TUMSHUKURU MUNGU KWA KILA JAMBO(Aprili 29/2013)
HAPPINESS KATABAZI vs.DPP.DK.FELESHI
Happiness Katabazi mwandishi wa habari za
mahakamani 'aka'(Mbea wa mahakamani) na rafiki yangu Mkurugenzi wa
Mashitaka(DPP) ,Dk.Eliezer Feleshi.(Aprili 15/2013
HONGERA JESHI LA POLISI KWA KUKAMILISHA HARAKA UPELELEZI KESI YA LWAKATARE
Na Happiness
Katabazi
APRILI 13 mwaka huu, kupitia mitandao yangu ya kijamii ya www.katabazihappy.blogspot.com na Facebook; happy katabazi niliweka makala yangu iliyokuwa na kichwa cha habari kisemacho ‘ Komeni kujadili mwenendo wa kesi ya Lwakatare nje ya mahakama’.
Kwa kifupi tu ndani ya makala hiyo nilikuwa nawakemea baadhi ya wanasiasa na waandishi wa habari ambao walikuwa wakiijadili mwenendo wa kesi hiyo nje ya mahakama ambayo mawakili wakuu wa serikali Ponsia Lukosi,
Prudence Rweyongeza na Peter Mahugo wanaoiendesha kesi hiyo tangu ilipofunguliwa kwa mara ya kwanza Machi 18 mwaka huu, na kisha kesi hiyo ikafutwa ikajafunguliwa Machi 20 mwaka huu na ikapewa Na.P1,7/2013, Machi 22 mwaka huu, kesi hiyo ilipokuja kwaajili ya kutajwa mbele ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, Alocye Katemana walisema wazi kuwa upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika na kesi hiyo ikaarishwa hadi Aprili 30 mwaka huu, itakapokuja kwaajili ya kutajwa.
Nikiri wazi kuwa baada ya kuiweka makala hiyo kwenye mitandao hiyo ilisomwa na wengi na kuwa wengine walionikosoa kwa hoja zisizo na mashiko kwani walishindwa kujikita kwenye hoja yangu iliyokuwa ikikemea makundi hayo iache tabia ya kuingiria uhuru wa mahakama na iliwasisitiza waheshimuwa mgawanyo madaraka.
Lakini kundi jingine lilinipongeza kwa makala hiyo na ninashukuru pia kwani kwa njia moja au nyingine mawazo yangu hayo yaliyokuwa yamewekwa kwenye makala hayo ambayo yalikuwa yakikataza baadhi ya wanasiasa na waandishi wa habari kaacha kuijadili kesi hiyo nje ya bunge kwani kufanya hivyo ni kuingilia uhuru wa mahakama.
Wiki iliyopita Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Angella Kairuki , Mbunge wa Kigoma Mjini Peter Serukamba na baadhi ya wabunge wengine wakati wakiwa bunge wakichangia hotuba ya Ofisi ya Rais, ambazo hotuba zao ziliwasilishwa bunge na waziri Steve Wassira , George Mkuchika, baadhi ya wabunge walikuwa wakichangia maoni ya bajeti hizo na wengine na walipokuwa wakitaka kuijadili kesi ya Lwakatare , Waziri Kairuki na Serukamba na Wasira walimwomba Spika wa Bunge Anna Makinda na Naibu wake Job Ndugai wawazuie wabunge wasijadili kesi ya Lwakatare kwani ipo mahakamani, na endapo bunge likiruhusu hilo ,ni wazi bunge litakuwa linaingia uhuru wa mahakaman.
Nawapomgeza viongozi hao kwani mawazo yao hayo yalishabiana na mawazo yangu hayo niliyokuwa nimeyaandika katika makala hiyo iliyokuwa na kichwa cha habari kisemacho “KOMENI KUJADILI KESI YA LWAKATARE NJE YA MAHAKAMA’.
Na siyo siri tangu bunge likataze jambo hilo lisijadiliwe nje ya mahakama naweza kusema katazo hilo limesaidia kwa kiasi fulani kwani wale wanasiasa na waandishi wa habari ambao walifikia mbali sana kwakusema kesi hiyo ni ya kubambika ,wamepunguza kasi ya kujadili kesi hiyo na watu tunajiuliza kasi ile ya kuijadili kesi hiyo ya kaka yangu Lwakatare nje ya mahakama imeishia wapi?
Itakumbukwa kuwa Aprili 22 mwaka huu, Kaimu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Issa Mungulu aliwaeleza waandishi wa habari kuwa upelelezi wa kesi tuhuma za ugaidi inayomkabili Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chadema, Wilfred Lwakatale na mwenzake Joseph Ludovick umekamilika na kwamba jeshi la polisi litapelekea jalada hilo kwa Mkurugenzi wa Mashitaka(DPP)-Dk.Eliezer Feleshi kwaajili ya hatua za kisheria kuhusu kesi hiyo.
Tamko hilo la Kaimu DCI-Mungulu kwa niaba ya jeshi la polisi ndiyo limenisukuma kuandika makala hii ya kulipongeza jeshi la polisi kwani limeanza kukamilisha upelelezi wake haraka hasa ukizingatia kesi hiyo iliyozua mjadala mkubwa nchini ilifunguliwa Machi 20 mwaka huu. Na Aprili 22, Jeshi la Polisi linautangazia umma kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika.
Hakika hatua hii ni ya kupongeza kwani imedhiirisha kuwa hivi sasa jeshi la polisi limeanza kuondokana na kusuasusa kwa kukamilisha haraka upelelezi wa kesi mbalimbali.
Naweza
kusema kwa kipindi cha mwaka huu, tu katika kesi ambazo zinafuatiliwa na umma
kwa karibu ,upelelezi wa kesi ya Lwakatare nao umechukua muda mfupi kukamilika
kwani kesi ya kwanza ambayo nimeiripoti pale katika mahakama ya hakimu mkazi
kisutu ambapo upelelezi ulichukua siku mbili kukamilika ni kesi ya jinai Na.125/2013,
Jamhuri dhidi ya wafuasi 53 wa Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu,Sheikh
Ponda Issa Ponda ilidumu mahakamani
hapo kwa siku 32 tu tangu ilipofunguliwa rasmi Februali 18 na kutolewa hukumu
Machi 21 mwaka huu.Ambapo Hakimu Sundi Fimbo aliwatia hatiani washitakiwa kwa
makosa matatu ya kufanya mkusanyiko haramu, kukaidi amri ya jeshi la polisi
ambapo kila kosa aliwahukumu kwenda jela mwaka mmoja,Na hivyo wafungwa hao
ambao hivi sasa wanaishi Magereza tofauti nchini wanatumikia adhabu ya mwaka
mmoja tu gerezani.
Kwa kuwa
mimi ni mwandishi wa habari za mahakamani kwa zaidi ya miaka 14 sasa, hupenda
kuzilipoti kesi nyingi tangu zinapofunguliwa hadi zinapomalizika na kesi
ikishatolewa uamuzi na mahakama nimejenga utaratibu wa kuandika makala inayohusu
kesi husika, hivyo hata hukumu ya kesi hiyo ya wafuasi wa Ponda baada ya
kutolewa hukumu, niliandika makala
ambayo niliiweka kwenye mitandao yangu ya kijamii yaani www.katabazihappy.blogspot.com
na Facebook.happy katabazi ; ambayo ilikuwa na kichwa cha habari kisemacho (HONGERA
OFISI YA DPP,POLE WAFUASI WA SHEIKH PONDA).
Ambapo ndani
ya makala hiyo nililipongeza jeshi la polisi kwa kukamilisha haraka tena kwa
kasi ya ajabu upelelezi wa kesi hiyo ya wafuasi wa Ponda, ambapo wasitakiwa
walitenda makosa Februali 15 mwaka huu,na Februali 18 wakafikishw a mahakamani,
na baada ya kusomewa mashitaka mawakili waandamizi wa serikali Bernad
Kongora, Bernad Kongora,Peter Ndjike,na Joseph Mahugo,walieleza
upelelezi umekamilika na kesho yake Februali 19, kesi hiyo ilikuja kwaajili ya
washitakiwa kusomewa maelezo ya awali na walisomewa na siku iliyofuata
mashahidi wa upande wa Jamhuri ambapo shahidi wa kwanza alikuwa Mkuu wa
upelelezi Kanda Maalum ya Dar es Salaam(ZDCO), Hemed Msangi alitoa ushahidi
wake.
