Header Ads

HIVI DAVID KAFULILA NI MZIMA KWELI?





Na Happiness Katabazi

MEI 11 mwaka huu, katika kipindi 45 kinachorushwa na Televisheni ya ITV alihojiwa Waziri Kivuli wa Viwanda na Biashara, David Kafulila ambapo alizungumzima mambo mbali mbali likiwemo suala la akaunti ya Tegeta Escrow.

Mbali na kuhojiwa katika kipindi hicho pia katika taarifa ya habari  ya ITV , Kafulila alihutubia wakazi wa Shinyanga ambapo alisema akubaliani na ripoti ya uchunguzi kuhusu tuhuma za kashfa ya sakata la Escrow iliyotolewa Mei 8 mwaka huu na Katibu Mkuu Kiongozi ,Balozi Ombeni Sefue ambayo ilimuona aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospiter Muhongo na aliyekuwa Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Eliakim Maswi kuwa hawana hatia.

Kafulila kupitia taarifa ya habari hiyo akiwajaza ujinga wakazi wa Shinyanga ambapo alisema hakubaliani na taarifa hiyo ya Ikulu na kwamba taarifa hiyo imewasafisha vigogo hao ambao hawakustahili kusafishwa na kwamba anaenda kulianzisha upya bungeni jambo hilo la Escrow kwasababu eti pia kwenye Escrow kuna nyaraka zilizoghushiwa na serikali iwataje waliokula fedha za Escrow kupitia benki ya Stanbic.

Katika kipindi DK 45 , baadhi ya mambo aliyoyazungumza alizungumzia pia  suala la Escrow kwamba linahusisha vigogo wengi  na serikali kwakuwa haina utawala bora haijawashughulikia ipasavyo vigogo hao na kwamba suala la Escrow lilisababisha shilingi kuporomoka na kuwa kuna nyaraka za serikali zilighulishiwa ili wapate fedha za Escrow na cha ajabu mtoaji rushwa kwa maofisa hao wa serikali, mahakama   na mtoaji rushwa James Lugemalira  hajakamatwa.

Itakumbukwa kuwa Bunge liloketi mwishoni mwa mwaka jana ndio lilofunga mjadala wa sakata la Escrow baada ya kutoa maazimio yaliyotokana na uchunguzi uliofanywa na Kamati ya PAC iliyokuwa ikiongozwa na aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA),Zitto Kabwe  ambaye alijizulu nafasi ya uenyekiti wa PAC na ubunge baada ya kufukuzwa uanachama na chama chake cha awali cha Chadema.

Katika makala yangu ya Mei 10 mwaka huu, iloyokuwa na kichwa cha habari kisemacho: ( ZITTO,KAFULILA NA WAZANDIKI WENZENU MMESHUSHUKA  SHUU!!!)

Moja ya aya makala hiyo niliaidi kuwa sitaacha Kafulila aendelee kuzungumzia suala la Escrow ndivyo sivyo na kwamba nitatumia karamu yangu kumhoji hivyo na leo tena nimetumia kalamu yangu kumhoji Kafulila kuhusu mambo ya Escrow aliyoyajadili jana.

Itakumbukwa pia Kafulila wakati alipokuwa mwanachama wa Chadema, wakati akiwa Chadema na kudaiwa kuleta chokochoko, Katibu Mkuu wa Chadema,Dk.Wilbroad Slaa alipohojiwa na vyombo vya habari kuhusu taarifa za Kafulila kuleta chokochoko ,Slaa alimfananisha Kafulila na sisimizi lakini pia wakati sakata la Escrow limeshika kasi aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Fredrick Werema ambaye alijiuzulu kwa kile alichokieleza kuwa ushauri wake umeeleweka vibaya alimfananisha Kafulila na Tumbili.Werema na Slaa walikuwa na sababu za kumpachika  majina hayo ambayo hayapendezi.

Katika sakata la Escrow , Kafulila alikuwa ni mtoa taarifa tu, Kamati ya PAC ikafanyia kazi taarifa yake na ikasoma bungeni matokeo ya uchunguzi wake na bunge liliibuka na maazimio yake ambayo iliitaka serikali iyafanyie kazi.

Na kweli serikali kupitia vyombo vyake vikaanza kufanyia kazi ikiwemo Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU), ikawafikisha mahakamani baadhi ya maofisa wa serikali kwa makosa ya kupokea rushwa tu  kutoka kwa James  Lugemalila na kesi hizo zinaendelea katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam.

