Header Ads

WAKO WAPI WALIOKUWA WAKIPINGA GESI ISIJE DSM?




 Na Happiness Katabazi

MEI 26 mwaka huu, niliandika makala iliyokuwa na kichwa cha habari kisemacho “Heko JWTZ,Polisi kudhitibi vurugu Mtwara’.

Makala hiyo niliitundika kwenye ukurasa wangu wa facebook; happy  katabazi .Blogg: www.katabazihappy.blogspot.com

Baadhi ya watu waliyosoma makala hiyo na kuitafsiri wao wanavyojua wao badala ya kujadili kile nilichokuwa nimekiandika mimi, walidiriki kunitolea maneno ya kashfa na wakaitimisha kuwaita baadhi ya wakazi wa Mtwara  ambao walikuwa wakifanya vurugu kwa kisingizio cha kukataa bomba la gesi lisije Dar es Salaam, kuwa ni mashujaa na kwamba wananchi wa mikoa mingine wanastahili kuwaunga mkono.

Kwa takribani miezi mitatu sasa hatujasikia tena  wale baadhi ya Wananchi wa Mtwara na Lindi wakifanya vurugu tena kwa kisingizio cha kuzuia gesi isije Dar es Salaam, wakati wakijua hawana mamlaka ya kuzuia.

Sote tunafahamu madhara yaliyotokana na vurugu zile za kihistoria zilizofanywa na baadhi ya wakazi wa Mtwara ambao ni dhahiri sasa wamelamba matapishi yao na wameudhiirishia umma kuwa hawawezi kupambana na dola, hawana msimamo, ni waoga , wanaogopa vipigo  na kufunguliwa kesi za jinai na kushi gerezani.

Kwani kipindi kile wanaanzisha maandamano na kusambanza vipeperushi walikuwa wakijitapa kuwa hawaogopi nguvu ya dola, vipigo na wapo tayari kufa kwaajili ya kuakikisha bomba la gesi haliletwi Dar es Salaam.

Tuwaulize wananchi wale leo hii mbona hatuwasikii tena adharani wakisimamia maneno yao ya kwamba hawaliogopi dola, kufunguliwa kesi, vipigimo ,kuwekwa gerezani?

Mbona yale maandamano yao yaliyokuwa yakichagizwa  kwa matumizi ya silaha za jadi, kupambana na polisi na kusambaza vipeperushi, mbona hatuyaoni tena?Kulikoni?.Mlijiita nyie ni mashushajaa sasa iweje leo hii mmetembezewa vipigo na watu ambao mimi binafsi si wezi kudiriki kuwa ni askari wa JWTZ kwani sina ushahidi na hilo na uongozi wa JWTZ umekanusha taarifa hizo, msalimu amri?

Hivi shujaa gani anasalimu amri kwa kuogopa kipigo?Shujaa haogopi kipigo.risasi wa virungu.Shujaa anapambana hadi tone la mwisho.Sasa mimi leo nasema wale wahuni waliokuwa wanafanya vurugu Mtwara kwa kisingizio cha gesi siyo mashujaa kama walivyojiita ,minawafananisha na ‘barafu’ kwani barafu linayeyuka.Na wananchi hao wameyeyuka haraka.

Hivi karibuni kumekuwa na taarifa ambazo zimekanushwa vikali na Jeshi la Ulinzi la Wananchi(JWTZ), kuwa askari wake ndiyo wamemwagwa Mtwara na Lindi na kwamba wanajeshi hao wamekuwa wakikamata  raia wasiyo na hatia  kuwapeleka kwenye Kambi ya Naliendele na Majimaji  na kuanza  kuwapiga,kuwabaka na kuwalawiti baadhi ya wananchi hao ambao wanapinga bomba la gesi lisiunganishwe kutoka Mtwara kuja Dar es Salaam.

Binafsi navieheshimu sana vyombo vyetu vya dola ikiwemo JWTZ kwani nafahamu mchango wake katika nchini yetu, hivyo kwakuwa limekanusha taarifa za wanajeshi wake kuhusika na vitendoi hivyo, name basi sina budi kuungana na jeshi hilo kupinga taarifa hizo ambazo kwanza hakuna mwananchi yoyote aliyebakwa amejitokeza  adharani au kwenda kuripoti kituo chochote cha polisi  na akalitaja jina lake na akatoa na ushahidi kuwa amebwaka au kupigwa na JWTZ.

