maslahi ya taifa letu.
Kwani hata nchi nyingi zilizoendelea ,waandishi wa nchi hizo walichangia mchango mkubwa wa taaluma yao katika kusukuma gurudumu la maendeleo. Waandishi wa habari katika nchi hizo zilizoendelea ,baadhi yao wameamua kubobea katika eneo fulani la kuripoti habari fulani.Mfano mwandishi wa habari anayeandika habari za Kitabibu au mazingira, basi mwandishi huyo anakuwa amesomea pia fani za Kitabibu na mazingira, lakini hapa kwetu hali ni tofauti na ndiyo maana kila kukicha baadhi ya waandishi wamekuwa wakiripoti habari zilizopotoshwa.

Wakati ni huu, tuache majungu, kutumiwa na wanasiasa uchwara tena kwa bei rahisi tu na wazi wazi kwa kutupangia tuandike habari hii kwa maslahi yao vyama vyao,majimbo au nyadhifa zao,tujiendeleze kielimu na  tubobee katika kuandika habari ambazo moyo na akili zetu  zinakutuma ujikite huko kwa nia njema.Naamini tufanya hivyo tutakuwa tunalisaidia taifa letu na mungu atalipa dhawabu.

Mwisho nirudie kwa kulipongeza jeshi la polisi kwa kukamilisha upelelezi wa kesi ya Lwakatare haraka, na pia nilitie moyo jeshi la polisi kwa kuendelea kukamilisha upelelezi katika kesi nyingine haraka zinazowakabili washitakiwa wengine wenye kesi mbalimbali kwani nimekuwa nikishuhudia kwa macho yangu ninapokuwa mahakamani naripoti kesi mbalimbali, washitakiwa na mawakili kesi zao zimekuwa zikiarishwa kwa zaidi ya hata mwaka mmoja kwa kile kinachodaiwa na upande wa jamhuri kuwa jeshi la polisi bado halijakamilisha upelelezi.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika.

Chanzo:www.katabazihappy.blogspot.com
 Facebook; happy katabazi ; Jumatano ,Aprili 24 mwaka 2013.



KORTINI KWA KUUZA MAENEO YA WAZI

Na Happiness Katabazi

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU), jana ilimfikisha katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu aliyekuwa  Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke, Steven Kongwa na mwenzake Revecotus Wachawendera, kwa makosa ya kuuza eneo la wazi lililopo eneo la  Mbezi.

Mbele ya Hakimu  Mkazi Agustina Mbando, Mwendesha Mashtaka toka Takukuru,Husein Mussa alidai washitakiwa walitenda kosa hilo kati ya Januari 2000 na Desemba 2001.

 Mussa alidai  washtakiwa hao walitenda kosa hilo wakati Kongwa alipokuwa na wadhifa wa Ofisa Mpimaji Ardhi wa Manispaa ya Jiji la Dar es Salaam na Wachawendera akiwa mpimaji wa ardhi katika Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi.

Alidai kati ya kipindi hicho waligawa bila kufuata taratibu za sheria ya mipango miji Kitalu namba 1/851 na kitalu namba 1/597 Block “L” eneo ambalo lilitengwa kwa ajili ya bustani.

Alilitaja kosa jingine ni la  kushindwa kutimiza wajibu wao kinyume na sheria, hivyo kama wapimaji ardhi kwa pamoja walikiuka sheria ya mipango miji kwa kugawa eneo hilo.

Hata hivyo washitakiwa hao walikana mashitaka na hakimu aliwapatia masharti ya adhamana ambayo waliyatimiza na akaairisha kesi hiyo Mei 20 mwaka huu itakapokuja kwaajili ya kutajwa.

Chanzo:www.katabazihappy.blogspot.com; Aprili 24 mwaka 2013.

GODBLESS LEMA AIBWAGA TENA CCM





Na Happiness Katabazi

Dar es Salaam. Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema ameibuka kidedea baada ya Mahakama ya Rufani kutupilia mbali maombi ya marejeo ya rufaa iliyomrejesha bungeni.

Maombi hayo yaliwasilishwa mahakamani hapo na makada watatu wa CCM mkoani Arusha, kupitia kwa Mawakili wao Alute Mughway na Modest Akida wakiiomba Mahakama ya Rufani ifanye marejeo ya hukumu yake hiyo kwa madai kuwa hukumu hiyo haikuwa sahihi.
Hata hivyo, jana Mahakama ya Rufani ilisikiliza maombi hayo kutoka kwa waombaji pamoja na hoja za wajibu maombi na kisha kutupilia mbali maombi hayo ikisema kuwa hayana msingi.
Uamuzi huo wa kutupilia mbali maombi hayo ulisomwa na Jaji Bernard Luanda, kwa niaba ya jopo la majaji wenzake lililokuwa likiongozwa na Engela Kileo na Salum Massati.
Hata hivyo, jopo hilo halikutoa sababu za kutupilia mbali maombi hayo na badala yake lilisema litatoa maelezo ya kina baadaye.
Majaji hao isipokuwa Kileo ndiyo waliosikiliza na kutoa hukumu ya rufaa iliyomrejesha Lema bungeni, ambayo ilikuwa inapingwa na makada hao wa CCM.
Awali, kabla ya kutupilia maombi hayo ya marejeo, mahakama hiyo ilitupilia mbali maombi ya waombaji hao kutaka suala hilo lisikilizwe na jopo la majaji saba.
Wakili Mughwai aliwasilisha maombi katika Mahakama ya Rufani akiomba marejeo ya rufaa yahamishwe katika jopo la majaji watatu na kupelekwa kusikilizwa na jopo la majaji saba kwa madai kuwa kuna jambo linatakiwa kushughulikiwa kutokana na mazingira yake.

Wakili wa Lema, Methods Kimomogoro alidai kuwa Wakili Mughwai amechanganya maombi hivyo kuleta utata na kwamba kama alikuwa akitaka yasikilizwe angeyapeleka katika utaratibu ulio sahihi.

