Header Ads

MAKUWADI WA WAGOMBEA URAIS CCM WADHIBITIWE








Na Happiness Katabazi
TANZANIA ni nchi ambayo wananchi wake kwa ridhaa yao waliamua taifa Lao liongozwe kwa utawala wa Sheria na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977.

Sisi wasomi wa fani ya Sheria tunasema Katiba ndiyo Sheria  mama na inapotekea Kifungu chochote Cha Sheria nyingine kina kwenda kinyume na Ibara yoyote ya Katiba , basi Kifungu hicho kitahesabika na Mahakama Kuwa ni Kifungu  batiri Kwani kina kwenda kinyume na Ibara Fulani ya Katiba ya nchi yetu.

Mapema wiki iliyopita Jaji Joseph Warioba aliibuka na kutaja sifa za mgombea urais ambaye anafaa kuiongoza  Tanzania baada ya uchaguzi Mkuu kumalizika Mwaka 2015. Miongoni mwa sifa alizozitaja Jaji Warioba alisema rais ajae awe kijana, wazo ambalo zimezua mjadala wengine wakimuunga mkono wengine wakimpinga.

Na Kwa upande mwingine naweza Kusema Kuwa mtazamo huo wa Warioba ndiyo Kama umewazindua usingizini makuwadi wa kambi za wagombea urais wa mwaka 2015 ambapo ni kweli makuwadi hao wamezinduka nakuanza kutumia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kuwafagilia wagombea wao watarajiwa wa kiti ha urais na kuwasiliba makada wa CCM ambao wanatajwatajwa kugombea urais.

Na sisi waandishi wa Habari  tusipokuwa makini na hawa baadhi ya wanasiasa uchwara wetu wa hapa nchi na makuwadi wao,  tutajikuta kuanzia wiki iliyopita hadi Oktoba  mwakani, tutajikuta vyombo vyetu vya habari tunashindwa kuchapisha Habari  za kuchochea maendeleo ya nchi  na Matokeo   yake tunaanza  kununuliwa na kukubali kuchezewa akili zetu na makuwadi wa wagombea watarajiwa wa Kiti Cha urais  Kuwa tunazipa kipaumbele Habari za Kuwafagilia wagombea wao.

Tuwe macho na mchezo huu machafu, Kwani binafsi Nina  uzoefu na hili Kwani Kipindi kile Cha kuelekea mchakato wa kumpata rais wa Mwaka 2005, Nilikuwa ni mwandishi wa gazeti la Mtanzania enzi Waliokuwa makuwadi wa wagombea urais Mwaka 2005 ,walianza mapema kuwaweka  mifukoni baadhi ya wahariri na waandishi  na hatimayeKukazuka misuguano ndani ya vyumba Vya Habari wa baina ya baadhi wahariri na wahariri kwa kushinikiza  baadhi ya wahariri wachapishe Habari na makala za kuwapamba wagombea urais wao.

Ibara ya 39(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 , inaanisha wazi sifa  za mtu  kuchaguliwa Kuwa   Rais wa Tanzania.

Ibara 39(1) (a) ni raia  wa kuzaliwa wa Jamhuri  ya Muungano kwa mujibu  wa Sheria  ya Uraia;
(b) Ametimiza  umri wa Miaka  arobaini:
(c) ni Mwanachama , na  mgombea  aliyependekezwa na Chama Cha siasa;
(d) ambazo sifa  za kumwezesha kuwa Mbunge  au Mjumbe  wa Baraza  la Wawakilishi; 

(e) Katika  Kipindi cha Miaka  Mitano  Kabla  ya Uchaguzi  Mkuu hajawahi  Kutiwa  hatiani Katika  Mahakama  yoyote  kwa kosa lolote  la kukwepa  kulipa  kodi yoyote  ya Serikali.