Pia watuhumiwa wengine ambao makosa yao hayaangukii katika jinai ,yameangukia katika makosa ya ukiukwaji wa maadili ya watumishi wa umma,wamefunguliwa mashauri katika Tume ya Sekretarieti ya Maadili ambao ni Professa Anna Tibaijuka, Andrew Chenge, Mnikulu  Shabani Gurumo na bado mashauri yao hayajatolewa weuamuzi.

Katika kuonyesha serikali imeyafanyia kazi kwa vitendo maazimio yale ya bunge ,pia ilimsimamisha kazi Maswi ili kupisha uchunguzi, Rais alimtimua kazi aliyekuwa Waziri wa Ardhi na Makazi Professa Tibaijuka , Muhongo alijiuzulu wadhifa wake na pia ikaunda timu ya kuchunguza tuhuma kama Profesa Muhongo,Maswi wanahusika  au la.

Ripoti ya uchunguzi iliyoyolewa na Mei 8 mwaka huu na Balozi Sefue imesema uchunguzi umebaini Muhongo na Maswi ni watu safi kwani hakuna ushahidi ulionyesha walishiriki kutenda makosa ya jinai au utovu wa maadili katika sakata la Escrow.

Hivyo  wapo huru na siyo mafisadi wa Escrow kama tulivyoamishwa na Kafulila,Zitto na wazushi wengine.

Kwa kuwa serikali imeishatekeleza maazimio ya bunge kwa sehemu kubwa,iweje leo hii suala la Escrow ambalo limeishamalizika, Kafulila ambaye alikuwa ni mtoa taarifa tu aibuke kwenye majukwaa ajiapize kuanzisha upya sakala la Escrow?

Inakuwaje tena Kafulila aibuke aseme kwenye Escrow kulikuwa na nyaraka zilizoghushiwa?

Kuonyesha Kafulila hivi sasa ni kama mtu aliyechanganyikiwa anapanda majukwaani na kufunga safari hadi kwenye TV kwenda kusema eti nyaraka zilighushiwa bila kuonyesha nyaraka hizo anazodai zimegushiwa.

Hilo suala la kughulishi ulilitolea taarifa katika vyombo husika?Kama ulilitolea taarifa mbona katika maazimio ya Bunge hatukusikia kuwa uchunguzi wao ulibaini nyaraka za serikali zilighushiwa  na vigogo wa serikai ili wapate fedha za Escrow?

Uchunguzi uliofanywa na Takukuru,Polisi,CAG haujabaini kuwepo makosa ya nyaraka za serikali kughushiwa ndiyo maana hakuna aliyeshitakiwa kwa makosa ya kughushi, wizi na ndiyo maana nasema nanitaendelea kusema wewe,Zitto na wazandiki wenzenu ni mlizushia watu na kuwaundia makosa ya wizi wakati hakuna makosa ya wizi waliyoyatenda.

Chombo chenye mamlaka ya kuchunguza na kuthibitisha kuwa nyaraka fulani imeghushiwa ni kitengo cha utambuzi wa Maandishi na ofisi yake ipo chini ya ofisi ya Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai(DCI) ,pale Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Dar es Salaam.

Tumuulize huyu Kafulila hayo mamlaka ya kuthibitisha nyaraka za Escrow eti zilighushiwa ameyapata wapi?

Maana hakuna mamlaka yoyote wala mtu yoyote yenye mamlaka ya kuthibitisha eti nyaraka fulani imeghushiwa au laa isipokuwa Kitengo hicho cha Utambuzi wa Maandishi kilichopo ndani ya Jeshi la Polisi(Forensque Bureu).

Labda mwenye ubongo wa sisimizi ndio anaweza kujitapata anayo mamlaka hayo ya kusema nyaraka fulani imeghushiwa wakati akijua hana mamlaka hayo.

Kuhusu hoja ya Kafulila jana kuwa serikali hii haina utawala bora; binafsi niliposikiliza jana kwenye Televisheni ,kwanza kauli yake ya kuiomba serikali iwataje majina ya vigogo waliochukuwa fedha za Escrow kwa kutumia Benki ya Stanbic ni wazi anaimani na serikali kuwa inauwezo wa kufanyakazi na ina utawala bora isipokokuwa ujinga wake ndio unamfanya aongee maneno ambayo ni hayawani anaweza kuyaongea ya kusema serikali haina utawala bora.

 Kama serikali haina utawala bora kitu gani kinakuwasha wewe Kafulila uombe serikali iwataje kwa majina vigogo unaodai waliiba fedha za Escrow kwa kutumia akaunti ya E
scrow?

Jana katika  kipindi Dk.45 jana, alitambulishwa kama Waziri Kivuli  wa Wizara ya Viwanda na Biashara.Katika mahojiano yake kwa wale tuliyoyafuatilia mwanzo hadi mwisho Kafulila hakuzungumzia mambo mengi yanayohusika na Wizara yake.