“Kanuni ya Nne ya Mahakama ya Rufaa, inasema hakuna kanuni rasmi inayowezesha jopo hili kuhamisha maombi ya marejeo kwenda kwenye jopo la majaji saba kwa ajili ya mapitio,” alisema Kimomogoro na kuongeza:“Labda kama maombi ya mapitio yangekubaliwa, wangekwenda hatua ya pili ya kuomba jopo la majaji saba.

Maombi haya hayajafuata utaratibu hivyo naomba Mahakama iyatupilie mbali kwa kuwa sababu za kisheria hazikidhi na Mahakama haina uwezo wa kuyatolea uamuzi.”

Wakili wa Serikali, Vicent Tangoh alimuunga mkono Kimomogoro na kuongeza kuwa hiyo inaonyesha hakuna maombi yoyote mbele ya Mahakama wala kitu cha kupeleka katika jopo la majaji saba.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Aprili 23 mwaka 2013.

DOSARI ZA KWAMISHA RUFAA YA DPP DHIDI YA ZOMBE




Na Happiness Katabazi

MAHAKAMA ya Rufaa nchini, jana ilijikuta ikishindwa kuanza kusikiliza rufaa iliyokatwa na Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP)-Dk.Eliezer Feleshi dhidi ya Aliyekuwa Mkuu wa upelelezi wa mkoa wa Dar es Salaam(ACP)-Abdallah Zombe na wenzake baada ya mahakama hiyo kubaini dosari katika hati ya kukata rufaa.

Rufaa hiyo Na.254/2009 inayosikilizwa na jopo la majaji watatu Edward Rutakangwa,Mbarouk Mbarouk na  Bethek aMila, ambayo jana ilikuja kwaajili ya kuanza kusikilizwa kwa siku mbili mfululizo , jaji Mbarouk kabla ya kuanza kusikiliza hoja za rufaa hiyo aliutaka upande wa mwomba rufaa(DPP), wameiweke sawa mahakama kuwa katika hati ya kukata rufaa ya ya kupinga hukumu ya mahakama kuu ya kesi ya mauji Na.26/2006 ya Zombe na wenzake inasomeka kuwa hukumu ya mahakama kuu iliyotolewa na Jaji wa mahakama ya rufaa   Salum Massati.

“Hebu mawakili wa mwomba rufaa ebu mtufafanulie hili, hati  yenu ya kukata rufaa inasema hukumu ya mahakama kuu ilitolewa na jaji wa mahakama ya rufaa (Massati)…sasa kama hukumu hii ilitolewa na jaji wa mahakama ya rufaa ebu tuwalize sasa nyie waomba rufaa, michokileta hapa mbele yetu ni ombi la mapitio, marejeo au?Maana majaji wa mahakama ya rufaa hawawezi kusikiliza rufaa inayotokana na hukumu iliyotolewa na jaji mwenzao wa mahakama ya rufaa, tunachokifanya ni kufanya marejo au mapitio;

“Jicho la mahakama limeona ni kama   hakuna rufaa mbele yake kwani  rufaa ya kesi ya jinai ni lazima iwe na hati ya kukata rufaa kwa mujibu wa Kanuni ya 68(1) cha Mahakama ya Rufaa’ nakuongeza kuwa kwa dosari hiyo mahakama inaona nikama hakuna rufaa iliyokatwa dhidi ya zombe na wenzake”alisema Jaji Mbarouk.

Jaji Rutakangwa aliwataka mawakili wanaomwakili DPP wajipe muda na wasome vizuri Ibara ya 119 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 ambayo inasomeka kama ifuatavyo:
“Jaji yoyote  wa Mahahakama ya Rufani hatakuwa na mamlaka  ya kusikiliza shauri lolote katika Mahakama Kuu  au katika mahakama ya hakimu  ya ngazi yoyote.:

“Isipokuwa kwamba iwapo jaji yeyote wa mahakama kuu atateuliwa  kuwa Jaji Mahakama ya rufaa, basi hata baaa ya kuteuliwa kwake kuwa jaji wa mahakama ya rufani,jaji huyo  aweza kuendelea kufanyakazi kazi zake katika mahakama kuu mpaka amalize  kutayarisha  na kutoa hukumu  au mpaka akamilishe shughuli nyingine yoyote  inayohusika na mashauri  ambayo yalikwisha anza kuyasikiliza kabla kabla  hajateuliwa  kuwa jaji  wa mahakama rufani, na kwamba ajili hivyo itakuwa  halali kwake  kutoa hukumu  au uamuzi  mwingine wowote unaohusika kwa kutumia  kutumia au  kutaja madaraka  aliyoshika kabla  ya kutueliwa  kuwa jaji wa mahakama ya rufani,  lakini endapo hatimaye hukumu hiyo au uamuzi  mwingine utapingwa kwa njia  ya rufaa itayofikishwa mbele ya  mahakama ya rufani,basi katika hali  hiyo jaji  huyo  wa mahakama ya rufani,hatakuwa  na mamlakaya kusikiliza  rufaa hiyo:inasomeka ibara hiyo.

Alisema mawakili wa mwomba rufaa walipaswa katika hati yao ya kukata rufaa waandike jaji Jaji Masati ambaye zamani alikuwa ni jaji wa mahakama kuu na sikuandika jaji wa mahakama ya rufaa.

Akijitetea mawakili wakuu wa serikali wanaomwakilisha DPP, Vitalis Timon, Prudence Rweyongeza, Mgaya Mtaki, Alexander Mzikila, Edwin Kakoraki alikiri dosari hiyo na akaomba mahakama hiyo iwapatie ruhusa ya kwenda kufanyia marekebisho dosari hiyo chini ya Kanuni ya 4(2),(2),(b) ya Sheria ya Mahakama ya Rufaa na kwamba hata jana walikuwa wapo tayari kufanyia marekebisho hati hiyo ya kukata rufaa ambayo jicho la mahakama limeona ina dosari na kisha  jana hiyo hiyo kuirejesha upya mahakamani.

