Header Ads

WANNNE WAONGEZWA KESI YA CHE MUNDUGWAO






Na Happiness Katabazi

HATIMAYE Wahudumu wa wawili wa Idara ya Uhamiaji jana walifikishwa kalifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, nakuunganishwa katika kesi ya wizi wa Paspoti 26 inayomkabili Mwanamuziki wa muziki wa Asili nchini, Chingwele Che Mundugwao na wenzake  ambapo hadi kufikia jana kesi hiyo imefanya kuwa na jumla ya washitakiwa tisa akiwemo raia mmoja wa Uingereza.

Wakili wa Serikali Lasdsalaus Komanya mbele ya Hakimu Mkazi Sundi Fimbo 
alidai kuwa kesi hiyo jana ilikuja kwaajili ya kujatwa lakini,pia upande wa jamhuri imekusudia kufanya mabadiliko ya hati ya mashitaka ambapo jana imeweza kuwaunganisha washitakiwa wawili wapya ambao ni wahudumu wa Idara ya uhamiaji Adam Athuman na Abdallah Salehe  na washitakiwa wengine wawili ambao walifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza Julai 18 mwaka huu ambao ni  Rajab Momba na Haji Mshamu katika kesi hiyo ya Che Mundugwao ambao inawashitakiwa watano na hivyo kufanya sasa kuwa na jumla ya washitakiwa tisa.

Washitakiwa wengine ni Che Mundugwao, Raia wa Uingereza Ahsan Iqbal au Ali Patel, Ofisa  Ugavi wa  Idara ya Uhamiaji Shemweta Kiluwasha, Injinia Keneth Pius wa Kikosi  cha Zimamoto na Uokoaji na mfanyabiashara Ally Jabir.


Hata hivyo washitakiwa hao walikanusha mashitaka hayo na kudai kuwa upelelezi bado haujakamilika na hivyo hakimu Fimbo aliarisha kesi hiyo hadi Agosti 5 mwaka huu, itakapokuja kwaajili ya kutajwa na akaamuru washitakiwa hao warejeshwe rumande kwasababu bado Mkurugenzi wa Mashitaka(DPP), Dk.Eliezer Feleshi hajaondoa hati yake ya kuwafungia dhamana mahakamani.


Akiwasomea mashitaka wakili Komanya alidai kuwa tarehe isiyofahamika washitakiwa walikula njama ya kutenda kosa. Aidha tarehe tofauti Dar es Salaam, Momba aliiba hati ya kusafiria yenye namba AB 651926 mali ya serikali.

Alidai washitakiwa hao wa nne na wanadaiwa tarehe isiyofahamika Dar es Salaam, walighushi hati ya kusafiria yenye namba hiyo, kuonesha ni halali na imetolewa na Idara ya Uhamiaji ya Tanzania jambo ambalo si kweli.

Juni 3 mwaka huu, Chemundugwao na wenzake walifikishwa kwa mara ya kwanza mahakamani hapo wakikabiliwa na makosa mbalimbali yakiwemo kosa la wizi wa paspoti 26, ambapo hata hivyo DPP aliwasilisha hati ya kuwafungia dhamana ambapo hadi sasa wapo gerezani.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Alhamisi, Julai 25 mwaka 2013.

No comments:

Powered by Blogger.