Header Ads

FREDRICK SUMAYE UPO SAHIHI

 

Na Happiness Katabazi
JUMAPILI iliyopita waziri mkuu mstaafu Fredrick Sumaye alifanya mkutano na waandishi wa habari na kueleza kusikitishwa kwake baadhi ya vyombo vya habari hapa nchini kuandika habari kuhusu yeye ambazo alidai hazina ukweli wowote na kwamba hana mpango wa kukiama chama chake cha CCM.

Sumaye ambaye alishindwa kwenye kinyang’anyiro cha kugombea ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM,wilayani Hanang’ mkoani Manyara,bila woga alisema CCM imegubikwa na rushwa ya kimtandao na kutaadhalisha kama tatizo hilo lisipotatuliwa mapema linawaweza kuleta madhara makubwa.

Lakini Sumaye alisema licha ya CCM kukabiliwa na tatizo hilo hayupo tayari kukiama chama hicho kama gazeti moja lilivyoandika wiki iliyopita kuwa anataka kuamia Chadema ni wazushi.Na alituasa sisi wanahabari kuzingatia maadili ya kazi yetu na siyo kuandika habari za uzushi ambazo mwisho wa siku Tanzania inaweza kujikuta inaingia kwenye machafuko kama nchi za jirani zilizowai kuingia kwenye vita ya wenyewe kwa wenyewe kwa sababu ya vyombo vya habari kuandika habari zilizokuwa zikiibua uhasama.

Bila kuchelewa mimi binafsi naunga mkono tamko hilo la Sumaye kwani amesema ukweli na ametumia haki yake ya Kikatiba iliyoanishwa wazi katika Ibara ya 18(a) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 inayosema hivi ‘kila mtu anao uhuru wa kuwa na maoni na kueleza fikra zake;”.

Nafahamu fika kuwa kuna watu watambeza Sumaye kuwa rushwa ndani ya CCM kaiona leo baada ya kushindwa nafasi ya ujumbe wa NEC ?, lakini minasema ni afadhali leo hii Sumaye ameweza kuwa jasiri na kutueleza tatizo hilo kwani hata Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Dk.Edward Hosea analifahamu fika tatizo hilo na ndiyo maana wakati wa uchaguzi Dk.Hosea amekuwa wakiwamwaga mashushushu wake kwenye chaguzi hizo.

Hii ni mara ya pili kwa Sumaye kuwahasa wanahabari, mara ya kwanza aliviasa vyombo vya habari aliposhinda kesi yake aliyoifungua Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam mwaka 2006 dhidi ya Gazeti la Tanzania Leo ambalo limekufa hivi sasa ambalo lilichapisha habari ya uongo ambayo ilisababisha Sumaye achukiwe na wananchi tena na kumbuka wakati habari hiyo inachapishwa taifa lilikuwa likikabiliwa tatizo la uhaba wa vyakula iliyosema Sumaye anamiliki Shilingi Trilioni tatu kwenye akaunti yake na Sumaye alishinda kesi,uongozi wa gazeti hilo ulishindwa kuleta ushahidi na haukuwa na huwezo kuwamlipa fidia Sumaye kama walivyoamriwa na mahakama na matokeo yake mmiliki wa gazeti hilo alienda kwenye mkutano ulioitishwa na Sumaye kwa waandishi wa habari na mmiliki huyo alienda kuomba msahama na kukiri habari ile ilikuwa ya uongo.

Na si Sumaye wala Dk.Hosea tu, hata Rais Jakaya Kikwete naye alishaitaka TAKUKURU kuwashughulikia wana CCM wanaoa rushwa na si hivyo tu Kikwete alishawai kusema ndani ya CCM watu hawaaminiani na kwamba mtu hawezi kumwachia glasi ya maji mwenzie kwa kuhofia kuthuliwa.Pia Kikwete alishawahi kusema ndani ya serikali unakuta Waziri asemeshani na Naibu wake au Katibu Mkuu wa wizara yake. Sasa misioni Sumaye amekosea wapi,nasisitiza yupo sahihi kama alivyokuwa Kikwete ambaye alitueleza siri hizo tena za hatari zinazowahusu wanachama wake na wateule wake ambazo tulikuwa hatuzijui.Nawapongeza viongozi wote hao kwa kuwa wawazi kwetu na tuwaunge mkono kwa uwazi huo siyo kuwalaumu.