Mengi sana amenzungumzia mambo yanayohusu wizara za wenzie mfano sakata la Escrow linaangukia Wizara ya Nishati na Madini, suala la Mabehewa linaangukia wizara ya Uchukuzi.

Je alienda kuhojiwa kwaajili ya kuwafulaisha Tembo waliomtuma  maana yeye Dk.Slaa alimpachika jina la Sisizimi? Ameumbuka kwani ndio alienda kuvurunda kabisa.Kafulila umefirisika kisera na kimkakati .

Na hayo uyalopokayo ni miongoni mwa tabia aliyonayo Sisimizi.

Maana Sisimizi anaweza kuingia kwenye Gunzi  la Mahindi  au mfupa  akalamba ,gunzi na mfupa huo ukikauka sisimizi huyo uondoka kesho yake anasahau kama jana alililamba lile gunzi na mfupa  anarudi kulamba katika gunzi na mfupa ule alioulamba jana ukakauka akifikiri ni gunzi na mfupa mpya.

Sasa Kafulila  ametuambia anataka kuibuka upya   na sakata la Escrow wakati mamlaka husika zimeishamaliza suala la Escrow.

Ndio maana nauliza hivi Kafulila ni mzima kweli au amechanganyikiwa?

Inavyonekana sasa Kafulila  ubunge kwake ni Escrow.Uchaguzi mkuu ukikaribia utakuwa unaibuka na Escrow?Ndio kampeni zako hizo?umeishiwa huna hoja kijana.

Ni wazi sasa Kafulila akafanyiwe maombi na kupewa ushauri wa Kisaikolojia haraka maana huwezi kuwa Mbunge mwenye akili timamu ambaye unafahamu zana nzima ya mgawanyo wa madaraka(Separation of Power) , halafu ukaamua kujitokeza hadharani kuzungumza ujinga kama anaouzungumza Kafulila ambaye ni wazi sasa ajitambui kuwa yeye katika sakata hili alikuwa ni mtoa taarifa na alipotoa taarifa ina maana alikuwa anaimani zitafanyiwa kazi na vyombo hivyo vya dola sasa imefika zamu ya dola kufanyia kazi maazimio ya mhimili wa bunge ambako Kafulila ndiko anakotokea na ukatoa taarifa yake, Kafulila anapinga.Hivi huyu Kafulila ni Mzima kweli?

Mbona wakati bunge linafanyia kazi sakata la Escrow mbona mhimili wa serikali wala Mahakama haukiliingilia bunge?Hivi Kafulia ni Mzima kweli?

Kuhusu hoja ya Kafulila aliyoitoa jana kuwa ataanzisha upya sakata la Escrow Bungeni.Minamuuliza Kafulila hivi lile bunge ni la mjomba au bibi yake?

Bunge letu limeanzishwa kwa mujibu wa Ibara ya 62 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977.

Hivyo bunge ni chombo kinachojiendesha kwa kanuni,sheria na taratibu.

Sasa katika Bunge lililoanza leo ,tayari bunge hilo limeishajipangia ratiba zake za kikao hicho sasa huyu Kafulila alivyosimama kule Shinyanga na kuwadanganya wakazi wa Shinyanga eti ataenda kulianzisha sakata la Escrow bungeni wakati ratiba iliyotolewa na Bunge mwishoni mwa wiki haionyeshi mahali popote kuwa bunge hilo limetenga nafasi kwa Kafulila ili awasilishe hoja mpya ya Escrow .

Ratiba ya kikao cha Bunge hili imesema wazi hili ni bunge la Bajeti siyo bunge la kujadili Escrow.

Wakazi wa Shinyanga mlipaswa mmsute Kafulila kwa kutumia ratiba hiyo ya bunge ni wazi Kafulila angekoma kuendelea kuwadanganya na kwa kifupi hana hayo mamlaka ya kufufua upya sakata la Escrow kwasababu tayari sakata hilo limeishafanyiwa kazi na sisi wasomi wa sheria tunasema mtu hawezi kushitakiwa mara mbili kwa makosa yale yale ambayo yameishatolewa uamuzi(Res Judicater ).

Ni wazi Kafulila ni mbumbumbu wa sheria na wananchi wa Jimbo la Kigoma Kusini kwa vitendo hivi unavyofanya binafsi sioni tena kama wanasababu ya kukuamini tena uendelee kuwa Mbunge wao .

Mbaya  zaidi bunge hili ni bungela Bajeti  siyo bunge la akaunti ya Tegeta Escrow  na  kuna dalili za wazi kabisa hili ni bunge  la mwisho kwako.