Hata hivyo mawakili wa wajibu rufaa Richard Rweyongeza, Majura Magafu, Denis Msafiri  walianza kwa kuishukuru mahakama kuwa jicho mahakama limeweza kubaini dosari hiyo na kwamba kwa dosari hiyo ni kwamba hakuna hati ya rufaa mbele ya mahakama hiyo na kwamba akaiomba mahakama ikatae kuwapa muda wa kufanyia marekebisho kwani tayari muda wa kukata rufaa umeishapita na kwamba kama wanataka kukata rufaa watalazimika kuwasilisha ombi la kuongezewa muda ambao ni siku 30 chini ya kanuni ya 68(1) ya Mahakama ya Rufaa.

‘Kwa sababu jicho la mahakama limeona dosari hiyo  sisi wajibu rufaa tunaomba mahakama iitupilie mbali rufaa hiyo kwani katika kesi za jinai kama hakuna hati ya kiapo ni wazi hakuna rufaa mahakamani iliyowasilishwa na DPP’alidai wakili Magafu.


Akijibu hoja hiyo wakili Vitalis alidai Kanuni ya 4(2),(a),(b) ya Mahakama ya Rufaa inaipa mamlaka kutoa amri ya kuwaruhusu kwenda kufanyia marekebisho hati hiyo ila wanakiri ni kweli hati yao yao waliyoitumia kukata rufaa ina mapungufu hayo.

Kwa upande wake jaji Rutakangwa alisema amezikilza hoja za pande zote mbili ni nzito na zina mvuto na kwamba jopo linaomba lipewe muda wa kwenda kuandaa uamuzi wake na kwamba uamuzi wao utakapokuwa tayari watazijulisha.  

Agosti 17  mwaka 2009, Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, ilitoa hukumu ya kihistoria ya kesi ya mauji ya watu wanne iliyokuwa ikimkabili Zombe na wenzake ambapo jaji Salum Massati ambaye hivi sasa ni jaji wa mahakama ya rufani aliwaachilia huru Zombe na wenzake ambao walikuwa wakikabiliwa na kesi hiyo kwa maelezo kuwa upande wa jamhuri ulishindwa kuleta ushahidi mzuri ambao ungewea kuishawishi mahakama hiyo iwaone washtakiwa hao wana hatia.


Baada ya hukumu hiyo ya mahakama kuu, DPP hakulidhishwa na hukumu hiyo Oktoba 7 mwaka 2009 akakata rufaa Mahakama ya Rufaa ,  kupinga hukumu hiyo ambayo kwa mujibu wa ratiba ya vikao vya mahakama ya rufaa,rufaa hiyo ilikuwa imepangwa kuanza kusikilizwa jana lakini ikashindikana.

Mbali na Zombe, washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni Christopher Bageni, Ahmed Makele, WP 4593 PC Jane Andrew, D 1406 Koplo Emmanuel Mabula, D 8289 DC Michael Shonza, D. 2300 Abeneth Saro, D.4656D/Koplo Rajabu Bakari na D.1317D/XP Festus Gwasabi na jana washtakiwa wote walifika mahakamani hapo.

Washitakiwa hao walidaiwa kuwa Januari 14, mwaka 2006 waliwaua wafanyabiashara watatu wa madini wa wilayani Ulanga, mkoani Morogoro; Ephraim Chigumbi, Sabinus Chigumbi na Mathias Lukombe pamoja na dereva teski Juma Ndugu, mkazi wa Dar es Salaam kwa madai kuwa walikuwa majambazi.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Aprili 23 mwaka 2013.

RUFAA YA DDP V ZOMBE KUANZA LEO




Na Happiness Katabazi
 
MAHAKAMA ya Rufaa nchini leo inatarajia kuketi Dar es Salaam na kuaza kusikiliza  rufaa iliyokatwa na   Mkurugenzi wa Mashtaka(DPP), Dk.Eliezer Feleshi dhidi ya aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Dar es Salaam (ACP), Abdallah Zombe na wenzake na kupinga hukumu iliyotolewa na Mahakama Kuu  katika kesi ya mauji Na.26/2006 ambayo iliwaachiria huru Zombe na wenzake.

Kwa mujibu wa ratiba ya vikao vya mahakama ya rufaa  ambayo gazeti hili imeona nakala ya ratiba hiyo, inaonyesha rufaa hiyo inayosubiriwa kwa shauku kubwa na umma itasikilizwa kwa siku mbili mfululizo yaani leo na kesho.

Rufaa hiyo itasikilizwa mbele ya majaji wa tatu wanaongozwa na Jaji Natharia Kimaro,Catherine Oriyo na Semistocles Kaijage.

Upande wa mwomba rufaa(DPP), unawakilishwa na jopo la mawakili waandamizi wa serikali saba ambao ni Mgaya Mtaki, Timon Vitalis,Edward Kakolaki, Angaza Mwipopo, Prudence  Rwenyongeza ,Alexanda Mzikila na Peter Njike .

Wakati upande wa wajibu rufaa unawakilishwa na mawakili wa kujitegemea Richard Rweyongeza na washtakiwa wengine wanatetewa na mawakili Majura Magafu, Denis Msafiri, Deodoras Ishengoma

Itakumbukwa kuwa Desemba 12 mwaka jana,rufaa ilikuja kwaajili ya kuanza kusikilizwa lakini ilishindikana kuanza kusikilizwa kwasababu Jaji Kaijage alikuwa mgonjwa.

Agosti 17  mwaka 2009, Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, ilitoa hukumu ya kihistoria ya kesi ya mauji ya watu wanne iliyokuwa ikimkabili Zombe na wenzake ambapo jaji Salum Massati ambaye hivi sasa ni jaji wa mahakama ya rufani aliwaachilia huru Zombe na wenzake ambao walikuwa wakikabiliwa na kesi hiyo kwa maelezo kuwa upande wa jamhuri ulishindwa kuleta ushahidi mzuri ambao ungewea kuishawishi mahakama hiyo iwaone washtakiwa hao wana hatia.


Baada ya hukumu hiyo ya mahakama kuu, DPP hakulidhishwa na hukumu hiyo Oktoba 7 mwaka 2009 akakata rufaa Mahakama ya Rufaa ,  kupinga hukumu hiyo ambayo kwa mujibu wa ratiba ya vikao vya mahakama ya rufaa,rufaa hiyo ilikuwa imepangwa kuanza kusikilizwa jana lakini ikashindikana.

