Header Ads

MRAMBA AYASUTA MASHITAKA YAKE

Na Happiness Katabazi

WAZIRI wa fedha wa zamani, Basil Mramba ameendelea kuyasuta mashitaka yanayomkabili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, na kudai kuwa siyo yeye aliyeiarika nchini kampuni ya Alex Stewart,wala kuiongezea mkataba wa nyongeza kampuni hiyo na wala kuiarifu kuwa ilikuwa imeteuliwa na serikali ya Tanzania kuwa imeshinda tenda na kwamba inahitajika kuja kufanyakazi hapa nchini wala kuingia mkataba na kampuni hiyo.

Mramba aliyasema hayo mbele ya jopo linaongozwa na Jaji John Utamwa, Sam Rumanyika na Hakimu Mkazi Saul Kinemela wakati alipokuwa akihojiwa na wakili wa Waziri wa Nishati na Madini wa zamani, Daniel Yona na Katibu Mkuu Mstaafu wa Wizara ya Fedha, Gray Mgonja, (Elisa Msuya na Profesa Leonard Shaidi), baada ya juzi wakili wa Mramba (Peter Swai) kumaliza kumuongoza mshitakiwa huyo kutoa utetezi wake.

Mramba ambaye alikuwa akijibu maswali ya wakili Msuya kwa kutumia nyaraka mbalimbali ambazo zinaonyesha ziliandikwa na Benki Kuu na kusainiwa na marehemu Gavana Daudi Balali zikionyesha kuwa ni BoT, ndiyo iliarika kampuni hiyo kuja kufanyakazi ya kukagua dhahabu nchini na siyo yeye kama inavyodaiwa katika kosa la pili katika hati ya mashitaka na upande wa jamhuri na kwamba ni Benki kuu ndiyo iliiandikia barua kampuni hiyo kuifahamisha kuwa imeshinda tenda na kwa hiyo BoT inaoipatia mkataba wa nyongeza wa kuendelea kufanyakazi ya ukaguzi wa madini.

“Kwanza nayashanga hayo mashitaka kuwa eti mimi na Yona na Mgonja ndiyo tuliiarika hapa nchini kampuni hiyo, ukweli umeanishwa kwenye nayaraka hizi ambazo zimetolewa mahakamani kama utambulisho ambazo zionyesha wazi ziliandikwa na BoT kwa kampuni hiyo sasa nashangazwa leo hii nashitakiwa mimi kwa kosa hilo ambalo halina ukweli wowote”alida Mramba.

Alindelea kudai kuwa aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Andrew Chenge katika barua yake ya Mei 2 mwaka 2003 aliyomuandikia Yona  nakala kwa waziri wa Fedha ,BoT katia maoni yake Chenge alisema anakubaliana na ushauri wa serikali wa kuileta nchini kampuni hiyo ije ifanyekazi  na kwamba hakukuwepo ulazima wa kulipeleka jambo hilo kwenye bodi ya ukaguzi wa dhahabu  na alitoa ushauri wa kisheria kuhusu mkataba huo ambao uliingiwa na BoT na kampuni hiyo kuwa taratibu zote zilifuatwa na akashauri kuhusu mkataba huo kuwa hauitaji leseni  na akaelekeza kuwa gharama za kodi, gharama za uendeshaji wa mradi huo zitabebwa na serikali.

Jana mawakili hao walimaliza kumhoji Mramba na ilikuwa ikitakiwa wakili Kiongozi wa upande wa Jamhuri Fredrick Manyanda aanze kumhoji Mramba lakini hata hivyo wakili Manyanda alidai hakuwa tayari jana kufanya hivyo anaomba akajiandae  lakini hata hivyo Jaji Utamwa aliamua kuiiarisha kesi hiyo hadi Novemba 28-30 mwaka huu, ambapo itakuja kwaajili ya mawakili wa serikali kuanza kumhoji Mramba na jaji huyo akatoa hati za wito wa kuitwa mahakamani mashahidi wa mshitakiwa huyo ambapo shahidi mmoja wapo ni Chenge.
Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Oktoba 12 mwaka 2012.

No comments:

Powered by Blogger.