Header Ads

HAMAD RASHI AITIA KITANZI CUF KORTINI

Na Happiness Katabazi

HATIMAYE mbunge wa Wawi Hamad Rashid Mohamed(CUF), na wenzake 10 jana waliwasilisha maombi madogo katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, wakiomba mahakama hiyo itamke kuwa uamuzi wa Baraza la Uongozi Taifa la chama hicho uliomvua uanachama yeye na wenzake ni batili.

Mbali na Hamad walalamikaji wengine Shoka Khamisi Juma, Doyo Hassan Doyo, Juma Said Sanani, Yassin Mrotwa,Kirungi Amir Kiurungi,Doni Waziri Mnyamani, Mohamed Faki Albadawi,Tamim Omari Tamim,Nanjase Haji Nanjase na Mohamed Massaga ambao wanatetewa na wakili Augustine Kusilika toka kampuni ya uwakili ya GF Law Chambers dhidi ya Bodi ya Udhamini ya chama hicho.

Ombi hilo ambalo nalo limepewa Na.1/2011 na limewasilisha chini ya hati ya dharula licha bado halijapangiwa tarehe ya kuanza kusikilizwa.

Kwa mujibu wa hati hiyo ya madai ambayo ina maombi manne, ombi la kwanza, Hamad na wenzake wanaiomba mahakama itoe amri kwa bodi ya baraza la wadhamini na wajumbe wa baraza kuu la chama hicho wajieleze ni kwanini wasitiwe hatiani kama wafungwa kesi ya madai kwa kitendo chao cha kudharau uamuzi wa upande mmoja uliotolewa na Januari 4 mwaka huu, ambayo iliwataka wadaiwa hao au mawakala wao wasifanye jambo lolote ambalo lilikuwa na lengo la kuwafukuza uanachama wadaiwa hadi ombi hilo dogo la lilotolewa uamuzi siku hiyo ya Januari 4 mwaka huu, litakapokuja kusikilizwa na pande zote mbili.

Katika ombi la pili, Hamad anaiomba mahakama itamke kuwa utaratibu wote uliofanywa na wadaiwa Januari 4 mwaka huu jioni mjini Zanzibar baada ya Jaji Agustine Shangwa wa Mahakama Kuu, kutoa uamuzi ule wa upande mmoja kuwa ni batili.

Ombi la tatu, walalamikaji hao wanaomba mahakama iwaamuru wadaiwa kulipa gharama za uendeshaji wa ombi hilo dogo na ombi la nne wanaiomba mahakama itoe amri nyingine itakazoona zinafaa.

Januari 4 mwaka huu, saa nne asubuhi Jaji Agustine Shangwa alitoa amri ya kuzuia Hamad Rashid na wenzake wasifukuzwe uanachama hadi maombi hayo madogo Na.1/2012 yatakapokuja kwaajili ya kusikilizwa na pande zote mbili na ilipofika saa 6:30 mchana ya siku hiyo Hatibu Omari ambaye ni mtumishi wa mahakama anayeshughulika na jukumu la kuwapelekea wahusika wa kesi mbalimbali hati za wito wa kuitwa mahakamani au amri zilizokwishatolewa na mahakama.

Na kwa mujibu wa nakala ya kiapo ambacho Tanzania Daima Jumatano inayo nakala yake, kilichoapwa na Omari , Januari 4 mwaka huu, katika kiapo kinamnukuu Omari akisema; “Nathibitisha kwamba nilipeleka uamuzi huo uliotolewa na Jaji Shangwa pale Buguruni kwenye ofisi Kuu ya chama cha CUF na Bwana Mikidadi ambaye nimemkuta hapo ofisini alikataa kupokea uamuzi huo bila sababu za msingi”alisema Omari katika kiapo chake.

Januari 4 mwaka huu, Jaji Shangwa akitoa uamuzi wake siku hiyo alisema Januari 3 mwaka huu, wadaiwa hao waliwasilisha ombi dogo dhidi ya Bodi ya Wadhamini ya chama cha CUF liliomba mahakama hiyo itoe uamuzi wa kwa kusikiliza upande mmoja ambao uamuzi huo utazuia Baraza Kuu la Taifa la CUF ambalo lilikuwa likiketi Januari 4 mwaka huu mjini Zanzibar , lisiwafukuze uanachama walalamikaji kwani endapo watavuliwa uanachama haki zao za Kikatiba kama wanachama wa chama hicho zitakuwa zimevunjwa.

Pia Hamad siku hiyo mbele ya Shangwa kupitia wakili wake wakiwasilisha hoja zao walidai sababu nyingine yakuwasilisha ombi lile ambalo lilikishwa tolewa uamuzi siku hiyo na jaji huyo ni kwamba tayari walishafungua kesi ya msingi mahakamani hapo ambayo bado haijatolewa uamuzi na katika madai yao ya msingi walalamikaji hao wanaipinga uhalali wa Kamati ya Nidhamu na Maadili iliyoundwa nje ya Katiba ya chama na wajumbe wa Kamati Kuu ambao ndani ya wajumbe wa Kamati hiyo tayari walishawahi kutokeza adharani kumuhukumu Hamad Rashid na wenzake kupitia mitandao ya mawasiliano kabla ya hata kamati hiyo ya Nidhamu na Maadili kuundwa ghafla hivi karibuni.

Akitoa uamuzi wa upande mmoja kutokana na maombi hayo yaliyowasilishwa na walalamikaji hao Januari 3 mwaka huu, Jaji Shangwa alisema kwa maoni yake kama kuna taaarifa ya dharula inayotaka walalamikaji kuvuliwa uanachama na kwamba taarifa hiyo itaatarisha haki zake zao za Kikatiba na hadhi ya wadhifa wao wa kisiasa.

“Natoa amri ya kumzuia mdaiwa na mawakala wake kuwavua uachama walalamikaji hadi ombi hili litakapokuja kusikilizwa kwa kudhuliwa na pande zote katika ombi hilo Februlia 13 mwaka huu”alisema Jaji Shangwa.

Chanzo:Gazeti la Tanzania la Jumatano, Januari 11 mwaka 2012.

No comments:

Powered by Blogger.