Ibara 39(2) Bila  ya kuingilia haki  na Uhuru  wa mtu  Kuwa  na  yake , kuamini dini atakayo, kushirikiana na wengine na kushiriki shughuli  za umma kwa mujibu  wa Sheria  za nchi , mtu  yeyote  hatakuwa  na sifa  za kuchaguliwa  kushika  Kiti Cha Rais wa Jamhuri ya Muungano  Kama Si Mwanachama na mgombea aliyependekezwa na Chama Cha siasa":

Ni kweli Ibara  ya 18 (a) ya Katiba ya nchi inasema ' kila mtu  anao Uhuru wa Kuwa na maoni na kueleza  fikra zake'.

Lakini je huu ni wakati mwafaka wa wazee wetu hawa kujitokeza adharani Kusema mgombea urais wa Mwaka 2015 awe kijana?  Hivi Ibara ya 39 ya Katiba inasema mgombea urais ajae awe ni kijana?. 

Huyo mgombea urais kijana Mbona basi hatuambiwi  ujana wake ni wa umri gani? au Tayari Katiba mpya imeishapatikana na Ibara ya kuruhusu mgombea urais kijana imeisha wekwe na imeanza kufanyakazi? Maana Ibara ya 39(1) (b) inasema mgombea urais awe Ametimiza Miaka 40. 

Binafsi mtu yoyote atakayeapishwa na Jaji Mkuu wa Tanzania baada ya uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015 kumalizika Kuwa ndiye rais wa Tanzania , minitamuunga mkono na nitamkubali Kuwa ndiye rais wa nchi yangu.

Lakini tujitazame sasa nchi yetu HIvi sasa inaelekea Kwenye Uchaguzi wa serikali za mitaa, badala ya kuamasisha wanachama wa vyama vyao na wananchi kwa ujumla kushiriki uchaguzi huo wa serikali za mitaa badala yake wazee wetu Hao wanatoa matamshi ambayo ni wazi yameibua misuguano Katika kambi za wagombea urais watarajiwa.

Minafikiri ni jambo Jema kwa sasa Kwa  vyombo Vya Habari kutoa kipaumbele kwa kuchapisha Habari za kuamasisha maendeleo zaidi na kuibua maovu na kutoa dira Katika mambo mbalimbali na kupaza  sauti za wanyonge kupitia kalamu Zenu, hawa " wanasiasa uchawara' wanaotumia makuwadi wao  ambao hivi sasa wamekuwa wakiwasaka waandishi wa wawaingize  kwenye kambi  zao kwa njia mbalimbali .

Makuwadi hao wengi wao wakiwa ni wanaume moja ya mbinu chafu wanayotumia kuwateka waandishi wajiunge na kambi zao ni fedha na kujaribu kuanzisha ghafla mahusiano ya kimapenzi na waandishi wa kike ambao wanachama waandishi Hao watawasaidia Katika kambi zao.

 Makuwadi hao  ambao HIvi sasa wa kujiunga  kwa Wingi  Kwenye  Facebook kwa majina yao halisi na ya kufikirika na kuomba  Kwakasi urafiki kwa waandishi wa habari ambao nao wamejiunga na facebook  ili kila siku wawe wanafanya mawasiliano na baadhi ya waandishi ili wajenge ukaribu kupitia facebook na kupata taarifa mbalimbali za kila siku za mwandishi husika na waandishi wengine, kutufuatilia nyendo zetu wanahabari eti tutakutanaga na watu gani, tu napenda nini, Mara wajisemesha wanataka kuanzisha magazeti hivyo wanataka waandishi wanaowataka wao wawapate mbinu za kitaaluma za jinsi ya kuanzisha magazeti na kutuahidi mishahara minono.

