Header Ads

UAMUZI KESI YA MGOMO WA WALIMU KESHO

Na Happiness Katabazi MAHAKAMA Kuu Divisheni ya Kazi Dar es Salaam, jana ilishindwa kutoa uamuzi wake kama ilivyoaidi katika maombi madogo yaliyowasilishwa na Katibu Mkuu Kiongozi na wenzake dhidi ya Chama cha Walimu(CWT), yaliyooiomba mahakama hiyo itoe amri ya muda ya kuzuia mgomo wa walimu unaoendelea chini nzima kwasababu mgomo huo ni batili. Mbali na Katibu Mkuu Kiongozi walalamikaji wengine ni Katibu Mkuu ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Na.1/2012 dhidi ya CWT wanaowakilishwa na mawakili wa waandamizi wa serikali Pius Mboya na Obadia Kameya. Ambapo wakili Kameya ambapo walalamikaji hao wanaomba mambo mawili ambayo wanaomba mahakama itamke mgomo huo ni batili kwasababu haujakidhi matakwa ya kifungu cha 26(1) cha Sheria ya Usuluhishi wa migogoro ya mwafanyakazi Na.6 ya mwaka 2003 ,ambapo kifungu hicho kinatoa utaratibu wa mtumishi wa umma azifuate kabla hajaanza kugoma ambapo zinataka mfanyakazi anayetaka kugoma kwanza atoe hati ya kukusudio la mgomo wa serikali siku 60. Jambo ambalo CWT hawakulizingatia kabla ya kutangaza nia yao ya mgomo ambayo waliitangza Julai 27 mwaka huu tena bila kuwapatia nakala ya kusudio hilo walalamikaji. Ombi la pili wakili Kameya anaomba mahakama hiyo itoe amri ya kuzuia kuendelea kwa mgomo batili kwasababu unaathiri wanafunzi na kuleta mashadhara makubwa ambayo hayalipiki kwani serikali imeweka mitaala ya elimu mashuleni na shule zimeweka muda wa vipindi kufundishwa hivyo kuendelea kuwepo kwa mgomo ni wazi kuna vuruga malengo ya mitaala na muda wa vipindi mashuleni. Wakili Kameya pia aliomba mahakama imumzuei Rais wa CWT,Gration Mukoba na wenzake kutoka kwenda tena kwenye vyombo vya habari kuelezea kesi ya msingi iliyopo mahakamani hapo kwani juzi walienda kwenye vyombo vya habari na kuizungumizia kesi hiyo jambo ambalo ni kinyume cha sheria na pia wanaiomba mahakama itoe amri ya kumtaka Mkoba kwenda kwenye vyombo vya habari kuuutangazia umma kuwa mgomo huo ni batili na awataka walimu wote warejee makazini. Mawakili hao wa serikali na wakili wa utetezi Gabriel Mnyele walianza kuwasilisha hoja zao tangu saa sababa mchana hadi saa kumi jioni, ambapo kwa upande wake Mnyele alidai mgomo huo wa walimu haujakiuka sheria zozote za nchi kwani umekithi matakwa ya Sheria Na. 4 ya Ajira na Mahusiano Kazini ya mwaka 2006, ambayo inamruhusu mfanyakazi wa serikali au sekta binafsi kutoa hati ya kusudio la kutaka kugoma ndani ya 48 kama walivyofanya CWT. Na kwa mujibu wa madai ya msingi wanayoyadai walimu hao ambayo ndiyo yamesababisha wagome ni kutaka kuishinikiza serikali iwaongezee mshahara kwa asilimia mia moja. Baada ya mawakili hao kumaliza kuwasilisha hoja zao saa 10:45 jioni katika mahakama ya wazi ndipo Jaji Sophia Wambura alisema amesikiliza hoja za pande zote mbili na akaairisha shauri hilo kwa nusu saa na kwamba akirejea tena ndiyo atatoa uamuzi wake kuhusu hoja hizo. Ilipika saa 12:6 jioni huyo aliingia kwenye ofisi yake badala ya ukumbi wa wazi wa awali aliokuwa akisikilizia kesi hiyo na kusema kwa kifupi tu ‘uamuzi wa malumbano hayo ya kisheria atautoa kesho saa nane mchana. Baada ya jaji huyo kumaliza kusema maneno hayo kwa kifupi, baadhi ya walimu waliokuwa wamefika mahakamani hapo walisikika wakisema na kuwapigia simu wenzao kwakuwa mgomo huko pale pale kwani mahakama haijatoa amri ya kuzuia mgomo wao. Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumatano, Agosti Mosi mwaka 2012.

No comments:

Powered by Blogger.