Header Ads

UPELELEZI KESI YA LWAKATARE BADO


Na Happiness Katabazi
 
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam,imearisha kesi ya kula njama na kutaka kuumua kwa sumu Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Mwananchi, Denis Msacky inayomkabili Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema),Wilfred Lwakatare na Ludovick Joseph.
Hakimu MKazi Alocye alisema kwakuwa kesi hiyo jana ilikuja kwaajili ya kutajwa na Wakili wa Serikali Mkuu, Ponsia Lukosi amedai upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika, mahakama yake inaiarisha kesi hiyo hadi Julai 22 mwaka huu, itakapokuja kwaajili ya kutajwa.

Wakili wa Lwakatare, Nyaronyo Kichere ambaye alifika mahakamani hapo  na Lwakatare ambaye yupo nje kwa dhamana, Ludovick yeye bado yupo gerezani kwasababu ameshindwa kutimiza masharti ya dhamana yaliyotolewa na mahakama hiyo Juni 11 mwaka huu, ambapo Hakimu Katema alisema ili washitakiwa wapate dhamana ni lazima kila mshitakiwa awe na wadhamini wawili wanaotoka taasisi zinazotambulika kisheria  ambapo kila  mdhamini atatakiwa asaini bondi y a sh.milioni 10 pamoja na washitakiwa wenyewe,washtakiwa hao kusalimisha  hati zao za kusafiria mahakamani na kutotoka  nje ya jiji la Dar  es Salaam bila ya kuwa na kibali cha mahakama. Lakini hadi jana Ludovick ameshindwa kutimiza masharti hayo nab ado anaendelea kusota gerezani.

Machi 18 mwaka huu, ilidaiwa na wakili wa serikali Mkuu Lukosi kuwa washitakiwa walitenda kosa hilo.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Julai 9 mwaka 2013.

No comments:

Powered by Blogger.