Wafuasi hao
walifanya maandamano haramu Februali 15 mwaka huu, wakitaka kwenda ofisi ya
DPP, ili wamshikinikize ili aweze kuindoa hati yake ya kumfungia Ponda dhamana aliyowasilisha
katika mahakama ya Kisutu siku ya kwanza Ponda na wenzake walipofikishwa
mahakamani Oktoba 18 mwaka jana, kwa makosa ya uchochezi na wizi wa malighafi
za Sh.milioni 59 .
Wakati kesi
ya Ponda na wenzake 49 inakuja kutolewa hukumu Mei 9 mwaka huu.
Kwani hakuna ubushi kuna kesi zinachukua zaidi ya mwaka mmoja upelelezi kukamilika na matokeo yake washitakiwa ambao wanakabiliwa na kesi zisizo dhamana kusota gerezani muda mrefu.
Na kwa mujibu wa makosa ya kesi inayomkabili Lwakatare, makosa hayo hayana dhamana hivyo Lwakatare tangu alipofunguliwa kesi anaishi katika Gereza la Segerea akisubiri hatima ya kesi yake.
Hivyo basi kitendo cha jeshi la polisi kuutangazia umma kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika ni wazi sasa umefanya kesi hiyo kupiga hatua nyingine ya kisheria. Kwani kesi hiyo ambayo Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu haina mamlaka ya kuisikiliza, mawakili wa serikali siku wakifika mahakamani na kuieleza mahakama kuwa upelelezi wa shauri umekamilika, hatua nyingine ya kisheria inayofuata ni kwa mujibu wa tarehe itakayopangwa na mahakama ni kwamba upande wa jamhuri kuwasomea washitakiwa hao maelezo ya kina ya kesi hiyo inayowakabili (Committal Proceeding) .
Baada ya ya zoezi hilo la kuwasomea (Committal Proceeding) , mahakama itatangaza kuifunga kesi hiyo katika mahakama hiyo ya hakimu mkazi na kisha jadala la kesi hiyo litaamishiwa Mahakama Kuu kwaajili ya kesi hiyo kuanza kusikilizwa rasmi,ambapo siku ya kwanza washitakiwa hao watasomea mashitaka yao na kisha wataruhusiwa kujibu (Plea).
Na hatua nyingine za kuletwa kwa mashahidi zitaendelea.Hadi hapo shauri hilo litapofikia tamati kwa mahakama kutoa maamuzi yake au DPP akiona hana haja ya kuendelea na kesi hiyo anaweza kuifuta kesi hiyo chini kifungu cha 91(1) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 2002.
Kwani fursa hiyo ya kujibu mashitaka hayo walinyimwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi,kwani mahakama ya hakimu mkazi haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo.
Kwa tamko hilo la jeshi la polisi kuwa upelelezi umekamilika ni wazi linaweza kuwa funzo pia kwa wale wote wakiwemo baadhi ya wanahabari wenzangu waliokuwa waikijadili kesi ya Lwakatare nje ya mahakama kwa kuandika makala na habari zenye mawazo ya kijinga ambayo hayana msingi wowote wa kisheria na yaliyokuwa na lengo la kutaka kuiondoa kesi hiyo ambayo imefunguliwa kwa mujibu wa Sheria za nchi ianze kujadiliwa nje na watu ambao hawana mamlaka ya Kimahakama.
Ni rai yangu kwa wale waandishi wote ambao walikuwa wakiandika makala zao kujadili kesi hiyo na wengine kufikia hatua ya kusema kesi hiyo ni ya kubambika, na wakati wakiandika kuwa kesi hiyo ni ya kubambika utafikiri walikuwa na ushahidi na hilo kumbe hawana , kama ni kweli wanampenda kaka yangu Lwakatare na siyo wanafki na walikuwa na lengo la kuipotisha kesi hiyo , basi wakusanye vielezo vyao vya kuonyesha kesi hiyo ni ya kubambika ili siku kesi hiyo itakapoanza kusikilizwa waje wawe mashahidi wa upande wa washitakiwa na waonyeshe vielelezo hivyo, maana kuzungumza jambo hilo kuwa mshitakiwa fulani amebambikiwa kesi wakati hufanyi jitihada zozote za kufika mahakamani siku ya kesi na kutoa vielelezo, hakutamsaidia mhusika na jamii itakuhesabu kuwa wewe ni mbumbumbu na mnfaki.
Napenda kuwaasa baadhi ya wanahabari wenzangu kuwa tujenge utaratibu wa kuheshimu mgawanyo madaraka, majukumu ya wanataaluma wenye taaluma zingine na kwamba tusikubali kugeuzwa kuwa ‘Microphone Political Party’. Tusimame kwenye maadili ya taaluma yetu kwaajili ya maslahi ya taifa letu.
Kwani hata nchi nyingi zilizoendelea ,waandishi wa nchi hizo walichangia mchango mkubwa wa taaluma yao katika kusukuma gurudumu la maendeleo. Waandishi wa habari katika nchi hizo zilizoendelea ,baadhi yao wameamua kubobea katika eneo fulani la kuripoti habari fulani.Mfano mwandishi wa habari anayeandika habari za Kitabibu au mazingira, basi mwandishi huyo anakuwa amesomea pia fani za Kitabibu na mazingira, lakini hapa kwetu hali ni tofauti na ndiyo maana kila kukicha baadhi ya waandishi wamekuwa wakiripoti habari zilizopotoshwa.
Wakati ni huu, tuache majungu, kutumiwa na wanasiasa uchwara tena kwa bei rahisi tu na wazi wazi kwa kutupangia tuandike habari hii kwa maslahi yao vyama vyao,majimbo au nyadhifa zao,tujiendeleze kielimu na tubobee katika kuandika habari ambazo moyo na akili zetu zinakutuma ujikite huko kwa nia njema.Naamini tufanya hivyo tutakuwa tunalisaidia taifa letu na mungu atalipa dhawabu.
Mwisho nirudie kwa kulipongeza jeshi la polisi kwa kukamilisha upelelezi wa kesi ya Lwakatare haraka, na pia nilitie moyo jeshi la polisi kwa kuendelea kukamilisha upelelezi katika kesi nyingine haraka zinazowakabili washitakiwa wengine wenye kesi mbalimbali kwani nimekuwa nikishuhudia kwa macho yangu ninapokuwa mahakamani naripoti kesi mbalimbali, washitakiwa na mawakili kesi zao zimekuwa zikiarishwa kwa zaidi ya hata mwaka mmoja kwa kile kinachodaiwa na upande wa jamhuri kuwa jeshi la polisi bado halijakamilisha upelelezi.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika.
Chanzo:www.katabazihappy.blogspot.com
Facebook; happy katabazi ; Jumatano ,Aprili 24 mwaka 2013.
KORTINI KWA KUUZA MAENEO YA WAZI
Na Happiness Katabazi
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU), jana ilimfikisha katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu aliyekuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke, Steven Kongwa na mwenzake Revecotus Wachawendera, kwa makosa ya kuuza eneo la wazi lililopo eneo la Mbezi.
Mbele ya Hakimu Mkazi Agustina Mbando, Mwendesha Mashtaka toka Takukuru,Husein Mussa alidai washitakiwa walitenda kosa hilo kati ya Januari 2000 na Desemba 2001.
Mussa alidai washtakiwa hao walitenda kosa hilo wakati Kongwa alipokuwa na wadhifa wa Ofisa Mpimaji Ardhi wa Manispaa ya Jiji la Dar es Salaam na Wachawendera akiwa mpimaji wa ardhi katika Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi.
