Header Ads

OFISA JKT KORTINI TENA KWA PEMBE ZA NDOVU

 
Na Happiness Katabazi
 
OFISA uvuvi  wa Jeshi la Kujenga Taifa(JKT) Suleiman Isanzu Chesana na anayekabiliwa na kesi ya kukutwa na meno ya Tembo yenye thamani ya Sh.bilioni nne, jana tena kwa mara nyingine amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam akikabiliwa na kesi nyingine  ya kukutwa na meno ya teambo Kg.781 yenye thamani ya Sh.bilioni 9.3.
 
Mbele ya Hakimu Sundi Fimbo, wakili Mwandamizi wa Serikali  Tumaini Kweka alidai kosa la kwanza ni la kujishughulisha na  nyara hizo za serikali bila kibali kinyume na sheria ya uhujumu uchumi na kwamba Mei 23 mwaka huu,  katika mpaka wa Malawi  na Tanzania   alikamatwa akisafirisha isivyo halali nyara hizo za serikali   zenye thamani ya Sh.bilioni 9.3 zikiwa zimefichwa  katika mifuko  ya sementi  wakidai wanasafirisha cementi na kwamba upelelezi bado haujakamilika.
 
Hata hivyo Hakimu Fimbo alimtaka mshitkiwa asijibu chochote kwasababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo na kwamba ni Mahakama Kuu ndiyo yenye mamlaka ya kusikiliza na akaiarisha kesi hiyo hadi  Julai 20 mwaka huu, itakapokuja kwaajili ya kutajwa na kuamuru mshitakiwa arejeshwe gerezani.
Julai 9 mwaka huu, mshitakiwa huyo, alifikishwa mahakamani hapo kwa hakimu mkazi Nyigulile Mwaseba  akikabiliwa na kesi ya kukutwa na meno ya tembo yenye thamani ya  Sh.bilioni  nne, ambapo pia hakimu Mwaseba siku hiyo alisema mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo na akaamuru apelekwe gerezani.
 
Wakati huo huo , Ramadhan Shabani na Pendo Msaki waliokamatwa na askari wa kikosi cha Kupambana na kuzuia dawa za kulevya katika Uwanja wa Mwalimu Julias Nyerere  mwishoni mwa wiki, jana walifikishwa mahakamani hapo wakikabiliwa na  makosa ya kula njama na kusafirisha dawa za kuleya zenye  uzito wa gramu  833.51 zenye thamani ya Sh 82,732,950 .
 
Katika kosa la pili linalomkabili  Pendo peke yake ni  la kusafirisha dawa za kulevya  nakwamba Julai 6 mwaka huu, katika uwanja wa mwalimu Nyerere alikamatwa  gramu 500.08  aina ya Heroine zenye thamani ya sh67,536,000. Upelelezi bado na hakimu akaamuru waende gerezani hadi  Julai 24 mwaka huu, kwaajili ya kutajwa na akasema mahakama yake haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo.
 
Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Julai 12 mwaka 2013.

1 comment:

Powered by Blogger.