Header Ads

TUMUACHE DPP AFANYE KAZI YAKE

Na Happiness Katabazi

ALHAMISI ya wiki hii, baadhi ya vyombo vya habari likiwamo gazeti hili, viliandika habari kwamba Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), Eliezer Feleshi, anadaiwa kumkingia kifua mmoja wa mawaziri aliyetakiwa kuingia katika mkumbo wa watu wanaofikishwa mahakamani, kwa tuhuma za matumizi mabaya ya madaraka na kuisababishia serikali hasara ya mabilioni ya shilingi.
Habari za uhakika ambazo gazeti hili lilizipata zilieleza kuwa mwanasiasa huyo ambaye kwa sasa ni mbunge wa jimbo moja lililo katika mikoa ya Kanda ya Ziwa, alinusurika kupelekwa mahakama ya Kisutu baada ya DPP kueleza wazi kuwa ushahidi wa kumburuza mahakamni haujajitosheleza.
Chanzo cha habari cha kuaminika kilizungumza na Tanzania Daima siku hiyo, kilidai kwamba hatua ya Ofisi ya Mwendesha Mashitaka (DPP) kumnusuru mwanasiasa huyo, imewashtua baadhi ya maofisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), ambao kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa wamekuwa wakilichunguza sakata la mwanasiasa huyo.
Mtoa habari wetu aliieleza gazeti hili kwamba kabla ya kuwasilishwa kwa DPP kwa ajili ya uchunguzi zaidi, maofisa wa Takukuru walikuwa wamejiridhisha kuhusu kukamilika kwa shauri hilo na kulipeleka kwa DPP kwa ajili ya hatua zaidi.
Alipotafutwa ili kuelezea taarifa hizo, Feleshi, alikanusha kuingia katika undani wa suala hilo na badala yake alibainisha wazi kuwa hawezi kufanya kazi kwa shinikizo au kwa kusikiliza taarifa za kuzusha zinazotolewa na watu kwa malengo yao, bali hufanya kazi kulingana na taaluma yake na hulifanyia uchunguzi wa kina kila faili analoletewa mezani kwake.
Awali ya yote napenda kutoa pongezi kwa serikali ya awamu ya nne kwa hatua yake ya kuanza kutoka kwenye usingizi mzito na kuanza kuwafikisha mahakamani baadhi ya watuhumiwa wakiwamo wale ‘wanaotaniwa’ na kuitwa vigogo (vigogo wako katika nchi za watu walioendelea), ambao wanatuhumiwa kwa makosa ya matumizi mabaya ya madaraka na wizi wa fedha za EPA katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam.
Nitakuwa si muungwana kama sitatoa pongezi katika hili, kwani nami nilikuwa miongoni mwa wananchi ambaye nilishiriki kikamilifu kwa miaka miwili mfululizo kwa kuandika makala za kuishinikiza serikali kuwachukulia hatua ya watuhumiwa wa makosa hayo.
Turejee kwenye hoja yetu, ambayo inadaiwa baadhi ya maofisa waandamizi hawajaridhishwa na hatua hiyo ya DPP ya kutomfungulia kesi mbunge huyo, kwanza naomba ieleweke wazi kuwa mtu anapaswa kuheshimu kazi na taaluma ya mwenzake, tukilifahamu hilo tutaweza kuheshimiana na kujenga nchi iliyo bora.
Tangu wananchi waanze kulivalia njuga suala la ufisadi, mikataba mibovu. Watanzania tunamkumbuka Mkurugenzi wa Takukuru, Edward Hoseah, baada ya kuchunguza kama mkataba wa kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond, aliutangazia umma kwamba mkataba huo hakuwa na harufu ya rushwa ndani yake, ulifuata sheria ya manunuzi ya umma na mkataba ulikuwa safi.
Baada ya taarifa yake hiyo, wananchi wa makundi mbalimbali walimpinga waziwazi hadi Bunge lilipoamua kuunda kamati ya kuchunguza mkataba huo uliojaa utata wa kila aina. Kamati hiyo iliongozwa na Dk. Harrison Mwakyembe ambaye Februari 6 mwaka huu, akisoma hotuba ya kamati yake, alisema wamebaini kampuni ya Richmond haikuwa na uwezo na kwamba sheria ya manunuzi haikufuatwa. Kwa sababu hiyo walioshiriki kuipa tenda kampuni hiyo hawakuzingatia maslahi ya taifa.
