Header Ads

KESI YA SAMAKI WA MAGUFULI-MELI HAIKUWA NA KIBALI CHA UVUVI-SHAHIDI

Na Happiness Katabazi

KAMISHNA Msaidizi wa Polisi(ACP) Charles Mkumbo(46) ameieleza Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, kuwa ndugu wawili wa raia wa kigeni 36 wanaokabiliwa na kesi ya uvuvi haramu katika Bahari ya Hindi katika kina kirefu cha Ukanda wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania walimpatia kibali cha uvuvi cha meli ya Tawariq 1 ambacho kilikuwa kimeisha muda wake.


ACP-Mkumbo alitoa maelezo hayo wakati akiongozwa kutoa ushahidi wake na wakili Mwandamizi wa Serikali Biswalo Mganga na Prosper Mwangamila alidai kuwa yeye ndiye aliyeongoza timu ya makachero wa Jeshi la Polisi kufanya upekuzi wa meli na washtakiwa hao alidai kuwa Machi 10 mwaka 2009 ambaye ndiye alikuwa Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalum ya Dar es Salaam(ZDCO) siku hiyo alikuwa bandarini na timu yake.

Mkumbo ambaye hivi sasa anafanyiakazi Makao Makuu ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai siku hiyo raia wawili China ambao ni Zhao na Xhu ambao nao ni washtakiwa walimfuata na kujitambulisha kwake kuwa wao ni mawakala wa Tawariq 1 ambao wametokea Mombasa na wakamtaka awaachie mara moja raia hao wa kigeni kwa madai kuwa walikuwa wakipita katika Bahari ya Hindi ukanda wa Tanzania kuelekea Mombasa nchini Kenya.

“Minilikataa kuwachiria huru na kuwaeleza nilipata taarifa za kipelelezi kuwa raia hao wakigeni walikuwa wakivua bila leseni kwenye eneo la Tanzania na kitendo hicho ni kosa ....na washtakiwa hao wakanijibu kuwa walikuwa na kibari cha kuvua na nikawataka wathibitishe hilo ndio Zhao leseni inayoirusu meli hiyo ivue;

“Niliisome hiyo leseni ambayo inayoonyesha imetolewa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa meli ya Tawariq 1 na kwamba leseni hiyo ilimalizika muda wake wa matumuzi Desemba 22 mwaka 2008.Ndipo nikaanza kutilia mashakata kauli hizo mbili wale ndugu zao wawili walisema washtakiwa hao walikuwa wakipita njia na meli yao wakielekea Mombasa na leseni hiyo inayonyesha imekwisha muda wake na mimi kama mpelelezi mkuu nilifikia uamuzi wa kuwakamata hata hao ndugu wawili na kuwaunganisha na washtakiwa hao wengine ambao jumla yake sasa wapo 36.

Aidha Mkumbo alidai kuwa hadi yeye na timu yake wanamaliza upelelezi kuhusu kesi hiyo hajawahi kupata mawasiliano toka ofisi za balozi zozote za kigeni wala Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa nchi kuhusu ukamatwaji wa meli hiyo.Jaji Agustine Mwarija aliairisha kesi hiyo hadi Jumatatu shahidi wa 13 atakapoanza kutoa ushahidi wake.Kesi hiyo imepangwa kusikilizwa mfululuzio hadi Mei 31 mwaka huu.

Machi 9 mwaka 2009 washtakiwa hao walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na makosa ya uvivu haramu katika kina kirefu cha habahari ya Hindi Ukanda wa Tanzania na kuharibu mazingira ya ukanda huo.Hadi sasa washtakiwa wanaendelea kusota rumande kwa kukosa dhamana.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumamosi,Mei 21 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.