Header Ads

UFISADI WA TANZANIA NI TISHIO HATA KWA SHETANI

Na Happiness Katabazi

KASHFA ya Benki Kuu ya Tanzania (BOT) ni kashfa kubwa ya ufisadi kuliko zote zilizowahi kutokea katika Bara la Afrika.

Kashfa za ufisadi ambazo zilikuwa zimetokea kwa nchi kamamNaigeria, ziliwahusu viongozi wa serikali kuibia serikali bila kuhusisha vyombo vya serikali.

Hivyo kila mara serikali na vyombo vyake nchini humo vilibaki katika ulingo wa kutetea Katiba na sheria za nchi.

Lakini katika kashfa hii ya BOT vyombo vya serikali ya Tanzania vimetumika kufanya ufisadi na hivyo kuvunja sheria za nchi.Kwahiyo tatizo siyo mfuko wa EPA kwa EPA ni tone katika bahari ya ufisadi inayogubika kwenye jiko letu la uchumi (BOT).

Sheria ya BOT inakataza BOT kushiriki au kujihusisha katika biashara.Je iliwezekanaje vifungu hivyo kukiukwa wakati bodi ya taasisi hiyo ipo,vyombo vya kuzuia rushwa na polisi vipo?. Kama bodi ya BOT iliona na kuidhinisha uvunjaji wa sheria huo utajiwajibisha wenyewe?

Mfano Dk. Balali ambaye alikuwa ni gavana amekuwa ni mjumbe katika makampuni yanayotajwa ni ya kifisadi ya Meremeta,Tangolg na mengineyo,Gavana huyo huyo ni Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi wa BOT iliyodhamini na kutoa fedha kwa makampuni hayo ya kifisadi.Makampuni hayo yamegundulika kuwa ni ya kifisadi yalifunguliwa ‘off show’ kwa maana ya kukimbia na kukwepa kodi.

Kumbe basi kwa makamuni haya kufunguliwa kwa ‘off show’,BOT ilikuwa inaidhinisha ufisadi wa kukwepa kodi na kukwepa mkono wa sheria ya Tanzania kwa vile Tangold ilifunguliwa Mortius na Meremeta ilifunguliwa Uingereza.

Yalipofilisika sheria ya ufilisi haikutumika kuteua mfilisi na wala hapakuwa na ushaidi wa mahesabu kwamba makampuni hayo yalifilisika kweli wala hapakuwa na wadai waliodai kwamba walifanyabiashara na makampuni hayo lakini BOT ililipoa gharama za madai hewa yatokanayo na kufilisa kwa Meremeta na Tangold.

Huu ni mfano tu kwamba bodi ya sasa ya BOT haina uwezo wa kukabili aina ya ufisadi uliojitokezakatika taasisi hiyo kwasababu bodi hiyo ni sehemu ya ufisadi huo.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali amu iliyopita alikuwa Andrew Chenge ambaye kwa sasa ni Waziri wa Miundo Mbinu na alikuwa ni mjumbe wa bodi ya Meremeta na Tangold, Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Gray Mgonja alikuwa mhumbe wa bodi hizo.

Sasa Rais Jakaya Kikwete anapompa Mwanasheria Mkuu wa Serikali kazi ya kudhibiti kuchunguza maovu yaliyotokea BOT, Mwanasheria Mkuu ana ubavu wa kumdhibiti mwanasheria mkuu aliyemtangulia hadi aombe vyombo

Vyambo vya dola vichunguze na kuchukua hatua za kisheria?

RaisKikwete ameangalia hoja ya EPA na kutengua uteuzi si sawa na kumfukuza kazi mtu. Hii na maana kwamba Balali bado ni mtumishi wa BOT na ana pata malupulupu sambambana kutibiwa kwa kuwa hajatuhumiwa na kosa lolote lile.

Hao wanaoumsifu rais kwa uamuzi wake wanamsifu kwalipi?.Pia rais katazama hoja ya EPA,akutazama hoja zingine ambazo ni kubwa kuliko hoja hiyo.