Ripoti hiyo ilisababisha aliyekuwa waziri mkuu, Edward Lowassa, Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dk. Ibrahim Msabaha, kujiuzulu nyadhifa zao baada ya kuhusishwa na kashfa hiyo.
Si hivyo tu, kwa wale tunaofutilia kwa karibu mwenendo wa mambo wa taifa letu, tutakumbuka kwamba mwaka jana wakati CCM ikiwa kwenye mchakato wa chaguzi za ndani, ni maofisa hao hao wa Takukuru waliwakamata wabunge wawili wa Kanda ya Kaskazini kwa tuhuma za rushwa na kuwafungulia kesi za rushwa.
Lakini hatimaye mahakama husika iliwafutia kesi zao baada ya kubaini hakuna na ushaidi wa kuwatia hatiani. Lakini wakati mahakama inatoa uamuzi huo wabunge hao waliokuwa wakigombea nafasi za uongozi kwenye chama hicho hawakuweza kugombea nafasi hizo, baada ya kuenguliwa kutokana na tuhuma hiyo ya rushwa, tukio lililohusishwa na mambo ya kisiasa.
Ni Takukuru hii hii iliyopeleleza baadhi ya tuhuma za watuhumiwa na kuwafikisha kwa ‘mbwembwe’ nyingi mahakamani, lakini sasa tunashuhudia vioja vya aina yake kwa mashahidi wanaokuja kutoa ushahdi katika kesi hizo zilifunguliowa na Takukuru, hasa kwa kutoonekana ushahidi wa kutosha wa kesi hizo zilizochunguzwa na Takukuru. (Angaliza: Kitendo cha serikali kupoteza kesi ni sawa na kupoteza heshima yake na fedha za walipa kodi – kwani hatimaye walioshinda hufungua kesi za madai dhidi ya serikali).
Kwa sababu hizo sioni sababu ya baadhi ya maofisa waandamizi wa Takukuru (wanajijua) ambao nisingependa kuwataja kwa majina katika makala hii, kuchachamaa kisirisiri kuwa ofisi ya DPP haijamburuza mahakamani kigogo huyo, ilhali wao wameshakamilisha uchunguzi. Kwa historia niliyoeleza hapo juu maofisa hao hawapaswi hata kidogo kumnyooshea kidole DPP ambaye ameonekana kujali zaidi taaluma yake ya sheria.
Wananchi wanakerwa mno na ufisadi uliokithiri kila pembe ya nchi hii, lakini kwa sababu DPP ameshatuahidi kwamba anayafanyia kazi makabrasha ya watuhumiwa wa EPA na mengineyo, kinachopaswa kufanywa hivi sasa ni kumpa muda DPP aitekeleze kazi yake bila shinikizo.
DPP ameonyesha wazi kuwa asingependa kuwaburuza mahakamani watu bila kuhakiki kwa kina kama kuna ushahidi wa kutosha kuwaburuza mahakamani, ili kukwepa kuiingiza serikali katika hasara ya kuwalipa fidia watu ambao baada ya kushinda kesi huidai fidia serikali kwa kuwadhalilisha.
Si siri kwa muda mrefu vyombo vya dola vimekuwa vikiwafungulia kesi baadhi ya wananchi kwa malengo yao binafsi, hali inayosababisha wananchi wasio na hatia kusota rumande, hali inayosababisha wananchi kujenga chuki na serikali yao.
Hakuna mtu aliye juu ya sheria au mwenye hakimiliki ya nchi hii, hivyo kila mmoja ana jukumu la kujenga nchi kulingana na nafasi yake. Hivyo tumpe nafasi Eliezer Feleshi na vijana wake wachambue kwa kina mafaili ya watuhumiwa wa EPA, mikataba mibovu na makosa mengine na wakijiridhisha wana ushaidi wawaburuze mahakamani bila kuchelewa.
Kama DPP atafanya kazi kwa msukumo wa kisiasa au kumfurahisha bosi kama wengine wanavyofanya kuliko taaluma yake ya kisheria, kuna kila dalili haki za watu kupotea pamoja na nchi kujikuta katika hasara kubwa baada ya watu kadhaa walioburuzwa mahakamani kushinda kesi walizofunguliwa.
Ni vema tukakawia lakini tukafikia. Kwani miongoni mwetu tunaochachamaa watu hawa wafikishwe mahakamani bila uchunguzi kukamilika, siku wakishinda kesi tutaanza kutoa maneno kadhaa ikiwa ni pamoja na kudai ‘wamewahonga’ mahakimu au kuburuzwa kwao mahakamani kulikuwa ni kwa lengo fulani. Tusifike huko, sote tuendelee kuibua maovu mengine na kupongeza pale serikali inapofanya vizuri..
Mungu ibariki Tanzania, Mungu Afrika.

