Header Ads

FM ACADEMIA WANAREKODI NYIMBO MPYA

 MuleMule FBI
Kingombe Blaise 'KingBlaise'





FM ACADEMIA WANAREKODI NYIMBO MPYA

Na Happiness Katabazi
BENDI ya FM Academia (Wazee wa Ngwasuma) ,hivi sasa wapo Studio  wanarekodi nyimbo mpya .

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Mhasibu wa bendi hiyo Calvin Mkinga alisema nyimbo ambazo zimeanza kurekodiwa ni wimbo wa Watabiri uliotungwa na Mulemule FBI na Bodaboda Kariakoo ulitungwa na Kingombe Blaise'Kingblaise'   na kwamba wanarekodi nyimbo hizo katika studio ya Metro, watunzi wa nyimbo hizo ni hapo pichani.


Mkinga alisema Redio na Televisheni zimetoa masharti kwa bendi za muziki wa dansi nchini kuwa ili ziwe zinapiga nyimbo za bendi za muziku wa dansi ni lazima bendi hizo zitunge nyimbo zitakazoimbwa kwa dakika chache kwani mifumo ya utangazaji iliyofungwa katika vituo vya redio na Televisheni ni mfumo wa kisasa ambao hautaki kupiga wimbo  wenye dakika nyingi,unaitaji wimbo uwe ni wa dakika nne tu.

' Wanamuziki wetu walizoea kutunga wimbo unaopigwa kwa dakika 15 sasa hivi sharti linataka watunge nyimbo zenye dakika nne na tayari wanamuziki wetu wameishatunga nyimbo kadhaa nazimeishaanza kurekodiwa na kwamba jumla wanatarajia kurekodi jumla ya nyimbo sita.alisema Mkinga.

Chanzo: Facebook: Happy Katabazi
Blog: www.katabazihappy.blogspot.com
0716 774494
Aprili 20 mwaka 2015.

No comments:

Powered by Blogger.