Header Ads

WASHITAKIWA WIZI NBC UBUNGO HURU

Na Happiness Katabazi

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam imewaachiria huru washitakiwa tisa kati ya kumi waliokuwa wakikabiliwa na kesi ya wizi wa sh milioni 168 kwa kutumia silaha mali ya Benki ya Taifa ya Biashara(NBC)Tawi la Ubungo maarufu kama ‘kesi ya mtandao’baada ya kuwaona hawana hati.


Sambamba na washitakiwa hao kuwaachia huru pia imemkuta na hatia ya katika makosa hayo mshitakiwa watano Rashid Eliakimu ambaye amehumiwa kwenda jela miaka 30. Na walioshinda kesi hiyo ni Ramadhan Dodo na mkewe Rahma Galos,Mashaka Mahengwa, Philipo Mpolea,John Mdesha,Martin Dashi,Jackson Isangu,Lucas Aloyce na Hussein Masoud ambao walikuwa wakitetewa na mawakili wa kujitegemea Majura Magafu,Shambwee Shitambala,Juvin.

Hukumu hiyo ambayo ilikuwa ikisubiriwa kwa hamu ilitolewa jana na Jaji Pelagia Khadai ambaye alianza kuisoma saa 6:08-7:50 huku akitumia lugha ya Kiswahili kusoma hukumu hiyo alianza kwa kusema ataisoma taratibu hukumu hiyo na kuitafsiri kwa lugha ya Kiswahili na mwananchi atakayechoka andoke mahakamani hapo taratibu ,siongee.

Jaji Khadai alianza kuuchambua ushahidi wa mashahidi 20 , na vilelezo vilivyoletwa na upande wa mashitaka alisema baada ya kuchambua ushaudi wa upande wa mashitaka , anakubaliana na hoja ua upande wa mawakili wa utetezi kwamba katika kesi hiyo upande wa Jamhuri umeshindwa kuleta kuleta ushahidi wa wa moja kwa moja au mazingira na pia ushahidi wa maungamo waliyoyatoa mashahidi haukufuta taratibu za kisheria na kuongeza kuwa hata utaratibu wa kufanyika kwa gwaride la utambuzi ulikiukwa.

Alisema shahidi wa kwanza na pili wa upande wa mashitaka ulimtaja mahakamani mshitakiwa wa 11(Masoud) lakini aliyekuja kumtambua Masoud kizimbani ni mtu ambaye hakuitwa kwenye kwenye gwaride la utambuzi , hivyo mahakama hii imeuona ushahidi wa mashahidi hao hauna sifa za kutosha kuishawishi mahakama hii imuone mshitakiwa huyo ana hatia.

“Pia hakuna kielelezo kilicholetwa mbele ya mahakama hii kinaonyesha mshitakiwa wa kwanza (Dodo) alitambuliwa kwenye gwaride la utambuzi lilofanyika Februali 18 mwaka 2006 lakini kielelezo ambacho ni rejista inaonyesha gwaride lilifanyika Februali 17 mwaka huo, sasa kwa mkanganyiko huu mahakama imeshindwa kuuamini ushahidi huo .... na mashahidi wote waliofika kutoa ushahidi waliambia mahakama hii kuwa siku hiyo wanatoa ushahidi ilikuwa ndiyo mara yao ya kwanza kuwaona washitakiwa hao”alisema Jaji Khadai.

Jaji Khadi ambaye muda mwingi wakati akisoma hukumu hiyo alionekana mwenye kutoka jasho usoni na kila mara alilazimika kutoa kitambaa chake cha mkononi kujifuta jasho alisema ,kwa mujibu wa shahidi wa pili, tatu walimtambua mshitakiwa wa kwanza lakini hawakupelekwa kwenye gwaride la utambuzi lilofanyika polisi na kisheria ndiyo unaotambulika na kutumika mahakamani.

“Mahakama hii imejiuliza je ushahidi dhidi ya mshitakiwa kwanza, na wanne unatosha?mahakama hii imeona ushahidi huo hautoshi kuwatia hatiani. Na ninakubaliana na upande wa utetetezi ,ushahidi wa mazingira uliomzingira mshitakiwa wa kwanza Ramadhan Dodo hautoshi kuishawishi mahakama hii imuone ana hatia kwani imeonyesha wazi kabisa gwaride la utambuzi lilifanyika miezi mitatu kabla ya mshitakiwa huyo kukamatwa”alisema Jaji Khadai.

Kuhusu washitakiwa wengine, hakuna gwaride la utambuzi lililofanywa na hakina shahidi aliyeeleza mahakama kuwa siku ya tukio Februali 2 mwaka 2006 aliwaona washitakiwa hao wakitenda kosa hilo la wizi wa kutumia silaha NBC Tawi la Ubungo.Na kuongeza kuwa mahakama inakataa utetezi ulitolewa na baadhi ya washitakiwa kwamba walichukuliwa maelezo polisi chini ya mateso makali kwani hakuna ushahidi ulioletwa unaonyesha washitakiwa walitoa maelezo chini ya mateso makali ya askari polisi.

Aidha alisema kisheria mshitakiwa anapofikishwa polisi anatakiwa achukuliwe maelezo ndani ya saa 48 lakini cha kushangaza washitakiwa walichukuliwa maelezo yao baada ya siku nne toka walipokamatwa na polisi na polisi walishindwa kuleta sababu za msingi au kifungu kilichowaruhusu kuwachukua maelezo washintakiwa nje ya sheria za nchi.