0755 312859
katabazihappy@yahoo.com:www.katabazihappy.blogspot.com

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima Jumapili Novemba 30 mwaka 2008



Na Happiness Katabazi

ALHAMISI ya wiki hii, baadhi ya vyombo vya habari likiwamo gazeti hili, viliandika habari kwamba Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), Eliezer Feleshi, anadaiwa kumkingia kifua mmoja wa mawaziri aliyetakiwa kuingia katika mkumbo wa watu wanaofikishwa mahakamani, kwa tuhuma za matumizi mabaya ya madaraka na kuisababishia serikali hasara ya mabilioni ya shilingi.
Habari za uhakika ambazo gazeti hili lilizipata zilieleza kuwa mwanasiasa huyo ambaye kwa sasa ni mbunge wa jimbo moja lililo katika mikoa ya Kanda ya Ziwa, alinusurika kupelekwa mahakama ya Kisutu baada ya DPP kueleza wazi kuwa ushahidi wa kumburuza mahakamni haujajitosheleza.
Chanzo cha habari cha kuaminika kilizungumza na Tanzania Daima siku hiyo, kilidai kwamba hatua ya Ofisi ya Mwendesha Mashitaka (DPP) kumnusuru mwanasiasa huyo, imewashtua baadhi ya maofisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), ambao kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa wamekuwa wakilichunguza sakata la mwanasiasa huyo.
Mtoa habari wetu aliieleza gazeti hili kwamba kabla ya kuwasilishwa kwa DPP kwa ajili ya uchunguzi zaidi, maofisa wa Takukuru walikuwa wamejiridhisha kuhusu kukamilika kwa shauri hilo na kulipeleka kwa DPP kwa ajili ya hatua zaidi.
Alipotafutwa ili kuelezea taarifa hizo, Feleshi, alikanusha kuingia katika undani wa suala hilo na badala yake alibainisha wazi kuwa hawezi kufanya kazi kwa shinikizo au kwa kusikiliza taarifa za kuzusha zinazotolewa na watu kwa malengo yao, bali hufanya kazi kulingana na taaluma yake na hulifanyia uchunguzi wa kina kila faili analoletewa mezani kwake.
Awali ya yote napenda kutoa pongezi kwa serikali ya awamu ya nne kwa hatua yake ya kuanza kutoka kwenye usingizi mzito na kuanza kuwafikisha mahakamani baadhi ya watuhumiwa wakiwamo wale ‘wanaotaniwa’ na kuitwa vigogo (vigogo wako katika nchi za watu walioendelea), ambao wanatuhumiwa kwa makosa ya matumizi mabaya ya madaraka na wizi wa fedha za EPA katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam.
Nitakuwa si muungwana kama sitatoa pongezi katika hili, kwani nami nilikuwa miongoni mwa wananchi ambaye nilishiriki kikamilifu kwa miaka miwili mfululizo kwa kuandika makala za kuishinikiza serikali kuwachukulia hatua ya watuhumiwa wa makosa hayo.
Turejee kwenye hoja yetu, ambayo inadaiwa baadhi ya maofisa waandamizi hawajaridhishwa na hatua hiyo ya DPP ya kutomfungulia kesi mbunge huyo, kwanza naomba ieleweke wazi kuwa mtu anapaswa kuheshimu kazi na taaluma ya mwenzake, tukilifahamu hilo tutaweza kuheshimiana na kujenga nchi iliyo bora.
Tangu wananchi waanze kulivalia njuga suala la ufisadi, mikataba mibovu. Watanzania tunamkumbuka Mkurugenzi wa Takukuru, Edward Hoseah, baada ya kuchunguza kama mkataba wa kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond, aliutangazia umma kwamba mkataba huo hakuwa na harufu ya rushwa ndani yake, ulifuata sheria ya manunuzi ya umma na mkataba ulikuwa safi.
Baada ya taarifa yake hiyo, wananchi wa makundi mbalimbali walimpinga waziwazi hadi Bunge lilipoamua kuunda kamati ya kuchunguza mkataba huo uliojaa utata wa kila aina. Kamati hiyo iliongozwa na Dk. Harrison Mwakyembe ambaye Februari 6 mwaka huu, akisoma hotuba ya kamati yake, alisema wamebaini kampuni ya Richmond haikuwa na uwezo na kwamba sheria ya manunuzi haikufuatwa. Kwa sababu hiyo walioshiriki kuipa tenda kampuni hiyo hawakuzingatia maslahi ya taifa.