Hoja ya EPA inausu ubadhilifu wa sh bil.133 lakini hoja moja inayohusu Minara pacha inaubadhilifu wa billion 523.Kwanini rais anawinda sungura badala ya kuiwinda tembo?.Au hana ubavu wakukabiliana na tuhuma hii?

Tuhuma ya kampuni ya Kagoda Agriculture Ltd ni tuhuma ya aibu kwasababu inaelezwa kuwa wakurugenzi ni maswahiba wa arais,ambaye anasemekana ni wanatamtandao kigogo,ambaye alitoa fedha nyingi katika uchaguzi Mkuu uliopita Yawezeekana kweli jina la mwanatanda huyu kigogo halipo kwenye wakurugenzi wa kampuni hiyo lakini kasoro hii ya kiufundi aiondoi tuhuma kubwa ya kwamba dola milioni 30,732,658.82 sawa na sh billion 40 walizopewa kampuni ya Kagoda wakati wa uchaguzi zilitumika kwa shughuli nyeti’kununulia kura’.

Kama hili lina ubishi basi waziri wa Fedha Zakia Meghji atuambie hizo shughuli nyeti za serikali zilizo gharamiwa na fedha hizo ni zipi?.

Kagoda ilisajiliwa Septemba 29 mwaka 2005 na kupewa hati ya usajili namba 54040 na ilichotewa mabilion wiki tano baadae kwa amri ya serikali.

Hata hivyo tangu lini kampuni binafsi yenye wakurugenzi wasiyojulikana uaminifu wao ikatumika kufanya shughu nyeti za siri za serikali?.

Je serikali ilishindwa kuunda kampuni za umma kwa madhumuni hayo?.Tunachokijua ni kwamba katika demokrasia haki ya kutumia fedha za walipa kodi inaendana na uwajibikaji wa wazi.

Aiwezekani ukaibuka ukiwa umejificha katika koti la usiri nyeti ya shughuli za serikali.

Rais aache unafki amevalia njuga fedha za EPA kwasababu zinawagusa wafadhili mwaka jana walichachama kwamba fedha zao zifanyiwe ukaguzi,ameacha fedha nyingi za Watanzania zitafunwe na washirika wake watafune wanavyotaka.Huu ni unafki na inauma kweli kweli.

Ninachosema ni kwamba mafisadi Watanzania ni wabaya kuliko shetani na wana tishia cheo cha shetani Mkuu ajulikanae kwa jina la Lusiferi.

Mungu ibariki Afrika Mungu inusuru Tanzania

0755312859;katabazihappy@yahoo.com;www.katabazihappy.blogspot.com.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumatano, Januari 23, 2008

2 comments:

Anonymous said...

Kumbuka kaka wataalamu wa dunia hii ni hatari. Utadhani kuwa ubadhilifu na ufisadi wote uko hapo tza tu, lakini ukweli ni kwamba umeenea kote. Waenezao haya ni wachache tu duniani. Na haya yalianza zamani.
Ingia website hizi uone.
http://judicial-inc.biz/slave_traders_.htm,
http://judicial-inc.biz/b.lood_diamonds.htm,
http://judicial-inc.biz/J_oran_va_der_sloot_supplement.htm,
http://judicial-inc.biz/thersea_heinz_kerry_bio.htm,
http://judicial-inc.biz/1.osephardim_of_curacao.htm,
http://judicial-inc.biz/j_history_caribbean_jews.htm,
http://www.blacksandjews.com/Jews.of.Black.Holocaust.ag.html,
http://sunray22b.net/slavery.htm,
www.jewwatch.com, www.erichufschmid.net, www.iamthewitness.com, www.prothink.org.

Anonymous said...

Hawa ndio maadui wa uhuru.
Waliyafanya ya kutisha ktk nchi hizi kwa kuwaweka kwenye madeni makuu. Je sisi wabongo watatufanyaje???
http://www.prothink.org/2007/12/jewish-role-in-african-slave-trade_29.html,
http://video.google.com/videoplay?docid=-1583154561904832383,
http://video.google.com/videoplay?docid=-7336845760512239683
Haya shime hebu tueneze ukweli huu.

Powered by Blogger.