Header Ads

' NJAGU" VALENTINO MULOWOLA KAIMU MKURUGENZI MKUU TAKUKURU





Na Happiness Katabazi

BINAFSI simfahamu Valentino Mulowola ,ila napenda Kumpa pongezi zangu za dhati kwa kuteuliwa na Rais Dk.John Magufuli Kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU ikiwa ni siku Chache tu tangu Rais Magufuli akutoe Polisi na Kukuteua Kuwa Naibu Mkurugenzi wa Takukuru na Leo ametangaza Kukuteua Kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru.

Watu waliokaribu na Valentino Mulowola  na waliwahi kufanya na wewe  kazi Katika Jeshi la Polisi yaani "Manjagu wenzake ' ambao ni nawaheshimu sana wamekuwa  wakinieleza wewe ni mchapakazi na muadilifu na ni Njagu kweli kweli.

Rai yangu kwako nakuomba ukafanye kazi hiyo Katika wadhifa huo mkubwa kwa mujibu wa Sheria na Kanuni ili uudhiirishie umma kuwa kweli wewe ni mchapakazi na utaendana na hiyo kasi ya Rais Magufuli maana mwenzio Dk.Hosea uteuzi wake umetenguliwa kwasababu Rais Magufuli kasema Hosea hawezi kwenda na kasi yake.Yangu Macho.

Usikubali kutumiwa na wanasiasa uchwara kuumiza watu wasiyo na hatia kwa Sababu tu unataka kuwafurahisha na kujikomba kwa watawala.

Hata Dk.Hosea Kabla ya Kuteuliwa Kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru naye aliteuliwa kwanza Kuwa Naibu wa Ofisi hiyo ambayo ilikuwa ikiongozwa na Marehemu Meja Jenerali Anatory Kamazima, licha Dk.Hosea alikaa kwa muda mrefu Kwenye Cheo Naibu Naibu Mkurugenzi wa Takukuru kuliko wewe ambaye umeshikilia Cheo cha Naibu Mkurugenzi kwa muda mfupi sana.

Sasa basi Waswahili wanasema hivi " Mwenzio akinyolewa na wewe Tia Maji". Dk.Hosea Leo huko aliko lazima Atakuwa anajisikia vibaya kwa uamuzi huo wa rais Magufuli dhidi yake ila wewe Leo unachekelea.

Narudia tena nenda kafanyekazi kwa Haki, Usikubali kutumiwa na wanasiasa,wala usiruhusu Wakubali vae kama Masharti Hao wanasiasa uchwara mAana hawanaga maana na wa fahamu na Mtangulizi wako Hosea anayafahamu sana maana alipambana nao kadri ya uwezo .

Usieende Kutengeneza kambi ndani ya Takukuru kwamba mfanyakazi Huyo alikuwa Kibaraka wa Hosea humtaki,usifanye hivyo.

Dk.Hosea kuna mazuri yake aliyafanya kama kiongozi Katika Taasisi hiyo na tuliyaona Kwani hivi sasa Chini ya Uongozi wa Hosea tumeshuhudia Ofisi za Takukuru zimesambaa Katika Wilaya nyingi nchini, na Mabaya yake usiyafuate na amazuri aliyoyaanza hakuyamaliza basi yaendeleze.

Nakutakia Afya njema na Mungu akupe busara na hekima yakuongoza Katika nafasi hiyo mpya watumishi wako .Taaluma na weledi ndiyo vita wale Katika kuendesha hiyo Ofisi usifanye ,usiruhusu vijana wako kuharakisha Kufungua Kesi mahakamani bila Kuwa na ushahidi wa kutosha mwisho wa siku mkaja kushindwa hizo Kesi.

Ofisi ya Takukuru chini ya Uongozi wako Ifanye kila linalowezekana kujiepusha na malalamiko Kuwa Takukuri inabambikia watu Kesi.

Mwisho sitaki kusikia na wewe unaiga hii old fasheni yakufanya ziara ya kushtukiza maana Manjagu hawana Michezo hiyo ya kitoto.

Nakutakia Sherehe njema ya Christmas na Mwaka Mpya Mulowola wewe na familia yako.

Chanzo: Facebook: Happy Katabazi
Blogg: Katabazihappy.blogspot.com
0716 774494
16/12/2015

No comments:

Powered by Blogger.