Ripoti hiyo ilisababisha aliyekuwa waziri mkuu, Edward Lowassa, Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dk. Ibrahim Msabaha, kujiuzulu nyadhifa zao baada ya kuhusishwa na kashfa hiyo.
Si hivyo tu, kwa wale tunaofutilia kwa karibu mwenendo wa mambo wa taifa letu, tutakumbuka kwamba mwaka jana wakati CCM ikiwa kwenye mchakato wa chaguzi za ndani, ni maofisa hao hao wa Takukuru waliwakamata wabunge wawili wa Kanda ya Kaskazini kwa tuhuma za rushwa na kuwafungulia kesi za rushwa.
Lakini hatimaye mahakama husika iliwafutia kesi zao baada ya kubaini hakuna na ushaidi wa kuwatia hatiani. Lakini wakati mahakama inatoa uamuzi huo wabunge hao waliokuwa wakigombea nafasi za uongozi kwenye chama hicho hawakuweza kugombea nafasi hizo, baada ya kuenguliwa kutokana na tuhuma hiyo ya rushwa, tukio lililohusishwa na mambo ya kisiasa.
Ni Takukuru hii hii iliyopeleleza baadhi ya tuhuma za watuhumiwa na kuwafikisha kwa ‘mbwembwe’ nyingi mahakamani, lakini sasa tunashuhudia vioja vya aina yake kwa mashahidi wanaokuja kutoa ushahdi katika kesi hizo zilifunguliowa na Takukuru, hasa kwa kutoonekana ushahidi wa kutosha wa kesi hizo zilizochunguzwa na Takukuru. (Angaliza: Kitendo cha serikali kupoteza kesi ni sawa na kupoteza heshima yake na fedha za walipa kodi – kwani hatimaye walioshinda hufungua kesi za madai dhidi ya serikali).
Kwa sababu hizo sioni sababu ya baadhi ya maofisa waandamizi wa Takukuru (wanajijua) ambao nisingependa kuwataja kwa majina katika makala hii, kuchachamaa kisirisiri kuwa ofisi ya DPP haijamburuza mahakamani kigogo huyo, ilhali wao wameshakamilisha uchunguzi. Kwa historia niliyoeleza hapo juu maofisa hao hawapaswi hata kidogo kumnyooshea kidole DPP ambaye ameonekana kujali zaidi taaluma yake ya sheria.
Wananchi wanakerwa mno na ufisadi uliokithiri kila pembe ya nchi hii, lakini kwa sababu DPP ameshatuahidi kwamba anayafanyia kazi makabrasha ya watuhumiwa wa EPA na mengineyo, kinachopaswa kufanywa hivi sasa ni kumpa muda DPP aitekeleze kazi yake bila shinikizo.
DPP ameonyesha wazi kuwa asingependa kuwaburuza mahakamani watu bila kuhakiki kwa kina kama kuna ushahidi wa kutosha kuwaburuza mahakamani, ili kukwepa kuiingiza serikali katika hasara ya kuwalipa fidia watu ambao baada ya kushinda kesi huidai fidia serikali kwa kuwadhalilisha.
Si siri kwa muda mrefu vyombo vya dola vimekuwa vikiwafungulia kesi baadhi ya wananchi kwa malengo yao binafsi, hali inayosababisha wananchi wasio na hatia kusota rumande, hali inayosababisha wananchi kujenga chuki na serikali yao.
Hakuna mtu aliye juu ya sheria au mwenye hakimiliki ya nchi hii, hivyo kila mmoja ana jukumu la kujenga nchi kulingana na nafasi yake. Hivyo tumpe nafasi Eliezer Feleshi na vijana wake wachambue kwa kina mafaili ya watuhumiwa wa EPA, mikataba mibovu na makosa mengine na wakijiridhisha wana ushaidi wawaburuze mahakamani bila kuchelewa.
Kama DPP atafanya kazi kwa msukumo wa kisiasa au kumfurahisha bosi kama wengine wanavyofanya kuliko taaluma yake ya kisheria, kuna kila dalili haki za watu kupotea pamoja na nchi kujikuta katika hasara kubwa baada ya watu kadhaa walioburuzwa mahakamani kushinda kesi walizofunguliwa.
Ni vema tukakawia lakini tukafikia. Kwani miongoni mwetu tunaochachamaa watu hawa wafikishwe mahakamani bila uchunguzi kukamilika, siku wakishinda kesi tutaanza kutoa maneno kadhaa ikiwa ni pamoja na kudai ‘wamewahonga’ mahakimu au kuburuzwa kwao mahakamani kulikuwa ni kwa lengo fulani. Tusifike huko, sote tuendelee kuibua maovu mengine na kupongeza pale serikali inapofanya vizuri..
Mungu ibariki Tanzania, Mungu Afrika.