Alidai kati ya kipindi hicho waligawa bila kufuata taratibu za sheria ya mipango miji Kitalu namba 1/851 na kitalu namba 1/597 Block “L” eneo ambalo lilitengwa kwa ajili ya bustani.
Alilitaja kosa jingine ni la kushindwa kutimiza wajibu wao kinyume na sheria, hivyo kama wapimaji ardhi kwa pamoja walikiuka sheria ya mipango miji kwa kugawa eneo hilo.
Hata hivyo washitakiwa hao walikana mashitaka na hakimu aliwapatia masharti ya adhamana ambayo waliyatimiza na akaairisha kesi hiyo Mei 20 mwaka huu itakapokuja kwaajili ya kutajwa.
Chanzo:www.katabazihappy.blogspot.com; Aprili 24 mwaka 2013.
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU), jana ilimfikisha katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu aliyekuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke, Steven Kongwa na mwenzake Revecotus Wachawendera, kwa makosa ya kuuza eneo la wazi lililopo eneo la Mbezi.
Mbele ya Hakimu Mkazi Agustina Mbando, Mwendesha Mashtaka toka Takukuru,Husein Mussa alidai washitakiwa walitenda kosa hilo kati ya Januari 2000 na Desemba 2001.
Mussa alidai washtakiwa hao walitenda kosa hilo wakati Kongwa alipokuwa na wadhifa wa Ofisa Mpimaji Ardhi wa Manispaa ya Jiji la Dar es Salaam na Wachawendera akiwa mpimaji wa ardhi katika Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi.
Alidai kati ya kipindi hicho waligawa bila kufuata taratibu za sheria ya mipango miji Kitalu namba 1/851 na kitalu namba 1/597 Block “L” eneo ambalo lilitengwa kwa ajili ya bustani.
Alilitaja kosa jingine ni la kushindwa kutimiza wajibu wao kinyume na sheria, hivyo kama wapimaji ardhi kwa pamoja walikiuka sheria ya mipango miji kwa kugawa eneo hilo.
Hata hivyo washitakiwa hao walikana mashitaka na hakimu aliwapatia masharti ya adhamana ambayo waliyatimiza na akaairisha kesi hiyo Mei 20 mwaka huu itakapokuja kwaajili ya kutajwa.
Chanzo:www.katabazihappy.blogspot.com; Aprili 24 mwaka 2013.
GODBLESS LEMA AIBWAGA TENA CCM
Na Happiness Katabazi
Dar es Salaam. Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema ameibuka kidedea baada ya Mahakama ya Rufani kutupilia mbali maombi ya marejeo ya rufaa iliyomrejesha bungeni.
Maombi hayo yaliwasilishwa mahakamani hapo na makada watatu wa CCM mkoani Arusha, kupitia kwa Mawakili wao Alute Mughway na Modest Akida wakiiomba Mahakama ya Rufani ifanye marejeo ya hukumu yake hiyo kwa madai kuwa hukumu hiyo haikuwa sahihi.
Hata hivyo, jana Mahakama ya Rufani ilisikiliza
maombi hayo kutoka kwa waombaji pamoja na hoja za wajibu maombi na kisha
kutupilia mbali maombi hayo ikisema kuwa hayana msingi.
Uamuzi huo wa kutupilia mbali maombi hayo ulisomwa
na Jaji Bernard Luanda, kwa niaba ya jopo la majaji wenzake lililokuwa
likiongozwa na Engela Kileo na Salum Massati.
Hata hivyo, jopo hilo halikutoa sababu za kutupilia mbali maombi hayo na badala yake lilisema litatoa maelezo ya kina baadaye.
Majaji hao isipokuwa Kileo ndiyo waliosikiliza na
kutoa hukumu ya rufaa iliyomrejesha Lema bungeni, ambayo ilikuwa
inapingwa na makada hao wa CCM.
Awali, kabla ya kutupilia maombi hayo ya marejeo,
mahakama hiyo ilitupilia mbali maombi ya waombaji hao kutaka suala hilo
lisikilizwe na jopo la majaji saba.
Wakili Mughwai aliwasilisha maombi katika Mahakama
ya Rufani akiomba marejeo ya rufaa yahamishwe katika jopo la majaji
watatu na kupelekwa kusikilizwa na jopo la majaji saba kwa madai kuwa
kuna jambo linatakiwa kushughulikiwa kutokana na mazingira yake.
Wakili wa Lema, Methods Kimomogoro alidai kuwa Wakili Mughwai amechanganya maombi hivyo kuleta utata na kwamba kama alikuwa akitaka yasikilizwe angeyapeleka katika utaratibu ulio sahihi.
“Kanuni ya Nne ya Mahakama ya Rufaa, inasema hakuna kanuni rasmi inayowezesha jopo hili kuhamisha maombi ya marejeo kwenda kwenye jopo la majaji saba kwa ajili ya mapitio,” alisema Kimomogoro na kuongeza:“Labda kama maombi ya mapitio yangekubaliwa, wangekwenda hatua ya pili ya kuomba jopo la majaji saba.
Maombi haya hayajafuata utaratibu hivyo naomba Mahakama iyatupilie mbali kwa kuwa sababu za kisheria hazikidhi na Mahakama haina uwezo wa kuyatolea uamuzi.”
Wakili wa Serikali, Vicent Tangoh alimuunga mkono Kimomogoro na kuongeza kuwa hiyo inaonyesha hakuna maombi yoyote mbele ya Mahakama wala kitu cha kupeleka katika jopo la majaji saba.
- Lema ashinda rufaa ya Ubunge Arusha mjini
- Upelelezi kesi ya Lwakatare umekamilika - Mkurugenzi
- Wabunge wazidi kuibana Serikali
- Msigwa: Kigogo wa CCM anauza pembe za ndovu
- Serikali yafunga viwanda vya nondo
- Samata aziponda Yanga, Simba
- Rais anayesumbua vichwa vya dunia
- Mawaziri ‘watoro’ Bungeni
- Wabunge Chadema waahidi kushambulia kwa mikutano
- Rufaa dhidi ya Zombe njiapanda
DOSARI ZA KWAMISHA RUFAA YA DPP DHIDI YA ZOMBE
Na Happiness Katabazi
MAHAKAMA ya Rufaa nchini, jana ilijikuta ikishindwa kuanza kusikiliza rufaa iliyokatwa na Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP)-Dk.Eliezer Feleshi dhidi ya Aliyekuwa Mkuu wa upelelezi wa mkoa wa Dar es Salaam(ACP)-Abdallah Zombe na wenzake baada ya mahakama hiyo kubaini dosari katika hati ya kukata rufaa.
Rufaa hiyo Na.254/2009 inayosikilizwa na jopo la majaji watatu Edward Rutakangwa,Mbarouk Mbarouk na Bethek aMila, ambayo jana ilikuja kwaajili ya kuanza kusikilizwa kwa siku mbili mfululizo , jaji Mbarouk kabla ya kuanza kusikiliza hoja za rufaa hiyo aliutaka upande wa mwomba rufaa(DPP), wameiweke sawa mahakama kuwa katika hati ya kukata rufaa ya ya kupinga hukumu ya mahakama kuu ya kesi ya mauji Na.26/2006 ya Zombe na wenzake inasomeka kuwa hukumu ya mahakama kuu iliyotolewa na Jaji wa mahakama ya rufaa Salum Massati.
“Hebu mawakili wa mwomba rufaa ebu mtufafanulie hili, hati yenu ya kukata rufaa inasema hukumu ya mahakama kuu ilitolewa na jaji wa mahakama ya rufaa (Massati)…sasa kama hukumu hii ilitolewa na jaji wa mahakama ya rufaa ebu tuwalize sasa nyie waomba rufaa, michokileta hapa mbele yetu ni ombi la mapitio, marejeo au?Maana majaji wa mahakama ya rufaa hawawezi kusikiliza rufaa inayotokana na hukumu iliyotolewa na jaji mwenzao wa mahakama ya rufaa, tunachokifanya ni kufanya marejo au mapitio;
“Jicho la mahakama limeona ni kama hakuna rufaa mbele yake kwani rufaa ya kesi ya jinai ni lazima iwe na hati ya kukata rufaa kwa mujibu wa Kanuni ya 68(1) cha Mahakama ya Rufaa’ nakuongeza kuwa kwa dosari hiyo mahakama inaona nikama hakuna rufaa iliyokatwa dhidi ya zombe na wenzake”alisema Jaji Mbarouk.
