Header Ads

UB KUWAFUNDA WATETEZI WA HAKI ZA BINADAMU EAC


 UB KUWAFUNDA  WATETEZI HAKI ZA BINADAMU 
Na Happiness Katabazi (UB)
CHUO Kikuu Cha Bagamoyo (UB) , Dar Es Salaam, kimendaa Mafunzo maalumu ya kuwajengea uwezo mpana watetezi  wa Haki za Binadamu toka nchi tano za Afrika Mashariki.

Akizungumza na Ofisa Habari wa (UB), Ofisa Mradi huo ambao unaendeshwa na Kitivo Cha Sheria Cha Chuo huko kwa kufadhiliwa na Akiba Uhaki  Foundation ya Nairobi Kenya, Teddy Sawaya ofisini kwake Kawe Beach Dar es Salaam,alisema  Mafunzo hayo yatashirikisha jumla ya wanafunzi 10.

Sawaya  ambaye ni Mhadhiri wa Sheria wa UB, (Pichani) alisema washiriki wa kozi hiyo ni watu  wanaotokea Katika Taasisi zinazojihusisha na Kazi ya utetezi wa Haki za binadamu na kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea wigi mpana   zaidi Katika eneo Hilo la utetezi wa Haki za binadamu,  watetezi Hao wa Haki za binadamu na Jamii kwa  ujumla.

Alisema Tayari washiriki wameishathibitisha kushiriki  Mafunzo hayo na kwamba Mafunzo hayo hatakuwa yakiendeshwa ndani ya madarasa  la Chuo Kikuu Cha Bagamoyo yaliyopo Kawe Beach Dar Es Salaam na Mafunzo yataanza rasmi Septemba 8  mwaka huu ambapo yatafunguliwa ramsi na Naibu Makamu Mkuu wa chuo hicho anayeshughulikia Fedha na Utawala, Dk.Elifuraha Mtaro mafunzo hayo yatamalizika  Februali 22 Mwaka 2015.

Hii ni Mara ya pili  kwa Chuo Kikuu cha Bagamoyo , kuendesha Mafunzo hayo   ya utetezi wa Haki za binadamu kwa kuudhuliwa   na washiriki toka nchi tano za Afrika Mashariki .Mara ya kwanza UB iliendesha kozi hiyo  Septemba 8- Oktoba 20 Mwaka Jana.

Chanzo: Facebook: University of Bagamoyo 
Website: www.uob.ac.tz
Septemba 4 Mwaka 2014



No comments:

Powered by Blogger.