0755 312859
katabazihappy@yahoo.com:www.katabazihappy.blogspot.com

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima Jumapili Novemba 30 mwaka 2008


Na Happiness Katabazi

ALHAMISI ya wiki hii, baadhi ya vyombo vya habari likiwamo gazeti hili, viliandika habari kwamba Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), Eliezer Feleshi, anadaiwa kumkingia kifua mmoja wa mawaziri aliyetakiwa kuingia katika mkumbo wa watu wanaofikishwa mahakamani, kwa tuhuma za matumizi mabaya ya madaraka na kuisababishia serikali hasara ya mabilioni ya shilingi.
Habari za uhakika ambazo gazeti hili lilizipata zilieleza kuwa mwanasiasa huyo ambaye kwa sasa ni mbunge wa jimbo moja lililo katika mikoa ya Kanda ya Ziwa, alinusurika kupelekwa mahakama ya Kisutu baada ya DPP kueleza wazi kuwa ushahidi wa kumburuza mahakamni haujajitosheleza.
Chanzo cha habari cha kuaminika kilizungumza na Tanzania Daima siku hiyo, kilidai kwamba hatua ya Ofisi ya Mwendesha Mashitaka (DPP) kumnusuru mwanasiasa huyo, imewashtua baadhi ya maofisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), ambao kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa wamekuwa wakilichunguza sakata la mwanasiasa huyo.
Mtoa habari wetu aliieleza gazeti hili kwamba kabla ya kuwasilishwa kwa DPP kwa ajili ya uchunguzi zaidi, maofisa wa Takukuru walikuwa wamejiridhisha kuhusu kukamilika kwa shauri hilo na kulipeleka kwa DPP kwa ajili ya hatua zaidi.
Alipotafutwa ili kuelezea taarifa hizo, Feleshi, alikanusha kuingia katika undani wa suala hilo na badala yake alibainisha wazi kuwa hawezi kufanya kazi kwa shinikizo au kwa kusikiliza taarifa za kuzusha zinazotolewa na watu kwa malengo yao, bali hufanya kazi kulingana na taaluma yake na hulifanyia uchunguzi wa kina kila faili analoletewa mezani kwake.
Awali ya yote napenda kutoa pongezi kwa serikali ya awamu ya nne kwa hatua yake ya kuanza kutoka kwenye usingizi mzito na kuanza kuwafikisha mahakamani baadhi ya watuhumiwa wakiwamo wale ‘wanaotaniwa’ na kuitwa vigogo (vigogo wako katika nchi za watu walioendelea), ambao wanatuhumiwa kwa makosa ya matumizi mabaya ya madaraka na wizi wa fedha za EPA katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam.
Nitakuwa si muungwana kama sitatoa pongezi katika hili, kwani nami nilikuwa miongoni mwa wananchi ambaye nilishiriki kikamilifu kwa miaka miwili mfululizo kwa kuandika makala za kuishinikiza serikali kuwachukulia hatua ya watuhumiwa wa makosa hayo.
Turejee kwenye hoja yetu, ambayo inadaiwa baadhi ya maofisa waandamizi hawajaridhishwa na hatua hiyo ya DPP ya kutomfungulia kesi mbunge huyo, kwanza naomba ieleweke wazi kuwa mtu anapaswa kuheshimu kazi na taaluma ya mwenzake, tukilifahamu hilo tutaweza kuheshimiana na kujenga nchi iliyo bora.
Tangu wananchi waanze kulivalia njuga suala la ufisadi, mikataba mibovu. Watanzania tunamkumbuka Mkurugenzi wa Takukuru, Edward Hoseah, baada ya kuchunguza kama mkataba wa kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond, aliutangazia umma kwamba mkataba huo hakuwa na harufu ya rushwa ndani yake, ulifuata sheria ya manunuzi ya umma na mkataba ulikuwa safi.
Baada ya taarifa yake hiyo, wananchi wa makundi mbalimbali walimpinga waziwazi hadi Bunge lilipoamua kuunda kamati ya kuchunguza mkataba huo uliojaa utata wa kila aina. Kamati hiyo iliongozwa na Dk. Harrison Mwakyembe ambaye Februari 6 mwaka huu, akisoma hotuba ya kamati yake, alisema wamebaini kampuni ya Richmond haikuwa na uwezo na kwamba sheria ya manunuzi haikufuatwa. Kwa sababu hiyo walioshiriki kuipa tenda kampuni hiyo hawakuzingatia maslahi ya taifa.