Jaji Rutakangwa aliwataka mawakili wanaomwakili DPP wajipe muda na wasome vizuri Ibara ya 119 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 ambayo inasomeka kama ifuatavyo:
“Jaji yoyote wa Mahahakama ya Rufani hatakuwa na mamlaka ya kusikiliza shauri lolote katika Mahakama Kuu au katika mahakama ya hakimu ya ngazi yoyote.:
“Isipokuwa kwamba iwapo jaji yeyote wa mahakama kuu atateuliwa kuwa Jaji Mahakama ya rufaa, basi hata baaa ya kuteuliwa kwake kuwa jaji wa mahakama ya rufani,jaji huyo aweza kuendelea kufanyakazi kazi zake katika mahakama kuu mpaka amalize kutayarisha na kutoa hukumu au mpaka akamilishe shughuli nyingine yoyote inayohusika na mashauri ambayo yalikwisha anza kuyasikiliza kabla kabla hajateuliwa kuwa jaji wa mahakama rufani, na kwamba ajili hivyo itakuwa halali kwake kutoa hukumu au uamuzi mwingine wowote unaohusika kwa kutumia kutumia au kutaja madaraka aliyoshika kabla ya kutueliwa kuwa jaji wa mahakama ya rufani, lakini endapo hatimaye hukumu hiyo au uamuzi mwingine utapingwa kwa njia ya rufaa itayofikishwa mbele ya mahakama ya rufani,basi katika hali hiyo jaji huyo wa mahakama ya rufani,hatakuwa na mamlakaya kusikiliza rufaa hiyo:inasomeka ibara hiyo.
Alisema mawakili wa mwomba rufaa walipaswa katika hati yao ya kukata rufaa waandike jaji Jaji Masati ambaye zamani alikuwa ni jaji wa mahakama kuu na sikuandika jaji wa mahakama ya rufaa.
Akijitetea mawakili wakuu wa serikali wanaomwakilisha DPP, Vitalis Timon, Prudence Rweyongeza, Mgaya Mtaki, Alexander Mzikila, Edwin Kakoraki alikiri dosari hiyo na akaomba mahakama hiyo iwapatie ruhusa ya kwenda kufanyia marekebisho dosari hiyo chini ya Kanuni ya 4(2),(2),(b) ya Sheria ya Mahakama ya Rufaa na kwamba hata jana walikuwa wapo tayari kufanyia marekebisho hati hiyo ya kukata rufaa ambayo jicho la mahakama limeona ina dosari na kisha jana hiyo hiyo kuirejesha upya mahakamani.
Hata hivyo mawakili wa wajibu rufaa Richard Rweyongeza, Majura Magafu, Denis Msafiri walianza kwa kuishukuru mahakama kuwa jicho mahakama limeweza kubaini dosari hiyo na kwamba kwa dosari hiyo ni kwamba hakuna hati ya rufaa mbele ya mahakama hiyo na kwamba akaiomba mahakama ikatae kuwapa muda wa kufanyia marekebisho kwani tayari muda wa kukata rufaa umeishapita na kwamba kama wanataka kukata rufaa watalazimika kuwasilisha ombi la kuongezewa muda ambao ni siku 30 chini ya kanuni ya 68(1) ya Mahakama ya Rufaa.
‘Kwa sababu jicho la mahakama limeona dosari hiyo sisi wajibu rufaa tunaomba mahakama iitupilie mbali rufaa hiyo kwani katika kesi za jinai kama hakuna hati ya kiapo ni wazi hakuna rufaa mahakamani iliyowasilishwa na DPP’alidai wakili Magafu.
Akijibu hoja hiyo wakili Vitalis alidai Kanuni ya 4(2),(a),(b) ya Mahakama ya Rufaa inaipa mamlaka kutoa amri ya kuwaruhusu kwenda kufanyia marekebisho hati hiyo ila wanakiri ni kweli hati yao yao waliyoitumia kukata rufaa ina mapungufu hayo.
Kwa upande wake jaji Rutakangwa alisema amezikilza hoja za pande zote mbili ni nzito na zina mvuto na kwamba jopo linaomba lipewe muda wa kwenda kuandaa uamuzi wake na kwamba uamuzi wao utakapokuwa tayari watazijulisha.
Agosti 17 mwaka 2009, Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, ilitoa hukumu ya kihistoria ya kesi ya mauji ya watu wanne iliyokuwa ikimkabili Zombe na wenzake ambapo jaji Salum Massati ambaye hivi sasa ni jaji wa mahakama ya rufani aliwaachilia huru Zombe na wenzake ambao walikuwa wakikabiliwa na kesi hiyo kwa maelezo kuwa upande wa jamhuri ulishindwa kuleta ushahidi mzuri ambao ungewea kuishawishi mahakama hiyo iwaone washtakiwa hao wana hatia.
Baada ya hukumu hiyo ya mahakama kuu, DPP hakulidhishwa na hukumu hiyo Oktoba 7 mwaka 2009 akakata rufaa Mahakama ya Rufaa , kupinga hukumu hiyo ambayo kwa mujibu wa ratiba ya vikao vya mahakama ya rufaa,rufaa hiyo ilikuwa imepangwa kuanza kusikilizwa jana lakini ikashindikana.
Mbali na Zombe, washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni Christopher Bageni, Ahmed Makele, WP 4593 PC Jane Andrew, D 1406 Koplo Emmanuel Mabula, D 8289 DC Michael Shonza, D. 2300 Abeneth Saro, D.4656D/Koplo Rajabu Bakari na D.1317D/XP Festus Gwasabi na jana washtakiwa wote walifika mahakamani hapo.
Washitakiwa hao walidaiwa kuwa Januari 14, mwaka 2006 waliwaua wafanyabiashara watatu wa madini wa wilayani Ulanga, mkoani Morogoro; Ephraim Chigumbi, Sabinus Chigumbi na Mathias Lukombe pamoja na dereva teski Juma Ndugu, mkazi wa Dar es Salaam kwa madai kuwa walikuwa majambazi.
Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Aprili 23 mwaka 2013.
RUFAA YA DDP V ZOMBE KUANZA LEO
Na Happiness Katabazi
MAHAKAMA ya Rufaa nchini leo inatarajia kuketi Dar es Salaam na kuaza kusikiliza rufaa iliyokatwa na Mkurugenzi wa Mashtaka(DPP), Dk.Eliezer Feleshi dhidi ya aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Dar es Salaam (ACP), Abdallah Zombe na wenzake na kupinga hukumu iliyotolewa na Mahakama Kuu katika kesi ya mauji Na.26/2006 ambayo iliwaachiria huru Zombe na wenzake.
Kwa mujibu wa ratiba ya vikao vya mahakama ya rufaa ambayo gazeti hili imeona nakala ya ratiba hiyo, inaonyesha rufaa hiyo inayosubiriwa kwa shauku kubwa na umma itasikilizwa kwa siku mbili mfululizo yaani leo na kesho.
Rufaa hiyo itasikilizwa mbele ya majaji wa tatu wanaongozwa na Jaji Natharia Kimaro,Catherine Oriyo na Semistocles Kaijage.
Upande wa mwomba rufaa(DPP), unawakilishwa na jopo la mawakili waandamizi wa serikali saba ambao ni Mgaya Mtaki, Timon Vitalis,Edward Kakolaki, Angaza Mwipopo, Prudence Rwenyongeza ,Alexanda Mzikila na Peter Njike .
Wakati upande wa wajibu rufaa unawakilishwa na mawakili wa kujitegemea Richard Rweyongeza na washtakiwa wengine wanatetewa na mawakili Majura Magafu, Denis Msafiri, Deodoras Ishengoma
Itakumbukwa kuwa Desemba 12 mwaka jana,rufaa ilikuja kwaajili ya kuanza kusikilizwa lakini ilishindikana kuanza kusikilizwa kwasababu Jaji Kaijage alikuwa mgonjwa.