Nakutakia maisha mema uraini,karibu sana uraini,kule uraini Kigoma Kusini kuna Migebuka na Mawese hakuna nyama choma kama  Chakonichako Bar iliyopo Dodoma.

Kafulila  ni wazi bado unaota ndoto za Escrow,ukilala ukiamkia unaota ndoto kuhusu Escrow, basi nenda kaonane na wakazi wa eneo la Tegeta wakupe eneo ujenge nyumba ili uishi hapo Tegeta ambako kutwa unataja Tegeta,Tegeta,Tegeta.

Ukurasa wa Escrow umefungwa na mamlaka husika ,PAC iliitimisha bungeni suala la Escrow,serikali imeshafanyiakazia sasa kuanza kuzungumzia tena jambo hilo ni kuwadharau wabunge wenzio ambao uliwaamini sana  na bunge kwa ujumla  likafanyakazi yake na PAC ikatoa ripoti yake.

Unaonekana sasa unapenda sana kupewa medani(Tuzo) zilizotengenezwa  na Sufulia (Shaba).Maana hao wanaharakati wenzio walikupa tuzo ya kufanikisha Escrow kwa pupa bila kusubiri kwanza  ripoti ya uchunguzi ya Ikulu ambayo imemuona Maswi na  Muhongo hawana hatia.

Kama unapenda sana kupewa medani nakushauri anachana na medani  ya sufulia (Shaba) nenda kasake  medani  za dhahabu kwa kushindana na mkimbiaji bingwa duniani wa riadha wa mbio fupi  ,Bolt  wa  nchini Jamaica  ili utunukiwe medani ya dhahabu .

Maana medani ile ya Shaba(Sufulia) uliyopewa na wanaharakati ambayo imepewa jina huku mitaani kuwa ni "Medani ya wajinga Duniani.

Hivi wewe Kafulila hiyo medani ya Shaba(sufulia) sijui ilitengenezwa pale Gerezani au Makoroboi mkoani Mwanza uliyopewa ,Hivi ulishawahi kujiuliza taasisi hiyo ilishawahi kumtunikiaga nani tuzo kama hiyo ambayo sasa inaonekana inakupa kiwewe?

Niitimishe kwa kumshauri kijana mwenzangu Kafulila acha kuchekesha walionuna, ajitambue ana mke na wakwe.

Sasa inapotokea leo hii unazungumza mambo hayo ya Escrow ambapo sisi wasomi wa sheria na wajuzi wa mambo tunamuona ni kama mtu aliyechanganyikiwa na hivyo heshima yako kushuka mbele ya watu wanaofikiri sawasawa.

Kafulila acha kudanganya umma, kisheria huna mamlaka ya kuanzisha upya sakata la Escrow, huna hayo mamlaka zaidi zaidi unachokifanya ni kujitutumua mbele ya  umma ambao wengine tunaofahamu huna mamlaka hayo tunaokuona ni mtu uliyokumbwa na kiwewe na kiwewe hicho kimesababishwa na ripoti ya Ikulu iliyomuona Professa Muhongo na Maswi hawana hatia.

Kafulila acha kudanganya umma na kufanya umma wa Tanzania wote hauna akili timamu,uzushi wako huo wa kuzusha uongo kipindi kile kuwa fedha za Escrow zimeibwa na vigogo wa Escrow ,zimeleta madhara makubwa kwa taifa kwani huo mdomo wako unaoendelea kuuchonga kama Samaki aina ya Chuchungi ndio ulisababisha wafadhili wasuse kutoa misaada na hivyo kuwa ni moja ya sababu ya shilingi kuporomoka na matokeo yake upatikanaji wa fedha kwa wananchi kumekuwa kugumu.

Hivi Kafulila unachokitafuta hasa ni kitu gani? Naona kuna kitu ambacho wewe unakijua sirini  unakitafuta basi hicho unachokitafuta kwa bidii hivi ipo siku utakipata.

Maana hata ukiendelee kulalama mithili ya mtu anayetaka kukata roho ,huna mamlaka ya kutengua uamuzi uliotolewa na Ikulu ambao ulimuona Muhongo na Maswi ambao uliwashupalia sana hawana hatia.Na pia huna mamlaka ya kuliamuru bunge lianze upya kushughulikia sakata la Escrow sasa ni vyema ufunge huo mdomo wako.

Mungu ibariki Tanzania

Chanzo: www.katabazihappy.blogspot.com

Facebook: Happy Katabazi
0716 774494

Mei 12 mwaka 2015.

No comments:

Powered by Blogger.