Hakuna ubishi kwa sisi tunafuatilia kwa undani na ukaribu siasa zinazofanywa na vyama vingi vya siasa kama CCM,Chadema,TLP. CUF tuhuma za rushwa zimekuwa kiibuliwa na wanachama wa vyama hivyo licha kwa upande wa vyama vingine vimekuwa vikikabiliwa na tuhuma za kupeana vyeo kwa mtindo wa undugu,fedha,kiukanda na rushwa ya ngono.

Sumaye ametusaidia kupaza sauti kuhusu rushwa nyakati za uchaguzi ndani ya chama hicho lakini pia binafsi namuuliza Sumaye yeye au wapambe wake nao hawakushiriki kwa namna yoyote hata kutoa rushwa ya senti moja kwa wapiga kura wale wa uchaguzi ule?Au naye Sumaye alitoa rushwa wapiga kura wakatafuta fedha zake na wakamchinjia baharini ndiyo maana kaamua kulalamika adharani?

Sikuwepo kwenye uchaguzi wa CCM wilaya ya Hanang’ hivyo inaniwia vigumu kumuhukumu Waziri Mary Nagu kuwa alitoa rushwa ndiyo akashinda U-NEC au Sumaye alitoa rushwa fedha zake zikaliwa bure.

Nigeukie hoja ya Sumaye alivyoviasa vyombo vya habari kuwa vizingatie maadili ,ni kweli namuunga mkono Sumaye kwani hata mimi nimeishawahi kuandika makala zaidi ya nne ya kuwaasa wanahabari wenzangu kuwa baadhi yetu tumekuwa tukiandika habari ambazo ni za uongo,uzushi,kuchafua watu wasiyo na hatia kwa makusudi jambo kwanza linadhalilisha taaluma ya habari na pia kuwaletea madhara makubwa watu wasiyo na hatia.

Ifike mahala sasa wale waandishi wahabari wenzetu wanaokubali kutumika vibaya kuandika habari zisizozingatia vigezo ambazo zinawazulia uongo na kuwachafua baadhi ya wananchi wenzetu wakiwemo viongozi,taasisi,vyama na serikali ambao wengine wana umri kama wazazi wetu kuwa na hofu ya Mungu na kuanza kujiuliza hivi habari hiyo ya uongo na uzushi unayoiandika dhidi ya watu hao ndiyo habari ya uongo na uzushi ingeandikwa dhidi yako au mzazi,mkeo,mume wako wako au ndugu yako ungejisikiaje?

Mnaowatendea ubaya kwa makusudi kupitia karamu zenu ni binadamu hawajatolewa Nyongo,wanaumia na wanapata madhara na kuwashushia heshima na wengine wanaweza kuvumilia na wengine hawana moyo wa kuvumilia na siku nao watakapoamua kutumia njia haramu kuwadhuru wanahabari wanaowachafua,tusijekulalamika wala kuandamana.

Kwani hata rais Kikwete mwaka 2008 alipokwenda Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kumtazama Mkurugenzi Mtendaji wa Gazeti la Mwanahalisi,Saed Kubenea aliyekuwa amelazwa hapo kwaajili ya kumwagia kimiminika kinachodhaniwa kuwa ni Tindikali usoni alitutaka waandishi wa habari tujilinde na kujiadhari kwani habari na makala tunazoandika siyo kila mtu anazifurahi ,kuna wengine zinawaumi wanashindwa kuvumilia wataamua kutushughulikia.

0716 774494

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Oktoba 12 mwaka 2012.

No comments:

Powered by Blogger.