Agosti 17 mwaka 2009, Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, ilitoa hukumu ya kihistoria ya kesi ya mauji ya watu wanne iliyokuwa ikimkabili Zombe na wenzake ambapo jaji Salum Massati ambaye hivi sasa ni jaji wa mahakama ya rufani aliwaachilia huru Zombe na wenzake ambao walikuwa wakikabiliwa na kesi hiyo kwa maelezo kuwa upande wa jamhuri ulishindwa kuleta ushahidi mzuri ambao ungewea kuishawishi mahakama hiyo iwaone washtakiwa hao wana hatia.
Baada ya hukumu hiyo ya mahakama kuu, DPP hakulidhishwa na hukumu hiyo Oktoba 7 mwaka 2009 akakata rufaa Mahakama ya Rufaa , kupinga hukumu hiyo ambayo kwa mujibu wa ratiba ya vikao vya mahakama ya rufaa,rufaa hiyo ilikuwa imepangwa kuanza kusikilizwa jana lakini ikashindikana.
Mbali na Zombe, washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni Christopher Bageni, Ahmed Makele, WP 4593 PC Jane Andrew, D 1406 Koplo Emmanuel Mabula, D 8289 DC Michael Shonza, D. 2300 Abeneth Saro, D.4656D/Koplo Rajabu Bakari na D.1317D/XP Festus Gwasabi na jana washtakiwa wote walifika mahakamani hapo.
Washitakiwa hao walidaiwa kuwa Januari 14, mwaka 2006 waliwaua wafanyabiashara watatu wa madini wa wilayani Ulanga, mkoani Morogoro; Ephraim Chigumbi, Sabinus Chigumbi na Mathias Lukombe pamoja na dereva teski Juma Ndugu, mkazi wa Dar es Salaam kwa madai kuwa walikuwa majambazi.
Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumatatu, Aprili 22 mwaka 2013.
MAUJI,MAUAJI JAMANI
Watanzania huyu ni binadamu mwenzetu ambaye leo alfajiri ya kuamkia leo Aprili 20 amekutwa na mauti.Sisi wakazi wa Mtaa wa Sinza 'C' eneo la Ukuta wa Posta maarufu kama ukuta wa Kesi ya Abdallah Zombe, leo saa 11 alfajiri tulijikuta tukiamkia kuona mwili wa marehemu huyo ukivuja damu katikati ya barabara na ukiwa umelazwa chini baada ya kuua na watu wasiyojulikana.Nikiwa kama raia mwema na Mwandishi wa habari baada yakufika eneo hilo la tukio nilichofanya nikumpigia Simu mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Ilala,ACP-Duwani Nyanda na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, ACP- Charles Kenyela kuwapa taarifa na kweli baada ya muda mchache waliwaagiza askari wao wakafika eneo la tukio na kuuchukua mwili huo ambao ulikuwa unavuja damu.Inasikitisha sana, na inaendelea kudhiirisha kuwa baadhi ya watanzania hivi sasa wamezidi kuwa na roho katili na hawana hofu ya mungu.(Picha na Happiness Katabazi)
Chanzo:www.katabazihappy.blogspot.com
Facebook:happy katabazi
Aprili 20 mwaka 2013.
HUKUMU YA KESI YA PONDA YAOTA MBAWA
Na Happiness Katabazi
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, jana ilishindwa kutoa hukumu ya kesi ya uchochezi na wizi wa malighafi zenye thamani ya Sh.milioni 59 inayomkabili Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu na wenzake 49 kwa maelezo kuwa hakimu aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo Victoria Nongwa hayupo na wala hajaituma hukumu hiyo kwa uongozi wa mahakama.
Hakimu Mkazi Alocye Katemana ndiye aliyeairisha kesi hiyo ambapo alianza kwa kusema kesi hiyo jana ilikuja kwaajili ya kutolewa hukumu, lakini hukumu hiyo haitatolewa kwasababu hakimu anayesikkiliza kesi hiyo hayupo na wala hajatuma hukumu ya kesi hiyo.
‘Kwa sababu hiyo naairisha kesi hii hadi Mei 2 itakapokuja kwaajili ya kutajwa na kwamba Mei 9 mwaka huu, itakuja kwaajili ya kutolewa hukumu na hivyo kuamuru mshitakiwa wa kwanza na watano(Ponda na Mukadamu Swalehe) kurudishwa rumande kwasababu hadi sasa Mkurugenzi wa Mashitaka(DPP).Dk.Elizer Feleshi ajaondoa hati yake ya kuwafungia dhamana.
Mwandishi wa habari hizi ambaye alifika mahakamani hapo tangu saa moja asubuhi ,alishuhudia kundi la watu zaidi ya mia moja wakiwa wamesimama nje ya uzio wa mahakama hiyo karibu na ofisi ya Maktaba ya Taifa tayari wakisubiri kuingia ndani ya geti la mahakama hiyo kwaajili ya kukaguliwa kwa vifaa maalum na wanausalama ambapo hata hivyo waliruhusiwa na kuingia ndani ya viwanja vya mahakama, lakini ni wafuasi wachache ndiyo walioruhusiwa ndani ya chumba cha wazi Na. mbili cha mahakama hiyo kwaajili ya kusikiliza kesi hiyo.
Baada ya kuarishwa kesi hiyo askari magreza waliondoka na msafara wa magari yao ambao ulikuwa ukiongozwa na askari polisi waliokuwa wamevalia sare na wale ambao hawajavalia sare za jeshi hilo, na wakati wakitoka ndani ya viwanja hivyo tayari kwaajili ya kuelekea katika gereza la Segerea anapoishi Ponda na Mukadamu ,wafuasi hao walianza kupaza sauti huku wakimpungia mkono Ponda na kusema ‘ Takbirii Abkbaru ’.
Aprili
3 mwaka huu:Mawakili
wa upande wa Jamhuri ,Tumaini Kweka na Jessy Peter na mawakili wa utetezi Juma
Nassor na Njama waliwasilisha majumuisho yao mahakamani hapo kwa njia ya
maandishi ambapo mawakili wa upande wa jamhuri waliiomba mahakama iwaone
washitakiwa wote wana hatia na wapewe adhabu kwa mujibu wa sheria.
Wakati
mawakili wa utetezi waliiomba mahakama iwaone washitakiwa hawana hatia na
iwaachilie huru kwa sababu hawakutenda makosa yanayowakabili na kwamba
upande wa jamhuri umeshindwa kuthibitisha kesi yao.
Machi
21 mwaka huu;Sheik
Ponda, mshitakiwa wa tano Mukadamu Swaleh walijitetea.Na washitakiwa wenzake wa
nne nao walijitetea siku hiyo na hivyo kufanya jumla ya washitakiwa 48 wa kesi
hiyo kumaliza kutoa utetezi wao.Na siku hii ndipo upande wa utetezi walifunga
utetezi wao na Hakimu Nongwa aliipanga tarehe ya jana ndiyo angetoa hukumu ya
kesi hiyo.
Machi
4 mwaka huu: Hakimu
Nongwa atoa uamuzi wake ambapo aliwaona washitakiwa wote wana kesi ya kujibu na
akatupilia mbali hoja ya mawakili wa utetezi iliyokuwa ikidai kesi hiyo ni ya
madai na kwamba ifutwe.
Oktoba 18 mwaka jana, Ponda na wenzake walifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza ambapo wakili mwandamizi wa serikali Tumaini Kweka alidai washitakiwa hao wanakabiliwa na makosa matano na makosa hayo ni kama yafuatayo.
shitaka
la kwanza ni la kula njama kinyume na kifungu 384 cha Sheria ya Kanuni ya
Adhabu ya mwaka 2012,kwamba Oktoba 12 mwaka huu, huko eneo la Chang’ombe
Markasi washitakiwa wote walikula kwa nia ya kutenda kosa hilo.
