Header Ads

MAREKANI KUIPIGA 'TAFU' UB






MAREKANI KUIPIGA 'TAFU'  UB

Na Happiness Katabazi
CHUO cha Southern University kilichopo  jimbo la Louisiana  nchini Marekani kimetoa tamko la pamoja na Chuo Kikuu cha Bagamoyo(UB) cha Tanzania  juu ya makubaliano kushirikiana .

Akizungumza na Mwandishi  wa habari hizo, Dk.Elifuraha Mtaro ambaye  ni Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Bagamoyo (UB), anayeshughulikia Fedha na Utawala, ofisini kwake Mikocheni kwa Warioba, jijini Dar es Salaam Leo alisema UB imepokea kwa Furaha tamko Hilo ambalo amelishika Katika picha inayombatana na habari hii.

Dk.Mtaro alisema tamko Hilo ambalo limesainiwa na Seneta wa Jimbo la Louisiana, Rick Gallot Jr, lilitolewa hivi karibuni Katika mkutano wa viongozi wa nchi za Afrika ambapo kwa Tanzania iliwakirishwa na Rais Jakaya na   mkutano huo uliitishwa  na Rais wa Marekani, Barack Obama.

Dk.Mtaro alisema kwa mujibu wa tamko Hilo Southern University  ambalo lilipata Baraka ya Seneti hiyo ambapo Seneti hiyo ya Louisiana ilitoa tamko la kiserikali  ambalo lilisisitiza  kwamba serikali ya jimbo Hilo   itaungana na serikali ya Tanzania  Katika kuendeleza  taaluma, utafiti na huduma  za Jamii Katika vyuo vikuu hivyo viwili.

 Imetolewa: Ofisa Habari wa Chuo Kikuu Cha Bagamoyo(UB)
Oktoba 21 Mwaka 2014.







No comments:

Powered by Blogger.