Kwa Bahati Mbaya au nzuri kuna baadhi ya waandishi wa Habari , Njama hizi za makuwadi hawa bado hawajazibaini  ila kikubwa Cha makuwadi hawa wanachokitaka hasa ni Kuwa karibu na Waandishi wa Habari ili waweze Kuwa wanapata taarifa zinazohusu kambi za mahasimu zao Kwani wanaamini nao Hao mahasimu wao nao wanatumia waandishi wa Habari na waandishi wa Habari tunasifika kwa sifa ya kutojua kutunza Siri na sifa hiyo imekuwa Ikitimiza kikamilifu na makuwadi wa kambi za wagombea urais kushikishana adabu.

 Ukimtazama Huyo mtu  anayemfuata  Mwandishi Kuwa eti anataka kuanzisha Gazeti, hafanani kabisa na hayo anayosema.Ni vichekesho vitupu. Ni hatari sana na Ujinga wa aina yake mgombea urais mtarajiwa kwa sasa kuwatumia makuwadi wake wa msafishe jina na wampambe na kuumuuza kupitia vyombo Vya Habari na Mitandao ya kijamii.

Mbinu  hii jamani ilishapitwa na wakati Kwani sio kila mbinu aliyoitmia  Mtu Fulani kufanikisha jambo Fulani kwa  wakati Fulani akafanikiwa kupitia mbinu hiyo, halafu na wewe Leo hii Katika mazingira yaliyokwisha badilika na wewe unaamua kutumia mbinu ile ile aliyotumia mwenzio Miaka 10 iliyopita  utafikiri unaweza kufanikiwa. Unaweza usifanikiwe Kwani kila zama na kitabu Chake jamani.

Tena kaunzia sasa serikali kupitia Idara ya Habari Maelezo iwe macho na Katika kutoa vibali Vya kusajiliwa magazeti mapya Kwani hawa makuwadi wa wanasiasa haw ashindwi kuanzisha magazeti kwaajili ya Kazi Moja ya kuchapisha Habari za kuchafua wagombea wenzao kwa kuzuliana Habari za uzushi na kampeni zikiisha magazeti Yao wanafunga.

Kambi yoyote ya mgombea urais HIvi sasa inaona  silaha  yake kubwa ya kupata ushindi ndani ya CCM ili apitishwe Kugombea urais, ni kambi iliyofirisika kimkamati mapema.

HIvi Karibuni Kamati ya Maadili ya CCM, ilitoa Adhabu kwa wanachama wake Kadhaa ambao iliwakuta na hatia ya kufanya kampeni za ugombea  urais Kabla ya wakati na ikawaweka chini ya uangalizi....lakini sasa Mbona HIvi Karibuni tumemsikia Naibu Waziri wa Mawasiliano , Sayansi na Teknolojia , January  Makamba Akisema Kuwa atagombea .

Hakuna Sheria ya nchi inayombana MTu kutangaza Mapema nia yake ya Kugombea urais Kabla ya wakati lakini Kamati ya Maadili ya CCM, iiliwatia hatiani akiwemo Edward Lowassa, Bernad Membe na wengine kwa maelezo Kuwa wamekiuka Maadili ya CCM kwa kufanya matendo yanayoonyesha wameanza kampeni mapema, sasa tuiulize CCM, Makamba haijamsikia ?Au Kunya anye Kuku akinya Bata Kaarisha ?

Maana Membe,Lowassa na wagombea wengine hadi sasa Hawajawahi kujitokeza adharani kutamka  Kuwa watagombea urais na walichukuliwa ikiwemo kupewa onyo Kali.

Ila  kilichopo mitaani na ndani ya vyumba Vya Habari ni kushuhudia  baadhi ya watu wanaojitambulisha Kuwa wapo karibu na Lowassa na Membe  kuwa makada hao maarufu ndani ya CCM na wapo 'msituni' wanajifua kimya kimya   na kwamba watagombea urais Mwaka 2015.Tusubiri Tuone.