Shitaka
la pili wakili Kweka alidai linawakabili washitakiwa wote ambalo ni la kuingia
kwa nguvu kwa nia ya kutenda kosa kinyume na kiufungu cha 85 na 35
cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu na kwamba Oktoba 12 mwaka huu,
huko Chang’ombe Markasi , kwa jinai wasipokuwa na sababu za
msingi washitakiwa hao waliingia kwenye kiwanja kinachomilikiwa
kampuni ya AgriTanzania Ltd kwania ya kujimilikisha kiwanja
hicho isivyo halali.
Kabla
ya washitakiwa hakubali au kataa shitala hilo Ponda aliripoka na kusema yeye
anakanusha shitaka hilo na kwamba washitakiwa wenzake nao wanalikanusha shitaka
hilo,jambo ambalo lilikataliwa na Hakimu Sanga ambaye alimrisha kila mshitakiwa
ajibu shitaka hilo kwa kinywa chake ambapo kila mshitakiwa kwa kinywa chake
alikanusha shitaka hilo kinyume na alivyokuwa anataka Ponda iwe kwa yeye
kukanusha shitaka hilo kwa niaba ya wenzake.
Wakili
Kweka alilitaja shitaka la tatu kuwa ni kujimilikisha kiwanja kwa
jinai kinyume na kifungu cha 86 na 35 cha sheria hiyo na kwamba kati ya
Oktoba 12-16 mwaka huu huko Chang’ambe Markasi pasipo na uhalali
wowote washitakiwa wote katika hali iliyokuwa ikipelekea
uvunjifu wa amani walijimilikisha kwa nguvu ardhi ya
kampuni ya Agritanza Ltd.
Shitaka
la nne, wakili Kweka alidai ni la wizi ambalo ni kinyume na kifungu cha
258 cha sheria ya Kanuni ya Adhabu ya mwaka 2002, na kuwa kati ya Oktoba
12-16 mwaka huu, washitakiwa hao waliiba vifaa na malighafi,matofali
1500,nondo,Tani 36 za Kokoto vitu vyote hivyo vikiwa na thamani ya Sh
59,650,000 mali ya kampuni ya Agritanza Ltd.
Aidha
shitaka la tano Kweka alidai ni la uchochezi ambalo linamkabili Sheikh Ponda
peke yake ambalo ni kinyume na kifungu cha 390 na 35 cha sheria
hiyo kwamba kati ya Oktoba 12-16 mwaka huu katika eneo hilo la Chang’ombe
Markasi kwa maelezo kuwa yeye ni Katibu wa Jumuiya na Taasisi za
Kiislamu(T) aliwashawishi wafuasi wake ambao ni washitakiwa hao
kutenda makosa hayo na kwamba upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.
“Mheshimiwa
hakimu pamoja na kuwasomea mashitaka hayo ambayo yanadhamana kwa mujibu wa
sheria, Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), Dk.Elizer Feleshi kwa mkono wake
amenituma kuwasilisha kwaniaba yake mahakamani hapo hati ya kufunga dhamana kwa
mshitakiwa wa kwanza (Ponda) peke yake chini ya kifungu cha 148(4) cha
Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 2012’alidai wakili Kweka.
Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Aprili 18 mwaka 2013.
MWANZO,MWISHO KESI YA SHEIKH PONDA HUU HAPA
*HUKUMU YA PONDA NI LEO APRILI 18
Na Happiness
Katabazi
FUATANA na
mwandishi wa makala haya Happiness Katabazi ambaye ni mwandishi wa habari za
mahakamani hapa nchini, ili uweze kufahamu kesi ya uchochezi na wizi wa
malighafi zenye thamani ya Sh.milioni 59 inayomkabili Katibu wa Jumuiya na
Taasisi za Kiislamu nchini, Sheikh Ponda Issa Ponda na wenzake 48,
ilipofunguliwa hadi kesho (Aprili 18) inapofikia
hatua ya mwisho kutolewa hukumu.
Mimi na
miongoni mwa waandishi wenzangu wa chache ambao mungu alitujalia uzima na afya
njema ambapo tuliweza kuifuatilia kesi hii tangu ilipofunguliwa rasmi mahakamani
hapo Oktoba 18 mwaka jana hadi kesho inapomalizika ,tuliweza kujifunza mambo
mengi ambayo yametupa faida sisi binafsi
ikiwemo faida ya kufahamu vyema jinsi ya aina ya kesi hii iliyohusisha
washitakiwa wengi ilivyoweza kuendeshwa na mawakili wa serikali na utetezi na
hakimu na wana usalama pia.
Kwani kesi
hii ya Ponda tangu ilipofunguliwa hadi kesho inatolewa hukumu, imekuwa
ikiendeshwa chini ya ulinzi mkali unaoratibiwa na wana usalama toka vyombo vya
ulinzi na usalama kwa njia zinaonekana na sizoonekana kwa urahisi.
Tunawashukuru
wana usalama wote walioendesha ulinzi siku ya kesi hii kwani walituwezesha hata
sisi waandishi wa habari za mahakamani kufanyakazi yetu kwa amani na uhuru
licha hapo mwanzo tulikuwa tukipokea vitisho kutoka kwa baadhi ya washitakiwa.
Aprili 18 mwaka huu; Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu
Mkazi Kisutu, Victoria Nongwa
,anatarajiwa kuketi katika kiti cha enzi na kutoa hukumu ya kesi hiyo
Na.245/2012 inayomkabili Ponda na wenzake.
Aprili 3 mwaka huu:Mawakili wa upande wa Jamhuri
,Tumaini Kweka na Jessy Peter na mawakili wa utetezi Juma Nassor na Njama
waliwasilisha majumuisho yao mahakamani hapo kwa njia ya maandishi ambapo
mawakili wa upande wa jamhuri waliiomba mahakama iwaone washitakiwa wote wana
hatia na wapewe adhabu kwa mujibu wa sheria.
Wakati
mawakili wa utetezi waliiomba mahakama iwaone washitakiwa hawana hatia na
iwaachilie huru kwa sababu hawakutenda makosa yanayowakabili na kwamba upande wa
jamhuri umeshindwa kuthibitisha kesi yao.
Machi 21 mwaka huu;Sheik Ponda, mshitakiwa wa tano
Mukadamu Swaleh walijitetea.Na washitakiwa wenzake wa nne nao walijitetea siku
hiyo na hivyo kufanya jumla ya washitakiwa 48 wa kesi hiyo kumaliza kutoa
utetezi wao.Na siku hii ndipo upande wa utetezi walifunga utetezi wao.
Machi 4 mwaka huu: Hakimu Nongwa atoa uamuzi wake ambapo aliwaona
washitakiwa wote wana kesi ya kujibu na akatupilia mbali hoja ya mawakili wa
utetezi iliyokuwa ikidai kesi hiyo ni ya madai na kwamba ifutwe.
Machi 6 mwaka huu:Washitakiwa kesi ya sheikh Ponda
waanza kujitetea mfululizo.Ambapo siku hiyu jumla ya washitakiwa saba
walijitetea.
Machi 7 mwaka huu: Jumla ya washitakiwa saba
walijitetea.
Machi 11 mwaka huu:Jumla ya
washitakiwa saba walijitetea.Hivyo hadi kufikia siku hiyo jumla ya washitakiwa
saba walikuwa wameishajitetea.
Machi 12 mwaka huu: Washitakiwa watatu tu ndiyo
walitoa utetezi siku hiyo na kufanya jumla ya washitakiwa waliotoa utetezi wao
kufikia 27.
Februali 18 mwaka huu: Mawakili wa pande zote mbili
wawasilisha kwa njia ya mdomo.Wakili wa upande wa Jamhuri Tumaini Kweka
awasilisha aiomba mahakama iwaone washitakiwa wote wana kesi ya kujibu
kwasababu upande wa jamhuri umeweza kuithibitisha kesi yake.
Na mawakili
wa utetezi nao waliomba mahakama iwaone washitakiwa hawana kesi ya kujibu
kwasababu jamhuri imeshindwa kuthibitisha kesi yao na kwamba kesi hiyo ni ya
madai ambayo inahusisha mgogoro wa ardhi hivyo ifutwe.
