Header Ads

VIGOGO SUMA JKT WAIGALAGAZA SERIKALI



HATIMAYE Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, jana Imemwachiria Huru  Mkurugenzi  wa Shirika Jeshi la Kujenga Taifa (SUMA JKT) Kanali Ayoub Mwakang’ata na maofisa wenzake sita wa jeshi Hilo waliokuwa wakikabiliwa na makosa Saba  ya matumizi mabaya ya madaraka.

Mbali  na Kanali Mwakang’ta washitakiwa wengine ni Kanali   Mkohi Kichogo,Luteni Kanali Paul Mayavi,Meja Peter Lushika, Sajenti John lazier,Meja Yohana Nyichi na Mkurugenzi wa Miradi ya Matrekta wa SUMA JKT- Kanali Felex Samilani.

Hukumu hiyo ya Kesi ya jinai Namba  163/2012  ilitolewa Jana asubuhi na Hakimu Mkazi Alocye Katemana ambaye Alisema alipata fursa ya kusikiliza Kesi hiyo tangu ilipofunguliwa,Wama. 2012 na hadi Jana Imefikia Tamati .

Hakimu Katemana Alisema ili kuthibitisha Kesi hiyo upande wa Jamhuri uliokuwa ukiwakilishwa na Wakili wa Taasisi ya Kuzia na Kupambanana Rushwa, Lizy  Kiwia  ulipata jumla ya mashahidi 10 na vielelezo 25 na upande wa utetezi ulileta jumla ya mashahidi Tisa na vielelezo vitano.

Hakimu Katemana alidai KWA washitakiwa wanakabiliwa na makosa ya matumizi Mabaya ya madaraka  yanayoangukia Katika Kifungu Cha 31 na 32 Cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana Na Rushwa ya Mwaka 2007 , Mahakama hiyo imejiuliza Kuwa ni kweli washitakiwa Hao walinufaina binafsi na makosa w aliyoyatenda? , Je mshitakiwa wa pili (Kichogo) na wasaba  (Samilani) walikuwa hawana madaraka ya kusaini  uamishwaji wa Fedha toka Akaunti ya Tacopa kwenda Suma JKT?, Je washitakiwa ambao ni wajumbe wa Bodi ya Tenda ya Suma JKT walikuwa hawana mamlaka ya kuidhinisha ununuzi wa vifaa Vya ujenzi? je washitakiwa hao walinufaika binafsi au watu wao wakaribu walinufaika kutokana na makosa wanaodaiwa kuyatenda?

Alisema upande wa jamhuri  umeshindwa kuleta  ushahidi unaonyesha mshitakiwa wa pili (kichogo)na Saba (Samilani) ambao  walikuwa watendaji wa TAcopa na ndiyo Waliokuwa wamepewa DHAMANA  na Tacopa ya kuidhinisha Fedha zitoke kutoka Katika Akaunti ya Tacopa Na.011103031763  kwenda Akaunti ya Suma JKT 011103017094 , hawakwa na maelekezo ya kifanya hivyo toka Bodi Suma Jkt na hawakuwa na madaraka hayo na wala siyo watendaji wa Tacopa na kwamba KWA kitendo hicho walijinufaisha binafsi au watu wenye uhusiano nao kwasababu hiyo Mahakama hiyo inawafutia kosa la Tatu, NNE, tano, Sita na Saba.

Kuhusu mshitakiwa wa kwanza, watatu, nne, tano, Sita ambao ni wajumbe wa Bodi ya SUMA JKT Kuwa  Machi 5 mwaka 2009 katika chumba cha mikutano cha ofisi ya SUMA JKT Dar es salaam,wakiwa ni wajumbe wa bodi na Bodi ya Tenda ya SUMA JKT kwa makusudi walitumia madaraka yao vibaya kwa kutoa maamuzi ya bodi hiyo ambayo yaliyoonyesha yametolewa na TAKOPA kwa madhumuni ya kununua magari na vifaa vya ujenzi bila kupata idhini ya kutoka Bodi ya ya Wakurugenzi ya TAKOPA.

' Hata makosa hayo pia yanayowahusu washitakiwa Hao wajumbe wa Bodi ya Suma JKT , upande wa jamhuri umeshindwa ya kuthibitisha Kuwa , je wajumbe Hao walikuwa hawana mamlaka ya kufanya hayo?Je walinufaika na maamuzi hayo binafsi? " Alisema Katemana.

