Header Ads

MKENYA KORTINI KWA KUIHUJUMU TCRA


Mkenya kizimbani kwa kuiujumu TCRA
Na Happiness Katabazi
RAIA wa   Kenya, Nelson Rading Onyango Jana amefikishwa  katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, akikabiliwa na  na  saba  likiwamo kosa la  kutoa huduma ya mawasiliano ya Kimataifa bila ya kuwa na leseni na kuisababishia hasara  Mamlaka ya Mawasiliano  nchini (tcra), zaidi ya Sh.ya zaidi ya Sh.bilioni  6.8 .

Wakili Mwandamizi wa serikali Tumaini Kweka Mbele ya Hakimu Devotha Kisoka   alidai kuwa   kati ya Julai 2010 na Novemba 2013 katika eneo  la Kariakoo  mshtakiwa huyo  kwa nia ovu alifanya udanganyifu  katika  matumizi ya kimtandao kinyume cha sheria.

Wakili Kweka  alidai kuwa  Onyango   kwa nia ovu  na udanganyifu  alikuwa akifanyisha huduma za mawasiliano ya Kimataifa huku akikwepa  kutumia njia halali za maalipo  ambazo zinatolewa na ( TCRA.

Shitaka la pili, Wakili Kweka alidai Kuwa mshitakiwa Huyo   anadaiwa kutoa huduma ya mawasiliano bila ya kuwa na leseni inayomruhusu kufanya hivyo.

Kweka  alidai kuwa  katika kipindi hicho, mshtakiwa huyo  bila ya kuwa na uhalali kisheria  alitoa huduma ya simu za Kimataifa  bila ya kuwa na leseni  inayotolewa na TCRA.

Mshtakiwa huyo  katika Shtaka la tatu anadaiwa kuwa   kati ya  Januari 2013 na Novemba 2013 akiwa katika eneo hilo la Kariakoo alitumia  kadi za simu ambazo hazijasajiliwa kama inavyotakiwa kisheria zenye  namba 0778350683,0778498179,0774395401,0774552099,0774552122,0774552138 na 0777225.

Alizitaja namba nyingine kuwa ni 07748802243,0774802250,0774802255,0774802265,07748022278,0777848892,0779579620,0779579848,0779663386,0779716796,0779716800,0779716804,0779716811,0779716812,0779716822 na 077971.

Shtaka la nne, mshtakiwa huyo   anadaiwa kuingiza nchi ni vifaa vya kielectroniki  bila ya kuwa na kibali kinachomruhusu kufanya hivyo.
Akiendelea kusoma mashtaka yanayomkabili  Onyango , Wakili Kweka alidai kuwa  siku isiyofahamika   aliingiza mitambo ya mawasiliano ambayo ni SIM Boxi  bila ya kuwa na kibali.

Wakili Kweka, shtaka la tano alidai kuwa licha ya kuingiza nchini mitambo hiyo bila ya kuwa na kibali mshtakiwa huyo, alisimika mitambo mine  ya mawasiliano  na kuiendesha  ambayo ni SM Boxi  zenye namba za siri  TX 2SN5600C5/05, TX2SN48002/K21, TX2SN102335A na  wa  Cisco  Router  iliyotengenezwa Cisco AS5300 mfululizo  yenye namba ya siri ASN 050-332-940 na AP12KGCAA.

Katika shtaka la sita, wakili huyo wa Serikali Mwandamizi alidai kuwa Onyango alitumia mitambo hiyo  ya Kielectroniki ambayo ilikuwa haijathibitishwa na TCRA.

Aliongeza kudai kuwa Novemba 22, 2013 Kariakoo , akiwa na ufahamu  kuwa mitambo hiyo haijathibitishwa na TCRA aliitumia.

Shtaka la saba, mshtakiwa huyo anadaiwa kusababisha hasara kwa mamlaka  husika ya TCRA  kati ya Julai 2010 na Novemba 2013  kwa kufanya huduma hizo za mawasiliano ya Kimataifa bila ya kuwa na leseni .

Ilidaiwa kuwa kati ya Julai 2010 na Novemba 2013 mshtakiwa huyo alichepusha  mawasiliano ya simu za Kimataifa  kwa kutumia namba hizo ambazo hazijasajiliwa  na TCRA  na kwamba kutokana na kitendo hicho aliisababishia mamlaka hiyo hasara ya Sh 6,842,880,000.00.
Baada ya kusomewa mashtaka hayo, mshtakiwa aliyakana yote na upande wa mashtaka ulidai kuwa upelelezi bado haujakamilika.

Hakimu Devotha Kisoka alimwambia mshtakiwa huyo kuwa kulingana na makosa hayo yanayomkabili dhamana ipo wazi hivyo alimtaka kutoa fedha taslimu mahakamani hapo Sh 3.4 bilioni na kuwa na wadhamini wawili wanaoaminika.

Akiendelea kutoa masharti  hayo ya dhamana, hakimu Kisoka alisema mdhamini mmoja kati ya wadhamini hao wawili awe ni mtumishi wa serikali  na mwingine atakayekubalika na mahakama na kwamba wadhamini wote hao watasaini bondi ya Sh  milioni 50.

Kesi  imeahirishwa hadi Aprili 8, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa na mshtakiwa alipelekwa rumande baada ya kushindwa kukamilisha masharti hayo ya dhamana.

Chanzo: Gazeti la Tanzania Daima la Alhamisi, Machi 27 Mwaka 2014

No comments:

Powered by Blogger.