Februali 25 mwaka huu: upande wa jamhuri uliifunga kesi yake
baada ya mashahidi wake wa tatu kumaliza
kutoa ushahidi wao.Ambao ni shahidi wa 17,
D/C F8586 Ismail wa kituo cha Polisi Chang’ombe, shahidi wa 15 ambaye ni
F3929 D/C ,Constebo Eliaeli (35) ,shahidi wa 16 ambaye ni Stationi Sajenti Amos wa kituo cha Polisi Kati . Hivyo kufanya
upande wa jamhuri kuwa umeleta jumla ya mashahidi 17 na wakatoa ushahidi na
ulileta jumla ya vielelezo 13.
Februali 22 mwaka huu: shahidi 12,13
wa upande wa jamhuri watoa ushahidi wao. Shahidi wa 13, Koplo
Masiku ambaye ni Askari kituo cha polisi Chang’ombe ,shahidi wa 14 wa upande wa
Jamhuri D/C Koplo Zakayo.
Februali 21 mwaka huu; Shahidi wa 12 ambaye ni Mkuu wa upelelezi wa Makosa ya
Jinai wa Mkoa wa Kipolisi Temeke(RCO), Ame Anange Anoqie alitoa ushahidi wake
ambapo alisisitiza kuwa Ponda na wenzake
siyo wamiliki halali wa kiwanja cha
Chang’mbe Markas na kwamba waliingia kwa jinai katika kiwanja hicho.
Februali 20 mwaka huu: Shahidi wa 11 wa upande wa jamhuri
amabye ni Mpelelezi Mkuu wa kesi hiyo, Inspekta Thobias Walelo (34), ambaye alitoa vielelezo
vilivyopokelewa na mahakama kama kielelezo cha nane ambapo ni mapanga, Jambia, mabango,vipaza
sauti,masufulia ,majenereta alieleza
kuwa baada ya kuwakamata washitakiwa hao wakiwa na majambia, visu, vipaza
sauti, viloba viwili vya unga wa sembe, mikeka,mabango, visu,sufulia ,ndoo za
plastiki.
Walelo
alidai kuwa yeye akiwa ni mpelelezi mkuu wa kesi hiyo yeye na askari wenzake
walioenda kuwakamata washitakiwa hao
waliamua kuwabeba washtakiwa hao kwenye magari ya polisi kwa awamu mbili
na kisha kuwapeleka katika kituo cha polisi Kijitonyama ambapo waliwafikisha
saa 12 asubuhi na kuanza kuwahoji ambapo waliwahoji hadi Oktoba 18 mwaka jana ,
washitakiwa hao walifikishwa kwa mara ya kwanza mahakamani hapo wakikabiliwa na
kesi.
Februali 19
mwaka huu: Mahakama ya imetupilia mbali pingamizi la mawakili
wa upande wa utetezi lilokuwa linataka mahakama hiyo isipokee kama kielelezo maelezo ya ungamo yaliyotolewa
na mshitakiwa wa tano katika kesi hiyo
Mkadamu Swaleh Abdallah,polisi kama
kielelezo.Uamuzi huo ulitokana baada ya kufanyika kesi ndogo(Trial within a
Trial),baada ya mawakili wa utetezi kutaka maelezo ya onyo ya Mukadamu
yasipokelewe kama kielelezo kwasababu maelezo hayo si yake.
Februali
18:
Shahidi wa nane, D/c-Sajenti Mkombozi Mhando alidai kuwa
Novemba 11 mwaka jana, alikuwa Kituo Kikuu cha Polisi Kati akiwa na timu
ya wapelelezi wenzake toka Temeke yeye alipewa jukumu la kumhoji mshitakiwa wa
tano, Mukadam abdallah Swaleh ambapo alimpa haki zake zote.
Na kuanzia leo hadi leo hukumu inamalizika ulinzi
ulikuwa ni waina yake wakati kesi ilipokuja ikija mahakamani kwaajili ya kutajwa
na kusikilizwa.Ulinzi wa kesi hii ulikuwa ni waina yake ukilinganisha na ulinzi
unaotolewa wakati wa kesi nyingine kwani kesi hii wana usalama uweka vifaa
maalum katika ofisi za mapokezi ya
mahakama kwaajili ya kuwakagua watu wanaoingia.
Februali
28 mwaka huu;shahidi wa sita ambaye ni fundi mwashi Hamis Salum Mkangama(30), Shahidi wa saba,
William Milanzi(43) wa upande wa jamhuri walitoa ushahidi wao.
Januari 17 mwaka huu: shahidi wa nne Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini la
(BAKWATA),Masoud Ikome(72), amedai kuwa
kiwanja kilichopo Chang’ombe Markas ni
mali halali ya kampuni ya Agritanza Ltd na siyo mali waislamu(Bakwata).
Shahidi wa tano ambaye ni miongoni mwa Wakurugenzi wa
Kampuni ya Agritanza Ltd, Afidhi Seif
Othman (42), aliambia mahakama
kampuni yake ya Agritanza Ltd ilibadilisha eneo la Chang’ombe na Bakwata na
kwamba yeye ndiye alikuwa mmiliki wa eneo la Kisarawe na ndiye aliyeipatia
Bakwata eneo hilo na Bakwata ikawapatia eneo la Chang’ombe na kwamba
mabadilishano hayo yalifanyika Oktoba 10 mwaka 2010.
Desemba 18 mwaka 2012: Ponda anaishi gereza la Segerea,alishindwa kuletwa mahakamani hapo ambapo
kesi yake ilikuja kwaajili ya kutajwa kwasababu wakili Kweka alidai amepokea
taarifa toka kwa maofisa wa jeshi la Magereza kuwa Ponda ni mgonjwa.
Novemba 29 mwaka 2012: Shahidi wa kwanza Katibu Mkuu wa Bakwata,
Suleman Said Lolila(61),amekanusha madai yaliyotolewa na Sheikh Ponda na wenzake kuwa Bakwata siyo chombo cha
kuwakilisha waislamu wote hapa nchini.Na siku hii ndiyo ilikuwa ni siku ya
kwanza mashahidi wa upande wa jamhuri kuanza kutoa ushahidi wake.
Novemba
15 mwaka 2012: Wakili wa upande wa
Jamhuri Tumaini Kweka aliwasomea maelezo
ya awali washtakiwa hao ambapo alidai Bakwata ni chombo ambacho kinawawakilisha
waislamu wote, lakini Ponda na wenzake walikanusha madai yao na kusema kuwa
Bakwata haipo kwaajili ya kuwawakilisha waislamu wote.
Novemba
8 mwaka 2012: Mukadamu Swalehe aunganishwa kwenye kesi
hii Na.245/2012 inayomkabili Ponda na wenzake na hivyo kufanya sasa jumla
washitakiwa kuwa ni 51.Na Mukadamu amekuwa ni mshitakiwa wa tano.
Mkurugenzi
wa Mashitaka (DPP), Dk.Elezer Feleshi aliwasilisha mahakamani hapo hati ya
kumfungua dhamana Mukadamu kwaajili ya maslahi ya taifa chini ya kifungu cha 148(4)
cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 2002.
Kwa upande wake hakimu Nongwa alisema makosa
yanayomkabili mshtakiwa huyo yana dhamana ila kwakuw DPP-Feleshi amewasilisha
hati ya kumfungia dhamana, mahakama imefungwa mikono,haiwezi kutoa dhamana
kwasababu sheria iliyotumiwa na DPP kumfungia dhamana mshtakiwa huyo na Ponda
zimetungwa na Bunge, mahakama yenye ipo kwaajili ya kuzifuata sheria hizo
zilizotungwa na bunge katika kutoa uamuzi hivyo akaamuru mshitakiwa huyo
amepelekwe gerezani.
Pia siku hiyo hakimu Nongwa aliwapatia dhamana
washitakiwa wote dhamana isipokuwa Ponda na Mukadamu kwasababu DPP alikuwa
amewasilisha hati ya kufunga dhamana ya washitakiwa hao wawili.
