Header Ads

ASKARI JKT AONGEZWA KESI YA MAUJI YA FUNDIKIRA

Na Happiness Katabazi

ASKARI wa Jeshi la Kujenga Taifa wa kikosi cha JKT Mbweni, MT 8567 Mohamed Ally Rashid ameunganishwa kwenye kesi ya mauaji ya Sechu Fundikira na kufanya idadi ya askari wa jeshi wanaokabiliwa na kesi hiyo kufikia watatu sasa.


Mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Genevetus Dudu, Wakili wa Serikali, Ester Kyala, akisoma mashitaka alidai Januari 23 mwaka huu, saa saba mchana maeneo ya Kinondoni Mwinjuma, mshitakiwa huyo na mwenzake walimuua Swetu Fundikira.

Mshitakiwa hakutakiwa kujibu chochote kwa sababu mahakama hiyo haina uwezo kisheria na kusikiliza kesi ya mauaji.

Washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni ambao walishafikishwa mahakamani ni Sajenti Roda Robert (42) wa kikosi cha JKT Mbweni na Koplo Ally Ngumbe wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania kikosi cha Kunduchi.

Kesi imeahirishwa hadi Machi 24 mwaka huu, itakapotajwa tena.

Chanzo;Gazeti la Tanzania Daima la Alhamisi,Machi 11 mwaka 2010

No comments:

Powered by Blogger.