Header Ads

KATABAZI NA JAJI FRANCIS MUTUNGI



Kaka yangu Jaji Francis Sales Mutungi Katabazi ambaye kwasasa ndiye Msajili wa Vyama Vya Siasa nchini, enzi zile akiwa na cheo cha Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Msajili wa Mahakama ya Rufaa nchini, Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma, Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, nilipata kufanyakazi nae kwa karibu ,mimi nikiwa Mwandishi wa Habari za Mahakamani na ofisa Mwandamizi wa Mhimili wa Mahakama.

Mara kwa mara Jaji Mutungi alikuwa akipenda kunieleza kuwa kiongozi mzuri au mtoaji mzuri wa maamuzi ni yule ambaye kabla ya kutolea uamuzi jambo lolote lile liloamsha hisia tofauti katika jamii au binafsi anakuwa kwanza ametulia kabisa na ameondokana na jazba na mihemko ya aina yoyote.

Kwani anaamini kutolea tamko,uamuzi jambo fulani linalohusu serikali na mamlaka zake kwa pupa unaweza kujikuta unatoa maamuzi mabovu. Na kwamba ni vema kiongozi,au mtu wa kawaida uchelewe kutoa uamuzi lakini siku ukitolea uamuzi jambo fulani au taarifa fulani ziwe zimemaliza tatizo.

Na Jaji Mutungi ni kiongozi wa aina hiyo ambaye hata lililipokuwa likitokea jambo linalohusu mhimili wa Mahakama au yeye binafsi alikuwa akurupuki kutolea msimamo.

Hata sisi 'Wambea wa Mahakamani' tulipokuwa tukimvamia ofisini kwake kumuomba atolee tamko masuala hayo alikuwa akisema tumpe muda atatolea tamko na kweli baada ya mihemko na jazba za watu kuhusu jambo fulani kupungua ndiyo alikuwa akiibuka huku akiwa na taarifa zenye takwimu na kutolea tamko.

Jaji Mutungi ambaye ni Msomi wa Sheria mwenye silika ya kujiamini, nitamkumbuka siku zote kwa mbinu hiyo aliyokuwa akinipatia,mwanzo nilikuwa simwelewi ila kwasasa nimekubaliana na mbinu yake hiyo.

Mungu akupe afya njema na maisha marefu na hekima na busara hasa katika mwaka huu wa uchaguzi Mkuu ambapo Ofisi yako ya Msajili wa Vyama vya siasa nayo inahusika kwa sehemu fulani.

Picha hii tulipiga wakati Mutungi akiwa Msajili wa Mahakama ya Rufaa nchini na kabla Rais Jakaya Kikwete ajamteua kuwa Jaji wa Mahakama Kuu na kisha kumteua kuwa Msajili wa vyama vya Siasa nchini.

By Happiness Katabazi, Aprili 25 mwaka 2015.

No comments:

Powered by Blogger.