Mbali na Zombe, washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni Christopher Bageni, Ahmed Makele, WP 4593 PC Jane Andrew, D 1406 Koplo Emmanuel Mabula, D 8289 DC Michael Shonza, D. 2300 Abeneth Saro, D.4656D/Koplo Rajabu Bakari na D.1317D/XP Festus Gwasabi na jana washtakiwa wote walifika mahakamani hapo.

Washitakiwa hao walidaiwa kuwa Januari 14, mwaka 2006 waliwaua wafanyabiashara watatu wa madini wa wilayani Ulanga, mkoani Morogoro; Ephraim Chigumbi, Sabinus Chigumbi na Mathias Lukombe pamoja na dereva teski Juma Ndugu, mkazi wa Dar es Salaam kwa madai kuwa walikuwa majambazi.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumatatu, Aprili 22 mwaka 2013.

MAUJI,MAUAJI JAMANI

Watanzania huyu ni binadamu mwenzetu ambaye leo alfajiri ya kuamkia leo Aprili 20 amekutwa na mauti.Sisi wakazi wa Mtaa wa Sinza 'C' eneo la Ukuta wa Posta maarufu kama ukuta wa Kesi ya Abdallah Zombe, leo saa 11 alfajiri tulijikuta tukiamkia kuona mwili wa marehemu huyo ukivuja damu katikati ya barabara na ukiwa umelazwa chini baada ya kuua na watu wasiyojulikana.Nikiwa kama raia mwema na Mwandishi wa habari baada yakufika eneo hilo la tukio nilichofanya nikumpigia Simu mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Ilala,ACP-Duwani Nyanda na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, ACP- Charles Kenyela kuwapa taarifa na kweli baada ya muda mchache waliwaagiza askari wao wakafika eneo la tukio na kuuchukua mwili huo ambao ulikuwa unavuja damu.Inasikitisha sana, na inaendelea kudhiirisha kuwa baadhi ya watanzania hivi sasa wamezidi kuwa na roho katili na hawana hofu ya mungu.(Picha na Happiness Katabazi)
Chanzo:www.katabazihappy.blogspot.com
Facebook:happy katabazi
Aprili 20 mwaka 2013.

HUKUMU YA KESI YA PONDA YAOTA MBAWA




Na Happiness Katabazi

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, jana ilishindwa kutoa hukumu ya kesi ya uchochezi na wizi wa malighafi zenye thamani ya Sh.milioni 59 inayomkabili Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu na wenzake 49 kwa maelezo kuwa hakimu aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo Victoria Nongwa hayupo na wala hajaituma hukumu hiyo kwa uongozi wa mahakama.

Hakimu Mkazi Alocye Katemana ndiye aliyeairisha kesi hiyo ambapo alianza kwa kusema kesi hiyo jana ilikuja kwaajili ya kutolewa hukumu, lakini hukumu hiyo haitatolewa kwasababu hakimu anayesikkiliza kesi hiyo hayupo na wala hajatuma hukumu ya kesi hiyo.

‘Kwa sababu hiyo naairisha kesi hii hadi Mei 2 itakapokuja kwaajili ya kutajwa na kwamba Mei 9 mwaka huu, itakuja kwaajili ya kutolewa hukumu na hivyo kuamuru mshitakiwa wa kwanza na watano(Ponda na Mukadamu Swalehe) kurudishwa rumande kwasababu hadi sasa Mkurugenzi wa Mashitaka(DPP).Dk.Elizer Feleshi ajaondoa hati yake ya kuwafungia dhamana.

Mwandishi wa habari hizi ambaye alifika mahakamani hapo tangu saa moja asubuhi ,alishuhudia kundi la watu zaidi ya mia moja wakiwa wamesimama nje ya uzio wa mahakama hiyo karibu na ofisi ya Maktaba ya Taifa tayari wakisubiri kuingia ndani ya geti la mahakama hiyo kwaajili ya kukaguliwa kwa vifaa maalum na wanausalama  ambapo hata hivyo waliruhusiwa na kuingia ndani ya viwanja vya mahakama, lakini ni wafuasi wachache ndiyo walioruhusiwa ndani ya chumba cha wazi Na. mbili cha mahakama hiyo kwaajili ya kusikiliza kesi hiyo.

Baada ya kuarishwa kesi hiyo askari magreza waliondoka na msafara wa magari yao ambao ulikuwa ukiongozwa na askari polisi waliokuwa wamevalia sare na wale ambao hawajavalia sare za jeshi hilo, na wakati wakitoka ndani ya viwanja hivyo tayari kwaajili ya kuelekea katika gereza la Segerea anapoishi Ponda na Mukadamu ,wafuasi hao walianza kupaza sauti huku wakimpungia mkono Ponda na kusema ‘ Takbirii Abkbaru ’.

Aprili 3 mwaka huu:Mawakili wa upande wa Jamhuri ,Tumaini Kweka na Jessy Peter na mawakili wa utetezi Juma Nassor na Njama waliwasilisha majumuisho yao mahakamani hapo kwa njia ya maandishi ambapo mawakili wa upande wa jamhuri waliiomba mahakama iwaone washitakiwa wote wana hatia na wapewe adhabu kwa mujibu wa sheria.

Wakati mawakili wa utetezi waliiomba mahakama iwaone washitakiwa hawana hatia na iwaachilie huru kwa sababu hawakutenda  makosa yanayowakabili na kwamba upande wa jamhuri umeshindwa kuthibitisha kesi yao.

Machi 21 mwaka huu;Sheik Ponda, mshitakiwa wa tano Mukadamu Swaleh walijitetea.Na washitakiwa wenzake wa nne nao walijitetea siku hiyo na hivyo kufanya jumla ya washitakiwa 48 wa kesi hiyo kumaliza kutoa utetezi wao.Na siku hii ndipo upande wa utetezi walifunga utetezi wao na Hakimu Nongwa aliipanga tarehe ya jana ndiyo angetoa hukumu ya kesi hiyo.