Tunachokiona na baadhi ya vyombo vya habari kuandika taarifa hizo, ambazo kisheria haziwezi kutumika kuwafungulia kesi za ubakaji au shambulio la kudhuru mwili hao wanaodaiwa kuwa ni askari wa JWTZ  kwa majina yao binafsi na siyo jeshi kama taasisi kubaka watu.

Katika makala yangu ile ya Mei 26 mwaka huu, nilisema wazi kuwa kuna msemo usemao ‘Vita haina macho’. Nilitumia msemo huo kwasababu nilijua mwisho wa siku kuna baadhi ya watu au vyombo vya dola ipo siku vitachoshwa na uhuni ule unaofanywa na wananchi wale na wataanza kuwachukulia hatua na wakati wakichukua hatua, yeyote atakayekuwa karibu na wale wanaoshukiwa kufanya vurugu zile.

Na kweli tumesikia kupitia vyombo vya habari vikiripiti kuwa watu wanaodaiwa ni wanausalama ambao wanaendesha opareshini maalum ya kuwashikisha  adabu wale wananchi wakarofi wanaopinga gesi isije Dar es Salaam, wakiwapiga na kuwajeruhi watu wasiyokuwa na hatia.

Kama taarifa hiyo ni ya kweli, basi hapo maana msemo wa ‘Vita haina macho’ unapotimia, kwani hao wanaodai leo wamepigwa na hao wanaodai kuwa ni wanausalama bila kosa, tuwaulize wao kama Watanzania na wakazi wa mikoa hiyo, kabla na baada ya vurugu zile waliisaidie nchi kwa kuakikisha wanatoa maoni yao ya kupinga vurugu zinazofanywa na wenzao kwa kisingizo cha bomba la gesi?

Au ndiyo vyombo vya habari vilikuwa vinaminya maoni ya wale wote waliokuwa wanapinga vitendo vya kihuni vilivyokuwa vikifanywa na wananchi wenzao walikuwa wakitumia njia za kihuni kupinga bomba za gesi lisije Dar es Salaam?

Au ndiyo tuseme sasa kwa kitendo hicho ndiyo kinawafanya wanahabari wa Mtwara hivi sasa kuishi kwa mashaka kwa kuhofia kupigwa na hao wanaodaiwa kuwa ni wanausalama na hao kundi la wananchi ambalo linapingana na agizo la serikali la kutaka gesi isiletwe Dar es Salaam?

Niitimishe kwa kusema kuwa Tanzania ni yetu sote, nishati yoyote inayopatikana ndani ya ardhi hii itatumika kwaajili ya watanzania wote na kwamba nyie wananchi mliokuwa mnapinga gesi isije Dar es Salaam, mlikuwa hamna mamlaka hayo, bali mlikuwa mnafanya uhuni tu ambao mwisho wa siku mmejikuta mkiangukia kwenye mikono ya dola, kwa kupigwa, kufunguliwa kesi na kuishia kusota gerezani na makazi yenu kuaribiwa na kuishi kwa wasiwasi kama ‘mnaoga Barazani’ kwa kuhofia vigipo kutoka kwa watu mnaodai ni wanausalama wa JWTZ wakati uongozi wa JWTZ umekanusha taarifa hizo na kusema kuwa jeshi hilo halijatoa maelekezo kwa wanajeshi wake kupiga raia.

Wanasiasa uchwara  na makundi mengine yaliyokuwa yanawajaza ujinga  ujinga huo wa kutumia njia za kihuni na vurugu kupinga bomba la gesi lisiletwe  Dar es Salaam, leo hii wamewasaliti, hawapo nanyi tena, mahakamani mnakwenda peke yenu, wao wamelala majumbani kwao na wake zao na watoto zao raha mustarehe.

Ndiyo kwanza serikali ipo katika hatua za mwisho za kuakisha bomba la gesi kutoka Mtwara kuja Dar es Salaam, linajengwa na nyie mkiendelea kushuhudia huku mkiwa mmefyata mkia.

Kama kweli nyie mlikuwa ni mashujaa na wapingaji wa hilo mlilokuwa mnalipinga kwa moyo safi, si hadi leo mngeendelea kusimamia kile mlichokuwa mkikiamini, na mngeakikisha bomba hilo halijengwi msingetishika na vitisho, vipigo lakini kwakuwa nyie mlikuwa ni bendera fuata upepo na mnatumika vibaya, mmesalimu amri?.