Minasema yote Kheli  na MUNgu hawatangulie ila kinachonikera ni hawa makuwadi wa baadhi ya watu wanaotajwa  Kugombea urais kuanza  mapema  kuwapigia chapuo wagombea wao na kuanza kutumia mbinu chafu za kuwachafua wagombea wenzao kupitia vyombo ya Habari na Mitandao  ya kijamii wakati bado muda rasmi wa kuanza kampeni haujatangazwa. 

Hata hivyo kuna taarifa zisizo rasmi huku mitaani zinadai Kuwa hawa vijana wanatajwatajwa Kugombea urais ni danganya toto na kwamba Hao vijana ( siyo Makamba) wanatumika Kama Chambo na baadhi ya makada maarufu wa CCM ambao Tayari kila kukicha wanatajwa Kuwa watagombea urais, ili wapoteze Lengo na hatimaye wananchi waanze kuwajadili vijana Hao Kumbe vijana Hao wanakazi Maalum ya kuwakinga wagombea husika wasizongwe kwa wakati huu na wananchi. Ipo siku Mungu  ataanika ukweli.

Ikumbukwe kuwa  miongoni mwa hawa walio jitokeza adharani HIvi sasa   kupendekeza eti rais ajae awe ni kijana, alipo ingia ramsi madarakani Rais Jakaya Kikwete,  Desemba 21 Mwaka 2005  , baadhi yao ndiyo waliokuwa wa kwanza kuinanga serikali inayoongozwa na rais (Kikwete), ambaye tuliaminishwa kuwa ni rais kijana.

Kwa Kuwa  Rais Kikwete ni   " Mkubwa wa Akili'  , aliwapatia madaraka mbalimbali karibu wote Waliokuwa wakosoaji wa serikali yake na walivyokosa haya wakosoaji  hao walikubali madaraka hayo kwa mikono miwili , wakachekelea   waliyopewa na rais Kikwete ambae alivyoingia madarakani walikuwa wanamuita ni rais ' mhuni, msanii, cheki bobu  na hana akili na hataweza kuingoza Tanzania na ni rais anayependa kuchekacheka ovyo ovyo hata Katika mambo yasiyostahili kucheka".

Waliokuwa wakimdhihaki Kikwete Wengi walikuwa wakiwaunga mkono waliokuwa wagombea wao wa urais Katika kampeni za uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2005" wagombea wao walishindwa.

 Wakaanza  kulipa kisasi kwa kuikosoa serikali ya awamu ya Nne inayoongozwa na Rais Kikwete,  lakini Kumbe serikali ya Kikwete nayo ilikuwa na vijana wake Kama Amos Makalla ambaye kwasasa ni Naibu Waziri wa Maji, walianza kujibu mapigo kwa wakosoaji wa serikali ya Kikwete na mwishowe Kikwete alikuja kuwatea wakosoaji Katika Nafasi mbalimbali ikiwemo Bunge la Katiba, Tume ya Marekebisho ya Katiba iliyokuwa Ikiongozwa na Jaji Warioba.

Hivyo serikali, CCM, Watanzania wote tuwe macho na watu wa haina hii Kwani Tusikubali kuruhusu msuguano huu uanze sasa kushika kasi tena kupitia vyombo Vya Habari ni wazi hata Habari za kimaendeleo kwa ujumla wake ,  habari kuhusu jinsi vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vinavyofanya kazi ya kuwadhibiti wahalifu  na kuakisha nchi yetu naendelea kuwa na amani na usalama, uchumi wetu, Kilimo, elimu sitakuwa hazisikiki kwa mapana yake Matokeo Habari za wagombea urais Mwaka 2015 ndiyo zitakuwa zinabeba uzito Kwenye vyombo Vya Habari. Tusikubali wendawazimu huu na Hao makuwadi wadhibitiwe mapema mAana siku zote wapambe wana Nguvu  kuliko wenye Mali.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika
Chanzo: www.katabazihappy.blogspot.com
Facebook: Happy Katabazi
Julai  8 Mwaka 2014.
Simu: 0716 774494


No comments:

Powered by Blogger.