Machi 4 mwaka huu:  Hakimu Nongwa atoa uamuzi wake ambapo aliwaona washitakiwa wote wana kesi ya kujibu na akatupilia mbali hoja ya mawakili wa utetezi iliyokuwa ikidai kesi hiyo ni ya madai na kwamba ifutwe.

Oktoba 18 mwaka jana, Ponda na wenzake walifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza ambapo wakili mwandamizi wa serikali Tumaini Kweka alidai washitakiwa hao wanakabiliwa na makosa matano na makosa hayo ni kama yafuatayo.
shitaka la kwanza ni la kula njama kinyume na kifungu 384 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu ya mwaka 2012,kwamba Oktoba 12 mwaka huu, huko eneo la Chang’ombe Markasi washitakiwa wote walikula  kwa nia ya kutenda kosa hilo.

Shitaka la pili wakili Kweka alidai linawakabili washitakiwa wote ambalo ni la kuingia kwa nguvu  kwa nia ya kutenda kosa  kinyume na kiufungu cha 85 na 35 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu  na kwamba  Oktoba 12 mwaka huu,  huko Chang’ombe  Markasi , kwa jinai  wasipokuwa na sababu  za msingi  washitakiwa hao waliingia  kwenye kiwanja kinachomilikiwa kampuni ya AgriTanzania  Ltd  kwania ya kujimilikisha  kiwanja hicho isivyo halali.

Kabla ya washitakiwa hakubali au kataa shitala hilo Ponda aliripoka na kusema yeye anakanusha shitaka hilo na kwamba washitakiwa wenzake nao wanalikanusha shitaka hilo,jambo ambalo lilikataliwa na Hakimu Sanga ambaye alimrisha kila mshitakiwa ajibu shitaka hilo kwa kinywa chake ambapo kila mshitakiwa kwa kinywa chake alikanusha shitaka hilo kinyume na alivyokuwa anataka Ponda iwe kwa yeye kukanusha shitaka hilo kwa niaba ya wenzake.

Wakili Kweka alilitaja shitaka la tatu kuwa ni  kujimilikisha  kiwanja kwa jinai kinyume na kifungu cha 86 na 35 cha sheria hiyo  na kwamba kati ya Oktoba 12-16 mwaka huu huko Chang’ambe  Markasi  pasipo na uhalali wowote washitakiwa wote  katika hali  iliyokuwa ikipelekea  uvunjifu wa amani  walijimilikisha  kwa nguvu ardhi  ya  kampuni ya Agritanza Ltd.

Shitaka la nne, wakili Kweka alidai ni la wizi  ambalo ni kinyume na kifungu cha 258  cha sheria ya Kanuni ya Adhabu ya mwaka 2002, na kuwa kati ya Oktoba 12-16 mwaka huu,  washitakiwa hao waliiba vifaa na malighafi,matofali 1500,nondo,Tani 36 za Kokoto vitu vyote hivyo vikiwa na thamani ya Sh 59,650,000 mali ya kampuni ya Agritanza Ltd.

Aidha shitaka la tano Kweka alidai ni la uchochezi ambalo linamkabili Sheikh Ponda peke yake  ambalo ni kinyume na kifungu cha 390 na 35 cha sheria hiyo  kwamba kati ya Oktoba 12-16 mwaka huu katika eneo hilo la Chang’ombe Markasi  kwa maelezo kuwa yeye ni Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu(T) aliwashawishi  wafuasi wake ambao ni washitakiwa hao  kutenda makosa hayo  na kwamba upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.

“Mheshimiwa hakimu pamoja na kuwasomea mashitaka hayo ambayo yanadhamana kwa mujibu wa sheria, Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), Dk.Elizer Feleshi kwa mkono wake amenituma kuwasilisha kwaniaba yake mahakamani hapo hati ya kufunga dhamana kwa mshitakiwa wa kwanza (Ponda) peke yake chini ya kifungu cha  148(4) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 2012’alidai wakili Kweka.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Aprili 18 mwaka 2013.

MWANZO,MWISHO KESI YA SHEIKH PONDA HUU HAPA




*HUKUMU YA PONDA NI LEO APRILI 18

Na Happiness Katabazi

FUATANA na mwandishi wa makala haya   Happiness Katabazi ambaye ni mwandishi wa habari za mahakamani hapa nchini, ili uweze kufahamu kesi ya uchochezi na wizi wa malighafi zenye thamani ya Sh.milioni 59 inayomkabili Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, Sheikh Ponda Issa Ponda na wenzake 48, ilipofunguliwa hadi  kesho (Aprili 18) inapofikia hatua ya mwisho kutolewa hukumu.

Mimi na miongoni mwa waandishi wenzangu wa chache ambao mungu alitujalia uzima na afya njema ambapo tuliweza kuifuatilia kesi hii tangu ilipofunguliwa rasmi mahakamani hapo Oktoba 18 mwaka jana hadi kesho inapomalizika ,tuliweza kujifunza mambo mengi  ambayo yametupa faida sisi binafsi ikiwemo faida ya kufahamu vyema jinsi ya aina ya kesi hii iliyohusisha washitakiwa wengi ilivyoweza kuendeshwa na mawakili wa serikali na utetezi na hakimu na wana usalama pia.

Kwani kesi hii ya Ponda tangu ilipofunguliwa hadi kesho inatolewa hukumu, imekuwa ikiendeshwa chini ya ulinzi mkali unaoratibiwa na wana usalama toka vyombo vya ulinzi na usalama kwa njia zinaonekana na sizoonekana kwa urahisi.

Tunawashukuru wana usalama wote walioendesha ulinzi siku ya kesi hii kwani walituwezesha hata sisi waandishi wa habari za mahakamani kufanyakazi yetu kwa amani na uhuru licha hapo mwanzo tulikuwa tukipokea vitisho kutoka kwa baadhi ya washitakiwa.

Aprili 18 mwaka huu; Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi  Kisutu, Victoria Nongwa ,anatarajiwa kuketi katika kiti cha enzi na kutoa hukumu ya kesi hiyo Na.245/2012 inayomkabili Ponda na wenzake.