Na hadi kesi hii
inamalizika kesho,washitakiwa hao wawili bado wanaendelea kuishi katika gereza
la Segerea kwasababu dhamana yao imefungwa na DPP tangu siku ya kwanza
walipofikishwa mahakamani hapo.
Oktoba 18 mwaka 2012: Ponda na wenzake walifikishwa kwa
mara ya kwanza mahakamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi Stewart Sanga, ambapo
wakili mwandamizi wa serikali Tumaini Kweka
alidai shitaka la
kwanza ni la kula njama kinyume na kifungu 384 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu
ya mwaka 2012,kwamba Oktoba 12 mwaka huu, huko eneo la Chang’ombe Markasi
washitakiwa wote walikula kwa nia ya
kutenda kosa hilo.
Shitaka la pili wakili Kweka alidai
linawakabili washitakiwa wote ambalo ni la kuingia kwa nguvu kwa nia ya kutenda kosa kinyume na kiufungu cha 85 na 35 cha Sheria
ya Kanuni ya Adhabu na kwamba Oktoba 12 mwaka huu, huko Chang’ombe Markasi , kwa jinai wasipokuwa na sababu za msingi
washitakiwa hao waliingia kwenye
kiwanja kinachomilikiwa kampuni ya AgriTanzania
Ltd kwania ya kujimilikisha kiwanja hicho isivyo halali.
Kabla ya washitakiwa hakubali au kataa
shitala hilo Ponda aliripoka na kusema yeye anakanusha shitaka hilo na kwamba
washitakiwa wenzake nao wanalikanusha shitaka hilo,jambo ambalo lilikataliwa na
Hakimu Sanga ambaye alimrisha kila mshitakiwa ajibu shitaka hilo kwa kinywa
chake ambapo kila mshitakiwa kwa kinywa chake alikanusha shitaka hilo kinyume
na alivyokuwa anataka Ponda iwe kwa yeye kukanusha shitaka hilo kwa niaba ya
wenzake.
Wakili Kweka alilitaja shitaka la tatu
kuwa ni kujimilikisha kiwanja kwa jinai kinyume na kifungu cha 86
na 35 cha sheria hiyo na kwamba kati ya
Oktoba 12-16 mwaka huu huko Chang’ambe
Markasi pasipo na uhalali wowote
washitakiwa wote katika hali iliyokuwa ikipelekea uvunjifu wa amani walijimilikisha kwa nguvu ardhi ya
kampuni ya Agritanza Ltd.
Shitaka la nne, wakili Kweka alidai ni
la wizi ambalo ni kinyume na kifungu cha
258 cha sheria ya Kanuni ya Adhabu ya
mwaka 2002, na kuwa kati ya Oktoba 12-16 mwaka huu, washitakiwa hao waliiba vifaa na
malighafi,matofali 1500,nondo,Tani 36 za Kokoto vitu vyote hivyo vikiwa na
thamani ya Sh 59,650,000 mali ya kampuni ya Agritanza Ltd.
Aidha shitaka la tano Kweka alidai ni la
uchochezi ambalo linamkabili Sheikh Ponda peke yake ambalo ni kinyume na kifungu cha 390 na 35
cha sheria hiyo kwamba kati ya Oktoba
12-16 mwaka huu katika eneo hilo la Chang’ombe Markasi kwa maelezo kuwa yeye ni Katibu wa Jumuiya na
Taasisi za Kiislamu(T) aliwashawishi
wafuasi wake ambao ni washitakiwa hao
kutenda makosa hayo na kwamba
upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.
“Mheshimiwa hakimu pamoja na kuwasomea
mashitaka hayo ambayo yanadhamana kwa mujibu wa sheria, Mkurugenzi wa Mashitaka
(DPP), Dk.Elizer Feleshi kwa mkono wake amenituma kuwasilisha kwaniaba yake
mahakamani hapo hati ya kufunga dhamana kwa mshitakiwa wa kwanza (Ponda) peke
yake chini ya kifungu cha 148(4) cha
Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 2012’alidai wakili Kweka.
Kwa upande wake wakili wa shitakiwa hao
Mansoor alidai anashangazwa na DPP-Dk.Feleshi kuwawasilisha hati hiyo ya
kumfungia Ponda dhamana wakati dhamana ni haki ya Kikatiba na kwamba hati hiyo
ya DPP imetaja sababu mbili ambazo ni mosi kwaajili ya usalama na sababu ya
pili ni maslahi ya jamhuri.Nakuongeza kuwa sababu hizo hazijafafanuliwa kwa
mabana na kudai kuwa washitakiwa wameishakaa kwa muda mrefu rumande na kwamba
mshitakiwa wanne ni mwanamke mwenye umri wa 100 hivyo anaomba wapatiwe dhamana.
Akijibu hoja hizo wakili wa serikali
Kweka alidai anashangazwa na hoja za wakili washitakiwa za kuikosoa hati hiyo
iliyowasilishwa na DPP kwasababu kifungu cha 184(4) cha Sheria Makosa ya Jinai,
kinasomeka wazi kuwa hati hiyo ya DPP
hata mahakama haiwezi kuipinga na kwamba inapowasilishwa mahakamani hati
hiyo mahakama inakuwa imefungwa mikono
na kwamba mwenye mamlaka ya kuiondoa makamani hapo ni DPP mwenyewe siku
atapoona inafahaa kuiondoa na sivinginevyo.
Hata hivyo hakimu Sanga alisema hivi
baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili; “Kama nilivyokwisha sema tangu
awali naingia kuanza kusikiliza kesi hii kuwa mimi siyo hakimu niliyepangwa
kusikiliza kesi hii ,aliyepangwa kusikiliza kesi hii ni Hakimu Victoria Nongwa
ambaye yupo kwenye semina kwahiyo endapo
pande zote mbili katika kesi hii mnataka kuwasilisha hoja zenu msubirini Hakimu
Nongwa akimaliza semina yake mje muwasilishe hoja hizo mbele yake”alisema
Hakimu Sanga.
Hata hivyo wakili washitakiwa Mansoor
alionekana kutoridhishwa na jibu hilo aliinuka na kumuomba hakimu Sanga
aiarishe kesi hiyo hadi leo ili washitakiwa 49 waletwe leo kwaajili ya kupatiwa
dhamana kwasababu makosa yao yanadhamana lakini hakimu Sanga alisema
haitawezekana kwasababu Hakimu Nongwa bado yupo kwenye semina na leo hatakuwepo
mahakamani hapo na hivyo akaamuru washitakiwa hao warejeshwe rumande hadi
Novemba mosi,kesi hiyo itakapokuja kwaajili ya kutajwa.
Baada ya
kesi hiyo kumaliza wanausalama walikuwa wamejazana kwa mtindo tofauti
ndani ya ukumbi huo wa mahakama waliwataka waandishi wa habari na watu wengine
watoke nje na ndani wabaki washitakiwa peke yake na wanausalama na kisha
wakatolea mlango wa nyuma washitakiwa hao na kisha kwenye kuwapakiza kwenye
mabasi ya Jeshi la Magereza, Karandika na Defenda tayari kwaajili ya kuanza
safari ya kupeleka gerezani ambapo
magari ya askari wa usalama Barabarani walilazimika kuifunga barabara
iliyopakana na mahakama hiyo kwa muda kwaajili ya kuruhusu msafara wa zaidi ya
magari saba yaliyokuwa yamebeba washitakiwa hao,wanausalama kuelekea gerezani.
Baadhi ya watu waliofika mahakamani hapo
kusikiliza kesi hiyo ,walizungumza na gazeti hili walisema wamefurahishwa na
hatua ya serikali ya kuwafikisha washitakiwa hao mahakamani kwani Tanzania ni
nchi inayoongozwa kwa Sheria na Katiba ya nchi na siyo sheria za dini ya
Kiisilamu.
Facebook:happy
katabazi :Aprili 18 mwaka 2013.
Simu.0716 -774494.