Header Ads

LOWASSA UACHE UONGO



Na Happiness Katabazi

NIMEMTAZAMA kupitia Televisheni ya ITV ,Mzee Edward Lowassa na kuisoma neno kwa neno hotuba yake  ya kutangaza nia leo katika Uwanja wa Sheikh Abeid Mkoani Arusha ya kugombea urais wa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nimebaini uongo wazi katika aya ya kwanza.

Haya hiyo katika hotuba hiyo inasomeka hivi;    HOTUBA YA MHESHIMIWA EDWARD LOWASSA   KWENYE MKUTANO NA WAANDISHI WA HABARI KWA AJILI YA KUTANGAZA NIA YA KUOMBA KUTEULIWA KUWA MGOMBEA WA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) KWA NAFASI YA URAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA).

Ukisoma kichwa hicho cha habari cha hotuba yake kimesema ( Hotuba ya Mheshimiwa Edward Lowassa  kwenye mkutano wake na Waandishi wa Habari......).

Sehemu ya hiyo aya Lowassa amedanganya  umma kuwa eti leo amezungumza na waandishi wa habari wakati akitangaza nia.

Ukweli ni kwamba Lowassa leo ametangaza nia mbele ya wafuasi wake katika mkutano wa adhara ambao wanamuziki wa muziki wa kizazi kipya,wasanii wa Kimasai wakiwa na mishale na silaha za jadi na mwanamuziki wa muziki wa Taarabu Hadija Kopa walitumbuiza.

Binafsi ni mwandishi wa habari kwa zaidi ya miaka 15 sasa,nimeisha shiriki  mikutano mbalimbali ya waandishi wa habari na vyanzo vya habari(source)  yaani (Press Conference).

Kitaaluma mkutano wa waandishi wa habari uhusisha waandishi wa habari na wale wanamsindikiza mtoa habari na mkutano na waandishi wa habari  katika eneo la mkutano.

Mkutano na waandishi wa habari haunaga  mbwembwe ,kualika makundi ya watu mbalimbali, wasanii,vibweka kama tulivyovishuhudia leo katika mkutano huo ,wafuasi wako kupaza sauti kusema Lowassa Rais,wanasiasa kupanda majukwaani   kumnadi mtoa habari(Lowassa), kama ulivyoshuhudia leo katika mkutano ile jinsi Kingunge Ngombale Mwilu, Kangi Lugola, Mtumishi wa Mungu Josephat Gwajima, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Arusha,Onesmo Ole Nangolo walivyokuwa wakimpigia debe Lowassa.

Kimsingi tukubaliane Lowassa kupitia aya hiyo ya hotuba yako ya leo amedanganya umma na amejidanganya yeye mwenyewe na kujionyesha asivyo makini katika baadhi ya mambo.

Hata kama hiyo hotuba uliandaliwa na waandishi wako wa hotuba unaowaamini,kama kweli wewe ni kiongozi makini na unayetaka kuwa rais wa nchi hii kwa kila njia, ulipaswa uisome kwanza hotuba hiyo neno  na  kwa dosari hii imedhirisha na wewe siyo makini.

Hadi ulikubali kuisoma hiyo hotuba mbele ya adhara ina maana ulikubaliana na mambo yote yaliyoandikwa kwenye hiyo hotuba ambapo baada ya wewe kuisoma jukwaani leo sisi wafuatiliaji wa mambo ndani ya muda mchache tumeibaini ina kasoro hiyo ya wazi kabisa tena kwenye kichwa cha habari.

Sasa hao waandishi wa hotuba yako utawachukulia maamuzi magumu? Maana umekuwa ukijinasibu wewe ni kiongozi unayeweza kuchukua maamuzi magumu kwa haraka.

Nakushauri anza kutoa maamuzi  magumu kwa hao waandishi wa hotuba yako hii ambayo ni hotuba ya kihistoria kwani hotuba hii ni ishara ya wewe kuanza safari ya matumaini kwenda Ikulu lakini tayari nimeibaini ina dosari hiyo.

Nyie waandishi wa hotuba ya Mzee Lowassa kuweni makini na kazi yenu, au kama mmetumwa kumuandikia ujinga huo mzee Lowassa katika hotuba zake ili atolewe kasoro kuwa sio makini,mseme maana waandishi wengi hivi sasa hamuaminiki mmekuwa kama wanawake Malaya wanaouza mihili yao  ambao wana mabwana wengi ili mradi wapate fedha upitia mihili yao.

Na hili linawezekana maana aingii akili mwandishi wa habari amuandalie hotuba mtu anayemuunga mkono afanye kosa la kiufundi kama hili tena katika kichwa cha habari.

Niitimishe kwa kumtaka Lowassa aache uongo.Ule ni mkutano wa adhara aliohutubia leo wakati akitangaza nia  na siyo mkutano wake na waandishi wa habari kama alivyodai katika hotuba yake. Hongera sana Mzee Lowassa kwa mkutano wako huo uliofurika watu wengi.Ila ukumbuke  msemo usemao ' Kuzikwa  na watu wengi sio kwenda Mbinguni.

Kila la kheri katika hiyo safari yako
Mungu ibariki Tanzania

Chanzo: www.katabazihappy.blogspot.com
0716 774494
Mei 30 mwaka 2015..

No comments:

Powered by Blogger.