Aprili 3 mwaka huu:Mawakili wa upande wa Jamhuri ,Tumaini Kweka na Jessy Peter na mawakili wa utetezi Juma Nassor na Njama waliwasilisha majumuisho yao mahakamani hapo kwa njia ya maandishi ambapo mawakili wa upande wa jamhuri waliiomba mahakama iwaone washitakiwa wote wana hatia na wapewe adhabu kwa mujibu wa sheria.

Wakati mawakili wa utetezi waliiomba mahakama iwaone washitakiwa hawana hatia na iwaachilie huru kwa sababu hawakutenda  makosa yanayowakabili na kwamba upande wa jamhuri umeshindwa kuthibitisha kesi yao.

Machi 21 mwaka huu;Sheik Ponda, mshitakiwa wa tano Mukadamu Swaleh walijitetea.Na washitakiwa wenzake wa nne nao walijitetea siku hiyo na hivyo kufanya jumla ya washitakiwa 48 wa kesi hiyo kumaliza kutoa utetezi wao.Na siku hii ndipo upande wa utetezi walifunga utetezi wao.

Machi 4 mwaka huu:  Hakimu Nongwa atoa uamuzi wake ambapo aliwaona washitakiwa wote wana kesi ya kujibu na akatupilia mbali hoja ya mawakili wa utetezi iliyokuwa ikidai kesi hiyo ni ya madai na kwamba ifutwe.

Machi 6 mwaka huu:Washitakiwa kesi ya sheikh Ponda waanza kujitetea mfululizo.Ambapo siku hiyu jumla ya washitakiwa saba walijitetea.

Machi 7 mwaka huu: Jumla ya washitakiwa saba walijitetea.

Machi 11 mwaka huu:Jumla ya washitakiwa saba walijitetea.Hivyo hadi kufikia siku hiyo jumla ya washitakiwa saba walikuwa wameishajitetea.

Machi 12 mwaka huu: Washitakiwa watatu tu ndiyo walitoa utetezi siku hiyo na kufanya jumla ya washitakiwa waliotoa utetezi wao kufikia 27.

Februali 18 mwaka huu: Mawakili wa pande zote mbili wawasilisha kwa njia ya mdomo.Wakili wa upande wa Jamhuri Tumaini Kweka awasilisha aiomba mahakama iwaone washitakiwa wote wana kesi ya kujibu kwasababu upande wa jamhuri umeweza kuithibitisha kesi yake.

Na mawakili wa utetezi nao waliomba mahakama iwaone washitakiwa hawana kesi ya kujibu kwasababu jamhuri imeshindwa kuthibitisha kesi yao na kwamba kesi hiyo ni ya madai ambayo inahusisha mgogoro wa ardhi hivyo ifutwe.

Februali 25 mwaka huu: upande wa jamhuri uliifunga kesi yake baada ya mashahidi  wake wa tatu kumaliza kutoa ushahidi wao.Ambao ni shahidi wa 17,  D/C F8586 Ismail wa kituo cha Polisi Chang’ombe, shahidi wa 15 ambaye ni F3929 D/C ,Constebo Eliaeli (35) ,shahidi wa 16 ambaye ni Stationi Sajenti  Amos wa kituo cha Polisi Kati . Hivyo kufanya upande wa jamhuri kuwa umeleta jumla ya mashahidi 17 na wakatoa ushahidi na ulileta jumla ya vielelezo 13.

Februali 22 mwaka huu: shahidi 12,13 wa upande wa jamhuri watoa ushahidi wao. Shahidi wa  13, Koplo Masiku ambaye ni Askari kituo cha polisi Chang’ombe ,shahidi wa 14 wa upande wa Jamhuri D/C Koplo Zakayo.

Februali 21 mwaka huu; Shahidi wa 12 ambaye ni Mkuu wa  upelelezi wa Makosa ya Jinai wa Mkoa wa Kipolisi Temeke(RCO), Ame Anange Anoqie alitoa ushahidi wake ambapo alisisitiza kuwa  Ponda na wenzake  siyo wamiliki halali wa kiwanja cha Chang’mbe Markas na kwamba waliingia kwa jinai katika kiwanja hicho.

Februali 20 mwaka huu: Shahidi wa 11 wa upande wa jamhuri amabye ni Mpelelezi Mkuu wa kesi hiyo, Inspekta Thobias Walelo (34), ambaye alitoa vielelezo vilivyopokelewa na mahakama kama kielelezo cha nane  ambapo ni mapanga, Jambia, mabango,vipaza sauti,masufulia ,majenereta  alieleza kuwa baada ya kuwakamata washitakiwa hao wakiwa na majambia, visu, vipaza sauti, viloba viwili vya unga wa sembe, mikeka,mabango, visu,sufulia ,ndoo za plastiki.

Walelo alidai kuwa yeye akiwa ni mpelelezi mkuu wa kesi hiyo yeye na askari wenzake walioenda kuwakamata washitakiwa hao   waliamua kuwabeba washtakiwa hao kwenye magari ya polisi kwa awamu mbili na kisha kuwapeleka katika kituo cha polisi Kijitonyama ambapo waliwafikisha saa 12 asubuhi na kuanza kuwahoji ambapo waliwahoji hadi Oktoba 18 mwaka jana , washitakiwa hao walifikishwa kwa mara ya kwanza mahakamani hapo wakikabiliwa na kesi.

Februali 19 mwaka huu: Mahakama ya imetupilia mbali pingamizi la mawakili wa upande wa utetezi lilokuwa linataka mahakama hiyo isipokee  kama kielelezo maelezo ya ungamo yaliyotolewa na mshitakiwa  wa tano katika kesi hiyo Mkadamu Swaleh Abdallah,polisi  kama kielelezo.Uamuzi huo ulitokana baada ya kufanyika kesi ndogo(Trial within a Trial),baada ya mawakili wa utetezi kutaka maelezo ya onyo ya Mukadamu yasipokelewe kama kielelezo kwasababu maelezo hayo si yake.