Ripoti hiyo ilisababisha aliyekuwa waziri mkuu, Edward Lowassa, Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dk. Ibrahim Msabaha, kujiuzulu nyadhifa zao baada ya kuhusishwa na kashfa hiyo.
Si hivyo tu, kwa wale tunaofutilia kwa karibu mwenendo wa mambo wa taifa letu, tutakumbuka kwamba mwaka jana wakati CCM ikiwa kwenye mchakato wa chaguzi za ndani, ni maofisa hao hao wa Takukuru waliwakamata wabunge wawili wa Kanda ya Kaskazini kwa tuhuma za rushwa na kuwafungulia kesi za rushwa.
Lakini hatimaye mahakama husika iliwafutia kesi zao baada ya kubaini hakuna na ushaidi wa kuwatia hatiani. Lakini wakati mahakama inatoa uamuzi huo wabunge hao waliokuwa wakigombea nafasi za uongozi kwenye chama hicho hawakuweza kugombea nafasi hizo, baada ya kuenguliwa kutokana na tuhuma hiyo ya rushwa, tukio lililohusishwa na mambo ya kisiasa.
Ni Takukuru hii hii iliyopeleleza baadhi ya tuhuma za watuhumiwa na kuwafikisha kwa ‘mbwembwe’ nyingi mahakamani, lakini sasa tunashuhudia vioja vya aina yake kwa mashahidi wanaokuja kutoa ushahdi katika kesi hizo zilifunguliowa na Takukuru, hasa kwa kutoonekana ushahidi wa kutosha wa kesi hizo zilizochunguzwa na Takukuru. (Angaliza: Kitendo cha serikali kupoteza kesi ni sawa na kupoteza heshima yake na fedha za walipa kodi – kwani hatimaye walioshinda hufungua kesi za madai dhidi ya serikali).
Kwa sababu hizo sioni sababu ya baadhi ya maofisa waandamizi wa Takukuru (wanajijua) ambao nisingependa kuwataja kwa majina katika makala hii, kuchachamaa kisirisiri kuwa ofisi ya DPP haijamburuza mahakamani kigogo huyo, ilhali wao wameshakamilisha uchunguzi. Kwa historia niliyoeleza hapo juu maofisa hao hawapaswi hata kidogo kumnyooshea kidole DPP ambaye ameonekana kujali zaidi taaluma yake ya sheria.
Wananchi wanakerwa mno na ufisadi uliokithiri kila pembe ya nchi hii, lakini kwa sababu DPP ameshatuahidi kwamba anayafanyia kazi makabrasha ya watuhumiwa wa EPA na mengineyo, kinachopaswa kufanywa hivi sasa ni kumpa muda DPP aitekeleze kazi yake bila shinikizo.
DPP ameonyesha wazi kuwa asingependa kuwaburuza mahakamani watu bila kuhakiki kwa kina kama kuna ushahidi wa kutosha kuwaburuza mahakamani, ili kukwepa kuiingiza serikali katika hasara ya kuwalipa fidia watu ambao baada ya kushinda kesi huidai fidia serikali kwa kuwadhalilisha.
Si siri kwa muda mrefu vyombo vya dola vimekuwa vikiwafungulia kesi baadhi ya wananchi kwa malengo yao binafsi, hali inayosababisha wananchi wasio na hatia kusota rumande, hali inayosababisha wananchi kujenga chuki na serikali yao.
Hakuna mtu aliye juu ya sheria au mwenye hakimiliki ya nchi hii, hivyo kila mmoja ana jukumu la kujenga nchi kulingana na nafasi yake. Hivyo tumpe nafasi Eliezer Feleshi na vijana wake wachambue kwa kina mafaili ya watuhumiwa wa EPA, mikataba mibovu na makosa mengine na wakijiridhisha wana ushaidi wawaburuze mahakamani bila kuchelewa.
Kama DPP atafanya kazi kwa msukumo wa kisiasa au kumfurahisha bosi kama wengine wanavyofanya kuliko taaluma yake ya kisheria, kuna kila dalili haki za watu kupotea pamoja na nchi kujikuta katika hasara kubwa baada ya watu kadhaa walioburuzwa mahakamani kushinda kesi walizofunguliwa.
Ni vema tukakawia lakini tukafikia. Kwani miongoni mwetu tunaochachamaa watu hawa wafikishwe mahakamani bila uchunguzi kukamilika, siku wakishinda kesi tutaanza kutoa maneno kadhaa ikiwa ni pamoja na kudai ‘wamewahonga’ mahakimu au kuburuzwa kwao mahakamani kulikuwa ni kwa lengo fulani. Tusifike huko, sote tuendelee kuibua maovu mengine na kupongeza pale serikali inapofanya vizuri..
Mungu ibariki Tanzania, Mungu Afrika.