Aidha Alisema KWA mujibu wa vielelezo ushahidi uliotolewa mahakamani unaonyesha washitakiwa kweli walikuwa wajumbe wa Bodi ya Tenda ya Suma JkT na kweli walikuwa vikao halali na waliidhinisha ununuzi wa vifaa hivyo wakifanya vitendo hivyo KWA kukidhi matakwa ya Sheria na siyo kuvunja Sheria Kama upande wa jamhuri ulivyodai.

Kuhusu kosa la Saba lilokuwa linawakabili washitakiwa wote   AMBAlo ni la kula Njama kinyume na Kifungu Cha 32 Cha Sheria ya TAKUKURU ya mwama2007 AMBAPO Kati ya Machi na MEI 2009 washitakiwa wakiwa wajumbe wa Tenda Bodi ya SUMA JKT, walikula Njama ya kuamisha mradi kutoka Akaunti ya Tacopa Kuja Akaunti ya suma JKT ambazo Akaunti hizo zipo Kwenye Benki ya NBC tawi la Corporate bila kufuata matakwa ya Kifungu Cha 156 Cha Sheria ya Fedha za Umma ya Kanuni zake ya Mwaka 2011 nalo limeshindwa kuthibitishwa.

" Kwa Kuwa kosa la Sita kimeshindwa kuthibitisha ni wazi kabisa kosa la Saba AMBAlo ni la kula Njama limeshindwa kuthibitika kwasababu hiyo Mahakama hii inawaachiria washitakiwa wote Katika jumla ya makosa yote Saba yanayowakabili na kuanzia sasa wapo Huru na upande ambao haujaridhika unaweza kukata RUFAA"-Alisema Hakimu Huyo na kusababisha ndugu na Jamaa kupiga makofi ya Furaha Hali iliyosababisha Hakimu awakataze ndugu na kwamba kitendo hicho ni kinyume na Sheria ya nchi.

MAKAMANDA Hao ambao waliosoma kuzungumzia hukumu hiyo, walionekana Kuwa na nyuso za Furaha na kukumbatia na ndugu na Jamaa na familia zao walifika mahakamani Hao kufuatilia hukumu hiyo.Hata hivyo wakati Hakimu Katemana Akita hukumu hiyo Wakili wa Takukuri Kiwia alikuwa akitikisa kichwa.
'
Mwaka 2012 Kesi hiyo ilipofunguliwa mahakamani hapo na kusababisha taharuki kubwa Katika Jamii , Wakili wa Serikali , Kessy alidai kosa la pili pia ni la matumuzi mabaya ya madaraka ambalo linawakabiliwa washitakiwa wote kuwa Machi 12 mwaka 2012 ,washitakiwa hao wakiwa ni wajumbe wa bodi ya Tenda ya SUMA JKT walitumia madaraka yao vibaya kwa kupitishia maazimio ya kununuliwa kwa magari na vifaa vya ujenzi ambavyo vilikuwa vimeishatumika kinyume na kifungu cha 58( 3) cha Sheria ya Mamunuzi ya Umma ya mwaka 2005.

Aidha alidai shitaka la tatu ni la matumizi mabaya ya madaraka linalomkabili mshitakiwa wa pili na wa saba( Kichogo, Samillan) ambapo Machi 16 mwaka 2009 wakiwa wajumbe wa bodi ya Tenda ya SUMA JKT waliamisha Sh 2,744,432,545 kupitia hundi Na.000010 kutoka akaunti ya TAKOPA Na.011103031753 kwa SUMA JKT akaunti Na.01110307094 ambazo akaunti hizo zote zipo katika katika Benki ya Taifa ya Biashara(NBC) bila kufuata matakwa ya kifungu cha 156 cha Sheria ya Fedha ya Umma na Kanuni zake ya mwaka 2001.

Shitaka la nne alidai linawakabili washitakiwa hao wawili yaani mshitakiwa wa pili na watatu ambalo pia ni la matumuzi mabaya ya madaraka ambalo walilitenda Aprili 3 mwaka 2009,wakiwa wajumbe wa bodi hiyo ambapo waliamisha sh 489,677,879.30 kupitia hundi Na.000011 kutoka TAKOPA akaunti Na.011103031763 kwa akaunti Na. 011103017094 ya SUMA JKT ambazo zote zipo kwenye benki ya NBC bila kufuata kanuni na matakwa ya kifungu cha 156 cha Sheria ya Fedha za Umma.

Chanzo: Gazeti la Tanzania Daima la Alhamisi, Aprili 24 Mwaka 2014

No comments:

Powered by Blogger.