“Ni kweli askari polisi iliwakamata watuhumiwa kwa lengo la kutokomeza ujambazi hapa nchini lakini cha kushangaza baadhi ya askari waliowakamata baadhi ya washitakiwa hao walikuja kusema historia ya nyuma kwamba washitakiwa hao waliwahi kufanya uhalifu katika maeneo mbalimbali wakati katika kesi hii kilichokuwa kinatakiwa wathibitishe tukio la ujambazi lilotokea Februali 2 mwaka 2006 na si vinginevyo...na katika mashahidi wote wa upande wa Jamhuri wameshindwa kuieleza mahakama kuwa waliowaona washitakiwa hao wakitenda kosa hilo siku hiyo”alisema Jaji Khadai.

Jaji Khadai alisema baada ya kuuchambua ushahidi huo alisema pia hukumu yake iliangalia ushahidi wa mazingira ambapo alisema kwa mujibu wa hati ya ushahidi wa upande wa Jamhuri, ulidai kuwa Dodo alikamatwa Kibaha Kontena akifanya njama za kufanya uhalifu na mshitakiwa wa pili ambaye ni mke wake na wala hakuna ushahidi ulionyesha mkewe alimshawishi afanye tukio hilo na hakuna ushahidi unaonyesha walifanya ujambazi.

Akiendelea kuchambua ushahidi wa upande wa Jamhuri ulisema mshitakiwa wa nne alikamatwa Kariakoo,wa tano alikamatwa Arusha, wa sita alikamatwa Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere inagawa mshitakiwa huyo alikataa alisema yeye alikamatwa nyumbani kwake.Mshitakiwa saba walidai walimkamata Kariakoo na mshitakiwa huyo alikana akasema yeye alikamatiwa Bukoba Mkoani Kagera na mshitakiwa nane walidai walimkamata Mbezi na wala hakubisha kwamba alikamatiwa eneo hilo na mshitakiwa wa tisa polisi walidai hawajui sehemu waliyomkamata haijulikani na mshitakiwa wa kumi walidai amekamatiwa Moshi.

“Katika ukamataji huu wa washitakiwa mahakama inaona nini kinafuata baada ya ukamataji huo .Mshitakiwa tano alikamatwa na akawapeleka polisi kwenye gari ambalo lilipopekuliwa lilikutwa na silaha hivyo bila mshitakiwa wa tano kuwapeleka kwenye gari hilo mshitakiwa wa kumi ambaye tayari alikuwa ameishakamatwa na polisi asingetajwa,hakuna ushahidi:

“Kwa maana hiyo basi mahakama inamuona mshitakiwa wa tani anajua jinsi gani silaha hizo zilitumika kwenye ujambazi hatakama hakutambuliwa na mashahidi na hizo silaha alizitumia kufanya uhalifu na watu wengine tusiwatambua na ambao hawapo hapa mahakamani..hivyo katika kuangalia uzito wa kesi hii mahakama imeangalia ushadi wa pande zote mbili na unamtia hatiani mshitakiwa wa tano kwenda jela miaka 30 kwa makosa mawili kati ya sita, kosa la kula njama na kuibia benki hiyo kwa kutumia silaha.

Baada ya kulimaliza kusoma hukumu hiyo aliwataka waendesha mashitaka Inspekta Emma Mkonyi na wakili wa seriklai Edger Luoga kuangalia washitakiwa hao kama wanakabiliwa na kesi nyingine waendelee kubaki gerezani na wasiokabiliwa na kesi nyingine waruhusiwe waende nyumbani.Pia hukumu hiyo ilipokewa kwa shangwe na washitakiwa na ndugu zao huku wengine wakitaja jina Yesu,Mtume Mhamad na mama wa mshitakiwa wa tano ambaye hakuweza kutambuliwa jina lake mara moja, alianza kulia na kusababisha ndugu zake kumsaidia kushuka ngazi na kumuingiza kwenye gari.

Hii ni kesi ya tatu kati ya kesi saba za wizi wa kutumia silaha katika taasisi mabenki na maduka ya kubadilishia fedha za kigeni, na zile za mauji ,washitakiwa hao wanashinda.Kesi ya kwanza ni ile ya ya mauji katika duka la kubadilisha fedha za kigeni la Namanga Bureud Change, Mkunguni na hii ya Nbc Ubungo.Kesi nyingine ambazo bado zinawakabili ni ile ya mauji ya Ubungo mataa wakati wakidaiwa kuiba fedha za benki ya NMB Tawi la Wami-Morogoro, Msimbazi, Maxson Berued Change na Standard Charted ambazo bado zinaendelea kuunguruma katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam na Mahakama ya Kisutu.

Tukio hili la wizi ya ubungo lilitikisa jijini la Dar es Salaam na vitongoji vyake kwani watu wanaodaiwa kuwa ni majambazi wanadaiwa walitumia silaha nzito kufanya uhalifu huo.Nilikuwa ni muendelezo wa matukuo ya ujambazi yaliyokuwa yakitokea ndani ya muda mfupi tu tangu Rais Jakaya Kikwete apishwe kuongoza taifa hili Desemba 21 mwaka 2005.

Mapema 2006 ilidaiwa mahakamani hapo washiatakiwa wote wanakabiliwa na makosa sita ya kula njama na wizi wa kutimia silaha kwamba Februali 2 mwaka 2006 saa tatu asubuhi katika tawi la NBC Ubungo waliiba Sh 168,377,275 na dola za kimarekani 1680 mali ya benki hiyo na hivyo kusababishwa kusota rumande toka wakati huo kwasababu kesi hiliyokuwa ikiwakabili haina dhamana kisheria.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Januari 15 mwaka 2010

No comments:

Powered by Blogger.