Header Ads

POLISI KORTINI KWA PEMBE ZA NDOVU


Na Happiness Katabazi

ALIYEKUWA askari wa Jeshi la Polisi   mwenye namba EX G5226 PC Ramadhani Selemani (27) wa Ukonga Polisi na wenzake jana alifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, akikabiliwa na kosa la kukutwa na pembe za ndovu zenye thamani ya Sh.21 mali ya serikali.

Wakili wa Serikali Mwanaisha Kombo mbele ya Hakimu Mkazi  Nyigulila Mwaseba alimtaja mshitakiwa mwingine kuwa  ni Hamis  Mwanga(22) mkazi wa Mbadala Zakhiem.

Wakili Kombo alidai kuwa  Julai 19 mwaka huu,  washitakiwa hao walikamatwa wakiwa  Pembe nne za Ndovu, na vipande 12 za pembe za ndovu  huko eneo la Tazara Dar es Salaam, nyara zote hizo zikiwa na thamani ya Sh.Milioni 21 mali ya serikali na kwa upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika.

Hata hivyo Hakimu Mwaseba aliwataka washitakiwa wasijibu chochote kwasababu  mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo na hivyo akaiarisha kesi hiyo Agosti 7 mwaka huu kesi hiyo itakapokuja kwaajili ya kutajwa na akaamuru washitakiwa warejeshwe rumande.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Alhamisi, Julai 25 mwaka 2013.

No comments:

Powered by Blogger.