Header Ads

BABU KURUDI URAIANI KESHO?

Na Happiness Katabazi

HATIMAYE mahakama ya Rufani nchini kesho inatarajia kutoa hukumu ya mrufani ambaye ni mwanamuziki mahiri wa muziki wa dansi nchini, Nguza Viking maarufu kwa jila la ‘Babu Seya’ na wanaye watatu.


Mbali na Babu Seya, warufani wengine ni Papii Kocha Nguza,Nguza Mbangu na Francis Nguza ambao wanatatewa wakili wa kujitegemea Mabere Marando na Hamidu Mbwezeleni toka Zanzibar.

Kwa mujibu wa hati za wito(summon) zilizotolewa na Msajili wa Mahakama ya Rufani, Francis Mutungi kwa Wakili wa wa wa kuitwa mahakamani kesho kwaajili ya kusikiliza hukumu itakayotolewa na mahakama hiyo, kwa Wakili wa warufani Mabere Marando na uongozi wa Gereza la Ukonga ambapo katika gereza hilo ili siku huyo uongozi wa gereza hilo uweze kuwaruhusu warufani hao kufika mahakamani kusikiliza hukumu yao.

Akilithibithitishia gazeti hili wakili Marando alisema:”Ni kweli leo (jana)nimepokea hati ya wito(summons)toka mahakama ya Rufani ikiniarifu mimi na wateja wangu tufike asubuhi katika mahakama hiyo ili tuweze kusikiliza hukumu itakayotolewa na majaji watatu ambao ndiyo walikuwa wakiliza rufaa yetu:

“Na ninakuhakikishia kwamba tayari wateja wangu(warufani)wameshapelekewa hati hiyo ya wito kule gerezani Ukonga na tumejiandaa kwenda kusikiliza na kuipokea kwa mikono miwili hukumu hiyo ambayo inavuta hisia za watu wengi”alisema Wakili Marando ambaye ni wakili maarufu nchini.

Januari 3 mwaka huu, jopo la majaji wa tatu wa mahakama ya rufani wanaongozwa na Jaji Nataria Kimaro, Salum Massati na Mbarouk Mbarouk walisikiliza kesi kwa siku moja rufaa hiyo ambapo mawakili wa rufani waliomba mahakama hiyo iwaachirie huru warufani hao kwani hukumu zilizowatia hatiani zilikuwa zimejaa dosari nyingi za kisheria.

Mawakili hao walidai kuwa kesi hiyo ilikuwa ni yakupangwa na kwamba hawajawahi kuona hukumu ya ovyo ya ina hiyo tangu waanze kufanyakazi ya uwakili kwa zaidi ya miaka 30 sasa.

Mawakili hao waliwasilisha sababu nne za kupinga rufaa ya Mahakama Kuu iliyotolewa na Jaji mstaafu, Thomas Mihayo na hukumu ilioyotolewa na aliyekuwa Hakimu Mkuu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, Addy Lyamuya, ambao wote waliwatia hatiani washitakiwa kwa makosa ya kujamiana na hivyo kuwafunga kifungo cha maisha jela.


aji na hakimu huyo kwakusema hayo hakitaka hukumu zao walikosea kisheria kwani sheria inaitaka mahakama kabla haijaanza kuchukua ushahidi wa mtoto ni lazima ijiridhishe mtoto huyo anaakili timamu na anaelewa maana ya kiapo na kisha irekodi hayo kwenye jarada la kesi lakini Hakimu Lyamuya hakufanya hivyo wala kuandika rekodi ya hayo”alida Marando.

Marando akiwalisha sababu hizo kwa kujiamini alidai kuwa kwa makosa hayo ya kisheria yaliyofanywa na hakimu na Lyamuya huyo hadi wakafikia uamuzi wa kufunga kifungo cha maisha warufani, ni wazi kabisa walikuwa wanapinga na sheria za nchi na maamuzi yaliyotolewa na majaji wa mahakama za hapa nchini kwenye kesi mbalimbali , ambazo alizitumia kusapoti hoja zake.