0755 312859
katabazihappy@yahoo.com:www.katabazihappy.blogspot.com

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima Jumapili Novemba 30 mwaka 2008

Na Happiness Katabazi

ALHAMISI ya wiki hii, baadhi ya vyombo vya habari likiwamo gazeti hili, viliandika habari kwamba Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), Eliezer Feleshi, anadaiwa kumkingia kifua mmoja wa mawaziri aliyetakiwa kuingia katika mkumbo wa watu wanaofikishwa mahakamani, kwa tuhuma za matumizi mabaya ya madaraka na kuisababishia serikali hasara ya mabilioni ya shilingi.
Habari za uhakika ambazo gazeti hili lilizipata zilieleza kuwa mwanasiasa huyo ambaye kwa sasa ni mbunge wa jimbo moja lililo katika mikoa ya Kanda ya Ziwa, alinusurika kupelekwa mahakama ya Kisutu baada ya DPP kueleza wazi kuwa ushahidi wa kumburuza mahakamni haujajitosheleza.
Chanzo cha habari cha kuaminika kilizungumza na Tanzania Daima siku hiyo, kilidai kwamba hatua ya Ofisi ya Mwendesha Mashitaka (DPP) kumnusuru mwanasiasa huyo, imewashtua baadhi ya maofisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), ambao kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa wamekuwa wakilichunguza sakata la mwanasiasa huyo.
Mtoa habari wetu aliieleza gazeti hili kwamba kabla ya kuwasilishwa kwa DPP kwa ajili ya uchunguzi zaidi, maofisa wa Takukuru walikuwa wamejiridhisha kuhusu kukamilika kwa shauri hilo na kulipeleka kwa DPP kwa ajili ya hatua zaidi.
Alipotafutwa ili kuelezea taarifa hizo, Feleshi, alikanusha kuingia katika undani wa suala hilo na badala yake alibainisha wazi kuwa hawezi kufanya kazi kwa shinikizo au kwa kusikiliza taarifa za kuzusha zinazotolewa na watu kwa malengo yao, bali hufanya kazi kulingana na taaluma yake na hulifanyia uchunguzi wa kina kila faili analoletewa mezani kwake.
Awali ya yote napenda kutoa pongezi kwa serikali ya awamu ya nne kwa hatua yake ya kuanza kutoka kwenye usingizi mzito na kuanza kuwafikisha mahakamani baadhi ya watuhumiwa wakiwamo wale ‘wanaotaniwa’ na kuitwa vigogo (vigogo wako katika nchi za watu walioendelea), ambao wanatuhumiwa kwa makosa ya matumizi mabaya ya madaraka na wizi wa fedha za EPA katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam.
Nitakuwa si muungwana kama sitatoa pongezi katika hili, kwani nami nilikuwa miongoni mwa wananchi ambaye nilishiriki kikamilifu kwa miaka miwili mfululizo kwa kuandika makala za kuishinikiza serikali kuwachukulia hatua ya watuhumiwa wa makosa hayo.
Turejee kwenye hoja yetu, ambayo inadaiwa baadhi ya maofisa waandamizi hawajaridhishwa na hatua hiyo ya DPP ya kutomfungulia kesi mbunge huyo, kwanza naomba ieleweke wazi kuwa mtu anapaswa kuheshimu kazi na taaluma ya mwenzake, tukilifahamu hilo tutaweza kuheshimiana na kujenga nchi iliyo bora.
Tangu wananchi waanze kulivalia njuga suala la ufisadi, mikataba mibovu. Watanzania tunamkumbuka Mkurugenzi wa Takukuru, Edward Hoseah, baada ya kuchunguza kama mkataba wa kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond, aliutangazia umma kwamba mkataba huo hakuwa na harufu ya rushwa ndani yake, ulifuata sheria ya manunuzi ya umma na mkataba ulikuwa safi.
Baada ya taarifa yake hiyo, wananchi wa makundi mbalimbali walimpinga waziwazi hadi Bunge lilipoamua kuunda kamati ya kuchunguza mkataba huo uliojaa utata wa kila aina. Kamati hiyo iliongozwa na Dk. Harrison Mwakyembe ambaye Februari 6 mwaka huu, akisoma hotuba ya kamati yake, alisema wamebaini kampuni ya Richmond haikuwa na uwezo na kwamba sheria ya manunuzi haikufuatwa. Kwa sababu hiyo walioshiriki kuipa tenda kampuni hiyo hawakuzingatia maslahi ya taifa.
