Header Ads

AG,MAHANGA WAOMBA KESI YA MPENDAZOE IFUTWE

Na Happiness Katabazi

MWANASHERIA Mkuu wa Serikali na Naibu Waziri Dk.Makongoro Maganga wamewasilisha mapingamizi matatu ya kuomba Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, iifute kesi ya kupinga matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 wa Jimbo la Segerea iliyofunguliwa na aliyekuwa mgombea wa Ubunge (CHADEMA) Fred Mpendazoe dhidi ya Mbunge wa sasa Mahanga, kwa madai kuwa hati ya madai ya kesi hiyo ina mapungufu.


Mbali na Mahanga ambaye anatetewa na wakili wa kujitegemea Jerome Msemwa,wadaiwa wengine katika kesi hiyo ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali na aliyekuwa msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la Segerea ambao wanatetewa na wakili wa serikali David Kamwaga.

Kesi hiyo ambayo ilikuja jana mbele ya Jaji Profesa Ibrahim Juma kwaajili ya kuanza kusikilizwa,wakili wa serikali alidai kuwa upande wa AG,una mapingamizi mawikili ambayo wanaomba ama kesi hati ya madai ya kesi hiyo ifanyiwe marekebisho au kesi ifutwe kwa kabisa kwasababu kuna baadhi ya paragrafu zimenasomeka kuwa Mpendazoe anaidi vituo 120 vya Kiwalani,vituo viwili vya Buguruni, vituo viwili vya Kipawa ambavyo vyote hivyo vilikuwa ni vituo vya kupigia kura na kura kura zake hazikuhesabiwa.

Wakili huyo wa serikali alidai pingamizi la kutaka kesi ifutwe ni kwa hati hiyo ya madai kushindwa kutaja majina ya majina ya wasimamizi wa Uchaguzi waliokiri kuwa kuna baadhi ya vituo walijumlisha kura za matokeo katka makaratasi ambayo hayakuwa yameandaliwa na Tume ya Uchaguzi kwaajili ya kujumlishia matokeo.

Kwa upande wake wakili Mahanga, Msemwa alianza kwa kudai kuwa yeye alikuwa na jumla ya mapingamizi mawili yakutaka kesi hiyo ifutwe lakini pingamizi moja kwa hiari yake ameamua kuliondoa na badala yake akawasilisha pingamizi moja ambalo linaomba kesi ifutwe kwasababu mlalamikaji alifungua kesi hiyo moja kwa moja kwa jaji wakati kesi hizo za usajili zinatakiwa katika hatua za awali zianze kusikilizwa na Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam.

Akipangua mapingamizi hayo, wakili wa Mpendazoe, Peter Kibatara aliomba mahakama hiyo iyatupilie mbali mapingamizi hayo kwasababu hayana msingi.Akichambua mapingamizi ya wakili wa serikali ,alidai kuwa kama kweli walikuwa wakitaka kufahamu majina ya vituo ambavyo kura zao hazikuhesabiwa na majina ya wasimamizi wa uchaguzi ambao walikiri kuwa walijumla kura katika karatasi ambazo hazijatolewa na Tume ya Uchaguzi, wadaiwa hao walipaswa wawasilishe maombi mahakamani ya kuomba upande mlalamikaji(Mpendazoe)awapatie majina ya vituo na majina ya wasimamizi hao na kuongeza kuwa Sheria ya Kesi za Madai ya mwaka 2002, inawataka wafanye hivyo na kwamba anashangaa wameshindwa kuwasilisha maombi hayo mahakamani badala yake wanakimbilia kuomba kesi ifutwe.

Wakili Kibatara akijibu pingamizi la Msemwa, alidai pingamizi hilo pia halina msingi kwani kiutaratibu siku zote mlalamikaji anayefungua kesi za madai jukumu lake nikuwasilisha hati yake ya madai katika masijala ya kesi za madai mahakamani na uongozi wa masijala hiyo ndiyo wenye jukumu la kupeleka hati hiyo ya madai kwa mamlaka husika ambapo mwisho wa siku mamlaka husika za mahakama ndiyo umpanga jaji wa kusikiliza kesi husika na kuongeza kuwa wao walifuata taratibu zote za kufungua kesi hiyo katika masijala ya madai mahakamani hapo na wakalipia ada kufungulia kesi na mwisho wa siku mahakama hiyo ndiyo iliyowapatia jina la jaji wa kusikiliza kesi hiyo.

Kwa upande wake Jaji Profesa Ibrahim Juma ambaye awali alipanga kuanza kusikiliza kesi mfululizo kuanzia jana hadi kesho, alisema amesikiliza hoja zote zilizowasilishwa na pande mbili na anaiarisha kesi hiyo hadi Juni 6 mwaka huu, ambapo siku hiyo atatoa uamuzi kuhusu hoja hizo.

Novemba mwaka jana Mpendazoe alifungua kesi ya kupinga matokeo ya Uchaguzi wa Jimbo hilo ambayo yalimtangaza mbunge wa sasa Dk.Mahanga kuwa ndiye mshindi kwasababu uchaguzi huo ulikiuka matakwa ya sheria ya Uchaguzi.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Alhamisi, Mei 26 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.