Header Ads

KADATTA .K.KADATTA AOMBA FEDHA ZA MATIBABU




Na Happiness Katabazi

MWANAMICHEZO maarufu nchini, Kadatta .K.Kadatta ameiomba serikali na umma umsaidie kumlipia gharama za matibabu ambazo zinazidi kuongezeka katika Hospitali ya Taifa ya Muhimimbili Dar es Salaam.

Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu kwa taabu huku akidai ana maumivu makali kichwani na kifuani,Kadatta ambaye aliwai kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Kinondo(KIFA), alisema amefikia uamuzi wa huo wa kuomba msaada huo baada ya kuona hana huwezo wa kugharamia gharama za matibabu ambazo zinazidi kuongezeka kila siku.

Kadatta alisema Jumamosi mchana wakati anatoka kumuangalia mjukuu wake Magomeni Mtaa wa Dosi Dar es Salaam, akiwa amesimama ilitokea pikipiki iliyokuwa inaendeshwa kwa mwendokasi na kisha ikamgonga na kukimbia ambapo wasamalia mwema walimbeba kwenye gari na kisha kumkimbiza katika Taasisi ya Mifupa Mosi, na kisha juzi kufanyiwa upasuaji wa mguu kulia ambapo imebainika amefunjika mfupa katika mguu wa wa kulia.

“Hivi jana juzi jioni ndiyo nimetolewa Moi na kisha kuletwa katika Wodi ya Sewaaji Na. 18 ambapo nimelazwa na nimewekewa vifaa maalum katika mguu wangu wa kulia siwezi kutembea na pia ninamaumivu makali sana kichwani na kifuani, na daktari ameshauri nikapigwe X-Ray kifuani na kichwani lijulikane tatizo ni nini:

“Kwa kweli ninamaumivu makali sana, na mbaya zaidi sina fedha za kujitibia, hivyo naomba wewe mwandishi wa habari ukautangazie umma kuwa mimi naomba umma wa watanzania wananisaidie kunichangia fedha ili niweze kuendelea kutibiwa hapa hospitalini…ila nashukuru uongozi wa hospitali unanipatia huduma”alisema Kadatta ambaye pia aliwai kuwa mwandishi wa makala za habari za michezo wa gazeti la Tanzania Daima.

Anayetaka kumsaidia Kaddata, atume mchango wake kupitia simu ya mkononi ya Kaddata ambayo ni 0787 777199.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumatano,Julai 4 mwaka 2013.

No comments:

Powered by Blogger.