Februali 18: Shahidi wa  nane, D/c-Sajenti Mkombozi Mhando   alidai kuwa  Novemba 11 mwaka jana, alikuwa Kituo Kikuu cha Polisi Kati akiwa na timu ya wapelelezi wenzake toka Temeke yeye alipewa jukumu la kumhoji mshitakiwa wa tano, Mukadam abdallah Swaleh ambapo alimpa haki zake zote.

Na kuanzia leo hadi leo hukumu inamalizika ulinzi ulikuwa ni waina yake wakati kesi ilipokuja ikija mahakamani kwaajili ya kutajwa na kusikilizwa.Ulinzi wa kesi hii ulikuwa ni waina yake ukilinganisha na ulinzi unaotolewa wakati wa kesi nyingine kwani kesi hii wana usalama uweka vifaa maalum katika ofisi za mapokezi  ya mahakama kwaajili ya kuwakagua watu wanaoingia.

Februali 28 mwaka huu;shahidi wa sita ambaye ni fundi  mwashi Hamis Salum Mkangama(30), Shahidi wa saba,  William Milanzi(43) wa upande wa jamhuri walitoa ushahidi wao.
Januari 17 mwaka huu:  shahidi wa nne   Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini la (BAKWATA),Masoud Ikome(72),  amedai kuwa kiwanja kilichopo Chang’ombe Markas  ni mali halali ya kampuni ya Agritanza Ltd na siyo mali waislamu(Bakwata).

Shahidi  wa tano ambaye ni miongoni mwa Wakurugenzi wa Kampuni ya Agritanza Ltd, Afidhi Seif  Othman (42),  aliambia mahakama kampuni yake ya Agritanza Ltd ilibadilisha eneo la Chang’ombe na Bakwata na kwamba yeye ndiye alikuwa mmiliki wa eneo la Kisarawe na ndiye aliyeipatia Bakwata eneo hilo na Bakwata ikawapatia eneo la Chang’ombe na kwamba mabadilishano hayo yalifanyika Oktoba 10 mwaka 2010.

Desemba 18 mwaka 2012: Ponda anaishi gereza la Segerea,alishindwa kuletwa mahakamani hapo ambapo kesi yake ilikuja kwaajili ya kutajwa kwasababu wakili Kweka alidai amepokea taarifa toka kwa maofisa wa jeshi la Magereza kuwa Ponda ni mgonjwa.
Novemba 29 mwaka 2012: Shahidi wa kwanza  Katibu Mkuu wa Bakwata, Suleman Said Lolila(61),amekanusha madai yaliyotolewa na Sheikh  Ponda na wenzake kuwa Bakwata siyo chombo cha kuwakilisha waislamu wote hapa nchini.Na siku hii ndiyo ilikuwa ni siku ya kwanza mashahidi wa upande wa jamhuri kuanza kutoa ushahidi wake.

Novemba 15 mwaka 2012: Wakili  wa upande wa Jamhuri Tumaini Kweka  aliwasomea maelezo ya awali washtakiwa hao ambapo alidai Bakwata ni chombo ambacho kinawawakilisha waislamu wote, lakini Ponda na wenzake walikanusha madai yao na kusema kuwa Bakwata haipo kwaajili ya kuwawakilisha waislamu wote.

Novemba 8 mwaka 2012: Mukadamu Swalehe aunganishwa kwenye kesi hii Na.245/2012 inayomkabili Ponda na wenzake na hivyo kufanya sasa jumla washitakiwa kuwa ni 51.Na Mukadamu amekuwa ni mshitakiwa wa tano.

Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), Dk.Elezer Feleshi aliwasilisha mahakamani hapo hati ya kumfungua dhamana Mukadamu kwaajili ya maslahi ya taifa chini ya kifungu cha 148(4) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 2002.

Kwa upande wake hakimu Nongwa alisema makosa yanayomkabili mshtakiwa huyo yana dhamana ila kwakuw DPP-Feleshi amewasilisha hati ya kumfungia dhamana, mahakama imefungwa mikono,haiwezi kutoa dhamana kwasababu sheria iliyotumiwa na DPP kumfungia dhamana mshtakiwa huyo na Ponda zimetungwa na Bunge, mahakama yenye ipo kwaajili ya kuzifuata sheria hizo zilizotungwa na bunge katika kutoa uamuzi hivyo akaamuru mshitakiwa huyo amepelekwe gerezani.

Pia siku hiyo hakimu Nongwa aliwapatia dhamana washitakiwa wote dhamana isipokuwa Ponda na Mukadamu kwasababu DPP alikuwa amewasilisha hati ya kufunga dhamana ya washitakiwa hao wawili.

Na hadi kesi hii inamalizika kesho,washitakiwa hao wawili bado wanaendelea kuishi katika gereza la Segerea kwasababu dhamana yao imefungwa na DPP tangu siku ya kwanza walipofikishwa mahakamani hapo.

Oktoba 18 mwaka 2012: Ponda na wenzake walifikishwa kwa mara ya kwanza mahakamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi Stewart Sanga, ambapo wakili mwandamizi wa serikali Tumaini Kweka  alidai  shitaka la kwanza ni la kula njama kinyume na kifungu 384 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu ya mwaka 2012,kwamba Oktoba 12 mwaka huu, huko eneo la Chang’ombe Markasi washitakiwa wote walikula  kwa nia ya kutenda kosa hilo.

Shitaka la pili wakili Kweka alidai linawakabili washitakiwa wote ambalo ni la kuingia kwa nguvu  kwa nia ya kutenda kosa  kinyume na kiufungu cha 85 na 35 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu  na kwamba  Oktoba 12 mwaka huu,  huko Chang’ombe  Markasi , kwa jinai  wasipokuwa na sababu  za msingi  washitakiwa hao waliingia  kwenye kiwanja kinachomilikiwa kampuni ya AgriTanzania  Ltd  kwania ya kujimilikisha  kiwanja hicho isivyo halali.

Kabla ya washitakiwa hakubali au kataa shitala hilo Ponda aliripoka na kusema yeye anakanusha shitaka hilo na kwamba washitakiwa wenzake nao wanalikanusha shitaka hilo,jambo ambalo lilikataliwa na Hakimu Sanga ambaye alimrisha kila mshitakiwa ajibu shitaka hilo kwa kinywa chake ambapo kila mshitakiwa kwa kinywa chake alikanusha shitaka hilo kinyume na alivyokuwa anataka Ponda iwe kwa yeye kukanusha shitaka hilo kwa niaba ya wenzake.

