Header Ads

MAFISADI WANAOMWAGA FEDHA MAJIMBONI WATAJWE

Na Happiness Katabazi

NITAKUWA ni mchawi ambaye ninakula nyama za watu kama ningeshindwa kuandika makala ya kuwapongeza baadhi ya wabuge wa ccm ambao wameendelea kuonyesha ushujaa mbele ya umma kwakupinga wanachoma wenzao ambao wanatuhuma za ufisadi.

Wabuge CCM waliojipambanua kupiga ufisadi ulioota mizizi kwa baadhi ya wanachama wenzao ni Spika wa bunge, Samuel ,Sitta,Dk.Harrison Mkwakyembe(Kyela),Christopher Sendeka(simanjiro),Fred mpendazoe(kishapu),Beatrice Shelukindo(Kilindi),Lucas selelii,John Shibuda(Maswa),James Lembei na mjumbe wa NEC, Nape Nnauye.

Makamanda hao wameka wazi msimamo wao kwamba bila kujificha wataendelea kupambanana ufisadi kwa sababu ni kikwazo cha maendeleo la taifa letu.

Nimelazimika kuandika makala hii kwasababu mimi nimiongoni mwa wananchi ambao tumekuwa tukikemea ufisadi unonywa na baadhi ya wananchi wenzetu walioshika nyadhifa mbalimbali ndani ya CCM na serikalini,lakini wakati tukikemea uovu huo kwa njia mbalimbali baadhi ya viongoi wa chama tawala walitupinga moja kwa moja.

Hivyo leo hii tunaposhuhudia wabunge wa CCM wakisimama majukwaani na kukiri kwamba ndani ya chama chao kweli kuna manyang’au napata faraja sana na kuanza kuamini lile somo letu la kupinga ufisadi wa mali za umma limenza kueleka hata kwa wabunge wa ccm.

Hivi karibuni makamanda hao wa ccm wameukuliwa wakisema kuna mafisadi wamemwaga fedha kwenye majimbo yao ili waangushwe kwenye uchaguzi ujao, binafsi nawataka makambana hao wawataje kwa majina hao mafisadi hao kwasababu wasipofanya hivyo wakae wakijua watakuwa wakiwajengea nguvu mafisadi ambazo hivi sasa hawana.

Kwasababu vyama vya upinzani walikwisha wakata miguu mafisadi kwahiyo makamanda hao wasitake kuwavalisha miguu ya bandia mafisadi.

Binafsi nilikuwa miongoni mwa wananchi tulioudhuria mkutano wa kihistoria ulioandiliwa na vyama vya upinzani pale uwanja wa mwembeyanga temeke mwaka juzi,ambapo Dk.Willbroad Slaa alianika orodha mafisadi na wala hakuficha jina la watuhumiwa hapo ambao miongoni mwa aliyowataja hivi sasa wameishaburuzwa mahakamani.

Kwahiyo kama wakina Dk.Mwakyembe wameamua kwa dhati kujiunga katika vita ya ufisadi ,basi waingie kwa gia ile ile vyama vya upinzani kwa kuwataja kwa majina hao mafisadi wanaotapanya fedha kwa malengo ya kuwang’oa wao ili wawekwe wagombea watakaokidhi matakwa ya mafisadi ili tuwajue na siwachague.

Ninachokiona kinachofanywa na wakina Mwakyembe ni kizuri kwasababu hapo nyuma tulisema ccm inanuka ufisadi,inakabiliwa na makundi,wanachama hawapiki chungu kimoja lakini Katibu Mkuu wa chama hicho,Yusuf Makamba alipinga wazi wazi,sasa leo hii wabunge wachama chake na mwenyekiti wa chama hicho rais Jakaya Kikwete wiki hii amekiri hayo na akaeleza wazi matatizo hayo yamebua chuki mbaya miongoni mwa wanachama hadi kufikia hatua ya kuhofiaa kutiliana sumu kwenye vinywaji.

Ipo haja ya kuwapa moyo wabunge hao wa ccm lakini wapinzani walivyoeleza ufisadi na kusem ccm ni chama cha mafisadi ,walieleza kwamba ufisadi upo ndani ya Itikadi na sera za chama hicho.Kwa hiyo wabunge hata mwenyekiti wao wakiamua kupambana na hilo wabadilishe Itikadi na sera za chama chao na kama hawawezi watoke huko wakajiuge na vyama vya upinzani ama waanzishe chama chao kwasababu huko siyo kwao.

Mimi ninachokiona kwa makanda hao,ile nyumba ya ccm siyo yao,watoke huko na kama hawataki kutoka ama watauwawa ama nao mwisho wa siku nao watageuka kuwa mafisadi na hili ni rais kufanyika kwani kila mmoja wao atatupiwa mfupa atafune.

Na ndicho ambacho tunaweza kusema walichokubaliana kwenye kikao cha Halmashauri kuu(NEC)hivi karibuni wakaunda kamati itakayosimamiwa na rais mstaafu Ally Hassan Mwinyi,Spika wa Bunge la Afrika mashariki mstaafu,Abdullahman Kinana na Makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa, Pius Msekwa,ni kamati ya kuwatafutia mifupa wabunge ‘vizabizabina’ili wapoe.

Kama rais kikwete amekiri kuwepo kwa chuki miongoni mwa wanachama wake na baadhi ya wanachama wake wakabilia na tuhuma za ufisadi na mambo hayo yameibua chuki kali anaunda kamati hiyo ya nini?

Nikweli kampeni zisizo rasmi zimeanza kuelekea uchaguzi mkuu wa mwakani, hilo aitushangazi hivyo hoja kama makamanda hao wanajitautia umaarufu kwenye majimbo yao na jamii na kwamba vita wanayopigana ni yakutaka kupigania majimbo yao ni ya kweli tupu.

Hivyo hatuwezi kuwalaumu wabunge hao kwamba wanajitafutia umaarufu ,hapana kwani kila mwasiasa anataka umaarufu.Kahiyo hoja ya kwamba makamanda hao wanajitafutia umaarufu haina msingi kwani hata viongozi wa vyama vya upinzani nao pia wanataka umaarufu.

Wanasema siku za mwizi ni arobaini ,kwani ni ccm hii iliwakejeli wapinzani kuwa inawapakazia sifa mbaya na kwamba chama hicho hakina mafisadi lakini leo hii wabunge wa ccm wanasema wapishana majukwaani kuthibitisha madai ya wapinzani kwamba ndani ya chama hicho kuna mafisadi.

Kwahiyo hata hizo kesi zilizofunguliwa mahakama za ufisadi wa fedha za umma na kesi tatu kubwa zinazotorajiwa kufunguliwa wakati wowote,zote ziliibuliwa na wapinzani kwahiyo ccm kamwe hawana la kutambia hapo kwani huwezi ukafanya ufisadi badala ya kuumbuliwa,tuisifu kwasababu imekiri uwepo w ufisdi.

Kwahiyo ccm aina hoja juu ya vita ya ufisadi kwakuwa kila wakalofanya kuhusu ufisadi wakae wakitambua waanzilishi wa vita hiyo ni vyama vya upinzani na makundi mengine ya kijamii vikiwemo vyombo vya habari.

Ikumbukwe tunaelekea uchaguzi mkuu mwakani,ccm wasijaribu kujitapatia sifa kupiti kupinga vita ufisadi.

Mungu ibariki Tanzania,mungu Ibariki afrika

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima Jumapili, Septemba 13, 2009
0716 774494

No comments:

Powered by Blogger.