Wahenga walisema ‘akili ni nyeweli kila mtu anazake’.Hivyo wananchi tusikubali kutumiwa vibaya na wanasiasa uchwara wanaotafuta umaarufu au kukamata dola kwa njia za kuamasisha maandamano, migomo haramu na vurugu,lugha za kukashifiana na kuzuliana uongo.

Kwani  mwisho wa siku ni sisi ambo tumekubali kutekeleza upuuzi huo wa wanasiasa ndiyo tunakuja kupata madhara ya moja kwa moja ya kuangukiwa na mkono wa dola.Na wakati tunashughulikiwa na mkono wa dola wanasiasa uchwara wale waliotushawishi kufanya vitendo vya uvunjifu wa sheria, wanatuacha solemba.

Tutambue sheria za nchi zipo na zinawashughulikia wale wote wanaozivunja, na kuna watu ambao wamepewa madaraka ya kuruhusu au kutoruhusu jambo fulani lifanyike au lisifanyike kwa niaba yetu.

Nawapongeza askari wanaodaiwa na baadhi ya wakazi wa Mtwara kuwa ni wa JWTZ kuwa wamekuwa wakiwapiga na kuwatesa wananchi wale kwa lengo la kuakikisha wananchi hao wanaachana na habari ya kupinga gesi isiletwe Dar es Salaam.

Kwani askari hao ambao mimi sijawaona na ninarudia kuwa sina uhakika kuwa ni wa JWTZ , wameweza kusaidia kutokomeza vitendo vya uvunjifu wa sheria vilivyokuwa vikifanywa na baadhi ya wananchi wa Mtwara.

Kwani uenda bila kundi hilo la askari wanaodaiwa kuwa ni wa JWTZ  wasingeingia mitaani na kuwaadhibu wananchi hao, uenda wananchi wale wangeendelea na kelele na na vitendo vyao vya uvunjifu wa sheria kwa kisingizio cha gesi hali ambayo ingesababisha hali ya uchumi, usalama huko Mtwara kudorora.

Mwisho napongeza vyombo vyote vya ulinzi na usalama kwa kuweza kudhibiti vurugu za wahuni wale waliokuwa na kisingizio cha kukaidi gesi isiletwe Dar es Salaam, kwani zilikuwa zinalitia doa taifa letu kwenye sura ya dunia.

Kwani ni wazi sasa nilichojifunza mimi hapa nchini hasa katika utawala wa serikali ya awamu ya nne inayoongozwa na Rais Jakaya Kikwete, wananchi wengi wanapenda sana kuongea, kuhukumu, bila kwanza kuwa na ushahidi na maelezo ya kutosha kuhusu jambo wanalolijadili na matokeo yake sehemu kubwa ya jamii yetu imekuwa ikiamini habari na taarifa hizo hata kama habari hizo zilitangazwa na vyombo vya habari kwa nia ovu ya ama kumchafua mtu, kundi au chama fulani kwa makusudi na kwa uongo na pindi dola linapoamua kutumia mamlaka yake wananchi wanafyata mkia.

Sasa tunapenda sana kuvunja sheria za nchi lakini pindi tunaposhughulikiwa na dola ndipo akili zinatukaa sawa, na tunakuwa na adabu. Sasa wale wakazi wa Mtwara waliokuwa wanafanya vurugu walikuwa hawajatiwa adabu, sasa wametiwa adabu kwa kufikishwa mahakamani.

Na hilo kundi linalodaiwa ni la askari wa JWTZ kutembezea kipigo ndiyo limesaidia sana kuwatia dabu wahuni wale na ndiyo maana hadi leo huko  Mtwara tunaelezwa hakuna watu kukaa vikundi vikundi, wala kuzungumzia masuala ya gesi inatoka au haitoki,watu wanafanyakazi za kujenga uchumi wanchi.

Na mkumbuke kuwa kifungu cha 21(2) cha  Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 2002, kinawapatia mamlaka polisi  kutumia nguvu kuwakamata wale wote wanavunja kwa makusudi sheria za nchi.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika.

Chanzo:Facebook; happy katabazi ;
0716 -774494
Julai 19 mwaka 2013.




No comments:

Powered by Blogger.