Ripoti hiyo ilisababisha aliyekuwa waziri mkuu, Edward Lowassa, Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dk. Ibrahim Msabaha, kujiuzulu nyadhifa zao baada ya kuhusishwa na kashfa hiyo.
Si hivyo tu, kwa wale tunaofutilia kwa karibu mwenendo wa mambo wa taifa letu, tutakumbuka kwamba mwaka jana wakati CCM ikiwa kwenye mchakato wa chaguzi za ndani, ni maofisa hao hao wa Takukuru waliwakamata wabunge wawili wa Kanda ya Kaskazini kwa tuhuma za rushwa na kuwafungulia kesi za rushwa.
Lakini hatimaye mahakama husika iliwafutia kesi zao baada ya kubaini hakuna na ushaidi wa kuwatia hatiani. Lakini wakati mahakama inatoa uamuzi huo wabunge hao waliokuwa wakigombea nafasi za uongozi kwenye chama hicho hawakuweza kugombea nafasi hizo, baada ya kuenguliwa kutokana na tuhuma hiyo ya rushwa, tukio lililohusishwa na mambo ya kisiasa.
Ni Takukuru hii hii iliyopeleleza baadhi ya tuhuma za watuhumiwa na kuwafikisha kwa ‘mbwembwe’ nyingi mahakamani, lakini sasa tunashuhudia vioja vya aina yake kwa mashahidi wanaokuja kutoa ushahdi katika kesi hizo zilifunguliowa na Takukuru, hasa kwa kutoonekana ushahidi wa kutosha wa kesi hizo zilizochunguzwa na Takukuru. (Angaliza: Kitendo cha serikali kupoteza kesi ni sawa na kupoteza heshima yake na fedha za walipa kodi – kwani hatimaye walioshinda hufungua kesi za madai dhidi ya serikali).
Kwa sababu hizo sioni sababu ya baadhi ya maofisa waandamizi wa Takukuru (wanajijua) ambao nisingependa kuwataja kwa majina katika makala hii, kuchachamaa kisirisiri kuwa ofisi ya DPP haijamburuza mahakamani kigogo huyo, ilhali wao wameshakamilisha uchunguzi. Kwa historia niliyoeleza hapo juu maofisa hao hawapaswi hata kidogo kumnyooshea kidole DPP ambaye ameonekana kujali zaidi taaluma yake ya sheria.
Wananchi wanakerwa mno na ufisadi uliokithiri kila pembe ya nchi hii, lakini kwa sababu DPP ameshatuahidi kwamba anayafanyia kazi makabrasha ya watuhumiwa wa EPA na mengineyo, kinachopaswa kufanywa hivi sasa ni kumpa muda DPP aitekeleze kazi yake bila shinikizo.
DPP ameonyesha wazi kuwa asingependa kuwaburuza mahakamani watu bila kuhakiki kwa kina kama kuna ushahidi wa kutosha kuwaburuza mahakamani, ili kukwepa kuiingiza serikali katika hasara ya kuwalipa fidia watu ambao baada ya kushinda kesi huidai fidia serikali kwa kuwadhalilisha.
Si siri kwa muda mrefu vyombo vya dola vimekuwa vikiwafungulia kesi baadhi ya wananchi kwa malengo yao binafsi, hali inayosababisha wananchi wasio na hatia kusota rumande, hali inayosababisha wananchi kujenga chuki na serikali yao.
Hakuna mtu aliye juu ya sheria au mwenye hakimiliki ya nchi hii, hivyo kila mmoja ana jukumu la kujenga nchi kulingana na nafasi yake. Hivyo tumpe nafasi Eliezer Feleshi na vijana wake wachambue kwa kina mafaili ya watuhumiwa wa EPA, mikataba mibovu na makosa mengine na wakijiridhisha wana ushaidi wawaburuze mahakamani bila kuchelewa.
Kama DPP atafanya kazi kwa msukumo wa kisiasa au kumfurahisha bosi kama wengine wanavyofanya kuliko taaluma yake ya kisheria, kuna kila dalili haki za watu kupotea pamoja na nchi kujikuta katika hasara kubwa baada ya watu kadhaa walioburuzwa mahakamani kushinda kesi walizofunguliwa.
Ni vema tukakawia lakini tukafikia. Kwani miongoni mwetu tunaochachamaa watu hawa wafikishwe mahakamani bila uchunguzi kukamilika, siku wakishinda kesi tutaanza kutoa maneno kadhaa ikiwa ni pamoja na kudai ‘wamewahonga’ mahakimu au kuburuzwa kwao mahakamani kulikuwa ni kwa lengo fulani. Tusifike huko, sote tuendelee kuibua maovu mengine na kupongeza pale serikali inapofanya vizuri..
Mungu ibariki Tanzania, Mungu Afrika.

0755 312859
katabazihappy@yahoo.com:www.katabazihappy.blogspot.com

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima Jumapili Novemba 30 mwaka 2008

No comments:

Powered by Blogger.