Header Ads

ZUNGU:KORTI ITUPE OMBI LA TAO

Na Happiness Katabazi

MBUNGE wa jimbo la Ilala(CCM) Musa Azzan ‘Zungu’ amewasilisha pingamizi la awali katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, akiomba mahakama hiyo itupilie mbali ombi la aliyekuwa mgombea wa jimbo hilo katika Uchuguzi Mkuu wa mwaka 2010,Hamad Tao linalotaka mahakama hiyo imsamehe kulipa dhamana ya kesi hiyo.

Katika kesi hii ya Uchaguzi Na.104/2010, Tao ambaye hana wakili anamshtaki mbunge wa Jimbo hilo Mussa Azzan anayetetewa na wakili wa kujitegemea Joseph Tadayo, aliyekuwa msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo, Tume ya Taifa ya Uchaguzi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambao wanatetewa na wakili wa serikali Rashid Karimu.Katika kesi ya msingi Tao anaimba mahakama itengue ubunge wa Zungu kwasababu hakushinda kihalali na taratibu za sheria ya Uchaguzi zilikiukwa.

Kesi hiyo ambayo ilikuja jana kwaajili ya kutajwa mbele ya Msajili wa Wilaya wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Amir Msumi wakili wa mdaiwa Zungu(Tadayo) aliambia mahakama amewasilisha pingamizi dhidi ya mlalamikaji(Tao) la kutaka mahakama ikatae ombi la mlalamikaji lakutaka mahakama hiyo itoe amri ya kumsamehe asilipe dhamana ya kesi hiyo ambayo ni sh milioni tano kwa kila mdaiwa;

“Tunaomba ombi la Tao litupwe kwasababu sheria ya Uchaguzi tya mwaka 2002 hairuhusu mahakama kumsamehe mlalamikaji asilipe dhamana ya kesi ya uchaguzi aliyoifungua dhidi ya wadaiwa…hivyo tunasisitiza ombi la mlalamikaji litupwe na mahakama hii imuamulu mlalamikaji huyo alipe sh milioni tano kwa kila mdaiwa aliyemshtaki”alisema wakili Tadayo.

Kwa upande wake Msajili Msumi alimtaka Machi 28 na akaiarisha kesi hiyo Aprili 5 mwaka huu , ili mahakama hiyo ije kusikiliza pingamizi hilo la awali lilowasilishwa jana asubuhi na mdaiwa ambaye ni mbunge wa Ilala Azzan.

Wakati huo huo ; kesho mahakama hiyo itaanza kusikiliza ombi la aliyekuwa mgombea ubunge wa Jimbo la Kawe kwa tiketi ya Chama Cha NCCR-Mageuzi,James Mbatia linaloiomba mahakama hiyo impangie kiwango nafuu cha fedha za kuweka dhamana mahakamani kwaajili ya kesi ya kupinga ubunge mbunge wa sasa wa jimbo jilo Halima Mdee(Chadema) na wenzake.

Msajili wa Wilaya wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Amir Msumi ambaye amepangwa kusikiliza katika hatua za awali kesi za uchaguzi wa majimbo ya mkoa wa Dar es Salaam,alisema kesi hiyo jana ilikuja kwaajili ya kupangiwa tarehe ya mahakama kusikiliza ombi la mlalamikaji(Mbatia) anayetetewa na wakili wa kujitegemea Mohamed Tibanyendera, pia alimwamuru wakili wa Mdee, Edson Mbogoro ambaye jana ndiyo ilikuwa ni mara yake ya kwanza kuudhuria kesi hiyo tangu ilipofunguliwa aakishe hadi saa tisa jioni jana awe amewasilisha mahakamani majibu ya kiapo cha Mbatia.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumatano, Machi 23 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.