“Lakini majaji katika rufaa ya Mahakama Kuu hakuna ushahidi ulitolewa unaonyesha warufani walibaka...hayo yalikuwa ni mawazo ya hakimu kwamba lazima Babu Seya na watoto wake waende gerezani....narudia tena sijawahi kuona hakimu wa aina hii na hukumu ya aina hii ambayo hakimu aliamua kuweka maoni yake binafsi kwani kinachowatia hatiani washitakiwa katika kesi zote ni ushahidi nasiyo maoni ya hakimu”

“Ni wajibu wa mahakama kutafakari ushahidi wa utetezi hata kama hauana uzito sasa huyu Lyamuya katika hukumu yake amewataja mashahidi wa utetezi waliokuja kutoa ushahidi bila kueleza mashahidi kwa mapana walieleza nini”

“Kwa mkanganyiko huu uliofanywa na Hakimu Mkazi Mwandamizi Lyamuya siyo tu alikosea kisheria nasema alifanya makusudi na alikuwa ameshaamua kuwapeleka jela warufani” alidai Marando kwa hisia kali.

Alihoji ni kilichofanya upande wa mashitaka kuficha ripoti ya daktari aliyewafanyia uchunguzi watoto hao wanaodaiwa walibakwa na warufani na kushindwa kuleta mashahidi ambao ni wanamuziki wa Bendi ya Achigo, mama wa Babu Seya na Mke wa Babu seya kwasababu waliona mashahidi hao wangewaumbua.

“Kesi hii ni ngumu kweyu sote na kama mahakama na sisitunaona warufani walifanya haya makosa tuwalaani ila mimi Marando nasema nimejiridhisha hawajafanya hayo makosa:

“Hivi tujiulize Kibaiolojia kweli inawezekana mtoto wa miaka sita apakwe na wanaume hawa(warufani)nyuma na mbele halafu mtoto wa umri huo aweze kutembea?Aiingii akilini hata kidogo nasema kesi hii ni ya kutunga kwani hata mwanamke mwenye umri wa utu uzima akifanyiwa unyama huo hawezi kutembea.”alidai Marando na kusababisha umati uliofurika kuendelea kuacha vinywa wazi kwa mshangao.

Akijibu hoja za mrufani, wakili Mkuu wa Serikali Justus Mulokozi ambaye alitumia nusu saa kujibu hoja hizo alidai kuwa kitendo cha shahidi kushindwa kumtambua mshitakiwa mahakamani siyo sababu inayopeleka ushahidi wa shahidi huyo kuonekana hauna thamani, jibu lilosababisha umati wa watu kuangua vicheko.

Mulokozi alidai pia mahakama ikiamini upande mmoja, halazimiki kuangalia upande mwingine lakini hata hivyo hoja hiyo ilipingwa vikali na Marando ambaye alidai kuwa hoja hiyo haikupaswa kutolewa na wakili mwandamizi kama Mulokozi kwani hoja hiyo inatofautiana na sheria za nchi na kauli hiyo ya wakili wa serikali imedhiirisha sasa ni kweli Lyamuya aliegemea uegemea ushahidi wa upande wa mashitaka tu.

Januari 27 mwaka 2005, aliyekuwa Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Thomas Mihayo ambaye kwa sasa amestaafu alitupilia mbali rufaa yao iliyokuwa ikipinga hukumu iliyotolewa na aliyekuwa Hakimu Mkuu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu,Addy Lyamuya ambaye aliwatia hatiani kwa makosa yote waliyokuwa wameshitakiwa nayo Juni 25 mwaka 2004.

Waomba rufani hao wanakabiliwa na makosa kumi ya kubaka watoto wa kike wenye umri kati ya miaka sita na nane na makosa mengine 11 ya kulawiti watoto wa kike wenye umri kama huo na kwamba wanadaiwa kutenda makosa hayo kati ya April na Oktoba 2003 eneo la Sinza kwa Remmy, jijini.

Aidha katika kesi hiyo mwalimu wa shule ya Msingi Mashujaa, Sigirinda Ligomboka, alishitakiwa kwa makosa mawili ya kumsaidia Babu Seya kutenda makosa ya kubaka na kulawiti kwa kuwaruhusu baadhi ya watoto hao kutoka madarasani.

Upande wa mashitaka ulileta mashahidi 24, ambao upande wa utetezi ulipinga vikali kutenda makosa hayo na uliita mashahidi nane.Katika hukumu yake Hakimu Lyamuya alitupilia mbali na utetezi wa Babu Seya na wanawe na akawatia hatiani kwa makosa hayo na hivyo kuwafunga kifungo cha maisha jela.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumatano, Februali 10 mwaka 2010

No comments:

Powered by Blogger.