Header Ads

MABAHARIA KESI YA SAMAKI WA MAGUFULI "HAKIELEWEKI"

Na Happiness Katabazi

HATIMAYE Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, jana ilisikiliza ombi la dhamana lililowasilishwa mahakamani hapo na upande wa utetezi katika kesi ya uvuvi haramu kwenye ukanda wa Bahari ya Hindi inayowakabili raia 36 wa kigeni.

Ombi hilo liliwasilishwa na mawakili wa utetezi Ibrahim Bendera na John Mapinduzi mbele ya Jaji Radhia Shekhe ambapo waliomba mahakama hiyo iwapatie dhamana wateja wao kwa kuwa mashtaka yanayowakabili yanadhaminika kwa mujibu wa kifungu cha 148 (6) na (7) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 2002.

“Tunaomba mahakama hii iwapatie wateja wetu dhamana hasa ukizingatia wamekaa rumande muda mrefu na makosa yanayowakabili yanadhaminika kwa mujibu wa kifungu hicho ila ni kweli nakili wateja wangu hawana mahali pa kuishi hapa nchini licha kwa sasa wanaishi gerezani,” alidai wakili Mapinduzi.

Kwa upande wake Wakili Mwandamizi wa Serikali Biswalo Mganga alidai kuwa upande wa Jamhuri hauna pingamizi na ombi hilo ingawa wanaiomba mahakama kabla haijakubali ombi hilo izingatie kwamba watuhumiwa hao si raia, hawana vibali vya kuishi nchini na kuendelea kwao kuwa mahabusu ni kwa usalama wa maisha yao pia.

“Tunaomba mahakama hii iwapatie wateja wetu dhamana hasa ukizingatia wamekaa rumande muda mrefu na makosa yanayowakabili yanadhaminika kwa mujibu wa kifungu hicho ila ni kweli nakili wateja wangu hawana mahali pa kuishi hapa nchini licha kwa sasa wanaishi gerezani. ”alidai wakili John Mapinduzi.

Hata hivyo Jaji Shekhe alisikiliza hoja za pande zote mbili na kuahidi kutoa uamuzi wa mahakama hiyo kwa maandishi.

Wakati huo huo Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, ililazimika kuairisha usikilizaji wa kesi ya kuomba rushwa ya sh milioni 10 inayomkabili aliyekuwa Mtangazaji wa Shirika la Utangazaji nchini(TBC1), Jerry Murro, na wenzake baada ya wakili wa utetezi Majura Magafu kushindwa kufika mahakamani.

Hakimu Mkazi Gabriel Mirumbe alisema kwa sababu hiyo ameahirisha usikilizwaji wa kesi hiyo hadi Januari 24, 25 na 26 mwaka huu kwa kuwataka wahusika wa pande zote kufika mahakamani.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Januari 18 mwaka 2011

No comments:

Powered by Blogger.