Wakili Kweka alilitaja shitaka la tatu kuwa ni  kujimilikisha  kiwanja kwa jinai kinyume na kifungu cha 86 na 35 cha sheria hiyo  na kwamba kati ya Oktoba 12-16 mwaka huu huko Chang’ambe  Markasi  pasipo na uhalali wowote washitakiwa wote  katika hali  iliyokuwa ikipelekea  uvunjifu wa amani  walijimilikisha  kwa nguvu ardhi  ya  kampuni ya Agritanza Ltd.

Shitaka la nne, wakili Kweka alidai ni la wizi  ambalo ni kinyume na kifungu cha 258  cha sheria ya Kanuni ya Adhabu ya mwaka 2002, na kuwa kati ya Oktoba 12-16 mwaka huu,  washitakiwa hao waliiba vifaa na malighafi,matofali 1500,nondo,Tani 36 za Kokoto vitu vyote hivyo vikiwa na thamani ya Sh 59,650,000 mali ya kampuni ya Agritanza Ltd.

Aidha shitaka la tano Kweka alidai ni la uchochezi ambalo linamkabili Sheikh Ponda peke yake  ambalo ni kinyume na kifungu cha 390 na 35 cha sheria hiyo  kwamba kati ya Oktoba 12-16 mwaka huu katika eneo hilo la Chang’ombe Markasi  kwa maelezo kuwa yeye ni Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu(T) aliwashawishi  wafuasi wake ambao ni washitakiwa hao  kutenda makosa hayo  na kwamba upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.

“Mheshimiwa hakimu pamoja na kuwasomea mashitaka hayo ambayo yanadhamana kwa mujibu wa sheria, Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), Dk.Elizer Feleshi kwa mkono wake amenituma kuwasilisha kwaniaba yake mahakamani hapo hati ya kufunga dhamana kwa mshitakiwa wa kwanza (Ponda) peke yake chini ya kifungu cha  148(4) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 2012’alidai wakili Kweka.

Kwa upande wake wakili wa shitakiwa hao Mansoor alidai anashangazwa na DPP-Dk.Feleshi kuwawasilisha hati hiyo ya kumfungia Ponda dhamana wakati dhamana ni haki ya Kikatiba na kwamba hati hiyo ya DPP imetaja sababu mbili ambazo ni mosi kwaajili ya usalama na sababu ya pili ni maslahi ya jamhuri.Nakuongeza kuwa sababu hizo hazijafafanuliwa kwa mabana na kudai kuwa washitakiwa wameishakaa kwa muda mrefu rumande na kwamba mshitakiwa wanne ni mwanamke mwenye umri wa 100 hivyo anaomba wapatiwe dhamana.

Akijibu hoja hizo wakili wa serikali Kweka alidai anashangazwa na hoja za wakili washitakiwa za kuikosoa hati hiyo iliyowasilishwa na DPP kwasababu kifungu cha 184(4) cha Sheria Makosa ya Jinai, kinasomeka wazi kuwa hati hiyo ya DPP  hata mahakama haiwezi kuipinga na kwamba inapowasilishwa mahakamani hati hiyo mahakama inakuwa imefungwa mikono  na kwamba mwenye mamlaka ya kuiondoa makamani hapo ni DPP mwenyewe siku atapoona inafahaa kuiondoa na sivinginevyo.

Hata hivyo hakimu Sanga alisema hivi baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili; “Kama nilivyokwisha sema tangu awali naingia kuanza kusikiliza kesi hii kuwa mimi siyo hakimu niliyepangwa kusikiliza kesi hii ,aliyepangwa kusikiliza kesi hii ni Hakimu Victoria Nongwa ambaye yupo kwenye semina  kwahiyo endapo pande zote mbili katika kesi hii mnataka kuwasilisha hoja zenu msubirini Hakimu Nongwa akimaliza semina yake mje muwasilishe hoja hizo mbele yake”alisema Hakimu Sanga.

Hata hivyo wakili washitakiwa Mansoor alionekana kutoridhishwa na jibu hilo aliinuka na kumuomba hakimu Sanga aiarishe kesi hiyo hadi leo ili washitakiwa 49 waletwe leo kwaajili ya kupatiwa dhamana kwasababu makosa yao yanadhamana lakini hakimu Sanga alisema haitawezekana kwasababu Hakimu Nongwa bado yupo kwenye semina na leo hatakuwepo mahakamani hapo na hivyo akaamuru washitakiwa hao warejeshwe rumande hadi Novemba mosi,kesi hiyo itakapokuja kwaajili ya kutajwa.

Baada ya  kesi hiyo kumaliza wanausalama walikuwa wamejazana kwa mtindo tofauti ndani ya ukumbi huo wa mahakama waliwataka waandishi wa habari na watu wengine watoke nje na ndani wabaki washitakiwa peke yake na wanausalama na kisha wakatolea mlango wa nyuma washitakiwa hao na kisha kwenye kuwapakiza kwenye mabasi ya Jeshi la Magereza, Karandika na Defenda tayari kwaajili ya kuanza safari ya kupeleka gerezani  ambapo magari ya askari wa usalama Barabarani walilazimika kuifunga barabara iliyopakana na mahakama hiyo kwa muda kwaajili ya kuruhusu msafara wa zaidi ya magari saba yaliyokuwa yamebeba washitakiwa hao,wanausalama kuelekea gerezani.

Baadhi ya watu waliofika mahakamani hapo kusikiliza kesi hiyo ,walizungumza na gazeti hili walisema wamefurahishwa na hatua ya serikali ya kuwafikisha washitakiwa hao mahakamani kwani Tanzania ni nchi inayoongozwa kwa Sheria na Katiba ya nchi na siyo sheria za dini ya Kiisilamu.


Facebook:happy katabazi :Aprili 18 mwaka 2013. 

Simu.0716 -774494.