Header Ads

URANIUM YAWAPELEKA JELA

Na Happiness Katabazi
 
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, imewahukumu watu wawili kwenda jela miaka mitatu kwa kosa la kukutwa wakilimi madini aina ya Uranium Kg. 6.5.
Hukumu hiyo ilitolewa jana na Hakimu Mkazi Gene Dudu ambaye aliwataja washitakiwa waliokuwa wakikabiliwa na kesi hiyo ya mwaka 2012 ni Duncan Mwananemela(41) na Silvia Mwemis (42) ambapo Julai  30 mwaka jana wakili wa serikali alidai washitakiwa hao wanakabiliwa na kosa la kukutwa wakimiliki  madini yenye mionzi mikali kinyume na kifungu cha 11(1),(2) cha Sheria  Na.7 ya  Nguvu   za Atomiki ya mwaka 2003.
 
Hakimu Dudu alisema ili kuthibitisha kesi hiyo upande wa jamhuri uliokuwa ukiwakilishwa na wakili wa serikali Charles Anindo ulileta mashahidi wa nne ambao wameweza kuthibitisha kesi yao na kwamba mahakama yake imefikia uamuzi wa kuwakuta na hatia wa kosa hilo washitakiwa wote wawili.
 
Na katika ushahidi wa jamhuri ulionyesha kuwa baada ya kupimwa madini yenye mionzi mikali waliyokutwa nayo washitakiwa ambayo walikuwa wameyaifadhi kwenye vyumba wanavyolala majumbani kwao, ni Uranium  na kwamba kisayansi  madini hayatakiwi kuwekwa karibu na makazi yanayoishi binadamu  kwani madini hayo ya madhara makubwa ambayo  yakiwekwa katika makazi ya watu yanasababisha  ulemavu, yanaaribu mfumo wa uzazi,kuaribu Ini na Figo na kwamba kama yatalazimika madini hayo kuwekwa kwa  watu  basi madini hayo yanatakiwa yafungwe  kitaalamu  ambapo licha yakuwa yamefungwa kitaalam madhara yatokayo na mionzi hiyo iliyofungwa kitaalamu na kukaa kwenye makazi wanayoshi binadamu yanaweza kujitoka miaka mitatu baadaye.
 
“Nawahukumu kwenda jela miaka mitatu au kulipa faini ya Sh.milioni tatu kwani sheria ya Nguvu ya Atomiki inatoa adhabu hiyo….lakini mahakama hii imewatizama washitakiwa wote na imeona hamna huwezo wa kulipa fidia hiyo na kwa mujibu wa utetezi wa washitakiwa walidai kuwa walikuwa hawaelewi na madhara yatokanayo na mtu kimiliki madini hayo ya kemikali ;
 
‘Hivyo basi mahakama hii licha imewahukumu kwenda jela miaka mitatu pia inaamuru washitakiwa waende gerezani kwa siku 14 kuanzia leo na katika kipindi cha siku hiyo watakuwa chini ya ungalizi wa maofisa wa Ustawi wa jamii ambao watakuwa wakiwaangalia kama wanatabia njema na kama wataonyesha tabia njema mahakama hiyo itakuja kuwabadilishia adhabu ambapo itakuja kuwapatia adhabu ya kuja kutumikia kifungo cha nje”alisema Hakimu Dudu.
 
Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Agosti 16 mwaka 2013.

No comments:

Powered by Blogger.