Header Ads

KESI YA VIGOGO WA SUMA JKT YAIVA

Na Happiness Katabazi MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kusutu Dar es Salaam, imesema Agosti 30 mwaka huu, upande wa jamhuri katika kesi ya kula njama na matumizi mabaya ya madaraka inayomkabili Mkurugenzi wa Shirika Jeshi la Kujenga Taifa (SUMA JKT) Kanali Ayoub Mwakang’ata na maofisa wenzake sita utawasomea maelezo ya awali. Hayo yalisemwa jana hakimu Mkazi Aloyce Katema jana muda mfupi baada ya wakili wa serikali Liz Kiwia kuikumbusha mahakama kuwa kesi hiyo jana ilikuja kwaajili ya kutajwa na kwamba wanaoiomba mahakama iwapangie tarehe ya kuja kuwasomea maelezo ya awali washitakiwa. Mbali na Kanali Mwakang’ta washitakiwa wengine ni Luteni kanali Mkohi Kichogo,Luteni Kanali Paul Mayavi,Meja Peter Lushika,Sajenti John lazier,Meja Yohana Nyichi na Mkurugenzi wa Miradi ya Matrekta wa SUMA JKT-Luteni Kanali Felex Samillan. Mawakili toka ofisi ya Kuzuia na Kupamba na Rushwa(TAKUKURU) wanaotetewa na wakili wa kujitegema Majura Magafu. Julai 2 mwaka huu, mawakili wa taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Dominsian Kessy na Ben Lincoln waliwafikisha washitakiwa hao mahakamani hapa kwa mara ya kwanza wakidaiwa kutenda kosa la kwanza ni la matumizi mabaya ya madaraka kinyume na kifungu cha 31 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ya mwaka 2007, inayowakabili washitakiwa wote. Wakili Kessy alidai kuwa Machi 5 mwaka 2009 katika chumba cha mikutano cha ofisi ya SUMA JKT Dar es salaam,wakiwa ni wajumbe wa bodi na Bodi ya Tenda ya SUMA JKT kwa makusudi walitumia madaraka yao vibaya kwa kutoa maamuzi ya bodi hiyo ambayo yaliyoonyesha yametolewa na TAKOPA kwa madhumuni ya kununua magari na vifaa vya ujenzi bila kupata idhini ya kutoka Bodi ya ya Wakurugenzi ya TAKOPA. Wakili Kessy alidai kosa la pili pia ni la matumuzi mabaya ya madaraka ambalo linawakabiliwa washitakiwa wote kuwa Machi 12 mwaka 2012 ,washitakiwa hao wakiwa ni wajumbe wa bodi ya Tenda ya SUMA JKT walitumia madaraka yao vibaya kwa kupitishia maazimio ya kununuliwa kwa magari na vifaa vya ujenzi ambavyo vilikuwa vimeishatumika kinyume na kifungu cha 58( 3) cha Sheria ya Mamunuzi ya Umma ya mwaka 2005. Katika hatua nyingine Mkuu wa Gereza la Kuu la Ukonga, Kamishina Msaidizi wa Magereza Estimi Mkwavi(58), alikuja kutoa ushahidi wake katika kesi ya kukutwa na simu gerezani inayomkabili aliyekuwa Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala wa Benki Kuu, Amatus Liyumba ambapo alidai Julai 27 mwaka 2011 akiwa na wadhifa huo aliletewa taarifa na Supretendant John, kuwa liyumba ambaye alikuwa mfungwa katika gereza hilo amekutwa na simu gerezani. Mawakili wa serikali Humphrei Maricky na Tumaini Kweka ambao walikuwa wakimuongoza ACP-Mkwavi kutoa ushahidi wao alidai kuwa baada ya kupata taarifa hizo aliagiza Liyumba aletwe ofisini kwake ili aweze kumhojia na Liyumba alipofika ofisini kwake walimhoji na alikiri kutenda kosa hilo ila akasema hajisikii vizuri hivyo anaomba atoe maelezo yake kwa njia ya maandishi na aliyatoa maelezo hayo ambayo yanonyesha Liyumba alikiri kukutwa na simu hiyo lakini hata hivyo wakili wa utetezi Majura Magafu aliiomba mahakama iisipokee karatasi hilo kwani ungamo hilo halijakidhi matakwa ya kifungu cha 48 na 58 cha Sheria ya Makosa ya Jinai ya mwaka 2002 ,ambapo vifungu hivyo vinatoa mamlaka kwa mlinzi wa amani na afisa wa polisi kuchukua ungamo la mshitakiwa yoyote na kwamba ungamo hilo halikuchukuliwa na mlinzi wa amani na ofisa wa polisi, hivyo Magafu akaomba mahakama isiipokee hiyo nyaraka inayoonyesha Liyumba alikiri kosa kwasababu ni batili kisherioa. Baada ya mvutano huo wa kisheria hakimu Mkazi Stewart Sanga aliarisha kesi hiyo hadi leo ambapo atakuja kutolea uamuzi wake wa amana nyaraka hiyo ipokelewe kama kielelezo au isipokelewe. Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Alhamisi, Agosti 2 mwaka 2012.

No comments:

Powered by Blogger.