Header Ads

CCM MNAIKUMBUKA FAMILIA YA MAREHEMU JOHN KOMBA?




Na Happiness Katabazi

KWA wiki Tatu sasa kuna kitu kinanisukuma niandike Kuuliza Swali hili ; " CCM inakumbuka familia ya aliyekuwa kiongozi wa bendi wa TOT,marehemu John Komba?

Kabla ya kampeni za uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015 niliiandika Wimbo wa CCM Mbele Kwa Mbele Uliotungwa na Komba na nilitabiri Kuwa Wimbo huo utakuja Kuwa ni Wimbo maarufu wakati wa kampeni zikianza  na utaibeba sana CCM na ndivyo ilivyokuwa Kuwa Kwani Wimbo ulikuja Kuwa maarufu sana ndani na nje ya nchi  kutokana na Maudhui yake.

Hivyo kuisababishia CCM kuzidi kupata mashabiki Wengi na hata kuna baadhi ya watu waliokuwa wameichukia  CCM, kupitia Wimbo huo wa CCM Mbele kwa Mbele Walijikuta wakianza kuipenda CCM na kuweka Wimbo huo Kwenye miito ya simu zao za mikononi,pikipiki,Kwenye Magari,kompyuta na baadhi ya maneno yaliyomo Kwenye Wimbo huo ya natumiwa mitaani na baadhi ya watu kufikisha ujumbe Fulani.

Lakini kwa bahati Mbaya Mtunzi wa Wimbo huo Komba alifariki mapema Kabla ya Wimbo wake aujaanza kupigwa Kwenye kampeni na hivyo haukuweza Kuwa Shuhuda wa jinsi Wimbo alioutunga ulivyojizolea Umaarufu.

Komba Enzi za Uhai wake alitunga nyimbo nyingi ambazo ziliiletea sifa CCM na ushindi pia. Wimbo wa CCM Mbele kwa Mbele tulishuhudia aliyekuwa mgombea urais wa CCM ambaye kwasasa ndiye rais wa Tanzania, Dk.John Magufuli alipokuwa jukwaani akinadi sera zake alikuwa akiutumia wimbo huo kupiga push up , kucheza kwa madoido Hali iliyosababisha na yeye kujiongezea wa shabiki wake ambao walimpa kura .

Je ,Rais Magufuli na Makamu wako wa Rais, Samia Suluhu maana ndiyo mmpo madaraka kwasasa na Wimbo huo ilitumika hasa kuwanadi wewe Magufuli,Samia na wabunge hivi mlishawahi kukaa chini kila mtu kwa nafasi yake minafikiria kwenda kumjulia Hali familia ya marehemu Komba nyumbani kwake au hata basi mmuite Mkewe ofisini wake mmjulie Hali ?

Au ndiyo mtasema mpo Bize sana na kufukuza watu kazi,kuwasimamisha watu kazi,kuamrisha Polisi wakamate watu wahalifu, kuvunjia nyumba wakazi wazi wa mabondeni na kufanya ziara za kushtukiza?

Ni Mwendawazimu peke ya anayeweza Kusema wimbo wa CCM mbele kwa Mbele haukuchangia ushindi CCM. Kama CCM mna ikumbuka   familia ya Komba Mungu awabariki ,ila kama hamuikumbuki familia yake itakuwa siyo jambo Jema na mtalaaniwa.

Nimesema hayo kwasababu wanasiasa Wengi wanatabia Moja Mbaya sana wanamtaka mtu na kumthamini mtu kinafki pale wanapokuwa wanaitaji ajenda Yao ikamilike kupitia mtu Fulani,akishafanikiwa hawana wanahabari nae.

Komba mchango wako wa utunzi, uimbaji hautasaulika ,umeacha harama ya kuigwa hasa sauti yako ambayo hadi sasa bado haijapatikana mtu wakuweza kuiga sauti yako.

Mungu ibariki Tanzania

0716 774494
Chanzo:Facebook.Happy Katabazi
Blogg: katabazihappy.blogspot.com
30/12/2015

No comments:

Powered by Blogger.